JF Photo Library: Mada maalum ya Picha za Zamani

Aiseee

Imetrend kumbe wamemkumbuka???

NJE YA MADA

Embu anayejua aniambie kuhusu Aina Maheda huyu mdada bibi mrembo wa wakati huo ilikuaje kuhusu maisha yake na sasa yuko wapi?
Mara baada ya kushinda taji hilo na kumaliza mwaka wake mmoja wa kazi za jamii, alipata ofa mbalimbali za kufanya kazi za mitindo nchini Afrika ya Kusini, na hatimaye kuhamia huko na kuishi huko kwa karibu miaka 10 ambapo aliweza kupata marafiki wa jinsia mbalimbali na kutokana na marafiki hao aliweza kupata mchumba Bwana Jean P. Guyeu, raia wa Ufaransa aliyekuwa akifanya kazi zake nchini Afrika ya Kusini. Mrembo huyo akiwa na mchumba wake huyo hatimaye walikuja nyumbani nchini Tanzania kufunga ndoa ambayo ilihudhuriwa na watu mbalimbali wakiwemo wajumbe wa Kamati ya Miss Tanzania . Kamati inayoendesha Mashindano ya urembo nchini iliyomuwezesha kumfikisha hapo alipo mrembo linda Maeda. Kwa sasa mrembo Aina na mume wake wanaishi jijini Cape Town, Afrika ya Kusini.
 
Huyu muhenga anaitwa oliver ngoma, alizaliwa mwaka 1959, gabon, alianza kutamba miaka ya 1989 na ngoma zake kama Adia, ngé, bane, ktk miondoko ya zouk (zuku) na sukuz, nkView attachment 2031159
Miaka ya 90 watu walipenda sana kuweka ngoma zake wakiwa safarini, zile costa za Dar - Tanga ilikuwa balaa....yaani unalala kabisa vile vimlima vya segera segera
 
by the time anapouwa miss mimi nilikuwa sina uchumi, kijana mdogo.... ila nilimpenda sana huyu binti ila yeye hakujua tu... ningemuoa
 
Hizi picha zako mkuu ukiziangalia aisee kuna mahali tulikwama [emoji3]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…