wakati wenzetu wanapambana na maisha kuboresha hali zao sisi tunapambania majina,mungu atusaidie.
mosi,kwenye maisha unaweza pewa jina la imani au utani au tukio au jina likawa maalumu kwa ajili watu wawili walioshibana na wakajipa jina maalumu hivyo kueana majina km kraf,abdullahman ,karl ,goetzen,herman castro,vladimir ,lumumba,seyyid,said, nk ni mapenzi baina ya aliepokea jina na alietoa au mapenzi ya wazazi na majina hayo yalikuwa na malengo ya kutunza kumbukumbu ,kudumisha urafiki,kumuepusha mtu na adui nk mfano wakati twining anaondoka au anaanza ugavana wtt wengi wa kikristo hasa upande wa kiprotestant walipewa majina hayo sio wote walimpenda twinning ila wengine ilikua tukio muhimu kwao.
pili,kiafrika hasa kitanzania wazee hawakuwa na uchifu wala usultani ila walikuwa na ufalme wakiamini maeneo waliokuwa wakisimamia ni nchi na sehemu kubwa ya uongozi ilikuwa kurithi au vita,kuingiza uchifu/chief na usultan/sultanate kwa kuhusisha tawala tukihusisha ya kutoka uarabuni au ulaya kwa maana ya ukristo na uislam si kuwatendea haki maana waarabu na wazungu walikuta kuna tawala za kiafrika km waliziboresha na kuzisaidia haimaanishi kuwa wao ndio walionzisha utawala wa milki za wakati huo za kiafrika.
tatu,tafiti za wasomi mara nyingi zinaegemea kwa mtu alie gharamia tafiti au mtazamo binafsi wa mwandishi,mfano mkwawa kuitwa sultan kwake haikua inshu kwa kua hakuona inampunguzia au inamuongezea chochote kwenye utawala wake.
nne,ni aibu mtu kujisifu kwa kuitwa john au abdala badala ya kujiita mareale,mirambo,mihambo,masanja,mgonja,mtosa,kibasila nk nk hii ina maanisha kuwa tunapenda kuabudu vya wenzetu hatuamin kuwa hata majina yetu yana hadhi,na km tumepata majina kwa ajili ya historia basi hata hivyo tafit zetu zitakuwa za kujikweza na hazina manufaa kwa jamii