Jifunze kuendesha (ku-control) nafsi ili kujikomboa katika vifungo na kuwa msaada kwa wengine

Naomba nitoe mchango wangu,,,,ndoto waweza zielezea kwenye uhalisia,vizuri kabisa. Changamoto ni ipi?
Nguvu zetu za kiroho ziko masafa ya chini,ndio maana akili ikiwa live(imeamka) inakumbuka nusu nusu au haikumbuki kabisa kuhusu nini kimeotwa.

Nijuavyo mpaka sasa...ndoto hutokea pale akili inapokuwa imelala(zile njia 5 za fahamu,ngozi,ulimi,masikio,macho na pua). Ndoto ni muda ambao mwili wa roho umetawala dimba,hausumbuliwi na akili imejaa illusion (ufeki).

Hakuna ndoto ya uongo,matukio ya kindoto ni kweli tupu,ile ni roho yako mwanadamu/kiumbe. Ni muda ambao roho inakuonesha yaliyopita,yaliyopo na yajayo. Issue ni kwamba tumetawaliwa sana na nafsi(akili) so tumevunja/hatuendani na kanuni za kiroho/kimasafa...ndio maana tunasahau sana tuyaotayo.

Kwenye ule utatu babkubwa.....MWILI,NAFSI NA ROHO huyu ndugu yetu nafsi anatuangusha sana,anashindwa kumjua vizuri roho na kumfuata. Sisi ni ROHO mwili na nafsi ni vitu vya kupotea. Bodi na engine vitakwenda lakini nguvu iliyosababisha viwepo itabakia.

Zingatia...nguvu haitengenezeki/ haiharibiki na wala haifi. Huamka na kulala basi. Tujifunze kuiamsha daima,ili tuitumie ipasavyo,NI ZAWADI YETU NA INDANI MWETU.
 
Mkuu,

Si nimeshakuambia kuwa ndoto zinatokana na mawzo yetu, ambayo tunayo conscious na subconscious, na ni vigumu kuyajua yote, hususan hayo subconscious, kwa hivyo, hata hizo ndoto zinazokuja kuwa za uhakisia hazishangazi, kwa sababu inawezekana ni kitu ulichoona au kusikia, ila huja ki register vizuri katika conscious mind?

Au huo mfano ndio unakutatiza? Si lazima kila mtu alale akisikiliza habari na kuota kilichosemwa kwenye habari, huo ulikuwa mfano tu kuelewesha namna moja hilo jambo linavyoweza kutokea, kwa nini unaiacha hoja ya msingi na kuufanya mfano unaoelezea hoja ya msingi kuwa ndiyo hoja ya msingi?

Why is it so hard to do abstract thinking and separate an example from the abstract concept?

Mkuu unaniuliza jinsi internal combustion engine ya gari inavyofanya kazi, nakuelezea mambo ya internal combustion engine inavyofanya kazi, nakupa mfano wa BMW yangu inavyofanya kazi, halafu unaukataa mfano kwa sababu wewe huna BMW?
 
"hata hizo ndoto zinazokuja kuwa za uhakisia hazishangazi, kwa sababu inawezekana ni kitu ulichoona au kusikia, ila huja ki register vizuri katika conscious mind?"



Huu mfano unanitatiza kweli....


Swali langu ni kuwa nilihitaji maelezo yako yaelezee ( kwa misingi ya sayansi ) ni kivipi uote jambo ambalo linakuja kwenye maisha ya ukweli,, Yani how unaota future na inatokea vile vile....

Nadhani hauna majibu, Na kuna sehemu umesema hatuwezi kujua kila kitu, Lakini mimi nakwambia kila kitu kipo wazi,


Kiroho unaweza kuona Past na future

Ndoto ambazo zinakuja kuwa matukio ya ukweli kama yalivyoonekana kwenye ndoto tunaofahamu kuhusu spiritualy tunasema roho iliona matukio, Na roho haipo limited na 'muda'.
 
Si kwamba sina majibu, tatizo unataka jibu fulani ambalo mimi silitoi.

Unataka habari za mambo jumbo ya roho, ambazo mimi sizikubali. Mimi naeleza mambo kwa kuangalia saikolojia na sayansi clinical.

Ukitatizwa na mfano, achana na mfano, chukua dhana ya msingi.

Kwamba, ndoto zinatokana na mawazo, mawazo yako katika conscious na subconscious level. Mawazo ya subconscious level ni vigumu hata wewe mwenyewe kujua kuwa unayo, kwa hiyo unaweza kujua kitu fulani kitatokea at the subconscious level (umeona, umesikia lakini hakija register at the conscious level), bila kukijua at the conscious level, ukakiota, halafu kikatokea.

Kikitokea unajiona umetabiri na kikatokea.

Nilitaka kutoa mfano mwingine ku illustrate hapa, lakini naona mifano inakuchanganya unatoka kwwnye dhana unajikita kwenye mfano.
 
Mwaka jana November.

Usiku wa kuamkia siku ambayo nlipokea taarifa ya msiba wa rafiki yangu ambaye nlisoma nae O level miaka hiyo, Ilikua hivi;

Nliota ndoto tukiwa wanafunzi wengi akiwemo marehemu rafiki yangu ambae nlikua nmeongozana nae, Lakini gafla nikajikuta nipo peke yangu tena sehemu nyingine nakatiza mtaa una watu wengi wamekusanyika na pilika za hapa na pale kama kuna jambo.

Nkamfuata mama mmoja nkamuuliza kuna shughuli gani hapo ? akanijibu kuna msiba, Hakuniambia ni msiba wa nani,

Wakati naendelea kusogea niulize mtu mwingine gafla nkashtuka kutoka usingizini kwasababu ya mlio wa cm, Kupokea naambiwa kuna msiba rafiki yako amefariki, wenge la usingizi wote ukakata muda ule ule...Ina maana nlianza kupata kwanza taarifa ndotoni japo sikujua aliefariki ni nani, Nikaja kupewa taarifa kamili na ile cm.

Sikushangaa kuhusu ndoto kwakua tayari nimeshazoea kuhusu ndoto za namna hii, nlibaki tu na hamaki na majonzi ya msiba wa rafiki yangu.
 
Ni kwasababu umegoma kuelewa/kukubali kuna mambo mengine nje ya unayoyafahamu.


Kama ungesema hauna unachofahamu kuhusu haya ningekuelewa, Na sio kuelezea mambo mengine ambayo hayahitaji unielezee kwakua nafahamu pia
 
Ndiyo hivyo nasema inawezekana kuna sehemu ulipata taarifa za msiba au mtu anayekaribia sana msiba uka zi register subconsciously, huku zi register consciously. Baadaye ukaenda kuota. Ndoto huwa hatuoti tu, zinatokana na mawazo.

Pia, inawezekana ni coincidence tu umeota msiba halafu ukapata habari za msiba. Ikitokea hivyo kama unaamini ndoto zinatabiri utaona huu utabiri.

Pia, huwa tunaota ndoto nyingi sana, tunazokumbuka ni chache tu, sasa mara nyingine inawezekana tunaota ndoto za msiba mara nyingi hatuzikumbuki, tukipata habari za msiba ndiyo tunakumbuka ndoto za msiba.

Kitu cha msingi ni kwamba, jinsi ubongo unavyofanya kazi, consciousness, mawazo, ndoto kuna mambo mengi sana bado hatujayaelewa vizuri, na kabla ya kukimbilia kusema tunaweza kutabiri mambo ya mbele kwa ndoto, na habari za "mambo ya kiroho" ambayo hayana ushahidi, inatupasa tufanye uchunguzi wa kisayansi wa kina kwanza.

Wazungu walikuja na elimu ya kutabiri kupatwa kwa jua na mwezi, down to the minute. Waafrika ambao hawakujua hiyo elimu walivyoona hivyo, wakaona huu uchawi, mtu atawezaje kutabiri kupatwa kwa jua?

Naam, kama una mawazo ya kusema uwezo wa kutabiri yajayo ni mambo ya kiroho, uchawi, clairvoyance, unaweza kukubali hivyo kirahisi tu.

But is that the case? No.

Leo tumeelewa sayansi ya kupatwa kwa jua na mwezi (eclipses), hatuhitaji kutaja uchawi wala mambo ya kiroho kuelezea hilo.

Kuna charts zinazoelezea kupatwa kwa jua kwa maelfu ya miaka in the future.

Follow the science. Haya mambo ya mumbo jumbo za roho ni maneno ya enzi za giza hayo tunatakiwa kuyapita kwenye ulimwengu huu wa sayansi.

Yani hata kama hatuna jibu, tunatakiwa tulitafute kisayansi, sio kuanza kupiga ramli kuhusu mambo ya kiroho hapa.
 
Ni kwasababu umegoma kuelewa/kukubali kuna mambo mengine nje ya unayoyafahamu.


Kama ungesema hauna unachofahamu kuhusu haya ningekuelewa, Na sio kuelezea mambo mengine ambayo hayahitaji unielezee kwakua nafahamu pia
Hakuna niliposema kuwa hakuna mambo mengine yaliyo nje ya ninayoyafahamu.

Mimi epistemology yangu ni ya kisayansi.

Ukishajua maana ya sayansi ni nini tu, umeshakubali kwamba kuna mambo mengine yapo nje ya ufahamu wako inabidi kuyachunguza.

Ila pia, naweza kujua kwamba habari za mumbo jumbo za roho ni za uongo. Bila kujua kila kitu.

Sihitaji kujua hesabu zote ili kujua kwamba square root ya 2 katika base ten math ni ndogo kuliko 2.

Sihitaji kujua mambo yote duniani ili kujua kuwa habari za kwamba watu wana uwezo wa kutabiri mambo yajayo kwa ndoto ni uongo. Kuna explanation nyingine nzuri tu kuelezea hata pale inapoonekana kama vike watu wametabiri mambo yajayo kwa ndoto.
 
Umerudi pale pale ambapo sikubaliani na wewe, Unawezaje kusema kuwa pengine nlipata taarifa za msiba ndio nkaota, Why nimuote muhusika huyo na siku hiyo ya tukio ?


[Yani hata kama hatuna jibu, tunatakiwa tulitafute kisayansi, sio kuanza kupiga ramli kuhusu mambo ya kiroho hapa.]

( Wote wanaoamini kiroho majibu yapo, na Spirituality si uchawi au ramli )

Anyways kwenye hitimisho yako
ndio nlikua nahitaji majibu ya kisayansi tangu mwanzo wa maswali yangu,

Kama ipo siku utanipa jibu kisayansi ntashukuru.
 
Ndio maana huwa nasema mambo mengine ni binafsi, Mengine hata hayakupaswa kujadiliwa kama hivi ilipasa niyaache tu,

Lengo langu ilikua ni kupata majibu kutoka kwako bila kuhusisha nachokifahamu ( kiroho )


Lakini sijapata majibu ya kuridhisha au kueleweka zaidi ya yale yale ambayo hata mimi nayafahamu pia.
 
Mkuu,

Ukishakubali kuwa kuna conscious na subconscious mind, tayari ushakubali huwezi ku account habari gani ulianza kuziota halafu ukazisikia kwa watu, na habari gani ulizisikia sehemu zikawa katika subconscious mind, ukaziota, halafu ukazisikia kwa watu consciously.

Na ukishindwa kufanya hiyo distinction tu, huwezi kusema hiki nimeanza kukiota halafu nikakisikia kwa watu.

Na ukishindwa kusema hivyo tu, huwezi kusema nimetabiri kitu kwa ndoto.

Habari za roho ni sawa na uchawi tu. Yote ni mambo ambayo yana defy logic na yanapingana na maelezo ya kisayansi.

Ukitaka tujikite kwenye majibu ya sayansi, kwanza itakubidi ututhibitishie uliota hivyo unavyosema uliota, isije kuwa unatupa stories tu. Sayansi inaenda na uhakiki.

Sasa, wewe unaweza kuthibitisha kwamba uliota hicho unachosema uliota?

Mimi naweza kusema siku moja kabla Lowassa hajafa niliota Lowassa anakufa kesho yake. Na akafa hivyo hivyo nilivyoota. Na hakuna sayansi inayoweza kuelezea hilo, hilo ni jambo la kiroho.

Na kweli, sayansi ikashindwa kuelezea hilo.

Lakini je, nikisema nimeota hivyo, hilo linahakikisha nimeota hivyo?

Tunahakikishaje nimeota hivyo kweli na sijawafunga kamba kutetea mada zangu ninazozipenda za uchawi tu?

Unaweza kuota kitu ambacho hakijatokea, ambacho hakiwezi kufanywa au kutabiriwa na mtu, halafu ukaja hapa kutupa data za uhakika zilizo precise, kabla kitu hicho hakijatokea, halafu turudi kuhakiki kama kitatokea kweli?

Kwa mfano, unaweza kuota ndoto ya kutuonesha Dow Jones Insustrial Average itaangukia wapi kwenye Stock Market kwa siku yoyote ya wiki hii kwa nuda wa saa 10 na dakika 15 jioni wa New York City?

Ukiweza kuota ndoto iliyokupa majibu ya namba exact, kitu kisichoweza kutabirika, ukapost hapa kabla ya muda huo, tukaja kuhakiki na kuona kweli, naweza kuanza kukusikiliza kwamba umeweza kutabiri yajayo kwa ndoto.

Sasa wewe unatuletea stories tu ambazo hatuwezi hata kuzihakiki, tutaaminije umeota unavyosema umeota?
 
Siyo tu hujapata majibu, hilo swali lako lenyewe lina maswali ambayo wewe hujayatolea majibu.

Tunahakikishaje kuwa umeota unavyosema umeota, na hutudanganyi?

Sayansi inataka vitu vinavyoweza kuhakikiwa, verifiable, mfano wako wa ndoto hauko verifiable.

Tutafute njia ya kuhakiki mambo.

Ota kitu kisichotabirika wala kuweza kupangwa na mtu, post hapa kabla hakijatokea, with specificity, weka tarehe, saa, dakika, kitakapotokea, halafu tuhakiki muda huo ukifika.

Unaweza kuota kitu kisichotabirika, kabla hakijatokea, ukaja hapa ku post kwamba kitatokea, kabla hakijatokea, halafu tukahakiki kwamba kitatokea au hakitatokea?

Hii itaondoa utata mwingi kwenye uhakiki.
 
Huyu mwandishi atakuwa baharesa au mo dewji yaani wengi utakuta wasimlizi wazuri ila yeye mwenyewe bado yuko hana hela au mafanikio
 
Doh! Okay
 
Mkuu siwezi kubishana na wewe, Hilo halikua lengo langu.
 
Nafikiri tumwache aliyeanzisha thread hii amalize jambo lake

Kama kuna mtu haamini uwepo wa Mungu naye aanzishe thread yake
Hii ni censorship sasa.

Mimi nilikuwa hata siujui huu uzi, nimeitwa kwa tag kwenye post namba 16. Katazame.

Sikuvamia tu uzi, nimeitwa kwa tag nije kuchangia. Kuna mtu alitaka kusikia mawazo yangu akaniita.

Wewe weka hoja yako.

Kama wengine wataiona mbovu, wana haki ya kusema hivyo.

Na wewe una haki ya kuitetea.

Yani unataka mtu alete hoja ya kula mavi ya mtu ili kuongeza protini halafu tukae kimya kwa kuogopa kuingilia thread ya mtu, wakati tunajua kula mavi kutaleta kipindupindu?

Ukileta thread zenye habari zisizoeleweka utaulizwa ujieleze vizuri tu.

Hiyo ndiyo maana ya JF Where We Dare To Talk Openly.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…