Jifunze namna Urusi alivyokwamisha "counteroffensive" ya Ukraine

Jifunze namna Urusi alivyokwamisha "counteroffensive" ya Ukraine

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Malalamiko kuwa vita vya kukomboa majimbo ya Ukraine sasa yako wazi kutoka kila upande.Kutoka kwa raisi wa Ukraine,makamanda wake ,askari wa kawaida na hata kutoka nchi za NATO ambazo zilichangia silaha nyingi kufanikisha hatua hiyo.

Kama alivyotabiri generali mstaafu wa Marekani bado kuna ukweli mwengine ambao umefichuliwa na askari wenyewe waliopelekwa mstari wa mbele kushirikia ukombozi huo.Wanasema kusonga mbele hata mita mia basi ni kazi kubwa.

Inajulikana kuwa katika vita kweli kunatumika mabomu ya kutegwa ardhini lakini hawakuwahi kufikiria kuwa Urusi ingetumia utitiri wa mabomu waliyokutana nayo. Hali hiyo inafanya kazi ya kutegua ili kutengeneza njia ya kupitwa na askari wa miguu iwe ngumu kupita kiasi.

Kawaida mabomu ya aina hiyo huzikwa chini mstari baada ya mstari lakini safari hii urusi imeyasia kama vile mpunga,unakutana nayo kila hatua .Vile vile kawaida yanakuwa ni aina za chuma ambayo huteguliwa na vikosi maalumu kwa kutumia metal detectori,; Lakini safari hii mabomu hayo ni ya plastic na yana sura nyingi mno kuanzia kama chupa za maji au vipande vya pipi.Wateguaji mabomu wenyewe wamekuwa wakiripukiwa na vibomu hivyo vinavyokata miguu yao.Vikundi vya uokozi navyo vinapokuja kuokoa wenzao nao yanawakuta kama ya wenzao.

Ili kutengeneza njia ya upana wa mita chache kupitika na kifaru kimoja kisogee mita chache mbele basi inaweza ikachukua siku kadhaa.

Pamoja na hivyo hiyo njia iliyosafishwa kwa shida Urusi baadae huwa wanairushia makombora ambayo yanatapakaza vibomu vyengine kuwafanya waliosonga mbele washindwe kurudi nyuma wakati huo huo wakiwalenga kwa shabaha kutoka helkopta zinazopiga kutoka mbali na mstari wa vita.

Haja ya askari kusonga mbele karibu na ngome za warusi imekuwa ya kuwahofisha sana askari wa Ukraine kwani kila wanapofanya hivyo ni kama kwamba wamejitenga na kukosa usaidizi wa wenzao.

Hofu iliyotanda sasa kwa jeshi la Ukraine ni kushindwa kutoa picha ya mafanikio ya haraka kwa NATO ili kuvutia misaada mipya ya silaha.
 
Ni kichaa tu au mwenda wazimu anaewaza kupigana na mrusi ktk dunia ya leo
Vita si lelemama na kuna kubwa la kujifunza kutoka majeshi yote duniani.Katika vita hakuna kusema sema ovyo na wala hakuna kupuuza kitisho cha adui hata akiwa mdogo.

Wakati Ukraine wanatangaza sana kuanza kukomboa maeneo Urusi ilipata muda mzuri kutengeneza ngome za kujilinda.

Eti sasa askari wa Ukraine wameamua kuviacha vifaru na magari ya deraya nyuma na wanakwenda kwa miguu baada ya kuwathibitikia vifaa hivyo havifai mbele ya ngome walizokutana nazo na ambazo hawakuzitarajia,Wanasema bila ndege za F16 hawawezi kupenya. kama vifaru vimeshindwa kupenywa itakuwaje kwa askari wa miguu na bunduki zoo moja moja.
 
Ni kibri na ubishi wa simba na yanga.Kivita mrusi sio mtu mzuri.Historia imetuambia na Macho yanatuonesha.
Mpaka leo mjerumani analia.Zelensky ameitumbukiza nchi kwenye janga ambalo sasa linazimaliza mpaka nchi za Ulaya.
Angalia hapo chini alivyoachwa mpweke kwenye mkutano wa NATO.
Uanachama alioutaka na sijui kwa faida ya nani kaambiwa bado mpaka ashinde vita.
1689568802959.png
 
Nenda kawaulize Napoleon Bonaparte na Adolf Hitler kuhusu Russia
Kwa ufupi Urusi ina uzoefu wa kupigana vita virefu na hatimae kushinda kuliko mataifa kama Marekani na nchi za Ulaya.
Kwa uzoefu huo hata aina za silaha wanazotumia huwa wanazitoa hatua kwa hatua kulingana na muda.
Mfano kwa sasa wakati Marekani imekubali kuipa Ukraine mabomu ya cluster.Putin kasema wanayo mengi sana Ukraine wakianza basi wao watamaliza.
 
Malalamiko kuwa vita vya kukomboa majimbo ya Ukraine sasa yako wazi kutoka kila upande.Kutoka kwa raisi wa Ukraine,makamanda wake ,askari wa kawaida na hata kutoka nchi za NATO ambazo zilichangia silaha nyingi kufanikisha hatua hiyo.
Wewe ni mrusi nini. Nadhani taarifa unazo za generali popov aliyetumbuliwa wiki iliyopita kwa kusema hali si shwari mstari wa mbele na askari wengi wanauliwa lakini ukweli unafichwa. Mimi na wewe tuko buza huku kwa mpalange sio urrus.
 
Halafu hata hizo s400 au pantsir sijui hamna kitu daraja muhimi
Malalamiko kuwa vita vya kukomboa majimbo ya Ukraine sasa yako wazi kutoka kila upande.Kutoka kwa raisi wa Ukraine,makamanda wake ,askari wa kawaida na hata kutoka nchi za NATO ambazo zilichangia silaha nyingi kufanikisha hatua hiyo...
hizo s400 au pantsir air defence vipi daraja limepigwa bomu tena na hii si mara ya kwanza. Kwa daraja muhimu kama lile.
 
Kwa ufupi Urusi ina uzoefu wa kupigana vita virefu na hatimae kushinda kuliko mataifa kama Marekani na nchi za Ulaya.
Kwa uzoefu huo hata aina za silaha wanazotumia huwa wanazitoa hatua kwa hatua kulingana na muda.
Mfano kwa sasa wakati Marekani imekubali kuipa Ukraine mabomu ya cluster.Putin kasema wanayo mengi sana Ukraine wakianza basi wao watamaliza.
Mmm warusi hizo cluster walisyaanza kuzitumia toka siku ya kwanza walinua ukrain hana hzo silaha acha porojo mkuu urusi choka mbaya kwa uchumi ovyo umeshawahi ona simu au bodaboda au jeans made in russia ? Wanatengeneza pombe batlika na vodka ziko kibao hapa bongo na silaha yale mavomu makali nao wanategemea chips toka kwa west. We hushangai drone tu anaagiza iran supa pawa na 2.
 
Mmm warusi hizo cluster walisyaanza kuzitumia toka siku ya kwanza walinua ukrain hana hzo silaha acha porojo mkuu urusi choka mbaya kwa uchumi ovyo umeshawahi ona simu au bodaboda au jeans made in russia ? Wanatengeneza pombe batlika na vodka ziko kibao hapa bongo na silaha yale mavomu makali nao wanategemea chips toka kwa west. We hushangai drone tu anaagiza iran supa pawa na 2.
Kuuza simu bodaboda jeans vinamahusiano gani nauhodari wavita???
Hitler alivokula kichapo Russia alikua anauza kitu gani kwani??
 
Kwa ufupi Urusi ina uzoefu wa kupigana vita virefu na hatimae kushinda kuliko mataifa kama Marekani na nchi za Ulaya.
Kwa uzoefu huo hata aina za silaha wanazotumia huwa wanazitoa hatua kwa hatua kulingana na muda.
Mfano kwa sasa wakati Marekani imekubali kuipa Ukraine mabomu ya cluster.Putin kasema wanayo mengi sana Ukraine wakianza basi wao watamaliza.
Hii itamletea shida ukrein zaidi mana wakati anangoja wafadhili mwenzake kawambia yapo stood yakutosha.

Sent from my SM-S920L using JamiiForums mobile app
 
Kuuza simu bodaboda jeans vinamahusiano gani nauhodari wavita???
Hitler alivokula kichapo Russia alikua anauza kitu gani kwani??
Hiyo ni lugha nyepesi ya kukuambia mtu kama wewe usielewa na wala huwezi kuelewa yaani vita inataka hela au uchumi imara. Putin anauza vitu vichache sana nje. Kabla ya vita dola 1 us ilikuwa sawa na r55 za urusi leo hii us1. = 92. Yaani watu wa kawaida wana hali mbaya. Ila ninavyohisi wewe hizi ni lugha ngumu kuelewa. Eti putin anaachia silaha kidogo kidogo. Hizo kinzal vip ni silaha ndogo. Ni moja wapo ya silaha anazotegemea putin na alisema hakuna nchi inayoweza kutengeneza.
Sisi wote tuko buza hapa bongo.
Huyo hitler alikuwa na uchumi imara vipi weww mbona unachekesha
 
Mmm warusi hizo cluster walisyaanza kuzitumia toka siku ya kwanza walinua ukrain hana hzo silaha acha porojo mkuu urusi choka mbaya kwa uchumi ovyo umeshawahi ona simu au bodaboda au jeans made in russia ? Wanatengeneza pombe batlika na vodka ziko kibao hapa bongo na silaha yale mavomu makali nao wanategemea chips toka kwa west. We hushangai drone tu anaagiza iran supa pawa na 2.
Mtu kama wewe kujibiwa ni kupoteza muda kabisa.
 
Mmm warusi hizo cluster walisyaanza kuzitumia toka siku ya kwanza walinua ukrain hana hzo silaha acha porojo mkuu urusi choka mbaya kwa uchumi ovyo umeshawahi ona simu au bodaboda au jeans made in russia ? Wanatengeneza pombe batlika na vodka ziko kibao hapa bongo na silaha yale mavomu makali nao wanategemea chips toka kwa west. We hushangai drone tu anaagiza iran supa pawa na 2.
Hizo ni bidhaa za kimachinga zinafanywa na nchi changa.Urusi anauza vitu vya meli meli na vya kutiririka kwenye mabomba kwenda Ulaya na wote wanamjua ndio maana wanaomba sana ule mkataba wa nafaka usife.
 
Back
Top Bottom