Jenerali Mabeyo, unayasikia yasemwayo na makomandoo wetu mahakamani kwenye kesi ya Mbowe?

Jenerali Mabeyo, unayasikia yasemwayo na makomandoo wetu mahakamani kwenye kesi ya Mbowe?

Kuna jamaa mtaani kwetu yupo kwenye miaka 48 anasema yeye kastaafu mwaka juzi,je nae atakuwa amefukuzwa ama niamini tu kastaafu kama alivyoniambia
Amekwambia kastaafu halafu ww unasema amefukuzwa
 
Hawa hawakuwa Makomandoo wa JWTZ wakati wanakamatwa.

Walikwishafukuzwa jeshini kwa utovu wa nidhamu.

Wakaamua kuwa Makomandoo wa mbowe na hatujui alitaka kuwatumia kwa kazi ipi.

Subirini mahakama iamuwe haki. Acheni kuwewseka ovyo mitandaoni .
Mm nakwambia hawa Jamaa kukikuwa na siri nzito sana nyuma yao.
 
Inaelekea JWTZ inathamini wanajeshi wakiwa na afya njema lakini pindi wakiumia au kupata maradhi wakiwa kazini inawatelekeza!

Amiri Jeshi Mkuu anapaswa kuangalia upya jambo hili kwani halina afya kwa ustawi wa jeshi letu.
ndo vijana wenzetu waelewe bora kukomaa tu mtaani na kazi zetu za kijungu jiko kuliko kukimbilia izo kazi unatimika kuumiza watanzania wenzako halafu ndo' kama tunayoyaona maana wakina adamoo na lingw'enya wote watoto wa wapiga kura yani wota kajamba nani unadhan mtoto wa mahita angetendewa ayo.
 
It's painful if that is what they went through and of which as per rules of law shouldn't have happened at all.
 
Mtani wangu na mkuu wangu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Jenerali Venance Mabeyo, nakusalimu na kukutakia kazi njema. Nakuuliza tu kizalendo: unayasikia au kuyasoma maneno yasemwayo na makomandoo wetu walio washtakiwa na mashahidi kwenye kesi ya ugaidi inayomkabili Freeman Mbowe na wenzake? Hakika, makomandoo hawa (ingawa kwasasa wote hawako tena jeshini/kazini) wanazungumza vya kushangaza na kuogofya.

Kuanzia Kusekwa/Adamoo, Ling'wenya hadi Mhina wa jana wamezungumzia kukamatwa kiholela; kuteswa; kutwezwa; kudhulumiwa na madhila mengine. Hawa walifunzwa kwa fedha zetu ili watulinde. Hawa walifunzwa kwa fedha zetu ili watupiganie. Hawa walifunzwa kwa fedha zetu ili watutetee. Hawa walifunzwa kwa fedha zetu ili waendeleze uzalendo na utii wao kwa nchi yetu. Kwanini wamepitishwa kwenye njia waisemayo?

Makomandoo wetu wamelalamika; wamelia; lakini hawana la kufanya hadi mwisho wa kesi. Wenzao wa 92 KJ na kwingineko wanajifunza nini? Wanapata ujumbe gani? Wanawaza nini? Wanawataja wenzao wengine kukamatwa na kuteswa pia. Wako wapi wale waliotajwa? Kazini? Hai? Ndugu yangu Mabeyo, utumishi wako umetukuka. Sina shaka nawe wala na jeshi unaloliongoza. Makomandoo hawa, kwa mujibu wao, waliathirika vitani. Wapewe haki zao. Wakumbukwe. Watendewe yaliyo mema.

Unaandika lakini mtani wangu Jenerali Mabeyo? Nitakuja pia nyumbani na ofisini kusisitiza hili

Wasiojulikana sasa wamejulikana?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kilosa, Morogoro)
Yaani ulichoandika hata hakieleweki.
 
Kwenye mkutano wa JWTZ na vyombo vya habari walisema jeshi haliajiri lakini linaandikisha,kama hujaajiriwa na umeandikishwa tu ndo chanzo cha kutelekezwa.
lakini jwtz kutelekeza komando haijakaa sawa.
pia komandoo kukamatwa/kutekwa kama kuku kuna siku hao polisi watapata wakinachokitafta,
hebu tujiulize kama makomandoo wote wako kama akina Adamoo au Bwile?
je walioko huko makambini wanachuliaje wenzao kuteswa tena na polisi?
au na wao kesho wakiwa mtaani yatawapata ya wenzao?
maswali mengi kuliko majibu
Na kinachoshangaza Bwire alikuwepo sana hapo O bay police zamani na ukiingia anga zake utakiona cha moto.
Leo anateswa yeye.
Maisha haya
 
Hawa hawakuwa Makomandoo wa JWTZ wakati wanakamatwa.

Walikwishafukuzwa jeshini kwa utovu wa nidhamu.

Wakaamua kuwa Makomandoo wa mbowe na hatujui alitaka kuwatumia kwa kazi ipi.

Subirini mahakama iamuwe haki. Acheni kuwewseka ovyo mitandaoni .

kujiajiiri kama board guard na kuwa Jambazi kipi bora au ilitakiwa wao na familia zao waFe njaaaa ; mbona yule ligumi enzi zake alikua analindwa na kama hao wannne
Mimi nafikiri kama wanapata kazi halali waachwe
Augustine Mrema enzi zake akiwa kwenye chati alikua analindwa na Capt Mohammed Posh ( ex CDO) na ndiye aliyemsaidia asife pale RaskaZone Tanga Baada ya taaa kuzimwa alimvua Mrema kibandiko akamvika mzeee mmoja alafu akamicha chini ya Meza yule mzeee walimrusha dirishani wakidhani mrema
 
Kama hao makomando ni magaidi Basi hata JWTZ nao ni magaidi.
 
So sadd brow

Kaz ngumu then unafanyiw mateso. Hii nchi kuna hatua itakuja kusimama.
Niliwaahi andika humu, ila shida ni kutafutana.


Mimi Kaka yangu ( mtoto wa mama mkubwa)

Wakiwa pale kambi ya ukomandoo Morogoro...

Posho zao wakawa hawapewi, wakaamua kuja Dar makao makuu JWTZ kulalamikia.


maajabu, wakapewa Kesi za Uhaini, uhujum, uasi, uporaji wa Mali za Raia.


Walikua vijana 60 wa Mafunzo ya ukomando

30 wakasamehewa ...30 Wakafungwa jela mwaka 2015 akiwemo Kaka yangu huyo.


Waziri Mkuu anajua, Mwinyi anajua, Mwanasheria Mkuu wa wakat huo anajua,Mkuu wa Majeshi alopita anajua ..maana suala lao lilijitokeza 2013 .


WAKAFUKUZWA KAZI BILA KUPEWA BARUA YA KUACHISHWA KAZI, BILA KUPEWA MAFAO YAO, IKUMBUKE TOKA HUO MWAKA 2013 MPAKA 2015 ,MISHAHARA YAO ILISIMAMISHWA.


Walikua kuachiwa mwaka 2017 kwa msamaha

mpaka naongea hii Leo, Hawa vijana wamejitahidi kutafuta haki zao sanaaa ,wametumia wanasheria wapiiii..suala lao linaminywa chini chini.






KWA sasa wamebaki vijana 29. ..baada ya mmoja maisha kumchanganya, akaungana kwenye ujambazi,... Alipigwa risasi.

Sent from my vivo 2015 using JamiiForums mobile app
 
Maana yake nn Mabeyo akawe jaji au una mananisha nn bwasheee?
We Taga, hebu zinduka usijifanye hamnazo;
Jaji ndo anawatesa?
Jaji ndo aliwafukuza kazi?
Jaji ndo mkuu wa kikosi kule ngerengere?

Gen. Mabeyo anaekezwa kwa sbb yy ndiye overall incharge na commander in chief ambaye anatakiwa kujua wapi wanajeshi wake wanapitia.
 
JWTZ hawana sera ya kuwalinda watu ambao wanakuwa trained kwa kiwango cha Ukomandoo, hawa jamaa walitelekezwa na wamepitia wakati mgumu mno.
Jeshi kwa ujumla halina business na ww ukishakuwa discharged from service.
Hawatelekezwa ila ni taratib za jeshi
 
Ndio kuna Sheria, hizo Sheria zao hazijali Haki ??? Yaan kumfukuza MTU bila kumpa barua??? Wala Mafao yake aloyatumikia muda wote huo!!!?.
Ukifukuzwa kaz hakuna mafao. Kwa sheria za nchi hii. Mafao wanapata walio staafishwa period
 
Inaelekea JWTZ inathamini wanajeshi wakiwa na afya njema lakini pindi wakiumia au kupata maradhi wakiwa kazini inawatelekeza!

Amiri Jeshi Mkuu anapaswa kuangalia upya jambo hili kwani halina afya kwa ustawi wa jeshi letu.
Majeshi yote yako hivyo. Ukipata shida ya kiafya ambayo wanaona itakuziia kuweza kutekeleza kaz za kijeshi wana ku discharge. Au unapangiwa idara zisizo na pyhsical activity nzito
 
Back
Top Bottom