Jenerali Ulimwengu: Inanichosha kusikia sifa za Rais kila dakika

Jenerali Ulimwengu: Inanichosha kusikia sifa za Rais kila dakika

Ifikie wakati tuache kuona kila anachofanya Raisi ni msaada kwetu na si majukumu yake.

Hizi sifa za uongo zimekuwa nyingi mpaka kuondosha mantiki ya uhalisia wa utendaji wake.

Alichosema Jenerali Ulimwengu

"Mimi inanichosha kusikia sifa za rais kila dakika. Rais ni mtu mwema nadhani. Lakini sio lazima tukae tunamsifu! Tunamsifu!. Maana yake Mwisho kama hauna critical thinking juu ya mkuu wako na kila siku ni kumsifu. Naanza kuwa na shaka kwamba hata akikosea utamsifu tu. Na waswahili wanasema kufanya hivyo ni kumpaka mafuta kwa mgongo wa chupa au wanavyosema waswahili unamcheza shere"
Tatizo ni vyombo vya habari Ili wakurushe hewani na kusikika ni lazima umsifu Rais.Ukizumgumza mawazo Yako tofauti na Rais hata kama ni mazuri,hutasikika na mtu,wanawaogopa wajiri wao ambao pia wanaogopa serikali kufungia vyombo vyao.Ni mfumo
 
Hakuna namna mzee, itabidi uzoee tu kizazi kimebadilika, ukosefu wa ajira umewafanya wengi kuwa watumwa wa kifikra, hata kama wana elimu zao vichwani.

Siku hizi uchawa ndio habari ya mjini, machawa wanaishi vizuri mjini zaidi ya waajiriwa wa sehemu mbalimbali.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Wanaochosha kusikiliZa ni hawa wenye vyeo. Mawaziri, RCs nk na wateulewote. Ukweli hata mimi nakerwa sana
 
Ifikie wakati tuache kuona kila anachofanya Raisi ni msaada kwetu na si majukumu yake.

Hizi sifa za uongo zimekuwa nyingi mpaka kuondosha mantiki ya uhalisia wa utendaji wake.

Alichosema Jenerali Ulimwengu

"Mimi inanichosha kusikia sifa za rais kila dakika. Rais ni mtu mwema nadhani. Lakini sio lazima tukae tunamsifu! Tunamsifu!. Maana yake Mwisho kama hauna critical thinking juu ya mkuu wako na kila siku ni kumsifu. Naanza kuwa na shaka kwamba hata akikosea utamsifu tu. Na waswahili wanasema kufanya hivyo ni kumpaka mafuta kwa mgongo wa chupa au wanavyosema waswahili unamcheza shere"
Anachoka yeye kama nani??
 
Ifikie wakati tuache kuona kila anachofanya Raisi ni msaada kwetu na si majukumu yake.

Hizi sifa za uongo zimekuwa nyingi mpaka kuondosha mantiki ya uhalisia wa utendaji wake.

Alichosema Jenerali Ulimwengu

"Mimi inanichosha kusikia sifa za rais kila dakika. Rais ni mtu mwema nadhani. Lakini sio lazima tukae tunamsifu! Tunamsifu!. Maana yake Mwisho kama hauna critical thinking juu ya mkuu wako na kila siku ni kumsifu. Naanza kuwa na shaka kwamba hata akikosea utamsifu tu. Na waswahili wanasema kufanya hivyo ni kumpaka mafuta kwa mgongo wa chupa au wanavyosema waswahili unamcheza shere"
akajambe
 
Hadi kusema Rais kamtoa jalalani, yaani mtu alikuwa lecturer chuo kikuu, kumbe lile lilikuwa jalala. Watu toka JPM waliamua kujizima network kabisa, na viongozi wanabariki ujinga sasa imekuwa trend, kila mtu anasifia tu.
Yaani ni aibu kwa Taifa

Kuna Kiongozi mmoja alinambia kuwa bila kufanya hivyo unaweza usiwepo kwenye mkeka wa Uteuzi.

Bora kubakia Mkulima wa kawaida kama nilivyo Mimi huku ukitunza heshima uliyonayo na maisha yanasonga 💪
 
Hata rais mwenyewe ana shida.

Kama mnakumbuka magufuli alimwambia kangi”unanitaja taja sana kumbe unafanya madudu”
Hawa UVCCM sio wajinga kama tunavyofikiri,ni watu ambao toka walipoamua kuingia huko ccm,walidhamilia kuwa wapigaji kwa njia yoyote itakayowezekana.
 
Kwa kweli inashangaza kila mbunge, kila mtendaji mkuu wa idara za serikali akisimama tu lazima amsifie rais kuwa ametoa fedha kujenga mradi fulani ashukuriwe. Mara rais katoa fedha za kujenga kituo cha afya, madarasa, barabara na mkadarasi yuko kazini. Mabango yamejaa kila sehemu rais atanapofanya ziara mikoani na wilaya, mwendo ni kumsifia tu kuwa katoa fedha za kujenga miradi ya wananchi kana kwamba si wajibu wake kufanya hivyo. Mpaka wenyeviti wa vijiji wanaimba mapambio ya kumsifia kwa kutoa fedha za kujenga miradi ya maji na vituo vya afya. Duh! hadi vijiweni wameanza kusifia rais kafanya vijiwe vyao mambo yawe mazuri
 
Muasisi wa huu upuuzi ni dhalimu ili kuhadaa umma kuwa anakubalika sana. Na kwakuwa watu wanapata ulaji kupitia hayo mapambio, hakuna namna upuuzi huo utaisha. Hadi aje kiongozi mwenye akili nzuri, au atakayeingia madarakani kwa uchaguzi halali.
True👍
 
Ifikie wakati tuache kuona kila anachofanya Raisi ni msaada kwetu na si majukumu yake.

Hizi sifa za uongo zimekuwa nyingi mpaka kuondosha mantiki ya uhalisia wa utendaji wake.

Alichosema Jenerali Ulimwengu

"Mimi inanichosha kusikia sifa za rais kila dakika. Rais ni mtu mwema nadhani. Lakini sio lazima tukae tunamsifu! Tunamsifu!. Maana yake Mwisho kama hauna critical thinking juu ya mkuu wako na kila siku ni kumsifu. Naanza kuwa na shaka kwamba hata akikosea utamsifu tu. Na waswahili wanasema kufanya hivyo ni kumpaka mafuta kwa mgongo wa chupa au wanavyosema waswahili unamcheza shere"
Mimi sijawahi kusikia Hapo zamani haya maneno ya sifa zilizopitiliza !!
Mpaka sasa sijaelewa impact yake ni nini !!
 
Kusema kweli inachosha sana,wanasiasa hawawezi kujenga hoja bila kutaja neo Rais........mi taarifa ya habari kwenye local channels niliacha kuangalia tangu enzi za JPM, maana DC,RC,MAWAZIRI,DAS,RAS,WAKURUGENZI etc wote wakiongea lazima neno Rais litajwe
Mpaka kero, nafikiri ni walaka unapita usipomtaja kwenye maelezo yako unaweza kuchukuliwa hatua, ila yule wa elimu sioni akimtaja hovyohovyo rais.
 
Machawa wana maisha mazuri kuliko ma profesa, Machawa wapo kwenye msafara wa rais. Na rais mwenyewe alishasema chawa wake waheshimiwe. Bila uchawa hapa mjini hutoboi.

Kibaya zaid uchawa umesambaa zaid mpaka kwenye level ya kaya, Wilayan, kwenye halmashauri, Kwenye vituo vya afya, Manes wanakuwa machawa wa wabunge, sijui meya, mkurugenzi nk, kwenye makampuni hivyo hivyo.

Hii issue ya uchawa imesababisha damage kubwa sana kwenye maadili ya vijana na ile spirit tuliyojengewa na Magu, ile ya Kupambana, Kuchapa kazi, kusukuma mambo ili yaende. Awamu hii, tunafundishwa kuwa machawa. Uchawa ndo habari ya mjini, lakin uchawa una ajiri watu wangapi, ni uharibifu usio wa kawaida wa jamii.
Mkuu una akili kama za Jiwe, pole
 
Back
Top Bottom