Jenerali Ulimwengu: Kuna Mtanzania alitufanya Mazuzu

Jenerali Ulimwengu: Kuna Mtanzania alitufanya Mazuzu

Ukisema shida ni ya wananchi, mm nakukatalia kwasababu Dar es salaam tu ambayo ndio kioo cha Tanzania, idadi kubwa hawajui hata umuhim wa kupiga kula je,hao wa vijijini hali ikoje?
Sijajua unanipinga ama unakubaliana na Mimi.
Sasa ikiwa Idadi kubwa wa wakaazi wa Dar hawapigi kura then why tuseme tatizo ni katiba na si watu?.
Tanzania ni nchi inayoweza ongozwa na yoyote yule awe Mweu, Mwerevu , Malaika ama Shetan. Ni yeye mwenyewe Rais akiamua kufanya atakavyo.
 
Sukuma gang, buana... Yaani tunasoma akina Hitler, Carl Peters... na wengineo wa 1800, 1900 na kitu. Leo eti hamtaki dikteta aliye kufa 17 march 2021 asisemwe?! Hivi mna akili kweli? Kuna somo pia linaitwa historia. Wamesoma akina Nyerere na wengine. Unasemaje - lifutwe kwenye mashule?
Akili zisizo angalia kwa mapana. Umesoma vitabu, ulishawahi kwenda Ujerumani ukakuta majungu ya Hitler kama hapa? JPM hajaandikiwa kitabu. Andikeni kitabu ijulikane wazi. Na inaonesha huna exposure, kwa taaria yako Hitler na watu wanatukuza itikadi yake hadi leo, nenda Ulaya hata Marekani.

Usioanishe historia za Carl Peters na majungu. Nadhani huna uelewa mzuri kujua nini nimeongelea. Na katika waandishi wazuri wanapoandika kitabu uangalia pande mbili. Za mazuri aloanya mtu na mabaya. Si kumtangaza mtu kwa mabaya tu!
Hilo neno sukuma gang kwangu naona kawaida hata ukiita mara kumi sibabaiki, kwa sababu akili upi uwaza mashambulizi na si uchambuzi wa kina.

Na inaonesha ujaelewa kabisa nilichokiongelea unarukia rukia tu. Sikulaumu ila uelewa wako ndo ulipoishia.
 
Rafiki, ujanisoma vizuri.
Nimesema[HATA] tukichukua katiba ya marekani, sijalinganisha katiba ya Marekani na Tanzania.
Katiba haiwezi simama bila watu wanaojitambua.
Sidhani kama unatutendea haki wananchi. Kilichopo na kinachofanywa na Rais wa Tanzania ni kutumia katiba mbovu tuliyonayo kututia woga wa kutufungulia mashtaka ya kutunga, kutufunga jela pasipo na haki, kutuua na maovu mengi.

Tukiwa na katiba ambayo Rais anafahamu akifanya maovu atachukuliwa hatua za kisheria bila kuchelewa atatenda haki na watu watakuwa na ujasiri wa kumwambia ukweli!
 
Kama una mazuri yake umekatazwa kuyasema? Anzisha uzi wa mazuri ya mungu-mtu wako. Usifunge watu midomo waliopitia mabaya ya yule dikteta kuyasema. Hili ni jukwaa huru. Wee ni nani mpaka ufunge watu midomo? Hata Muumbaji wetu ametupa uhuru wa kuchagua kati yake na shetani.

Mzee Mwinyi alisema maisha ni hadithi. Jiandikie hadithi yako nzuri wakati ukiwa hai. Kama ulikuwa mtu wa kutukana, kuua, mwenye hasira, mwonevu, mvunja katiba, mwongo... km huyo kipenzi chako ndio hadithi yako hiyo uliyojiandikia. Haiwezi kubadilika baada ya kuzikwa.

Unataka umlazimishe Lissu aliyepigwa risasi kwa amri ya yule jambazi amsifu? Hautafanikiwa. Kama una sifa zake nzuri, anzisha uzi. Watu tuliathirika na udikteta wake hatutaacha kusema. Kama kujinyonga, jinyonge.

Eti sina exposure! Jifariji tu. Ujerumani nimesoma (MSc Heidelberg) na Kijerumani naongea, angalau cha kuombea maji. Hakuna watu wanamsifia Hitler Ujerumani ya leo. Kuna kundi dogo sana la watu wanaitwa neo-nazis ndio wanakubali sera zake. Ni dogo kama mlivyo Sukuma gang kwa sasa hapa Tanzania.

Yaani unataka nimsome kwenye kitabu dikteta ambaye nimeishi maisha yake nikiwa mtu mzima? Sihitaji kusoma vifo vya akina Mawazo, Azory na wengineo kwenye vitabu. Sihitaji kusoma kuenguliwa kwa wagombea kwenye chaguzi eti kwenye vitabu ama kura za kwenye mabegi za 2020 kwenye vitabu. Ni mambo niliyoshuhudia.

Nadhani umepata elimu ya kutosha bure.
Akili zisizo angalia kwa mapana. Umesoma vitabu, ulishawahi kwenda Ujerumani ukakuta majungu ya Hitler kama hapa? JPM hajaandikiwa kitabu. Andikeni kitabu ijulikane wazi. Na inaonesha huna exposure, kwa taaria yako Hitler na watu wanatukuza itikadi yake hadi leo, nenda Ulaya hata Marekani.
Usioanishe historia za Carl Peters na majungu. Nadhani huna uelewa mzuri kujua nini nimeongelea. Na katika waandishi wazuri wanapoandika kitabu uangalia pande mbili. Za mazuri aloanya mtu na mabaya. Si kumtangaza mtu kwa mabaya tu!
Hilo neno sukuma gang kwangu naona kawaida hata ukiita mara kumi sibabaiki, kwa sababu akili upi uwaza mashambulizi na si uchambuzi wa kina.
Na inaonesha ujaelewa kabisa nilichokiongelea unarukia rukia tu. Sikulaumu ila uelewa wako ndo ulipoishia.
 
Sidhani kama unatutendea haki wananchi. Kilichopo na kinachofanywa na Rais wa Tanzania ni kutumia katiba mbovu tuliyonayo kututia woga wa kutufungulia mashtaka ya kutunga, kutufunga jela pasipo na haki, kutuua na maovu mengi.

Tukiwa na katiba ambayo Rais anafahamu akifanya maovu atachukuliwa hatua za kisheria bila kuchelewa atatenda haki na watu watakuwa na ujasiri wa kumwambia ukweli!
Ni hivi, hata hiyo katiba nzima ikipatikana bado Rais wa Tanzania anaweza fanya chochote na asifanywe chochote.
There's no law in the jungle.
 
Generali ulimwengu ni mtu hatari aliejawa na roho mbaya kupindukia. Aende kwao Rwanda akajaribu kufanya haya anayoyafanya hapa asikilizie muziki wake. Anadhani yeye anafahamu kila kitu na chochote anachotaka yeye kifuatwe. Hiyo ndiyo demokrasia?
 
JPM alishakufa, haijalishi alifanya mazuri au mabaya....hebu sasa tupambane na yetu sisi tuliohai na tuache kulialia, He has done his part, tuwe na shukrani, kama wengine mnamuona alitufanya mazuzu wapo wanaoona alikuwa the best pia, na hii ipo kwa kila binadamu..
 
Back
Top Bottom