Pre GE2025 Jeshi msipotambua umuhimu wenu, mtatumika vibaya kwa maslahi ya wanasiasa na wala siyo kwa maslahi ya Taifa

Pre GE2025 Jeshi msipotambua umuhimu wenu, mtatumika vibaya kwa maslahi ya wanasiasa na wala siyo kwa maslahi ya Taifa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Hili suala la jeshi kuamriwa kufanya usafi kila vyama vya upinzani vinapotangaza maandamano halikubaliki.

Wote tunalia hali ngumu ya maisha ikiwemo wanajeshi pamoja na familia zao na viongozi wa serikali wako kimya, halafu wanapotakiwa kufanya kitu walau hata kwa shinikizo la maandamano, wanakimbilia Kuomba wanajeshi wetu wakafagie barabara na kuokota makopo! Kweli jamani?!! Hapana. Hii haikubliki kabisa.

Wanajeshi tumikieni maslahi ya nchi na wananchi wake na wala siyo viongozi wa hovyo wanaotusababishia hali ngumu kutokana na matumizi yao ya anasa huku raia tunaumia.

Jitambueni nyinyi ni watu wa muhimu sana kwa nchi na mnapaswa kuheshimiwa na siyo kutumika.
Tanzania ni nchi ya amani sana. Kama ingekuwa West Africa au America, kw hali ya uozo wa uongozi, ufisadi na kuuzwa rasilimali za nchi jeshi lingekuwa lilishafanya mapinduzi ya kijeshi ili kuilinda nchi isipotee, na viongozi wengi waliokuwa madarakani kupigwa risasi au kufungwa. Lakini sio Tanzania, hilo halitatokea kamwe, sisi ni watu wa amani.
 
Hoja yako imekaa kisiasa mno. Kwani Usafi hauwezi kufanyika siku nyingine isipokuwa siku hiyo ambayo hao jamaa walishapanga maandamano?
Tukumbuke na kuzingatia kwamba endapo yatatokea maafa (kama maandamano yatafanyika) mm na ww tutahusika kwa namna moja au nyingine e.g. Kuzika/rambirambi, kukosa amani siku hiyo - maduka/fremu na shughuli /huduma zitatatizika, huenda wakahusika Ndg au Jamaa zetu humo.
Mchuma janga hula na wakwao.
nadhani walioandaa maandamano haramu wanaweza endelea na ratiba zao na wenye mipango ya usafi pia wakafanya kwa sehemu yao.

shida au kikwazo kiko wap kama sio kupigana chabo mipango ya wengine ukataka iwe yako.....

Shughuli hizo zote mbili na wahusika wake wala hazifanani wala kulandana....

hiyo ya kufa na kuzikana ni ya Mungu na huyo Mungu ni wetu sote. Ukifa tutaambatana na wanaotarajia kufa siku zingine tutakuzika na tutakusahau huko kaburi. Nikifa mie pia kwa Neema na Baraka za Mungu nitazikwa na kusahaulika huko kaburi,

Hivyo ndivyo binadamu tulivyo....
 
Hoja yako imekaa kisiasa mno. Kwani Usafi hauwezi kufanyika siku nyingine isipokuwa siku hiyo ambayo hao jamaa walishapanga maandamano?
Tukumbuke na kuzingatia kwamba endapo yatatokea maafa (kama maandamano yatafanyika) mm na ww tutahusika kwa namna moja au nyingine e.g. Kuzika/rambirambi, kukosa amani siku hiyo - maduka/fremu na shughuli /huduma zitatatizika, huenda wakahusika Ndg au Jamaa zetu humo.
Mchuma janga hula na wakwao.
nadhani walioandaa maandamano haramu wanaweza endelea na ratiba zao na wenye mipango ya usafi pia wakafanya kwa sehemu yao.

shida au kikwazo kiko wap kama sio kupigana chabo kwenye mipango isohusu.....
Shughuli hizo zote mbili na wahusika wala hazifanani wala kulandana....

hiyo ya kufa na kuzikana ni ya Mungu na huyo Mungu ni wetu sote. Ukifa tutaambatana na wanaotarajia kufa siku zingine tutakuzika na tutakusahau huko kaburi. Nikifa mie pia kwa Neema na Baraka za Mungu nitazikwa na kusahaulika huko kaburi,

Hivyo ndivyo binadamu tulivyo
 
Kama kuna kazi inahitaji kiwango cha juu kabisa cha Nidhamu ya Utii basi ni Jeshi, mpaka hayo yanatokea wakubwa zao tayari wana taarifa ivo hapo wapo kutimiza majukumu yao.
 
Tanzania ni nchi ya amani sana. Kama ingekuwa West Africa au America, kw hali ya uozo wa uongozi, ufisadi na kuuzwa rasilimali za nchi jeshi lingekuwa lilishafanya mapinduzi ya kijeshi ili kuilinda nchi isipotee, na viongozi wengi waliokuwa madarakani kupigwa risasi au kufungwa. Lakini sio Tanzania, hilo halitatokea kamwe, sisi ni watu wa amani.
Hata Babeli walisema hivyo hivyo kwamba haiwezi kuanguka, lakini mwisho wa siku ilianguka
 
nadhani walioandaa maandamano haramu wanaweza endelea na ratiba zao na wenye mipango ya usafi pia wakafanya kwa sehemu yao.

shida au kikwazo kiko wap kama sio kupigana chabo kwenye mipango isohusu.....
Shughuli hizo zote mbili na wahusika wala hazifanani wala kulandana....

hiyo ya kufa na kuzikana ni ya Mungu na huyo Mungu ni wetu sote. Ukifa tutaambatana na wanaotarajia kufa siku zingine tutakuzika na tutakusahau huko kaburi. Nikifa mie pia kwa Neema na Baraka za Mungu nitazikwa na kusahaulika huko kaburi,

Hivyo ndivyo binadamu tulivyo
Katika hali halisi ya kawaida, RC au DC ni walinzi wa Amani katika maeneo yao. Ninachoangaliza hapo ni Je, RC na DC wanaohusika wamechukua Tahadhari? mbona wameshaanza kuyaita ni maandamano haramu? unajua maandamano yana mambo mengi. Wapo watu wenye nia ovu ndani ya hayo maandamano japokuwa yanaitwa ni maandamano ya Amani.
Halafu wanaofanya usafi ni wanajeshi(Askari). Je, huoni huo ni mtego ili isemekane waliwazuia
Jeshi lipo Kwa mujibu wa katiba na majukumu yake yapo wazi,pia maandamano yameruhusiwa na katiba ya nchi yetu,hivyo sio kosa kuandamana.
Mkuu, huoni kwamba yanatengenezwa mazingira mtego ili ionekane waandamanaji walifanya kosa la kutatiza shughuli ya kufanya usafi i.e. waliwazuia kwa makusudi askari wakitekeleza amri Halali ya Mkuu wa Mkoa?
 
Hii kweli ni dharau😞,Eti RC ana amrisha jeshi kufanya Usafi 😭
Hivi RC anatoa wapi Uthubutu wa kuliamrisha jeshi? Kama ingekuwa analiamrisha jeshi kutuliza ghasia au uvunjifu wa amani angeeleweka. Lakini hii ya askari kushika mfagio na kuzoa taka sio.
 
Hivi RC anatoa wapi Uthubutu wa kuliamrisha jeshi? Kama ingekuwa analiamrisha jeshi kutuliza ghasia au uvunjifu wa amani angeeleweka. Lakini hii ya askari kushika mfagio na kuzoa taka sio.
Basi bora hata ingekuwa kwa kruta wa JKT, lakini JWTZ na FFU?!
Hapa Chalamila kazingua sana.
Halafu hata mabosi wake wako kimya kuonesha wanaunga mkono
 
Katika hali halisi ya kawaida, RC au DC ni walinzi wa Amani katika maeneo yao. Ninachoangaliza hapo ni Je, RC na DC wanaohusika wamechukua Tahadhari? mbona wameshaanza kuyaita ni maandamano haramu? unajua maandamano yana mambo mengi. Wapo watu wenye nia ovu ndani ya hayo maandamano japokuwa yanaitwa ni maandamano ya Amani.
Halafu wanaofanya usafi ni wanajeshi(Askari). Je, huoni huo ni mtego ili isemekane waliwazuia

Mkuu, huoni kwamba yanatengenezwa mazingira mtego ili ionekane waandamanaji walifanya kosa la kutatiza shughuli ya kufanya usafi i.e. waliwazuia kwa makusudi askari wakitekeleza amri Halali ya Mkuu wa Mkoa?
actually yangekuepo ya Amani yaloongozwa na hawa ndugu, shida ingekua kwa RCauDC but fojo ndio taaluma yao hawa jama, ndio utambulisho wao,

Yaani mtu anakwambia anakwenda kujinyonga kisha unamwambia nendraa kajinyonge....

Akijinyonga na kufa unaanza kulia, kuomboleza na kujuta na unge unge nyingi 🐒
 
Wakuu wa mikoa ,wakuu wa wilaya,wakurugenzi nk nchi nzima ni wengi sana,wasilidhalilishe jeshi letu hiyo kazi waifanye niliowataja hapo juu.
 
Back
Top Bottom