Duh! watanzania kweli vichwa, maana ni kweli hiyo moja imechukua 5 years , sasa 6 miaka mingapi? na amebakiwa na na muda gani wa kufanya hivyo? miaka 30? maana 6 mara 5 ni 30.
Haya ukija meli kubwa huko ziwa victoria inabidi tufanye uchambuzi, je inachukua muda gani kutengeneza hiyo Meli, na je hiyo order ameisha iweka? maana kwa jinsi serikali yake inavyo fanya kazi hiyo order tu itachukua miaka mitano, halafu baada ya hapo wanaweza wakalipa hela na adhabu juu(iwe penaly au faini) na meli mwisho wa siku wakaiacha.. rejea issue ya vitambulisho na wale jamaa wa Kenya toka wakati/kipindi cha Mwinyi, akaja Mkapa na sasa Kikwete akisaidiana na Masha/membe, vitambulisho bado ni gumzo na hela tulisha lipa kwa mkandarasi wa kwanza na nyumba tulijenga, sasa tuna msubiri huyu mkandarasi wa Sasa, nafikiri tutanunua ndege zetu na kuwa na ka-ATC ketu, ndege ya Masha ni dar-Mza, na Membe ni Lindi-Dar, ya muheshimiwa ni Bagamoyo-to Ulaya-Amerika-far east-Carebean nk. akiwa nchini anawaambia tu dogo masha au membe mi nataka kufika kijijini kidogo, basi wanatoa ndege zao.