Jiji la Dar es Salaam ndio nguzo kuu kwenye kufanikiwa, vijana kimbilieni huko

Jiji la Dar es Salaam ndio nguzo kuu kwenye kufanikiwa, vijana kimbilieni huko

Japo umewafunua watu macho na nimekubali ulichoandika ila hapa umefeli kama kweli uliacha biashara iliokua inaingiza pesa vizuri na kwenda ualimu ambao kila mwezi wa tano wanasubiri kusikia mishahara imeongezwa au bado umekwama sana labda kama biashara ziligoma na kwa upambanaji ulioandika sidhani kama ingekua rahisi kuacha biashara hata kama ni ngumu
Mkuu nakuelewa, naijua familia yangu vizuri, ninacho amini naweza kufanya hizo harakati ndani ya ualimu huu, Lakini kwa sababu ya mkoa nilipo naona ni miyeyusho sana, hakika nitarudi dar es salaam kuendeleza mapambano.
 
Soma uelewe, nimekwambia dar ni sehemu nzuri ya kuanza kwa mtu asiyekua na kitu, Kuliko huko mikoani. swala la kwenda kwenye ajira ilo ni swala kingine mkuu wengine wazazi wetu huko vijijini wanaona ajira ni Kila kitu kuliko hizo harakati zako, Niko na mtaji wa kutosha kwa Sasa wa kufanya harakati Lakini location nilipo ndio naona kama harakati sizisomi....Niko njiani kurudi huko mambo yakitiki.
Sawa.
 
Hata hao wafanya biashara huko mikoani wengi wao kuna level wakifika huwa wanahamishia biashara zao Dar.
Dar kuna mzunguko mkubwa sana wa Noti.
Ukibisha shauri yako.
 
Kama kweli kwenye business yako ungekuwa unapata pesa ya kutosha kuzidi mshahara wa mwalimu i bealive wazazi wako wangekushauri ukomae na biashara tu badala ya kuajiriwa tena secta yenye mshahara finyu kama uwalimu, lakini kwa vile biashara ilikuendea mlama ukawa huna budi tu kwenda huko u-teacher so acha propaganda za kitoto.
Wazazi wanaangalia sana security mkuu, labda tu wanatofautiana padogo lakini wazazi wengi hasa wale ambao umri umeenda humwambii kitu kuhusu ajira serikalini.
 
Mkuu naona umekariri maisha ingawa ni kweli dar kuna mzinguko mkubwa wa hela na ni rahisi kutoboa ila kusema kwamba ni vigumu kutoboa mkoani kwangu ni big no! Mikoani kuna fursa kibao km utajipanga vizuri unatoboa asubuhi na mapema otherwise uwepo kwenye mikoa inaondekeza ukabila km moshi na kagera
 
Kungekua hakuna mzunguko wa biashara hao watu wa mikoani ungewaona huko kuja kuchukua bidhaa?

Akili yako na juhudi zako za kupambana ndio zitakazofanya utoboe kwenye haya maisha
hata mbinguni hakitaingia kinyonge naamini zaidi katika bidii na utashi wa mtu kupambana ...lazima utoboe na maisha yabadilike kutoka ulivokuwa
 
Ukitaka Kutoboa maeneo yoote hayo we kuwa MGANGA haijalishi wa ukweli au Uongo.....



Utapiga Helaa mpk uzikimbie
 
Hapa nazungumzia nyanja za mafanikio kwa sisi wasakatonge, nimezaliwa Moshi-kilimanjaro nimezunguka pande Nyingi za Tanzania Lakini dar-es salaam ndio Kila kitu kwa mtu ambae ana chachu ya mafanikio.

MWANZA
Ukienda Mwanza na hakika asilimia 100% utashindwa kujua uanzie wapi umalize wapi, labda uchague kua machinga na shida ya kua machinga ni bidhaa kutoka, unaweza kupigwa doro kuanzia asubuhi mpaka jioni mpaka utamani kurudi Kijijini kitu ambayo uwezi kuikuta dar Maeneo kama buhongwa, igoma ndio wamejaa machinga na wengi wao ni mwendo wa doro, useme ufungue labda frame kupata katikati ya Jiji ni ngumu huwezi kupata kama una mtaji mdogo. (Usisahau wasukuma wanauza kwa madawa)..kwahiyo na conclude kwa kusema Mwanza sio sehemu nzuri kwa anaeanza kutafuta maisha. Labda ufanye kuzunguka minadani kupeleka bidhaa pande za Magu na kwimba.

MOROGORO.
Ni sehemu nzuri ya kuishi sio kutafuta Hela itakuchukua miaka mingi kuanza Kuona mafanikio, Huu mji ni kama njia ya kwenda dar watu hakuna kabisa, wafanyabiashara wa jumla kutoka pembezoni mfano ifakara, kilombero wakifata mzigo ni moja kwa moja dar, kwa sababu ya ukaribu kijana usijichanganye kwenda Morogoro kuanza kutoka chini.

ARUSHA
Huku na penyewe mambo ni Yale Yale tu kwa msakatonge labda Uwe machinga kwa kumwaga chini "sendozi" za kina dada jioni mitaa ya mianzini Hapo au stand (jiandae kukimbizwa na migambo), frame uwezi kupata mjini Ukiwa na mtaji mdogo.

Kwanini nasema dar es salaam ndio Kila kitu? Fanya wepesi uje mjini, dar es salaam chochote unauza ukipata location nzuri, Kuna watu waliofanikiwa kwa umachinga wakiwa manzese,ilala mbagala,mbezi,chanika, mbande,kigamboni n.k unaweza usifanye mishe zako kariakoo na Bado ukatoboa, ni kwa sababu muingiliano ni mkubwa.

....nilikua nanunua viatu vya wadada kariakoo namwaga pale manzese nauza kuanzia asubuhi mpaka usiku saa 4, guess nitakua nimekusanya shingapi? Mtaji nilioaanza nao ni kama laki 7 Lakini progress unaiona na mtaji unakua, je huko Kigoma, Mpanda, Bariadi unaweza kumwaga viatu barabarani na usiuze hata kimoja.

Nilifanya harakati za viatu hapo karume nachukua viatu ndani kwa jumla namwaga nje, ndani ya mwezi nikawa na pointer wengi sana Pamoja na wafanyabiashara wa jumla kutoka mikoani huko naanza kuuza saa 11 usiku kufika saa 2 asubuhi jamaa zangu wa gairo nawahesabia mzigo wote tunapatana nachukua changu, hivi nitajie mkoa gani hii inafanyika? Labda Hapo Soko la mtumba memorial Moshi tena kwa kiwango kidogo.

Nimefanya harakati Nyingi sana hapo na Kila harakati niliofanya ilinilipa, mpaka nikaondoka Jiji ilo. Mikoani Huku mzunguko hamna, pesa ni ngumu, ukifungua harakati wachawi ni wengi sana, Sasa kijana unakaa Kigoma, Mpanda Katavi, Babati, Njombe, Shinyanga na unaridhika kabisa?

Sasa hivi Niko vijijini huku na mtaji Sasa Lakini Cha kufanya sikioni naona kama nitazika pesa.

Tokeni huko nendeni kwenye Jiji lenye pesa nyingi.

Vipi waliofanikiwa ni wengi pia au
 
Hapa nazungumzia nyanja za mafanikio kwa sisi wasakatonge, nimezaliwa Moshi-kilimanjaro nimezunguka pande Nyingi za Tanzania Lakini dar-es salaam ndio Kila kitu kwa mtu ambae ana chachu ya mafanikio.

MWANZA
Ukienda Mwanza na hakika asilimia 100% utashindwa kujua uanzie wapi umalize wapi, labda uchague kua machinga na shida ya kua machinga ni bidhaa kutoka, unaweza kupigwa doro kuanzia asubuhi mpaka jioni mpaka utamani kurudi Kijijini kitu ambayo uwezi kuikuta dar Maeneo kama buhongwa, igoma ndio wamejaa machinga na wengi wao ni mwendo wa doro, useme ufungue labda frame kupata katikati ya Jiji ni ngumu huwezi kupata kama una mtaji mdogo. (Usisahau wasukuma wanauza kwa madawa)..kwahiyo na conclude kwa kusema Mwanza sio sehemu nzuri kwa anaeanza kutafuta maisha. Labda ufanye kuzunguka minadani kupeleka bidhaa pande za Magu na kwimba.

MOROGORO.
Ni sehemu nzuri ya kuishi sio kutafuta Hela itakuchukua miaka mingi kuanza Kuona mafanikio, Huu mji ni kama njia ya kwenda dar watu hakuna kabisa, wafanyabiashara wa jumla kutoka pembezoni mfano ifakara, kilombero wakifata mzigo ni moja kwa moja dar, kwa sababu ya ukaribu kijana usijichanganye kwenda Morogoro kuanza kutoka chini.

ARUSHA
Huku na penyewe mambo ni Yale Yale tu kwa msakatonge labda Uwe machinga kwa kumwaga chini "sendozi" za kina dada jioni mitaa ya mianzini Hapo au stand (jiandae kukimbizwa na migambo), frame uwezi kupata mjini Ukiwa na mtaji mdogo.

Kwanini nasema dar es salaam ndio Kila kitu? Fanya wepesi uje mjini, dar es salaam chochote unauza ukipata location nzuri, Kuna watu waliofanikiwa kwa umachinga wakiwa manzese,ilala mbagala,mbezi,chanika, mbande,kigamboni n.k unaweza usifanye mishe zako kariakoo na Bado ukatoboa, ni kwa sababu muingiliano ni mkubwa.

....nilikua nanunua viatu vya wadada kariakoo namwaga pale manzese nauza kuanzia asubuhi mpaka usiku saa 4, guess nitakua nimekusanya shingapi? Mtaji nilioaanza nao ni kama laki 7 Lakini progress unaiona na mtaji unakua, je huko Kigoma, Mpanda, Bariadi unaweza kumwaga viatu barabarani na usiuze hata kimoja.

Nilifanya harakati za viatu hapo karume nachukua viatu ndani kwa jumla namwaga nje, ndani ya mwezi nikawa na pointer wengi sana Pamoja na wafanyabiashara wa jumla kutoka mikoani huko naanza kuuza saa 11 usiku kufika saa 2 asubuhi jamaa zangu wa gairo nawahesabia mzigo wote tunapatana nachukua changu, hivi nitajie mkoa gani hii inafanyika? Labda Hapo Soko la mtumba memorial Moshi tena kwa kiwango kidogo.

Nimefanya harakati Nyingi sana hapo na Kila harakati niliofanya ilinilipa, mpaka nikaondoka Jiji ilo. Mikoani Huku mzunguko hamna, pesa ni ngumu, ukifungua harakati wachawi ni wengi sana, Sasa kijana unakaa Kigoma, Mpanda Katavi, Babati, Njombe, Shinyanga na unaridhika kabisa?

Sasa hivi Niko vijijini huku na mtaji Sasa Lakini Cha kufanya sikioni naona kama nitazika pesa.

Tokeni huko nendeni kwenye Jiji lenye pesa nyingi.
Anawaingiza Cha kike huyu
 
Maisha popote penye riziki mkuu, mi Kuna sehemu npo mwaka wa 2 huu yaani nahisi kama nilichelewa kupajua yaani siwezi kwenda popote hata uniambie wapi

Hapa nimejipa likizo ijumaa narudi huko, na hakuna hata network ya internet huko, lazima ndo pananiweka mjini na napakubali kinoma
Mkeo mjini umemwachia nani?
Usalama upo kweli?
Usije ukawa unatafuta pesa sana na wenzio wanatafuna mkeo sana.
Joking boss.!!
 
Back
Top Bottom