Jeshi la Polisi kujipa jukumu la kuchunguza mauaji ya askari, ni sawaswa na kesi ya nyani kumpa ngedere

Jeshi la Polisi kujipa jukumu la kuchunguza mauaji ya askari, ni sawaswa na kesi ya nyani kumpa ngedere

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Jeshi la Polisi nchini limejipa jukumu la kuchunguza mauaji yaliyotokea kwenye daraja la selander, ambapo mtu mmoja anayefahamika kwa jina la Hamza, aliwafyatulia risasi askari watatu na mlinzi mmoja wa kampuni ya SGA na kuwaua wote na askari wengine kadhaa kujeruhiwa na hatimaye yeye mwenyewe kuuawa na askari waliokuwa wakilinda doria eneo hilo

Kuna hadithi nyingi zinazosemwa semwa kuhusu nia ya huyo kijana aliyewafyatulia risasi askari hao.

Kuna wengine wanadai kuwa huyo kijana alikuwa analipiza kisasi kwa askari hao, baada ya kumdhulumu dhahabu zake ambazo alikuwa akiziuza.

Hebu tujiulize hivi hawa hawa Polisi watatoa ripoti bila kuuficha ukweli, hata kama ripoti hiyo itasema chanzo cha mauaji hayo ni wao Polisi kufanya dhuluma hiyo ya kumpora dhahabu zake huyo kijana??

Hata ukiangalia mazingira ya mauaji hayo, kwa huyo kijana kuwa-target maaskari watupu na kuwaacha raia, inadhibitisha tetesi hizo.

Ni kwanini basi isiundwe Tume huru ya kuchunguza chanzo cha mauaji hayo, Tume hiyo ihusishe na wataalam wengine kwa mfano majaji wastaafu, wanasiasa maarufu toka kwenye vyama vya siasa, na kadhalika na kadhalika.

Ninavyoona Mimi, kuunda Tume ya uchunguzi, ya maaskari watupu, ni sawaswa na kesi ya nyani kumpa ngedere!

Ni dhahiri hapo hata hayo matokeo ya uchunguzi wa Tume hiyo unaweza kuyabashiri
 
Acha polisi wafanye kazi yao.
Kazi iendelee
 
Jamaa waamua kupigana na polisi mwenye bastola baada ya kuona anawafuata fuata ilihali wameshampa rushwa!!!
 
Jeshi la Polisi nchini limejipa jukumu la kuchunguza mauaji yaliyotokea kwenye daraja la selander, ambapo mtu mmoja anayefahamika kwa jina la Hamza, aliwafyatulia risasi askari wawili na mlinzi mmoja wa kampuni ya SGA na kuwaua wote na askari wengine kadhaa kujeruhiwa na hatimaye yeye mwenyewe kuuawa na askari waliokuwa wakilinda doria eneo hilo

Kuna hadithi nyingi zinazosemwa semwa kuhusu nia ya huyo kijana aliyewafyatulia risasi askari hao.

Kuna wengine wanadai kuwa huyo kijana alikuwa analipiza kisasi kwa askari hao, baada ya kumdhulumu dhahabu zake ambazo alikuwa akiziuza.

Hebu tujiulize hivi hawa hawa Polisi watatoa ripoti bila kuuficha ukweli, hata kama ripoti hiyo itasema chanzo cha mauaji hayo ni wao Polisi kufanya dhuluma hiyo ya kumpora dhahabu zake huyo kijana??

Ni kwanini basi isiundwe Tume huru ya kuchunguza chanzo cha mauaji hayo, Tume hiyo ihusishe na wataalam wengine kwa mfano majaji wastaafu, wanasiasa maarufu toka kwenye vyama vya siasa, na kadhalika na kadhalika.

Ninavyoona Mimi, kuunda Tume ya uchunguzi, ya maaskari watupu, ni sawaswa na kesi ya nyani kumpa ngedere!

Ni dhahiri hapo hata hayo matokeo ya uchunguzi wa Tume hiyo unaweza kuyabashiri
Kifupi Jeshi la Polisi limekosa weledi. Wanaacha kuwa na mipango ya kuwa na Jeshi linaloenda na wakati, wamebaki kutumikia Watawala na kutengeneza na kulinda Madeal yao.

Hapa hakuna Jeshi.....ndio maana kutwa wako na Petty issues tu. Aibu, ndio maana Denmark wanaondoka.
 
Kila siku nikisema hapa kuwa Tanzania haina serikali bali kuna genge la wahuni ambao wanajiita ni Serikali huwa naonekana kuwa ni mhaini.

Nchi yenye Serikali haiwezi kufanya kituko kama hiki anachoelezea mleta uzi.
Ni kweli kabisa

Hivi inawezekana vipi kuwa yule kijana, isemekane kuwa mauaji yale aliyafanya kwa kulipiza kisasi kwa hao Polisi, kutokana na kudhulumiwa dhahabu yake, halafu hao Polisi wajipe jukumu la kujichunguza??
 
Ni kweli kabisa

Hivi inawezekana vipi kuwa yule kijana, isemekane kuwa mauaji yale aliyafanya kwa kulipiza kisasi kwa hao Polisi, kutokana na kudhulumiwa dhahabu yake, halafu hao Polisi wajipe jukumu la kujichunguza??
Ni maajabu ya ajabu sana mkuu.
 
Kila siku nikisema hapa kuwa Tanzania haina serikali bali kuna genge la wahuni ambao wanajiita ni Serikali huwa naonekana kuwa ni mhaini.

Nchi yenye Serikali haiwezi kufanya kituko kama hiki anachoelezea mleta uzi.
Inawezekana wewe ndio kituko. Jeshi la Polisi lazima lichunguze jinai au uhalifu kama huu maana ndio kazi yake ya msingi.
Kama ukisema hilo jeshi lisiwepo kabisa kwa sababu zako nitakuelewa.
Lakini kama lipo lazima lichunguze.
Je unaweza ku-share uzoefu wako, sehemu zingine Mapolisi wakishambuliwa specifically kama hivi, huwa anachunguza nani?!
 
Kwanini tunasita kusema: muuwaji alieuwa askari wetu polisi na kujeruhi raia ni mtanzania mwenye asili ya kisomali?
20210826_013705.jpg
 
Back
Top Bottom