TUMKUMBUKE MWANAMUZIKI PEPE KALLE
Mnamo Novemba 30, 1951 katika Jiji la LeopordVille kwa sasa{KINSHASA} huko Kongo ya Mbelgiji kwa sasa {Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo} alizaliwa mtoto aliyepewa jina la Kabasele Yampanya.
Alikuwa mtunzi, mwimbaji wa muziki wa soukous na kiongozi wa bendi ya Empire Bakuba. Pepe Kale aka Tembo Jitu la Miraba Minne alikuwa bingwa wa miondoko ya soukous na kiongozi wa bendi ya Empire Bakuba, ambayo ilikuwa maarufu katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Watanzania wengi tutaendelea kumkumbuka mwanamuziki huyu hasa wakati alipokuja nchini mwetu na kutikisa majiji ya Arusha, Dar es Salam na Mbeya.
Wakati wa ujio wake hapa Tanzania, Pepe Kalle ambaye sauti yake ilikuwa nyembemba na nyororo, alifuatana na wanamuziki akiwemo mipiga wa gita la besi Lofombo na waimbaji akina Papy Tax, Dilu Dilumona na Djo Djo Ikomo.
Pepe Kalle aliyefariki Novemba 28, 1998 kwa ugonjwa wa moyo akiwa na umri wa miaka 47.
View attachment 2743695
Sent using
Jamii Forums mobile app