We Masatu
Acha kunizulia mambo ati. Tanzania Njema amesema CCM inajisafisha kwa kuondokana na rushwa; mimi nisema katu asilani CCM ni ile ile yenye kukumbatia rushwa. Waanzie wapi kujisafisha ili hali wameingia kwa rushwa? Waanze wapi kujisafisha chamani wakati serikalini wanajichafua kwa rushwa? Waanze wapi kujisafisha chamani wakati chaguzi za chama mwaka huu toka chini zilikuwa na rushwa? Lakini wasema upinzani ujisafishe; lini upinzani umejichafua kwa rushwa kama CCM ili ujisafishe?
Msinitie vidole vya macho Asha mie. Nataka tu mnieleze nielewe, na mnanijua humu-nikielezwa nikaelewa huwa nakubali kuelewa.
Hivi Masatu nawewe CCM? Nishawishi basi nami nijiunge. CCM ya Kikwete ina lipi jipya?
Asha
Bibie,
Labda hapa tukubaliane kutokubaliana, mtazamo wangu kuhusu posting ya TN ni kama nilivyoeleza hapo juu, kimsingi nakubaliana na alichosema TN, hata hivyo hayo ni maoni yangu kama mtu binafsi.
Kwa upande mwingine naheshimu mawazo yako ingawa sikubaliana nayo.
Suala kama mimi ni CCM au la nadhani hilo langu binafsi na halitakusaidia kama utajua, kwa msingi huo huo swali la ushawishi wangu kwako kujiunga na CCM nitakuwa nimelijibu pia