Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

Hapa tu tuombe kwa Mungu atupe neema ya utulivu na yanayobaki tumkabidhi yeye.......hivi viumbe bila goti kwa Mungu ni ngumu. Naimagine Mama J wa watu ni wale wife material na ratiba zake ziko Well fixed, ana upendo mwenyewe maana mpaka kanisani analea watoto ila bado mwanaume kachepuka na kuzaa juu dah
 
Sio tu kukuzidi uzuri unaanza kuimagine alikua anakuja home mnapiga na story, anabeba na mwanao[emoji1787][emoji1787] anatoka nae out alooo hapana Insider asiseme saiz mambo ni mengi sana
Ila huyo Iryn ni mnafiki.. Ningekua mama J ningemchukia na ningemhisi tu anatoka na mume wangu ningempiga STOP kuja kwangu hata simshirikishi Insider. Ningemwambia kabisa Ache kiherehere na shobo.

Sembuse saiv eti nipewe taarifa kazaa na mume wangu aaaahh. Unakumbuka zile picha za zanzibar maneno yalivyomtoka mama J? Hizo ni picha sasa sembuse mtoto,. Aloooo. Insider baba kaa na siri yako.

Mwambie huko mbeleni, ila usifiche hilo suala la mtoto but not now baba.
 
Kabisa ni mnafki sababu kama alijua anampenda Insider angekeep distance na familia yake, matukio yanauma zaidi ukipigwa na mtu wako wa karibu....ndiposa nakazia kama hii story ni ya kweli Insider akae na hii siri mpaka baadae sana
 
Hahahaaaa kwa kweli ni Mungu tu my dear atusaidie pia tusiweke matarajio makubwa sana kwa wenza wetu muhimu tujipende tu wenyewe, tujijali sisi, tusibebe maumivu nafsini mwetu ili tuishi kwa amani tu. Mi anasemaga ntafanya wajibu wangu kwakua napaswa kufanya na ninapenda kuufanya lakini haitamzuia huyu Baba kufanya alitakalo kulifanya, Ni yeye mwenyewe tu
Na Mungu wake basi
 
Yes as in wajibu wa mwanamke ni kutii basi sisi tutimize wajibu, the rest tumuachie Mungu[emoji119]

Sent from my SM-A042F using JamiiForums mobile app
 
Nakuelewa SANA..... yaaani ogopa Sana mnafiki(mtu wa karibu anaekuzunguka) watu wanataka ndugu yetu awe na Iryn iwe jua au mvua lakini hawavuti picha maisha halisi

Yaani inaumiza na kukera vibaya mno unapogundua rafiki yako ni msaliti wa ndoa yako...Kuna msemo unasema hakuna hakunaga Siri baina ya watu wawili yaani itajulikana tu Ipo siku na wanawake wa kichaga walivyo serious ngoja tuone sijui itakuwaje
 
December nitakuja Dodoma na Mama Ariana, usicheze mbali [emoji2763]🤏[emoji2532]
Mkuu thanks kwa burudani, kuna watu huenda wanataka kufungua codes, tafadhari usijaribu kumsikiliza yeyote eti anaomba namba amtumie j zawadi etc. Ataona jina ila najua uko smart sana.
 

Mkuu sijasoma updates zozote za huu uzi, mention yako na ya karena ndio zimenisogeza hapa...

Ngoja nisome nione kama kuna kitu kipya zaidi ya ile Episode ya 70
 
Umetisha halafu umemaliza kibabe...."bora ukajifiche Gaza*. Hahahaha.
 
Umesema kweli, ni bora mama j asikie insider ana mtoto na mwanamke asiyemjua ila siyo aliyejifanya best wake. Atachukua kila kitu cha iryn humo ndani.
 
INSIDER MAN kuna story humu something like wema ni akiba jamaa alikuwa na demu bongo then akaokota dodo la kupendwa na demu wa kizungu mtoto wa kishua , mademu wote wapata mimba ila akaamua kuoa mbongo kwasababu ya mama yake ndo alimchagua mbongo, alijaribu kuachana na yule mzungu ikashindikana na walifanikiwa kupata mapacha, mwisho wa siku mkewe huyu mbongo aligundua wakazungumza yakaisha na mke akabariki yule mzungu akawa bi mdogo, na mzungu akawachukuwa watoto wa mke wa jamaa akaenda kuwalea huko nje so watoto bi mkubwa na bi mdogo walilelewa pamoja ..
 
Mind you.....palikua na MZUNGU[emoji1787][emoji1787][emoji1787] Hapa mtanange ni ngozi nyeusi tupu
 
Nakazia, tujupende na kujijali wenyewe, hata ubibindike vipi, akiamua kuchepuka atachepuku tu.
 
Wakati mwingine una compromise ili maisha yaende.
 
Iryn ni mjanja sana. Insider upo katika situation mbaya. Even if you don't tell Mama J, she will na anajua Mama J will not accept/like sharing and she will leave.
 
Eti bro Watu8 katiba ya kibazazi inasemaje? Amchane mama J kabla hawajaanza process za kubariki ndoa au akaushe mpaka watakapofunga ndoa aje agundue tu mwenyewe kwamba jamaa ana familia nyingine na Iryn?? Ila wanaume mna siri daaahh🙌🙌

Sasa ninaweza kuchangia baada ya kumaliza kusoma kipande cha ziada...

Kwenye ibara zetu za katiba huwa tunasimama na wahenga ya kwamba "kitanda hakizai haramu"...

Lakini kwenye situation ya bazazi mwenzetu INSIDER MAN aliboronga mahali pamoja hapo nyuma kwa kuwafanya Mama J na Iryn kuwa marafiki kwa kiwango cha kuwafanya wajione ni mtu na dadaye, hata uwe bazazi sugu kiasi gani usiruhusu mchepuko ukawa rafiki na 'maza hausi'...

Ushauri:
1. Suala la mahusiano yake na Iryn liendelee kuwa siri kwa sasa, la sivyo hiyo ndoa anayotarajia na Mama J haitakuja kutokea, kama ni kumpa taarifa iwe ni miaka ijayo huko...

2. Nimeona kuna mahali jamaa kaandika ana mpango wa kumpeleka mtoto na Iryn nyumbani kwa wazazi, hii naona haitakuwa busara kwamba wazazi wajue lakini mwanamke aliyesalitiwa hajui chochote, itakuwa kama 'zereu' fulani hivi...

3. Aendelee kumjali Mama J na kumuhudumia kama mke kwa kiwango kisichomithilika, hii itafanya siku atayovunja habari kwa Mama J huenda moyo wa mwanamke huyu wa kichaga utakubali matokeo...
 
Mwenyewe naona hii ni sawa.

Insider my dear zingatia hili..
 
Kiukweli anatakiwa hili jambo aliweke wazi mapema kama tu anataka kuishi nao wote kama wake zake, tatizo litakuja pale tu

Mama J atakapokuwa anawaza muda wote Iryn na Baba J walimfanya mjinga wakijifanya ni mtu na Boss na hata Iryn kutengeneza urafiki naye akifika hapo hiyo hasira atakayokuwa nayo haielezeki

Hakuna kitu kinauma kama mtu kukudanganya kwa kudhamiria kabisa na halafu ukagundua alikuwa anakudanya lazima uwe na Mungu tu kukababiliana na hilo bila hivyo shetani lazima atimize lengo lake kupitia wewe

Lakini kingine kizuri Iryn hana mpango wa kuishi Bongo kwa hivyo hakutakuwa na mikwaluzano na mama J, cha muhimu tumuombee mama J awe muelewa asiwachukie watoto wa mwenzie ili wawe na uhuru wa kuishi na baba yao kama watataka wenyewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…