Mkuu mbona watu wanaitana sana "msenge" mitaani?Soma vizuri mkuu
Hata huko magharibi kuna wachache wanatamani maisha ya kupiga watoto na wanawake ila ndio hivyo wanazidiwa nguvu na wale waliostaarabika zaidi kwa hiyo wanabaki kutamani wangeishi kama nyie.No mkuu nmetolea mfano tu , mmonyoko wa maadili ni mkubwa sana kwa wenzetu tofauti kabisa na kwetu , pia hata wao wanapenda sana jinsi sisi tulivyo naongea kitu ninachokijua na sio nilichosikia mkuu .
😁😁 ngoja tusichape tuone itakuajeMbona nchi zetu tunazochapa wototo zimejaa rushwa, uongo, ufisadi, kesi za kubambikia, ukwepaji kodi, uchepukaji, uvivu n.k?!
Ukweli mtupuMtoto hupewa adhabu akifanya makosa Kwa dhamiri.
Bahati mbaya Watoto wengi HUFANYA Makosa Bila dhamiri yàani Bila kujua ni Makosa.
Hivyo unapompiga inamtengenezea chuki zaidi ya kujifunza.
Kwa Bahati mbaya zaidi Wazazi wengi ni Wabinafsi, wakatili àmbao hujijali waô wènyewe.
Mzazi lazima uwe na Sifa ya Ualimu. Kumpiga Mtoto mara nyingi huleta matokeo Hasi kuliko matokeo chanya.
Fikiria Mtoto chini ya Miaka 14 unampiga mafimbo mengi kisa hajafua nguo Zake. Kumbe Mtoto mwenyewe hajafanya kusudi kutokufua Bali amesahau.
Sasa wewe kama siô chizi ni nini?
Au unampiga Mtoto Kisa kapoteza au kuangusha Pesa uliyomtuma akanunue maandazi. Mtoto hajafanya makusudi.
Kûna namna ya kudili na Makosa ya Mtoto hasa Yale àmbayo hajafanya kusudi.
"Mda mwingine tusipuuze desturi zetu na kuiga za watu ambazo kiundani zina madhara yake pia" Kaka umenena vyema 100%.Sisi wa africa bila kunyukwa hatuendi jamii nyingi tunazotamani kuziiga nao wana mambo yao ya ajabu , sio kitu cha ajabu watoto wakizungu kuwaambia wazazi wao wanavutiwa na mahusiano ya jinsia moja na kwao ni kawaida tu.
Mda mwingne tusipuuze desturi zetu na kuiga za watu ambazo kiundani zina madhara yake pia.
Jamii yetu ina maadili au ina uoga na unafiki?Hizo nchi ambazo watoto hawachapwi zina mmonyoko mkubwa wa maadili pia ,sisi tunajiona hatuna maadili ila ukitembelea kwa wenzetu utaona bado sisi tuna maadili sana😁
Bora tukae kwenye huo uoga na unafki mkuu, wenzetu wamevurugwa asee😁Jamii yetu ina maadili au ina uoga na unafiki?
Hili huwa mnalipimaje? Maadili yanaendana na ustaarabu , kitu ambacho waafrica ni 0.Hizo nchi ambazo watoto hawachapwi zina mmonyoko mkubwa wa maadili pia ,sisi tunajiona hatuna maadili ila ukitembelea kwa wenzetu utaona bado sisi tuna maadili sana😁
Umeibua hoja moja nzuri sana.Watoto wanatofautiana sana. Ni ngumu wote kufit kwenye mfumo mmoja.
Nawafahamu watoto kadhaa ambao hawajawahi kuchapwa na wana maadili mazuri kuliko watoto wanaochapwa. Hao ni watoto wa marafiki zangu ambao ni wazungu waliooa wabongo.
Tatizo kubwa la wabongo wasiochapa ni kuwa wanadekeza. Mtoto haambiwi limits zake. Anajihisi malkia au mfalme ndani ya nyumba.
Wenzetu hawachapi lakini hawadekezi, wengi wao wako firm na wana rules za familia wanafuata.
wewe hukupigwa?Kupiga mtu yeyote yule(hasa asie na uwezo wa kukurudishia) ni hatua ya juu kabisa ya uonevu.
Jiulize, wewe ukikosea, ni nani huwa anakupiga?