Jeshi Sudan laelekea kushinda vita

Jeshi Sudan laelekea kushinda vita

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Upepo wa mapambano kati ya majenerali wawili nchini Sudan unaonekana kubadilika ghafla dhidi ya Hemedti.

Jeshi linaloongozwa na generali Burhani limesema kwa sasa wananchi wate waliobaki mjini Khartoum wabaki ndani na wasichungulie madirishani kwani wameanza kutumia vifaru kushambulia kutoka pembe zote ili kuwang'oa askari wa genrel Hemedti.

Hii ni baada ya kampeni ya takriban wiki tatu ya kushambulia kutoka angani kupiga karibu na ikulu,makao makuu ya jeshi na uwanja wa ndege ambako RSF walifanikiwa kuyashikilia.

Hali inaonekana ni mbaya kwa RSF kwani wameishia kushikilia maeneo muhimu ya Khartoum tu na kubakisha maeneo yote mpaka Port Sudan chini ya udhibiti ya jeshi.Hilo limetoa fursa kwa jeshi kujitengenezea nguvu kubwa ya kuukomboa mji mkuu wa Khartoum.
 
Kwani Mrusi yupo upande upi hapo
Hali imebadilika.Mwanzoni mrusi alisemekana kuwa upande wa RSF kwani amewarahisishia kuchimba dhahabu na Marekani upande wa serikali. Serikali ya Misri upande wa jeshi (serikali) na Umoja wa falme za kiarabu upande wa RSF kwa vile waliwahi kuwasaidia askari wa kupigana Yemen.
Maelezo ya Hemedti kwamba generali Burhani ana mafungamano na utawala wa kiislamu uliopita na kwamba ndio unaomlinda Omar Albashir umebadili fikra za Misri na UAE ambao wote juu ya kwamba ni waislamu lakini huwa hawaupendi Uislamu uwe mfumo wa utawala.
Wanachi wengi wa Sudan hata wasipopenda Omar Albashir na watu wake warudi madarakani lakini wanapendelea utawala wa kiislamu kuliko mifumo mingine.Hivyo watamuunga mkono AlBurrhani ambaye anaweza akakosa msaada wa Misri aliyekuwa karibu kumpatia kila msaada anaoutaka. Pamoja na hivyo RSF kwa sasa hawana nguvu na nidhamu ya kijeshi na utawala wa kupanua maeneo wanayoyashikilia ambayo yanaishia jiji la Khartoum
RSF wameshindwa hata kutetea na kuleta nidhamu ya jimbo la Darfour ambako awali ilitajwa wana wafujasi wao wengi zaidi.
Mrusi hashughulishwi sana na siasa za utawala wa kiislamu kama ilivyo kwa Amerika na washirika wake akina Misri,hata Urusu kwenyewe yuko bega kwa bega na Ramzan Kadyrov wa Chechnya.Hivyo angeweza kumsaidia Dagalo wa RSF lakini kwa sasa vita vyake na Ukraine havimpi nafasi ya kutoa msaada wa kisilaha.
Ndio maana kushindwa kwa RSF kwa kutumia nyenzo za ndani za nchi ambazo ziko kwa jenerali Burhani zaidi ni kukubwa.
 
Vipi kuhusu wale wagalatia wenzako walioambiwa wafunge bila kula mpaka wakafa ili waende mbinguni fasta,wao hizo ndio mind set za kisasa?
Tuko Sudan ostadh kwa msaada wa picha tupo huku kwa wavaa kobazi tusitoke njee ya uwanja wa vita by the way kama kobazi hazi kutoshi usi shindane nazo waachie madina [emoji16][emoji16]
1223374803.jpg
 
Mrusi upande wa serikali US upande wa RSF patamu hapo
Acha uongo, wanamgambo wa RSF wanashirikiana na kundi la Wagner la Urusi, UAE na Libya. Jeshi la Sudan linapewa nguvu kwa mbali na Egypt, Saud Arabia na Kwa mbali Israel. Ndio maana RSF waliziaribu ndege za Saud Arabia na Egypt pia wanashambulia ndege za nchi nyingi zinazokuja kutoka raia wao. Kiufupi nchi nyingi za dunia zipo upande wa jeshi la Sudan, ila Urusi, Libya na UAE wanawasaidia wanamgambo wa Dagalo/Hemedt.
 
Vipi kuhusu wale wagalatia wenzako walioambiwa wafunge bila kula mpaka wakafa ili waende mbinguni fasta,wao hizo ndio mind set za kisasa?
Wale hawakubeba bomu wala silaha ,japo walidanganywa ,walifanya kwa hiari Yao bila kumsumbua yyte na kutaka madaraka wala nini , kule Sudan wanakimbiza kutawala mpaka kuharibu nchi ,utatawalje maskini wasio na lishe ,ule ni ujinga wakupitiliza
 
Hawa wavaa kobazi wana mind set za kizamani kwamba uki ishika Ikulu tu tayar wewe ni raisi
Hapo ndipo Hemedti alipokosea mahesabu.Ameshikilia ikulu,uwanja wa ndege na tv na redio na bado hajaweza kushinda.Silaha alizonazo ni hafifu mno.Hajaweza kuipiga hata ndege moja zinazomdondoshea mabomu asubuhi na jioni.Zaidi mipaka karibu yote ya nchi haiko mikononi mwake ndio port Sudan meli zinaendelea na kazi ya kubeba wakimbizi na kuleta mizigo.
 
Kwani Mrusi yupo upande upi hapo
RSF anaungwa na Libya, Russia na tajiri UAE.
Misri awali aliunga jeshi la serikali ila amekwama kwa sababu mbili:

1. Alimuunga mkono jeneral haftar WA Libya ila kashindwa kuchukua nchi na mbaya HAFTAR sasa anaunga RSF.
2. UAE ndiye mfadhili mkuu wa Misri kwa sasa financially kwa hiyo misri hataki kumkosa UAE kwani.

Kimsingi RSF wanawapiganaji wengi kiliko jeshi na wazoefu.
 
Mrusi upande wa serikali US upande wa RSF patamu hapo
Pale Sudan Urusi yupo pande zote. RSF wapo na Wagner kwa sababu ya madini na Russia serikali iko na serikali na ilitaka kujenga naval base.
UAE iko na RSF ili izidi kununua madini ya black market, madini mengi Afrika yanayopita njia za panya huuzwa Dubai. Saudi Arabia iko na RSF waliipatia wapiganaji kwenye vita ya Yemen ambayo inaelekea kuisha.
Libya yule General Khalifa Haftar muasi anawaunga mkono RSF walimsaidia wapiganaji dhidi ya serikali ya Libya.

Egypt iko na serikali, na nchi nyingine. Marekani iko na serikali isipokuwa inapinga ujenzi wa Russian naval base, na pande zote mbili zinapenda sana kujihusisha nayo zinajipendekeza.
 
Back
Top Bottom