Jeshi la Polisi lawakamata watuhumiwa 4 kati ya 6 waliofanya tukio la kumlawiti binti wa 'Yombo'. Wasema binti yupo salama

Jeshi la Polisi lawakamata watuhumiwa 4 kati ya 6 waliofanya tukio la kumlawiti binti wa 'Yombo'. Wasema binti yupo salama

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
11.jpg
22.jpg

Jeshi la Polisi ningependa kutoa taarifa ya uchunguzi wa tukio ambalo lilisambazwa katika mitandao ya kijamii kupitia picha mjongeo (video clip) kuanzia Agosti 2, 2024 ikimwonyesha binti mmoja akifanyiwa vitendo vya ukatili.

Uchunguzi uliofanyika hadi sasa umefanikisha kumpata binti aliyefanyiwa ukatili huo na amehifadhiwa eneo salama na anaendelea kupata huduma zinazostahili kupewa mtu aliyefanyiwa ukatili wa aina hiyo.

Aidha uchunguzi umebaini tukio hilo lilifanyikia eneo la Swaswa katika Jiji la Dodoma mwezi Mei 2024.

Pia soma: Watuhumiwa wa mande ya Ubakaji na ulawiti waliotumwa na afande wakamatwa

Pia hadi sasa uchunguzi umefanikisha kukamatwa watuhumiwa wanne kati ya sita ambao walipanga na kutekeleza uhalifu huo. Watuhumiwa hao wamekamatiwa mkoani Dodoma na Mkoa wa Pwani ambao ni Clinton Honest Damas kwa jina maarufu Nyundo, Praygod Edwin Mushi, Amini Lord Lema na Nikson Idala Jakson.

Jeshi la Polisi lingependa kueleza pia limefanikiwa kukamata watuhumiwa wanne huko Dar es Salaam waliokiuka sheria na kusambaza picha mjongeo wa tukio hilo kwenye mitandao ya kijamii ambao ni Frora Mlombola, Aghatha Mchome, Madatha Jeremiah Budodi na James Nyanda Paulo.

Pia watuhumiwa wanne wamekamatwa kwa tuhuma za kutengeneza na kusambaza taarifa za uongo mitandaoni zinazosema RIP.

Binti aliyebakwa na kulawitiwa akutwa amefariki. Taarifa nyingine ya uongo inasema Mama wa binti huyo amedondoka na kufariki. Watuhumiwa wawili wamekamatwa huko Arusha na wawili Mkoani Dar es Salaam ambao majina yao ni Amos Lwiza, Adam Dongo, Venance Mallya na Isack Elias.

Uchunguzi unaendelea kukamilishwa sambamba na kuwasaka watuhumiwa wawili ambao bado wamejificha ili wafikishwe mahakamani. Kwa hawa ambao bado wamejificha kama kuna yeyote anayefahamu wamejificha kwake atoe taarifa na asipofanya hivyo wakikamatwa wakiwa nyumbani au kwenye makazi yake atakamatwa na kufikishwa Mahakamani.

Jeshi la Polisi lingependa kutoa onyo kwa baadhi ya watu ambao hawana mamlaka ya kufanya hivyo waache tabia ya kwenda kwenye eneo ambalo lilitajwa kuwa huyo binti anaishi wakimtafuta yeye na familia yake ili wawahoji au kuwaona. Kufanya vitendo vya aina hiyo ni kuwatweza utu wao na kuwatonesha majeraha waliyonayo mioyoni mwao.

Imetolewa na:
David A. Misime - DCP
Msemaji wa Jeshi la Polisi
Makao Makuu ya Polisi
Dodoma, Tanzania
 
Hili jeshi la polisi sio poa kwa kukamata watu! Ww jifanye tu invincible utajikuta kituo cha polisi hutaamini.
Halafu inaonekana wale wendawazimu wamepanda mtumbwi wa vibwengo hadi majina yao yametajwa sio kawaida hapa naona watu wakila 50+ years in prison
 
Jeshi la Polisi limetangaza kuwakamata Watuhumiwa Wanne kati ya 6 waliopanga na kutekeleza Ukatili wa Kingono dhidi ya binti aliyeonekana katika Video iliyosambazwa Mitandaoni hivi karibuni

Kwa mujibu wa taarifa ya Polisi, waliokamatwa ni Clinton H. Damas (Nyundo), Praygod E. Mushi, Amini L. Lema, na Nikson I. Jackson ambao wamepatikana Dodoma na Pwani.
20240809_164412.jpg
20240809_164416.jpg
 
Back
Top Bottom