Jifunze kilimo cha nyanya

Shukrani mkuu kwa maelezo yaliyonyooka japo jina lako ni Yumbayumba. Ngoja nikusanye nguvu ili nami nianze kulima hiyo nyanya inayoitwa Asila, kwa sasa wacha kwanza nikomae na hizi mbegu za kawaida maana hii Asila itanitoa Damu.
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji85][emoji85] jina lisikubabaishe mkuu, sawa mkuu ww jipange tu
 
Shukrani mkuu kwa maelezo yaliyonyooka japo jina lako ni Yumbayumba. Ngoja nikusanye nguvu ili nami nianze kulima hiyo nyanya inayoitwa Asila, kwa sasa wacha kwanza nikomae na hizi mbegu za kawaida maana hii Asila itanitoa Damu.

Hapana unakosea usilime eneo kubwa mapato kidogo anza na eneo dogo upate zaidi,hata robo eka inatosha kuanzia,lima mbegu bora maana mbegu bora mmea mmoja ni kg10 wala hizi za kawaida mmea mmoja ni kg3 sasa huoni eneo kubwa la hizi za kawaida mavuno unapata kwenye eneo dogo,ekari moja ya za kawaida inapitwa mavuno na robo ekari ya nyanya bora
 

Dahh! Aisee umenipa mwanga zaidi, kumbe unaweza kuta mazao ninayopata katika hekari mbili kwa kutumia mbegu ya kawaida kwa mbegu ya kisasa ni sawa na Nusu heka.
 

kwahy mkuu unapendekeza mbegu gani?
 
mkuu nahitaji kwenda nunua mbegu ya nyanya kesho kkoo,,embu nitofautishie mbegu za kawaida na za kisasa zinakuwaje?

Nitashkuru ukinisaidia kuniorodheshea list ya mbegu za kisasa na bei zake

nalimia maeneo ya kimbiji dsm

Ahsante.
 
Mbegu za kisasa zipo nyingi sn tafuta ambayo una uwezo nayo si lazima asila
Mkuu naomba nisaidie atleast majina 5 ya mbegu za kisasa na bei zake,,nahitaji kwenda kuchkua kesho

Na nitajuaje hii ni ya kisasa au ni ya kawaida?
 
Mkuu naomba nisaidie atleast majina 5 ya mbegu za kisasa na bei zake,,nahitaji kwenda kuchkua kesho

Na nitajuaje hii ni ya kisasa au ni ya kawaida?
Mbegu za kisasa hybrid
1) Assila f1
2)Eden f1
3)Anna f1
4)Monica f1
5)Imara f1
Kuhusu bei zinatofautiana duka na duka

Kuhusu kutofautisha mbegu za kawaida na za kisasa tofauti ya kwanza ndio hiyo mbegu za kisasa lazima ziandikwe hybrid, hata bei zake tofauti na za kawaida
 
Hiyo anna na eden mara nyingi zinatumika kwenye green house. Na zinaenda juu sana karibu mita mbili mpaka mbili na nusu!!

Kama unalima nje chukua assila maana zinafanya njema sana wakati wa ukame, nazo ni ndefu sana ila hazikutii anna f1!!

Nb: hizi mbegu zinazaa sana na zinahitaji matunzo sana na ujitahidi uweke fito zikianza kukua!!
Mkuu naomba nisaidie atleast majina 5 ya mbegu za kisasa na bei zake,,nahitaji kwenda kuchkua kesho

Na nitajuaje hii ni ya kisasa au ni ya kawaida?
 
Nashkuru sana mkuu,,ila hiyo Assila nimepita kwnye coments nimeona ni ghali mno ila ngoja tuone.

Mm nalima kwnye open space na udongo ni wa kichanga
 
Shukrani mkuu,
 
Mbegu za kisasa ziko nyingi sana sababu kila kampuni ya mbegu inakua nazo ila la kwanza mbegu za kisasa nyinyi wanaandika f1 mbele ya jina ila kuna kampuni kama Rijk zwaan wao mbegu zao zote za kisasa.
Ziko nyanya fupi,saizi ya kati na ndefu. Kama unalima nnje nyanya saizi ya kati (semi determinate) zinakufaa zaidi mfano mchache ni

Kipato f1 (east west)
Imara f1 (east west)
Jarrah rz (rijk zwaan)
Assila f1
Etc
Ndefu kuna
Montezul (rijk zwaan)
Anna f1
Vicyory f1 (east west)
 
Kuna tofauti gani kati ya ndefu na fupi kwenye mazao??
 
Kuna tofauti gani kati ya ndefu na fupi kwenye mazao??

Fupi inakaa miezi mitatu inakua imeisha inatoa nyanya juu kwenye kichwa cha mche,mavuno unavuna mengi kwa wakati mfupi sababu kila shina linaachwa hivyo ikiwa na mashine manne inamaana ni zaidi ya kg 2 utavuna kwa wiki kwa kila mmea,mmea mfupi mpaka kuisha chotara nyingi ni kg 10 kwa mche mmoja ila za kienyeji fupi ni kg 2 mpaka 3 kwa mche mmoja.

Ndefu hazina mwisho wa kukua hivyo uvunwa sita mpaka nane na hata zaidi kutegemea na huduma yako,ndefu hukupa wastani wa chini kg 20 kwa shina moja ila uvunaji wake kila wiki ni kichane kimoja ambacho mara nyingi huwa kg 1
 
Mkuu kuna dawa ulisema ulitumia kwa ajil ya kantangaze inaitwa Trysel km nlisoma vzur,,inapatikana wp na ni sh ngap? mana nimezunguka kkoo maduka yote hakuna
 
Mkuu kuna dawa ulisema ulitumia kwa ajil ya kantangaze inaitwa Trysel km nlisoma vzur,,inapatikana wp na ni sh ngap? mana nimezunguka kkoo maduka yote hakuna
Nilinunua 35,000/= sijui kwann kariakoo hakuna ila jaribu kuulizia wana dawa gani za kantangaze maana madawa kila siku yanatoka mapya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…