Jicho la kisheria kuhusu uhalali wa barua ya Spika Ndugai kujiuzulu

Jicho la kisheria kuhusu uhalali wa barua ya Spika Ndugai kujiuzulu

achana na C in C huyo ndo kwaheri ya kuonana.
barua ikosewe au ipatiwe keshaambiwa Hana chake
 
Sio HATAKI huyo kaambiwa na Mama.
Kwa akili za ndugai ulitegemea atajiuzulu mwenyewe?
Hakuwa hata na Hilo wazo.mama.kapiga msumali wa mwisho OUT.
Anaonekana ni msaliti maana serikali na bunge lao ni MOJA.
Sasa Leo ndugai anataka kuacha kula nyama za watu lazma atanyooshwa tu
Ngugai hataki tena hiyo kazi....
Hawezi kubadili tena kinachoendelea...
Sheria ina upande wake...
 
Hivyobasi, nakubaliana na wote wanaotoa maoni ya kisheria kuwa barua/taarifa ya Spika Job Yustino Ndugai ya kujiuzulu kwake haikuwa halali. Anapaswa kuandika, kusaini na kuwasilisha taarifa yake kwa mujibu wa Katiba. Katibu Mkuu wa CCM, namshauri, kujiweka mbali na mtego huu wa kikatiba. Ingekuwa sahihi kuandikiwa Katibu Mkuu wa CCM kama Ndugai angetaka kuachia uanachama wake wa CCM.
Naunga mkono hoja kwa asilimia 100% chini ya mia.
P
 
Naunga mkono hoja kwa asilimia 100% chini ya mia.
P
Asante kaka Pascal
 
Nikiri wazi kuwa nami, nikiwa mtanzania wa kawaida na mfuatiliaji mzuri wa mambo ya kisiasa na kijamii, nimekuwa nikifuatilia kwa ukaribu sakata lililopelekea Spika Job Yustino Ndugai kuandika barua ya kujiuzulu nafasi yake ya Spika. Nimefuatilia pia mjadala ulioibuka kuhusu uhalali wa barua yake ya kujiuzulu Uspika. Kama Msomi wa sheria (neno lililokuwa likimkwaza Mjiuzulu) nawiwa kuchangia katika hoja hii.

Nimepata fursa, ingawa si kubwa sana, kupitia Ibara za Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sura Nambari 2 ya Sheria za Nchi yetu (Katiba) na Kanuni za Kudumu za Bunge (Toleo la 2016) ili kuona utaratibu wa kufuatwa pale Spika anapotaka kujiuzulu. Nimepitia nyaraka hizi kwakuwa ndizo hasa zinazounda na kuendesha Bunge kwa kiwango kikubwa. Kanuni tajwa za Bunge zimetungwa chini ya Ibara ya 89 ya Katiba.

Nilianza na Kanuni za Kudumu za Bunge. Neno 'kujiuzulu' limetajwa mara sita kwenye Kanuni husika. Ni kuhusu maazimio ya kuwaondoa madarakani Rais, Makamu wa Rais, Spika na Naibu Spika. Kuhusiana na Spika, kujiuzulu kwake kunaelezwa kwenye Kanuni ya 137 Fasili ya 6. Ni pale ambapo Spika anajiuzulu kabla ya uamuzi wa hoja ya Bunge ya kumuondoa madarakani. Namna ya kujiuzulu huku, kwa mujibu wa Kanuni na Fasili tajwa ni kutoa maelezo yake Bungeni. Kimsingi, ni wakati wa kikao cha Bunge. Kwa Ndugai hakukuwa na hoja ya aina hiyo.

Kanuni za Bunge hazisemi wala hazitoi utaratibu wowote wa namna ya kujiuzulu kwa Spika pale ambapo hakuna hoja ya kumuondoa madarakani ndani ya Bunge kwa mujibu wa Kanuni ya 137 nzima. Lakini, Katiba inatoa majibu. Ibara ya 149, Ibara Ndogo ya 1 kifungu (c) inamtaka Spika anayetaka kujiuzulu kuwasilisha taarifa yake ya maandishi aliyoitia saini yake kwenye Bunge. Kwangu mimi, 'kwenye Bunge' kunamaanisha kwa Mtendaji Mkuu katika Ofisi ya Bunge ambaye ni Katibu wa Bunge kwa mujibu wa Ibara ya 87, Ibara ndogo ya 2.

Kwakuwa Kanuni za Bunge ziko kimya kuhusu utaratibu wa Spika kujiuzulu bila ya uwepo wa hoja ya kumuondoa madarakani Bungeni, matakwa ya Katiba LAZIMA yatimizwe. Ndiyo kusema, taarifa ya kujiuzulu kwa Spika LAZIMA iwasilishwe kwa Katibu wa Bunge na si vinginevyo. Si sawa wala sahihi kwa Spika kuwasilisha taarifa ya kujiuzulu kwake kwa Katibu Mkuu wa CCM badala ya Katibu wa Bunge. Haikuwa sahihi pia Katibu wa Bunge kunakiliwa TU barua husika.

Hivyobasi, nakubaliana na wote wanaotoa maoni ya kisheria kuwa barua/taarifa ya Spika Job Yustino Ndugai ya kujiuzulu kwake haikuwa halali. Anapaswa kuandika, kusaini na kuwasilisha taarifa yake kwa mujibu wa Katiba. Katibu Mkuu wa CCM, namshauri, kujiweka mbali na mtego huu wa kikatiba. Ingekuwa sahihi kuandikiwa Katibu Mkuu wa CCM kama Ndugai angetaka kuachia uanachama wake wa CCM.


Hii ni nzuri kwa wapenda drama za siasa na sheria. Kwa sisi wadau wa kimaendeleo na demokrasia spika Ndugai harudi kuwa spika hivyo tufikirie mbele badala ya kupoteza muda na kitu ambacho tunajua kitaishia hapo🤔
 
Nikiri wazi kuwa nami, nikiwa mtanzania wa kawaida na mfuatiliaji mzuri wa mambo ya kisiasa na kijamii, nimekuwa nikifuatilia kwa ukaribu sakata lililopelekea Spika Job Yustino Ndugai kuandika barua ya kujiuzulu nafasi yake ya Spika. Nimefuatilia pia mjadala ulioibuka kuhusu uhalali wa barua yake ya kujiuzulu Uspika. Kama Msomi wa sheria (neno lililokuwa likimkwaza Mjiuzulu) nawiwa kuchangia katika hoja hii.

Nimepata fursa, ingawa si kubwa sana, kupitia Ibara za Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sura Nambari 2 ya Sheria za Nchi yetu (Katiba) na Kanuni za Kudumu za Bunge (Toleo la 2016) ili kuona utaratibu wa kufuatwa pale Spika anapotaka kujiuzulu. Nimepitia nyaraka hizi kwakuwa ndizo hasa zinazounda na kuendesha Bunge kwa kiwango kikubwa. Kanuni tajwa za Bunge zimetungwa chini ya Ibara ya 89 ya Katiba.

Nilianza na Kanuni za Kudumu za Bunge. Neno 'kujiuzulu' limetajwa mara sita kwenye Kanuni husika. Ni kuhusu maazimio ya kuwaondoa madarakani Rais, Makamu wa Rais, Spika na Naibu Spika. Kuhusiana na Spika, kujiuzulu kwake kunaelezwa kwenye Kanuni ya 137 Fasili ya 6. Ni pale ambapo Spika anajiuzulu kabla ya uamuzi wa hoja ya Bunge ya kumuondoa madarakani. Namna ya kujiuzulu huku, kwa mujibu wa Kanuni na Fasili tajwa ni kutoa maelezo yake Bungeni. Kimsingi, ni wakati wa kikao cha Bunge. Kwa Ndugai hakukuwa na hoja ya aina hiyo.

Kanuni za Bunge hazisemi wala hazitoi utaratibu wowote wa namna ya kujiuzulu kwa Spika pale ambapo hakuna hoja ya kumuondoa madarakani ndani ya Bunge kwa mujibu wa Kanuni ya 137 nzima. Lakini, Katiba inatoa majibu. Ibara ya 149, Ibara Ndogo ya 1 kifungu (c) inamtaka Spika anayetaka kujiuzulu kuwasilisha taarifa yake ya maandishi aliyoitia saini yake kwenye Bunge. Kwangu mimi, 'kwenye Bunge' kunamaanisha kwa Mtendaji Mkuu katika Ofisi ya Bunge ambaye ni Katibu wa Bunge kwa mujibu wa Ibara ya 87, Ibara ndogo ya 2.

Kwakuwa Kanuni za Bunge ziko kimya kuhusu utaratibu wa Spika kujiuzulu bila ya uwepo wa hoja ya kumuondoa madarakani Bungeni, matakwa ya Katiba LAZIMA yatimizwe. Ndiyo kusema, taarifa ya kujiuzulu kwa Spika LAZIMA iwasilishwe kwa Katibu wa Bunge na si vinginevyo. Si sawa wala sahihi kwa Spika kuwasilisha taarifa ya kujiuzulu kwake kwa Katibu Mkuu wa CCM badala ya Katibu wa Bunge. Haikuwa sahihi pia Katibu wa Bunge kunakiliwa TU barua husika.

Hivyobasi, nakubaliana na wote wanaotoa maoni ya kisheria kuwa barua/taarifa ya Spika Job Yustino Ndugai ya kujiuzulu kwake haikuwa halali. Anapaswa kuandika, kusaini na kuwasilisha taarifa yake kwa mujibu wa Katiba. Katibu Mkuu wa CCM, namshauri, kujiweka mbali na mtego huu wa kikatiba. Ingekuwa sahihi kuandikiwa Katibu Mkuu wa CCM kama Ndugai angetaka kuachia uanachama wake wa CCM.

Upo uwezekano mkubwa kuwa hiyo barua ni fake, lakini mwenyewe ameamua kuliacha hili swala liende hivyo hivyo kuepuka kuendeleza mvurugano!
 
Nchi ya hovyo sana hii... halafu Chongolo kwa umbumbumbu wake akaaja front kusema kapokea barua ambayo haikufuata utaratibu. Huenda hii barua imeandikwa na maccm yenyewe ili kumfurahisha mwenyekiti.
Chongolo kupokea na kutoa taarifa ni sawa kwa upande wa chama.
Hata hivyo, katiba haihusishi chama kwenye mchakato huu. Mambo yanayohusu mihimili ya dola au serikali lazima katiba ifuatwe na kuheshimiwa.
 
Nchi ya hovyo sana hii... halafu Chongolo kwa umbumbumbu wake akaaja front kusema kapokea barua ambayo haikufuata utaratibu. Huenda hii barua imeandikwa na maccm yenyewe ili kumfurahisha mwenyekiti.

Kuna chance kubwa kwamba hiyo barua kweli ni ya CCM wenyewe!
 
Nakumbuka na wewe ni mmoja ya watu mliosalimu amri mbele ya jiwe na kuanza kuandika ugoro humu kama kuku aliyekatwa kichwa..
Back to the topic umedadavua vizuri kisheria ila uwege na misimamo na sio kutikiswa kidogo unaikimbia familia.
Hilo jamaa ni mwanasheria jinga Sana kuwahi tokea Kama ni kweli mwanasheria
 
Nashauri serikali isije kukosea ikamlipa mafao ya u-spika.
Huyu mtu ameondoka kwa kashfa na hajamaliza muda wake!
Tusitumie vby fedha za walipa kodi jamani, ale vihela vya ubunge vinamtosha!
Mbona hujahoji kiasi gani kimetumika kuandaa video royal tour au zile zilizotumika sherehe ya Uhuru mwezi uliopita wakati tuna shida kibao hapa nchini pamoja na watoto nusu waliochaguliwa kwenda chuo kikuu kukosa mikopo
 
Watanzania na dunia mzima inajua kwamba Ndugai kajiuzulu uspika. Hiyo ndo fact. We ukatae ni shauri yako na hakuna kitacho badilika. Huo ndo ukweli. Lakini kama ni school/academic discussion haya!
Mawazo ya watu wanaofanya mambo kiholela holela. Watu wasioamini ktk taratibu na sheria. Ili mradi liende.

Yote hii kukosa elimu hata ile ya kufuta ujinga.
 
Majivuno ndio yamemuangusha. Huwezi kusema " mama yenu juzi hapa kaenda kukopa" wakati huo mkopo ulipitia kwenye kamati ya bunge. Ndugai anatafuta maslahi ya kisiasa Kama angekuwa mkweli asingekubali pesa za walipa Kodi ziwalipe wabunge wasiokuwa na sifa.
Tutajuaje ikiwa kama hata hiyo kamati ya Bunge ilishinikizwa kukubali huo mkopo, na Job akajawa presha kisha 'kuropoka'?
 
Hilo jamaa ni mwanasheria jinga Sana kuwahi tokea Kama ni kweli mwanasheria
Mkuu hadi leo huamini kuwa mimi ni Mwanasheria? Halafu, chuki zako kwangu zinatokana na nini hasa? Utakuja kufa kwa roho mbaya mkuu
 
Mawazo ya watu wanaofanya mambo kiholela holela. Watu wasioamini ktk taratibu na sheria. Ili mradi liende.

Yote hii kukosa elimu hata ile ya kufuta ujinga.
Kama ndugai hakufuata taratibu ya kujiuzulu anaweza poteza mafao yake. Ila tarajia spika mpya muda si mrefu ujao.
 
Siamtume hata bodaboda akaichukue kutoka Kwa katibu wa ccm,ipelekwe huko Kwa katibu wa bunge? kwani shida Iko wapi?
 
Kilichofanyika ni sahihi kikatiba..👇👇
Kinachotakiwa kupelekwa ni "TAARIFA iliyo sainiwa"...Taarifa yaweza kuwa BARUA/NAKALA YA BARUA/PRESS RELEASE n.k.

SURA YA KUMI NA MOJA
149(1)
(C)Iwapo mtu huyo ni Spika au Naibu Spika wa Bunge basi taarifa hiyo ya kujiuzulu ataiwasilisha kwenye Bunge.
 
Nikiri wazi kuwa nami, nikiwa mtanzania wa kawaida na mfuatiliaji mzuri wa mambo ya kisiasa na kijamii, nimekuwa nikifuatilia kwa ukaribu sakata lililopelekea Spika Job Yustino Ndugai kuandika barua ya kujiuzulu nafasi yake ya Spika. Nimefuatilia pia mjadala ulioibuka kuhusu uhalali wa barua yake ya kujiuzulu Uspika. Kama Msomi wa sheria (neno lililokuwa likimkwaza Mjiuzulu) nawiwa kuchangia katika hoja hii.

Nimepata fursa, ingawa si kubwa sana, kupitia Ibara za Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sura Nambari 2 ya Sheria za Nchi yetu (Katiba) na Kanuni za Kudumu za Bunge (Toleo la 2016) ili kuona utaratibu wa kufuatwa pale Spika anapotaka kujiuzulu. Nimepitia nyaraka hizi kwakuwa ndizo hasa zinazounda na kuendesha Bunge kwa kiwango kikubwa. Kanuni tajwa za Bunge zimetungwa chini ya Ibara ya 89 ya Katiba.

Nilianza na Kanuni za Kudumu za Bunge. Neno 'kujiuzulu' limetajwa mara sita kwenye Kanuni husika. Ni kuhusu maazimio ya kuwaondoa madarakani Rais, Makamu wa Rais, Spika na Naibu Spika. Kuhusiana na Spika, kujiuzulu kwake kunaelezwa kwenye Kanuni ya 137 Fasili ya 6. Ni pale ambapo Spika anajiuzulu kabla ya uamuzi wa hoja ya Bunge ya kumuondoa madarakani. Namna ya kujiuzulu huku, kwa mujibu wa Kanuni na Fasili tajwa ni kutoa maelezo yake Bungeni. Kimsingi, ni wakati wa kikao cha Bunge. Kwa Ndugai hakukuwa na hoja ya aina hiyo.

Kanuni za Bunge hazisemi wala hazitoi utaratibu wowote wa namna ya kujiuzulu kwa Spika pale ambapo hakuna hoja ya kumuondoa madarakani ndani ya Bunge kwa mujibu wa Kanuni ya 137 nzima. Lakini, Katiba inatoa majibu. Ibara ya 149, Ibara Ndogo ya 1 kifungu (c) inamtaka Spika anayetaka kujiuzulu kuwasilisha taarifa yake ya maandishi aliyoitia saini yake kwenye Bunge. Kwangu mimi, 'kwenye Bunge' kunamaanisha kwa Mtendaji Mkuu katika Ofisi ya Bunge ambaye ni Katibu wa Bunge kwa mujibu wa Ibara ya 87, Ibara ndogo ya 2.

Kwakuwa Kanuni za Bunge ziko kimya kuhusu utaratibu wa Spika kujiuzulu bila ya uwepo wa hoja ya kumuondoa madarakani Bungeni, matakwa ya Katiba LAZIMA yatimizwe. Ndiyo kusema, taarifa ya kujiuzulu kwa Spika LAZIMA iwasilishwe kwa Katibu wa Bunge na si vinginevyo. Si sawa wala sahihi kwa Spika kuwasilisha taarifa ya kujiuzulu kwake kwa Katibu Mkuu wa CCM badala ya Katibu wa Bunge. Haikuwa sahihi pia Katibu wa Bunge kunakiliwa TU barua husika.

Hivyobasi, nakubaliana na wote wanaotoa maoni ya kisheria kuwa barua/taarifa ya Spika Job Yustino Ndugai ya kujiuzulu kwake haikuwa halali. Anapaswa kuandika, kusaini na kuwasilisha taarifa yake kwa mujibu wa Katiba. Katibu Mkuu wa CCM, namshauri, kujiweka mbali na mtego huu wa kikatiba. Ingekuwa sahihi kuandikiwa Katibu Mkuu wa CCM kama Ndugai angetaka kuachia uanachama wake wa CCM.
Hakuna utawala wa sheria katika nchi hii. Kuna wizara ya katiba na sheria, inayotakiwa kuangalia maswala kama hayo. Tangu enzi za Magufuli, katiba na sheria nyingi zimevunjwa, wao wanaupiga usingizi. Ndugai speaker wa binge linalo tunga sheria, hana muda kupitia sheria hata inayosimamia analotaka kulitenda binafsi!
 
Samahani mkuu. Wewe hiyo barua umeiona wapi? Maana sote tumeona press release ila barua ya kujiuzulu haijawekwa hadharani

Jambo la pili umekubali kuwa kanuni za bunge ziko kimya; je ni wapi ktk katiba ilipoandikwa spika anatakiwa kuandika barua yenye saini na ielekezwe kwa katibu?

Mimi nilichoona katiba imesema spika atoe taarifa ktk bunge; bunge limekiri kupata taarifa ya kujiuzulu kwake. Kwa msingi huo utaratibu umezingatiwa. Suala la kumwandikia katibu wa chama chake ni hiyari yake
Nikiri wazi kuwa nami, nikiwa mtanzania wa kawaida na mfuatiliaji mzuri wa mambo ya kisiasa na kijamii, nimekuwa nikifuatilia kwa ukaribu sakata lililopelekea Spika Job Yustino Ndugai kuandika barua ya kujiuzulu nafasi yake ya Spika. Nimefuatilia pia mjadala ulioibuka kuhusu uhalali wa barua yake ya kujiuzulu Uspika. Kama Msomi wa sheria (neno lililokuwa likimkwaza Mjiuzulu) nawiwa kuchangia katika hoja hii.

Nimepata fursa, ingawa si kubwa sana, kupitia Ibara za Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sura Nambari 2 ya Sheria za Nchi yetu (Katiba) na Kanuni za Kudumu za Bunge (Toleo la 2016) ili kuona utaratibu wa kufuatwa pale Spika anapotaka kujiuzulu. Nimepitia nyaraka hizi kwakuwa ndizo hasa zinazounda na kuendesha Bunge kwa kiwango kikubwa. Kanuni tajwa za Bunge zimetungwa chini ya Ibara ya 89 ya Katiba.

Nilianza na Kanuni za Kudumu za Bunge. Neno 'kujiuzulu' limetajwa mara sita kwenye Kanuni husika. Ni kuhusu maazimio ya kuwaondoa madarakani Rais, Makamu wa Rais, Spika na Naibu Spika. Kuhusiana na Spika, kujiuzulu kwake kunaelezwa kwenye Kanuni ya 137 Fasili ya 6. Ni pale ambapo Spika anajiuzulu kabla ya uamuzi wa hoja ya Bunge ya kumuondoa madarakani. Namna ya kujiuzulu huku, kwa mujibu wa Kanuni na Fasili tajwa ni kutoa maelezo yake Bungeni. Kimsingi, ni wakati wa kikao cha Bunge. Kwa Ndugai hakukuwa na hoja ya aina hiyo.

Kanuni za Bunge hazisemi wala hazitoi utaratibu wowote wa namna ya kujiuzulu kwa Spika pale ambapo hakuna hoja ya kumuondoa madarakani ndani ya Bunge kwa mujibu wa Kanuni ya 137 nzima. Lakini, Katiba inatoa majibu. Ibara ya 149, Ibara Ndogo ya 1 kifungu (c) inamtaka Spika anayetaka kujiuzulu kuwasilisha taarifa yake ya maandishi aliyoitia saini yake kwenye Bunge. Kwangu mimi, 'kwenye Bunge' kunamaanisha kwa Mtendaji Mkuu katika Ofisi ya Bunge ambaye ni Katibu wa Bunge kwa mujibu wa Ibara ya 87, Ibara ndogo ya 2.

Kwakuwa Kanuni za Bunge ziko kimya kuhusu utaratibu wa Spika kujiuzulu bila ya uwepo wa hoja ya kumuondoa madarakani Bungeni, matakwa ya Katiba LAZIMA yatimizwe. Ndiyo kusema, taarifa ya kujiuzulu kwa Spika LAZIMA iwasilishwe kwa Katibu wa Bunge na si vinginevyo. Si sawa wala sahihi kwa Spika kuwasilisha taarifa ya kujiuzulu kwake kwa Katibu Mkuu wa CCM badala ya Katibu wa Bunge. Haikuwa sahihi pia Katibu wa Bunge kunakiliwa TU barua husika.

Hivyobasi, nakubaliana na wote wanaotoa maoni ya kisheria kuwa barua/taarifa ya Spika Job Yustino Ndugai ya kujiuzulu kwake haikuwa halali. Anapaswa kuandika, kusaini na kuwasilisha taarifa yake kwa mujibu wa Katiba. Katibu Mkuu wa CCM, namshauri, kujiweka mbali na mtego huu wa kikatiba. Ingekuwa sahihi kuandikiwa Katibu Mkuu wa CCM kama Ndugai angetaka kuachia uanachama wake wa CCM.
Y
 
Mm binafsi naona tatizo co ktb au sheria tatizo ni utashi wa viongozi mf ktb iliyopo ni mara ngapi tunaona viongozi wakiivunja?hatua8 zipi zimechukuliwa au nani kakemee bussines as usual wt wanaapa kuilinda na kuitetea ktb lakini hao hao ndio wanaivunja na sheria zo wazi ukivunja ktb unatakiwa ufukuzwe kazi lakini nani kafukuzwa sbb hakuna anayejali hivyo ata tukiwa na ktb mpya nani atailinda na kuitetea jama viongoz ni walewale wasiokuwa na utashi wananchi tunatakiwa tuwe watetezi tukiona kuingoz anavunja jtb tuseme no
No, tena no kubwa. Viongozi wa Tanzania wamejipa uungu mtu, wamejitungia sheria hawagusiki. Hatuna uwezo wa kuwashitaki kwa upotofu wowote watakao ufanya. Lakini uwezo wa kuwazomea hata tukiwa gizani huo tunao. Tuwambie no, tena no kubwa.
 
Back
Top Bottom