Je, Watoto wanaolelewa bila vipigo hawana maadili?

Je, Watoto wanaolelewa bila vipigo hawana maadili?

Siku ya kwanza kwenda shule mzazi anakuambia uwe makini wasije wakakuibia .

Hapo ukiangalia unaenda boarding school 🤔🤔🤗😁 maadili sisi hatuna
Mkuu ninao marafiki zangu huwa wanatamani sana wawe kama sisi , ndio maana nchi nyingi za ulaya na America kwa sasa wanavutiwa ki mahusiano na watu kutoka Africa sababu ni hiyo ya maadili.

Mume kupewa pole au kuulizwa kama amekula ,hiyo kwa wenzetu ni kituko sisi bado tupo kwenye reli mkuu😁😁😁
 
Watoto wanatofautiana sana. Ni ngumu wote kufit kwenye mfumo mmoja.

Nawafahamu watoto kadhaa ambao hawajawahi kuchapwa na wana maadili mazuri kuliko watoto wanaochapwa. Hao ni watoto wa marafiki zangu ambao ni wazungu waliooa wabongo.

Tatizo kubwa la wabongo wasiochapa ni kuwa wanadekeza. Mtoto haambiwi limits zake. Anajihisi malkia au mfalme ndani ya nyumba.

Wenzetu hawachapi lakini hawadekezi, wengi wao wako firm na wana rules za familia wanafuata.
 
Hizo nchi ambazo watoto hawachapwi zina mmonyoko mkubwa wa maadili pia ,sisi tunajiona hatuna maadili ila ukitembelea kwa wenzetu utaona bado sisi tuna maadili sana😁
Nimeishi na waarabu hawana tabia hizo za kuchapa na watoto wao wamenyooka balaa! Wajapani nao pia hawana tabia hizo ila ndio wanaongoza duniani kuwa na discipline. Mi nadhani waafrica hatutaki kutoka nje ya box kifikra kufikiria njia mbadala za malezi isiwe lazima fimbo pekee yake. Halafu pia si waafrica muda wa kukaa na watoto wetu sometimes unakuwa ni changamoto sana nadhani hii pia inachangia
 
Nimeishi na waarabu hawana tabia hizo za kuchapa na watoto wao wamenyooka balaa! Wajapani nao pia hawana tabia hizo ila ndio wanaongoza duniani kuwa na discipline. Mi nadhani waafrica hatutaki kutoka nje ya box kifikra kufikiria njia mbadala za malezi isiwe lazima fimbo pekee yake. Halafu pia si waafrica muda wa kukaa na watoto wetu sometimes unakuwa ni changamoto sana nadhani hii pia inachangia
Hahaha inaleta maana mkuu, kuna siku tulitembelea hifadhi fulani tukaona sokwe anamchapa mwanae bakora za kutosha😁😁
 
Nimeishi na waarabu hawana tabia hizo za kuchapa na watoto wao wamenyooka balaa! Wajapani nao pia hawana tabia hizo ila ndio wanaongoza duniani kuwa na discipline. Mi nadhani waafrica hatutaki kutoka nje ya box kifikra kufikiria njia mbadala za malezi isiwe lazima fimbo pekee yake. Halafu pia si waafrica muda wa kukaa na watoto wetu sometimes unakuwa ni changamoto sana nadhani hii pia inachangia
Waafrika wengi kutumia akili na kufikiri nje ya box ni kama kujichosha na kupoteza muda
 
Sisi wa africa bila kunyukwa hatuendi jamii nyingi tunazotamani kuziiga nao wana mambo yao ya ajabu , sio kitu cha ajabu watoto wakizungu kuwaambia wazazi wao wanavutiwa na mahusiano ya jinsia moja na kwao ni kawaida tu.

Mda mwingne tusipuuze desturi zetu na kuiga za watu ambazo kiundani zina madhara yake pia.
Kuna watu wanachapa hadi wake zao na hawaelewi ukiwaambia mwanamke hatakiwi kuchapwa!🤣
Kwa kina FaizaFoxy maustadh wanatembeza mboko vibaya sana madrasa!
 
Waafrika wengi kutumia akili na kufikiri nje ya box ni kama kujichosha na kupoteza muda
Sie waafrika kukuta baba amerudi nyumbani mapema anawaita watoto wake na kuwauliza wana changamoto gani wanazopitia huwa ni nadra sana! Huwa ni mwendo wa amri na vipigo tu! Kumbe sometimes kuna changamoto watoto wanapitia zinazofanya wawe na tabia za ajabu.
 
kwa hyo unataka kuniambia viongozi wa serikali wanaoiba hela za umma hawakuchapwa udogoni? Asilimia 80 ya watanzania maadili yetu ni mabovu licha ya kuchapwa sana fimbo udogoni wengi wetu ni wezi, wachepukaji. Sio wastaarabu na tabia nyinginezo za ovyo

Mi ukiniuliza km fimbo zimetusaidia kwenye suala la maadili ntakujibu zimefeli pakubwa sababu wengi wetu zimetufanya tuwe na nidhamu ya uoga. Tunaonyesha nidhamu mbele ya wazazi ila tukiwa pekee yetu tunafanya mambo ya ajabu
Fimbo kwa watoto ni tabia za kijima za karne ya 17, ni jambo la hovyo sana kumchapa mtoto, wanaochapa watoto wenyewe wengine ni walevi wa kupindukia, mafisadi, wachepukaji, wakwepa kodi n.k
 
Back
Top Bottom