Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

EPISODE 14

“A TRUE STORY BY INSIDER MAN”

Nikamshukuru Iryn kwa out then nikawasha gari tuondoke tukalale, wakati tumevuka geti la Kidimbwi kuna gari ilikuja kwa spidi sana na ikatugonga “BOOM”. Ilisikika sauti ya Iryn “Mamaaaa…….”.

TUNAENDELEA…………….

Lilikua ni tukio la fasta sana ambalo lilitupa mshtuko kupelekea Iryn kutoa sauti ya nguvu. Jamaa alitugonga kwa nyuma na kwa spidi sana, palepale ilibidi nishuke na watu walikua wameanza kusogea pale kwa kasi.

Muda huu magari ndo yalikua yanaingia kwa kasi na kutoka, Uber ndo zilionekana kuwa busy sana hili eneo.

Eneo ambalo jama alitugonga ilikua ni kabla hujafika kwenye corner ya kwanza inayokata kushoto kama umetoka kidimbwi.

Baada ya kushuka niliangalia gari upande wa nyuma nikaona jamaa alikua amevunja bampa la nyuma, taa zote mbili za nyuma na sehemu ya nyuma ya boneti ilikua imebonyea.

Jamaa gari yake ilikua ni Prado zile za zamani ila ilikua na ngao mbele. Jamaa alikua bado hajashuka kwenye gari ikabidi nimgongee dirishani atokee nje, ili tuongee.

Baada ya kumgongea dirishani lakini jamaa hakutoka ni kama alikua na dharau, hichi kitendo kilizidi kunipa hasira sana. Na muda huo askari mgambo wanaolinda eneo hili walikua wameshafika eneo la tukio.

Kwa upande mwingine foleni ilizidi kuwa kubwa sana maana hakuna gari zilizokuwa zinatoka wala kuingia pale Kidimbwi. Na muda huo Iryn alikua kashatoka kwenye gari, akaja akanishika mkono.

Kwa tukio liliokuwa limetokea pale mwenye kosa alikua ni jamaa, maana yeye ndo alinigonga kwa nyuma, napia sheria ziko wazi hivyo hakukuwa na haja ya kumtafuta mchawi ni nani.

“Huyu fala anadharau sana, anamakosa ila hataki kutoka nje. Watu kama hawa ndo wakuwatia makofi”. Ilisika sauti ya dereva wa bodaboda aliyekuwa kwenye bodaboda yake.

Watu walizidi kumiminika hasahasa madereva wa magari walikua wamefika kuona nini tatizo, na wengi walikuwa wanapatwa na hasira kuona jamaa hataki kutoka kwenye gari.

Jama alikuwa na demu wake ambaye alikuwa amekaa upande wa mbele, dem alikuwa kama anamwomba jamaa atoke nje. Kwa upande mwingine Mgambo walikua wamemgongea jamaa ashuke na madereva pia walikua wameanza kumgongea kwa fujo, maana jamaa alikuwa anafanya mambo ya kizamani sana, afu pia ya kishamba.

Baada ya muda jamaa akashuka na alionekana mtu ambaye amelewa hakuwa na akili zake.

“We ms*** unazingua baada ya hili suala mlimalize mapema wewe unaleta mapozi, acha ufala sisi madereva hatuko hivo.” Hii ilikua ni sauti ya jamaa ambaye alikua ni dereva akimwambia jamaa.

Foleni ilizidi kuwa kubwa na kupelekea watu kuzidi kumiminika pale, maana hakukua na gari inayotoka wala kuingia.

MGAMBO: “Bro siku nyingine usifanye ujinga kama huu hili kosa ni lako, ulipaswa kushuka na myajenge haraka.”

JAMAA : “Samahani bro! Tunaweza ongea kuhusu hili private?”

Jamaa alikua akiniomba tuongee private.

MGAMBO : “Hakuna haja kuongea private, cha msingi tumsikilize jamaa hapa atasemaje”

Palepale alitokea jamaa ambaye ni dereva wa Uber na akatoa hesabu na gharama za vifaa na utengenezaji.

“Hii ni IST ya 2006 taa za nyuma moja ni 180,000/= kwa mbili ni 360,000/=. Bampa hilo halifai tena gharama zake ni 250,000/=, kunyoosha hio boneti na kupaka rangi hapo andaa 100,000 kwa jumla hapa ni 710,000/=. Kama jamaa atakuchaji na usumbufu juu yake ila gharama za hapo ni uhakika. Hii gari kali sana bado mpya naona umeshaitia ngeu tayari.”

Muda huu pia Iryn alionekana kunionea huruma sana maana alikua anajua gari itakua ya boss, hakuwai kuuliza kama gari ni yangu au laah! na mimi pia nilikuaga siwaambii wateja kama gari yangu.

IRYN : “Insider unafanyaje sasa?, I can feel you, I’m really sorry.”

MIMI: “Jamaa kama atatoa hizo cost no problem tutatamaliza”

IRYN: “Atakubali sasa?”

Muda huo Mgambo akawa amekuja upande wangu akiniuliza maamuzi yangu ni nini juu ya hili jambo. Upande mwingine madereva walitamani sana hili jambo liishe mapema maana tungesema tusubir traffic kwa muda ule isingekua rahisi kwa Traffic kufika mapema.

Nikamuuliza jamaa alokua anatoa hesabu za matengenezo kama anauhakika na zile bei alizotaja, na madereva wengi wa Uber walikuwepo pale wakasema ni sahihi.

MIMI: “Kama jamaa atakua tayari kutoa hizo gharama sina shida naye anipe 750,000/=. Hio 40,000 iwe kama usumbufu wa kunipotezea muda kwenda garage.”

Kwa upande wa jamaa aliyenigonga ni kama hakua tayari maana alisema hana hela na hicho kiasi ni kikubwa sana kwa upande wake.

DEREVA UBER: “Hivi wewe jamaa una akili kweli? Mshukuru hata jamaa ni mwelewa na mstaarabu sana, kwanza hapo umelewa tukiita traffic hapa unakesi nyingi sana, kama unayo hio amount mpe jamaa tuondoke foleni imeshakua kubwa sana.”

Na muda huu uongozi wa Kidimbwi ulikua umefika pale kutoa usuluhishi.

JAMAA: “Hiki kiasi cha Pesa kwa sasa sina, mpaka niongee na Mzee au tutatumia Bima ya gari, bima yake ni kubwa.”

DEREVA UBER: “Bro embu kuwa serious Kama ni Bima ya gari inamaana tusubiri traffic waje kupima? na Bima inachukua muda mrefu kutoa majibu, jamaa asubiri majibu ya Bima?, hata mimi siwezi kukubalia.”

Kulikua na kelele za madereva wengi walikua ni Uber na walionekana kuwa na hasira sana huu usiku.

MIMI: “Kama jamaa anataka Bima ndo itahusika, bhasi anipe gari yake nimwachie hili akatengeneze, gari ikikamilika na mimi nitakukabidhi lako unaonaje mzee?”

Watu walionesha kufurahishwa na hii kauli yangu na waliiunga mkono. Jamaa baada ya kusikia hii kauli ni kama alishindwa cha kusema.

Uongozi wa pale Kidimbwi, Mgambo walikua wakiongea namna ya kupata solution, palepale Iryn akaanza kuongea.

IRYN: “Bro haya ni maisha tu, leo inaweza kuwa kwako, kesho ikawa kwetu. Hili suala tunataka liishie kirafiki ili kila mtu akaendelee na maisha yake. Hatuwezi kupelekana police kwa jambo dogo kama hili, ukisema utumie Bima kwanza itachukua muda mrefu sana, pili sisi tutaendelea kukusubiri mpaka bima itakapokuwa tayari?. Kwanza hapo umelewa, Traffic wata recommend wewe ndo mwenye makosa do you really think bima watapitisha claim yako?, hata kama ni Comprehensive kwa Tanzania hii sio rahisi. Na huo muda ambao unafuatilia upo tayari kutulipa muda wetu wa kusubiri?, naona unaleta masikhara kwenye vitu serious.”

Iryn aliongea na kila mtu aliona dada kaongea point sana,

JAMAA: “Nimeelewa ila sasa nitapataje hii pesa kwa sasa na muda huu ni usku hata kuwapigia wazazi ni ngumu kwa muda huu.”

IRYN : “Ni simple tu, unatumia simu gani?”

JAMAA : “Iphone”

IRYN : “Ilete tuione”.

Na muda huo dem wa jamaa alikua kashuka kwenye gari. Jamaa alikwenda kwenye gari na akatoka na simu

IRYN : “Hii ni iphone 12 Pro. Unaweza kuweka bond hapa afu kesho ukipata hio hela unapewa simu yako, simple like that.”

Watu walioneshwa kuyakubali mawazo ya Iryn na waliunga mkono hoja kwa 100%. Jamaa alisogea pembeni na demu wake ni kama walikua wanajadili kuhusu hili jambo, baada ya dakika 2 wakarudi.

JAMAA: “Bhasi sawa haina shida acha niweke simu Bond”

IRYN : “Itabidi tuandikishiane”

Palepale zikatafutwa karatasi na peni sijui zilitokea wapi kwa muda mle, jamaa mmoja alikua ameleta notebok na peni. Iryn akaomba leseni zetu za gari, mimi nikaitoa kwenye gari lakini jamaa alikua hana leseni, ikabidii tumwombe NIDA.

Tuliandikishiana pale makubaliano baina yetu na upande wa mashahidi “Mimi nilikua na Iryn, jamaa alikua na demu wake, Mgambo 1, na Dereva wa Uber aliyekuwepo pale kama shahidi”.

“Simu yako utawasiliana na jamaa asubuhi au utawasiliana na mimi kwa namba hizo, Jitahidi uwe mkweli maana ikipita kesho tutakwenda Police maana ushahidi wa Picha na haya makubaliano upo.”

Baada ya kuandikishiana kila mtu alisaini na jamaa akatoa line kwenye simu yake akatukabidhi simu, akapiga picha yale makubaliano kupitia simu ya demu wake na mashahidi wengine wakafanya hivyo, na mchezo ukaisha kihivyo kwa ule usiku.

Ilituchukua kama dakika 45 kutoka eneo la Kidimbwi kutokana na ile foleni kubwa. Tulivyofika kwa Zena pale nikafanya kurequest usafiri kwa ajili ya Iryn, na nikapata Uber pale chap, tukaagana na Mimi nikarudi home kulala.

*********

Asubuhi niliamka mapema sana ili kuwapa taarifa wateja zangu “Maggy na Mama 2” kuhusu ajali niliyopata na wakanielewa. Wakati naongea na Mama wa2 akaomba badae tuonane jioni pale Rainbow.

Saa 2 asubuhi Iryn alinipigia simu kujua maendeleo yangu na pia aliuliza kama jamaa kanicheki na nikamwambia jamaa hajanicheki bado.

Saa4 Jamaa ndo alinipigia simu na saa 6 mchana tukakubaliana tuonane pale Morocco. Jamaa aliomba tuonane pale sababu yeye alikua anakaa Magomeni. Baada ya muda huo tulionana na jamaa na akanikabidhi kiasi changu cha Pesa 750,000/=, nilizihesabu zile Pesa na zilikua zimetimia.

Palepale nilitoa karatasi nikaandika kwa nyuma kuonesha tumekabidhiana tayari. Mimi nikaondoka na uelekeo wa Gerezani kutengeneza gari, sababu nilijua pale Gerezani mimi ni mwenyeji hata sitapata shida kwenye kutengeneza gari.

Baada ya kuachana na jamaa nilimpigia simu Iryn nikamwambia nimeshaonana na jamaa na amenipa pesa tayari, akanambia nipitie kwake navyorudi.

Nilifika pale Gerezani nikamtafuta fundi wangu ambaye nilikuaga nafanya naye kazi kwenye ofisi yangu kipindi kile. Jamaa baada ya kuiona gari akanambia hapa chap leoleo tunaimaliza kazi.

Huyu Fundi wangu ni mtaalam sana kwenye masuala ya upakaji rangi yuko vizuri sana. Tulinunua taa za nyuma OG za mtumba pale Ilala pamoja na bampa ya nyuma.

Nakumbuka taa 2 tulilipia 320,000/= na bampa tulilipia 220,000/=. Mpaka jioni gari ilikua imeshakamilika tayari utafikir sio ile ambayo ilikua imebondwa nyuma.

Baada ya kutoka Gerezani moja kwa moja nilikwenda kwa Iryn maana alinambia nipitie kwake navyotoka mjini. Nilipitia pale Namanga madukani nikanunua mtindi maziwa litre 3, Iryn alinambiaga anapenda sana mtindi, hivyo nikafanya kumsaprizi.

“Nilikua nafanya haya ili kuendelea kumvuta Iryn karibu yangu, maana nilikua naingiza pesa nyingi sana kupitia yeye. Iryn alikua tayari mtu muhimu sana kwangu, nilikua namuheshimu sana.”

Nilifika kwake usiku tayari ulikuwa nikaingiza gari ndani, bhasi na yeye alikua katoka tayari na alikua amezunguka upande wa nyuma kulitizama gari.

Na mimi nilikua nimeshuka na dumu la mtindi, Iryn baada ya kugundua ni mtindi alifurahi sana. Bhasi tukaanza kuondoka kuelekea ndani huku tunapiga story.

IRYN: “Gari imependeza sana utafikiri haikugongwa jana Insider.”

MIMI: “Umeona eeh, jamaa nilompelekea alikuaga Fundi wangu ni mtaalamu”

IRYN: “Kwani ulishawai kuwa na Garage?”

MIMI: “Hapana ilikua kama workshop flani hivi , nilikua napiga piga rangi na kupolish magari.”

IRYN: “Sasa ilikuaje mpaka ukaifunga?”

MIMI: “Nimefunga kwa muda but nitarud tena kwenye business. Nilipisha ujenzi wa barabara”

IRYN: “Pole, unaona sasa una mambo mengi ila hujawai nishirikisha kabisa”

MIMI: “Ndomana hata yule Muajemi niligundua atakuja kuwa asset hapo baadae maana anadili na Lubricants atanisadia huko mbeleni.”

Muda huu tulikua tuko seblen tunaendelea na maongezi…..

IRYN: “So Bossy wako umempa taarifa kuhusu gari?”

MIMI: “Hapana sijamwambia kabisa, kuna vitu unavunga tu. Hata ningemwambia asingekua na msaada angeishia kupata presha tu.”

Iryn alikua hajui kama hii ni gari yangu pia usajili wa gari nilitumia jina la wife. Na mimi sikuwai kumwambia gari kama yangu.

IRYN: “Okay nice, ni uamuzi mzuri. Insider una ni hide mambo yako ujue.”

Muda huu alikua kama amenuna, na mimi ikabidi nimsogelee karibu.

IRYN : “Insider niache bhana..”

MIMI : “Sikia kama unataka kujua kuhusu mimi, nitakwambia tena kwa vitendo sawa?, aya nambie umepika nini?”

Iryn baada ya kusikia maneno hayo aliishia kutabasamu.

IRYN: “Twende jikoni ukaone.”

Alikua amepika tambi na Kuku, kwenye suala la mapishi dada pia alikua yuko vizuri sana. Mimi nikapakua nikaanza kula maana nilikua nina njaa sana, sikula mchana.

IRYN: “Insider unakumbuka kesho?”

MIMI: “Yeah si tunakwenda kwa mama Janeth?”

IRYN : “kumbe unakumbuka”

Na muda huu simu ilianza kuita, kucheki alikua ni mama wa2, nikapokea tukaanza kuongea pale. Mama wa2 alikua ananiuliza niko wapi maana anaona kimya simtafuti. Na mimi nikamwambia ndani ya nusu saa nitakua pale, na yeye akasema nitamkuta Rainbow

IRYN: “Insider huyo nani?”

MIMI: “Mteja wangu huyu”

IRYN: “Seems like mna appointment usikuu huu”

MIMI: “Yeah anataka kunilipa pesa zangu za mshahara huwa namchukua asubuhi kila siku”

IRYN: “Sasa kwanini asikupe hiyo kesho?, mpaka akupe usiku?”

MIMI: “Yuko likizo ndomana, pia amenambia kuna kazi ya kufanya naye tukabargain”

IRYN: “Mmh sawa, watu na appointment zenu za usiku”

Muda huu tena simu yangu ilianza kuita na mama yangu mzazi ndo alikua anapiga simu, sababu nilijua mama atakua anapiga simu kuhusu suala la Mama J sikutaka kuipokea simu yake. Nikasema nitaongea naye nikianza kutoka kwa Iryn, nilijua mama lazima anipe vichambo.

IRYN : “Naona anakupigia tena simu na hutaki kupokea, pokea tu.”

Mimi sikumjibu kitu niliamua kunyamaza, wakati huu nilikua niko busy na msosi. Yeye akaamua kuivuta simu aangalie ni nani anayenipigia.

Sasa Iryn alivyoona Mama ndo anapiga ni kama alipatwa na ka aibu, mawazo yake yote yalikua ni atakua Mama wa2 niliyetoka kuongea naye muda sio mrefu.

IRYN: “Kwanini humpokelei mama simu.?”

MIMI: “Mama kuna kazi alinipa sasa sijaifanikisha ndo nawaza hapa jibu la kumpa, maana hatonielewa kabisa.”

IRYN: “Mmhh sawa bhana, sio vizuri huwezi jua anakupigia akwambie nini.”

MIMI: “Nitampigia soon.”

Nilitoka pale kwa Iryn nikamwaga na yeye alitoka kunifungulia geti, tukakubaliana kesho mchana tukutane kwaajili ya kwenda Masaki.

Muda huo niliendesha gari kwa kasi sana kuelekea pale Rainbow Mbezi Beach. Nilifika pale na nilimkuta akinywa Savannah kama kawaida yake.

MIMI : ”Nakuona Mama mkwe unakimbiza taratibu”

MAMA WA2: “Ndo nini kuniweka hivi utafikiri namsubiri Mr.”

MIMI: “Samahani, hesabu zangu kidogo zilifeli ila sijakuweka sana hata hivyo, nitakuongezea Savannah moja ya kukusubilisha.”

MAMA WA2 : “Insider bhana unajua wewe unavituko sana alokwambia mimi nahitaji Savannah ni nani?”

MIMI : “Sasa unataka nini? Maana kuwa mkwe wako umenikazia”

MAMA WA2 : “Mwanangu mdogo yule wewe ukome.”

MIMI: “Afu sijawai mwona embu nioneshe hata picha ili nianze kuandaa hata posa.”

Mama wa2 akatoa simu akanionesha picha za Bint yake ambaye ndo mtoto wake wa kwanza wa kike. Na huyu mtoto wake alikua Advance form 5. Tuseme Mama wa2 amebarikiwa kuwa na watoto wazuri sana, afu wote baba zao ni tofauti.

MAMA WA2 : “Insider mwanangu mpaka amalize chuo ndo hapo mambo mengine yatafata. Hata wewe huyu sio size yako.”

MIMI: “Sema hutaki kuona bint yako anaolewa na Dereva wa Uber, huyo ni size yangu kabisa”

Muda huo dada alikua kaja pale kunisikiliza bhasi nikamnong’oneza aje na Savanna 2 na Heineken 1.

MAMA WA2 : “Insider unafikir sitamani kuwa na Mkwe kama wewe?, napenda upapambanaji wako. Najua hapo una elimu yako nzuri tu ila uneamua kupambana na Plan B hujataka kuajiriwa kama sisi.”

MIMI: “Unafikiri sipendi kuajiriwa? Sema sina connection tu.”

MAMA WA2 : “Umesomea nini?”

MIMI : “Uchumi”

MAMA WA2 : “Nikikutafutia connection upo tayari kufanya kazi?”

MIMI: “Why not, nikamkonyeza” na yeye akatabasamu.

Na muda huu dada alikua kaleta vinywaji, sasa Mama wa2 alishangaa kuona Savannah 2 kwaajili yake napia kuona mimi nimeagiza Heineken.

MAMA WA2 : “Kwahiyo kweli umeamua kuagiza Savannah?”

MIMI : “Yeah kwani nimefanya vibaya?”

MAMA WA2 : “Ahsante nilijua unanidanganya, na wewe pia kumbe ni mtumiaji wa pombe?”

MIMI : “Hapana leo nimeamua kunywa kwa ajili yako, seems like you don’t need my company here.”

MAMA WA2 : “No I’m happy, hata hivyo nilikua nishakunywa 2 tayari. Nikinywa nyingi zitaenda kunisumbua tu.”

MIMI : “Umeniitia nini kwanza nje na mshahara wangu,?”

MAMA WA2 : “Insider jumamosi nataka unipeleke Bagamoyo kabla sijamaliza likizo yangu.”

MIMI : “Bagamoyo unaenda kula bata?”

MAMA WA2 : “Nataka nikapunguze stress za maisha kule.”

MIMI : “Kwahiyo na mimi niandae pamba?, ili ukanilishe bata.?”

MAMA WA2 : “Ndo maana yake unafikiri nitakwenda na nani? Kama sio wewe?.”

MIMI : “Sawa imeisha hio, Bossy wangu.”

MAMA WA2 : “ I am not your Bossy”

MIMI : “Bhasi mama mkwe wangu kipenzi”

MAMA WA2 : “Gari umefanikiwa kuitengeneza?”

MIMI : “ Yeah muda sana si unajua ile ni ofisi siwezi kuchukua muda mrefu, nitakula wapi?”

MAMA WA2 : “Pole sana, so kesho kama kawaida asubuhi?”

MIMI : “Ndo maana yake, kesho asubuhi nitapita asubuhi kumchukua mtoto.”

Tulikaa na mama wa2 pale, akanikabidhi malipo yangu na mimi nikaondoka kurudi home kulala.

Wakati niko njiani nilimpigia simu mama na tukaongea kuhusu suala la Mama J. Nikamweleza mama ishu ilivyokua na mama aliishia kunilaumu sana kwa lile tukio na kunikanya nisurudie tena ule upumbavu. Akaomba nifanye juu chini tuyamalize mapema maana haileti picha nzuri kabisa. Nilimuahidi mama nitahakikisha tunayamaliza na Mama J na muda huo nilikua nimewasili home tayari.

Baada ya kuingia ndani kama kawaida yangu niliingia kuoga baada ya hapo nikasema acha nimpigie simu Prisca nimjulie hali maana toka jana sijaongea naye na yeye alikua hajanitafuta kabisa.

Nilimpigia simu baada ya kuita kwa sekunde kadhaa akawa amepokea;

PRISCA: “Hi Insider, naona umeamua kunipigia”

MIMI: “Hapana mrembo, Samahani nilikua nimebanwa sana na jana nilipata ajali.”

PRISCA: “Ajali ya nini? Mbona sikuelewi?”

MIMI : “Ya gari ila nishasovu tayari kuna mtu alinigonga kwa nyuma”

PRISCA: “Oohh I am really sorry”

MIMI : “How are you feeling today?”

PRISCA : “Kinda good, Insider do you love me?”

MIMI : “Yes I do, why?”

PRISCA : “I think you do not, nimekwambia jana naumwa but you don’t even care. Uko busy na mambo yako.”

MIMI : “I care about you, kesho nitakuja chuo kukuona sawa?”

PRISCA: “Okay, Goodnite byee”

Muda huu nilikua nawaza kumfanya Prisca kuwa kamchepuko kangu lakini nilibaini huyu mtoto angenisumbua sana. Prisca ni aina ya wale wanawake wanaopenda sana kudekezwa na kupetiwa petiwa, na pia ni aina ya wanawake ambao wakipenda wanapenda kweli.

Sasa mimi wanawake wa dizaini hii siwawezi kwakweli kwenye historia ya maisha yangu. Suala la kumbembeleza na kumdekeza mwanamke kama movie za Kikorea mimi siwezi.

Sasa nilikua nawaza kwa upande mwingine Mama J toka ajifungue ilikua miezi 9 tayari ila kuna muda nilikua sipati mahitaji yangu ya kitandani. Sometimes nilikua namwonea huruma na malezi ya mtoto alikua anachoka sana na ukizingatia Junior alikua analipenda sana nyonyo. Nikawaza nimfanye Prisca kma mchepuko ila nitamwambia ukweli aamue mwenyewe kama yuko in or out.

TUTAENDELEA 22:00
Saa za EAT
 
Siku story ikiisha ntajaribu kufungua baadhi ya codes [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
EPISODE 15

“A TRUE STORY BY INSIDER MAN”

TUNAENDELEA

Jumanne asubuhi niliweza kuongea na Muajemi na kama kawaida alikua anauliza jambo lake limefikia wapi. Nikamwambia lipo pazuri na asiwe na haraka soon mambo yatakua mazuri.

Jumanne hii pia nilikua na miadi na Iryn kwaajili ya kumpeleka kwa Mama Janeth ambaye alisema kwake ni kama mama mlezi.

Niliwasili pale kwa Iryn na hii siku Iryn hakunitafuta kwenye simu kabisa, niligonga mlango na akafungua. Baada ya kunifungulia mlango na kunikaribisha alikimbilia jikoni, alionekana anapika wakati huo.

Mimi nilikua nimetulia pale seblen kama Baba mwenye nyumba sina hata habari. Baada ya dakika kadhaa Iryn alianza kuniita;

“Insider……”

MIMI: “Nambie Mummy”

IRYN : “Unaweza kupika ugali?.”

MIMI: “Yeah, kitu kidogo hicho, nije nikusaidie?

IRYN : “Nataka nile ugali leo nimepika samaki”

MIMI : “Mimi nisingekuwepo nani angekusongea?”

IRYN : “Ningepika wali, njoo bhasi na mimi nijifundishe.”

MIMI : “Mrembo kama wewe kuzungusha ule mwiko utaweza.?”

IRYN: “Shida yako unanichukuliaga poa sana”

Nilienda pale jikoni nikabandika maji kwaajili ya kupika ugali, na muda huo Iryn macho yake yote yalikua kwangu.

IRYN : “Insider upo vizuri sana ungekua Ulaya sahivi ungekua unafanyia kazi moja ya 5 - star hotel.”

MIMI: “Shida connection tu, angalia vizuri stage zote nazo fanya kesho sitokusaidia.”

Akanipiga na teke mguuni, lilikua teke la kichokozi flani hivi.

Nilisonga ule ugali vizuri mpka ukaiva na ulikuwa laini, bhasi Iryn alishangaa sana.

MIMI : “Na wewe unakulaga ugali?”

IRYN: “Na mwaka sijala ila naupenda sana. Nimeona stage zote kesho nitakusongea ugali wangu.”

Tulikula ule Ugali na Iryn alikwenda kujiandaa,
Baada ya hapo tuliondoka na kuelekea Masaki kwa Mama Janeth. Sikutaka kuuliza tunakwenda kufanya nini huko ila nilisubiri aniambie mwenyewe.

MIMI: “So mama Janeth ndo alikua rafiki wa Mama yako?”

IRYN: “Yeah, pia ndo alikua msaidizi wa Mama kazini kwa cheo, mama alikua coördinator yeye alikua kama Assistant. Nje na hapo walikua pia marafiki wakubwa sana.”

MIMI: “Leo hajakwenda kazini?”

IRYN: “Alikua safari karudi Jumapili nahisi watakua wamempa off”

Tulifika Masaki mapema na moja kwa moja tulikua getini kwa Mama Janeth yeye alikua anakaa karibu na zahanati ya IST, ukishavuka ukuta wa IST kuna kibarabara cha vumbi kinakata kushoto.(INTERNATIONAL SCHOOL OF TANGANYIKA).

Tulifunguliwa na Mlinzi na muda huo Mama Janeth alikua katoka nje kibarazani. Bhasi baada ya sisi kushuka kwenye gari, Mama Janeth alitoka kibarazani na Iryn naye alitembea kwa spidi wakakumbatiana.

“Waow my daughter I have missed you so much”

ili onekana ni watu ambao wamemisiana sana n hawajaonana kwa muda mrefu.

Mama Janeth alikua ni Mzungu na pia alikua anajua kuongea kiswahili vizuri kabisa. Tulikaribishwa ndani na muda ule ule zikaletwa popcorn kwenye vibakuli, Iryn akaanza maongezi na Mama Janeth. Na Iryn alichukua nafasi hiyo kunitambulisha kwa Mama Janeth kama mimi ni rafiki yake kwa hapa Dar.

Maongezi makubwa ambayo nilikua nikiyaskia ni pamoja na suala la nyumba alizoacha Mama Iryn. Mama Janeth alikua anamwambia Iryn haoni sababu ya kuendelea kuzisimamia zile nyumba wakati Iryn yupo.

Nyumba zilikua zimepangishwa na hivyo walikubaliana wale wapangaji watakapo maliza mikataba yao bhasi Iryn ataanza kuwa incharge. Pia walikubaliana kwenda kuzitembelea hizo nyumba zote siku ya alhamis.

Kwa upande wa biashara walizokuwa wanafanya na Mama yake, Mama Janeth alisema zinakwenda vizuri na akamwambia wakimaliza mazungumzo watakwenda kuitembelea Saloon.

Pia walizungumza suala la kubadilisha taarifa za kampuni ambapo Iryn angekua Director. Na sababu alikua na Bachelor ya Usimamizi wa Biashara kwake lisingekua shida, na Mama Janeth alifurahi maana aliamini Iryn angeenda kuwa msaada mkubwa kwenye biashara kutokana na elimu yake.

Iryn alikubali kuanza mchakato wa kubadilisha hizo taarifa za kampuni na wakawa wanaplan pale. Mama Janeth alimwambia Iryn kuhusu Mwanasheria watamtumia wa palepale ofisni, yeye atume TIN na documents zingine muhimu.

Baada ya hayo mazungumzo kuisha walikuja kudiscuss suala la mafao ambayo mama yake alikua anaweka kama kiinua mgongo.

Mama Janeth aliikwenda ndani na akarudi na bahasha mbili za (A4) ambapo bahasha moja nyeupe yenye nembo ya Blue ya organization, akatoa form moja pale na akaamwambia Iryn anatakiwa kuzijaza kwa makini sana.

“Hizi form utaondoka nazo Iryn kasome kwa makini sana angalia mshahara wa mama yako toka anajiliwa, total utakayopata uta times 30%. Nimekuwekea salary slips zote toka mama yako ameanza mkataba na Organization.”

Hio bahasha ya kaki ina taarifa za kampuni yetu na kila kitu kinachohusu kampuni. Pia kuna form za mikopo ipo humo ambayo mimi na mama yako tulikopa kupitia kampuni yetu, utapitia kwa makini ujue kiasi kilichokopwa na tulichorudisha. Kuna taarifa zote humo utaziona, kama kuna sehemu utakwama bhasi utanipigia simu mwanangu.

Mama Janeth alionekana kumpenda sana Iryn kweli kweli. Muda huo mimi nilikua kama mpenzi msikilizaji maana sikua nachokuzungumza pale, niliishia kula popcorn mpaka zikaisha.

Ni mazungumzo yaliyochukua masaa 2 na baada ya kumaliza walikubaliana alhamisi siku watakayo onana bhasi Iryn aende na zile form.

Muda huo Mama Janeth alikwenda ndani na akarudi na Camera aina ya Canon na akaomba niwapige picha na Iryn. Alinielekeza namna ya kupiga na mimi bila kukosea nikawapiga picha pale.

Tulitoka hapo tukaenda kwenye Saloon palepale Masaki na ilionekana kuwa busy sana. Mama Janeth akamtambulisha Iryn kwa wale wafanyakazi kama Bossy wao mpya akiwa kama mrithi wa Mama yake, hapo ndo wakajua Iryn alikua ni mtoto wa Marehemu. Ilikua ni Saloon kubwa tu ambayo inafanya mambo mengi sana mpaka kupamba maharusi.

Baada ya kilakitu na mazungumzo yao kukamilika waliagana na Mama Janeth aliendelea kubaki pale saloon. Baada ya kutoka hapo Iryn akasema twende Coco beach nikale mihogo, nimeimiss.

Muda mfupi tulikuwa tumewasili pale Coco na wakati tunaingia walionekana watu wakiifukuzia gari, si mnajua pale Coco ukienda jinsi watu wanavyo gombania mteja?.

Tulipark gari yetu vizuri na baada ya kushuka kwenye gari, Iryn alinambia nimfuate. Alionekana mtu ambaye anayajua mazingira vizuri ya pale. Tulikwenda na tukaa sehemu moja ipo na mwishoni huku, tukatulia pale huku tukipulizwa na upepo mzuri wa Bahari.

Kuna Kaka alikuja pale na alioneka kufahamiana na Iryn vizuri tu.

“Sister karibuni sana, karibuni jamani”

IRYN : “Nataka mihogo mizuri laini na mishikaki. Utaleta mihogo 4 na mishikaki 20.”

MIMI: “Mbona unaagiza mishikaki mingi sana hivyo?”

IRYN : “Kaka pia niitie yule wa madafu. Insider akileta ndo utajua kwanini nimeagiza mingi hivo.”

MIMI : “Sawa Bossy wangu mimi siwezi kupinga.”

IRYN: “Afu hilo jina silipendi, hujui tu.”

MIMI : “Sasa unataka nikuite nani? Kwani wewe sio Bossy wangu.?

IRYN: “Niite jina langu, simple tu.”

Na muda huo jamaa wa dafu alikua kafika wakati tukiwa kwenye mazungumzo, jamaa akatukatia madafu 2 pale na Iryn akamwambia jamaa amkatie mengine 2 ya kuondoka nayo.

IRYN: “kaka kama mabaya sikulipi, kama unajua ya leo sio mazuri bora usikate”

“Dada mimi ndo mtaalamu wa madafu hapa umefika hata usiwe na wasiwasi.”

Jamaa baada ya kutukatia madafu na kuondoka story ziliendelea pale taratibu huku tukifurahia utamu wa dafu.

IRYN : “Insider unapaona pale?”

MIMI: “Pale ndo ilikua siku yangu ya mwisho kumpiga mama picha”

Na muda huo Iryn alitoa simu kwenye mkoba na alinionesha picha alokuwa kampiga mama yake eneo lile. Alinionesha picha zingine za Mama yake nyingi tu ambazo walikua pamoja na zile ambazo na mama yake alikua peke yake.

Nikaomba anioneshe na picha za Baba yake, bhasi akanionesha picha ambazo walikuwa pamoja yaani yeye, baba na Mama yake. Pia akanionesha picha ambazo alikua na Baba yake.

Baba yake Iryn alikua ni Mzungu ila alikua ni M-South Africa, Iryn alinambia origin ya Baba yake ni Uholanzi.

Mama yake Iryn alikua mzuri sana alikua na ule urangi wa ki-Ethiopia nafikiri sote tunajua Waethiopia walivyobarikiwa kwa uzuri. Na Iryn alifanana na sana na mama yake na alichukua kidogo kwa Baba yake kutokana na picha nilivyoziona na yeye alikiri hivo kafanana sana kwa mama.

Muda huo jamaa alikua kaleta mihogo na mishikaki na hapo ndo nikagundua kwanini Iryn aliagiza mishikaki mingi.

IRYN : “Insider umeelewa sasa kwanini niliagiza mishikaki mingi?”

MIMI : “Nimeelewa ni vidogo sana asee. Ila ni vitamu sana.”

IRYN : “Mimi na mama tulikuaga tunakuja hapa tunakula mihogo na mishikaki na tulikua tunakaa hapa.”

MIMI: “Nashangaa kuona hata wewe unakula mihogo.”

IRYN : “Shida yako Insider unanichukulia mimi kama slay queens, pole yako.”

MIMI : “Jinsi ulivyo ni ngumu mtu kukuelewa, mrembo kama wewe kula mihogo ni ajabu sana, hii waachie akina Mwajuma”

IRYN: “Napenda sana traditional foods”

Muda huu pia nilikua nawaza namna ya kumuingia kuendeleza mada ya Muajemi, maana ile pesa yake nilikua naipigia malengo sana.

MIMI: “Afu unakumbuka kule Kidimbwi ulisema tutadiscuss ishu ya Muajemi, nasubiri jibu lako ili nimpe kirungu chake.”

Muda huu Iryn alikua akiniangalia….

IRYN: “Si anataka tuonane? Haina shida, nikigundua ni Important person nitamkip close.

MIMI : “Hayo ni wewe ila nahisi atakua ni Potential sana, hata kwangu pia.”

IRYN : “Kwani wewe Insider una mipango gani ?”

MIMI: “Na mpango wa kufungua biashara ya Lubricants, atlist nina experince nayo.”

IRYN : “Good, I love your hustles. Sitaki kukuuliza maswali but you promised utaniambia kuhusu wewe.”

MIMI: “Usijali hata home nitakupeleka, ukale ugali wa mlenda.”

IRYN: “I will be waiting for that day”

MIMI: “Muajemi tunameet naye lini?

IRYN: “Alhamis tukimaliza mizunguko tunaonana naye, you said he can be trusted but I trust you”

MIMI: “Nipe tano bhasi”

Ile kunipa tano nikampa tano ya nguvu akaanza kulalamika pale… “Au au… ndo nini hivi Insider…”

Nikamwambia inuka bhana inuka bhana nataka nikusaprize.

Nikamwinua nikampeleka pale aliponionesha alimpiga picha mama yake. Nikamwambia anipe simu yake nimpige picha, bhasi akaweka mapozi nikampiga picha za kutosha.

Licha ya yote kuna mambo ambayo nilikua namfanyia Iryn sababu nilijua anaya miss kutoka kwa mwanaume. Jamaa yake Grizz alikua Ufaransa ambapo nilikua najua lazima atakua na demu kule, hakuna mapenzi ya mbali kwnye Dunia hii. Na yale mambo nilokua namfanyia alikua akiyafurahia sana tena sana, hata kitendo cha kumpiga picha alifurahi sana.

Tukalipia ile Bill kwa jamaa na sisi tukaondoka pale Coco, sasa wakati tuko kwenye gari Prisca alikua anapiga simu, nikakumbuka nilimuahidi nitakwenda kumuona chuo na sikwenda lazima atakua kamind. Muda huo na mimi sikusita palepale nikapokea simu yake, tukaongea na nikamwambia nitakwenda kwao kumwona.

Tulikwenda na Haile selassie Road na tulikuja kutokea pale Kanisani “St peters”, sasa wakati tuko pale mataa tunasubiri folen, ile mitaa huwa wanauzaga sana maua. Nilipata wazo nimnunulie Ua Iryn kama zawadi nifanye kumsaprize na ua, nikamwita dogo mmoja akaja chap na maua.

“Dogo maua unauzaje?

“Bro park gari pale tuongee vizuri.”

Muda huu Iryn alikua akiniangalia ni kama alikua anajiuliza Insider ananua ua kwa ajili ya nani? Na alikua akitizama kinachoendelea kwa makini, na mimi nilimsoma akili yake.

“Dogo kwani hapa huwezi fanyia biashara? Pale mataa hatutoki sahivi si unaona kuna traffic pale?.”

“Bro haya utanipa elfu 20 na haya elfu 30”

Nilipiga jicho kali na nikalipenda Ua moja lilikua jekundu afu ni zuri sana,

“Nimelipenda hili, dogo bei za maua nazijua vizuri nipe bei za jioni mimi nilipie.”

“Bro hilo top nipe 25 hata wewe si unaliona lilivyo zuri?”

Japo nilikua najua bei yake ni 20k bhasi sikutaka kubargain naye sana na nikatoa pesa nikampa kiroho safi na palepale nikapandisha kioo cha gari.

Sikutaka kumpa Iryn nafasi ya kuongea hata kidogo na nikamkabidhi lile ua palepale.

“This gift is for you mummy”

Ni kama Iryn alipigwa na shock hakuamini kama lile ua lilikua ni kwaajili yake ni ilikua saprizi moja ya kutotegemea. Kama ni point bhasi pale nilibeba point 10, na muda huo Iryn alikua anafuraha sana.

Nikamwambia Iryn hii ni zawadi yangu kwako kwa yote unayonifanyia, sina uwezo wa kukunulia saa ya gharama, sina uwezo wa kununulia necklace ya gharama, lakini kwa hiki kidogo naomba ukipokee kwa mikono miwili.

“No Insider It’s means alot to me, Ahsante sana kwa hii zawadi hujui to what do I feel right now. Nashukuru sana hii ni zawadi kubwa sana kwangu hujui tu.”

Wakati tuko njiani Iryn aliendelea kulitizama lile ua kwa furaha sana.

Tulifika kwake nikapark gari pale getini nje, nikamfungulia geti nikamsindikiza mpaka kwake na nikamfungulia mlango. Nikamuaga nawai tutawasiliana badae bhasi na palepale akanihug kwa nguvu, aisee nililifeel lile joto lake na lilikua amazing [emoji2956] afu lile OG.

Tukaachana pale na mimi uelekeo ulikua ni kwenda kuonana na Prisca, sasa wakati niko njiani nilikua nawaza zawadi ya kumpeleka Prisca. Ua ndo ilikua zawadi nzuri kwake lakini mazingira yalikua magumu kurudi tena pale namanga. Niliwaza sana lakini sikuona zawadi ya kumchukulia, nikasema nitaingia pale Shoppers hapohapo nitajua cha kumpelekea.

Hatimae nilifika pale Shoppers Mbezi Beach na nikazama ndani lakini huwezi amini hata sikuona cha kumnunulia. Nilizunguka mle ndani kama mtalii na nikaishia kununua popcorn na bubblegum “Mentos” zinakuwaga kwenye vikopo vidogo hivi.

Na muda mfupi nilikua getini kwao, nikampigia simu akanambia niingie ndani daah “what the fvck” nilijisemea moyoni. Sikutegemea angenambia niingie ndani, na muda huo mlinzi alikua kafungua geti tayari.

Muda huo nikijifikilia jamaa akaja akanambia amesema uingie ndani,

“Prisca ameanza ujinga gani huu…..”. Nilishindwa kataa nikaingia nikapark gari na yeye alikua katoka tayari kunipokea.

Nikampa ule mfuko nilokuja nao akanambia niingie ndani, sikuweza kukataa maana wanasema maji ukishayavulia nguo sharti uyaoge.

Nikaingia ndani nikamkuta Mary yuko seblen, lakini pia pale seblen palikua na dada mkubwa mmoja na madogo wawili wa kike.

Mary alivyoniona akanisalimia pia akanikaribisha kwa tabasamu.

MARY: “Insider leo umeamua uingie ndani”

MIMI: “Nimeingia sababu ya mgonjwa lasivyo nisingethubutu”

MARY: “Hakuna anachoumwa huyo anakusumbua tu.”

Prisca alinitambulisha kwa ndugu zake na alinza na yule dada mkubwa ambaye alinitambulisha kama Mamdogo wake, hakuishia hapo akawatambulisha wale madogo wa2 wakike ni wadogo zao. Hapo nikajua kumbe familia yao wako watoto wa4 lakini wote ni wa kike.

Na muda huo dada alikua kaniletea juice na mimi nikaanza ikaifakamia palepale. Ofcourse sikuwa confident sana mle ndani ukizingatia Mwanaume nilikua peke yangu naye koroma mle ndani.

MARY : “Insider leo utanipa namba yako ya simu, sometimes huwa nahitaji huduma ila nashindwa kukupata.”

Wakati anaongea hivyo, alipigwa jiko kali sana na Prisca

MIMI: “Haina shida, Prisca ameshindwa kukupa?”

MARY : “Insider Prisca hawezi kunipa namba yako, na sijui kwanini hataki niwe na namba yako.”

MIMI: “Lete simu nikuandikie hapahapa.”

Na muda uleule Mary alikuja akaa pembeni yangu, nikamwandikia namba na akabaki palepale hakuondoka.

Muda huu Mamdogo wao alikua akiniangalia kwa macho ya kiwizi wizi, nikama mtu ambaye alikua anasikia story zangu ila alikua hajapata bahati ya kukutana na mimi. Prisca naye muda wote alikua kimya hakusema neno lolote.

PRISCA: “Insider can we talk private?”

MIMI: “Yeah,sure”

Tulitoka pale tukakaa kibarazani lakini nilikua sijiamini kabisa maana nimeingilia Himaya ya watu. Prisca japo alinitoa wasiwas kwamba wazazi wake sio minder hawana shida kabisa.

Pale kibarazani kulikua na coach vidogo flani hivi vi-nne na meza ndogo duara ya kioo.

MIMI: “Nambie unaendeleaje Mummy”, nilikua ninamshika mashavu.

PRISCA : “Safi tu”

MIMI: “Mbona kinyonge sana? Umepooza sana, shida nini?.”

PRISCA : “Insider you fvcked me hard that day, but now am okay”

MIMI: “Ooh sorry, seems like unataka tena.”

Prisca kama alipata na ka-aibu fulani ila aliishia kutabamu na akachange mada. Lakini mimi nilielewa anachohitaji.

PRISCA : “Nimefurahi umeingia ndani leo.”

MIMI : “Nimeingia leo sababu unaumwa ila hutoniona tena humu ndani.”

PRISCA : “Usijali hata mimi nitakuja kwenu.”

Nikaona huyu mwanamke ameanza kuleta mambo ya kichawi, aje kwangu kufanya nini?

MIMI: “Mimi nasepa hata hivyo muda umekwenda, na muda huo ilikua saa1 usiku na madakika tayari”

Na muda huo Mary alikua amekuja pale kibarazani na akakaa.

MARY : “Insider unavyoondoka nishtue nataka unipe lift.”

MIMI: “Mimi ndo naondoka hapa, nilikua na mpango wa kuja kuwaaga huko ndani.”

Tukaondoka pale na Mary tukaingia kwenye gari hao tukaondoka.

MIMI: “Unaelekea wapi.?”

MARY : “Nataka kwenda stationery na kazi ya kufanya nataka nimpe mtu kazi. Insider wewe unakaa wapi?”

MIMI: “Mimi nakaa Massana kule.”

MARY : “Pale si pana stationery nzuri”?

MIMI : “Yeah ipo”

MARY : “Twende hapo.”

MIMI: “Ila sitokurudisha utarequest”

MARY : “Sawa”

Wakati tuko njiani tulikua tunapiga story mbalimbali na Mary akili yake ilionekana kukomaa sana. Tulifika pale Massana nikamdrop kwenye stationery mimi nikaondoka, nikamwambia ukirudi home utanijulisha.

Mimi nilivyorudi kama kawaida niliingia bafuni, baada ya hapo nikachukua laptop yangu nikaanza kuangalia mipango yangu. Pia mimi nilikua nimeandaa Excel sheet ambayo nilikua naweka taarifa za biashara kila siku kwa nilichoingiza na kutoa. Kama mafuta nilikua nachukua risiti kila napo jaza ili zinisaidie katika mahesabu, mwisho wa mwezi ndo nilikua napiga accounting za mwezi husika hasa kwenye mapato na matumizi na faida iliyopatikana.

Baadae kidogo Iryn alinipigia simu na tuliongea sana hii siku kwenye simu kuliko zote. Na zaidi aliifurahia sana ile zawadi ya UA akanambia mtu wa mwisho kumpa zawadi ya Ua alikua ni mama yake. Na mimi ndo nimekua mtu wa kwanza kumpa zawadi hio baada ya kifo cha mama yake. Tuliongea sana na simu na akaomba kesho niende kwake nikamsaidie kuzipitia zile form pamoja.

TO BE CONTINUED.
Mambo yamenoga
 
Hivi wakuu mpaka hapa tulipofikia kila moja list yako ya GREATEST Story tellers wa JF ni ipi?. Mimi japo sijasoma nyingi lakini hawa jamaa wafuatao nawaheshim
1. leadermoe R.I.P
2. UMUGHAKA
3. INSIDER MAN
4. LwandaMagere
5. Bado Sijasoma nyingine ila kuna room ya kupatikana wa nafasi hii km nikikuta story matata [emoji3]
For me

Analyse and @lara1 ndo watu hatari sana.

After all, hao ni kati ya storytellers wanaojali muda na hisia za wasomaji.


Wengine anaweza kukwambia story ya kweli, lakini ni story! haijulikani muda hasa ni upi.

Once a day? A week? or what....
 
Sawa kaka tunaisubiri[emoji1666]
I appreciate Mkuu

Thank You[emoji120]
EPISODE 14

“A TRUE STORY BY INSIDER MAN”

Nikamshukuru Iryn kwa out then nikawasha gari tuondoke tukalale, wakati tumevuka geti la Kidimbwi kuna gari ilikuja kwa spidi sana na ikatugonga “BOOM”. Ilisikika sauti ya Iryn “Mamaaaa…….”.

TUNAENDELEA…………….

Lilikua ni tukio la fasta sana ambalo lilitupa mshtuko kupelekea Iryn kutoa sauti ya nguvu. Jamaa alitugonga kwa nyuma na kwa spidi sana, palepale ilibidi nishuke na watu walikua wameanza kusogea pale kwa kasi.

Muda huu magari ndo yalikua yanaingia kwa kasi na kutoka, Uber ndo zilionekana kuwa busy sana hili eneo.

Eneo ambalo jama alitugonga ilikua ni kabla hujafika kwenye corner ya kwanza inayokata kushoto kama umetoka kidimbwi.

Baada ya kushuka niliangalia gari upande wa nyuma nikaona jamaa alikua amevunja bampa la nyuma, taa zote mbili za nyuma na sehemu ya nyuma ya boneti ilikua imebonyea.

Jamaa gari yake ilikua ni Prado zile za zamani ila ilikua na ngao mbele. Jamaa alikua bado hajashuka kwenye gari ikabidi nimgongee dirishani atokee nje, ili tuongee.

Baada ya kumgongea dirishani lakini jamaa hakutoka ni kama alikua na dharau, hichi kitendo kilizidi kunipa hasira sana. Na muda huo askari mgambo wanaolinda eneo hili walikua wameshafika eneo la tukio.

Kwa upande mwingine foleni ilizidi kuwa kubwa sana maana hakuna gari zilizokuwa zinatoka wala kuingia pale Kidimbwi. Na muda huo Iryn alikua kashatoka kwenye gari, akaja akanishika mkono.

Kwa tukio liliokuwa limetokea pale mwenye kosa alikua ni jamaa, maana yeye ndo alinigonga kwa nyuma, napia sheria ziko wazi hivyo hakukuwa na haja ya kumtafuta mchawi ni nani.

“Huyu fala anadharau sana, anamakosa ila hataki kutoka nje. Watu kama hawa ndo wakuwatia makofi”. Ilisika sauti ya dereva wa bodaboda aliyekuwa kwenye bodaboda yake.

Watu walizidi kumiminika hasahasa madereva wa magari walikua wamefika kuona nini tatizo, na wengi walikuwa wanapatwa na hasira kuona jamaa hataki kutoka kwenye gari.

Jama alikuwa na demu wake ambaye alikuwa amekaa upande wa mbele, dem alikuwa kama anamwomba jamaa atoke nje. Kwa upande mwingine Mgambo walikua wamemgongea jamaa ashuke na madereva pia walikua wameanza kumgongea kwa fujo, maana jamaa alikuwa anafanya mambo ya kizamani sana, afu pia ya kishamba.

Baada ya muda jamaa akashuka na alionekana mtu ambaye amelewa hakuwa na akili zake.

“We ms*** unazingua baada ya hili suala mlimalize mapema wewe unaleta mapozi, acha ufala sisi madereva hatuko hivo.” Hii ilikua ni sauti ya jamaa ambaye alikua ni dereva akimwambia jamaa.

Foleni ilizidi kuwa kubwa na kupelekea watu kuzidi kumiminika pale, maana hakukua na gari inayotoka wala kuingia.

MGAMBO: “Bro siku nyingine usifanye ujinga kama huu hili kosa ni lako, ulipaswa kushuka na myajenge haraka.”

JAMAA : “Samahani bro! Tunaweza ongea kuhusu hili private?”

Jamaa alikua akiniomba tuongee private.

MGAMBO : “Hakuna haja kuongea private, cha msingi tumsikilize jamaa hapa atasemaje”

Palepale alitokea jamaa ambaye ni dereva wa Uber na akatoa hesabu na gharama za vifaa na utengenezaji.

“Hii ni IST ya 2006 taa za nyuma moja ni 180,000/= kwa mbili ni 360,000/=. Bampa hilo halifai tena gharama zake ni 250,000/=, kunyoosha hio boneti na kupaka rangi hapo andaa 100,000 kwa jumla hapa ni 710,000/=. Kama jamaa atakuchaji na usumbufu juu yake ila gharama za hapo ni uhakika. Hii gari kali sana bado mpya naona umeshaitia ngeu tayari.”

Muda huu pia Iryn alionekana kunionea huruma sana maana alikua anajua gari itakua ya boss, hakuwai kuuliza kama gari ni yangu au laah! na mimi pia nilikuaga siwaambii wateja kama gari yangu.

IRYN : “Insider unafanyaje sasa?, I can feel you, I’m really sorry.”

MIMI: “Jamaa kama atatoa hizo cost no problem tutatamaliza”

IRYN: “Atakubali sasa?”

Muda huo Mgambo akawa amekuja upande wangu akiniuliza maamuzi yangu ni nini juu ya hili jambo. Upande mwingine madereva walitamani sana hili jambo liishe mapema maana tungesema tusubir traffic kwa muda ule isingekua rahisi kwa Traffic kufika mapema.

Nikamuuliza jamaa alokua anatoa hesabu za matengenezo kama anauhakika na zile bei alizotaja, na madereva wengi wa Uber walikuwepo pale wakasema ni sahihi.

MIMI: “Kama jamaa atakua tayari kutoa hizo gharama sina shida naye anipe 750,000/=. Hio 40,000 iwe kama usumbufu wa kunipotezea muda kwenda garage.”

Kwa upande wa jamaa aliyenigonga ni kama hakua tayari maana alisema hana hela na hicho kiasi ni kikubwa sana kwa upande wake.

DEREVA UBER: “Hivi wewe jamaa una akili kweli? Mshukuru hata jamaa ni mwelewa na mstaarabu sana, kwanza hapo umelewa tukiita traffic hapa unakesi nyingi sana, kama unayo hio amount mpe jamaa tuondoke foleni imeshakua kubwa sana.”

Na muda huu uongozi wa Kidimbwi ulikua umefika pale kutoa usuluhishi.

JAMAA: “Hiki kiasi cha Pesa kwa sasa sina, mpaka niongee na Mzee au tutatumia Bima ya gari, bima yake ni kubwa.”

DEREVA UBER: “Bro embu kuwa serious Kama ni Bima ya gari inamaana tusubiri traffic waje kupima? na Bima inachukua muda mrefu kutoa majibu, jamaa asubiri majibu ya Bima?, hata mimi siwezi kukubalia.”

Kulikua na kelele za madereva wengi walikua ni Uber na walionekana kuwa na hasira sana huu usiku.

MIMI: “Kama jamaa anataka Bima ndo itahusika, bhasi anipe gari yake nimwachie hili akatengeneze, gari ikikamilika na mimi nitakukabidhi lako unaonaje mzee?”

Watu walionesha kufurahishwa na hii kauli yangu na waliiunga mkono. Jamaa baada ya kusikia hii kauli ni kama alishindwa cha kusema.

Uongozi wa pale Kidimbwi, Mgambo walikua wakiongea namna ya kupata solution, palepale Iryn akaanza kuongea.

IRYN: “Bro haya ni maisha tu, leo inaweza kuwa kwako, kesho ikawa kwetu. Hili suala tunataka liishie kirafiki ili kila mtu akaendelee na maisha yake. Hatuwezi kupelekana police kwa jambo dogo kama hili, ukisema utumie Bima kwanza itachukua muda mrefu sana, pili sisi tutaendelea kukusubiri mpaka bima itakapokuwa tayari?. Kwanza hapo umelewa, Traffic wata recommend wewe ndo mwenye makosa do you really think bima watapitisha claim yako?, hata kama ni Comprehensive kwa Tanzania hii sio rahisi. Na huo muda ambao unafuatilia upo tayari kutulipa muda wetu wa kusubiri?, naona unaleta masikhara kwenye vitu serious.”

Iryn aliongea na kila mtu aliona dada kaongea point sana,

JAMAA: “Nimeelewa ila sasa nitapataje hii pesa kwa sasa na muda huu ni usku hata kuwapigia wazazi ni ngumu kwa muda huu.”

IRYN : “Ni simple tu, unatumia simu gani?”

JAMAA : “Iphone”

IRYN : “Ilete tuione”.

Na muda huo dem wa jamaa alikua kashuka kwenye gari. Jamaa alikwenda kwenye gari na akatoka na simu

IRYN : “Hii ni iphone 12 Pro. Unaweza kuweka bond hapa afu kesho ukipata hio hela unapewa simu yako, simple like that.”

Watu walioneshwa kuyakubali mawazo ya Iryn na waliunga mkono hoja kwa 100%. Jamaa alisogea pembeni na demu wake ni kama walikua wanajadili kuhusu hili jambo, baada ya dakika 2 wakarudi.

JAMAA: “Bhasi sawa haina shida acha niweke simu Bond”

IRYN : “Itabidi tuandikishiane”

Palepale zikatafutwa karatasi na peni sijui zilitokea wapi kwa muda mle, jamaa mmoja alikua ameleta notebok na peni. Iryn akaomba leseni zetu za gari, mimi nikaitoa kwenye gari lakini jamaa alikua hana leseni, ikabidii tumwombe NIDA.

Tuliandikishiana pale makubaliano baina yetu na upande wa mashahidi “Mimi nilikua na Iryn, jamaa alikua na demu wake, Mgambo 1, na Dereva wa Uber aliyekuwepo pale kama shahidi”.

“Simu yako utawasiliana na jamaa asubuhi au utawasiliana na mimi kwa namba hizo, Jitahidi uwe mkweli maana ikipita kesho tutakwenda Police maana ushahidi wa Picha na haya makubaliano upo.”

Baada ya kuandikishiana kila mtu alisaini na jamaa akatoa line kwenye simu yake akatukabidhi simu, akapiga picha yale makubaliano kupitia simu ya demu wake na mashahidi wengine wakafanya hivyo, na mchezo ukaisha kihivyo kwa ule usiku.

Ilituchukua kama dakika 45 kutoka eneo la Kidimbwi kutokana na ile foleni kubwa. Tulivyofika kwa Zena pale nikafanya kurequest usafiri kwa ajili ya Iryn, na nikapata Uber pale chap, tukaagana na Mimi nikarudi home kulala.

*********

Asubuhi niliamka mapema sana ili kuwapa taarifa wateja zangu “Maggy na Mama 2” kuhusu ajali niliyopata na wakanielewa. Wakati naongea na Mama wa2 akaomba badae tuonane jioni pale Rainbow.

Saa 2 asubuhi Iryn alinipigia simu kujua maendeleo yangu na pia aliuliza kama jamaa kanicheki na nikamwambia jamaa hajanicheki bado.

Saa4 Jamaa ndo alinipigia simu na saa 6 mchana tukakubaliana tuonane pale Morocco. Jamaa aliomba tuonane pale sababu yeye alikua anakaa Magomeni. Baada ya muda huo tulionana na jamaa na akanikabidhi kiasi changu cha Pesa 750,000/=, nilizihesabu zile Pesa na zilikua zimetimia.

Palepale nilitoa karatasi nikaandika kwa nyuma kuonesha tumekabidhiana tayari. Mimi nikaondoka na uelekeo wa Gerezani kutengeneza gari, sababu nilijua pale Gerezani mimi ni mwenyeji hata sitapata shida kwenye kutengeneza gari.

Baada ya kuachana na jamaa nilimpigia simu Iryn nikamwambia nimeshaonana na jamaa na amenipa pesa tayari, akanambia nipitie kwake navyorudi.

Nilifika pale Gerezani nikamtafuta fundi wangu ambaye nilikuaga nafanya naye kazi kwenye ofisi yangu kipindi kile. Jamaa baada ya kuiona gari akanambia hapa chap leoleo tunaimaliza kazi.

Huyu Fundi wangu ni mtaalam sana kwenye masuala ya upakaji rangi yuko vizuri sana. Tulinunua taa za nyuma OG za mtumba pale Ilala pamoja na bampa ya nyuma.

Nakumbuka taa 2 tulilipia 320,000/= na bampa tulilipia 220,000/=. Mpaka jioni gari ilikua imeshakamilika tayari utafikir sio ile ambayo ilikua imebondwa nyuma.

Baada ya kutoka Gerezani moja kwa moja nilikwenda kwa Iryn maana alinambia nipitie kwake navyotoka mjini. Nilipitia pale Namanga madukani nikanunua mtindi maziwa litre 3, Iryn alinambiaga anapenda sana mtindi, hivyo nikafanya kumsaprizi.

“Nilikua nafanya haya ili kuendelea kumvuta Iryn karibu yangu, maana nilikua naingiza pesa nyingi sana kupitia yeye. Iryn alikua tayari mtu muhimu sana kwangu, nilikua namuheshimu sana.”

Nilifika kwake usiku tayari ulikuwa nikaingiza gari ndani, bhasi na yeye alikua katoka tayari na alikua amezunguka upande wa nyuma kulitizama gari.

Na mimi nilikua nimeshuka na dumu la mtindi, Iryn baada ya kugundua ni mtindi alifurahi sana. Bhasi tukaanza kuondoka kuelekea ndani huku tunapiga story.

IRYN: “Gari imependeza sana utafikiri haikugongwa jana Insider.”

MIMI: “Umeona eeh, jamaa nilompelekea alikuaga Fundi wangu ni mtaalamu”

IRYN: “Kwani ulishawai kuwa na Garage?”

MIMI: “Hapana ilikua kama workshop flani hivi , nilikua napiga piga rangi na kupolish magari.”

IRYN: “Sasa ilikuaje mpaka ukaifunga?”

MIMI: “Nimefunga kwa muda but nitarud tena kwenye business. Nilipisha ujenzi wa barabara”

IRYN: “Pole, unaona sasa una mambo mengi ila hujawai nishirikisha kabisa”

MIMI: “Ndomana hata yule Muajemi niligundua atakuja kuwa asset hapo baadae maana anadili na Lubricants atanisadia huko mbeleni.”

Muda huu tulikua tuko seblen tunaendelea na maongezi…..

IRYN: “So Bossy wako umempa taarifa kuhusu gari?”

MIMI: “Hapana sijamwambia kabisa, kuna vitu unavunga tu. Hata ningemwambia asingekua na msaada angeishia kupata presha tu.”

Iryn alikua hajui kama hii ni gari yangu pia usajili wa gari nilitumia jina la wife. Na mimi sikuwai kumwambia gari kama yangu.

IRYN: “Okay nice, ni uamuzi mzuri. Insider una ni hide mambo yako ujue.”

Muda huu alikua kama amenuna, na mimi ikabidi nimsogelee karibu.

IRYN : “Insider niache bhana..”

MIMI : “Sikia kama unataka kujua kuhusu mimi, nitakwambia tena kwa vitendo sawa?, aya nambie umepika nini?”

Iryn baada ya kusikia maneno hayo aliishia kutabasamu.

IRYN: “Twende jikoni ukaone.”

Alikua amepika tambi na Kuku, kwenye suala la mapishi dada pia alikua yuko vizuri sana. Mimi nikapakua nikaanza kula maana nilikua nina njaa sana, sikula mchana.

IRYN: “Insider unakumbuka kesho?”

MIMI: “Yeah si tunakwenda kwa mama Janeth?”

IRYN : “kumbe unakumbuka”

Na muda huu simu ilianza kuita, kucheki alikua ni mama wa2, nikapokea tukaanza kuongea pale. Mama wa2 alikua ananiuliza niko wapi maana anaona kimya simtafuti. Na mimi nikamwambia ndani ya nusu saa nitakua pale, na yeye akasema nitamkuta Rainbow

IRYN: “Insider huyo nani?”

MIMI: “Mteja wangu huyu”

IRYN: “Seems like mna appointment usikuu huu”

MIMI: “Yeah anataka kunilipa pesa zangu za mshahara huwa namchukua asubuhi kila siku”

IRYN: “Sasa kwanini asikupe hiyo kesho?, mpaka akupe usiku?”

MIMI: “Yuko likizo ndomana, pia amenambia kuna kazi ya kufanya naye tukabargain”

IRYN: “Mmh sawa, watu na appointment zenu za usiku”

Muda huu tena simu yangu ilianza kuita na mama yangu mzazi ndo alikua anapiga simu, sababu nilijua mama atakua anapiga simu kuhusu suala la Mama J sikutaka kuipokea simu yake. Nikasema nitaongea naye nikianza kutoka kwa Iryn, nilijua mama lazima anipe vichambo.

IRYN : “Naona anakupigia tena simu na hutaki kupokea, pokea tu.”

Mimi sikumjibu kitu niliamua kunyamaza, wakati huu nilikua niko busy na msosi. Yeye akaamua kuivuta simu aangalie ni nani anayenipigia.

Sasa Iryn alivyoona Mama ndo anapiga ni kama alipatwa na ka aibu, mawazo yake yote yalikua ni atakua Mama wa2 niliyetoka kuongea naye muda sio mrefu.

IRYN: “Kwanini humpokelei mama simu.?”

MIMI: “Mama kuna kazi alinipa sasa sijaifanikisha ndo nawaza hapa jibu la kumpa, maana hatonielewa kabisa.”

IRYN: “Mmhh sawa bhana, sio vizuri huwezi jua anakupigia akwambie nini.”

MIMI: “Nitampigia soon.”

Nilitoka pale kwa Iryn nikamwaga na yeye alitoka kunifungulia geti, tukakubaliana kesho mchana tukutane kwaajili ya kwenda Masaki.

Muda huo niliendesha gari kwa kasi sana kuelekea pale Rainbow Mbezi Beach. Nilifika pale na nilimkuta akinywa Savannah kama kawaida yake.

MIMI : ”Nakuona Mama mkwe unakimbiza taratibu”

MAMA WA2: “Ndo nini kuniweka hivi utafikiri namsubiri Mr.”

MIMI: “Samahani, hesabu zangu kidogo zilifeli ila sijakuweka sana hata hivyo, nitakuongezea Savannah moja ya kukusubilisha.”

MAMA WA2 : “Insider bhana unajua wewe unavituko sana alokwambia mimi nahitaji Savannah ni nani?”

MIMI : “Sasa unataka nini? Maana kuwa mkwe wako umenikazia”

MAMA WA2 : “Mwanangu mdogo yule wewe ukome.”

MIMI: “Afu sijawai mwona embu nioneshe hata picha ili nianze kuandaa hata posa.”

Mama wa2 akatoa simu akanionesha picha za Bint yake ambaye ndo mtoto wake wa kwanza wa kike. Na huyu mtoto wake alikua Advance form 5. Tuseme Mama wa2 amebarikiwa kuwa na watoto wazuri sana, afu wote baba zao ni tofauti.

MAMA WA2 : “Insider mwanangu mpaka amalize chuo ndo hapo mambo mengine yatafata. Hata wewe huyu sio size yako.”

MIMI: “Sema hutaki kuona bint yako anaolewa na Dereva wa Uber, huyo ni size yangu kabisa”

Muda huo dada alikua kaja pale kunisikiliza bhasi nikamnong’oneza aje na Savanna 2 na Heineken 1.

MAMA WA2 : “Insider unafikir sitamani kuwa na Mkwe kama wewe?, napenda upapambanaji wako. Najua hapo una elimu yako nzuri tu ila uneamua kupambana na Plan B hujataka kuajiriwa kama sisi.”

MIMI: “Unafikiri sipendi kuajiriwa? Sema sina connection tu.”

MAMA WA2 : “Umesomea nini?”

MIMI : “Uchumi”

MAMA WA2 : “Nikikutafutia connection upo tayari kufanya kazi?”

MIMI: “Why not, nikamkonyeza” na yeye akatabasamu.

Na muda huu dada alikua kaleta vinywaji, sasa Mama wa2 alishangaa kuona Savannah 2 kwaajili yake napia kuona mimi nimeagiza Heineken.

MAMA WA2 : “Kwahiyo kweli umeamua kuagiza Savannah?”

MIMI : “Yeah kwani nimefanya vibaya?”

MAMA WA2 : “Ahsante nilijua unanidanganya, na wewe pia kumbe ni mtumiaji wa pombe?”

MIMI : “Hapana leo nimeamua kunywa kwa ajili yako, seems like you don’t need my company here.”

MAMA WA2 : “No I’m happy, hata hivyo nilikua nishakunywa 2 tayari. Nikinywa nyingi zitaenda kunisumbua tu.”

MIMI : “Umeniitia nini kwanza nje na mshahara wangu,?”

MAMA WA2 : “Insider jumamosi nataka unipeleke Bagamoyo kabla sijamaliza likizo yangu.”

MIMI : “Bagamoyo unaenda kula bata?”

MAMA WA2 : “Nataka nikapunguze stress za maisha kule.”

MIMI : “Kwahiyo na mimi niandae pamba?, ili ukanilishe bata.?”

MAMA WA2 : “Ndo maana yake unafikiri nitakwenda na nani? Kama sio wewe?.”

MIMI : “Sawa imeisha hio, Bossy wangu.”

MAMA WA2 : “ I am not your Bossy”

MIMI : “Bhasi mama mkwe wangu kipenzi”

MAMA WA2 : “Gari umefanikiwa kuitengeneza?”

MIMI : “ Yeah muda sana si unajua ile ni ofisi siwezi kuchukua muda mrefu, nitakula wapi?”

MAMA WA2 : “Pole sana, so kesho kama kawaida asubuhi?”

MIMI : “Ndo maana yake, kesho asubuhi nitapita asubuhi kumchukua mtoto.”

Tulikaa na mama wa2 pale, akanikabidhi malipo yangu na mimi nikaondoka kurudi home kulala.

Wakati niko njiani nilimpigia simu mama na tukaongea kuhusu suala la Mama J. Nikamweleza mama ishu ilivyokua na mama aliishia kunilaumu sana kwa lile tukio na kunikanya nisurudie tena ule upumbavu. Akaomba nifanye juu chini tuyamalize mapema maana haileti picha nzuri kabisa. Nilimuahidi mama nitahakikisha tunayamaliza na Mama J na muda huo nilikua nimewasili home tayari.

Baada ya kuingia ndani kama kawaida yangu niliingia kuoga baada ya hapo nikasema acha nimpigie simu Prisca nimjulie hali maana toka jana sijaongea naye na yeye alikua hajanitafuta kabisa.

Nilimpigia simu baada ya kuita kwa sekunde kadhaa akawa amepokea;

PRISCA: “Hi Insider, naona umeamua kunipigia”

MIMI: “Hapana mrembo, Samahani nilikua nimebanwa sana na jana nilipata ajali.”

PRISCA: “Ajali ya nini? Mbona sikuelewi?”

MIMI : “Ya gari ila nishasovu tayari kuna mtu alinigonga kwa nyuma”

PRISCA: “Oohh I am really sorry”

MIMI : “How are you feeling today?”

PRISCA : “Kinda good, Insider do you love me?”

MIMI : “Yes I do, why?”

PRISCA : “I think you do not, nimekwambia jana naumwa but you don’t even care. Uko busy na mambo yako.”

MIMI : “I care about you, kesho nitakuja chuo kukuona sawa?”

PRISCA: “Okay, Goodnite byee”

Muda huu nilikua nawaza kumfanya Prisca kuwa kamchepuko kangu lakini nilibaini huyu mtoto angenisumbua sana. Prisca ni aina ya wale wanawake wanaopenda sana kudekezwa na kupetiwa petiwa, na pia ni aina ya wanawake ambao wakipenda wanapenda kweli.

Sasa mimi wanawake wa dizaini hii siwawezi kwakweli kwenye historia ya maisha yangu. Suala la kumbembeleza na kumdekeza mwanamke kama movie za Kikorea mimi siwezi.

Sasa nilikua nawaza kwa upande mwingine Mama J toka ajifungue ilikua miezi 9 tayari ila kuna muda nilikua sipati mahitaji yangu ya kitandani. Sometimes nilikua namwonea huruma na malezi ya mtoto alikua anachoka sana na ukizingatia Junior alikua analipenda sana nyonyo. Nikawaza nimfanye Prisca kma mchepuko ila nitamwambia ukweli aamue mwenyewe kama yuko in or out.

TUTAENDELEA 22:00
INSIDER MAN kwanin wateja ulikuwa uwaambii kama gari ni yakooo
 
EPISODE 15

“A TRUE STORY BY INSIDER MAN”

TUNAENDELEA

Jumanne asubuhi niliweza kuongea na Muajemi na kama kawaida alikua anauliza jambo lake limefikia wapi. Nikamwambia lipo pazuri na asiwe na haraka soon mambo yatakua mazuri.

Jumanne hii pia nilikua na miadi na Iryn kwaajili ya kumpeleka kwa Mama Janeth ambaye alisema kwake ni kama mama mlezi.

Niliwasili pale kwa Iryn na hii siku Iryn hakunitafuta kwenye simu kabisa, niligonga mlango na akafungua. Baada ya kunifungulia mlango na kunikaribisha alikimbilia jikoni, alionekana anapika wakati huo.

Mimi nilikua nimetulia pale seblen kama Baba mwenye nyumba sina hata habari. Baada ya dakika kadhaa Iryn alianza kuniita;

“Insider……”

MIMI: “Nambie Mummy”

IRYN : “Unaweza kupika ugali?.”

MIMI: “Yeah, kitu kidogo hicho, nije nikusaidie?

IRYN : “Nataka nile ugali leo nimepika samaki”

MIMI : “Mimi nisingekuwepo nani angekusongea?”

IRYN : “Ningepika wali, njoo bhasi na mimi nijifundishe.”

MIMI : “Mrembo kama wewe kuzungusha ule mwiko utaweza.?”

IRYN: “Shida yako unanichukuliaga poa sana”

Nilienda pale jikoni nikabandika maji kwaajili ya kupika ugali, na muda huo Iryn macho yake yote yalikua kwangu.

IRYN : “Insider upo vizuri sana ungekua Ulaya sahivi ungekua unafanyia kazi moja ya 5 - star hotel.”

MIMI: “Shida connection tu, angalia vizuri stage zote nazo fanya kesho sitokusaidia.”

Akanipiga na teke mguuni, lilikua teke la kichokozi flani hivi.

Nilisonga ule ugali vizuri mpka ukaiva na ulikuwa laini, bhasi Iryn alishangaa sana.

MIMI : “Na wewe unakulaga ugali?”

IRYN: “Na mwaka sijala ila naupenda sana. Nimeona stage zote kesho nitakusongea ugali wangu.”

Tulikula ule Ugali na Iryn alikwenda kujiandaa,
Baada ya hapo tuliondoka na kuelekea Masaki kwa Mama Janeth. Sikutaka kuuliza tunakwenda kufanya nini huko ila nilisubiri aniambie mwenyewe.

MIMI: “So mama Janeth ndo alikua rafiki wa Mama yako?”

IRYN: “Yeah, pia ndo alikua msaidizi wa Mama kazini kwa cheo, mama alikua coördinator yeye alikua kama Assistant. Nje na hapo walikua pia marafiki wakubwa sana.”

MIMI: “Leo hajakwenda kazini?”

IRYN: “Alikua safari karudi Jumapili nahisi watakua wamempa off”

Tulifika Masaki mapema na moja kwa moja tulikua getini kwa Mama Janeth yeye alikua anakaa karibu na zahanati ya IST, ukishavuka ukuta wa IST kuna kibarabara cha vumbi kinakata kushoto.(INTERNATIONAL SCHOOL OF TANGANYIKA).

Tulifunguliwa na Mlinzi na muda huo Mama Janeth alikua katoka nje kibarazani. Bhasi baada ya sisi kushuka kwenye gari, Mama Janeth alitoka kibarazani na Iryn naye alitembea kwa spidi wakakumbatiana.

“Waow my daughter I have missed you so much”

ili onekana ni watu ambao wamemisiana sana n hawajaonana kwa muda mrefu.

Mama Janeth alikua ni Mzungu na pia alikua anajua kuongea kiswahili vizuri kabisa. Tulikaribishwa ndani na muda ule ule zikaletwa popcorn kwenye vibakuli, Iryn akaanza maongezi na Mama Janeth. Na Iryn alichukua nafasi hiyo kunitambulisha kwa Mama Janeth kama mimi ni rafiki yake kwa hapa Dar.

Maongezi makubwa ambayo nilikua nikiyaskia ni pamoja na suala la nyumba alizoacha Mama Iryn. Mama Janeth alikua anamwambia Iryn haoni sababu ya kuendelea kuzisimamia zile nyumba wakati Iryn yupo.

Nyumba zilikua zimepangishwa na hivyo walikubaliana wale wapangaji watakapo maliza mikataba yao bhasi Iryn ataanza kuwa incharge. Pia walikubaliana kwenda kuzitembelea hizo nyumba zote siku ya alhamis.

Kwa upande wa biashara walizokuwa wanafanya na Mama yake, Mama Janeth alisema zinakwenda vizuri na akamwambia wakimaliza mazungumzo watakwenda kuitembelea Saloon.

Pia walizungumza suala la kubadilisha taarifa za kampuni ambapo Iryn angekua Director. Na sababu alikua na Bachelor ya Usimamizi wa Biashara kwake lisingekua shida, na Mama Janeth alifurahi maana aliamini Iryn angeenda kuwa msaada mkubwa kwenye biashara kutokana na elimu yake.

Iryn alikubali kuanza mchakato wa kubadilisha hizo taarifa za kampuni na wakawa wanaplan pale. Mama Janeth alimwambia Iryn kuhusu Mwanasheria watamtumia wa palepale ofisni, yeye atume TIN na documents zingine muhimu.

Baada ya hayo mazungumzo kuisha walikuja kudiscuss suala la mafao ambayo mama yake alikua anaweka kama kiinua mgongo.

Mama Janeth aliikwenda ndani na akarudi na bahasha mbili za (A4) ambapo bahasha moja nyeupe yenye nembo ya Blue ya organization, akatoa form moja pale na akaamwambia Iryn anatakiwa kuzijaza kwa makini sana.

“Hizi form utaondoka nazo Iryn kasome kwa makini sana angalia mshahara wa mama yako toka anajiliwa, total utakayopata uta times 30%. Nimekuwekea salary slips zote toka mama yako ameanza mkataba na Organization.”

Hio bahasha ya kaki ina taarifa za kampuni yetu na kila kitu kinachohusu kampuni. Pia kuna form za mikopo ipo humo ambayo mimi na mama yako tulikopa kupitia kampuni yetu, utapitia kwa makini ujue kiasi kilichokopwa na tulichorudisha. Kuna taarifa zote humo utaziona, kama kuna sehemu utakwama bhasi utanipigia simu mwanangu.

Mama Janeth alionekana kumpenda sana Iryn kweli kweli. Muda huo mimi nilikua kama mpenzi msikilizaji maana sikua nachokuzungumza pale, niliishia kula popcorn mpaka zikaisha.

Ni mazungumzo yaliyochukua masaa 2 na baada ya kumaliza walikubaliana alhamisi siku watakayo onana bhasi Iryn aende na zile form.

Muda huo Mama Janeth alikwenda ndani na akarudi na Camera aina ya Canon na akaomba niwapige picha na Iryn. Alinielekeza namna ya kupiga na mimi bila kukosea nikawapiga picha pale.

Tulitoka hapo tukaenda kwenye Saloon palepale Masaki na ilionekana kuwa busy sana. Mama Janeth akamtambulisha Iryn kwa wale wafanyakazi kama Bossy wao mpya akiwa kama mrithi wa Mama yake, hapo ndo wakajua Iryn alikua ni mtoto wa Marehemu. Ilikua ni Saloon kubwa tu ambayo inafanya mambo mengi sana mpaka kupamba maharusi.

Baada ya kilakitu na mazungumzo yao kukamilika waliagana na Mama Janeth aliendelea kubaki pale saloon. Baada ya kutoka hapo Iryn akasema twende Coco beach nikale mihogo, nimeimiss.

Muda mfupi tulikuwa tumewasili pale Coco na wakati tunaingia walionekana watu wakiifukuzia gari, si mnajua pale Coco ukienda jinsi watu wanavyo gombania mteja?.

Tulipark gari yetu vizuri na baada ya kushuka kwenye gari, Iryn alinambia nimfuate. Alionekana mtu ambaye anayajua mazingira vizuri ya pale. Tulikwenda na tukaa sehemu moja ipo na mwishoni huku, tukatulia pale huku tukipulizwa na upepo mzuri wa Bahari.

Kuna Kaka alikuja pale na alioneka kufahamiana na Iryn vizuri tu.

“Sister karibuni sana, karibuni jamani”

IRYN : “Nataka mihogo mizuri laini na mishikaki. Utaleta mihogo 4 na mishikaki 20.”

MIMI: “Mbona unaagiza mishikaki mingi sana hivyo?”

IRYN : “Kaka pia niitie yule wa madafu. Insider akileta ndo utajua kwanini nimeagiza mingi hivo.”

MIMI : “Sawa Bossy wangu mimi siwezi kupinga.”

IRYN: “Afu hilo jina silipendi, hujui tu.”

MIMI : “Sasa unataka nikuite nani? Kwani wewe sio Bossy wangu.?

IRYN: “Niite jina langu, simple tu.”

Na muda huo jamaa wa dafu alikua kafika wakati tukiwa kwenye mazungumzo, jamaa akatukatia madafu 2 pale na Iryn akamwambia jamaa amkatie mengine 2 ya kuondoka nayo.

IRYN: “kaka kama mabaya sikulipi, kama unajua ya leo sio mazuri bora usikate”

“Dada mimi ndo mtaalamu wa madafu hapa umefika hata usiwe na wasiwasi.”

Jamaa baada ya kutukatia madafu na kuondoka story ziliendelea pale taratibu huku tukifurahia utamu wa dafu.

IRYN : “Insider unapaona pale?”

MIMI: “Pale ndo ilikua siku yangu ya mwisho kumpiga mama picha”

Na muda huo Iryn alitoa simu kwenye mkoba na alinionesha picha alokuwa kampiga mama yake eneo lile. Alinionesha picha zingine za Mama yake nyingi tu ambazo walikua pamoja na zile ambazo na mama yake alikua peke yake.

Nikaomba anioneshe na picha za Baba yake, bhasi akanionesha picha ambazo walikuwa pamoja yaani yeye, baba na Mama yake. Pia akanionesha picha ambazo alikua na Baba yake.

Baba yake Iryn alikua ni Mzungu ila alikua ni M-South Africa, Iryn alinambia origin ya Baba yake ni Uholanzi.

Mama yake Iryn alikua mzuri sana alikua na ule urangi wa ki-Ethiopia nafikiri sote tunajua Waethiopia walivyobarikiwa kwa uzuri. Na Iryn alifanana na sana na mama yake na alichukua kidogo kwa Baba yake kutokana na picha nilivyoziona na yeye alikiri hivo kafanana sana kwa mama.

Muda huo jamaa alikua kaleta mihogo na mishikaki na hapo ndo nikagundua kwanini Iryn aliagiza mishikaki mingi.

IRYN : “Insider umeelewa sasa kwanini niliagiza mishikaki mingi?”

MIMI : “Nimeelewa ni vidogo sana asee. Ila ni vitamu sana.”

IRYN : “Mimi na mama tulikuaga tunakuja hapa tunakula mihogo na mishikaki na tulikua tunakaa hapa.”

MIMI: “Nashangaa kuona hata wewe unakula mihogo.”

IRYN : “Shida yako Insider unanichukulia mimi kama slay queens, pole yako.”

MIMI : “Jinsi ulivyo ni ngumu mtu kukuelewa, mrembo kama wewe kula mihogo ni ajabu sana, hii waachie akina Mwajuma”

IRYN: “Napenda sana traditional foods”

Muda huu pia nilikua nawaza namna ya kumuingia kuendeleza mada ya Muajemi, maana ile pesa yake nilikua naipigia malengo sana.

MIMI: “Afu unakumbuka kule Kidimbwi ulisema tutadiscuss ishu ya Muajemi, nasubiri jibu lako ili nimpe kirungu chake.”

Muda huu Iryn alikua akiniangalia….

IRYN: “Si anataka tuonane? Haina shida, nikigundua ni Important person nitamkip close.

MIMI : “Hayo ni wewe ila nahisi atakua ni Potential sana, hata kwangu pia.”

IRYN : “Kwani wewe Insider una mipango gani ?”

MIMI: “Na mpango wa kufungua biashara ya Lubricants, atlist nina experince nayo.”

IRYN : “Good, I love your hustles. Sitaki kukuuliza maswali but you promised utaniambia kuhusu wewe.”

MIMI: “Usijali hata home nitakupeleka, ukale ugali wa mlenda.”

IRYN: “I will be waiting for that day”

MIMI: “Muajemi tunameet naye lini?

IRYN: “Alhamis tukimaliza mizunguko tunaonana naye, you said he can be trusted but I trust you”

MIMI: “Nipe tano bhasi”

Ile kunipa tano nikampa tano ya nguvu akaanza kulalamika pale… “Au au… ndo nini hivi Insider…”

Nikamwambia inuka bhana inuka bhana nataka nikusaprize.

Nikamwinua nikampeleka pale aliponionesha alimpiga picha mama yake. Nikamwambia anipe simu yake nimpige picha, bhasi akaweka mapozi nikampiga picha za kutosha.

Licha ya yote kuna mambo ambayo nilikua namfanyia Iryn sababu nilijua anaya miss kutoka kwa mwanaume. Jamaa yake Grizz alikua Ufaransa ambapo nilikua najua lazima atakua na demu kule, hakuna mapenzi ya mbali kwnye Dunia hii. Na yale mambo nilokua namfanyia alikua akiyafurahia sana tena sana, hata kitendo cha kumpiga picha alifurahi sana.

Tukalipia ile Bill kwa jamaa na sisi tukaondoka pale Coco, sasa wakati tuko kwenye gari Prisca alikua anapiga simu, nikakumbuka nilimuahidi nitakwenda kumuona chuo na sikwenda lazima atakua kamind. Muda huo na mimi sikusita palepale nikapokea simu yake, tukaongea na nikamwambia nitakwenda kwao kumwona.

Tulikwenda na Haile selassie Road na tulikuja kutokea pale Kanisani “St peters”, sasa wakati tuko pale mataa tunasubiri folen, ile mitaa huwa wanauzaga sana maua. Nilipata wazo nimnunulie Ua Iryn kama zawadi nifanye kumsaprize na ua, nikamwita dogo mmoja akaja chap na maua.

“Dogo maua unauzaje?

“Bro park gari pale tuongee vizuri.”

Muda huu Iryn alikua akiniangalia ni kama alikua anajiuliza Insider ananua ua kwa ajili ya nani? Na alikua akitizama kinachoendelea kwa makini, na mimi nilimsoma akili yake.

“Dogo kwani hapa huwezi fanyia biashara? Pale mataa hatutoki sahivi si unaona kuna traffic pale?.”

“Bro haya utanipa elfu 20 na haya elfu 30”

Nilipiga jicho kali na nikalipenda Ua moja lilikua jekundu afu ni zuri sana,

“Nimelipenda hili, dogo bei za maua nazijua vizuri nipe bei za jioni mimi nilipie.”

“Bro hilo top nipe 25 hata wewe si unaliona lilivyo zuri?”

Japo nilikua najua bei yake ni 20k bhasi sikutaka kubargain naye sana na nikatoa pesa nikampa kiroho safi na palepale nikapandisha kioo cha gari.

Sikutaka kumpa Iryn nafasi ya kuongea hata kidogo na nikamkabidhi lile ua palepale.

“This gift is for you mummy”

Ni kama Iryn alipigwa na shock hakuamini kama lile ua lilikua ni kwaajili yake ni ilikua saprizi moja ya kutotegemea. Kama ni point bhasi pale nilibeba point 10, na muda huo Iryn alikua anafuraha sana.

Nikamwambia Iryn hii ni zawadi yangu kwako kwa yote unayonifanyia, sina uwezo wa kukunulia saa ya gharama, sina uwezo wa kununulia necklace ya gharama, lakini kwa hiki kidogo naomba ukipokee kwa mikono miwili.

“No Insider It’s means alot to me, Ahsante sana kwa hii zawadi hujui to what do I feel right now. Nashukuru sana hii ni zawadi kubwa sana kwangu hujui tu.”

Wakati tuko njiani Iryn aliendelea kulitizama lile ua kwa furaha sana.

Tulifika kwake nikapark gari pale getini nje, nikamfungulia geti nikamsindikiza mpaka kwake na nikamfungulia mlango. Nikamuaga nawai tutawasiliana badae bhasi na palepale akanihug kwa nguvu, aisee nililifeel lile joto lake na lilikua amazing [emoji2956] afu lile OG.

Tukaachana pale na mimi uelekeo ulikua ni kwenda kuonana na Prisca, sasa wakati niko njiani nilikua nawaza zawadi ya kumpeleka Prisca. Ua ndo ilikua zawadi nzuri kwake lakini mazingira yalikua magumu kurudi tena pale namanga. Niliwaza sana lakini sikuona zawadi ya kumchukulia, nikasema nitaingia pale Shoppers hapohapo nitajua cha kumpelekea.

Hatimae nilifika pale Shoppers Mbezi Beach na nikazama ndani lakini huwezi amini hata sikuona cha kumnunulia. Nilizunguka mle ndani kama mtalii na nikaishia kununua popcorn na bubblegum “Mentos” zinakuwaga kwenye vikopo vidogo hivi.

Na muda mfupi nilikua getini kwao, nikampigia simu akanambia niingie ndani daah “what the fvck” nilijisemea moyoni. Sikutegemea angenambia niingie ndani, na muda huo mlinzi alikua kafungua geti tayari.

Muda huo nikijifikilia jamaa akaja akanambia amesema uingie ndani,

“Prisca ameanza ujinga gani huu…..”. Nilishindwa kataa nikaingia nikapark gari na yeye alikua katoka tayari kunipokea.

Nikampa ule mfuko nilokuja nao akanambia niingie ndani, sikuweza kukataa maana wanasema maji ukishayavulia nguo sharti uyaoge.

Nikaingia ndani nikamkuta Mary yuko seblen, lakini pia pale seblen palikua na dada mkubwa mmoja na madogo wawili wa kike.

Mary alivyoniona akanisalimia pia akanikaribisha kwa tabasamu.

MARY: “Insider leo umeamua uingie ndani”

MIMI: “Nimeingia sababu ya mgonjwa lasivyo nisingethubutu”

MARY: “Hakuna anachoumwa huyo anakusumbua tu.”

Prisca alinitambulisha kwa ndugu zake na alinza na yule dada mkubwa ambaye alinitambulisha kama Mamdogo wake, hakuishia hapo akawatambulisha wale madogo wa2 wakike ni wadogo zao. Hapo nikajua kumbe familia yao wako watoto wa4 lakini wote ni wa kike.

Na muda huo dada alikua kaniletea juice na mimi nikaanza ikaifakamia palepale. Ofcourse sikuwa confident sana mle ndani ukizingatia Mwanaume nilikua peke yangu naye koroma mle ndani.

MARY : “Insider leo utanipa namba yako ya simu, sometimes huwa nahitaji huduma ila nashindwa kukupata.”

Wakati anaongea hivyo, alipigwa jiko kali sana na Prisca

MIMI: “Haina shida, Prisca ameshindwa kukupa?”

MARY : “Insider Prisca hawezi kunipa namba yako, na sijui kwanini hataki niwe na namba yako.”

MIMI: “Lete simu nikuandikie hapahapa.”

Na muda uleule Mary alikuja akaa pembeni yangu, nikamwandikia namba na akabaki palepale hakuondoka.

Muda huu Mamdogo wao alikua akiniangalia kwa macho ya kiwizi wizi, nikama mtu ambaye alikua anasikia story zangu ila alikua hajapata bahati ya kukutana na mimi. Prisca naye muda wote alikua kimya hakusema neno lolote.

PRISCA: “Insider can we talk private?”

MIMI: “Yeah,sure”

Tulitoka pale tukakaa kibarazani lakini nilikua sijiamini kabisa maana nimeingilia Himaya ya watu. Prisca japo alinitoa wasiwas kwamba wazazi wake sio minder hawana shida kabisa.

Pale kibarazani kulikua na coach vidogo flani hivi vi-nne na meza ndogo duara ya kioo.

MIMI: “Nambie unaendeleaje Mummy”, nilikua ninamshika mashavu.

PRISCA : “Safi tu”

MIMI: “Mbona kinyonge sana? Umepooza sana, shida nini?.”

PRISCA : “Insider you fvcked me hard that day, but now am okay”

MIMI: “Ooh sorry, seems like unataka tena.”

Prisca kama alipata na ka-aibu fulani ila aliishia kutabamu na akachange mada. Lakini mimi nilielewa anachohitaji.

PRISCA : “Nimefurahi umeingia ndani leo.”

MIMI : “Nimeingia leo sababu unaumwa ila hutoniona tena humu ndani.”

PRISCA : “Usijali hata mimi nitakuja kwenu.”

Nikaona huyu mwanamke ameanza kuleta mambo ya kichawi, aje kwangu kufanya nini?

MIMI: “Mimi nasepa hata hivyo muda umekwenda, na muda huo ilikua saa1 usiku na madakika tayari”

Na muda huo Mary alikua amekuja pale kibarazani na akakaa.

MARY : “Insider unavyoondoka nishtue nataka unipe lift.”

MIMI: “Mimi ndo naondoka hapa, nilikua na mpango wa kuja kuwaaga huko ndani.”

Tukaondoka pale na Mary tukaingia kwenye gari hao tukaondoka.

MIMI: “Unaelekea wapi.?”

MARY : “Nataka kwenda stationery na kazi ya kufanya nataka nimpe mtu kazi. Insider wewe unakaa wapi?”

MIMI: “Mimi nakaa Massana kule.”

MARY : “Pale si pana stationery nzuri”?

MIMI : “Yeah ipo”

MARY : “Twende hapo.”

MIMI: “Ila sitokurudisha utarequest”

MARY : “Sawa”

Wakati tuko njiani tulikua tunapiga story mbalimbali na Mary akili yake ilionekana kukomaa sana. Tulifika pale Massana nikamdrop kwenye stationery mimi nikaondoka, nikamwambia ukirudi home utanijulisha.

Mimi nilivyorudi kama kawaida niliingia bafuni, baada ya hapo nikachukua laptop yangu nikaanza kuangalia mipango yangu. Pia mimi nilikua nimeandaa Excel sheet ambayo nilikua naweka taarifa za biashara kila siku kwa nilichoingiza na kutoa. Kama mafuta nilikua nachukua risiti kila napo jaza ili zinisaidie katika mahesabu, mwisho wa mwezi ndo nilikua napiga accounting za mwezi husika hasa kwenye mapato na matumizi na faida iliyopatikana.

Baadae kidogo Iryn alinipigia simu na tuliongea sana hii siku kwenye simu kuliko zote. Na zaidi aliifurahia sana ile zawadi ya UA akanambia mtu wa mwisho kumpa zawadi ya Ua alikua ni mama yake. Na mimi ndo nimekua mtu wa kwanza kumpa zawadi hio baada ya kifo cha mama yake. Tuliongea sana na simu na akaomba kesho niende kwake nikamsaidie kuzipitia zile form pamoja.

TO BE CONTINUED.
[emoji24]
 
Mama wawili anaenda kupunguza stress na INSIDER sijui nini cha zaidi kitatokea huko
Iryne hataki kuitwa boss anataka aitwe kwa jina lake na kamfungikia INSIDER mengi ila INSIDER bado hajafunguka kwa lolote
Prisca huyo nae wa moto dada yake kachukua namba sijuo itakuaje
INSIDER daa umekula maisha nasubiri episode ya 16.
 
Back
Top Bottom