Jifunze mapishi na namna mbalimbali za kupika mkate

Jifunze mapishi na namna mbalimbali za kupika mkate

kwnza nakushangaa sana ujuee yaani hapa tunapika mkate wewe umeleta abari za kunanhilu acha watu tupike mkate bana!!!

btw propose leo nikupikie nn kwa ajili ya new yr eve.

nb unapikiwa kama mtu baki si kama swtlo sawa??

Haaaaa haaaa nimeipenda hii . . . . Kaizer Mchuchu ndo unaondoka huo . . . . step by step . . . hadi utaishia. Chezeya Superman weye! Hamna cha Kungwi wala Kigoli wala Mwali!
 
Last edited by a moderator:
uzuri kelele za chura hazimnyimi tembo kunywa maji atiiii.

Toka lini Mwizi akakubali kuwa ni Mwizi bila kubambwa. Tushukuru tu tego halikufanya kazi! Poa kufa na tai shingoni mi bana naondoka na Mkate sitaki.
 
haya jamani leo ni siku nyingine ambayo ninataka tupike mkate kwaajili ya familia.
mkate

mkate ni chakula ambacho huliwa wakati wa kufungua kinywa.hupikwa kwa kutumia unga wa ngano ama wa muhogo lakin huwa na kiasi kukubwa cha wanga na hivyo unapotumiwa kama kifungua kinywa hukusudiwa kumpatia mlaji nguvu na joto mwilini.

sasa tuangalie jinsi ya upish wa mkate.

mahaitaji:
a) unga wa ngano kg 1 (kwa familia yenye watu wengi let say 4)
b)hamira gm 50
c)mayai 4
d) chumvi kijiko kimoja cha chai
e)sukari nijiko 2 vya chakula
f) maziwa fresh robo l500 ml kama unauwezo kama la basi tumia maji.

njia.

1) chekecha unga wa ngano kwenye chekeche ili kuondoa particles kubwa pamoja na kuingiza hewa ndani ya chembe za unga.

2) weka hamira chumvi pamoja na suukari kisha koroga kwa mkono hadi uchanganyike vizuri kabisa.

3) koroga mayai yako 4 pembeni kwenye bakuli kisha mimina koroga yachanganyike ndipo uyamimine kwenye mchanganyiko wako uyachanganye kwa mikono.

4) tia maziwa kwenye mchanganyiko wako na kisha ukande unga kwa vidole vyako hadi ulainike uwe kama wa kupikia chapati. hakikisha wakat unaukanda usizidishe maji manake kadiri unga unavyozidi kuumuka ndivyo unavyozidi kuwa laini. wakati wa kukanda kunja vidole vyako vinne na uvitumie kukandia unga usitoboe unga kwa vidole kwani hautaukanda zaidi ya kuutoa hewa tu.

5) chukua chombo chako cha kukokea kipake blue band kwa ndani kisha kata unga kwa size ya chombo chako na uutengeneze kwa umbo la tin yako ndipo uuweke. kama huna baking tins za mkate waweza kutumia hata tin ya cake ila uzikate kwa maumbo ya mstatili. kama nacho hiki huna basi tumia sufuria yako ipake blue band ukate unga kwa umbo la viduara uueke ndani visiwe vikubwa sana yawe na umbo dogo la wastani tu.

6) washa oven yako kwa nyuzi joto 120 dk kabla, kisha weka chombo chako cha kuokea na funga mlango. subiria baada ya dk 30 mkate wako utakuwa umesha iva. ii kujua kama umeiva vizuri chukua kitu chenye ncha kali choma kwenye mkate basi kile chombo kikitoka kikavu jua mkate wako uko tayari.

zima jiko na toa mkate wako nje uweke pakavu ili upoe. kumbuka kwamba mkate kwa ajili ya afya hufaa uliwe siku moja baada ya kuokwa. hapa ahauwa na ladha nzuri zaid na huwa umesha lainika vya kutosha. usiufunike mkate wako kama bado haujapoa usije ukajaa mvuke. na usiuweke kwenye unyevu.
mkate huu waweza kuutumia kutengenezea sand wich ama kuliwa jinsi ulivyo tu.

haya basi nawatakieni mapish mazuri kwaajili ya sikukuu ya x-mass na mwaka mmpya.

mke mwezangu AshaDii nakuomba uwaekee ile picha ya mkate tunayopikaga nyumbani kwajili ya chai

Ubarikiwe sana! Na kuna ule mkate wa bakhresa una ladha nzuri na mlaini mapishi yake yanakuaje? Kuna kitu wanaongeza?
Wabheja sana.
 
Last edited by a moderator:
Ubarikiwe sana! Na kuna ule mkate wa bakhresa una ladha nzuri na mlaini mapishi yake yanakuaje? Kuna kitu wanaongeza?
Wabheja sana.

ila bakhressa anatengeneza aina tofaut za unga wa ngano kwaajili ya mapish tofauti. ukipata home baking four ni tofauti na golden baking flour na ni tofauti na ule wa maandazi, mikate na ni tofauti na wa keki. nilichogundua kwa wao hutumia aina ya unga wa ngano ule wa mkate wenyewe nafkiri kuna vitu ule unga umeongezwa ama la basi ni shayiri .sasa sina hakika sana na aina ya unga unaotumika.

lakin pish hili la mkate ukilimudu vyema basi mkate wake huwa na ladha tamu sana na ni mlain kuliko hata huo wa bakhressa.
 
ila bakhressa anatengeneza aina tofaut za unga wa ngano kwaajili ya mapish tofauti. ukipata home baking four ni tofauti na golden baking flour na ni tofauti na ule wa maandazi, mikate na ni tofauti na wa keki. nilichogundua kwa wao hutumia aina ya unga wa ngano ule wa mkate wenyewe nafkiri kuna vitu ule unga umeongezwa ama la basi ni shayiri .sasa sina hakika sana na aina ya unga unaotumika.

lakin pish hili la mkate ukilimudu vyema basi mkate wake huwa na ladha tamu sana na ni mlain kuliko hata huo wa bakhressa.

Tatizo huku kwetu mikani hatuna selection ya unga, ykienda dukani sanasana utapata product za pembe. Ok na kuhusu mayai kwenye mkate mkate unaweza kukaa muda gani bila kuharibika ikiwa umeutia mayai? Maana nipika keki ya mayai ikabidi niwa4s waile yote siku yapili nilihisi kuharibikiwa..
 
Mdogo wangu gfsonwin mkate huu hapa nimeleta.... Kuna lingine dear?

Chef+Issa+Mkate+mweupe+%252822%2529.jpg

duh naomba nije nile... unaonekana tamuuuu, we kweli mtalaamu tena siyo wa mkate tu

gfsonwin ntakuja unifundishe kupika makaron, na chuku chuku
 
Mahitaji

Mchele kikombe 1
Tui la nazi kikombe 3/4- 1
Hamira 1 teaspoon
Hiliki kiasi
Ute wa yai 1
Sukari 3/4 kikombe

Namna ya kutaarisha

1)Roweka mchele usiku 1
2)Saga kwenye blenda mchele,hamira,tui la nazi,hiliki hadi viwe laini..
3)weka sehemu ya joto ili uimuke..
4)washa oven moto kiasi 300-350°..mimina sukari na ute wa yai kwenye mchanganyiko wako then changanya vizuri...
5)weka sufuria jikoni mafuta kidogo yakipata moto mimina mchanganyiko wako
6)baada ya dakika 5-10 mkate ukishaanza kushikana funika kwa ufuniko then weka kwenye oven hadi uwive na kuwa rangi ya brown
7)subiria mkate upoe ndipo uukate vipande vipande
8)mkate wa kuminina tayari kwa kuliwa..
 

Attachments

  • 1385406258832.jpg
    1385406258832.jpg
    23.4 KB · Views: 742
  • 1385406276350.jpg
    1385406276350.jpg
    21.2 KB · Views: 720
ha haaa, msinicheke jamani, haya mapishi na yale ya vitumbua nimechemsha mbaya.... nitajaribu kwa kufwatilia haya maelezo yako.
kwa nini nikipikaga huu mkate au vitumbua vyangu havigandi, yaani vinachemka tuuu kama uji, lol!

Hakuna kuchekana hapa best,mi vitumbua sijawahi kujaribu kabisa ila mkate nishajaribu. Wakati naanza nilichotoa Mungu ndio anajua ila sikuchoka mpaka kikaeleweka!
 
Hakuna kuchekana hapa best,mi vitumbua sijawahi kujaribu kabisa ila mkate nishajaribu. Wakati naanza nilichotoa Mungu ndio anajua ila sikuchoka mpaka kikaeleweka!
Afadhali umenitia moyo best....
mimi nimejaribu vitumbua mara kadhaa....
mara wananiambia vile vikaangio havijazoea mata sijui nini. kwa kifupi huwa naishia kuchemsha uji kwenye mafuta.....
nikaamua kujiachia zangu
 
Mahitaji

Mchele kikombe 1
Tui la nazi kikombe 3/4- 1
Hamira 1 teaspoon
Hiliki kiasi
Ute wa yai 1
Sukari 3/4 kikombe

Namna ya kutaarisha

1)Roweka mchele usiku 1
2)Saga kwenye blenda mchele,hamira,tui la nazi,hiliki hadi viwe laini..
3)weka sehemu ya joto ili uimuke..
4)washa oven moto kiasi 300-350°..mimina sukari na ute wa yai kwenye mchanganyiko wako then changanya vizuri...
5)weka sufuria jikoni mafuta kidogo yakipata moto mimina mchanganyiko wako
6)baada ya dakika 5-10 mkate ukishaanza kushikana funika kwa ufuniko then weka kwenye oven hadi uwive na kuwa rangi ya brown
7)subiria mkate upoe ndipo uukate vipande vipande
8)mkate wa kuminina tayari kwa kuliwa..
Mkate unavutia machoni wallahi waonekana mtam dah!
 
ha haaa, msinicheke jamani, haya mapishi na yale ya vitumbua nimechemsha mbaya.... nitajaribu kwa kufwatilia haya maelezo yako.
kwa nini nikipikaga huu mkate au vitumbua vyangu havigandi, yaani vinachemka tuuu kama uji, lol!
Usivunjike moyo shosti endelea kujaribu tu!mapishi mengine mpaka uyajaribu mara kadhaa ndo yanakubali...na ukikosea aina ya mchele tu au kuchujua huo unga haviwi!
 
Afadhali umenitia moyo best....
mimi nimejaribu vitumbua mara kadhaa....
mara wananiambia vile vikaangio havijazoea mata sijui nini. kwa kifupi huwa naishia kuchemsha uji kwenye mafuta.....
nikaamua kujiachia zangu
Wanadai kikaango ukikiunguzia machicha ya nazi kinakuwa sawa,sijui pana ukweli hapo?
farkhina naomba ya mkate wa ufuta na mkate wa tambi.
 
Last edited by a moderator:
ha haaa, msinicheke jamani, haya mapishi na yale ya vitumbua nimechemsha mbaya.... nitajaribu kwa kufwatilia haya maelezo yako.
kwa nini nikipikaga huu mkate au vitumbua vyangu havigandi, yaani vinachemka tuuu kama uji, lol!

Hahahahaha moto weka mdogo mdogo then usiweke mimaji mengi...
 
Back
Top Bottom