JF Photo Library: Mada maalum ya Picha za Zamani

JF Photo Library: Mada maalum ya Picha za Zamani

b2598f4a06d50d61a268ad342d46faae.jpg
 
Kulia kwangu ni mshindi wa Medali ya Shaba katika Ndondi kwenye All African Games mwaka 1978 Algiers nchini Algeria, Lucas Msomba. Kwa sasa Msomba, baadaye refa maarufu wa ngumi za kulipwa anaumwa na amekatwa mguu. Yupo Kibaha kwa Mathias, eneo linaitwa Jamaica ndio amejenga huko na anaishi huko. Kwa wadau wa boxing, atakayeguswa na ana nia ya kumsaidia anichek DM.
FB_IMG_1708713412961.jpg
 
Arusha hiyo miaka ya 60. Naiona mbele hapo Peugeot 403 Familly ikizunguka hapo kwa utulivu sana na gereji ya SUBZALI hapo kwenye kona. Hapo kulikuwa na makutaniko ya barabara tatu, yaani Babati Road, Ngoliondoi Road na Sokoine Road, ila kama kuna mabadiliko basi tukumbushane. Karibu sana.
FB_IMG_1708887225407.jpg
 
Timu ya Taifa ya Uganda, Uganda the Cranes ilipotembelea Uingereza mwaka 1956. Jamaa aliyeonyeshwa kwa alama ya mshale aliamua kuingia kifusi akapata Chuo huko na baadaye kusoma vyuo vingine vingi. Alikuwa Mwafrika wa kwanza kutoroka akiwa ziara za michezo. Mwaka 1966 aliandika kitabu maarufu sana kiitwacho “The song of Lawino”. Huyo ndiye mwandishi nguli aliyeitwa Okot p’Bitek. Picha hii ni ya taasisi ya Juba Fastlinks Investments
FB_IMG_1709202793295.jpg
 
Back
Top Bottom