Chief Wingia
JF-Expert Member
- Jul 12, 2013
- 2,653
- 4,744
Kwa mila za zamani mkubwa akifariki basi yule mdogo mume analithi yote aliyokua nayo mkubwa. Hivyo wewe hapo unahitajika kusimama katika nafasi ya marehemu..
Wewe si mzaliwa wa kwanza ila unabaraka za mzaliwa wa kwanza aliyetangulia. Simama katika nafasi yako sasa
Ndio ukubwa huo..ndio ghalama ya kua mkubwa.Kweli mkuu yaani mpka mda mwingine nagombana na mke wangu kwa kutotumiza majukumu yangu ya family yangu wakati pesa inaisha kwa kuwasaidia wadogo zangu kwa mambo yao nk, nakumbuka mpaka nilichelewa kuingiza umeme ktk kibanda changu kwa mda wa miaka kama 4 wakati huo mdogo wangu namsomesha shule ya private ada laki 8 plus nauli na chakula kila siku nampa kwa mwaka ilikuwa ni pesa ndefu wakat umeme ilikuwa ni laki 3 plus gharama za wayaling nk... Naamini Mungu atanilipa kwa mambo yanoyowatendea wadogo zangu
Yupo tayari mkewe asiavae nguo kwenye Eid au Xmass ili tu wadogo zake walipiwe ada, ukikuta mzaliwa wa kwanza anayejitambua na kusimamia majukumu yake hufanya kila kitu ili tu ndugu zake wasipitie tabu alizozipita na wazazi wake wakati anazaliwa.
"Aisifuye mvua, ujue imemnyea" imegusa wengi nami nikiwa mmoja wao mkuu!Mate kwani kuna tatizo gani.?
Kuna tatizo kubwa la uelewa.Ondoa shaka Ndugu yangu mpendwa. Mada imewalenga Wazaliwa wa Kwanza ambao wapo pande zote. Muumba wetu ni mmoja tunaemwabudu na yeye hana Dhehebu.
Nikupe tu mfano rahisi: Safari toka Dom kwenda Dar, wako watakaosafiri kwa basi, watakaoruka kwa ndege, watakaotumia pikipiki na hata watakaotumia miguu. Hao wote watamaliza safari yao salama kufika Dar. Ndivyo ilivyo ktk kufika kwa Muumba wetu.
Tatizo ni nini.?Kila mtu kwa Mungu ana hadhi sawa. Tofauti zinazoweza kuwa za vipaji zina lengo la kutajirishana kwa manufaa ya wote.
Hakuna mtu bora kwa maana ya hadhi ya binadamu kwa Mungu.
Mawazo kwamba wazaliwa wa kwanza ni potential au hawafanikiwi katika uchumi nakadhalika hayana ukweli wowote; ni hisia tu.
Mungu amemuumba mtu kwa lengo moja tu, mtu amjua, ampenda na amtumikie.
Kuna vitu vinavyofanya mtu awe potential au kinyume chake. Katika hivyo vitu wazazi wakichukuwa nafasi ya kwanza na jamii ndio huandaa mwelekeo wa mtoto.
Hapa kuna suala la elimu, mafundisho na uelewa wa mambo. Elimu, mafundisho na uelewa mambo ukikosekana watoto huangamia.
Tatizo ni upotoshaji; andiko lako linapotosha.Tatizo ni nini.?
Nimekosea wapi mate..?
Je ww ungeelezeajeKuna tatizo kubwa la uelewa.
Suala la Mungu halifafanuliwi kama safari ya kutoka Dodoma kwenda Dar es Salaam au kwingine kokote. Kuelewa hivi ni makosa makubwa.
Hapa kuna suala la taratibu zinazoongoza na kutawala hivyo vyombo, unalifafanuaje.