Jeshi la Polisi huu si mchezo wa watoto, ni janga kwa wazazi

Jeshi la Polisi huu si mchezo wa watoto, ni janga kwa wazazi

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2013
Posts
21,741
Reaction score
26,735
Kuna tangazo Azam Tv linalohusu tamasha la watoto litakalofanyika mwezi wa 8 Oyterbay kwenye uwanja wa kijani zamani kulikuwa dipu ya kuogeshea mbwa, moja ya "mchezo" ni wa kulenga shabaha kwa kutumia bunduki bandia, huu kwa watoto wenye wazazi wanaomiliki bunduki ambao ni wengi kulingana na eneo unaweza usiishie hapo bali utafika nyumbani siku yoyote ile mtoto atakapojisikia kuiba bunduki ya baba na kulenga shabaha.

Hivi waliouandaa mchezo huo kwa watoto walifikiria nini, mtoto alenge shabaha kwa bunduki bandia ili iweje! Ninaliomba jeshi la polisi lisiuruhusu mchezo huo na mingine isiyofaa kwa watoto, pia iwe imakagua michezo yote ya watoto, ninakumbuka huko nyuma mjini Morogoro wakati wa sherehe za nanenane kuna mtoto alifariki baada ya kuanguka kwenye pembea ya kuzunguruka, hii ilitokana na kukosa ukaguzi wa kuona mnyororo unaotakiwa kumshika kama haupwai.
 
Kuna tangazo Azam Tv linalohusu tamasha la watoto litakalofanyika mwezi wa 8 Oyterbay kwenye uwanja wa kijani zamani kulikuwa dipu ya kuogeshea mbwa, moja ya "mchezo" ni wa kulenga shabaha kwa kutumia bunduki bandia,
Naunga mkono hoja, hii michezo si sahihi kwa watoto mimi binafsi hata bunduki au silaha za bandia huwa siwanunulii watoto.
 
Heeee, twende kwenye airsoft battle au paintball uone show,, kulenga shabaha wasema polisi wakataze wakat watu tuna simulate battle na airsoft match, watu wengine bhana[emoji2211][emoji2211]
Mkuu umri umeshaenda kajitegemee bana. Unaona sasa umebaki kung'ang'ania kucheza playstation na mpwa wako mtoto wa shemeji Yako hapo sofani sebuleni kwa shemeji Yako.
 
Mkuu umri umeshaenda kajitegemee bana. Unaona sasa umebaki kung'ang'ania kucheza playstation na mpwa wako mtoto wa shemeji Yako hapo sofani sebuleni kwa shemeji Yako.
Airsoft na paintball sio PS,, ni battle simulation guns zenye bb's balls au paintballs guns kama hizo hapo chini,, waweza nunulia mkeo na watoto mcheze nyuma ya nyumba,, ila angalizo vaa mask zinaumiza zikikupigaView attachment 2288939
HTB1_vgtSXXXXXbMXXXXq6xXFXXXo.jpg
View attachment 2288940
 
Mkuu umri umeshaenda kajitegemee bana. Unaona sasa umebaki kung'ang'ania kucheza playstation na mpwa wako mtoto wa shemeji Yako hapo sofani sebuleni kwa shemeji Yako.
Karibu kwa kaka yangu kwa ajili ya chakula cha jioni,, and this sunday kuna match karibu mno [emoji2211][emoji2211]
 
Mhn! Wanawake wanapenda Security huwenda waandaji wanajaribu kutatua shida za wanawake kwa kuwa na walinzi wengi (just a joke).

kiukweli binafsi huwa simwelewi hata mzazi anayemnunulia mwanaye pastola ya kuchezea hivi tunadhamilia watoto wawe walinzi wa watoto wenzao au wawe majambazi? na wazazi tulivyo wazembe tutakuwa tunakenua meno! sasa inapotokea mtoto wako wa kike kalengwa na wa kiume baada ya miaka michache hamalizi shule kapigwa mimba! vitu vingine vinanafasi na tafsiri ngumu kwenye ulimwengu wa Roho si kila kitu kiko sahihi.

Ama haitoshi ikitokea je watu na inawezekana wasiwe waandaaji wakinuizia kuwa watu watoto wote waliolengwa risasi na watolewe kama sadaka kwa biashara yangu. kwa hiyo eneo la kulengwa linakuwa madhabahu na wanaolenga ndio makuhani wa kupeleka sadaka kuzimu na hivi mmesema yanafanyika wapi? kulikuwa na dimbwi la kuoshea nini? na nini ni alama ya nini?

Kazi ipo siharibu biashara za watu na kuwanyima watoto wetu wapendwa raha kwa sasa ila kama mjomba anavyosema "tusisahau vibwaya ili tuje tucheze ngoma yetu ya kishenzi"!
 
mhn! Wanawake wanapenda Security huwenda waandaji wanajaribu kutatua shida za wanawake kwa kuwa na walinzi wengi ( just a joke).
kiukweli binafsi huwa simwelewi hata mzazi anayemnunulia mwanaye pastola ya kuchezea hivi tunadhamilia watoto wawe walinzi wa watoto wenzao au wawe majambazi? na wazazi tulivyo wazembe tutakuwa tunakenua ha kwa sasa ila kama mjomba anavyosema "tusisahau vibwaya ili tuje tucheze ngoma yetu ya kishenzi"!
[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Heeee, twende kwenye airsoft battle au paintball uone show, kulenga shabaha wasema polisi wakataze wakat watu tuna simulate battle na airsoft match, watu wengine bhana[emoji2211][emoji2211]
Huu si wa kwenye simu au kompyuta, huu ni halisi. Kuna visa vimewahi kutokea vya watoto kuchukua bunduki za baba zao na "kuzichezea".
 
Mhn! Wanawake wanapenda Security huwenda waandaji wanajaribu kutatua shida za wanawake kwa kuwa na walinzi wengi (just a joke).

kiukweli binafsi huwa simwelewi hata mzazi anayemnunulia mwanaye pastola ya kuchezea hivi tunadhamilia watoto wawe walinzi wa watoto wenzao au wawe majambazi? na wazazi tulivyo wazembe tutakuwa tunakenua meno! sasa inapotokea mtoto wako wa kike kalengwa na wa kiume baada ya miaka michache hamalizi shule kapigwa mimba! vitu vingine vinanafasi na tafsiri ngumu kwenye ulimwengu wa Roho si kila kitu kiko sahihi.

Ama haitoshi ikitokea je watu na inawezekana wasiwe waandaaji wakinuizia kuwa watu watoto wote waliolengwa risasi na watolewe kama sadaka kwa biashara yangu. kwa hiyo eneo la kulengwa linakuwa madhabahu na wanaolenga ndio makuhani wa kupeleka sadaka kuzimu na hivi mmesema yanafanyika wapi? kulikuwa na dimbwi la kuoshea nini? na nini ni alama ya nini?

Kazi ipo siharibu biashara za watu na kuwanyima watoto wetu wapendwa raha kwa sasa ila kama mjomba anavyosema "tusisahau vibwaya ili tuje tucheze ngoma yetu ya kishenzi"!
Miaka michache iliyopita wakati wa maonesho ya Sabasaba Dar. ziliuzwa bunduki eti za watoto japo zilikuwa na uwezo wa kujeruhi, watu walizigimbea na polisi walipokuja kushtuka mkeka ulikuwa unaanuliwa na sinia laenda kuoshwa! Ni kwamba waandaaji wa maonesho hawakukagua bidhaa zinazoingizwa kwenye maonesho, huo ulikuwa uzembe hatari.
 
Airsoft na paintball sio PS,, ni battle simulation guns zenye bb's balls au paintballs guns kama hizo hapo chini,, waweza nunulia mkeo na watoto mcheze nyuma ya nyumba,, ila angalizo vaa mask zinaumiza zikikupigaView attachment 2288939View attachment 2288942View attachment 2288940
Ondoa angalizo, mtoto ni mtoto atajificha nyuma ya ukuta na kumlenga mpita njia kisha anakimbia huku akicheka kwa kumpiga, achana na mchezo usiokuwa salama. Kuna jamaa yangu alimnunulia mjukuu wake kibastola kinachowekwa vijiti vya plastiki japo vikikupata vinaumiza kidogo, nilipovijaribu na kuona matokeo yake vile vijiti niliviharibu na nilimjulisha muhusika na alinielewa.
 
Huu si wa kwenye simu au kompyuta, huu ni halisi. Kuna visa vimewahi kutokea vya watoto kuchukua bunduki za baba zao na "kuzichezea".
And airsoft na paintball ni uhalisia tena inauma,,, kwanza bunduki lazima ikae kwa safe sababu hata mtoto asiyecheza airsoft anaweza mkandika mzee au akajiumiza mwenyewe kama bunduki imewekwa vibaya,, acheni singizia michezo hii,, kwa upumbavu unaofanywa na wazazi wa kutoweka silaha zao sehemu salama
 
Ondoa angalizo, mtoto ni mtoto atajificha nyuma ya ukuta na kumlenga mpita njia kisha anakimbia huku akicheka kwa kumpiga, achana na mchezo usiokuwa salama. Kuna jamaa yangu alimnunulia mjukuu wake kibastola kinachowekwa vijiti vya plastiki japo vikikupata vinaumiza kidogo, nilipovijaribu na kuona matokeo yake vile vijiti niliviharibu na nilimjulisha muhusika na alinielewa.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Wabongo bhana
 
Back
Top Bottom