Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

Alooooooooo.
kilichobaki kwenye huu uzi ni kuutelekeza baada ya mwezi mmoja ndio nitarudi maana mimi sipendi mambo ya kufatanafatana kila masaa kama vile kumbikumbi.
 
EPISODE 17
“A TRUE STORY BY INSIDER”

Muda huu mimi macho yangu yote yalikua yamelenga kwenye zile Box nijue Muajemi kaweka nini mle ndani?, japo zilikua hazinihusu ila nilitamani sana kujua ndani kuna nini.

TUNAENDELEA………

Muda ule zilionekana Box 3 zikiwa mezani hata Iryn mwenyewe ni kama alikua kapagawa maana alikua hajui aanze kufungua box gani muda ule. Upande wangu nilikua natamani kujua kuna nini mle ndani.

IRYN: “Insider nianze na lipi hapa?”

MIMI: “Anza na hayo madogo afu malizia kubwa.”

IRYN: “Pink or orange?”

MIMI: “Pink”

Iryn akatoa ile bahasha na ndani kulikua na kibox ambacho ufunguaji wake ni kama una press kwa pembeni ndo kinafunguka.

Bhasi baada ya kupress ndani kulikua na necklace nzuri sana yenye kidani cha jiwe la Tanzanite na chain ya gold, ilikua ni necklace nzuri sana na palepale nilianza kuiona furaha ya Iryn.

IRYN: “Insider this is pure Tanzanite and pure Gold”

MIMI: “Embu ivae tuone”

Na palepale Iryn aliivaa ile necklace shingoni na ilikuwa imemkaaa perfect utafikir kama alipimwa vile na vipimo, Muajemi alikadiria mlemle hata Iryn alishangaa sana.

IRYN: “Insider hii necklace gharama yake si chini ya 20 million.”

MIMI: “Iryn unafikir haya mambo mimi nayajua bhasi? Mimi nikienda kariakoo napata chain yangu ya 10k na sina habari.”

Na muda huu tuliamia kwenye bahasha ya orange, na Iryn akaifungua ile bahasha na ndani kulikua na vibox viwili (2). Kibox kimoja ndani kulikuwa na Bracelets na kibox kingine kulikua na watch. Bracelet ilikua ina mix ya gold na Tanzanite na ilikua nzuri balaa, saa nayo ilikua ni ya gold.

MIMI: “Hio saa ni bei gani kwa experince yako.”

IRYN: “Hii Chanel watch inacheza kwenye 5 million na hii Bracelet si chini ya 7 million.”

MIMI: “Unataka kunambia hizi gifts mpaka sasa zimecost si chini ya million 30?”

IRYN: “Tena itakua zaidi ya hapa.”

MIMI: “Watu mnanyota za kupendwa asee, mimi hata kupewa zawadi ya boxer sijawai pata.”

IRYN: “Mmmh Insider wewe ni muongo san, hiyo bahasha kubwa ya purple ifungue wewe.”

Nilishika ile bahasha ya purple na nikaichana na wote hapo tulikua tunashauku ya kujua ndani kuna nini. Baada ya kuichana kulikua na Box jeupe, nikalichana lile box kwa juu na nikaanza kutoa vitu vilivyokuwa vimepangwa kwa juu.

Nilianza kutoa kibox cha kwanza kilikua cheupe na kilisomeka “AirPods Pro”, nikatoa kibox kingine kilisomeka “Magsafe charger” , nikatoa kibox cha tatu kilisomeka “Apple watch”. Hapo sasa ndo nikamalizia na box la mwisho ambalo ilikua ni “Iphone 13 Pro Max”.

Lakini Iryn niliona hii zawadi ya simu dizaini kama hajaifurahia kabisa.

MIMI: “Mbona hili box kama hujalipenda?”

IRYN: “Insider hiyo simu utaondoka nayo nimekupa.”

MIMI: “Unanipaje wakati ni zawadi yako?”

IRYN: “Insider huko ndani na simu kibao na zote ni mpya hata sijawai zifungua, hii sasa itakua ni simu ya 12 napewa kama zawadi. Afu huwezi amini nilishasahau uko ndani kama nina simu”

MIMI: “Aiseee mbona una hatari hivyo, yaani unakaa na duka la simu chumbani?”

IRYN: “Ndo hivyo huwa napewa zawadi na watu tofauti sasa huwa naziwekaga kwenye droo tu, mimi natumia simu mbili tu kwa sasa zinanitosha sana.”

MIMI: “Iryn una bahati na unanyota nzuri sana.”

IRYN: “Maybe, ichukue hio simu na vitu vyote vilivyokua kwenye hilo Box, naona unatumia hiyo iphone X ni kadogo sana kwako.”

Ofcourse nilikua natumia Iphone X muda huo na toka niinunue hii simu ilikua ni mwaka tayari.

MIMI: “Thank you Bossy wangu.”

IRYN: “Huna haja ya kushukuru, wewe ni mtu muhimu sana kwangu.”

MIMI: “Ukiskia unalala maskini na unaamka tajiri ndo hii sasa, Insider leo hii namiliki macho 3 aisee, Ahsante sana.”

IRYN: “Hahaha Insider unanifurahishaga sana, ndomana nisipokuona huwa najikuta nakumiss, una vituko sana.”

MIMI: “Iryn mimi sina cha kukulipa ila nakuahidi kukupeleka ukale kitimoto”

IRYN: “Really? Umejuaje kama napenda kula kitimoto?”

MIMI: “Wakati tunatoka pale Kigamboni nilisikia mnaongea na mama Janeth kuhusu nguruwe”

IRYN: “Kumbe ulikua busy na sisi wala sio barabarani.”

MIMI: “Iryn kichwa cha hesabu hiki.”

MIMI: “Kweli kabisa hata sikushangai, nasubiri hiyo siku ya kwenda kula kitimoto.”

MIMI: “ASAP, wewe kuwa na subira tu.”

Bhasi nilikaa na Iryn pale mpaka saa 4 usiku na tulipiga sana story huu usiku. Nikamwaga nakwenda kulala, akanisindikiza tukawa bado tunapiga story pale nje kwake kibarazani.

Tulitoka nje nilikopark gari na nikam-hug pale kwa nguvu ile kama namvuta upande wangu, nilikua nimeegemea gari na tukaendelea kuongea huku nimeizungusha mikono yangu vizuri kwenye kiuno chake.

Iryn alikua na kiuno laini sana yaani kumshika kiunoni vile nilikua na sense zile njia za kiuno na yeye alikua ametulia tulii, na huku nikivuta harufu nzuri ya mwili wake. Nilijikuta muda ule internet ikianza kusoma 5G kwa kasi sana, tuliendelea kuongea huku tuko zero distance na yeye alikua ananiangalia usoni kwa tabasamu, the way ungetuona ungesema sisi ni wapenzi kabisa.

IRYN: “Insider najua sahivi una appointment zako huendi kulala.”

MIMI: “Sinaga appointment zozote usiku labda za wateja, si unajua nategemea hii kazi ili nile?”

IRYN: “Kuna mtu ulikua unaongea naye wakati tuko pale “Pizza hut” kwamba utakwenda kumuona ndomana nasema wewe huendi kulala.”

MIMI: “Hahahaa hamna bhana, yule ni jirani yangu nakoishi, alisema nikirudi nimwone.” (Ilibidi nimdanganye tu).

Na muda huu alitoka yule jamaa anayekaa Apartment ya tatu (Jirani) alituangalia na dizaini kama alikua haamini anachokiona mbele yake. Jamaa alitusalimia na sisi tulimjibu na yeye akaendelea na safari yake.

Nilimuaga pale kwa Iryn na baada ya kuingia kwenye gari nilicheki simu nikakuta misd call 5 za Mary na pia Muajemi alikua kanipigia simu.

Palepale nilimpigia Mary na akasema amemaliza mambo yake na ananisubiri yuko Havanna “opposite na Oryx filling station”. Nikamwambia soon nitakuwa nimefika hapo.

Nilifika pale Havanna na muda huo ilikua saa 5 kasoro, niliingia pale na nilimkuta amekaa kwa ndani anakunywa wine. Wakati naingia alikua hanioni,

MIMI: “Hi Mary”

MARY: “Insider umeniweka sana na simu zangu hupokei kabisa.”

MIMI: “Muda ule nilikwambia kama nitawai kurudi ningekucheki au hukunielewa?”

MARY: “Sasa ndo usipokee simu?”

MIMI: “Mary nadhani unaijua fika kazi yangu, siruhusiwi kupokea simu kabisa na ilikua silence hata sikusikia, afu nilikua na mteja nimezunguka naye leo siku nzima.”

MARY: “You look great, sijawai kukuona ukichomekea unapendeza namna hii.”

MIMI: “Ahsante siku moja moja sio mbaya.”

MARY: “Umependeza sana Insider.”

Muda huu wakati naongea naye nilikua nimesimama na yeye alikua amekaa kaunta kwenye viti virefu. Na mimi nikakaa pembeni yake, nikaagiza nipewe glass, maana wine ilikua nyingi sana kwenye chupa, tukaendelea na story zetu.

MIMI: “Hivi ningechelewa kurudi ingekuaje?”

MARY: “Ningekusubiri tu, najua ungenipigia tu.”

MIMI: “Na kama simu ingekua imekata chaji?”

MARY: “Ningemaliza wine yangu ningeondoka.”

MIMI: “Mimi kesho natakiwa kuamka mapema sitakaa sana hapa ujue.”

MARY: “Insider nitakaa na wewe hapa mpaka wanavyofunga.”

Baada ya kuona Mary hataki mimi kuondoka pale mapema ilibidi nimuahidi tutatoka out siku na hapa ndo akakubali.

MIMI: “Nitakutoa out bhasi, ili tuwe na muda mrefu wa kuongea, how about this?”

MARY: “Promise?”

MIMI: “I promise”

Nilitumia kama dakika 45 kuwa naye pale Havanna na muda huu, Mary alikuwa akiniuliza kinachoendelea kati yangu na Prisca, na nikamwambia hakuna kinachoendelea kati yetu.

Ilibidi nimpeleke Prisca mpaka kwao na nikamwacha getini mimi nikaondoka kurudi kwangu, na muda huo ilikua inafukuzia saa6 za usiku

Nilirudi home na kama kawaida yangu lazima niingie kuoga, kiukweli nilijikuta nam-miss mama J wangu. Nyumba ilionekana kuwa ya ajabu sana bila wao, muda kama huu nikirudi home nilikua nikicheza na jembe langu Junior, nilijikuta nawa miss sana, nilitamani sana kumpigia simu Mama Junior lakini nikaacha.

Nilitoa lile box kwa mara nyingine nikaitoa ile simu nikaingalia tena, nilikua siamini kwakweli kama Iryn aliweza kunipa.

Muda uleule nilitoa simu nikampigia simu Iryn, na baada ya muda alipokea na tukaanza kuongea.

MIMI: “Hi mummy.”

IRYN: “Ushafika home?”

MIMI: “Nimefika sio muda sana.”

IRYN: “Nilijua umepitia kwenye appointment zako za usiku.”

MIMI: “Hahaa, usiniwazie hivyo bhana, appointment zinakuwaga za kikazi.”

IRYN: “I know Insider, don’t worry.”

MIMI: “I just wanted to say thank you. Thank you for everything, unajua Iryn wewe ni mtu muhimu sana kwangu.”

IRYN: “Insider usiwe na wasiwasi, you have done alot to me.”

MIMI: “Kama ni mzani hauko balansi kabisa.”

IRYN: “Insider kesho tutaendelea na ratiba zetu za usiku uwe ontime, mimi na usingizi byee…”

MIMI: “Byee”

Iryn yule mwanamke alikua na roho nzuri sana, hakuwa mchoyo na alikua na utu sana. Unajua sometimes nilikua nawaza Iryn anaweza akawa sio kiumbe wa kawaida kabisa. Kupitia Iryn nilipata pesa nyingi sana, licha ya hapo nilipata connection za watu mbalimbali.

Iryn hakuwa na dharau kabisa na aliniheshimu sana na alikua akinishirikisha mambo yake sana.
Upande mwingine heshima iliongezeka sana hasa nikiwa naye, hakua demu wangu ila nikitembea naye nilikuwa najiona ni moja ya wanaume wenye bahati ya kuongozana na Mrembo mkali.

Baada ya kumaliza kuongea na Iryn, nikakumbuka wakati niko na Mary pale Havanna Prisca alikua akipiga simu sana na sikupokea simu zake muda ule, hivyo ikabidi nimpigie tuongee. Nilimpigia simu na ndani ya sekunde chache aliipokea simu yangu;

MIMI: “Nambie mrembo”

PRISCA: “Safi tu”

MIMI: “Unaendeleaje?”

PRISCA: “I am doing great”

Niligundua kama Prisca hayuko sawa maana alikua akitoa majibu ya mkato sana na sio kawaida yake.

MIMI: “Mbona kama mnyonge sana?”

PRISCA: “Insider unataka niseme nini?, you don’t even care about me, you just wanted to open my legs and run”

Ofcourse maneno ya Prisca yalinichoma sana, na nilijiona na hatia sana ni kama nilikua na umiza hisia zake. Pia hakua demu wangu, maana sijawai mtongoza ni kama mwanamke ambaye alijipa tiketi kwamba tayari tuko kwenye mahusiano.

MIMI: “Prisca huko unafika mbali sana, unajua nilikua busy sana leo.”

PRISCA: “You are always busy, you never have time for me anymore.”

MIMI: “Prisca naomba tutafute siku tuongee sawa?”

PRISCA: “Okay”

MIMI: “Goodnight” na nikakata simu.

Niliwaza pale hivi huyu Prisca bado sijamtongoza ila kama tayari kashajipa tiketi tayari yuko kwenye mahusiano na mimi. Niliwaza pale kitandani nimpotezee au niendeleee naye maana niliona Prisca ni kama bomu la nyuklia, kuna siku litakuja kulipuka na yakawa majanga.

Nilikuwa pale kitandani nikiendelea kutafakari juu ya ile simu lakini nikapata wazo hii simu acha nimpe mama J wangu. Niliwaza hivyo sababu mimi niliona kutumia ile simu ingekua risk, muda wote niko barabarani ningeweza kuibiwa tu. Nilichukua maamuzi ya kumpa simu mama J, na nikasema mimi nitachukua simu yake “Iphone Xs Max” kidogo kubwa, na ipo kikazi hata ikiibiwa sio ghali kama hii iphone 13.

********

Ijumaa ratiba zangu ziliendelea kama kawaida nilikwenda kwa Mama wa2 ile asubuhi kumchukua mwanae na yeye alikua ameamka. Mama wa2 alikuja pale nje na mwanae na tukaanza kuongea, na moja ya mazungumzo yetu alinambia nitampeleka Bagamoyo “The Horizon”, na alinisisitiza sana nisije nikamchinjia baharini na mimi nilimtoa hofu.

Baada ya kumdrop mwanae pale Mikocheni nilimptia Maggy na tukaelekea Posta. Sasa wakati tuko njian Maggy alinambia jumamosi kutakua nakazi ya siku nzima, lakini nilimwambia nina mteja wa kumpeleka Bagamoyo bhasi lile dili nikampa jamaa yangu Kizoka.

Saa 5 asubuhi Muajemi alinipigia simu na tuliongea sana kwani alifurahi sana na alinikubali sana. Akaomba badae jioni tuonane pia ana mazungumzo mengi na mimi, na mimi nilimkubalia, hivi unaanzaje kumgomea Tajiri??.

Hii siku nilipiga sana kazi, bhasi kuna mteja nilimchukua karibu na Mahakama ya mirathi “Temeke” alikua ni Msomali. Nilimtoa pale ilikua jioni na nikamdrop kule kurasini, njiani tulikua tunapiga story sana na alikua anajua Kiswahili vizuri tu. Baada ya kumdrop Msomali pale Kurasini aliomba namba yangu ya simu na mimi nikampa akasema atakua ananicheki sana tu, nikamwambia ahsante bossy. (Sasa huyu Msomali tutamkuta huko mbele).

Muda huo ilikua jioni tayari nikampigia simu Muajemi anipe Location, akanambia niende moja kwa moja mpaka Msasani. Baada ya dakika 10 akanirudia tena, akanambia tukutane pale “Golden fork” Mikocheni.

Nilidrive gari mpaka pale na yeye alikua bado hajafika eneo la tukio na sikutaka kumpigia simu kabisa. Na muda ule alikuja dada pale mezani kunisikiliza na mimi niliagiza juice ya nanasi.

Baada ya dakika 20 Muajemi ndo alifika eneo la tukio na alinipigia simu, baada ya kupokea simu akaniuliza kama nimefika, nikamwambia nimefika muda sana.

Na ndani ya dakika 3 alikua kashafika sehemu niliyokuwa nimekaa, na yeye kama kawaida aliagiza coffee.

MUAJEMI: “Bro mambo vipi?”

MIMI: “Freshy kaka za toka jana?”

MUAJEMI: “Kaka jana ilikua siku nzuri sana” alikua akicheka.”

MIMI: “Jana sikutaka kukupigia simu kabisa, sikutaka kukuharibia siku. Hahahahahaha!”

MUAJEMI: “Bro yule mrembo ni Malaika, jana nilijikuta nataka kupoteza confidence, na yule mwanamke anajiamini sana, she’s very smart & clever.”

MIMI: “Bila shaka mliongea mengi sana.”

MUAJEMI: “Kaka tuliongea mengi sana na kama ulivyonambia nimefanikiwa kwa asilimia kubwa. Na amenipa kazi ya kumnunulia mashine za saloon, tayari nimesha order mpaka jumatatu zitakua zimefika.”

MIMI: “Ukifanikisha hilo nafikiri utakua na nafasi nzuri ya kumpata.”

MUAJEMI: “Wewe ndo unatakiwa unipe mbinu ili nimpate kirahisi.”

MIMI: “Bro ukweli Iryn mimi sina mazoea naye sana ni “Unpredictable” hatabiriki kabisa, kuna kipindi tunacheka, kuna muda anakua kauzu. Ila pia sipendi kuingilia maisha yake personal, kama nilivyokwambia kipindi kile kuwa ana boyfriend na ninamjua vizuri. Hayo mengine ni wewe maana mimi siwezi kuingilia maamuzi yake, ila mbinu niliyokupa kama utakwenda nayo vizuri utawin.”

MUAJEMI: “Kweli kaka hivi wazazi wake wako hapahapa?”

MIMI: “Jana hamkuongelea hili?”

MUAJEMI: “Bro! tuliongea sana mambo ya biashara.”

MIMI: “Nakwambia ila ibaki kuwa siri yako.”

MUAJEMI: “No problem, I promise”

MIMI: “Mama yake alifariki ila Baba yake yuko South Africa, na mama yake alikua anafanyia kazi Organization X.”

MUAJEMI: “Mama yake alikua anafanyia kazi Organization kubwa sana kwakweli, ndomana Iryn anaoneka hana shida na Pesa.”

MIMI: “ Kama nilivyokwambia siku ile, Iryn hana shida na pesa kabisa, pesa anazo.”

MUAJEMI: “Now I believe, na kuhusu mzee wake?”

MIMI: “Ukweli kuhusu mzee wake sijui sana kuhusu yeye ila Iryn alinambia ni mfanya Biashara.”

MUAJEMI: “Pole yake, nafikiri jana ningemwuliza haya ningekua nimejua mengi.”

MIMI: “Bro afadhali hata hukumwuliza haya, maana Iryn hapendagi kuongelea kabisa habari za mama yake, subiri kwanza mfahamiane vizuri then muulize.”

MUAJEMI: “No problem, unajua hizi habari huwa zinaumiza sana.”

MIMI: “Msasani ndo unaishi?”

MUAJEMI: “Yeah, nina mke wangu pale. Insider nina wake 2, huyu wa Tanzania ni mke mdogo, mke mkubwa yuko Saudi Arabia. Iryn akikubali nitamfanya awe mke wangu wa 3, Dini yangu pia inaniruhusu”

MIMI: “Matajiri mnataka kumiliki warembo wazuri tu, sisi maskini acha tuendelee kupambana na level zetu.”

MUAJEMI: “Iryn nimetokea kumpenda sana.”

MUAJEMI: “Nilimwambia Iryn jana nataka twende Zanzibar na Dubai, mimi, yeye na wewe na alisema atajifikiria.”

MIMI: “Sijakaa nikaongea naye toka tuachane jana, kama atanishirikisha nita mconvince sana, maana mimi hata kupanda ndege sijawai.”

MUAJEMI: “Hahahaa Bro! Ndege utapanda tu usijali.”

Tuliongea mambo mengi sana na Muajemi muda ule na pia sikutaka kufungua CODE zote kumuhusu Iryn, nilikua makini sana. Tulitumia saa 1 mazungumzo yetu Na baada ya hapo alisema tuongozane mpaka Parking alikokuwa amepaki gari.

Tulifika pale Parking na alikua kapark Marcedes Benz “GLE- class -Coupe” rangi ya Pearl na ilikua inang’aa sana. Hii gari ilitaka kuendana kimuundo na “BMW X6”.

Na muda ule Muajemi alinambia niingie ndani ya gari, ile kuingia ndani ya gari nilikua nikishangaa uzuri wa ile gari mle ndani. Nilijisemea moyoni kuna watu hii Dunia wanaishi na wanakula maisha sisi wengine tunawasindikiza tu.

Muajemi alitoa bahasha ya kaki kwenye droo na akanikabidhi.

“Bro ile ahadi yetu ni hii hapa”

Muajemi alinishukuru sana kwa jana na akasema mambo mazuri yako njiani. Tuliagana pale na mimi nikaenda moja kwa moja kwenye gari yangu “IST”. Nilifungua ile bahasha na nilitoa bunda 5 za noti za elfu 10 na palepale nikajua zile ni million 5. Muajemi alifanya kuniongezea milion 2, nilifurahi sana kwakweli muda ule.

Nilifurahi sana maana niliona mipango yangu inakwenda vizuri upande wa pesa, niliwasha gari na kuondoka pale kuelekea kwa Iryn na wakati niko njiani alipiga simu na nikamwambia niko njiani soon nitakuwa pale kwake.

Na muda uleule nilimpigia simu dada Tyna wa pale Airport nikamwambia anisaidie kupata tiketi ya kwenda Dodoma jumapili na jumatatu nitarudi, akasema hilo limekwisha na soon atanitumia contol number nilipie.

Saa 2 kasoro ndo niliwasili kwa Iryn na nilipark gari nje getini, nikaingia ndani. Hii siku nilikua nimependeza sana kwani asubuhi nilikwenda kazini nikiwa nimechomekea utafikiri nakwenda ofisini.

Niligonga mlango na Iryn alitoka kunifungulia mlango, baada ya kuniona alishangaa sana ni kama hakuamini ndo mimi Insider ambaye nimechomekea.

IRYN: “Insider umependeza sana kwakweli”

MIMI: “Thank you Mummy”

IRYN: “You look so Handsome, ulikua unafanya Uber au?”

MIMI: “Ndio ndo natoka ofisni hapa.”

IRYN: “Insider unaipenda sana kazi yako, unani inspire sana kwakweli. Insider nenda kale bhana muda umekwenda mimi nikamalizie kuvaa, tuondoke.”

Niliingia jikoni nikapakua chakula na nikaanza kula na yeye alikua amekwenda kujiandaa, na muda huo Tyna alikua kanitumia control number nilipie na palepale nikalipia kupitia simu TZS 420,000/=.

Suala la kupanda ndege kwenda Dodoma sikutaka kuleta ubahili kabisa maana nilikua nahitaji kwenda na kurudi haraka Dsm. Na muda huo Tyna alipiga simu akanambia ananitumia ticket zangu kwenye whatsapp na pia jumapili tutaonana.

Iryn alitoka pale na hao tukaaondoka pale na muda wote Iryn alikua akiniangalia sana.

IRYN: “Insider leo umenisapriz sana,”

MIMI: “Tunakwenda wapi kwanza”

IRYN: “Tunakwenda Hotel moja iko kawe”

MIMI: “Njia unaijua? Maana hii hotel sijawai fika kabisa.”

IRYN: “Hata mimi sijawai fika, tutatumia Map.”

Hii hotel kama unatokea round about kawe ukiwa na Mwaikibaki Road, ipo nyuma kabla hujafika Kawe mzimuni. Kuna kabarabara ka vumbi kanaingia kulia afu pia kuna bango lina direct jinsi ya kufika pale hotelini.

Tulifika pale na Iryn akaniacha Parking na yeye alikwenda ndani kuonana na mteja wake. Na mimi nikashusha kiti nikalala maana nilikua nimechoka sana hii siku.

Nilikuja kushtuka baada ya kusikia simu ikiita na ghafla ikakata, nikaichukua simu yangu kucheki ni Iryn na palepale nikaona message ambayo ilikua imetumwa dakika 15 zilizopita ikisema,

“Insider naomba uje hotelin ndani haraka
I’m in danger, please. Room No. 222”

NB: Kutokana hili tukio lilitokea nimeona haitakuwa busara kuitaja hii hotel sababu za kibiashara na usalama.

TO BE CONTINUED

Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu
 
Kabla sijausoma niwatag kwanza walioomba kutagiwa
mtani21 na Dadii
 

Daaaah hatari[emoji122][emoji122][emoji122][emoji122]
Lakini mkuu jumamosi mbali[emoji23][emoji23][emoji23]
Unatuacha na bonge la alosto,kuna saa na jaribu ku imagine jinsi mtoto irene alivyo basi unanichanganya[emoji23][emoji23]
Anyway all is Good!
 
Aloooooooooooo
Tumeanza kuingia deep sasa
 
Kaka hongera sana ila kaka jumamosi mbali mkuu fanya kesho kama itakupendeza kaka! Maana huu ni ulevi wetu
 
Haya The body guard katoe msaada kwa boss wako Iryn.😊
Dakika 15 ni nyingi sana kwenye threat🙄
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…