Jezi ipi kali kati ya Simba na Yanga?

Jezi ipi kali kati ya Simba na Yanga?

Vunjabei alishailipa Simba hela, kazi imebaki kwake kuzirudisha. Nadhani umekuwa mvivu tu wa kufuatilia mikataba. Ngoja nikukumbushe:
Mkataba wa Simba na Vunjabei ni kwamba Vunjabei ametoa 2B kwa Simba, atauza kwa bei yoyote na kwa wingi wowote, anabaki kuzitafuta kuzirudisha kwenye mauzo. Hii ni pre paid
Mkataba wa Yanga na GSM ni kwamba anatafuta kwanza wateja, atauza kwa bei yoyote na kwa wingi wowote, ila kila jezi ataipa Yanga sh. 1,300/=. Hii ni post paid

Wakati Simba hatawakuwa na haja ya kufuatilia Vunjabei ameuza jezi ngapi, Yanga wao inabidi wafuatilie GSM ameuza jezi ngapi ili asije akawapiga, maana kila jezi itakayouzwa wana vihela hapo
Sasa hapo si ndo rahisi Yanga kupigwa na GSM maana anaweza kusema jezi sijauza kumbe anauza kwa mlango wa nyuma
 
Sasa hapo si ndo rahisi Yanga kupigwa ..... anaweza kusema jezi sijauza kumbe anauza kwa mlango wa nyuma
Kama unakumbuka juzi hapa, walipozindua tu jezi zikahadimika, baada ya siku nne zikawa zinatafutwa kwa tochi. Unaweza ukadhani eti mashabiki wamechangamkia mzigo ukaisha, lakini kumbe kuna mzigo mkubwa umepelekwa maduka ya muuzaji fulani, huko bado kuna mashaka kama uongozi wa Yanga unafahamu hilo
 
Kama unakumbuka juzi hapa, walipozindua tu jezi zikahadimika, baada ya siku nne zikawa zinatafutwa kwa tochi. Unaweza ukadhani eti mashabiki wamechangamkia mzigo ukaisha, lakini kumbe kuna mzigo mkubwa umepelekwa maduka ya muuzaji fulani, huko bado kuna mashaka kama uongozi wa Yanga unafahamu hilo
Wanasema mzigo umeisha wakati Sunderland unapatikana ,jiulize imekwaje Sunderland wauze jezi ya Yanga wakati zamani walikuwa wanauza za Simba
 
Hmna jezi humuu
20210903_123956.jpg
 
Truth be told...ushabiki kando

Timu zote zina jezi kali (home and away kits), kasoro kidogo tu kwenye jezi ya Simba ni hayo maneno kuzunguka ufito wa kola hapo mbele...

Kit ya Yanga ile njano na Simba ile nyeupe, binafsi naziona zitauzika sana kwa mashabiki maana zinavalika...

Kit #3 na ile ya michezo ya kimataifa, timu zote hazijaitendea haki hiyo kit...

Kwa ujumla tumejitahidi sana wabongo kwenye masuala ya jezi, kwa walio wapenzi wa mpira wa miaka yote mnaweza mkakumbuka yale majezi ya zamani ya timu zetu, mtu kama Steven Mapunda alikuwa akivaa jezi utadhani kashonewa nguo iliyomzidi umri...
 
Kama unakumbuka juzi hapa, walipozindua tu jezi zikahadimika, baada ya siku nne zikawa zinatafutwa kwa tochi. Unaweza ukadhani eti mashabiki wamechangamkia mzigo ukaisha, lakini kumbe kuna mzigo mkubwa umepelekwa maduka ya muuzaji fulani, huko bado kuna mashaka kama uongozi wa Yanga unafahamu hilo
[emoji16][emoji23]
 
Truth be told...ushabiki kando

Timu zote zina jezi kali (home and away kits), kasoro kidogo tu kwenye jezi ya Simba ni hayo maneno kuzunguka ufito wa kola hapo mbele...

Kit #3 na ile ya michezo ya kimataifa, timu zote hazijaitendea haki hiyo kit...

Kwa ujumla tumejitahidi sana wabongo kwenye masuala ya jezi, kwa walio wapenzi wa mpira wa miaka yote mnaweza mkakumbuka yale majezi ya zamani ya timu zetu, mtu kama Kevin Mapunda alikuwa akivaa jezi utadhani kashonewa nguo iliyomzidi umri...
[emoji23]
 
Wanasema mzigo umeisha wakati Sunderland unapatikana ,jiulize imekwaje Sunderland wauze jezi ya Yanga wakati zamani walikuwa wanauza za Simba
Wote hawa Sandalend na GSM ni washabiki wa mnyama, ila sema tu biashara unafanya na yeyote
 
Ngoja leo niwafundishe kitu mashabiki. Kuna ushabiki wa kinazi na ushabiki wa kimpira.

Kujadili uzi upi ni mkali ni swala la perspectives (mtizamo). Hapa ndio wengi tunaangukia kwenye unazi. Sio rahisi mshabiki wa kambi A aseme uzi wa kambi B ndio mzuri. Hata siku moja.

Lakini kuna kuwa objective (zingatia facts). Hapa kwa mwenye mtizamo wa hivi hata kama yupo kambi A anaweza kusema uzi wa kambi B ni mzuri.

Mimi nipo kundi la pili. Mimi pia ni mshabiki wa Simba. Jersey zote ni nzuri. Lakini ya Yanga ni nzuri kuliko ya Simba. Moja ya sababu zilizofanya jezi ya Simba kupungua ubora ni wingi wa maandishi.

Otherwise designs zote ni nzuri ila kusema kweli jezi ya Yanga imeizidi ya Simba kidogo.
 
Ili kupima ukali wa jezi ni vyema kuiona kwa macho kuliko kwa kutumia picha. Camera inaweza kuipamba kitu kionekana tofauti na uhalisia. Na ndio maana Simba wameenda kuzioneshea jezi zao baharini ili tu kuipa muonekano mzuri mtu avaapo na kupigwa picha na Yanga nao wametafuta location ambayo mvaaji wa jezi akipiga picha itampendeza. Nitatia neno baada uzi zote mbili kuona kwa kuzishika mkononi.
 
Back
Top Bottom