Je Zanzibar Inahitaji Truth & Reconciliation Comm。Kuponya Makovu ya Mapinduzi, ili Upinzani Ukishinda,Upewe?。Sis & Bro,Can You Please Do The Needfu?。

Je Zanzibar Inahitaji Truth & Reconciliation Comm。Kuponya Makovu ya Mapinduzi, ili Upinzani Ukishinda,Upewe?。Sis & Bro,Can You Please Do The Needfu?。

Kwa attitude za Wanzanzibar wengi kuhusu watanganyika, sishauri serikali ifanye maridhiano hivi karibuni.

Upinzani ukishika Zanzibar Hapana Shaka Muungano utavunjika
 
Mkuu Pascal
Mimi naona kitu cha kufutwa ni msamiati wa mapinduzi, mfano leo hii kuita serikali ya mapinduzi Zanzibar si sawa. SUK imejumuisha CCM na ACT, na walienda kwenye sanduku la kura, right? Sasa kuna justification gani kuiita serikali ya mapinduzi? CCM na ACT wamempindua nani na lini?

Hili neno linatumiwa na wahafidhina walioko CCM ambao hawako tayari kwa uchaguzi huru na haki Zanzibar. Wanajua waliingia madarakani kwa kupindua na kwenye uchaguzi huru hawawezi shinda. Nakubaliana nawe bila reconciliation hakuna amani ya kweli Zanzibar, maana hata huu uchaguzi ujao uwezekano wa ACT kushinda ni mkubwa ila kama enzi za Jecha watatangazwa CCM. Hii itakuwa hadi lini?

Naunga mkono hoja
 
Ahsante kwa darasa, lakini nadhani linakinzana kwa kiasi fulani na kumbukumbu sahihi za kihistoria! Sultan alikuwa mkoloni.

Zanzibar, an island off the coast of East Africa, was colonized by several powers throughout its history:

1. Portuguese Colonization (1498–1698):

The Portuguese were the first Europeans to colonize Zanzibar. They controlled the island as part of their trade routes along the East African coast.

2. Omani Arab Rule (1698–1890):

In 1698, the Sultanate of Oman took control of Zanzibar, establishing it as a key center for the Indian Ocean trade, particularly in spices and slaves. In 1840, Sultan Said bin Sultan moved the Omani capital to Zanzibar, further cementing its importance.

3. British Protectorate (1890–1963):

In 1890, Zanzibar became a British protectorate under an agreement between Britain and Germany. Although the sultans continued to rule in name, the British effectively controlled the island’s administration.

Zanzibar gained full independence from British influence in 1963, becoming a constitutional monarchy under the Sultan. However, a revolution in 1964 overthrew the sultanate, and shortly thereafter, Zanzibar merged with mainland Tanganyika to form the United Republic of Tanzania.
Hapa tofauti ni nini?
 
Wanabodi,
Makala yangu kwenye Nipashe ya Jumaoili ya Leo。

Leo Tarehe 12 January 2025, imedondokea siku ile ile ya Januari 12, 1964, ilikuwa ni siku ya Jumapili. Leo Tanzania inaadhimisha miaka 61 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, wakati Wazanzibari wengi wanashereheka kuyapongeza Mapinduzi hayo (na wengine hadi kuyapa utukufu kwa kuyaita Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, ambalo neno Utukufu, kwa dini mbili kuu, Wakristu na Waislamu, Utukufu ni kwake tuu na wake tuu, Mwenyeenzi Mungu, hivyo kuita kitu kingine chochote kitukufu ni kama kufuru!), kuna Wazanzibari wengine, japo wachache, siku hii ni siku ya kumbukumbu mbaya, kwa kuwapoteza wapendwa wao, kutokana na umwagwaji damu wa Mapinduzi hayo na baada ya Mapinduzi.

Hivyo makala hii ni swali Je Zanzibar Inahitaji Truth & Reconciliation Commission ili Kuponya Makovu ya Mapinduzi, ili Upinzani Ukishinda,Upewe?。Hili ni ombi kwa Sister wangu na Brother wangu,yaani Kaka mtu na Dada Mtu, Can You Please Do The Needfu?。

Hakuna ubishi kabisa, kuwa Mapinduzi ya Zanzibar, yameleta kheri, lakini ni ukweli mchungu pia yameleta shari iliyosababishwa na umwagaji damu mkubwa uliosababisha maumivu makubwa kwa waliopinduliwa ambao wanaishi na makovu ya Mapinduzi hadi leo!。

Kule kwenye mtandao maarufu kuliko mitandao yote ya kijamii nchini Tanzania, Jamii Forums, shamra shamra za kuisubiria siku hii, zilianza siku nying kabla kushamirishwa na Fake News kuwa Sultan mpinduliwa anarejea Zanzibar kufanya ziara rasmi na atahudhuria maadhimisho ya leo. December 28 lilipanda bandiko hili Zanzibar Kumpokea Sultan Jamshid: Ziara ya Kihistoria Baada ya Miaka 60 Uhamishoni

Hilo la Sultani kurejea mimi nikalidaka na kulitolea mapendekezo yangu kumi kwa SMZ.

Ndipo kaka yangu mmoja, kutoka Zanzibar, naomba kumtaja kwa jina moja tuu Kaka Chalz, ni kaka yangu alinipokea RTD, ile mwaka 2000, akatufundisha kazi ya utangazaji, hivyo tunawaheshimu sana kaka zetu hawa, na hata tunapokosea, hawaachi kutupigia simu kuendelea kutuongoza mpaka leo mpaka kesho, Asante Kaka Chale!.

Basi Kaka Chale akaniuliza una uhakika na chanzo chako cha habari kuwa hii ni habari ya kweli?, nikamjibu kwa vile imetangwa na Jamiiforums, kwa jina maarufu JF, ni chombo cha kuaminika, ingekuwa fake, JF inatumia mfumo wa Jamii Check kubaini fake news na kuzifuta, hivyo itakuwa kweli.

Ndipo nikaipitia ile habari kwa mara ya pili kuisoma source, nikakuta ni jamaa yuko Oman!, nikamtafuta kaka yangu mwingine Zanzibar huyu ni Mzee Salim Said Salim, mwandishi wa siku nyingi, tunamuita jina la Mzee SSS, yeye ana nasaba kidogo na ukoo wa Sultan, ukitaka kumtibua SSS, mwambie Mapinduzi Matukufu!. Salim akawapandia kwa simu, Oman, familia ya Sultan wakakanusha kuwa ni fake news!. Asante Mzee SSS!.

Ndipo nikawasiliana na Mkuu Maxence Mello, chapisho langu likaondolewa, na nikabandika chaousho jingine Story ya kurejea kwa Sultan wa Zanzibar ni Fake News! JF Tumelishwa Tango Pori!. Asante Kaka Chale kuniwezesha kuupata ukweli
ila chapisho la msingi halikuondolewa mpaka leo lipo. Nikamrudia Kaka Chale, nikamshukuru kwa angalizo lake, ila nikamwambia baadhi ya yale mapendekezo yangu 10, mengine ni valid, yafanyiwe kazi!. Baada ya hii fake news, jibu la familia ya Sultan alilotoa, ndilo likanijulisha bado kuna watu wana machungu na Mapinduzi yale.

Watu hawa wapoozwe!, waponywe!。 Na Baada ya ujumbe huo mkali kutoka Oman, masikini sultani akaitwa na Mola wake!TANZIA - Aliyekuwa Sultani wa Mwisho Zanzibar, Sultan Sayyid Jamshid Al Said, Afariki Usiku Huu, Omani, usikute ni hii fake news ya jf imemsababishia mtu kifo!。

Huu ni mwaka wa uchaguzi, na hakuna ubishi siasa za Zanzibar, licha ya uwepo wa SUK, bado zinaathiriwa na mzimu wa machozi, jasho na damu, zilizomwaika na kufukiwa bila kufanyiwa hitma, na kuna watu wana makovu ya machungu ya mapinduzi yale,wakija kushika madaraka,kuna watu watakoma!。

Hivyo matokeo ya baadhi ya chaguzi za Zanzibar, ni matokeo yale yale ya ule uchaguzi wa mwaka 1963. Mfano mzuri ni uchaguzi wa mwaka 2015, kuna msemo wa Kiingereza unaosema numba haziongopi!.

Matokeo ya NEC ya uchaguzi wa 2015 kwa Zanzibar, yamethibitisha pasi shaka kuwa uchaguzi wa Zanzibar wa 2015, kama usinge futwa, Maalim Seif Shariff Hamad wa Chama cha Wananchi CUF ndie angelikuwa mshindi wa uchaguzi wa rais wa Zanzibar kwa kutumia kigezo cha matokeo ya uchaguzi wa urais wa JMT, uliosimamiwa na NEC kule Zanzibar ambao uchaguzi haukuwa na dosari, katika uchaguzi huo, mgombea wa UKAWA, Edward Ngoyai Lowassa, alimshinda mgombea wa CCM, Dr. John Pombe Magufuli.

MGOMBEA KURA HALALI ASILIMIA
DR. JOHN POMBE MAGUFULI
194,317 46.5%
EDWARD NGOYAYE LOWASSA 211,033 50.50%
IDADI YA KURA HALALI 417,882
Hii maana yake Zanzibar upinzani unaweza kushinda, sasa kwa vile bado kuna hostilities za machungu ya Mapinduzi, siku upinzania ukishinda Zanzibar, kutaibuka kulipiza kisasi!.

Mwaka 2015 niliandika Iwapo CCM itashindwa Zanzibar, Nini Majaaliwa ya Muungano?
Nilishauri kisha nikashauri Kumuepushia aibu ya Kushindwa, CCM isimsimamishe Dr. Shein hili halikufanyika,na matokeo ndio yale ikabidi watu wafunike kombe。。。

The like scenario naiona Zanzibar 2025,hivyo nashauri
  1. Zanzibar ianzishe truth and reconciliation commission watu waruhusiwe to vent,hivyo to heal machungu ya mapinduzi。
  2. Decemba 10 iwe ni siku ya mapumziko ya uhuru wa Zanzibar,sio lazima iadhimishwe kwa shamra shamra,inaweza kubadili jina ikaitwa Sultan Day。
  3. Neno Matukufu kwenye Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar,lisiendelee kutumika,yaitwe tuu Mapinduzi ya Zanzibar na vibwagizo Mapinduzi Daima, na Tutayalinda kwa gharama yoyote, tuachane nayo ili kuponya wapinga mapinduzi
  4. Falsafa ya 4R za Samia,itumike hadi Zanzibar,mshindi wa kweli wa uchaguzi wa Zanzibar atangazwe,mfano mzuri ni huu Elections 2015 - Imethibitishwa pasi na shaka kuwa ni kweli kabisa, Zanzibar, Maalim Seif na CUF ndio walioshinda na ili kumuondolea posibility ya aibu ya kushindwa,nimetoa ushauri hapa kwenye HII mada。
Hivyo nawashauri Dada yangu Rais Samia, na kaka yangu rais Dr. Mwinyi, kubalini kutibu makovu ya Mapinduzi, ili kuzimaliza siasa za hostilities, ikitokea upinzani umeshinda Zanzibar, hakuna haja kufunika kombe tena mwanaharamu apite, iwe ni kupokezana kwa amani na upendo. Miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar, Tuyaenzi kwa 4R za Rais Samia?, JMT Tuitendee Haki Zanzibar?, Tuwatendee Haki Wazanzibari? Mshindi Halali Apewe?

Namalizia kwa lile swali la msingi la uzi huu Je Zanzibar Inahitaji Truth & Reconciliation Comm。Kuponya Makovu ya Mapinduzi, ili Upinzani Ukishinda,Upewe?。Sis & Bro,Can You Please Do The Needfu?。

Heri ya Mapinduzi.

Paskali.
Naunga mkono hoja.....

Zanzibar wanahitaji mno tume ya ukweli na maridhiano hasa kuhusu kilichotokea 12/1/ 1964.
 
Hapa tofauti ni nini?
Tofauti ni kwamba Sultan alirejeshewa na Waingereza control ya Zanzibar na kuifanya kuwa constitutional monarchy. Kumbuka, baada ya Oman Arab Rule na Zanzibar kuwa British Protectorate, Sultan hakufungasha virago vyake. Aliendelea kutumiwa na Waingereza kama colonial administrator hadi aliporejeshewa control. Sultan hakuwa Mzanzibar. Alikuwa mkoloni. Period!
 
Tofauti ni kwamba Sultan alirejeshewa na Waingereza control ya Zanzibar na kuifanya kuwa constitutional monarchy. Kumbuka, baada ya Oman Arab Rule na Zanzibar kuwa British Protectorate, Sultan hakufungasha virago vyake. Aliendelea kutumiwa na Waingereza kama colonial administrator hadi aliporejeshewa control. Sultan hakuwa Mzanzibar. Alikuwa mkoloni. Period!
Kwa hiyo ilipinduliwa serikali ya mkoloni wa uingereza?
 
Paskali haoni kama Sultan alikuwa mkoloni.
Siyo kwa sababu kwa muda ambao Sultani na jamii yake walikaa Zanzibar walichanganyika na watu wa asili ya Zanzibar ndio maana kwa hoja ya Pascal kuwa reconciliation ni muhimu kwani kuna wazanzibari wengi ambao huwezi kuwanyang'anya uzanzibari wao lakini wana asili ya alikotoka Sultani. Mfano uchaguzi wa 2015 matokeo yake, je unaona ufumbuzi wake ni nini? Waendelee kumtumia Jecha?
 
Siyo kwa sababu kwa muda ambao Sultani na jamii yake walikaa Zanzibar walichanganyika na watu wa asili ya Zanzibar ndio maana kwa hoja ya Pascal kuwa reconciliation ni muhimu kwani kuna wazanzibari wengi ambao huwezi kuwanyang'anya uzanzibari wao lakini wana asili ya alikotoka Sultani. Mfano uchaguzi wa 2015 matokeo yake, je unaona ufumbuzi wake ni nini? Waendelee kumtumia Jecha?
Sultan alikuwa mtawala wa kiarabu mwenye hadhi ya kifalme; hakuna Mzanzibar (hata mwenye asili ya kiarabu) aliyekuwa na authority ya kumuweka au kumuondoa Sultan madarakani.

So, ukimng’oa dictator wa kikoloni, kuna sababu gani ya kufanya reconciliation?
 
Wanabodi,
Makala yangu kwenye Nipashe ya Jumaoili ya Leo。

Leo Tarehe 12 January 2025, imedondokea siku ile ile ya Januari 12, 1964, ilikuwa ni siku ya Jumapili. Leo Tanzania inaadhimisha miaka 61 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, wakati Wazanzibari wengi wanashereheka kuyapongeza Mapinduzi hayo (na wengine hadi kuyapa utukufu kwa kuyaita Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, ambalo neno Utukufu, kwa dini mbili kuu, Wakristu na Waislamu, Utukufu ni kwake tuu na wake tuu, Mwenyeenzi Mungu, hivyo kuita kitu kingine chochote kitukufu ni kama kufuru!), kuna Wazanzibari wengine, japo wachache, siku hii ni siku ya kumbukumbu mbaya, kwa kuwapoteza wapendwa wao, kutokana na umwagwaji damu wa Mapinduzi hayo na baada ya Mapinduzi.

Hivyo makala hii ni swali Je Zanzibar Inahitaji Truth & Reconciliation Commission ili Kuponya Makovu ya Mapinduzi, ili Upinzani Ukishinda,Upewe?。Hili ni ombi kwa Sister wangu na Brother wangu,yaani Kaka mtu na Dada Mtu, Can You Please Do The Needfu?。

Hakuna ubishi kabisa, kuwa Mapinduzi ya Zanzibar, yameleta kheri, lakini ni ukweli mchungu pia yameleta shari iliyosababishwa na umwagaji damu mkubwa uliosababisha maumivu makubwa kwa waliopinduliwa ambao wanaishi na makovu ya Mapinduzi hadi leo!。

Kule kwenye mtandao maarufu kuliko mitandao yote ya kijamii nchini Tanzania, Jamii Forums, shamra shamra za kuisubiria siku hii, zilianza siku nying kabla kushamirishwa na Fake News kuwa Sultan mpinduliwa anarejea Zanzibar kufanya ziara rasmi na atahudhuria maadhimisho ya leo. December 28 lilipanda bandiko hili Zanzibar Kumpokea Sultan Jamshid: Ziara ya Kihistoria Baada ya Miaka 60 Uhamishoni

Hilo la Sultani kurejea mimi nikalidaka na kulitolea mapendekezo yangu kumi kwa SMZ.

Ndipo kaka yangu mmoja, kutoka Zanzibar, naomba kumtaja kwa jina moja tuu Kaka Chalz, ni kaka yangu alinipokea RTD, ile mwaka 2000, akatufundisha kazi ya utangazaji, hivyo tunawaheshimu sana kaka zetu hawa, na hata tunapokosea, hawaachi kutupigia simu kuendelea kutuongoza mpaka leo mpaka kesho, Asante Kaka Chale!.

Basi Kaka Chale akaniuliza una uhakika na chanzo chako cha habari kuwa hii ni habari ya kweli?, nikamjibu kwa vile imetangwa na Jamiiforums, kwa jina maarufu JF, ni chombo cha kuaminika, ingekuwa fake, JF inatumia mfumo wa Jamii Check kubaini fake news na kuzifuta, hivyo itakuwa kweli.

Ndipo nikaipitia ile habari kwa mara ya pili kuisoma source, nikakuta ni jamaa yuko Oman!, nikamtafuta kaka yangu mwingine Zanzibar huyu ni Mzee Salim Said Salim, mwandishi wa siku nyingi, tunamuita jina la Mzee SSS, yeye ana nasaba kidogo na ukoo wa Sultan, ukitaka kumtibua SSS, mwambie Mapinduzi Matukufu!. Salim akawapandia kwa simu, Oman, familia ya Sultan wakakanusha kuwa ni fake news!. Asante Mzee SSS!.

Ndipo nikawasiliana na Mkuu Maxence Mello, chapisho langu likaondolewa, na nikabandika chaousho jingine Story ya kurejea kwa Sultan wa Zanzibar ni Fake News! JF Tumelishwa Tango Pori!. Asante Kaka Chale kuniwezesha kuupata ukweli
ila chapisho la msingi halikuondolewa mpaka leo lipo. Nikamrudia Kaka Chale, nikamshukuru kwa angalizo lake, ila nikamwambia baadhi ya yale mapendekezo yangu 10, mengine ni valid, yafanyiwe kazi!. Baada ya hii fake news, jibu la familia ya Sultan alilotoa, ndilo likanijulisha bado kuna watu wana machungu na Mapinduzi yale.

Watu hawa wapoozwe!, waponywe!。 Na Baada ya ujumbe huo mkali kutoka Oman, masikini sultani akaitwa na Mola wake!TANZIA - Aliyekuwa Sultani wa Mwisho Zanzibar, Sultan Sayyid Jamshid Al Said, Afariki Usiku Huu, Omani, usikute ni hii fake news ya jf imemsababishia mtu kifo!。

Huu ni mwaka wa uchaguzi, na hakuna ubishi siasa za Zanzibar, licha ya uwepo wa SUK, bado zinaathiriwa na mzimu wa machozi, jasho na damu, zilizomwaika na kufukiwa bila kufanyiwa hitma, na kuna watu wana makovu ya machungu ya mapinduzi yale,wakija kushika madaraka,kuna watu watakoma!。

Hivyo matokeo ya baadhi ya chaguzi za Zanzibar, ni matokeo yale yale ya ule uchaguzi wa mwaka 1963. Mfano mzuri ni uchaguzi wa mwaka 2015, kuna msemo wa Kiingereza unaosema numba haziongopi!.

Matokeo ya NEC ya uchaguzi wa 2015 kwa Zanzibar, yamethibitisha pasi shaka kuwa uchaguzi wa Zanzibar wa 2015, kama usinge futwa, Maalim Seif Shariff Hamad wa Chama cha Wananchi CUF ndie angelikuwa mshindi wa uchaguzi wa rais wa Zanzibar kwa kutumia kigezo cha matokeo ya uchaguzi wa urais wa JMT, uliosimamiwa na NEC kule Zanzibar ambao uchaguzi haukuwa na dosari, katika uchaguzi huo, mgombea wa UKAWA, Edward Ngoyai Lowassa, alimshinda mgombea wa CCM, Dr. John Pombe Magufuli.

MGOMBEA KURA HALALI ASILIMIA
DR. JOHN POMBE MAGUFULI
194,317 46.5%
EDWARD NGOYAYE LOWASSA 211,033 50.50%
IDADI YA KURA HALALI 417,882
Hii maana yake Zanzibar upinzani unaweza kushinda, sasa kwa vile bado kuna hostilities za machungu ya Mapinduzi, siku upinzania ukishinda Zanzibar, kutaibuka kulipiza kisasi!.

Mwaka 2015 niliandika Iwapo CCM itashindwa Zanzibar, Nini Majaaliwa ya Muungano?
Nilishauri kisha nikashauri Kumuepushia aibu ya Kushindwa, CCM isimsimamishe Dr. Shein hili halikufanyika,na matokeo ndio yale ikabidi watu wafunike kombe。。。

The like scenario naiona Zanzibar 2025,hivyo nashauri
  1. Zanzibar ianzishe truth and reconciliation commission watu waruhusiwe to vent,hivyo to heal machungu ya mapinduzi。
  2. Decemba 10 iwe ni siku ya mapumziko ya uhuru wa Zanzibar,sio lazima iadhimishwe kwa shamra shamra,inaweza kubadili jina ikaitwa Sultan Day。
  3. Neno Matukufu kwenye Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar,lisiendelee kutumika,yaitwe tuu Mapinduzi ya Zanzibar na vibwagizo Mapinduzi Daima, na Tutayalinda kwa gharama yoyote, tuachane nayo ili kuponya wapinga mapinduzi
  4. Falsafa ya 4R za Samia,itumike hadi Zanzibar,mshindi wa kweli wa uchaguzi wa Zanzibar atangazwe,mfano mzuri ni huu Elections 2015 - Imethibitishwa pasi na shaka kuwa ni kweli kabisa, Zanzibar, Maalim Seif na CUF ndio walioshinda na ili kumuondolea posibility ya aibu ya kushindwa,nimetoa ushauri hapa kwenye HII mada。
Hivyo nawashauri Dada yangu Rais Samia, na kaka yangu rais Dr. Mwinyi, kubalini kutibu makovu ya Mapinduzi, ili kuzimaliza siasa za hostilities, ikitokea upinzani umeshinda Zanzibar, hakuna haja kufunika kombe tena mwanaharamu apite, iwe ni kupokezana kwa amani na upendo. Miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar, Tuyaenzi kwa 4R za Rais Samia?, JMT Tuitendee Haki Zanzibar?, Tuwatendee Haki Wazanzibari? Mshindi Halali Apewe?

Namalizia kwa lile swali la msingi la uzi huu Je Zanzibar Inahitaji Truth & Reconciliation Comm。Kuponya Makovu ya Mapinduzi, ili Upinzani Ukishinda,Upewe?。Sis & Bro,Can You Please Do The Needfu?。

Heri ya Mapinduzi.

Paskali.
Kumbuka kwenye Moja ya vitu tunavyo jihusia sisi Watanzania Kwa ujumla wetu na kumbumbusha mtu anae elekea njia isiyo sahihi: nikwamba
Vita sio kitu kizuri
Mshindi na mshidwa lazima watapoteza vijana wao
Mifano mingi tumeiishi
"Mlengwa mkuu WA vita ni mtu"
Taifa limeamua kusherehekea ushindi japo damu ilitumwagika
tunao mashujaa wakuwaenzi
 
Sultan alikuwa mtawala wa kiarabu mwenye hadhi ya kifalme; hakuna Mzanzibar (hata mwenye asili ya kiarabu) aliyekuwa na authority ya kumuweka au kumuondoa Sultan madarakani.

So, ukimng’oa dictator wa kikoloni, kuna sababu gani ya kufanya reconciliation?
Kwa nini Jecha alihusika kufuta uchaguzi baada ya CUF kushinda? Wakoloni walikuja kupiga kura kuwakataa wanamapinduzi?
 
Kwa nini Jecha alihusika kufuta uchaguzi baada ya CUF kushinda? Wakoloni walikuja kupiga kura kuwakataa wanamapinduzi?
Hata bara hilo linaweza kutokea. In fact, zipo sehemu nyingi wapinzani wamewahi kuenguliwa kwa technicalities ambazo hazina mashiko!
 
Hata bara hilo linaweza kutokea. In fact, zipo sehemu nyingi wapinzani wamewahi kuenguliwa kwa technicalities ambazo hazina mashiko!
Swala siyo kuenguliwa, majority ya wapiga kura wanaokipigia kura ACT, CUF na kabla ya hapo umma party wana asili moja na inajulikana, mostly wapemba na wenye asili ya kiarabu. Au utawanyang'anya uzanzibari wao?
 
Kaka Paskali,
Ninachokishangaa sana kwenye reconciliation za hapa kwetu TZ;
Mkuu Ngali, Ngalikihinja, kwanza asante kutembelea uzi huu, maswali yako ni maswali ya msingi sana.
1. Hakusemwagwi watu wanatakiwa au wana-reconcile kwenye nini
Ni kweli hili halisemwi, kwenye yale Mapinduzi na baada ya Mapinduzi, kuna damu zilimwagika, wenye fursa na uwezo walikimbia Zanzibar akiwemo Sultan na familia yake ya watu 46. Wasio na uwezo walibaki Zanzibar na mpaka leo wanaishi na makovu ya mapinduzi!.

Kuna mambo mabaya maovu yalitokea baada ya mapinduzi miongoni mwake ni yale yaliyosababisha kifo cha Karume, yasemwe wazi watu wa vent, yaishe!.
2. Hakusemwagwi nani na nani wanatakiwa wali-reconcile
Waliopindua wa reconcile na waliopinduliwa!.
3. Hukusemwagwi wamekoseana nini hao wanaotakiwa ku-reconcile
Kwenye truth and reconciliation, maovu yaliyofanywa na mapinduzi yanatajwa, waliopindua wanasema lengo lilikuwa kupindua na sii kumwaga damu, wanaomba msamaha kwa damu zilizomwagika, wanawafuta jasho wana mapinduzi walio sahaulika, wanawafuta machozi walio lia. Wanasoma kisomo cha wote, they bury the hatchet and start afresh.
Reconciliation zetu zipo very blind..!!
Its true, kwasababu Kiafrika hatuna utamaduni wa ku reconcile, mimi mwenyewe yalinikuta.

Nilioa nikiwa young at 25 wife 21, classmate TSJ, from college straight altareni!.

Mwenzangu akapata scholaship ya 4 years US, nikamsindikiza, we have our two kids ni US subjects, mimi nikarejea Bongo, si unajua tena Usukuma, Uafrika, Uswahili, si nika jiachia!.
Niliporudi US nikawa mkweli kwa wife!, kumbe kuwa mkweli sana kosa!. Wife mpaka leo kagomea US, hivyo mimi ikanibidi kuendeleza Usukuma na Auafrika, ila kukitokea zile ajali za magoli ya mipira ya kona na mechi za ugenini, unakomaa na kukausha kau kau.

Huyu mtu ndie mgombea urais wa Zanzibar 2025 kupitia ACT, angalia hapa nilisema nini kuhusu mtu huyu. Dkt. Shein Mfute Kazi Haraka, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Kabla Hajamwaga Sumu Hii

Kisha angalia hapa nilishauri nini Ushauri wa Bure kwa Dkt. Hussein Mwinyi: Mfute Kazi Haraka Othman Masoud Kabla Hajaendelea Kueneza Sumu

Msikize anasema nini kuhusu muungano Kuhusu Muungano, Makamo wa Kwanza wa Zanzibar, Adai ni Zanzibar Pekee iliyopoteza Sovereignty, Je Yuko Sahihi?
P
 
Swala siyo kuenguliwa, majority ya wapiga kura wanaokipigia kura ACT, CUF na kabla ya hapo umma party wana asili moja na inajulikana, mostly wapemba na wenye asili ya kiarabu. Au utawanyang'anya uzanzibari wao?
Hawapokwi ushindi kwa sababu wana asili ya kiarabu bali ni kwa sababu wao ni wapinzani. Hata bara CCM ikishindwa uchaguzi, itafanya yale yale inayofanya Zanzibar. Kwa mtazamo wangu, solution ya issue ya Zanzibar sio kufanya reconciliation ya mapinduzi bali ni kufuata sheria za uchaguzi. Chaguzi lazima ziwe free and fair.
 
Mwenzangu akapata scholaship ya 4 years US, nikamsindikiza, we have our two kids ni US subjects, mimi nikarejea Bongo, si unajua tena Usukuma, Uafrika, Uswahili, si nika jiachia!.
Niliporudi US nikawa mkweli kwa wife!, kumbe kuwa mkweli sana kosa!. Wife mpaka leo kagomea US, hivyo mimi ikanibidi kuendeleza Usukuma na Auafrika, ila kukitokea zile ajali za magoli ya mipira ya kona na mechi za ugenini, unakomaa na kukausha kau kau.
Teh teh teh 😃 😃 😃 kwa hiyo na wewe unahitaji 'reconciliation' Ili mkeo arejee kwako ?
 
Back
Top Bottom