Jeshi la Polisi: Hakuna ushahidi kuwa Freeman Mbowe alishambuliwa. Alikuwa ametoka kwa Joyce Mukya. Alikuwa amelewa chakari

Dah,huyu ni kiongozi wa juu sana wa chama,sasa kwenye hizo kumbi za starehe usiku alikua anatafuta nini?na walinzi wake nao walikuwa wapi?mi nadhani walinzi wake wana cha kujibu hapo,wanawezaje kumuacha bosi getini kabla hajaingia ndani,huu ni uzembe wa hali ya juu kama kweli walikuwepo...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unauliza cctv bongo?,,hizo vitu hazipo

Acha upotoshaji usio na msingi wowote, CCTV zipo, na hizo zikitolewa kilichonaswa, kila mtu ataanza kuweka ukweli wake kufuatia kinachoonekana kwenye hizo footage. Haya mengine sijui ripoti ya polisi, maelezo ya Mbowe, au mtoto wake, kimada wake, wabunge nk ni siasa tu.
 
Polisi wameamua Kuja na taarfa ambazo mtu kama mimi mchunga ng'ombe naweza kuztoa toka malishoni Bila comnvincing evidence?watu waliosomeshwa kwa kodi za wanyonge wameamua Kuja na majibu mepesi kiasi hiki?

Unaweza tumia facts za kitoto kujustify ukweli wa tukio lile?... Niliapa mwanangu asome sana...ila kama atakuja niambie ni msomi wa kiasi cha kuingia kwenye kazi fulani fulani ikiwemo hii basi...ajue si mtoto wangu asilani!! Hakuna kitu kinauma nimetumia gharama zangu kupika ubongo wa mtoto halafu aje ageuke hivi stakubali!!!

Nilitegemea wawambie wananchi kwa kutumia footage camera tukio Zima lilivokua kama movement za watu zilikuepo au lah picha zongeonyesha..kweli MTAA mzima cctv Kamera hazikuepo?je nyumba haikua na Kamera ili kujustify tukio lile? Msomi unaweza Sema jirani ndy uthibitisho je kama jirani ni adui yako?

Sjui taifa linaelekea wapi..kudharilishana kufedheheshana imegeuka desturi katka taifa la Mwlm Nyerere!!! ?
 
Bado najaribu kujiuliza kwanini CCTV footage zinakwepwa kwenye hili tukio. Haya mengine ni sehemu tu kuupata ukweli. Lakini ukweli halisi ni kupatikana CCTV footage, kisha kila mtu ataanza kuweka ukweli wake kuanzia hapo.
Kuna watchmen,hawakuona wala kusikia,hao washambuliaji wamepenyea wapi?
Ni kazi ya mbowe sasa kutoa counter allegations,kumbuka safari hii dereva kapatikana na kahojiwa chap chap,na unajua IQ ya madereva ilivyo ndogo,tusubiri mwamba nae atueleze,
 
Mimi sipendi ccm ila kwa hili, chadema wanatakiwa kuja na ushahidi wa kutosha. Mimi binafsi ni kitu kimoja tu kinachonifanya nisiamini madai ya CCM. Huwezi angguka kwenye ngazi ukavunjika mguu. Sana sana utateguka.
 
Tatizo ndugu zetu wa polisi hawaaminiki kivile kwahiyo nusu ukweli nusu uongo
 
Wametumia maneno yale yale aliyoyasema spika "alilewa chakari" hivi Police walikosa maneno ya kuandika hadi waseme kile alichokisema spika?
 
TUWE N AKIBA YA MANENO, USHAHIDI WA KIDAKTARI NI MUHIMU UTHIBITISHE KAMA KWELI UKIANGUKA KWENYE NGAZI HUUMI KISOGO BALI UTAUMIA MGUU WA KULIA HADI KUFANYIWA OPERATION.

TUNASUBIRI.
Madaktari wanaendeshwa na mihemko ya kisiasa na utashu wa Wana siasa wa the CHAMA chakavu
 
Ni uzembe mkubwa,dreva anatakuwa ahakikishe boss kaingia ndani na mlango umefungwa ndipo ageuze,hawa watu wanafanya vitu locally sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…