Jifunze kilimo cha nyanya

Jifunze kilimo cha nyanya

NYANYA ni zao linalopendwa kutumiwa....kunogesha chakula, chakula kilichowekwa NYANYA huwa na radha nzuri inayomvutia mlaji
8abd5c2d5a678ccee53030d33702d3d4.jpg

Wakulima wengi hutamani kulima zao hili wengi huandika FAIDA na kusahau kujadili kuhusu HASARA zisababishwazo na kilimo cha zao hili.

6d8b4994ba24a2b378205b4e964f6e35.jpg

Kiukweli NYANYA inaweza ikakutoa ukafanikiwa ki maisha ila inaweza vile vile ikakupa hasara kubwa ukajuta kufanya kilimo cha zao hili.
50e4ae8e855e61b91d1907f5af0ca828.jpg

Andaa matuta vizuri lakini naomba nikwaMbie ndugu msomaji kila aina ya Tuta ina mahala pake na ardhi yake maalum hivyo ni bora kuichunguza ardhi yako vizuri maana kwa udongo wa kichanga ukiweka matuta ni dhahiri udongo utapelekwa na maji...kipindi cha kumwagilia.

e9f17163709b78b1b026c292755412aa.jpg

Zingatia nafasi katika upandaji wa zao hili la nyanya nafasi inayopendekezwa ni cm50 kutoka mche hadi mche mwingine .... usipande zao hili pasipo kufuata kanuni ya nafasi ya cm50 maana zao hili lina majani na ukipanda kwa kubananisha sana utasababisha joto kuzidi, vile vile matawi yakigusana kutoka mche mmoja kwenda mche mwingine unaweza kusababisha miche iambukizane magonjwa.
b4a1e3cc16e8ad7ea456c06797837e7b.jpg

Kwa kawaida zao hili huchukua siku 72 hadi 120 kupanda hadi kuanza kuvuna...
Zao la nyanya ni zao linalofyonza sana rutuba hivyo hakikisha ardhi unaiboresha kwa kuiweka mbole mara kwa mara...kwa mbolea za dukani Urea, dap, N.p.k, can na nyinginezo hakikisha unafuata maelekezo ya mtaalaam kabla ya kutumia hizo mbolea...mbolea ya Samadi au za mifugo hakikisha mbolea hizo ziwe zimekauka kabisa ziwe kama unga au kavu maana mbolea za mifugo zikiwa mbichi zitasababisha miche kuungua...na inaweza kudumaa pia.
7150f6744a80dee402843bbefbcd671b.jpg

Nyanya inashambuliwa sana na wadudu ambao hupelekea zao hili kupata magonjwa hivyo kabla hujapanda zao hili hakikisha unaanda shamba na kupiga dawa za wadudu pamoja na dawa za magonjwa za ukungu. Ni vigumu sana kutibu nyanya pindi utakapoanza kuona dalili kwenye mche ulioathiriwa na magonjwa. Hivyo kipindi chote cha uhai wa nyanya ni lazima kuzingatia matumizi ya dawa.
ca2f57debc94abbba252f182e284aa24.jpg

Endapo utagundua baadhi ya miche imepata maambukizi muone mtaalam wa madawa akushauri ukishindwa kuutibu ni bora ukaung'oa uo mche maana nayo huambukizana magonjwa kama tunavyoambukizana binaadam.
9837d975b574e846df9ae1c390193abe.jpg

Uhai wa nyanya unategemea Maji, Mbolea na Dawa japo baadhi ya wataalam hushauri kuongeza na busta...ila ndani ya baadhi ya hizi booster kuna kemikali inayozuru afya zetu...kama utaamua kutumia booster yoyote weka akilini kuwa ndani ya booster kuna kemikali...
Hivyo kwa ushauri wangu...ni bora mkulima ukatumia mbolea asilia, na maji....dawa usitumie mara kwa mara...
Tumia dawa wakati wa kuandaa shamba...
Tumia dawa kukinga magonjwa ya ukungu...
Tumia dawa kuangamiza wadudu waharibifu...
Tumia dawa kutibu miche iliyoathirika...
Ila dawa isitimike kwa kiwango kikubwa...na hakikisha unafata maelekezo ya dawa yaliyopo kwenye kibandiko.
eceb415d9ec4f6b0eb4786894ab9f747.jpg

Kama utaihudumia miche ya nyanya vizuri kwa kuweka mbole pindi inapohitajika, kumwagia maji japo kwa wiki mara tatu...na hakikisha siku za kumwagia unamwagia asubuhi na jioni...Nyanya inaweza kuanza kutoa Vitumba (maua) ndani ya wiki ya 5 hadi ya 6 tuu tokea ulipoipanda.
d3f406d0fa02d3a8d74bbf6109f8c683.jpg

Unapopuliza madawa kuwa makini sana maana kipindi ambacho nyanya imeanza kutoa maua ni kipindi ambacho nyanya inahitaji uangalizi wa hali ya juu wanaita (INTENSIVE CARE)...kuna baadhi ya dawa ni marufuku kabisa kugusa maua hayo kwani hukausha kabisa hayo maua....
2cd57fd8c143a8a84a1aebb70a29f26f.jpg

Zao hili lina faida sana ukinunua mbegu kutoka kwa wauzaji makini unaweza kupata zaidi ya kilo 5 kwa kila mche japo zipo mbegu zinazo zaa hadi kilo 12 na kuendelea...na zipo pia mbegu ambazo ukianza kuvuna na ukiihidumia vizuri unaweza kuvuna zaidi ya miezi 6 hadi mwaka.
2681922792c78397862e020d87762e35.jpg

Hasara kwenye kilimo cha nyanya mara nyingi husababishwa na uzembe....nasema ni uzembe kwasabu wengi tumejikuta tunakimbilia kilimo kwakuwa jirani amenunua pikipiki kwaajiri ya kilimo...na watu wengi husifia faida waliyopata pasipo kueleza na hasara walizopata....hivyo ukipiga dawa isiyosahihi upo uwezekano wa kuikosa miche yote....
Ukiweka mbolea vibaya upo uwezekano wa kuiunguza miche yote...
Usipo mwagia maji unaweza kuipoteza miche yote...
Usipo weka dawa kwa wakati unaweza kupoteza miche yote...hivyo ni jukumu letu wakulima kuzingatia uwekaji sahihi wa mbolea...kuzingatia uwekaji wa maji si lazima umwagie maji mengi eti ili kesho usimwagie mwagia majo kiasi cha kutosha ila usimwagie maji hadi matope yatapakae huku na huko...nyanya haihitaji maji kwa muda mrefu...itaoza....
Weka dawa kwa wakati...hapo utashinda na utapata faida ya uhakika....
Nimeona nichangie mawazo yangu juu ya kilimo hiki cha nyanya .....nakaribisha maoni
MuNgU akubariki sana.
Naomba namba kiongozi
 
Niliona kwamba nyanya unaweza vuna katika stage tatu zikishakomaa na zinabadilika rangi kwa mtiririko huu Green, Pink na Red kutokana na mwonekano huo sasa unavuna. Je, mkuu kuna wanaovuna zikiwa bado hazijapata wekundu?

Nyanya ni kweli zikikomaa zina hizo stage 3 ulizozitaja.
  • Green ni nyanya mbichi hazifai kuchumwa
  • Pink sisi tunaita mapera hizi pia uwa hatuchumi labda bei iwe kubwa sn siku hiyo ndio utachuma hadi mapera
  • Red ndio nyanya zinazotakiwa kuchumwa
Swala la kusema eti tuchume mapema sababu zinaenda mbali hiyo haituhusu, atajua mwenyewe mnunuzi, huwa tunauza nyanya shambani na tunachuma red tu, atajua mwenyewe anapeleka wapi.

Kuna madhara makubwa ukichuma hadi mapema

Kwanza ujue nyanya zinaongezeka kila mchumo sasa ukichuma hadi mapera inamaana unapunguza mavuno ya mchumo ujao na unapunguza michumo pia.

Kwa kifupi utakuwa unamfurahisha mfanyabiashara huku unajimaliza wewe mwenyewe.
 
Morogoro wilaya gani mkuu? Je, ni kilimo cha mvua au umwagiliaji? Msimu ni lini?
Tuna misimu miwili, wa kwanza huu wa masika tunalima mwezi wa tatu

Wa pili ni wa kumwagilia huu unaanza mwezi wa sita
 
Kunashamba nimepata hapa morogoro karibu na mto ngerengere
95657148cca5edea0e05a648f1b4700e.jpg
fa2bb22842db0ce9533366dd3a0e4bc0.jpg
d60d03fec192c39f4fa4877ad5a4657d.jpg
df3ab6863e7d1b00f9f3a8920ae3380b.jpg


Heka wanauza 350,000/=
Naombeni ushauri nichukue?
Wanasema mto huwa unakauka kipimdi flan hivyo wana tengeneza malambo hapo kwenye mto wanaanza kulimia maji ya nkuwa kwenye mchanga chini
 
95657148cca5edea0e05a648f1b4700e.jpg
fa2bb22842db0ce9533366dd3a0e4bc0.jpg
d60d03fec192c39f4fa4877ad5a4657d.jpg
df3ab6863e7d1b00f9f3a8920ae3380b.jpg


Heka wanauza 350,000/=
Naombeni ushauri nichukue?
Wanasema mto huwa unakauka kipimdi flan hivyo wana tengeneza malambo hapo kwenye mto wanaanza kulimia maji ya nkuwa kwenye mchanga chini
Udongo wake upoje? Kuna vitu vya kuzingatia wakati wa kununua shamba usiangalie maji na bei tu
 
Udongo wake ni kichanga na mfinyanzi katikati ya izo dongo mbili. Huyo mtu analimaga hoho na nyanya na ngogwe
 
Udongo wake ni kichanga na mfinyanzi katikati ya izo dongo mbili. Huyo mtu analimaga hoho na nyanya na ngogwe
Mm sijaliona shamba siwezi kukushauri ununue au usinunue ila uwa tunakodi kwanza ukiridhika nalo ndio unanunua

Tafuta mtu muaminifu anayelijua shamba vzr ndio atakushauri
 
Mm sijaliona shamba siwezi kukushauri ununue au usinunue ila uwa tunakodi kwanza ukiridhika nalo ndio unanunua

Tafuta mtu muaminifu anayelijua shamba vzr ndio atakushauri
Shughuli ipo kwenye kukodi alafu uweke hela zako hapo kwenye kungoa visiki, kusafisha shamba. Alafu unaacha baadaye unasepa kwingine.. Sema lakini kuna kijana mmoja hapo pembeni kuaza nyanya heka mbili kapiga 24million . Na aridhi ina rutuba kwa kuwa ilikuwa pori muda mrefu.. Jamaa anakwambia wala hakuweka mbolea zaidi ya dawa kadhaa tu za kuzuia wadudu..
 
Kuna kuna limwa mahindi zaidi ila wachache walio na maeneo pepmbezon mwa mto ndio wanalima mbogo mboga
Kama wanalima zaidi mahindi basi hilo shamba lina kichanga kingi halifai kwa kilimo cha nyanya ndomana wanalima mbogamboga

Hata na ww ukinunua itabidi ulime mazao hayohayo wanayolima wao
 
Kama wanalima zaidi mahindi basi hilo shamba lina kichanga kingi halifai kwa kilimo cha nyanya ndomana wanalima mbogamboga

Hata na ww ukinunua itabidi ulime mazao hayohayo wanayolima wao
Hivi shamba linalo faa kwa nyanya linatakiwa kuwa na udongo gani??
 
Hivi shamba linalo faa kwa nyanya linatakiwa kuwa na udongo gani??
Nyanya inahitaji udongo wa mfinyanzi, kwanza unatunza maji pia una rutuba

Kama shamba lina kichanga utafosi kulima nyanya ila huwezi kupata matokeo mazuri
 
Kwanza ungetakiwa ujue unataka kulima nini ndio ujue shamba gani ununue, shamba la nyanya na la mahindi tofauti
 
Back
Top Bottom