Jina lake ni Abdulrauf Songea Mbano siyo Songea Mbano Sultani wa wangoni wakati wa vita vya Majimaji 1905 - 1907

Mimi mwenzako ni mhehe kabisa, najua vyema historia ya kabila langu, kama uislam ungekuwepo Iringa kwa hizo karne unazozisema wewe basi Iringa ingekuwa imejaa dini ya uislam...lakini kinyume chake uislam Iringa upo sehemu chache sana hasa Iringa mjini nao ulikuzwa na watu wanaoitwa wakonongo watu waliotoka tabora huko....nenda hata huko kalenga kwenyewe ambako ilikuwa ngome ya Mkwawa utakuta uislam haujaenea.....leo hii useme mkwawa aliitwa abdalah hakuna ambaye Iringa atakuelewa.....hata ukoo wake wenyewe asilimia kubwa ni wakristo na si waislam.....kwahiyo hoja yenu haina uhalisia zaidi ya udini ndo maana naipinga na naishangaa
 
Hassan Mambosasa,
Kama wewe unahisi ulifichwa sisi wenzako hayo yote tunayafahamu ndo maana nasema nyie hoja hii umeiambatanisha na udini kuliko uhalisia....hata ushahidi wa mazingira tu utakukatalia....uislam wake ulijulikana na familia zaidi na si watu wake....ndio maana hilo jina abdalah halijulikani....
 
Mtoa mada lengo lako nimelifahamu sana wala hakuna utafiti ulioufanya.Haya mambo ya kiimani wakati mwingine yasitawale sana vichwani, ngoja niishie hapo
Mpyana...
Hii hofu uliyonayo wewe haikuanza kwako na wala haikuanza leo.

Hii hofu ndiyo iliyofanya historia ya kweli ya TANU na uhuru wa Tanganyika iingie katika matatizo.

Ikiwa wewe nimwenjeji hapa jamvini utakuwa umenisoma katika mijadala hii.

Hofu hii ndiyo iliyofanya pia historia ya Majimaji nayo iingie katika matatizo na ndiyo tupo hapa sasa tunajadili.

Hofu hii ndiyo pia iliyofanya historia ya Mapinduzi ya Zanzibar nayo iingie katika mtafaruku mkubwa hadi ilipokuja kuandikwa na Dr. Harith Ghassany nami nikiwa ''Research Assistant,'' wa utafiti ule.

Kuwa sijafanya utafiti ukipenda naweza nikakuwekea hapa tafiti zangu na zimechapwa na zinasomwa ulimwengu mzima katika vyuo vikuu vinavyosomesha African History.

Sasa sijui nani anatumia imani yake vibaya.

Yule anaeivuruga historia kwa hofu yake akidhani anailinda imani yake au yule anaeiweka sawa?
 
Sawa ni mwislam and then??
Mtemikwilla,
Kinachofuatia ni kuwa taarifa ambayo kwa miaka ilikuwa haifahamiki
inakuwa inafahamika na kuongoeza elimu katika somo.

Sasa ukifika hapa linakuja swali kwa nini Waislam walipambana na wakoloni?
Hebu angalia picha hizi kisha unambie inakupa funzo au ujumbe gani?:


Kushoto Mwinjuma Mwinyikambi, Makisi Mbwana Julius
Nyerere na Mshume Kiyate Uchaguzi wa Rais 1962



Mshume Kiyate na Baba wa Taifa 1964.

Mtemikwilla,
Unawajua wazalendo hawa na mchango wao katika kupigania uhuru
wa Tanganyika?

Unajua sababu kwa nini historia ya uhuru ilipoandikwa hawa waliifuta?
Unaweza hata kukisia kwa mbali sababu za haya yote?
 
Unalifahamu jina la chifu wa wahehe wa sasa
 
Mohamed Said,
Yaani kuna watu wapumbavu sana,hebu tuambieni what 'Islam "as a religion had to do with majimaji war,
Usitaje majina yao kwamba kwa vile ni ya ki arabu,basi hiyo ilikuwa silaha tosha katika mapambano.

Je kabla ya kwenda vitani,watu waliitwa wengine wakakataa,lakini viongozi wa " kiislam"kwa kutumia mahubiri misikitini,wakaweza kuwashawishi waumini,kwamba kupigana vita ni wajibu wao!!!,
Nao wananchi,kwa ushawishi wa dini,wakaingia vitani!??,ni kweli ilitokea hivi??

Kuna watu wanatuaminisha,kwamba Uhuru wa TZ,uliletwa na waislam,kwa sababu shughuri za kudai Uhuru,zilifnyika dar, na dar ni pwani,wenyeji wengi ni Islam,kwahiyo Uhuru uliletwa na waislam,
Nataka niwaulize,mnafikiri,Tanganyika ni Dar pekeyake,harakati nyingi zipo zilizocfanyika nje ya Dar,
Hata mapambano ya kupinga ukoroni,yalifanywa na watemi wengi wa makabira mbali mbali,.
Jamani msipotoshe historia,

Kwanini mnakuwa na obsessation na uislam,
Radical Muslim,wanaamini kwamba wa Islam bora ni wazungu wa USA,na UK,ila hawajijuhi tu,kila jambo zuri,lazima liambatanishwe na u Islam!!?

JWTZ kwa miaka kadhaa iliyopita,imekuwa na wenyeji wengi wa musoma,je ni sahihi kusema na kuweka kwenye historian kwamba, mipaka ya nchi hii,na vita vyote turivyopigana,wamepigana wakurya,wajita,waluo,wakati sisi wazaramo,wamakuwa,na wakwere,tunakura madafu na ngisi!!!??kweli?

Wahaya ni wasomi wa kwanza nchi hii,je ni sahihi,kusema,maendeleo ya kitaaluma yameletwa na wahaya.

Al shababy,boko haram,daesh,wote hawa ni Islam,au Arabs kwa majina,na dini wanayoamini,je 100yrs kutoka Leo,ni sahihi kusema,uislam,ndio dini ambayo imezalisha vikundi vya kigaidi dunia nzima,kwamba dini hiyo inamchango mkubwa sana ktk ugaidi.???

Pale Zenj,takwimu zinaonyesha,vitendo vya kuwatendea watoto vibaya,sodomization,vimekithiri sana,sasa ukitegemea 99%ya wenyeji ni Islam,je ni sahihi kusema,dini inamchango mkubwa,ktk hili,?kama sio,kwamba hawa waharifu wanatenda haya kwa tabia zao chafu,sio dini inayowasukuma,then,hata wale walipigana vita,walisukumwa na uzalendo wao,bila kujari,majina yao ni Joseph,yusufu,Ashraf,Ali,
Islam had nothing to do with their patriotism,
Uislam,upo mpaka sasa,mbona huo uzalendo hatuuoni,Ndani ya siasa(CUF),Somalia,Libya,
 
JUAN MANUEL,
Juan...
Umeghadhibika na kutumia neno, ''upumbavu.''
Hii ni moja ya ibra ya historia hii kila inapoelezwa ghadhabu zinapanda.

Umesema mengi na sitoweza kukujibu yote.
Nina swali moja tu kwako.

Kwa nini historia hii inakukera?
 
My consign is nn kimepelekea wewe kutaja uislam? Kwa nn usitaje majina yao kukosewa au kutoandikwa kwa makusudi.
Mtemikwilla,
Kilichonifanya nitaje Uislam ni kuwa baada ya uhuru zilifanyika jitihadi
ya kuifuta historia ya Uislam katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Kwa ajili hii nikaamua kufanya kuiandika ili watu waamue nani mkweli
kati ya historia rasmi iliyoandikwa na Chuo Cha Kivukoni ipi ya kweli
ipi ya uongo:

 
wangoni hatuna sultan
Mack...
Nakuwekea hapa nukuu kutoka kwa wanahistoria Wazungu walivyomwandika Songea Mbano
tena kwa kumtaja kwa jina la Rauf:

''This letter written to Sheikh and Sultan Mataka bin Hamin Massaninga reads:

Sultan Songea bin Ruuf writes: To the Shaykh and Sultan Mataka bin Hamis Massaninga. Greetings, etc. I am sending you a letter through Kazembe. We have received an order from God that the Europeans must leave the country. We are in the process of fighting them here. I believe that we have long since been reconciled,[so] send me your children, so that we may make an alliance. I had wanted to send you some cattle as a gift, but am not able to

do so, as the war which God desired is continuing. Send me a hundred riflemen, and support me in storming the Boma (Songea).

I am also sending you a flask of the Prophet Muhammad, which contains the means for conquering the Europeans. Have no doubt about it, it possessed great power. And when we have taken the Boma (Songea), we shall go on the stations on the Nyasa together, you and I. Now, let us forget our old quarrels.

This bottle, with a da’wa, has been sent by Chinyalanyala himself, the war leader. He also sends the container (kombe), and sends you many greetings.

If your men will come, then Chinyalanyala himself will come and will give you many of the holy things.

Hassan bin Isma’il greets you.

Many salutations,

Sultan Songea bin Ruuf.” [1]


[1] C.H. Becker, ‘Material for the Understanding Islam in German East Africa’, Tanzania Notes and Records, No. 68, February, 1968, p.58.

Barua hii aliyoandikiwa Sheikh, Sultan Mataka bin Hamin Massaninga inasema:

Sultan Songea bin Ruuf anasema: Kwa Sheikh Sultan Mataka bin Hamin Massaninga. Asalaam Aleikum, Ninakuletea barua kupitia Kazembe. Tumepata amri kutoka kwa Mwenyezi Mungu kuwa Wazungu lazima waondoke nchini. Tupo katika kupigananao hapa. Naamini tumeshapatana muda mrefu, (kwa hiyo) niletee wanao, ili tufanye ushirikiano. Nilitaka kukuletea mifugo kama zawadi, lakini sipo katika hali ya kuweza kufanya hivyo, kwa kuwa vita ambavyo Mwenyezi Mungu amevitaka vinaendelea. Niletee watumiaji bunduki mia moja, na niunge mkono katika kulivamia Boma (Songea).

Ninakuletea chupa ya Mtume Muhammad, ambayo ndani yake ipo nguvu ya kuwashinda Wazungu. Usiwe na shaka nayo, ina uwezo mkubwa. Tutakapoliteka Boma (Songea), tutakwenda kwenye vituo katika Nyasa pamoja, mimi na wewe. Hivi sasa tusahau ugomvi wetu wa zamani.

Chupa hii, na daíwa, imeletwa na Chinyalanyala mwenyewe, kiongozi wa vita. Ameleta vilevile kombe, na anakupa salamu nyingi.

Endapo watu wako watakuja, Chinyalanyala mwenyewe atafika na atakupa vitu vingi vilivyo vitukufu.

Hassan bin Ismaíil anakusalimu.

Salam nyingi,

Sultan Songea bin Ruuf.
 
Wee jamaa naona kabisa udini unakusumbua kwa kiwango cha BRT
 
JUAN MANUEL,
Nimesoma vizuri comment yako sasa kuna kitu umenitatiza, je ni sahihi kuisema historia ya jwtz ukitaja askari walipokuwa wakitoka bila kuutaja mkoa wa Mara? Kumbuka zamani watu walikuwa wakilazimishwa kuingia jeshi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…