Hapa nitapita kimya kimya kumuangalia binam kikaangoni!..🙂
Back then nakumbuka ID yako ilikuwa ni Caps zote (nahisi ile ID ulikuwa na madini zaidi ya hili). Baadae ukaaga kwamba unaaga kwamba unaachana na JF, baada ya muda sana ukarudi kwa ID hiyo hiyo ila ukabadilisha Caps kama inavyoonekana sasa.
Swali:
Asante.
- Ni kipi kilikuondoa JF?
- Kwa nini uliamua kurudi?
- In terms of giving and receiving hapa JF (knowledge wise), uzani unalalia wapi zaidi kwako? Do you give more or receive more?
- How would you rate JF (1 - 10) as a knowledge tool?
Msimamo wangu ni ule ule: tunahitaji mabadiliko makubwa sana kwenye mfumo wa elimu kama tunataka kwenda na kasi ya dunia.Mkuu Malcom Lumumba, unaionaje nchi yetu Tanzania, ndani ya miaka 20 ijayo hasa katika suala la elimu? Na unatoa mchango gani kuendeleza elimu ya nchi?
Moderator ndiyo aliweka majina madogo, mimi nilitaka MALCOM LUMUMBA.
Nini kiliniondoa na kunirudisha hapa JF: Naomba hili nilielezee siku nyingine mkuu.
Kuhusu kupata maarifa: JF kwangu ni chombo bora kabisa kwasababu huwa nafahamu nini watanzania wengi wasomi wanawaza.
Rating ya JF: Hapa naomba niipe JF 8,hizo mbili nawanyima kwasababu ya Credibility ya habari na vyanzo na siyo tatizo lao.
Swali gumu sana hili: Lakini ntajitahidi kujibu kwa kadiri ya uwezo wangu.
Nianze na matatizo, kuna suala zima la mabadiliko ya hali ya hewa, Ongezeko la watu duniani, Ukuaji wa teknolojia kubwa bila uwajibikaji wowote na Ongezeko la umasiki duniani. Haya yananiogopesha sana na yatakuja kuleta madhara makubwa sana.
Lakini napata matumaini kwasababu, siku hizi nguvu ya siasa ya dunia iko kwenye mikono ya taasisi za kimataifa (Power Devolution) na siyo nchi binafsi, hivyo ni rahisi sana kufanya mazungumzo na kuzuia matatizo ya kimataifa. UN ina udhaifu wake mkubwa lakini katika kufanya mambo mengine imesaidia sana, kama suala la elimu, wakimbizi, afya, kutatua majanga mbalimbali na mazungumzo. Tumekaa zaidi ya miaka 70 bila matatizo makubwa kwasababu ya UN, AU, ARAB LEAGUE bila kusingekuwa na mazungumzo kabisa na matatizo yangekuwa makubwa sana.
Pia upande mwingine teknolojia inaleta tumaini, genetic engineering inaweza kutuondolea kabisa magonjwa kama kansa na kumfanya mwanadamu aishi miaka mingi zaidi. Teknolojia mpya za anga zinatupa matumaini makubwa kwamba kuna siku wanadamu wanaweza wakaishi sayari nyingine,...
Haya machache....
Katiba mpya lazima ije mkuu, kama tunataka nchi itoke hapa ilipo. Wao wanasema mbona Marekani haijawahi kubadilisha katiba mimi nawaambia nyie ni waongo na hamjasoma sheria vizuri. Katiba siyo kitabu, katiba ni hali ya kisiasa (Political Situation) ambapo nchi inakuwa chini ya mfumo wa kisheria ambao unafahamika na raia wake kama ndiyo chombo cha kuongoza nchi. Hivyo baada ya kupata uhuru mwaka 1776 ile lose-confederacy ya Marekani ilikuwa inaongozwa na katiba ambayo haikuandikwa. Uingereza hawakutaka kuandika kwasababu waliona madhara ya kuwa na katiba ya kuandika. Haya ni mawazo ya Jaji Barnaba Samata na siyo mimi binafsi.Mkuu, unaona kuna haja ya Katiba Mpya hapa Tanzania? Kama jibu ni ndiyo, nini kifanyike kushindikiza serikali ilete katiba mpya??
Katiba mpya lazima ije mkuu, kama tunataka nchi itoke hapa ilipo. Wao wanasema mbona Marekani haijawahi kubadilisha katiba mimi nawaambia nyie ni waongo na hamjasoma sheria vizuri. Katiba siyo kitabu, katiba ni hali ya kisiasa (Political Situation) ambapo nchi inakuwa chini ya mfumo wa kisheria ambao unafahamika na raia wake kama ndiyo chombo cha kuongoza nchi. Hivyo baada ya kupata uhuru mwaka 1776 ile lose-confederacy ya Marekani ilikuwa inaongozwa na katiba ambayo haikuandikwa. Uingereza hawakutaka kuandika kwasababu waliona madhara ya kuwa na katiba ya kuandika. Haya ni mawazo ya Jaji Barnaba Samata na siyo mimi binafsi.
Hivyo Marekani ilibadilisha katiba kutoka ile isiyoandikwa na kuandika katiba mpya mwaka 1787, waliona umuhimu wa katiba mpya. Kwanini sisi tuogope mabadiliko ndugu yangu ????. Kinachochekesha ni kwamba katiba ya Marekani imepita leo, kesho yake ikapelekwa bungeni ifanyiwe marekebisho kwasababu watu walipinga baadhi ya vitu vya mle.
Kuna mengi sana ya kuyabadilisha kwenye hii nchi ndugu yangu, hasahasa kuweka miiko mipya kwa Raisi wa nchi, Bunge na Mahakama. Kuna vitu hii mihimili inatakiwa ibadilishiwe...
Asante for a comprehensive answer! Mkuu, unasema kuwa "siku hizi nguvu ya siasa ya dunia iko kwenye mikono ya taasisi za kimataifa (Power Devolution) na siyo nchi binafsi" lakini the trend around the world is getting more nationalistic. USA kuna Trump na Make America Great Again na anapuuziya maswala ya climate change, China is also flexing its military muscles in the South China Sea, etc. Is there a way to stop countries with narrow, nationalistic policies from endangering 'global stability'?
sasa nakuelewa.hongera mkuuuMimi ni Mwanasheria japo sasa nimesoma tofauti kidogo katika huo usomaji wangu wa sheria.
Nimejikita katika masomo ya Uchumi wa Kimataifa (International Economics Law), Sheria za Kimataifa (International Law), Sheria za Vita (International Humanitarian Law), Sheria za makosa ya jinai ya kimataifa (International Criminal Law), Haki za Binadamu (International Human Rights Law), Masomo ya Sheria za Wakimbizi (Immigration and Refugee Law), Sheria za Anga na Usafirishaji (Aviation Law), Sheria za Umoja wa Ulaya (European Union Law), Sheria za Uwekezaji (Investment Law)na mengineyo mengiii...........................
Kwanza kabisa World Economic Forum siyo chombo ambacho kinaendesha Uchumi wa Dunia, ni Forum kwa ajili ya mazungumzo mbalimbali ya kiuchumi. Lakini upande wa pili sasa, nadhani sisi Afrika tupambane na GATT na TRIPS ambavyo vinatuhusu moja kwa moja. Tupambane na mikataba ya kimataifa ya uwekezaji kwenye hii Forum hata tusipokwenda haidhuru sana kwasababu wenye sauti ni matajiri.Uchumi wa Kimataifa (International Economics Law)
• Unahisi Afrika inatendewa haki kwenye mikutano ya Davos au tunaenda kama wasindikizaji?.
Sheria za Kimataifa (International Law)
Katika mikataba ya kimataifa ambayo siipendi basi ni hii ifuatayo:• Ni sheria ipi kandamizi kwa mataifa ya kiafrica inayotumika sana.
Sheria za makosa ya jinai ya kimataifa (International Criminal Law)
Kilichotokea Crimea kinaangukia sanasana kwenye Public International Law na siyo International Criminal Law. International Criminal Law inahusika na uhalifu wa kivita wa mtu moja moja. Sasa kimtazamo wa kisheria, kitendo cha Vladmir Putin kuvamia Crimea kijeshi ni Act of Aggression ambacho ni kinyume kabisa na Mkataba wa Kimataifa uitwao The Kellog-Briand Pact wa mwaka 1927 unaozuia nchi kutumia vita kama sera ya nchi. Lakini upande wa pili wametumia sheria ya kimataifa hiyohiyo kujistify Aggression kwa kutumia The Principle of Self-Determination kwa kufanya referendum.• Nini mtizamo wako kilichotokea crimea.
Haki za Binadamu (International Human Rights Law)
LGBT siyo haki za binadamu: Kitafsiri haki za binadamu ni "Inherent entitlements that enable human beings to develop certain faculties". The right to life develops faculties like happiness and prosperity, what does homesexuality develop ??? (Nothing)• Nini mtazamo wako kuhusu LGBT Tanzania.
Sheria za Umoja wa Ulaya (European Union Law)
Kihistoria Charles De Gaulle wa Ufaransa hakutaka kabisa Uingereza iingie kwenye Umoja wa Ulaya kipindi hicho unaitwa The European Economic Community. Uingereza wenyewe hawakutaka kuingia kwenye ule umoja hadi Winston Churchill akasema hivi "I love the French and Belgiums, but we must not allow ourselves to be pulled down to that level" Uingereza wao walianzisha The European Free Trade Area lakini baada ya kuona Umoja wa Ulaya unapiga hatua ndiyo akaamua kujiunga nao, alituma maombi mara ya kwanza wakamkatalia, alikuja kuruhusiwa baada ya Charles De Gaulle kutoka mwaka 1969.• Unaiongeleaje Brexit!, upo upande upi?
Mkuu mala ya kwanza kujiunga Jf nilijiita Mzizi mkavu baada ya kugundua kwamba id ziko duplicated niliwaomba mod wanibadili na kuniita Zero iQ, ukiniuliza uliwaza nini kujiita hivyo sina jibu kwa sababu ilikuja AutomaticNa mimi nina swali kwa mtoa mada,ID yangu ya kwanza nilipoingia JF nilikuwa najiita ZERO IQ mwaka 2013 badaye niliibadilisha.Je kwa ww ni kitu gani kilicho kuvutia hadi kutumia ID hiyo?
Checks and Balances ni Legal Theory ambayo ina supplement the set backs kwenye The Doctrine of Separation of Powers. Hivyo ungeanza na kuuliza kwamba: Je, nchini kwetu kuna Separation of Powers ??? kinadharia na kiutendaji ipo nusu-nusu (Partial). Maana kipindi cha watu kama wakina Mzee Nyalali na Samata ulikuwa husikii serikali na mahakama vinavutana na kila mtu alijua mipaka yake. Japo kuna sehemu Nyerere alishawahi kuwavamia majaji ofisini kwao na kunyang'anya mafaili na hata kuwatishia lakini yote tisa kulikuwa na mipaka sana. Lakini sasa siku zinavyoenda hata Separation of Powers inakuwa ni Myth tu ndiyo maana nasema tuweka mipaka ya Raisi kupitia katiba mpya.Nisamehe narudi mara kwa mara na maswali, lakini majibu yako, mkuu, yananisisimua! Kwenye katiba ya marekani kuna 'checks and balances' ambayo inamzuia mwenye mamlaka kutumia mamlaka vibaya. Je, katiba yetu ya sasa inayo hizi "checks and balances'???!
Ok but kwa mie kuna wimbo wa mabeste unaitwa chupa moja nilikuwa naupenda na katika mistari yake ali mention neno IQ zero akiwa na maana baada ya kulewa chupa moja ya bia akaona kila kitu ni sawa.Mkuu mala ya kwanza kujiunga Jf nilijiita Mzizi mkavu baada ya kugundua kwamba id ziko duplicated niliwaomba mod wanibadili na kuniita Zero iQ, ukiniuliza uliwaza nini kujiita hivyo sina jibu kwa sababu ilikuja Automatic
Sent using Jamii Forums mobile app
Siku hizi haupo kabisa, na ulikuwa ni utamaduni ambao tuliiga kutoka kwa waingereza tu. Siku hizi hata ukiingia chambers unakutaka na Jaji kavaa shati la Batiki na hana shida, mimi nilibaki nacheka sana tu. Japo nisema kabisa suala zima la Legal Practice sijahusika nalo kwa muda mrefu sana, mimi nahusika na Research na mambo mengineyoMkuu, nashukuru sana kwa kunijuza mambo mengi kwa undani! Swali langu la mwisho: Sijawahi kufika mahakamani, lakini kwenye movies nawaona majaji na mawakili wakiwa wamevaa mawigi (wanasema ni nyewele ya kondoo). Je, utaratibu huu upo hapa kwetu na ni nini sababu ya kuvaa mawigs (kuficha upara???) Asante sana na usiku mwema, mkuu Malcom Lumumba!