Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

SEASON 02
CHAPTER 34

“BY INSIDERMAN”

PREVIOUS:
Wakati tukiendelea na maongezi, nilimuona Iryn akija mahali tulipokuwa na alikuwa amependeza sana. Sister alimuona na alianza kumuangalia kwa makini, kwani alihisi kwamba ndiye Iryn. Iryn, baada ya kutufikia, alianza kumwangalia sister kwa umakini. Sister aliamua kusimama, na wakaanza kuangaliana kwa kimya, bila hata mmoja kuzungumza na mwingine.

CONTINUE:

Sister alibadili mwelekeo wa macho yake, akalenga macho yake kwenye tumbo la Iryn kwa umakini mkubwa. Ilikuwa kama haamini kile anachokiona sasa hivi.

Iryn ndiyo alikuwa wakwanza kuongea pale;

IRYN: “Hi wifi.”

SISTER: “Iryn, ni vizuri kuona umerejea salama, lakini ulituacha na wasiwasi mkubwa. Kwanini ulikuwa hupatikani, hasa ukiwa katika hali kama hii?.” Na alimpa ishara ya kuketi.

IRYN: “Nisamehe sana wifi, nilikuwa katika kipindi kigumu sana, na nilihisi kama natakiwa kujitenga kwa muda, nilihitaji muda wa kutafakari mambo.”

SISTER: “Umejua jinsi tulivyokuwa na wasiwasi? Tulikuwa na hofu kubwa kwa sababu ya hali yako, ilitubidi kuja Afrika Kusini kukutafuta!"

IRYN: “Naelewa kabisa, na najuta kwa kile kilichotokea. Hivi sasa, nipo tayari kuelezea kila kitu na ninaomba msamaha kwa maumivu yote niliyowasababishia."

SISTER: “Tunakupenda na tunakujali, hatuwezi kukaa kimya wakati hatujui ulipo na hali yako."

IRYN: “Nashukuru sana kwa juhudi zenu, sikutaka kuwafanya mtaabike. Nilikuwa nikihangaika na mambo mengi, lakini sasa najua kuwa nilikosea kutowasiliana nanyi.”

SISTER: “Tuna furaha kwamba umerejea salama, lakini tafadhali, usitufanye tena kuwa na hofu kama hii. Siku nyingine usijitenge kiasi hicho, nipo hapa kukusaidia changamoto yoyote unayopitia."

IRYN: “Afadhali ningekuwa nakujua ningeweza kuja kwako unisaidie, nimejifunza, na ninaahidi kwamba sitafanya hivyo tena. Nawashukuru kwa uvumilivu wenu na kwa upendo wenu. Naomba mnipokee tena, tuwe na amani."

SISTER: “Embu niambie tatizo lilikuwa ni nini? Brother kwa upande wake alifunguka vya kutosha, ningependa kusikia kutoka kwako, tatizo lilikuwa ni wapi?.”

Baada ya kuona sister yuko serious sana, ilibidi niwaage ili niwape uhuru wa kuongea na nikaondoka kwenda room.

Baada ya kufika room nilimpigia simu Mary maana alikuwa kanipigia sana, kipindi niko na Sister, hivyo nilitamani sana kumsikia alichotaka kuzungumza nami. Nilimpigia simu na kwa haraka alipokea tukaanza maongezi pale na alionekana kununa;

MIMI: “Hi my baby.”

MARY: “Why didn’t you pick up the phone?”

MIMI: “Sorry bae, nilikuwa naongea na sister, I miss you.”

MARY: “Please! Insider, tell me the truth, do you really love me?”

MIMI: “Yes, I do love you. Why are you asking me this?”

MARY: “Since Iryn karudi, huna mapenzi tena kwangu, you know, I feel bad.”

MIMI: “Don’t be my love, nikirudi Dar es Salaam tutaspend vya kutosha, just me and you.”

MARY: “Unarudi lini?”

MIMI: “Kufikia jumapili nitakuwa nimerudi, pia nataka tuongee suala la mtoto.”

MARY: “Don’t be too late, I miss you badly.”

MIMI: “Bye, see you then.”

Baada ya kuongea na Mary, nilimpigia simu Hilda maana tangu Iryn aje Dodoma hatukuwa na mwasilino yoyote. Hilda aliniomba msamaha kwa kumpa Iryn namba yangu ya simu, lakini nilimwambia alifanya jambo jema, hivyo hakuna haja ya kuwa na wasiwasi.

Hilda alinipa taarifa kwamba mama Janeth kasafiri tena. Vilevile, Asmah na Sumaiya wananiulizia sana. Nikiwa na hayo akilini, niliendelea kumsisitiza Hilda kwamba asije thubutu kuitoa namba yangu.

Baada ya lisaa kupita, Iryn alinitumia ujumbe uliosomeka;

“Darling, sisi tumehamia kwenye rooftop. Kwenye begi langu kuna simu mpya, naomba uje nayo. Pia, niambie nikuagizie nini?”

Nika reply;

“Seafood 😋😋”

Nilifungua begi lake nikaona simu mpya ya iPhone 14 Pro Max, nikajisemea kuwa hii lazima itakuwa zawadi ya dada. Nilitafuta bahasha, nikaiweka na kuelekea huko. Kwa mbali niliwaona wakiongea na kucheka, nami nikavuta kiti nikakaa.

Muda huu walikuwa busy sana wakipiga story mbalimbali kuhusu Ethiopia na tamaduni zao. Kwa upande wa dada yangu, alikuwa akishangaa sana kumuona Iryn akijitahidi kuongea Kiswahili. Ingawa Iryn anaongea Kiswahili, sio fasaha kabisa, kuna baadhi ya maneno yanamsumbua, kama vile neno “ugali” ambalo yeye anasema “ungali.”

Muda wote wakiongea mimi nilikuwa kimya, kwani sikutaka kuingilia maongezi yao. Nilitoa ushirikiano pale nilipohitajika tu. Sister alipendekeza kwamba jumapili twende Serengeti kutalii na turudi jumanne, na Iryn alifurahi sana kusikia mapendekezo haya kutoka kwa dada yangu.

Muda ulikuwa umeenda, hivyo sister alituaga na aliniomba sana niende nyumbani kesho ili nikamsalimie na shemeji. Kabla ya kuondoka, Iryn alimpa dada ile zawadi, na sister alishukuru sana, akasema ataifungulia mbele ya safari.

Tulimkampani sister mpaka nje kwenye parking alikokuwa amepark gari yake. Walikumbatiana kwa hisia, nami nikamalizia kwa kumkumbatia pia. Baada ya hapo, sister akaondoka.

Iryn alikuwa na furaha sana baada ya kuonana na sister yangu, na alisema nimebahatika sana kuwa na dada anayejitambua na kuongeza kwamba amempenda sana dada yangu. Kwa upande wangu, sikutaka kumuuliza walichoongea na dada, kwa sababu nilijua kuwa ningemwona dada yangu kesho.

Baada ya kufika chumbani, alinivuta kitandani kwa haraka. Kilikuwa ni kitendo cha haraka sana, kisha akapanda juu yangu, akianza kuvua gauni lake. Ndani, alikuwa hajavaa chochote, na alichukua mikono yangu miwili akaiweka tumboni mwake, akionyesha jinsi alivyotaka niwe nalichezea tumbo lake. Kisha, alinyanyuka kidogo, akaikamata magazine, na kuanza kuiingiza taratibu, kwa ajili ya kutengeneza njia ya mtoto. Baada ya kazi ndefu alichoka sana na aliishia kulala palepale juu yangu.

Saa nne asubuhi, nilienda nyumbani kwa sister Sakina. Bahati nzuri, nilimkuta shemeji naye aliishia kunikaribisha, kwani ilikuwa muda mrefu hatujaonana. Kwa upande mwingine nilikuwa nikiwashangaa madogo kwani walionekana kukua sana, kwa sababu ni muda mrefu sana tangu nilipowaona mara ya mwisho.

Sister aliaga anakwenda jikoni kupika na alituacha pale seblen na shemeji yangu. Tulijadili mambo mengi, kuanzia changamoto za maisha ya kila siku hadi ndoto zetu za baadaye. Mazungumzo yetu yalikuwa na mvuto na yalijaa hekima, na nilipokea maoni ya thamani na muhimu kutoka kwake.

Kwa upande wangu, nilimkaribisha kwa moyo mkunjufu aje kwangu kusalimia pale atakapokuwa Dar es Salaam. Aliahidi kuja, lakini aliongeza kuwa tatizo langu ni kwamba huwa namtenga sana.

Baada ya kupata chakula cha mchana, tulitoka nje mimi na dada yangu na tukakaa kibarazani kwa ajili ya maongezi. Kitu kikubwa nilichotaka kufahamu ni maongezi yao ya jana akiwa na Iryn;

SISTER: “Mke wako hajakwambia?”

MIMI: “Sikutaka kumuuliza, nilijua leo tutaonana, hivyo nitajua.”

SISTER: “Tuliongea mambo mengi sana, mengi tulishaongea siku ile. Ukweli ulizingua sana, una bahati sana ni vile dada anakupenda.”

MIMI: “Nakusikiliza dada yangu.”

SISTER: “Yeye anasema wewe huna hatia, yeye ndo aliamua kuibeba mimba bila kukushirikisha. Amenifungukia kwamba anakupenda sana ndomana aliamua kubeba mimba na hayuko tayari kuharibu mahusiano yako na mama J.”

MIMI: “Mmh sawa, mama J atakuwa tayari kukubaliana na hili jambo?”

SISTER: “Nimemwambia huoni umefanya maamuzi ya haraka ambayo yatapelekea mafarakano kwenye mahusiano yake na mama J?”

MIMI: “Akasemaje?”

SISTER: “Ameahidi kuwa mstari wa mbele kuhakikisha kwamba siri hii itabaki kuwa yenu pekee. Bro! hali hii tayari imetokea, na lazima ukubali kwamba ulikosea sana. Mimi kama dada yako siwezi kukulaumu sometimes inakuwa ni mipango ya Mungu. Mtoto ni damu yetu, hatuwezi mkataa, hivyo inabidi niendelee kuwa naye karibu aone tuko pamoja.”

MIMI: “Vipi kuhusu home kwa mama na mama J tutawaambiaje?”

SISTER: “Tunawaambia au utawaambia wewe? Naona umeshaanza kuniingiza taratibu kwenye msala wako.”

MIMI: “Nakutegemea sana kwa hili maana bila wewe siwezi.”

SISTER: “Subiri kwanza ajifungue, then mambo mengine yaendelee, usiwe na haraka.”

MIMI: “Sawa dada yangu nashukuru kwa hili.”

SISTER: “Usijali tutapanga, ila sasa utulie sitaki kusikia umemzalisha mwanamke mwingine au unachepuka tena, tutagombana.”

MIMI: “Sawa dada yangu.”

SISTER: “Kama mwanamke umempata kwa hili acha nikupe sifa kaka yangu.”

Tuliishia kucheka wote na kuendelea na mipango mingine kuhusu Iryn. Nilishinda pale nyumbani kwa dada yangu hadi jioni, kisha nikaondoka kurudi hotelini kwa sababu Iryn alikuwa anapigia simu sana.
*****
Asubuhi na mapema ya Jumapili, sister alifika hotelini tayari kwa safari ya kuelekea Serengeti. Gari la kukodi kwa ajili ya tour lilikuja kutuchukua hotelini, na tulianza safari yetu saa 4 asubuhi.

Ilikuwa safari ndefu ya takriban masaa saba hadi tulipowasili Serengeti National Park, na tukafikia Four Seasons Safari Lodge. Kufikia muda huo, giza lilikuwa limeingia, hivyo tuliamua kupumzika, tukisubiri siku inayofuata kwa shauku ya kuanza safari yetu ya kutalii.

Asubuhi na mapema, baada ya kupata kifungua kinywa kizuri, tulianza safari yetu ya kwenda kuanza utalii. Tulikuwa na hamu kubwa ya kuona mandhari na wanyama wa porini. Bahati nzuri, tulikuwa na mwenyeji mzuri ambaye alituongoza na kutuelekeza mbugani kwa ufanisi mkubwa.

Tulitembea huku tukifurahia kila hatua, tukiona wanyama mbalimbali kama vile simba, tembo, na twiga. Hali ya utulivu ilitawala, na tulikuwa na amani kwani mwenyeji wetu alitufanya tujisikie salama. Hatukuwa na wasiwasi hata kidogo, kwani kila kitu kilipangwa kwa uangalifu. Kila kona ya mbuga ilitupa uzoefu mpya na wa kipekee, na tulifurahia kila dakika tuliyokuwa huko.

Tulitumia siku mbili za kipekee pale Serengeti, tukifurahia uzuri wa mandhari na wanyama wa porini. Kila siku ilikuwa na jambo jipya la kuvutia, na muda ulionekana kupita haraka. Siku ya jumatano asubuhi, tuliondoka Serengeti na tukarudi Arusha kwa ndege ya binafsi.

Tulipofika Arusha, tulijiandaa kwa safari nyingine ya kurudi Dar es Salaam. Hapo ndipo tuliagana na dada yetu. Alikumbatiana na Iryn kwa hisia nyingi, na kisha akaondoka huku akitabasamu. Ilikuwa siku yenye hisia mchanganyiko, furaha kwa muda mzuri tuliotumia pamoja na huzuni kidogo kwa kuagana.

Katika zile siku mbili tulizotumia Serengeti, jambo la kufurahisha zaidi lilikuwa kuona jinsi Iryn na dada yangu walivyotokea kuelewana sana. Ingawa mwanzoni walikuwa hawafahamiani sana, muda tuliotumia pamoja uliwapa fursa ya kuzungumza na kufahamiana zaidi. Walikuwa wakicheka, wakishirikiana mawazo, na hata kupanga mambo ya baadaye kwa furaha kubwa.

Kila wakati tulipokuwa tukifanya utalii, mara nyingi walikuwa wakiendelea na mazungumzo yao ya ndani, wakionekana kufurahia urafiki mpya uliokuwa ukichanua kati yao. Ilikuwa faraja kwangu kuona jinsi walivyojenga uhusiano wa karibu kwa muda mfupi.

Tulipofika Dar es Salaam, tulielekea moja kwa moja Coral Hotel. Wakati tuko njiani, Iryn aliniambia angependa twende tena Zanzibar kwa mara nyingine. Hata hivyo, kutokana na hali aliyokuwa nayo, nilimkatalia kwa upole na kumwambia, 'Kwa sasa hapana, tulia tu, upo kwenye kipindi muhimu cha karibu kujifungua, hivyo unapaswa kupumzika.'

Tulipokuwa hotelini, tulipanga kutafuta apartment ya kuishi kwa muda wa kipindi hiki atakachokuwepo Dar es Salaam, kabla ya kurudi Afrika Kusini. Alisema tutakaa kwa wiki mbili, kisha ataondoka kwenda Afrika Kusini kwa ajili ya kujifungua.

Kesho yake, tulipoamka, tayari tulikuwa tumeanza mwezi mpya wa sita. Kwa upande wa Iryn, hali yake ya ujauzito ilikuwa imeendelea sana. Tumbo lake lilikuwa kubwa, na alikuwa akionesha dalili za kuchoka, hali iliyokuwa ya kawaida kwa hatua aliyokuwa nayo. Nilipomuangalia, niligundua pia kuwa alionesha ishara za karibu za kujifungua muda wowote.

Siku hiyo, tuliondoka hotelini mapema ili kwenda kuonana na dalali, tukiwa na lengo la kuangalia apartments. Tulitembelea apartment tatu, kila moja ikiwa na sifa tofauti. Hata hivyo, apartment iliyotuvutia zaidi ilikuwa ile iliyokuwa nyuma ya Coco Plaza. Ilikuwa na mandhari nzuri na ilikidhi mahitaji yetu kikamilifu. Baada ya kuitazama kwa umakini, hatukusita kufanya uamuzi. Tulifanya malipo palepale bila kuchelewa, tukiwa na furaha kwa kupata sehemu nzuri ya kuishi.

Baada ya kumalizana na dalali, tuliondoka kuelekea ofisini. Tulipofika, tulikuta mazingira yakiwa kimya sana, kana kwamba kila mtu alikuwa bize au hapakuwa na shughuli nyingi. Tulipoingia ndani, Nollie alikuwa pale kwenye mapokezi, na aliponiona, alishangaa sana na alikuja kunisalimia.

Haikuchukua dakika nyingi, Hilda akaja kwa kasi na kunikumbatia kwa furaha. Hapo ndipo hali ya utulivu ilibadilika kabisa, ndani ya muda mfupi, lobi ilijaa watu. Wafanyakazi walikusanyika huku sura zao zikionyesha furaha kubwa. Kila mtu alionekana kufurahi kuniona, lakini kilichonigusa zaidi ni jinsi Winny alivyoonyesha furaha ya pekee. Alionekana kweli mwenye furaha kuniona, hasa kwa sababu hawakuwa na taarifa zangu kwa muda mrefu. Siku hiyo ilikuwa ya kipekee, ilijaa shangwe na hisia za kukutana tena na watu wa karibu.

Nilitoka nje kukaa kibarazani nikiwa na Hilda na tukaanza maongezi na alionekana kufurahi sana;

HILDA: “Insider nimefurahi sana kukuona, pia naona furaha yako imerudi tena,”

Nilicheka kwanza;

MIMI: “Soon naenda kuwa baba wa watoto wawili lazima niwe na furaha.”

HILDA: “I’m sorry nilishindwa kuvumilia nikampa namba Iryn, lakini nimefurahi mmeyamaliza.”

MIMI: “Usijali Hilda, ulifanya jambo zuri sana.”

HILDA: “Weeh! Hapa ofisini kila mtu anakusifia hawaamini kama kweli Iryn kakubali kuzaa.”

MIMI: “Achana na wanawake wa humu ndani, ndomana Asmah alikuwa anajifungia ndani.”

HILDA: “Umenikumbusha, halafu Asmah anakuuliza sana, ana wasiwasi sana juu yako, naomba umtafute.”

MIMI: “Nitamcheki, nafikiri tutaenda ofisini kwake.”

HILDA: “Ndo umerudi mazima? Nikukabidhi ofisi yako.”

MIMI: “Wewe endelea Hilda, ushachukua kiti changu, sina jeuri ya kukutoa, pia kwasasa na mambo mengi siwezi kurudi ofisini.”

HILDA: “What? Najua utarudi tu, Iryn anakutegemea.”

MIMI: “Naona una simu mpya kitu fourteen.”

HILDA: “Zawadi kutoka kwa wifi yangu Iryn.”

MIMI: “Hongera sana unastahili pongezi kwakweli hata mimi nitakupa zawadi.”

HILDA: “Zawadi gani?”

Kwa kumnong’oneza;

MIMI: “D*ck.”

Hilda aliishia kunipiga kwa ngumi ya mgongo kwa utani, kisha tukaendelea na mazungumzo mengine. Baadae Iryn alitoka na akasema tuondoke twende Mikocheni kumwona Lucy.

Nilirequest Uber ili atupeleke Mikocheni, na ndani ya muda mfupi tuliwasili na kisha tukaingia ndani. Tulipofika, wafanyakazi wa pale walishangilia kwa furaha baada ya kuniona. Ilikuwa ni furaha ya kukutana tena, na niliendelea kupiga nao stori huku tukicheka na kushirikiana mawazo.

Hata hivyo, kelele zetu zilimvuta Lucy kutoka ofisini kwake. Alipotuona, alimkumbatia Iryn kwa furaha, lakini mimi hakutaka hata kunisalimia. Japokuwa hali hiyo ilinifanya nijisikie vibaya kidogo, nilijaribu kuweka hali ya utulivu kwa muda huo.

Iryn aliusoma mchezo mzima ulitokea pale na aliishia kunikonyeza. Nilijua kilichomchukiza Lucy ni suala la kutopatikana kwa simu, hivyo nilipanga kuongea naye pembeni, ili tumalize tofauti zetu.

Mchana tuliamua kutoka kwenda Golden Fork kwa ajili ya kupata lunch ya pamoja na timu nzima ya pale ofisini. Ilikuwa ni chakula cha pamoja, ambapo kila mmoja alionekana kufurahia muda huo. Baada ya kumaliza, tulirudi tena ofisini tukiwa na hali ya kuridhika.

Muda ulipokwenda, niliona ni bora nijaribu kuongea na Lucy ili tuondoe ule ukimya na kutoelewana. Hata hivyo, jitihada zangu hazikufanikiwa. Lucy alionekana kukerwa na hakutaka kuongea nami kabisa. Aliniambia moja kwa moja kuwa hataki kuniona. Maneno hayo yalinichoma, lakini nilijua kuna jambo kubwa zaidi lililokuwa likimtatiza, hivyo niliamua kumpa nafasi ili apate utulivu.

Hatukutumia muda mrefu pale ofisini, hivyo tuliondoka kurudi Masaki. Tulianza kwa kupitia Coral Hotel kuchukua mabegi yetu, kisha tukaelekea kwenye apartment. Baada ya kufika, tulikaa na kutulia kwenye balconi, tukipiga story kwa utulivu;

IRYN: “Baby, please twende Zanzibar tukatembee hata siku mbili, umenikatalia kufanya Baby shower hata Zanzibar?”

MIMI: “Hali yako si unaiona? Nina wasiwasi ndomana.”

IRYN: “Mimi kujifungua bado, I think kuanzia tarehe 20 huko, ndo kwanza tarehe 1.”

MIMI: “Unaona hata wewe huna uhakika unaonaje tukienda kujihakikishia hospital?”

IRYN: “No problem, na kama niko sahihi tutaenda sindio?”

MIMI: “Deal.”

IRYN: “Badae nitaenda kumsalimia Mama J, nipe namba zake niawasiliane naye.”

MIMI: “Usijaribu wala kuthubutu kwenda kuonana naye, utaleta matatizo tu.”

IRYN: “Why? Hivi hujui kwamba nisipoenda ndiyo atazidi kuamini anachowaza ni kweli?. Acha niende nikamsalimie nijifanye kama sijui kinachoendelea, hii itasaidia kumuweka sawa, trust me.”

Niliwaza pale nikaona anachoongea ni sahihi,

MIMI: “Sawa, lakini mpigie simu mwambie uko Dar unataka kwenda home kumsalimia, uone atajibu nini.”

Nilimpa namba ya mama J, na bila kusita akampigia simu. Kwa kuwa alitumia namba ngeni, alijitambulisha kwanza, kisha wakaanza mazungumzo. Walizungumza mambo mengi, na baadaye akamweleza nia yake ya kwenda nyumbani, na mama J wangu akamkubalia.

Kipindi chote wanaongea sikio langu lilikuwa makini sana likidaka mawimbi, baada ya kumaliza kuongea, alinigeukia;

IRYN: “I told you, sasa nitafanya jambo moja muhimu sana, nikifika pale home nitaweka sawa hili jambo linalomsumbua.”

MIMI: “Sawa.”

Nilipanga kwamba Iryn akienda kuonana na mama J, bhasi na mimi nitumie muda huu kuonana na Mary ili tuyajenge.

Saa 11 jioni tulienda SALI Hospital kwa ajili ya kuangalia maendeleo ya ujauzito kwa ujumla. Tulipofika, vipimo vilichukuliwa kwa umakini, na muda mfupi baadaye matokeo yalitolewa. Ilikuwa ni furaha isiyo na kifani kwangu, kwani nilijihakikishia kuwa mtoto alikuwa wa kike. Pia, daktari alituambia kwamba Iryn angeweza kujifungua kuanzia tarehe 24, jambo lililonifanya nijisikie zaidi kujiandaa kwa ajili ya siku hiyo muhimu. Tafrija na msisimko kuhusu ujio wa mtoto wetu yalikuwa wazi kwetu sote.

Kwa ujumla, daktari alisema maendeleo ya mtoto ni mazuri, pamoja na afya ya mama, jambo lililotupa utulivu zaidi. Alinipa pia ushauri wa umuhimu wa kuwa karibu na Iryn wakati huu wa mwisho wa ujauzito, kwani ni kipindi nyeti kinachohitaji uangalizi wa karibu. Maoni yake yalinifanya nione uzito wa jukumu langu la kumsaidia na kumfariji zaidi tunaposubiri siku ya kujifungua.

Baada ya hapo, Iryn aliondoka kwa Uber kwenda home kuonana na mama J, nami nilitoa simu mfukoni, kisha nikampigia Mary. Simu iliita kwa mara ya kwanza bila kupokelewa na nikapiga tena kwa mara ya pili, haikupolewa. Wakati nikijifikiria cha kufanya, yeye ndo alinipigia na nikapokea pale;

MIMI: “Mke wangu upo busy? Au ndo bado umenichukia?”

MARY: “Nilikuwa mbali na simu.”

MIMI: “Niko Dar naomba tuonane. Upo wapi now?”

MARY: “Niko home, tukutane wapi?”

MIMI: “Triple 7 pazuri zaidi kwa kukutana.”

MARY: “After 30 minutes nitakuwa nimefika.”

MIMI: “Sawa nami naanza kutoka hapa.”

Nilirequest uber wa kunilipeleka Triple 7 na baada ya kufika nilimkuta Mary kawasili tayari akinisubiri. Nilivuta kiti nikakaa, kisha nikamsalimia na tulianza kuangaliana pale;

MIMI: “Nimekumiss sana mummy.”

MARY: “Ulisema unarudi jumapili na leo ni alhamisi unaona jinsi ulivyo muongo?”

MIMI: “Sorry, nadhani nilikwambia kinachoendelea. Iryn kaniganda sana kwa kipindi hiki naomba uwe uvumilivu, akiondoka kwenda South tutaenjoy.”

MARY: “Sawa baby, mimi nakumiss sana ndomana unaona nakusumbua.”

MIMI: “I know mpenzi wangu, vipi kuhusu lile jambo letu? Bila shaka umeshajifikiria vya kutosha.”

Mary aliniangalia muda huu, nami nilimshika lips zake nikawa nazichezea;

MARY: “Utawezaje kutumudu wote? Iryn karudi soon atakuwa na mtoto wako, mama J ana mtoto mkubwa, still bado unataka na mimi nikuzalie.”

MIMI: “Sijakuelewa hapa, kuwamudu kivipi? Kipesa au?. Mpaka nikasema hivi nimeona naweza, lakini sio lazima ndomana nikakupa muda wa kujifikiria juu ya hili. Pia tambua hustahili haya maisha mummy, you need someone better atakayekupenda na kukuoa kabisa.”

MARY: “Bora niwe na mwanaume nayempenda kuliko kuwa na mwanaume nisiyempenda. Sipendi kufake juu ya hili, maana mahusiano ni suala nyeti sana, sitaki kuharibu future ya kijana wa mtu sababu ya hili.”

MIMI: “Upo sahihi, but naamini utampata hata mimi utanisahau.”

MARY: “Maybe, Baby nimekuona natamani tukafanye.”

MIMI: “Are we discussing this today at this time?”

MARY: “Yes! Please.”

Niliwaza pale, na ukweli alionesha kuhitaji sana game, lakini nilifikiri nikaona si sawa, niende nikalale na Mary then nirudi tena kwa Iryn?. Hapana, haiwezekani.

MIMI: “Mummy nisikilize kwa makini sana, naomba uvumilie Iryn soon anaondoka, tutaenda Zanzibar tukaenjoy sawa?”

MARY: “Baby, really? Even for just 1 hour? It’s impossible.”

MIMI: “Naomba nielewe Mary wangu, kutokana na hali ya Iryn kwasasa, kufanya na wewe si sawa..”

Mary alikubali kwa shingo upande, Japo alionesha kuchukia, lakini sikuwa na jinsi maana ningekuwa ni mpumbavu kama ningemkubalia na tuliagana pale akaondoka kwenda home, nami nikarudi Masaki.

Nimerudi kwenye apartment, lakini Iryn bado hajarudi wala hakuna dalili yoyote ile, nikaanza kupatwa na wasiwasi juu ya Iryn. Niliwaza nimpigie simu, nikaona ni wazo baya, hata kumtumia ujumbe niliona niache. Muda huu nilimpigia simu Lucy, lakini naye hakupokea nikaamua kumpotezea maana niliona anafanya utoto sasa.

Iryn alirudi home saa 4 za usiku na alianza kunipa mkasa mzima wa kilichokuwa kinaendelea kule Mbezi beach akiwa na mama J.

Baada ya kuachana na hospitali, Iryn alielekea nyumbani ambapo alielekezwa na mama J hadi alipoifikia makazi mapya. Alipofika, alikaribishwa vizuri na kupokelewa kwa furaha.

Iryn alifurahi sana kumuona Junior, alimpigia kelele kwa furaha na kumnyanyua juu. Junior alionekana kufurahia sana kama kawaida yake, na Iryn alishangaa kuona jinsi alivyokuwa akikua kwa kasi. Utundu wa Junior ulikuwa umeongezeka zaidi tofauti na zamani, jambo lililomshangaza na kumfurahisha Iryn kwa pamoja.

Walianza maongezi pale seblen na wife alizidi kumshangaa Iryn kuwa na tumbo kubwa sana;

MAMA J: “Karibu sana Iryn ni muda mrefu sana umepita bila kuonana.”

IRYN: “Ni kweli nilikuwa busy na masomo na nikaenda ufaransa kwa baba mtoto kutulia, si waona hali yangu ilivyo kwasasa?”

MAMA J: “Naona, sijui niseme pole au hongera maana soon unakuwa mama kamili.”

IRYN: “Hahahahaa soon tu hata sio mbali. Insider hapatikani kwenye simu na pia kaacha kazi, amekwambia?”

Iryn alianza kutafuta gia ya kumuingia mama J;

MAMA J: “Hapana hajanambia kama kaacha kazi, lakini anapatikana kwa namba nyingine na yuko Dodoma.”

IRYN: “Na hii ndo sababu ya mimi kuja Dar, maana nashindwa kuelewa kwanini aache kazi na hakuna jambo lolote baya tulilomfanyia.”

MAMA J: “Suala la kuacha kazi, mimi ndo nalisikia kwako, alinambia yuko Dodoma kuna project ameenda zianza na atarudi mambo yakikaa sawa.”

IRYN: “Okay! Mimi nimekuja kuwasalimia, nilihisi atakuwepo na yeye, kama hayupo bhasi utanipa namba zake nitampigia simu.”

Baada ya maongezi mafupi anasema waliingia jikoni wakapika chakula pamoja, kisha wakala na waliendelea na story za hapa na pale. Habari njema Iryn alimuahidi mama J kuwa watashirikiana pamoja katika kufanya biashara ya vipodozi, pindi tu atakapo maliza chuo.

Kwa upande mwingine lengo lake halikifanikiwa sababu mama J hakutaka kufunguka kabisa kuhusu ugomvi wetu. Iryn anasema kwa asilimia kubwa aliweza kumuweka sawa kisaikolojia.

Tulianza kupanga mipango ya kwenda Zanzibar kwaajili ya mapumziko na maandalizi ya ujio wa mtoto wetu. Kwa upande wake alitamani sana twende Nungwi na tutafute hotels ambazo ziko karibu na maeneo ya kule.

Bila kupoteza muda, nilianza mara moja kufanya utaratibu wa kuandaa usafiri, huku yeye akiangalia hoteli ya kufikia. Kwa upande wangu, nilifanikiwa kupata boti ya saa 3 asubuhi.

Asubuhi tuliondoka kuelekea Posta, lakini tulianza kwa kupitia maduka ya nguo. Tulinunua nguo kadhaa na vitu vingine vingi. Baada ya hapo, tulikwenda KADOO kufanya exchange ya pesa, kisha tukaelekea ferry kwa ajili ya safari.

Safari ya kuelekea Zanzibar ilianza kwa utulivu, mawimbi madogo ya bahari yakigonga pembeni mwa boti yetu. Tulipowasili, upepo wa baharini ulitukaribisha huku tukiona gari ya hoteli ikitufikia kwa haraka, tayari kutupeleka Nungwi. Nilikuwa na shauku ya kujua zaidi, tunafikia hotel gani maana sikupata taarifa kutoka kwake juu ya hotel aliyopata.

“Tunaenda Riu Palace Hotel," Iryn alisema kwa tabasamu laini, baada ya mimi kumuuliza tutaenda wapi. Jina hilo lilinifanya nitafakari. Nilikuwa sijawahi kuisikia hoteli hiyo kabla, na hata nilipokumbuka safari zangu zote, haikuwa kwenye orodha ya sehemu nilizowahi kufikiria kutembelea.

Nilitabasamu kisha nikamuuliza tena. “Ni wapi huko?” Nilimuuliza huku nikimwangalia kwa udadisi. Aligeuza uso wake na kutazama nje ya dirisha, upepo ukicheza na nywele zake. "Subiri utaona," alijibu kwa sauti ya upole.

Ulikuwa ni mwendo wa lisaa na nusu maana tulikuwa tunaenda taratibu sababu ya hali yake, hivyo dereva alikuwa makini sana. Tuliwasili kwenye hoteli ya Riu Palace, mahali pazuri tulipopumzika na kufurahia mandhari ya bahari. nilianza kushangaa mazingira ya hotel maana ni mazuri sana na baada ya kuingia reception tulipokelewa vizuri sana na tukapelekwa mpaka room yetu.

Room ilikuwa ni private nzuri afu kubwa, kitanda kikubwa, kuna sofa kubwa mbili pamoja na TV kubwa ya inch 65 ikiwa juu ya showcase, bila kusahau min bar. Ukitoka nje unakutana na terrace kubwa yenye private pool kubwa, na sun loungers. Nilibaki nikiishangaa ile room maana ilikuwa ikivutia sana nami niliwaza kwa haraka nikajisemea hapa lazima mama kijacho wangu ametoboka sana;

MIMI: “Baby, mbona umechukua room kubwa sana utafikiri tunakaa mwezi?”

IRYN: “Yeah si waona hali yangu, nahitaji nafasi na faragha ndomana nimechukua hii. Twende swimming kwanza tukapoteze muda then, tukale.”

MIMI: “Tukale kwanza hapa nilipo nina njaa balaa.”

Tulienda kwenye moja ya restaurant ya pale hotelini, na macho yangu yaliendelea kuangaza huku na kule, nikishangazwa na uzuri wa mazingira. Ukimya wa bahari na upepo laini ulijaza kila pembe ya mahali pale, huku mandhari yakitufanya tusahau kabisa uchovu wa safari. Ilikuwa ni sehemu iliyotengenezwa kwa ustadi wa hali ya juu, kila kipengele kilionekana kuakisi uzuri wa asili ya pwani ya Zanzibar.

Mhudumu alifika kwa tabasamu, akatusikiliza kwa upole. Bila kusita, tuliagiza sahani za seafood, samaki waliokaangwa kwa ustadi, kamba, na chaza safi, na kinywaji tuliagiza fresh juice.

Baada ya chakula, tulirejea chumbani kupumzika kidogo, na kuhusu swimming, nilimwambia asijali, kwani muda bado upo. Aliniegemea kwa upole, akitabasamu kwa shukrani, kisha akalala kitandani huku nami nikifikiria kuhusu kile kilichokuwa kimesalia kwenye siku yetu.

Usiku ulipoingia, baada ya kupata chakula cha jioni tulirejea chumbani. Kulikuwa na utulivu wa kipekee, sauti ya mbali ya mawimbi ikipiga kwenye pwani. Tulikaa kwa muda mfupi, tukipumzika, kisha wazo la kwenda kuogelea lilinijia.

"Nadhani huu ni muda mzuri wa kupoteza muda kwa kuogelea," nilimwambia Iryn, naye akatabasamu, akakubali bila kusita.

Tulifika kwenye swimming pool, mwanga wa usiku uking'aa juu ya maji, ukitengeneza mandhari tulivu. Tulijitosa kwenye maji, hali ya baridi ikitufanya tuhisi kama tumekumbatiwa na dunia. Tuliongea kidogo, tukicheka, na kupoteza muda kwa furaha, tukisahau kila kitu kingine nje ya wakati huo. Ni kama dunia yote ilikuwa kimya, tukabaki sisi wawili tu, tukifurahia usiku wa pwani ya Zanzibar. Tulitumia muda mwingi sana tukiswim pamoja na kupeana mahaba motomoto na, baadae tulirudi kulala.
*****

Ilikuwa Jumamosi tulivu tulipoamua kutembea kando ya ufukwe, karibu na hoteli. Mawimbi laini yaligusa miguu yetu kwa upole, huku tukitembea tukishikana mikono. Upepo mwanana ulituzunguka, ukibeba hewa safi ya bahari na kutufanya tusahau dunia nzima.

Baada ya muda, tulianza kucheza majini, kama watoto wadogo tukiwa wenye furaha. Nilichukua picha nyingi za kumbukumbu pamoja na video, tukifurahia wakati huo wa kipekee. Upekee wa kila picha ulikuwa na hadithi ya uhai wa furaha yetu.

Katikati ya mchezo wetu, tulikutana na kundi la wazungu, wanawake wawili na mwanaume mmoja. Walivutiwa na sisi, na mazungumzo yakaanza kama marafiki wa muda mrefu. Walituambia kuwa walikuwa Zanzibar kwa kazi na kufikia hoteli ileile tuliyofikia. Mazungumzo yaliendelea, na ingawa tulikuwa wageni kwao, upendo wao kwetu ulionekana dhahiri. Siku iligeuka kuwa nzuri zaidi, kwa furaha na urafiki usiotarajiwa.

Siku nzima tuliitumia ufukweni, na mwishowe tulirudi hotelini tukiwa tumechoka lakini wenye furaha tele. Tulifika saa moja usiku, tukaoga ili kuondoa uchovu wa mchanga na maji ya bahari, kisha tukajiandaa kwenda kupata chakula cha jioni.

Baada ya chakula, tuliamua kwenda bar kupoteza muda na kufurahia usiku. Kama kawaida, niliagiza Heineken, huku Iryn akiagiza mocktail. Hewa ya usiku ilikuwa ya utulivu, na sauti za mbali za muziki zilifanya eneo hili kuvutia sana.

Saa 6 za usiku tulirudi room kulala sababu Iryn alionesha kuchoka sana, hivyo sikuwa na budi ya kumrudisha kulala. Baada ya kurudi Iryn alinambia tumbo linamuuma, hivyo nimsaidie kumkanda kanda kwa mbali. Nilichukua maji ya vuguvugu nikawa namkanda kwa juu, taratibu na baadae akalala.

Asubuhi baada ya kuamka niliamua kutoka nje na kwenda kukaa kwenye sun lounger nikipata jua tamu la asubuhi pamoja na upepo wa bahari. Nilikuwa mtu ambaye nimetulia sana nikifikiri mambo mengi sana kwa wakati mmoja.

“Naenda kuwa baba wa watoto wawili, soon Iryn atajifungua. Hivyo, majukumu kwangu yanaongezeka kuanzia matunzo ya mtoto na mama yake.”

Nikiwa nimendelea kutulia nilisikia sauti laini ya mama kijacho wangu Iryn, ikiniita;

“Darling.”

Na ile kugeuka namuona akielekea kwa swimming kuogelea, nami niliinuka nikamfuata ndani ya swimming.

“Baby si jana tu ulikuwa unalalamika tumbo linauma?”

“Ndio, lakini sasa niko good. Ni maumivu ya kawaida ambayo kila mwanamke huwa anayapitia hasa kabla ya kujifungua.”

Iryn alionekana kuwa na nguvu sana, mpaka nilishangaa licha ya kuwa na mimba ya miezi 8, lakini bado alikuwa anatembea vizuri, hakuwa akideka kabisa. Ukiachana na hayo bado alizidi kuonekana mzuri, umbo lake likikuwa linavutia barabara.

Tuliishia kuogelea wote mle ndani ya swimming na bila wasiwasi wowote tulianza kuwekana. Ni private room yenye terrace kubwa, hakuna mtu wa kusogea wala kutuona na kutufuatilia, It was just a part of our private life. Baadae tulienda kulala kwenye sun loungers na tuliendelea kupiga story pale;

IRYN: “Baby nilikuona umetulia ulikuwa unawaza nini?”

MIMI: “Nilikuwa nawaza kuhusu maisha, naenda kuwa baba wa watoto wawili soon na wote watahitaji matunzo.”

Iryn aliniangalia kisha akanishika kidevu changu kwa mahaba;

IRYN: “Darling, hili ndo linakufanya uwaze, like seriously?”

MIMI: “Yes! Hata kama una pesa bado matunzo ya mtoto yananihusu kama baba, hio ni damu yangu lazima niijali na kuitunza.”

IRYN: “Sawa nafurahi kuona una mipango juu ya huyu mtoto. Naomba tuongee mambo muhimu kuhusu future yetu na mtoto.”

MIMI: “Sawa mummy nakusikiliza.”

IRYN: “Kwanza nakuhitaji pale ofisini uendelee kuwa manager. Mali zangu zote za huku Dar naomba uendelee kuwa msimamizi, pia nampango wa kufungua restaurant na kampuni ambayo wewe utakuwa Director wa hii kampuni mpya.”

MIMI: “Suala la kurudi ofisini mimi sina shida, kwanza naomba uyamalize na mama.”

IRYN: “Jumatatu tukirudi Dar tutaenda kuonana naye.”

Tulirudi ndani kujiandaa kwaajili ya kwenda kupata lunch na Iryn alivaa gauni nzuri ya kujisitiri na alionekana kupendeza zaidi kuliko kawaida. Ujauzito wake ulimfanya awe na uzuri wa kipekee, na kila tulikopita, watu walikuwa wakimshangaa na kumtazama kwa furaha na shauku.

Hii restaurant tuliyoenda ilikuwa ya wazi halafu kulikuwa na watu wengi sana wakila na kupiga story na asilimia kubwa ni foreigners. Muda huu tukipata lunch kwa upande mwingine Mary alikuwa anapiga simu na nilimtumia ujumbe kuwa nitamcheki baadae.

Haikuchukua muda akareply kwa kutuma emoji;

MARY: “😭😭😭”

Nilireply kwa kumuandikia;

MIMI: “Mummy nitakupigia simu mpenzi wangu niko na mama kijacho hapa.”

Iryn alianza kuongea muda huu;

IRYN: “Baby unachat na nani?”

MIMI: “Dada wa dukani kanicheki kuhusu mzigo, halafu sijatuma odda kwa supplier, ndiyo nimemwambia anitumie namba za mzigo ulioisha.”

IRYN: “Alright, tukirudi Dar tutaongea kuhusu na hii biashara yako. Kingine nataka kama kampuni tukupangie nyumba uishi Masaki uwe karibu na ofisi.”

MIMI: “Nyumba ya kuishi mimi na familia nitahitaji vyumba viwili au vitatu. Na bajeti yake si chini ya $1000. Hizo pesa ni bora mnipe tu ili nijenge nyumba yangu ya kukaa.”

IRYN: “Utajengea wapi kwa Dar es Salaam?”

MIMI: “Nina kiwanja nilinunua Mapinga, nitaenda kujenga kule.”

IRYN: “Mapinga ndiyo wapi?”

MIMI: “Iko pwani kama unaenda Bagamoyo.”

IRYN: “Kutoka city centre mpaka huko kuna umbali gani.”

MIMI: “Kutokea Mwenge mpaka Mapinga ni kama 30km.”

IRYN: “Mbali sana, kwanini usijenge Kigamboni, ni kuzuri sana. Yule kaka agent wetu wa real estate alisema ana viwanja sehemu nzuri sana na atanipa kwa bei poa, unaonaje?”

MIMI: “Tatizo la Kigamboni kumekaa kushoto sana hasa kwa mimi mtu wa mishemishe siwezi kuishi kule. Daraja liko mbali na vivuko vinazingua sana, Kigamboni labda kwa uwekezaji sawa ila kuishi hapana.”

IRYN: “Tafuta kiwanja sehemu yoyote utakayoipenda, then niambie ili tuanze ujenzi. Tafuta ramani nzuri ya nyumba unayoipenda pamoja na makadirio ya gharama za ujenzi, halafu utanipa feedback.”

MIMI: “Are you sure?”

IRYN: “You don’t trust me now?. Sikutegemea kabisa kama ungekataa kuishi Masaki na badala yake umesema tukupe pesa ili ufanye ujenzi, hii inaonesha ni jinsi gani unawaza future na mimi kama mama mtoto wako nitakusaidia kwa hili, na naomba usijisikie vibaya, sijakuhonga ila ninafanya kwa upendo wangu.”

MIMI: “Ahsante sana mummy, sikutegemea kama kuna siku utanisaprize kama leo.”

IRYN: “Baby, hivyo ni vidogo tu, na vingi vinakuja na utafurahi. Toka tufahamiane hujawahi kunipiga vizinga, kuniibia, wala kuwa na tamaa ya kitu chochote kutoka kwangu. Wewe ni mwanaume wa tofauti sana, licha ya mambo yote yaliyo tokea kwenye kampuni still uliendelea kuipigania kampuni na hujaonesha tamaa. Nafikiri hujui what do I feel about you right now, mapenzi yangu kwako yameongezeka, nimegundua nina mwanaume sahihi ambaye ni mpambanaji.

Nilimkatisha;

MIMI: “Baby, huna haja ya kusema hayo yote ni wajibu wangu kama manager na pia wewe ni kama mke kwangu, hii kampuni ni yote sote.”

IRYN: “Nitakuwa mwanamke wa ajabu sana kama nitashindwa kurudisha fadhila kwa haya yote uliyofanya.”

Iryn alionekana mwenye furaha isiyoelezeka. Nilitazama tabasamu lake na nikahisi furaha yangu kuwa naye, tukijua kuwa hivi karibuni tutakuwa na furaha nyingine ya kumpokea mtoto wetu. Ilikuwa siku ya kukumbukwa, tuliyohisi kuwa karibu zaidi na tayari kwa safari mpya ya maisha yetu.

Usiku tulianza kupanga nguo kwaajili ya safari yetu ya kurudi Dar es Salaam. Muda huu Sister alinipigia simu tukaongea na baadae akaomba kuongea na Iryn na habari kubwa alikuwa akimjulia hali pamoja na maendeleo yake kwa ujumla.

Jumatatu, tuliondoka kutoka hotelini, ambapo kama ilivyo ada kwa Iryn, alitoa shukrani kwa wahudumu waliotuhudumia kwa huduma bora waliotupatia. Gari ya hotel ilitupeleka mpaka bandarini kwaajili ya safari ya kurudi Dar es Salaam.

Tuliondoka saa sita mchana kwa kutumia boat, na tulifika Dar es Salaam saa nane mchana. Baada ya kufika, nilirequest usafiri wa kutupeleka Masaki. Mara baada ya kuingia kwenye apartment yetu, tulipumzika kwani tulikuwa na uchovu mkubwa kutokana na safari.

Saa moja usiku, Iryn aliamka na kuanza kujiandaa kwa ajili ya kuonana na mama Janeth. Alipendekeza twende wote, lakini nilimwambia kuwa kwa sasa ni bora aende peke yake. Nilimwambia kwamba baada ya kumaliza huko, nitakuwa na nguvu ya kuonana na mama pia.

TO BE CONTINUED.
EP 34
Benaire
 
Na wanawake huwa wanajua kulipiza vibaya hatari. Hapo maji utaita mma.
Kuna jamaa mmoja alioa na kazaa na mkewe watoto 3 ila jamaa alikuwa kicheche kama Insider hivi.
Mke wake alikuwa mzuri mpole, ila sasa yule mwanamke alivyochoka na mauzauza ya jamaa, alimbwaga mazima. Sasa hivi huyo mama kaolewa na mzungu kabisa jamaa hadi leo anajuta.
Wanawake huwa wanavumilia sana ila wakichoka malipizo yake ni balaa nyengine
Mm huwa sielewi mwanaume mzima unasema mwanamke analipiza kwa kuliwa hahahhahahha no ujinga ujinga
 
Tatizo la waja wanataka tufanane mawazo, stori ukishaiweka public jiandae kwa positive na negative critism so far hata INSIDER MAN mwenyewe anajua kuna pande mbili za maoni na mpaka leo anazipokea zote bila kuchukia wala kulalamika. Refer waleta story wengine ukienda kinyume na wanachotaka kusikia wao huwa wanazira kabisa ila its been a year bado anaileta tena kwa uhalisia wake bila kuwaplease baadhi ya watu.

So sio kwamba tunahukumu bali tunatoa maoni kutokana na tulivyoelewa sisi kamwe wote hatuwezi kuwa na maoni yanatofanana sometime angle yako unaweza kuona ni namba 9 ila mimi naona ni namba 6 ila wote tukawa sawa
Upo sahihi kila mtu ana parception zake, cha muhimu ni msg.
 
Hivi nyie story mnaisoma vizuri kweli? Si kuna mwanamke mwingine Insider alipitaga nae na mama Jr alijua na mgogoro hu ulitatuliwa na huyu huyu sister? Someni story mkiwa na positive mind, msisome mkiwa tayari mna majibu yenu kichwani au chuki or mapenzi kwa mtu. Kule volume 1, kuna watu walikua tayari wana team, yaani team mama J na team Iryn, sijui walikua wanawake or wanaume. Hi story according to mwandishi ni matukio ya nyuma, yaliisha pita, we are not sure kama bado wanaendelea na boss lady or not though ile Benz aliopewa kama zawadi it sound bado anayo, kaulizia spear hapo juu. Tuburudike, tujifunze. Ningekua bado kijana ningeokota madini mengi sana humu, mojawapo ni hi, "Uaminifu ni MTAJI" pia jifunze kusamehe waliokukosea, ukiwa na chuki kwa waliokukosea ni kama kujiadhibu mwenyewe, check tukio la mama wawili but mwamba kaenda kwa mama wawili, kamchukua Pili na katoka nae out na zawadi kamnunulia zawadi kama alivo ahidi, sasa hvi deni na gilt imebaki kwa mama wawili. Ukijikita kwenye mapenzi tu; hutapata kitu cha kujifunza.
Sikujua kama kichwani una vitu, good analysis
 
Hivi nyie story mnaisoma vizuri kweli? Si kuna mwanamke mwingine Insider alipitaga nae na mama Jr alijua na mgogoro hu ulitatuliwa na huyu huyu sister? Someni story mkiwa na positive mind, msisome mkiwa tayari mna majibu yenu kichwani au chuki or mapenzi kwa mtu. Kule volume 1, kuna watu walikua tayari wana team, yaani team mama J na team Iryn, sijui walikua wanawake or wanaume. Hi story according to mwandishi ni matukio ya nyuma, yaliisha pita, we are not sure kama bado wanaendelea na boss lady or not though ile Benz aliopewa kama zawadi it sound bado anayo, kaulizia spear hapo juu. Tuburudike, tujifunze. Ningekua bado kijana ningeokota madini mengi sana humu, mojawapo ni hi, "Uaminifu ni MTAJI" pia jifunze kusamehe waliokukosea, ukiwa na chuki kwa waliokukosea ni kama kujiadhibu mwenyewe, check tukio la mama wawili but mwamba kaenda kwa mama wawili, kamchukua Pili na katoka nae out na zawadi kamnunulia zawadi kama alivo ahidi, sasa hvi deni na gilt imebaki kwa mama wawili. Ukijikita kwenye mapenzi tu; hutapata kitu cha kujifunza.
Hapo kwa mama wawili mwamba katushinda wengi. Huwezi nilaza polisi hii ya TZ na utegemee ukaribu wa aina yoyote tena kutoka kwangu.
 
SEASON 02
CHAPTER 37

BY INSIDERMAN”

PART A

Siku ile nilipokutana na Asmah, nilimwambia kwamba afocus zaidi kwenye maisha yake. Nia yangu haikuwa kumuumiza au kumvunja moyo, bali nilihisi ni muhimu kukaa naye mbali kwa muda ili nirekebishe mambo kati yangu na Iryn. Pia, nilitamani Asmah apate nafasi ya kutafuta mtu ambaye atakuwa sahihi kwake, kwa maisha yake ya mbele.

Tangu siku ile tulipoonana, Asmah amekuwa akinipigia simu mara kwa mara na kuomba tukutane. Hata hivyo, mara zote nimekuwa nikimkatalia kwa visingizio vya kuwa na shughuli nyingi, nikimwambia nitamtafuta baadaye, lakini ukweli ni kwamba sijawahi kufanya hivyo.

Wakati nikiwa Tabora, tuliwasiliana na nikampa ahadi kwamba tutakutana Jumatatu mara tu nitakaporudi Dar ili tuzungumze na tuliweke sawa hili jambo. Niliporudi nyumbani, Asmah alinipigia simu mara nyingi, lakini sikujua kwa wakati huo kuwa alinitafuta sana. Kumbe, mama kijacho alikuwa anaziona simu na ujumbe wake kabla mimi sijapata nafasi ya kuona.

Katika kipindi hiki ambacho Iryn ni mjamzito, nilijitahidi kuepuka ugomvi wowote naye. Simu yangu kubwa mara nyingi nilikuwa namuachia kwa sababu sikuwa na chats zozote zenye utata. Mary, kwa upande mwingine, alikuwa anajua kinachoendelea, na tulikuwa tunawasiliana kwa kutumia namba mpya niliyokuwa natumia nikiwa Dodoma. Pia, Mary alishauri tuendelee kutumia namba hiyo mpya ili Prisca asigundue chochote kinachoendelea kati yetu.

Wakati nikiwa na Iryn pale sebuleni, simu ya Asmah ilipoita tena, Iryn alichoka na hali hiyo na akaamua kuipokea mwenyewe. Alionekana kushindwa kuvumilia zaidi, huku wivu ukiwa unamsumbua.


CONTINUE:

Mimi muda huu sikuwa na uwezo wowote wa kumzuia, hivyo niliamuacha aongee naye na aliweka loud speaker.

IRYN: “Asmah, habari yako.”

Asmah hakutegemea kwamba Iryn angekuwa ndiye anayepokea simu, na ghafla akawa mpole.

ASMAH: “Ooh! Bossy, habari yako.”

IRYN: “I'm good. What's your problem? You have been calling Insider nonstop."

ASMAH: “Alinambia yuko Tabora msibani, nilitaka kujua kama karudi.”

IRYN: “What is really going on between you and Insider? Please tell me the truth."

ASMAH: “Nothing is going on between us. He is one of my closest friends, and I really appreciate that."

IRYN: “Asmah, why are you doing this? I know you’re lying to me. Why are you disrespecting me like that? Fu**cking with my Man, and you know I’m pregnant with his child.”

ASMAH: "I didn't mean what I said."

IRYN: “You know I gave you all my respect, but you still sneak around and sleep with my Man. Usione nimenyamaza kimya, najua kila mchezo mnaocheza. Nilitegemea ungekuwa na heshima zaidi kwangu hasa baada ya mimi kuwa mjamzito, lakini hujali hata kidogo."

ASMAH: “What are you talking about.?”

IRYN: “Are you just pretending not to know what I’m talking about? You’re such a bad bitch, mpuuzi kabisa…..”

Nilipoona Iryn ameanza kupandisha hasira, ilibidi nimtulize na kumnyang’anya simu kwa sababu alikuwa amevuka mipaka. Alisimama kwa hasira, akaibamiza simu yangu kwa nguvu kwenye sakafu, na kisha akaelekea chumbani.

Nilishindwa kuelewa kwa nini Iryn alikuwa na hasira kubwa kiasi hiki, wakati Asmah hakuwa amesema chochote kibaya. Nilipoinama na kujaribu kuokota simu yangu, niligundua kwamba skrini ilikuwa imevunjika, betri ilikuwa imevimba, na sehemu nyingine zilikuwa zimeharibika. Nilimfata chumbani, lakini mlango ulikuwa umefungwa. Nilisikia sauti ya kilio kutoka ndani, na ilikuwa ni kilio cha maumivu makali.

Baby, please fungua mlango.”

Nilianza kugonga mlango pale, lakini hakuonesha dalili za kufungua

Baby, naomba tuongee. Tafadhali fungua mlango, mpenzi wangu."

Bado alibaki kimya na hakuzungumza chochote, aliendelea kulia kwa sauti kubwa. Hali hii ilinisababisha nijisikie vibaya sana, na niliona kama nimemkosea sana.

Niliamua kurudi seating room na kukaa kwenye sofa huku nikitafakari namna ya kutatua hali hii. Niliwaza kwa haraka nikaona ni busara niwe mpole na kumuomba msamaha ili kuepusha matatizo, ukizingatia hali aliyonayo kwasasa hatakiwa kuwa katika hali hii.

Ilipita nusu saa, lakini bado hakuonyesha dalili za kufungua mlango, na hapa nikaingiwa na wasiwasi kwa kuwa nilihisi anaweza kufanya jambo lolote baya. Nilimgongea tena, lakini hakutaka kufungua mlango. Hali hii iliponitatiza zaidi, nikaona ni bora nimtafute Claire kwa msaada, kwani sikuwa na jinsi nyingine ya kumsaidia Iryn.

Kumpata Claire ikawa ni shida maana simu yangu imezingua, nikaanza kuchanganyikiwa maana kuondoka na kumuacha peke yake mle chumbani ni jambo lisingewezekana kwanza ni hatari.

Baada ya kufikiri sana nikakumbuka home ninasimu nyingine ambayo inanamba ya Claire, hivyo nilimpigia simu mama J. Baada ya kumpigia alisema yuko chuo, hivyo ikabidi nimpigie Elena dada wa nyumbani na kumuelekeza.

Ndani ya dakika 5, Elena alinitumia namba ya Claire na bila kuchelewa nikampigia simu;.

MIMI: “Mambo, it’s me Insider.”

CLAIRE: “Hey! Insider mambo.”

MIMI: “Mambo mabaya shem wangu, naomba uje home haraka, please.”

CLAIRE: “Kuna nini? Iryn anataka kujifungua?”

MIMI: “Just come, please.”

CLAIRE: “I will be there soon”

Ndani ya dakika 15 Claire alifika na alikuwa akihema sana kama mtu ambaye alikuwa anakimbizwa, na alianza kuniuliza ni nini kinaendelea?

MIMI: “Claire, Iryn kajifungia ndani chumbani ni lisaa limepita, hataki kufungua mlango.”

CLAIRE: “Na hii simu vipi mbona imepasuka, mlikuwa mnagombana?”

MIMI: “Hapana, ni hasira zake ndo kaibamiza simu chini.”

CLAIRE: “Shem niambie ni nini kinaendelea ili nijue namna ya kuongea na Iryn, usinidanganye.”

MIMI: “Sikia Claire, huu sio muda wa kuanza kuulizana kinachoendelea, Iryn amejifungia na lisaa limepita, anaweza fanya jambo baya. Please, naomba unisaidie kuongea naye, ili afungue mlango, mengine tutaongea.”

CLAIRE: “Iryn, alikuwa analalamika sana, amekumiss, sasa umerudi mmegombana, mapenzi yenu siyawezi asee.”

Tuliongozana hadi mlango wa chumbani, na CLAIRE alianza kumuita Iryn kwa sauti ya upole. Baada ya kusikia sauti ya Cami, Iryn alijibu kwa hasira kwamba hataki kabisa kuniona mimi, na alitaka niondoke maeneo hayo.

CLAIRE: “Shem wewe ondoka, acha mimi niongee naye, akikaa sawa nitakupigia simu uje.”

Sikutaka kuwa mbishi juu ya hili, hivyo nilichukua funguo ya gari na kuondoka maeneo haya na akili yangu iliniambia nenda kwa Asmah. Saa yangu ilikuwa inasoma ni saa 10 jioni, nilihisi lazima Asmah atakuwa ofisini muda huu, nikaelekea moja kwa moja mpaka ofisini kwake.

Baada ya kufika nilipark gari parking ya nje kabisa na nikaingia ndani, nilikuwa niko spidi sana hata mapokezi sikusalimia. Nilimkuta Asmah yuko ofisini na moja ya mfanyakazi mwenzie na baada ya kuniona alisimama na kuja usawa wangu.

“Insider are you okay?.”

Sikutaka hata kuongea naye, nilimshika mkono na kuanza kuondoka naye pale ofisini, hata jamaa aliyekuwa naye alibaki akishangaa, kilikuwa ni kitendo cha haraka sana. ‘In a blink of an eye’.

Asmah alianza kulalamika pale,

“Wait, where are you taking me?”

Sikuwa hata nikimsikiliza muda huu, tulipofika nje ya geti nikampa ishara aingie ndani ya gari na akafanya hivyo, hata yeye alikuwa mpole na alianza kuogopa. Mlinzi alishuhudia lile tukio, lakini hakutaka kuingilia maana ananijua vizuri sana, hivyo alikuwa mpole.

Baada ya kuingia ndani ya gari tulianza kuangaliana na Asmah alionekana kuwa na wasiwasi sana;

MIMI: “Unajua kosa lako ni nini?”

ASMAH: “Insider, sikujua kama Iryn atapokea.”

Na nilimkatisha maongezi yake;

MIMI: “Umeniletea matatizo kwa mama kijacho wangu, unapiga simu wakati unajua fika naishi naye kwasasa na nilikupa taarifa mapema kuwa nitakucheki.”

ASMAH: “Insider, I’m really sorry, lakini haya yote wewe ndo sababu kaa ukijua hilo.”

MIMI: “Unamaanisha nini?”

ASMAH: “Umenichunia sana hadi najisikia vibaya, pale napokukumbuka.”

MIMI: “Mimi sijakuchunia kama unavyosema, ila nilikwambia kwasasa niache nifocus na maisha yangu. Kila siku nagombana na Iryn, juu yako, kwasasa sitaki haya yatokee ndomana nikakwambia vile. Pia, tambua natamani sana upate mwanaume atakayekupenda na kukuoa.”

ASMAH: “Stage niliyofikia, kukaa mbali na wewe ni ngumu. Insider nimekuzoea sana ujue, nawezaje kukaa mbali na wewe kwa yote uliyonifanyia?. Umejitoa sana kwangu, kipindi kile nimepata ajali, bado umenisaidia mambo mengi sana, najiona nina deni kwako.”

MIMI: “Huna haja ya kuwa na deni, sababu nilifanya toka moyoni na sihitaji unilipe. Asmah naomba utambue kwamba nakupenda sana, asingekuwa Iryn, huenda tungekuwa wapenzi na asingekuwa mama J, ningekuweka ndani kabisa.”

ASMAH: “Unataka kusema nini?.”

MIMI: “Upendo niliokuwa nao kwako, kwasasa umehamia kwa Iryn. Na sitaki kumpoteza kisa wewe, naomba uheshimu hili, yule ni mke wangu tayari na nitarajia kupata mtoto soon.”

ASMAH: “Hongera sana kwa kutarajia kupata mtoto soon.”

MIMI: “Please, move on kwa usalama wangu na wa kwako pia, tutaendelea kushirikiana kwenye mambo mengine, lakini tuwe na mipaka. Kwa mara ya kwanza leo Iryn, amepaniki live na ametoa maneno makali juu yako.”

ASMAH: “Hata mimi nimeogopa sana, kwa mara ya kwanza nazifeel hasira zake, na sikutoa neno lolote baya.”

MIMI: “Wasiwasi wake, mimi na wewe tuko kwenye mahusiano ya siri, kipindi hiki cha ujauzito amekuwa na wivu sana.”

ASMAH: “Sasa nafanyaje?

MIMI: “Mpigie simu, omba kuonana naye ili muongee juu ya hili, naamini atakubali muonane.”

ASMAH: “Insider mimi naogopa ujue.”

MIMI: “Mpigie simu sahivi, mwambie unataka kukutana naye, ukionana naye atatulia.”

Asmah alitoa simu yake mfukoni na akampigia Iryn, simu iliita bila kupokelewa, akapiga kwa mara ya pili, ndiyo kupokelewa na akamwambia dhumuni lake ni kuonana ili waongee na Iryn alimkubalia, akasema anamtumia location.

ASMAH: “Mimi naogopa siwezi kwenda.”

MIMI: “Sasa unaogopa nini?, nenda kajisafishe na unisafishe na mimi. Usikubali kitu chochote kile atakachokuuliza, wewe ni mtu mzima utajua utaongea nini.”

ASMAH: “What if kama anaushahidi kwamba we had sex.?”

MIMI: “I don’t think so, nafikiri kuna mtu kamjaza haya maneno, Iryn hana ushahidi juu ya hili.”

ASMAH: “Unajuaje kama hana evidence? Na ameongea vile mbele yangu.”

MIMI: “I know her, ingekuwa kweli anazo mimi ningejua tu, Asmah niamini mimi. You have to clean up the mess for me.”

ASMAH: “Sawa acha niende, kama kuna lolote nitakupigia simu.”

MIMI: “Nipigie kwa namba hii kama utapata shida, nitakuwa around.”

Baada ya kuachana na Asmah nilienda Cocobeach- Wavuvi kempu kutulia. Niliagiza heineken zangu mbili huku namsubiri Asmah. Muda huu nilitumia kuchat na Claire, nilimuuliza kuhusu maendeleo ya Iryn ana akasema yuko sawa, japo alilia sana. Nilimuuliza Iryn anafanya nini kwasasa, akasema amekaa kwa balconi na yuko na mgeni, nikajua ni Asmah wala si mwingine.

Kwa upande mwingine, Claire aliendelea kuniuliza shida ni nini, kwani hata Iryn hakuwa amemwambia sababu halisi ya ugomvi wetu. Nilimwambia aendelee kuwa mpole, na kwamba Iryn mwenyewe atamwambia tu chanzo cha ugomvi wetu.

Iryn ni mmoja wa wanawake ambao hawapendi kuweka maisha yao public, ni mtu ambaye anajali sana faragha ya mambo yetu ya ndani na hataki kuyaeleza kwa watu wengine. Hata kitendo kile cha kumpiga kule hotelin kilibaki kuwa siri yake pekee, hakuna mtu yeyote aliyemwambia kuhusu hilo.

Baada ya masaa mawili kupita na hakuna dalili za Asmah kunicheki, nilianza kuingiwa na wasiwasi. Nilijiuliza kwa nini anachelewa kutoka na nini kinaendelea?. Nilijaribu kufikiria kuhusu kumtumia ujumbe, lakini nikaona kwamba ilikuwa ni wazo baya.

Baada ya nusu saa, Asmah alipiga simu na kuniuliza nilipo. Nikamwambia aje Cocobeach tukutane. Ndani ya muda mfupi alifika Cocobeach na alisema yuko karibu na chupa ya Cocacola akinisubiri.

Nilitoka pale Wavuvi, nikamchukua Asmah, na nikaendesha gari kwa kasi hadi karibu na mitaa ya restaurant ya ‘Amigos’. Huko ndipo nilipokipaki gari na kuanza mazungumzo.

MIMI: “Nipe mrejesho wa mlichozungumza na mama kijacho.”

ASMAH: “Kila kitu kipo sawa kwasasa, nimeongea naye muda mrefu sana na amenielewa. Nimesema ukweli kwamba mimi na wewe tulikuwa kwenye mahusiano zamani wakati tumefahamiana, lakini tuliachana na kwasasa sisi ni marafiki.”

MIMI: “Una uhakika amekuelewa?”

ASMAH: “Trust me japo nimebanwa sana, juu yako. Alisema yeye yuko tayari kutuacha tuendelee na mahusiano, huenda yeye ndiye amedandia treni la watu. Nimemwambia Insider anakupenda sana na hayuko tayari kukupoteza na kila siku anajidai utamzalia mtoto wa kike.”

MIMI: “Umefanya jambo la muhimu sana, ahsante.”

ASMAH: “Nimekubali matokeo, japo nilikupenda sana naomba uendelee na Iryn, kwa heshima na wadhifa wake.

MIMI: “Leo ndo unakiri kuwa unanipenda sana?.”

ASMAH: “Ni kweli, kipindi umeanza mahusiano na Iryn nilikuwa naumia sana hujui tu.”

Simu yangu ilianza kuita na kuangalia ni Iryn alikuwa anapiga simu, nilimuonesha Asmah kuwa Iryn anapiga, naye akasema nipokee haraka. Baada ya kupokea aliniuliza niliko, nikamwambia niko Cocobeach, akasema nirudi home mapema.

Ilikuwa ni saa mbili usiku tayari, hivyo sikutaka kupoteza muda na nilimuaga Asmah kwa kumpa ahadi ya kuonana naye hivi karibuni na nikaondoka kurudi home.

Nilitumia muda mfupi sana kufika, kuingia ndani nawaona wamekaa sebleni, nami nikaketi pembeni ya mama kijacho. Wakati huu
Claire alikuwa akitabamu, kana kwamba kuna kitu anataka kuongea. Haikuchukua muda na aliaga anaondoka kurudi kwake, maana alikuwa na majukumu mengine ya kufanya.

Nilimpa kampani mpaka kwake na tukiwa njiani tulikuwa tunaongea na kubwa alisema, Iryn hajasema chanzo cha ugomvi wetu. Pia, aliendelea kusisitiza kwamba Iryn ananipenda sana. Baada ya kufika kwake, nilimshukuru sana kwa msaada wake na tukaagana pale, nami nikageuza kurudi home.

Baada ya kufika, Iryn alikuwa amekaa kwa balconi, hivyo nilienda na nikakaa pembeni yake. Palikuwa na hewa safi na upepo wa bahari ukipiga eneo hili kwa utulivu sana. Tulianza kuangaliana pale, nami niliamua kuvunja ukimya;

MIMI: “Nambie mke wangu, upo tayari tuongee?”

IRYN: “I’m listening.”

MIMI: “Mummy, mimi na Asmah hatuko kwenye mahusiano naku-apia kwa hili. Usipende kusikiliza maneno ya wabongo, hakuna anayependa kuona mimi niko na mwanamke mrembo kama wewe.”

IRYN: “Lazima niwe na maswali, kwanini Asmah tu, akupigie simu nonstop?. Mchana kabla ya kwenda lunch, alipiga simu mara 3 na bado akatuma message akilalamika sana kuwa unamtenga. Kwa haya yaliyotokea, na ninajua fika wewe na Asmah mlikuwa na historia unafikiri nitawaza nini?.”

MIMI: “Nakwambia ukweli, lastweek niliongea na Asmah akae mbali na mimi, na haya yote ni kwasababu yako, sikutaka uendelee kuwa na wasiwasi juu ya ukaribu wetu.

Ilibidi nimueleze ukweli kuhusu mipango yangu juu ya Asmah, ili aweze kuelewa na sikuona haja kumficha juu ya hili.

IRYN: “Unajielezea sana, nimekuelewa tuachane na haya.”

MIMI: “Baby, I don’t want another woman, and I”ll never disrepect you or my daughter like that.”

IRYN: “Unakumbuka tulikubaliana kwamba mtoto akiwa wa kike jina utampa wewe?”

MIMI: “Yes! Darling, unataka nikutajie jina kabisa?”

IRYN: “Don’t tell me hujaandaa jina bado.”

MIMI: “Niliandaa mummy, from today nitakuita ‘mama Ariana’, do you like the baby’s name?”

IRYN: “Yeah, it’s a beautiful name, and I like it. Thank you baba Aria.”

Furaha yetu ilirudi kama zamani na nilimwambia tuende chumbani tukalale maana muda ulikuwa umeyoyoma tayari.

Saa nne asubuhi nilitoka kwenda Mikocheni kuonana na Lucy, pia nilitamani sana tumalize tofauti zetu. Nilipofika pale ofisini niliweza kuonana na Lucy, bila kupoteza muda nilianza kumuomba radhi kwa kumkosea.

Lucy kwa upande wake alisema, aliumia sana kwa kitendo cha mimi kwenda Dodoma bila kumuaga wala kumtafuta, halafu nikawa nawasialiana na Hilda kwa siri, hiki ndo kilimuuma sana. Lucy, aliendelea kusema kwamba hakutegemea mimi ningemfanyia vile, ukizingatia sisi ni washikaji wa muda mrefu sana.

Ukweli nilikuwa nimemkosea sana, hivyo niliendelea kumuomba radhi na baada ya kumuelekeza sana dhumuni la mimi kufanya vile, hapa ndiyo aliweza kunielewa na kunisamehe.

Tulianza kuongea masuala mengine kwa ujumla na kubwa lilikuwa sakata la Asmah. Alinisisitiza sana kama nina mahusiano ya siri na Asmah, bhasi niache mara moja, kwani Iryn alimpigia simu na kulalamika kwamba anahisi kuna jambo linaendelea kati yangu na Asmah.

Baadae tulianza kuongea masuala ya ofisi maana landlord alikuwa ameanza kusumbua tuondoke, kwani alitoa taarifa mapema.

MIMI: “Iryn kaniachia hili suala nifanye maamuzi, wewe ndo manager wa hapa, unashaurije.?”

LUCY: “Hii location ilikuwa nzuri sana na imekaa kimkakati, tunapata wapi tena eneo zuri kama hili?”

MIMI: “Wateja wako wanaokuja hapa ni loyal customers?.”

LUCY: “Ndiyo na wageni wanakuja wengi sana.”

MIMI: “Nimewaza sana asubuhi nikaona ni bora ofisi ihamie Masaki. Tutaepusha cost nyingi sana, pia Masaki hatulipi pango bado pana nafasi kubwa ya kutosha.”

LUCY: “Kumbuka Mikocheni, tulitarget na wale wa kipato cha kati, tukihamia Masaki si tutawakosa hawa customers.?”

MIMI: “Bei zitabaki kuwa zilezile, na sikuzote mteja anafuata huduma bora, ukiwaambia tumehamia Masaki watakuja tu. Halafu, ijumaa tutakuwa na kikao asubuhi, fikiria hili vizuri na kesho unipe majibu ili tufanye maamuzi mapema.”

LUCY: “Sawa bossy, nipe muda nijifikirie juu ya hili.”

Baada ya maongezi marefu na Lucy, nilimuacha aendelee na majukumu yake huku mimi nikiendelea kukagua ofisi kwa ujumla.

Nilipigiwa simu na mama wawili, na wakati nilipoipokea, sauti ya Pili ilisikika. Alinisalimia na kusema kwamba nimewatenga sana, tofauti na zamani. Maneno haya yaliniuma sana, hivyo nikamuuliza yuko wapi. Alisema yupo ofisini kwa mama yake, na nikamwambia nitakuwa hapo baada ya lisaa.

Baada ya kumaliza ukaguzi, nilimuaga Lucy kisha nikaondoka kwenda ofisini kwa mama wawili. Nilipowapa taarifa kwamba nimefika, walikuja haraka, na Pili alinikumbatia mara tu alipoona.

Tulianza mazungumzo na mama wawili, ambapo habari kuu ilikuwa kuhusu mpango wa binti yake kusoma nje. Nilimuuliza Pili kama anaridhia kusoma nje, na alithibitisha. Baada ya hapo, nilimuomba Pili atupishe ili niweze kuzungumza na mama yake kwa faragha.

Mama wawili alifurahi sana kuniona na aliniuliza kuhusu agenda yangu Dodoma. Nikamwambia project nayoifanya kule na alinipongeza kwa hatua hii, kisha tukandelea na mazungumzo mengine kwa muda mrefu. Baada ya mazungumzo, niliomba niondoke na Pili na kumrudisha baadaye. Mama wawili hakuwa na tatizo na ombi hilo na aliniruhusu.

Niliondoka na Pili kwenda Mlimani na lengo langu lilikuwa kutimiza ahadi ya kumpa zawadi ya simu niliyomuahidi baada ya kumaliza shule. Pale Mlimani, nilionana na jamaa yangu, nikamwambia anipe bei ya iPhone 12, kisha nikampa nafasi Pili achague rangi ya simu anayoipenda. Ilikuwa ni surprise ambayo Pili hakutegemea, na alifurahi sana. Baada ya hapo, tukaenda kula pizza pamoja.

Jioni, nilimrudisha Pili kwa mama yake ofisini, ambapo mama wawili alifurahi sana na kunishukuru kwa zawadi niliyompa Pili. Baada ya hapo, nikaondoka kuelekea Masaki kuonana na Hilda ili nimpe taarifa kuhusu kikao kilichopangwa ijumaa.

Nilimshirikisha Hilda kuhusu mpango wa kufunga branch ya Mikocheni na kuwaleta Masaki, na yeye alikubaliana na wazo hili na kusema ni zuri. Nilimpa taarifa za kikao kilichopangwa na nikamwambia aandae ripoti zake vizuri ili aweze kujibu maswali pindi atakapoulizwa.

Muda ulikuwa umeenda, hivyo nikarudi nyumbani ili niwahi kumpikia mama kijacho. Mara tu baada ya kufika, aliniambia ana hamu ya kula chips na yai. Hapo hapo nikatoa simu na kumpigia Sele ili aandae sahani mbili na firigisi. Nikamuaga naenda kuzifuata, lakini akasema tuende wote, kwani amechoka kukaa ndani peke yake, hivyo tukaondoka kwenda kwa Sele.

Sele alishangaa sana kumuona Iryn akiwa mjamzito tena mimba kubwa, na alisema tuingie ndani tukae tusubiri kwani chips ziko jikoni. Iryn kwa upande wake, alisema anakulia palepale na aliagiza atengenezewe zingine za kuondoka nazo.

Baada ya Iryn kuingia ndani, nilibaki nikipiga story na sele;

SELE: “We mhuni unabalaa hujataka kuchelewesha, umemjaza upepo mrembo.”

MIMI: “Hata ile siku nakuuliza mahindi, yeye ndo alihitaji.”

SELE: “Bossy umetisha sana, unakojolea pazuri sana. Mwanamke kama huyu unapataje nguvu ya kuchepuka?.”

Tuliishia kucheka nami, nikaingia ndani kwa mama kijacho wangu ili tule.

Baada ya kumaliza kula, nilimlipa Sele pesa yake na alikata sahani mbili tu, moja alitoa offa kwa mama kijacho wangu, Iryn alifurahi na tukaondoka maeneo haya.

Baada ya kurudi nyumbani, Iryn alikwenda kulala, nami nilitumia nafasi hiyo kuwasiliana na Mary. Nilitamani kujua mpango wake wa kurudi Dar, na alisema kwamba anarudi kesho, Jumatano, pamoja na Jane. Alitamani sana tungeonana, lakini nilimkatalia na kumwambia avumilie hadi Jumamosi, kwani Iryn ataondoka hiyo siku.

PART B

Siku ya Alhamisi ile asubuhi, Iryn alinipa taarifa kuhusu ujio wa dada yake kutoka Ethiopia na alisema ataingia usiku sana. Nilimuuliza atafikia wapi? Akasema anafanya mpango ili afikie Sea cliff hotel.

Saa tano asubuhi, aliniaga kuwa anakwenda kwa mama Janeth kuonana na Jessie, hivyo nilimpa kampani ya ride hadi kwa mama, kisha nikaondoka kuelekea ofisini.

Nilikuwa nakazi ya kukagua hesabu za mauzo vizuri, kwani ni muda mrefu ulikuwa umepita pasipo kufanya ukaguzi. Niliweza kubaini matatizo madogo ambayo ambayo Hilda aliweza kuyajibia, hivyo nikaendelea kupitia ripoti na kuzicompile.

Saa 10 jioni, nilipigiwa simu na Iryn, kisha akaomba niende Mikocheni na alimpa simu jamaa ili anielekeze. Jamaa kunielekeza yalikuwa ni maeneo ya karibu na Shopperz, hivyo bila kupoteza muda niliondoka kuelekea huko.

Ndani ya muda mfupi nilikuwa nimewasili na jamaa alinielekeza hadi napark gari kwenye moja ya showroom ya magari. Sasa, baada ya kushuka ndiyo namuona Iryn na Jessie wamekaa na nikatembea mpaka usawa wao nikawasalimia.

Muda huu Jessie alikuwa ananiangalia tu, namimi nilikuwa namzingua pale;

IRYN: “Darling, follow me.”

Nilimfuata kwa nyuma, hadi ilikokuwa imepark Marcedes Benz.

IRYN: “Darling, hii gari ni nzuri? Unaionaje?”

MIMI: “Ni nzuri sana, halafu hii colour naona unique kwa benz.”

IRYN: “Mimi na Jessie wote tumeipenda.”

Alimuita jamaa ambaye ana asili ya uarabu na akamwambia aiotoe nje ili tuondoke nayo, na palepale aliomba account namba ili afanye malipo. Mimi nilikuwa sijui kinachoendelea kwakweli, nilihisi moja kwa moja gari ni ya Jessie.

Benz ilitolewa showroom mpaka nje kwaajili ya kuondoka, gari ilikuwa ni nzuri ikivutia sana. Aliniita akasema niache taarifa zangu kwaajili ya usajili, hapa sasa ndo nikahisi gari itakuwa yangu.

Sikutaka kubisha na nikafanya kama alivyosema. Jamaa aliahidi kwamba kesho kufikia saa 4 asubuhi kila kitu kitakuwa sawa, hivyo tukachukue plate namba. Baada ya malipo kufanyika, tuliondoka na Jessie akaondoka na ile Audi, wakati sisi tukaondoka na ile Benz. Uvumilivu ulinishinda na nikaanza kuuliza maswali;

MIMI: “Baby, bado sijui kinachoendelea kuhusu hii gari.”

IRYN: “Mimi kama MD, ofisi imekununulia gari ili iwe inakusaidia kwenye majukumu yako pamoja na ya ofisi.”

Niliishiwa hata niseme nini maana sikutarajia kuona Iryn akinifanyia surprise kama hii. Nilikuwa bado siamini kama kweli hii benz nayoendesha kweli ni yangu.

MIMI: “Baby nashukuru sana, hata sijui niseme nini kwahaya yote unayonifanyia. May God bless you.”

IRYN: “Kampuni ina imani kubwa sana na wewe, na hii ni moja ya shukrani yangu. Mimi bado sijakupa zawadi, ila nitaanza kwanza na nyumba mengine yatafuata.”

Tulienda mpaka kwenye apartment yetu, tukapark ile gari, kisha tukaondoka tena na Jessie kumrudisha kwa mama. Baada ya kurudi nilianza kuiangalia ile Benz kwa mara nyingine tena, jinsi ilivyo nzuri na kuvutia, na niliishia kutabasamu.

Kesho yake, ijumaa tulikutana kwaajili ya kikao kifupi ambacho kilihusisha viongozi tu, na tulifanyia pale Giraffe hotel, Mbezi Beach. Kikao kilianza saa 4 kamili asubuhi na kilihusisha watu sita tu, pamoja na Iryn.

Iryn alishukuru sana uongozi wa kampuni kwa kujitoa katika kipindi kigumu, hasa wakati ambapo hatukuwa na mawasiliano. Kama MD, aliahidi kuongeza mshahara kwa 30% kwa viongozi kutokana na kazi nzuri waliyofanya. Hakuishia hapo, aliongeza kuwa baada ya kikao, atatoa zawadi kwa wote.

Baada ya bossy kuongea, nilisimama kutoa taarifa ya mwenendo wa kampuni pamoja na kuifunga branch ya Mikocheni. Lucy na Hilda, walikuwa wanajua kinachoendelea kasoro wengine walikuwa hawajui, hivyo walibaki wakishangaa baada ya kuzisikia taarifa hizi;

IRYN: “Why? I didn’t expect you would come up with this bad idea.”

Nilianza kuwaeleza sababu ya kufanya maamuzi haya;

MIMI: “Tumejadili suala hili kwa undani pamoja na Hilda na Lucy. Tumeona kuwa gharama tunazolipa kwa pango ni kubwa sana, na kuongezeka kwa gharama za umeme, maji, vibali vya leseni na mamlaka nyingine ni mzigo mkubwa. Badala ya kutafuta ofisi mpya, ni bora wateja wetu wa Mikocheni waje Masaki. Hii itatusaidia kupunguza gharama nyingi na kuongeza faida kubwa. Kwa hivyo, tunataka ufahamu kuwa maamuzi haya tumeyachunguza kwa makini na hatuja kurupuka."

Baada ya kuwapa sababu ya kuifunga ofisi ya Mikocheni, kila mtu alinyamaza kimya akifikiria maana ni sababu ambayo ilimake sense vichwani mwao na baada ya dakika kupita, Iryn alianza kuongea.

IRYN: “Mnashaurije juu ya hili, lengo tupate maamuzi sahihi, kila mtu ajaribu ku-assess risks kabla ya kukubali haya maamuzi.”

Baada ya majadiliano ya dakika 20, kila mtu aliunga mkono wazo langu la kuhamishia branch Masaki. Bossy akatoa maelekezo tuanze taratibu mapema ili tusigombane na mwenye nyumba.

Ni kikao kilicho chukua masaa 2 na baada ya kumaliza, tulipata lunch ya pamoja bila kusahu kupiga picha za ukumbusho, nami nilitumia nafasi hii kupiga picha na mama kijacho wangu, kama ukumbusho wa ujauzito wake.

Baada ya kumaliza kila kitu, tuliwaaga na kuelekea Sea cliff hotel kuonana na dada yake ambaye aliingia Dar usiku sana, akitokea Ethiopia.

Tulipofika hotelini, tulimsubiri pale reception na haikuchukua muda alitoka na wakaishia kukumbatiana na Iryn. Dada yake yuko vizuri pia, sio wa kitoto ni mzuri kwelikweli, ila bado hafiki kwa Iryn.

IRYN: “This is Insider, my boyfriend. Do you recognise him?”

VIVIAN: “Of course I do. How are you, brother-in-law?”

MIMI: “I’m fine and happy to see you again."

Mkononi, Viviani alikuwa ameshika kimfuko kidogo na alimpa Iryn, naye akanikabidhi mimi na alinikonyeza, ile kuangalia ndani kuna nini, naona si simu, nikavunga.

Baada ya maongezi mafupi, tuliongozana mpaka parking ili tuondoke, njiani macho yote yalikuwa kwetu. Kwanza niliona ufahari sana kuongozana na wanawake warembo duniani, ni wanaume wachache sana wenye bahati kama hii.

Kwa upande mwingine Sister yangu alinipa taarifa kwamba yuko Airport na anatarajia kuingia Dar, jioni. Nilimpa taarifa Iryn na alisema tufanye booking ya room palepale Sea cliff hotel mapema.

Saa 10 jioni, tuliondoka kwenda JNIA kumpokea dada yangu. Iryn aligoma kabisa kubaki nyumbani na Vivian, alisema haitakuwa vizuri ikiwa nitakwenda peke yangu kumpokea dada yangu wakati yeye yupo

Baada ya kufika JNIA, tulikaa sehemu ya kusubiri abiria. Kama ilivyo kawaida, kila mtu aligeuka kumtizama Iryn kutokana na uzuri wake wa kipekee. Alikuwa kivutio maalum pale, akiwa na mimba yake.

Ndani ya nusu saa, sister aliwasili na waliishia kukumbatiana na wifi yake kisha tukapotea eneo hili. Tulianza kwanza kupitia Sea cliff hotel, ambapo tuliacha mabag yake, kisha tukaelekea home.

Apartment ilikuwa imechangamka sana maana walikuwa wanawake watatu wakipiga story, huku wakicheka. Mimi niliamua kuwapa space na nilienda kutulia chumbani nikipanga mambo yangu.

Nilitoa ile simu kwenye mfuko na ilikuwa ni Iphone 14 kama ileile aliyoivunja hadi rangi na niliweka laini yangu. Nilimpigia simu mama J kumpa taarifa kwamba kesho nitarudi, lakini ni kama aliipokea hii taarifa kwa kutojali.

Wakati huu, nilipata ujumbe kutoka kwa Asmah ambao ulisomeka anataka kuacha kazi, ilikuwa ni taarifa mbaya kwangu, hivyo nikampandia hewani. Nilimuuliza kwanini anataka kuacha kazi, akasema yeye ameamua hivyo kwani anataka kurudi shule kusoma. Nilifunga mazungumzo kwa kumpa ahadi ya kuonana kesho ili tuzungumze vizuri kuhusu suala hili, kwani ilikuwa ni ghafla sana.

Saa 2 usiku, tulitoka kwenda kupata dinner ya pamoja pale Karambezi Café. Wao waliendelea kuzungumza, na story zao nyingi zilikuwa zinahusu leba, wakati mimi nilikuwa nasikiliza kwa sikio la kuiba huku nikijifanya nipo bize na simu

Wakati naongea na dada yangu, nilimshukuru sana kwa kujitoa kwake na kukubali kwenda South Africa. Baada ya masaa mawili kupita, tuliagana ili wajiandae mapema kwa ajili ya safari ya kesho. Walielekea hotelini na sisi tukaelekea kwenye apartment yetu.

Usiku ulikuwa mrefu sana kwani nilikuwa nakazi ya mwisho kuhakikisha barabara inakuwa safi kwaajili ya mtoto kupita. Baada ya kazi ya muda mrefu, japo niliichafua sana, lakini mama kijacho aliridhika na kazi yangu na tukalala.

Asubuhi na mapema nilimuamsha ili tujiandae kwaajili ya safari. Baada ya hapo tuliondoka kuelekea Sea cliff hotel, ambapo tuliwachukua akina sister na tukaelekea Airport. Baada ya kuwasili pale JNIA tulipiga tena picha za mwisho kama ukumbusho, kisha tukachoma ndani.

Nilianza maongezi deep na Iryn na kubwa nilimtakia kila la kheri katika kuanza safari yake mpya ya kuwa mama na nilimpa ahadi ya kwenda South Africa kujumuika naye.

IRYN: “Baba Aria, nakupenda sana na naomba uheshimu hili. Kama nilivyokuahidi before, sitoweza kuwa na mwanaume mwingine zaidi yako, napenda sana nikuzalie mtoto mwingine baada ya huyu.”

Nilipenda sana kusikia akiniita Baba Aria na nilimshika mkono wake nikauweka pajani;

MIMI: “Wewe ni mke wangu tayari, nitaangalia namna ya kuwaoa wote, kuhusu watoto hata ukitaka dozen kwangu ni kazi ndogo.”

IRYN: “Promise me unakuja lini South?”

MIMI: “Mama Aria, ninaomba kwanza nikae na familia yangu, nime-mmiss sana mwanao Junior na mama J. Nitakuja before hujajifungua natamani niwe na wewe leba hadi unajifungua.”

Iryn alifurahi sana kusikia maneno matamu kutoka kwangu na tuliagana kwa kukumbatiana maana muda wa kucheck-in ulikuwa umewadia. Niliwaaga akina sister pamoja na Viviani na niliwaambia nitawaona soon, na kabla ya kuondoka Iryn alinikumbatia kwa mara nyingine tena.

Niliondoka pale JNIA nikiwa na furaha sana, na niliwasha gari kuondoka kurudi Masaki.

Baada ya kufika kwa apartment nilipark vizuri gari, Audi maana nilikuwa naiacha pale, kisha niliingia ndani kuchukua bag, pamoja na funguo za benz yangu, nikaanza safari ya kwenda home, Mbezi Beach.

Katika maisha yangu, hakuna siku niliwaza kama nitakuja kumiliki benz, lakini ndoto yangu ilitimia kwa kuendesha benzi kali. Barabarani nilikuwa mdogo mdogo sana, kama vile namuendesha bibi harusi. Baada ya kufika home, nilimpigia simu Elena akatoka kunifungulia gate.

Junior alikuwa amesimama kibarazani akishangaa gari, kwani anapenda sana magari na baada ya kuniona baba yake, alikuja spidi nikamnyanyua juu. Na alianza kulilia aingie ndani ya gari, bhasi nilimfungulia mlango akaanza kunyonga steering.

Kwa upande mwingine, nilishtuka kuona gari yangu nyingine siioni na baada ya kuuliza, Elena alisema mama J kaondoka nayo. Niliuliza kwani anajua kuendesha? Akanijibu ndio ni mwezi sasa anaiendesha, nilibaki nikishangaa.

Nilifurahi kusikia wife amejua kuendesha gari, kwani ilikuwa ni hatua nzuri kwa upande wetu. Nilikuwa nimechoka sana pamoja na usingizi, hivyo nilienda chumbani kulala. Kwa bahati mbaya sikuweza kulala mapema sababu Junior alikuwa akinisumbua sana.

Jioni, baada ya kuamka niligundua kwamba mama J karudi na nilienda seblen kukaa, lakini nilimsikia akiongea na simu huku akicheka kwa mbali. Nilitulia pale seblen nikishangaa TV na zilipita dakika tano, bado mama J anaongea na simu. Nilihisi haya si maongezi ya kawaida na nilisogea mpaka dirishani kusikiliza, maana alikuwa kasimama pale kibarazani.

Na aliendelea kuongea, tena kwa sauti ya chini, haya ni baadhi ya maneno aliyokuwa anajibu;

Ndiyo, najua… ah, nimekumisi sana

Wewe pia unajua jinsi unavyonifanya nijisikie… usijali, nitakutafuta muda"

Tutaonana tena, usijali.


Baada ya kuona amemaliza kuongea na simu, nilirudi chumbani kwa spidi ya kunyata ili asinishtukie. Baada ya dakika 5 alirudi chumbani na nilijifanya nimelala, aliweka simu chaji akaondoka. Niliamka kwa lengo la kuikagua simu yake, kwa bahati mbaya alikuwa kabadilisha passcode, hivyo nikawa sina option nyingine.

Nilipata wazo nikague mkoba wake, na nikaona kuna risiti za Samakisamaki, Elements, KFC na nyinginezo. Nilianza kukagua za KFC zilionesha tarehe ya leo, za Elements zilionesha ni weekend iliyopita, lakini kilicho nishangaza zilionesha zimeprintiwa saa 4 usiku.

Nilibaki najiuliza mama J sio mtu wa marafiki wala kutoka out, huku Samakisamaki, Elements alikuwa na nani?. Huyu mtu waliokuwa wanaongea wote kwenye simu ni nani? Hapa sasa nikahisi kuna SOMETHING FISHY kinaendelea.

ITAENDELEA
Rasmi, Mama J anakojozwa na mhuni mmoja
 
IRYN anaona Insider ndo mtu pekee wa kusimamia mali zake sababu jamaa ana
  • Akili ya kusimamia biashara
  • Hana Tamaa
  • Intelligent

Vijana kuna vitu vingi sana vya kujifunza hapa, na wengi wetu tunasoma juujuu, jamaa ametupa code nyingi sana.

Insider ni mpambanaji, anzia pale alipoacha kazi na kuanza biashara ya Uber, ni wachache sana tungekuwa na huu uthubutu.

Amepitia ups & downs nyingi kwa Iryn, bado hakutaka kuwa mnyonge aliendelea na misimamo yake.

Yametokea matatizo kwenye kampuni, alikuwa na uwezo wa kuiba hela akasepa, lakini alikuwa mbele kuhakikisha kampuni inasimama. Jamaa kaenda Dodoma kuanzisha kampuni zake, hivi ungekuwa wewe ndo Iryn utamchukuliaje Jamaa?.

Mwanaume ukiweza kuwa na unique characteristics, hawa wanawake watakusumbua sana tena sana. Iryn ameona something unique kwa Insider hadi kamzalia mtoto. Mwanamke kwenye suala la kuzaa na mtu, huwa hawakurupuki asee, wako makini sana.

Rudi kwa suala la mama wawili, jamaa kasamehe kiroho safi na bado kampa zawadi binti yake. Yule dada yake Junior, anampango wa kumpeleka shule akasome.
Ni wangapi tuna moyo kama huu?,
 
Na wanawake huwa wanajua kulipiza vibaya hatari. Hapo maji utaita mma.
Kuna jamaa mmoja alioa na kazaa na mkewe watoto 3 ila jamaa alikuwa kicheche kama Insider hivi.
Mke wake alikuwa mzuri mpole, ila sasa yule mwanamke alivyochoka na mauzauza ya jamaa, alimbwaga mazima. Sasa hivi huyo mama kaolewa na mzungu kabisa jamaa hadi leo anajuta.
Wanawake huwa wanavumilia sana ila wakichoka malipizo yake ni balaa nyengine
Sio wanawake yaani watu wenye Kariba ya upole au utulivu wako hivi
 
IRYN anaona Insider ndo mtu pekee wa kusimamia mali zake sababu jamaa ana
  • Akili ya kusimamia biashara
  • Hana Tamaa
  • Intelligent

Vijana kuna vitu vingi sana vya kujifunza hapa, na wengi wetu tunasoma juujuu, jamaa ametupa code nyingi sana.

Insider ni mpambanaji, anzia pale alipoacha kazi na kuanza biashara ya Uber, ni wachache sana tungekuwa na huu uthubutu.

Amepitia ups & downs nyingi kwa Iryn, bado hakutaka kuwa mnyonge aliendelea na misimamo yake.

Yametokea matatizo kwenye kampuni, alikuwa na uwezo wa kuiba hela akasepa, lakini alikuwa mbele kuhakikisha kampuni inasimama. Jamaa kaenda Dodoma kuanzisha kampuni zake, hivi ungekuwa wewe ndo Iryn utamchukuliaje Jamaa?.

Mwanaume ukiweza kuwa na unique characteristics, hawa wanawake watakusumbua sana tena sana. Iryn ameona something unique kwa Insider hadi kamzalia mtoto. Mwanamke kwenye suala la kuzaa na mtu, huwa hawakurupuki asee, wako makini sana.

Rudi kwa suala la mama wawili, jamaa kasamehe kiroho safi na bado kampa zawadi binti yake. Yule dada yake Junior, anampango wa kumpeleka shule akasome.
Ni wangapi tuna moyo kama huu?,
True
 
Back
Top Bottom