Jezi zilizokamatwa sio feki ni michezo ya Kariakoo, Sandaland kazidiwa maarifa

Jezi zilizokamatwa sio feki ni michezo ya Kariakoo, Sandaland kazidiwa maarifa

Jaribu tena baadae, namba uliyopiga kwa sasa haipatikani.

Mara ya nwisho kupanda public transport Tanzania ni mwendokasi tu, nalo nilipanda nami nisipitwe.

AlhamduliLlah, sijawa na sababu ya kupanda daladala wala public transport yoyote.

Nikiwa hai naisubiri SGR nayo niionje.
Bila shaka hata ndege huwa unapanda private jet mashaallah
 
Bibi ana kiherehere halafu hakuna asilolijua yeye kila kitu anakijua , ovyo kweli huyo bibi na ana mdomo mchafu kama choo cha stendi
Basi miaka hiyo akijifanya anaishi Canada ilikuwa shida tupu.. Siku nilipokuja kumuumbua kwamba hayuko Canada yuko hapo Kariakoo alipotea jukwani wiki nzima [emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nyie vijana FaizaFoxy na Mshana Jr naona mnatuharibia uzi hapa, hebu mmoja aanzishe uzi muanze kuchambana tutakuja kushuhudia ila si kuwaachanisha!.

Inaonekana mnajuana na ilikuwa hivi huko nyuma ila kwa sasa kila mtu njia yake, hapa mmoja anapunguza nyongo tu kwa mwenzake 😂!.
mambo ya jf hayo wengine hawapo kwa sasa hahaaaaaa
 
Huyo bibi hana anachojuwa kuhusu soko la kariakoo na wazee wa misheni town ndani yake.

Tukija kwenye sakata la jezi feki. Kwanza hili halijaanza leo wa jana hii ishi na kipindi kirefu huko nyuma jezi nyingi feki zimeshauzwa sana mtaani na mhusika wa haya yote ni huyo GSM. Mwaka 2021 kuna sakata GSM Kuhusishwa na kuuza jezi za simba feki sizani kama hili ulishawahi kulisikia ??

Hivyo hii ya juzi kuhusu jezi feki ilikuwa ni kimtia doa mshindani wake ila nyuma ya sakata GSM anahusika kwa kiasi kikubwa
GSM ajajikita kwenye biashara za nguo zaidi ya jezi za Yanga,GSM kaa uulize macartels wako wengi tena kubwa lao kabla ya ujio wa GSM alikua anashirikiana hadi na viongozi wa vilabu kutengeneza jezi fake,kuna msimu Yanga ilivaa jezi 8 na tracksuit juu,kama una kumbukumbu nzuri kuna match Yanga waliingia na tracksuit ikiwa joto kali,ujio wa GSM kwenye uwekezaji wa jezi umewaumiza waagizaji jezi fake kwa kiasi kikubwa,na baada ya GSM kuingia kwenye jezi hata simba nao wakashtuka wakamleta vunja bei japo nae alikua nyuma ya hao hao,labda huko kwenye shida zingine ila kwenye jezi fake GSM aihusiki hata chembe
 
Kumtaja mtu mwenye mzigo kama ule unatakiwa nawe uwe fit sana.. Kwakuwa utakuwa tayari umetangaza vita ya visasi

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu ni kweli kabisa Kkoo kuna umafia sana. Hata kwa mfano ukiwa na idea kali unataka uifanye halafu mtaji wako mdogo utashangazwa kuona ndani ya muda mfupi kuna wababe wameingiza mzigo kama wako makontena kadhaa na anauza bei karibu tu na uliyouziwa wewe China. Yaani automatically unaanza kuwa mteja wake. Kkoo kuna watu wana hela hadi kero. Kuna mama mmoja wa kikinga anauza masweta ya shule. Akiagiza samples ni 3000pcs wakati wajasiriamali wadogo wakiagiza 1000pcs jasho limewatoka. Kwenye mambo ya nguo kuna manyangumi hapo Kkoo.
 
Labda tunaweza kuziita feki (bandia) kutokana na ubora usiokidhi viwango.. Lakini kubwa ni kwamba mwenye dhamana ya kuziagiza hajatoa kibali kwa mwingine yoyote kuagiza kusambaza na kuuza

Kilichotokea Kariakoo ni uleule umafia ubabe na ushushushu wa biashara za pale mahali unaofanywa na ma tycoon, madon na makontawa wenye pesa zao ndefu na wenye connection mpaka ndani kama sio juu kabisa
Hawa ma tycoon na madon wana nyoka wao mashushushu wanaowaletea taarifa kila bidhaa mpya ama ya msimu inapokamata soko.. Na hawa hucheza na timing ya Mwenyezi mzigo husika. Wao wanachotaka ni sample tu ya mzigo halisi ama soft copy yake

Wewe mwenye mzigo wako unapopanda ndege uende ukaandae oda yako izalishwe wenzako wanakuwa wameshafikisha kila kitu huko kupitia nyoka wao walioko huko

Kwenye hizi biashara kubwa za Kariakoo zinazotegemea kuzalishwa kwa oda huko nje kuchelewa siku moja tuu umechelewa mno! Kwahiyo unapofika huko (mostly China) kuelewana bei mpaka kuanza uzalishaji unaweza kuchukua si chini ya siku mbili ukijumlisha na mbili za safari ni siku nne

Huo ni muda mwingi mno kwa waliokwisha kutangulia... Kwahiyo kwa kila hatua wewe utaachwa nyuma si chini ya wiki moja

Huku ukiwa hujui kinachoendelea unafanya fasta ili ukawe wa kwanza kuingiza mzigo sokoni lets say container za ko 3 au 4 hivi!.. Wakati mzigo wako umefika bandarini unajiandaa kuutoa mara unapata taarifa ama unaona mzigo kama huo huo tayari uko sokoni tena kwa bei poa zaidi..[emoji23]

Umeingiza container 4 mwenzako kaingiza 10 na kashaweka mzigo sokoni.. Usipokuwa na roho ngumu unaweza kujinyonga! Sasa hapo uchaguzi ni wako uuze sawa na yeye, au umuuzie yeye mzigo wote kwa bei atakayokupangia ama ubaki na mzigo wako ukudodee.. Hiki kwa vyovyote ndio kilichompata Sandaland lakini yeye pengine kakataa unyonge kaamua kukisanua!

Maswali muhimu sana!
1. JE WAHUSIKAN WATACHUKULIWA SHERIA?
2. Je mzigo utataifishwa na kuharibiwa?
3. Je mzigo utauzwa kwenye mnaba na kuachwa uingie sokoni?

Swali namba 1.
Mpaka sasa mamlaka akiwemo Sandaland mqenyewe wameshikwa na kigugumizi kumtaja mhusika! Hili si gumu na halihitaji uchunguzi mkubwa kwakuwa mzigo umeagizwa kupitia nyakara zote halali
Bank account
Jina la muagizaji
Mahali mzigo unapoenda
TIN ninja.. Sasa kuna uzito gani kumuweka wazi mhalifu?

Swali no 2
Je mzigo utataifishwa na kuharibiwa? Hapa kesi ikienda mahakamani pengine kunaweza kujitokeza mambo ya hakimiliki na patent copyright .. Kama ikithibitika mzigo hauna nyaraka halali za umiliki na malighafi iliyotumika ni chini ya viwango kuna uwezekano mkubwa mzigo kutaifishwa na kuteketezwa

Swali no 3
Je utauzwa kwenye mnada na kuachwa uingie sokoni?
Hapa hili linaweza kutokea kama ikithibitika material iliyotumika ni bora inakidhi viwango ila tu kuna shida kwenye nyaraka za umiliki (patent copyright)
Hapa kuna mengi
Mwenyezi patent copyright anaweza kupewa haki ya kuununua mzigo na kama akishindwa ukauzwa kwa mnada kwa mwenye uwezo

Hiki ndio kinasubiriwa na hao madon.. Kwasasa wako kimya wanasoma mchezo huku wakicheza michezo nyuma ya pazia..
Hii ni mojawapo ya sinema za kuvutia kariakoo kama ile ya vitenge na ni ngumu kutabiri mwisho wake

Je sterling atakufa? Usikose part 2

Zaidi soma: Umafia, ubabe na ujasusi wa biashara za Kariakoo | Page 18 Umafia, ubabe na ujasusi wa biashara za KariakooView attachment 2794379

Sent using Jamii Forums mobile app
Hizi ni biashara za watu wakubwa ndani ya serikali na chama dola. Usishangae kusikia majina ya watoto wa viongozi wakuu yakitajwatajwa
 
Hizi ni biashara za watu wakubwa ndani ya serikali na chama dola. Usishangae kusikia majina ya watoto wa viongozi wakuu yakitajwatajwa
Trust me hawatatajana.. Kinachofanyika sasa ni kusikilizia tuu.. Kama pressure ikizidi atatafutwa mbuzi wa kafara aswekwe ndani kwa 'makubaliano maalum' Kisha adhaminiwe..

Kesi ya vitenge iliishia wapi?
Kesi ya bomba la mafuta Kigamboni je?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
GSM ajajikita kwenye biashara za nguo zaidi ya jezi za Yanga,GSM kaa uulize macartels wako wengi tena kubwa lao kabla ya ujio wa GSM alikua anashirikiana hadi na viongozi wa vilabu kutengeneza jezi fake,kuna msimu Yanga ilivaa jezi 8 na tracksuit juu,kama una kumbukumbu nzuri kuna match Yanga waliingia na tracksuit ikiwa joto kali,ujio wa GSM kwenye uwekezaji wa jezi umewaumiza waagizaji jezi fake kwa kiasi kikubwa,na baada ya GSM kuingia kwenye jezi hata simba nao wakashtuka wakamleta vunja bei japo nae alikua nyuma ya hao hao,labda huko kwenye shida zingine ila kwenye jezi fake GSM aihusiki hata chembe
Basi waziri wa michezo atuambie ni nani muhusika. Mbona kaa kimya pamoja na naibu wake Mwana FA
 
Back
Top Bottom