Jeff Lea: Simba hamfiki mbali kwa ulinzi ule

Jeff Lea: Simba hamfiki mbali kwa ulinzi ule

VUMBI LA CONGO LIMEKUTANA NA ALKASUSU.[emoji23][emoji23][emoji23]
Mungu ibariki Tanzania Mungu ibariki simba
 
Akiongea leo asubuhi katika kipindi cha michezo cha Efm mchambuzi nguli wa mpira Jeff Lea asema kwa safu ile ya ulinzi wa Simba dhidi ya Dodoma Jiji jana, mabeki wao wameonesha udhaifu mkubwa sana hivyo kama watakutana na timu yenye washambuliaji wazuri basi hawatafiki mbali katika ligi ya mabingwa Afrika.

Mimi namuunga mkono kwa 100% kwa mbaaaali naona mtu akienda kuchezea goli 5 kwa kila mechi ya ugenini.

Msijenge chuki, fanyieni kazi mapungufu yenu Simba
Wachambuzi au jazba zetu

Sent from my Nokia 3.2 using JamiiForums mobile app
 
Akiongea leo asubuhi katika kipindi cha michezo cha Efm mchambuzi nguli wa mpira Jeff Lea asema kwa safu ile ya ulinzi wa Simba dhidi ya Dodoma Jiji jana, mabeki wao wameonesha udhaifu mkubwa sana hivyo kama watakutana na timu yenye washambuliaji wazuri basi hawatafiki mbali katika ligi ya mabingwa Afrika.

Mimi namuunga mkono kwa 100% kwa mbaaaali naona mtu akienda kuchezea goli 5 kwa kila mechi ya ugenini.

Msijenge chuki, fanyieni kazi mapungufu yenu Simba
Jeff lea ndo nani?......Eti nguli wa uchambuzi
 
Ila wachambuzi wa bongo nyoso sana. Kunawakati nlkua nafuatilia tabiri za watu wa clouds na kuzibetia hasahasa shafii dauda, kwakwel nilichana pesa vbaya mno. Badae nikawa naenda kinyume naye, kila akiitabiri mechi nabetia kinyume chake, huwezi amini Kati ya mechi 11 alzotabiri mm nkabetia kinyume chake mechi saba nilikula pesa na mechi nne tu ndio nilikosa.
 
Hata ukimpa pesa harudi hapa! katelekeza uzi wake mwenyewe!! Ngoja nijaribu kumwita! Renzo njoo kwenye uzi wako usome hapa:
Dhidi ya Mbabane Dar kabla ya mechi
Leo mnapigwa hapa hapa nyumbani
Baada ya mechi
Simba 4
Mbabane 1
Mnaenda kufa kwao

Marudiano kwao
Mbabane 0
Simba 4
Mmekutana na vibonde hapo ndio mwisho wenu

Dhidi ya Nkana Dar
Mlikufa 2-1 kwao leo mnakufa tena safari ishaisha hiyo
Baada ya mechi
Simba 3
Nkana 1
Kimyaaaaaa 🤣

Makundi
Al Ahly
Simba
As Vita
Js Saoura
Waarabu wawili na m-Congo mmoja hapo Simba anashika mkia na yule jamaa ndio akapigilia msumari kabisa kwa kutuita Under Dog wa kundi

Dar Simba dhidi ya Js Saoura
Waarabu wamekuja kuwapiga hapa hapa nymbn
Baada ya mechi
Simba 3
Saoura 0
Hawa sio waarabu ni wapemba ngoja waje Ahly 🤣

Simba dhidi ya Ahly Dar (kabla)
Sasa leo ndio wamekuja waarabu wenyewe Taifa linaingia ktk aibu nyingine Cairo hamsa na leo hamsa tena
Ramadan Subhi wamemchukua kwa mkopo wa paun billion 10 thamani yake kikosi kizima cha Simba hakifikii thamani hiyo
Baada ya mechi
Simba 1
Ahly 0
Mmebahatisha tu lkn hampiti shughuli mtaiona ktk mechi ya mwisho dhidi ya As Vita hamsa zingine hapa hapa

Simba dhidi ya As Vita Dar
Leo sasa ndio mwisho wa safari mnakufa tena nyingi
Baada ya mechi
Simba 2
As Vita 1
Hamna lolote nyie mnawapulizia dawa wapinzani ndio mnashinda 🤣
Yani kutoa hongera kwao imekua ngumu sana wanageuka vinyonga kila leo kwa kauli zao

Dhidi ya Plateau (Nigeria)
Kabla ya mechi leo Taifa linaingia kwenye aibu kubwa mnaenda kufa nyingi jamaa kila game wanashinda tano tano Enyimba kafa 5 na wengine kibao ni hamsa au 4G
Baada ya mechi
Plateau 0
Simba 1
Wanakuja kupindua matokeo Dar

Leo sasa mnakufa hapa hapa (kabla)
Baada ya mechi Dar
Simba 0
Plateau 0
Mmeshindwa kuwafunga kwenu hata hao wabovu ngoja muone Platinum

Dhidi ya Platinum Bulawayo,Zimbabwe.
Mnakufa nyingi leo
Platinum 1
Simba 0
Chikwende,Chikwende..na kelele kibao na huo ndio mwisho wa safari mnakufa tena Dar

Mechi ya marudiano Dar
Kabla ya mechi
Chikwende leo atakuepo tena
Kwa beki zenu hizo wazee Wawa na Onyango hapo Chikwende na wenzake wanakuja kufanya mauaji tena
Baada ya mechi
Simba 4
Platinum 1
Simba hawashindi mpk mapaka 🤣
Hongera ni ngumu sana kutoa na maneno kila siku yanabadilika

Makundi
Al Ahly
Simba
As Vita
El Merreck
Daaah aibu imerudi tena kwa Taifa zile hamsa hamsa zinarudi tena

As Vita dhidi ya Simba (Congo)
Leo ndio zile hamsa zinajirudia aibu kwa Taifa kila baada ya dkk kadhaa goli,As Vita hatari sana kwao,mara watapakiwa mkongo n.k
Baada ya mechi
As Vita 0
Simba 1
Sasa hivi As Vita hamna timu wameuza sana wachezaji wao 🤣

Hivi ndivyo ambavyo kila siku maneno yanabadilika wanakua vinyonga na wepesi kukana maneno yao ya awali

Simba mnawatesa sana watani mana sio wapinzani,kila wakichagua waume nyie mnaua wanatafuta mwingine mnaua wanapata sana shida hawa wajane

Na nyie wajane fc mjifunze kutoa hongera hata mara moja moja mtabadilisha mabwana mpk lini? mafanikio ya Simba ni mafanikio ya Taifa pia sbb tunawabeba nyie mwende kutembea na kurudi lkn hamna shukrani aibu yenu wenyewe

Tuliwakera sana 2018/19
Msimu huu 2020/21 kero zitaongezeka sbb hatuna nyumbani wala ugenini pagumu kwetu ni Cairo tu na tunauhakika wa kuvuka na kucheza hatua ijayo

Kila siku vitu vizuri tunafanya sisi,wanaume ni sisi,watu wa historia nzuri ni sisi,watu wa ushindi ni sisi,watu wa kulitangaza taifa ni sisi,watu wa kuleta heshima kwa Taifa ni sisi ila watu wa kuharibu ni nyie,watu wa kutia aibu ni nyie,watu wa kushindwa ni nyie,watu wa kuumia (maumivu) kila siku ni nyie,watu wa wivu ni nyinyi yani mnateseka sana..
Kabla ya mechi: Simba kwa difensi hii haifiki mbali!! Baada ya mechi: Simba 1 Vita 0, Renzo & company wanakimbia uzi wao wenyewe!! Poleni, wahenga walisema wivu mbaya!!
Hivi ni kweli Renzo kwa akili yako, kufikia kucheza hatua ya makundi klabu bingwa ya Afrika hapo ni kuishia karibu?? Hivi huko shuleni mlisomea ujinga au? Ukweli ni kwamba Simba imeshafika mbali tayari kwa beki ile ile unayoidharau kiwivu wivu!

Poleni sana

Simba Nguvu Moja


TUNAWAKERA EEE!!
Kimeumana leo mkuu, Sasa hivi simba tunawataka Bayern kwanza😂😂
 
Kama Leo George amechambua kiufundi hasa yule jamaa anaijua kazi yake halafu hana upendeleo.
Wachambuzi Tz ni George Ambangile na Ali kamwe hao wengine huwa wanajadili matukio yanayotokea
 
Akiongea leo asubuhi katika kipindi cha michezo cha Efm mchambuzi nguli wa mpira Jeff Lea asema kwa safu ile ya ulinzi wa Simba dhidi ya Dodoma Jiji jana, mabeki wao wameonesha udhaifu mkubwa sana hivyo kama watakutana na timu yenye washambuliaji wazuri basi hawatafiki mbali katika ligi ya mabingwa Afrika.

Mimi namuunga mkono kwa 100% kwa mbaaaali naona mtu akienda kuchezea goli 5 kwa kila mechi ya ugenini.

Msijenge chuki, fanyieni kazi mapungufu yenu Simba
Wanapoambiwa wasiwe watabili au kuwa na akiba ya maneno ona ss

Sent from my Nokia 3.2 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom