Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

EPISODE 70
A TRUE STORY BY INSIDER MAN

FINAL EPISODE


PART I
Kitendo cha Iryn kusema tuachane ilikuwa ni trap ameniwekea na kubwa alitaka kujua mienendo yangu na Asmah. Iryn alikuwa hana imani kabisa na Asmah maana alikuwa anaamini mimi na Asmah tuna mahusiano ya siri sana hata kitendo cha kumpandisha cheo alitaka tuwe close ili abaini kama kuna something fishy kinaendelea kati yetu.

Bossy lady aliniwekea mashushushu/maspy wa kufuatilia movement zangu zote hasa nikiwa na Asmah, kuna ambao walikuwa pale ofisini na wengine wa nje. Nilivyokuwa ninatoka na Asmah kwenda kumtembeza kwaajili ya mazoezi ya mguu alikuwa anapata hizi taarifa.

Taarifa za kwenda apartment ya Asmah alikuwa anapata hizi taarifa kupitia hawa mashushushu wake ambao walikuwa wananifuatulia na Asmah kila move. Hawa mashushushu wake mimi siwafahamu hata sikujua kama ninafuatiliwa namna hii.

Baada ya Asmah kurudi kazini akiwa mgonjwa ukaribu wetu uliongezeka sana ukizingatia nilikuwa nampa kampani ya mazoezi, kwenda kula lunch na hata kumpa lift ya usafiri mpaka kwake. Kitendo cha mimi kuwa karibu sana na Asmah yeye alihisi sisi ni wapenzi wa muda mrefu sana na aliumia sana kwa hili.

Kwanini Iryn alifanya hivi?

CONTINUE…..


Niliichana ile bahasha kwa juu na nikatoa barua ambayo ilikuwa imekunjwa na baada ya kuifungua niliona ameandika mambo mengi sana kwenye ile karatasi na mimi sikutaka kuisoma, nikaendelea kuangalia vitu vingine vilivyokuwa kwenye ile bahasha.

Ndani ya bahasha kulikuwa na bahasha nyingine ndogo na baada ya kuifungua nilitoa picha tatu (3) ndogo za black and white na ile kuziangalia vizuri nilijua zimeprintiwa baada ya kuchukua vipimo vya “Ultra sound”. Pia ndani ya ile bahasha ndogo kulikuwa na form inayoonesha matokeo ya vipimo na pale juu ilikua imeandikwa “Saifee hospital” na niliisoma kwa makini sana na nikagundua Iryn ana ujauzito wa week 4 tayari.

“Ooh shit Iryn ana mimba yangu? Impossible”
Na muda huu nilianza kuingiwa na wasiwasi juu ya Iryn na niliwaza anaweza kutoa ile mimba kwa hasira zake, acha niende kwake mapema before it’s too late. Kwa upande mwingine ile barua sikutaka kuisoma kabisa maana niliona haina umuhimu na mimi sikutaka kujua alivyokuwa kaviandika mle ndani.

Muda huu nikiwa bado kwenye mawazo niliendelea kuwaza,

“Huenda Iryn aliamua kukaa mbali na mimi baada ya kujua ana ujauzito wangu, acha niende kwake ndo nitajua vizuri hukohuko.”

Kwa upande mwingine Asmah alikuwa akiendelea kupiga simu na ilibidi nimtumie ujumbe wa kumwambia nimepata emergence na nitamrudia badae kidogo.

Niliondoka pale ofisini kwa spidi sana kuelekea kwa Iryn na baada ya kuwasili pale kwake niliiona Audi ikiwa pale parking na nikajua huyu yupo ndani na mimi nilipanda kwenda kwake kwa spidi sana.

Nilifungua na kuingia ndani na pale seblen kulikuwa na bag kubwa kama mtu ambaye anataka kusafiri na ilibidi niende mpaka chumbani kwake na nilimkuta akipanga nguo kitandani. Kwa upande wake alishtuka baada ya kuniona ni kama hakutegemea angeniona muda ule pale kwake, na muda huu hasira zake zilianza kupanda kwa kasi sana na akasimama.

IRYN: “Insider what are you doing here? get out of my sight. I don’t want to see you again.”

MIMI: “Baby calm down please, unatumia hasira naomba nisikilize, tuzungumze hili jambo.”

IRYN: “Umenielewa nilichokwambia? Sitaki kukuona hapa naomba uondoke.”

Mkononi nilikuwa nimeshika ile bahasha na nikaifungua nikatoa zile picha za nikamuonesha,

MIMI: “Hiki ndo kimenileta hapa tujadili maana una damu yangu na haya mengine uliyoandika sijasoma na sitaki kujua uliandika nini.”

Na nikachana chana ile bahasha mbele yake huku anashuhudia.

“Baby naomba tukae chini tuongee please, I need just 5 minutes.”

Iryn hasira zilizidi kumpanda na alianza kutoa kigugumizi na koo lilianza kuvimba, ukweli sikuwahi kuona hasira za Iryn kama hii siku.

IRYN: “In..si..der I said get out before I do something bad.”

MIMI: “Really? Something bad?, I know you can do it, letme help you.”

Nilifungua drow ya bedside na nikatoka gun nikaiweka kitandani,

“Take it and do whatever you want”

Nilipiga magoti chini ile “Hands on your knees” na niligeukia upande wa mlango ili nisione action atakayoichukua, muda huu hata mimi akili zangu zilikuwa zimerukwa na nilikuwa siogopi kufa kabisa.

Baada ya dakika niliona mtu akinishika bega na akaanza kuongea,

IRYN: “Insider please stand up.”

Na machozi yalikuwa yakimtoka mithili ya chemichem na macho yalikuwa mekundu sana,

MIMI: “Can’t you do it?”

Na mimi nilisimama tukawa tunaangaliana na nilimsogelea nikaanza kumfuta machozi yake kwa kitambaa changu na haikuchukua muda tukaanza kupeana denda za pupa. Alikuwa kavaa skin jeans, tayari kwa kuondoka na niliishusha mpaka usawa wa magoti na nikamgeuza na kumuinamisha ashike kitanda na nilichomeka mashine kwa nyuma. Pia alikuwa kasuka rasta ndefu na nilizikunja zile rasta zake kwenye mkono wangu, kama mtu anaye endesha farasi na nikawa nahit kwa spidi sana. Niseme hata mimi sikuwa kwenye akili yangu na nilisikia akianza kulalamika pale,

IRYN: “Insider stop I am pregnant.”

Lakini mimi hata sikuwa na habari naye kabisa, muda huu nilikuwa busy sana kutafuta bao la kufutia machozi,

IRYN: “Baby you’re hurting me stop it.”

Ilibidi nimuache na muda huu risasi ziliruka kwa spidi sana na ziliishia kumchafua paja zake kwa nyuma maana wazungu walitoka wengi sana. Muda huu nilimvua nguo zote na zoezi likaanza upya tena ni kama tulikuwa tume-misiana na minyanduo iliendelea mpaka tukawa hoi.

Tulikwenda kuoga na baada ya kutoka bafuni tulikuwa tumelala kitandani na mimi nilikuwa nachezea tumbo lake taratibu sana kama nalibusu kitovuni na wakati nalichezea alikuwa akitabasamu sana,

MIMI: “Baby ulikuwa unakwenda wapi? ndo ulitaka kunikimbia baba mtoto?”

IRYN: “Ungechelewa usingenikuta hapa na jumapili nilikuwa naondoka kwenda south, kila kitu nilikuandikia kwa barua but for now It does not matter.”

MIMI: “Ndo ujue wewe ni wangu na ulikuja Tanzania kwaajili yangu, unataka kusahau ni jinsi gani nimekupambania mpaka leo tumefikia hapa.?”

IRYN: “I appreciate that, Insider unaniumiza sana hisia zangu nashindwa kuelewa wewe Mwanaume unanini? Why I can’t let you go?. I used to love Grizz but when comes to you hit me different why?…why?.”

MIMI: “Mimi leo nataka tumalize mzizi wa fitina, wewe ushakua mama mtoto wangu na una damu yangu tay…..”

Iryn alinikatisha pale maongezi yangu,

IRYN: “Insider nambie wewe na Asmah mna siri gani? please be honesty.”

MIMI: “Leo na confess kila kitu kwako nataka tuachane na hizi drama, Asmah sijawahi kuwa naye kwenye mahusiano ila tumesex kipindi kile naanza kwenda Masaki kuchukua na kupeleka bidhaa ndo tulifahamiana na kupelekea hivyo, lakini mpaka sasa hatujawahi kukutana tena, niseme ilikuwa ni bahati mbaya.”

IRYN: “Leo umesema ukweli nilikuwa najua hili kwa muda mrefu sana, na bado unakwenda kwake mpaka sasa na juzi tu umeshinda na Asmah mpaka saa 4 usiku taarifa zako ninazo zote.“

MIMI: “Ni kweli kwa Asmah nimekwenda mara 2 usiku na nilikuwa nampa lift mpaka kwake, wewe unaelewa fika Asmah ni mgonjwa na mimi ndo nilikuwa namsadia kufanya mazoezi ya mguu na kama napata muda nilikuwa nampeleka kwake, lakini hakuna tulichokuwa tunafanya na yeye anaheshimu hili.”

IRYN: “Doesn’t make sense to me, anyway labda nimwambie kitu ambacho ulishindwa kufahamu kipindi nimekutumia ile voice note.”

MIMI: “Unataka kusema uliniwekea trap?”

IRYN: “Exactly na nilifanya makusudi.”

Iryn alinambia baada ya kutambua ana mimba yangu aliona ni bora ajitenge mbali na mimi ili nisijue na alikuwa anawaza abebe au asibebe maana alikuwa hana imani na mimi kabisa. Kwa upande wake aliamua kutengeneza trap ili ajue tabia yangu, kwani aliamini mimi siwezi kukubali kuishi bila mchepuko na wasiwasi wake ulikuwa kwa Asmah na alitafuta spy wake wa kufuatilia movement zangu na Asmah.

MIMI: “Kwa hili umezingua sana ni vile una damu yangu nisingekusamehe, na kwanini umeshika mimba bila ridhaa yangu?”

IRYN: “Stupid question, you cummed inside me and now pretending to ask why I’m pregnant?, ulitakiwa ufurahi sijafanya maamuzi mabaya kwa mambo unayo fanya.”

MIMI: “Alright mimi nimepokea hili jambo kwa mikono miwili na niko tayari kuwa baba, lakini naomba kwasasa usije home maana mama J kashaanza kuhisi something fishy kinaendelea kati yetu.”

IRYN: “Naomba umuheshimu mama J, mimi nimechagua kuwa hivi ila Insider letme tell you something, nikija kubaini una mwanamke mwingine nje na mimi huyu mtoto hutakuja kumuona machoni mwako, kama kweli unampenda huyu mtoto bhasi naomba utulie, sasa fanya mistake kama utakuja kumuona mwanao na niko serious sitanii.”

MIMI: “Mimi nimechagua mtoto na naomba uniamini mimi sina huo ujinga please.”

IRYN: “I’m just warning you usije ukafikiri natania fanya ujinga na hutokuja kuniona mimi na mwanao.”

MIMI: “Baby usindoke mpaka mwisho wa mwezi nataka niendelee kukaa na wewe na Ahsante kwa kunibebea mtoto najua hii ni heshima umenipa.”

IRYN: “Sawa darling mimi nitaondoka mwisho wa mwezi kwaajili yako.”

Saa yangu ilikuwa inaonesha ni saa 5 usiku na mimi nilisema siwezi kulala pale kwa Iryn, lazima nirudi home, hivyo ilibidi nimuage.

MIMI: “Baby mimi naondoka kwenda home see you tomorrow mapema.”

IRYN: “No problem msalimie mama J.”

Tulitoka wote mpaka parking na aliniaga kwa kuni kiss shavuni na nikaondoka maeneo yale, lakini wakati niko njiani nilikuwa nawaza sana suala la mimba ya Iryn, nilihisi kama ndoto hivi na nikajisemea kesho nitakwenda naye hospital ili na mimi nikajihakikishie.

Nilijisemea kama kweli nitaprove Iryn ana mimba yangu nitamfanya kuwa mchepuko wangu wa siri na siji kuchepuka na mwanamke mwingine yoyote. Hata ile kauli yake aliyosema nikifanya ujinga sitamwona mtoto ilikuwa ikinijia sana kichwani na kutoka na nilishindwa kujua kwanini asisitizie sana hili.

Asubuhi niliamka mapema sana, niliingia kuoga na nikaondoka kwenda kwa Iryn. Baada ya kuwasili pale kwake alikuwa bado kalala na ilibidi nimpigie simu na akatoka kunifungulia mlango.

MIMI: “Good morning mama kijacho.”

IRYN: “Hahaha good morning too darling, bora umekuja mapema ili twende na supermarket tukipata breakfast.”

MIMI: “Twende nikakusaidie kuandaa breakfast.”

Tuliingia jikoni wote na yeye alikuwa anapika chapati za maji na mimi nilikuwa nina tengeneza soup. Wakati tunapata breakfast nilimwambia tutakwenda hospital wote ili nikajihakikishie kuhusu mimba yake.

Mchana tuliondoka kwenda Masaki na tulianza kwenda SALI International hospital ambayo ipo Masaki near na Coral hotel. Baada ya kufika pale na kufuata taratibu zote tulipelekwa chumba special kwaajili ya kuchukuliwa vipimo vya ultra sound na mimi nilikuwa pembeni nikishuhudia.

Ukweli niliweza kujihakikishia kwa macho yangu Iryn ni mjamzito na nilimsogelea Iryn akiwa bado kalala na nikamkiss,

MIMI: “Baby you’re going to be a mom, I’m proud of you.”

Kwa upande wake Iryn alikuwa na furaha sana kwakweli na doctor alikuwa anaongea pale afu alikuwa mhindi,

DOC: “Hongereni sana mimba ni salama na haina shida kabisa na hakikisha unamlinda mjamzito anakuwa salama na anakula chakula bora.”

MIMI: “Doc hili ondoa shaka kabisa.”

Nilichukua simu yake na nikampiga picha akiwa vilevile tumbo wazi kama ukumbusho.

Doctor alitupongeza san na alitupa ushauri na akasema itapendeza tukichukua vipimo kwa wote mpaka vya damu. Tuliona ni ushauri mzuri ukitegemea tunakwenda kuwa wazazi ni busara tukajuana, baada ya vipimo majibu yalionesha sisi ni wazima wa afya kabisa na hatuna kasoro wala shida yoyote.

Tuliondoka hospital kwa furaha sana na tulikwenda moja kwa moja mpaka Salon, ilituchukua chini ya dakika 5 kuwasili ofisini na nilipark gari tukaingia ndani.

Baada ya kuingia ndani Hilda aikuwa yuko pale reception na tukamsalimia wote kwa pamoja na Iryn alikuwa anapita kila room kuwasalimia wafanyakazi na mimi nilikwenda ofisini.

Ndani ofisini alikuwepo Asmah na baada ya kuniona alianza kunimind sana kwa kumchomesha jana ukizingatia tulikuwa tumekubaliana vizuri kabisa. Kwa upande wangu ilibidi nimwombe msamaha kwa suala la jana na nikampa sababu za uongo ili atulie.

Haikuchukua muda Iryn aliingia ofisini na akakaa kwenye coach na akawa anaongea na Asmah pale,

IRYN: “Asmah mpenzi wangu unaendeleaje na mguu wako?”

ASMAH: “Niko poa dear, thanks kwa Insider kanisaidia sana mpaka nimekuwa sawa.”

Kwa upande wangu nilijifanya niko busy na mambo yangu kama siwasikii vile kumbe sikio langu lilikuwa linadaka mawimbi vizuri sana.

IRYN: “Alinambia alikuwa anakupigisha tizi, I’m glad umepona

ASMAH: “Thank you so much bossy, Insider ana Roho nzuri sana.”

IRYN: “Asmah wewe sijawai kukupa gift ila nitakupa gift nzuri sana, mimi nitaondoka soon nataka nikuachie ukumbusho.”

ASMAH: “Jamani unaondoka kwenda wapi tena?”

IRYN: “Nakwenda shule dear.”

ASMAH: “Thank you bossy nitashukuru sana.”

Saa 3 usiku tuliondoka pale ofisini na tulipitia pale Golden fork Mikocheni kupata dinner kwanza. Baada ya kuwasili pale tulitafuta angle nzuri ya pembeni tukakaa na tukaagiza chakula,

MIMI: “Baby wewe ni mjamzito tayari sitegemei kuona unatumia kilevi.”

IRYN: “I know baby siwezi nikatumia kilevi wala chochote chenye negative effects kwa mtoto tumboni. Baby leo si tunakwenda kulala wote?”

MIMI: “Baby nitarudi home sitaki kumkera mama J wangu, but good news anaondoka jumatano na familia yao kwenda kumalizia msiba Moshi so tutakuwa wote.”

IRYN: “Sawa no problem but nimekumiss sana”

MIMI: “Kesho nitakuja asubuhi na mapema kwako nikuf*ck mpaka useme poo.”

IRYN: “No problem wewe wahi home.”

Tulikaa pale mpaka saa 4 usiku na tukaondoka Iryn ndo alisimamia usukani na alinipeleka mpaka kwangu maana kupitia gari pale kwake niliona uvivu.

Baada ya kurudi home nilikuta wife na bibi wamelala lakini dada na Junior walikuwa seblen wamekaa, tangu Junior aanze kutembea alikuwa mgumu sana kulala na kukesha kwake ilikuwa ni kawaida. Niliingia room kuoga na baada ya hapo nilirudi seblen kumchukua Junior na tukaenda kulala.

Asubuhi niliamshwa na mama J na alikuwa akijaandaa kwenda kanisani,

WIFE: “Baba J hauendi church leo?”

MIMI: “Leo siendi mke wangu nimechoka sana afu kuna sehem nataka kwenda.”

WIFE: “Jana hujarudi na gari umeiacha wapi?”

MIMI: “Ndo huko nataka kwenda jana gari ilinizingua ipo kwa fundi.”

WIFE: “Mapema hivi? wamekuuzia mkweche bora ungeagiza Japan tu.”

MIMI: “Tatizo dogo tu sema jana tulikosa kifaa maduka yalikuwa yamefungwa.”

WIFE: “Na hii Dualis ya watu unarudisha lini?

MIMI: “Dada mpaka ajifungue nitampelekea gari yake, ameomba niendelee kukaa nayo, church leo unakwenda misa ya pili?”

WIFE: “Ratiba yangu ya kanisani ndo inaonesha hivyo, byee mimi naondoka mpenzi wangu.”

MIMI: “Niombee na ukirudi naomba tudiscuss suala la dada.”

WIFE: “Sawa pia tunaondoka jumatano kwenda Moshi kumalizia msiba na sina hela kipindi hiki.”

MIMI: “Badae tutaongea hili.”

Baada ya wife kuondoka sikutaka hata kwenda bafuni kuoga na nilijisemea nitaoga hukohuko kwa Iryn, nilibadilika chap na nikachukua bodaboda nikaondoka.

Niliwasili kwa mama kijacho wangu mapema sana na baada ya kuingia ndani yeye alikuwa jikoni anaosha vyombo na nilimkumbatia kwa nyuma, tukaanza kuongea pale,

IRYN: “Baby ulikuwa hupokei simu zangu.”

MIMI: “Nilikuwa nimepanda bodaboda nisingeweza kupokea, umepika nini nasikia njaa hapa.”

IRYN: “Kuna maziwa mkate na maini”

MIMI: “Acha nijisevie wewe endelea na kazi zako.”

IRYN: “Badae itabidi nikamsalimie mama J na Junior.”

MIMI: “Sawa ni wewe tu ila utakwenda peke yako”

IRYN: “No problem I will go there alone.”

Baada ya kupata chai mimi nilikwenda kuoga na baada ya nusu saa Iryn alikuja chumbani na tukaanza kwichikwichi pale, ila ilikuwa ni ile kwichi ya taratibu sana maana alikuwa mjamzito.

Mchana tuliamua kwenda kubarizi beach na tulikwenda Malaika beach haipo mbali na apartment yake. Wakati tuko pale tulikuwa tunaongea masuala mengi na kuhusu masomo yake huko South Africa, kwa upande wangu nilitaka kujua atawezaje kusoma akiwa na mimba?

MIMI: “Baby unakwenda shule utaweza mikiki na hali hii?”

IRYN: “Baby hata sio tatizo masters haina mambo mengi na nitafanya vizuri.”

MIMI: “Claire best yako yuko wapi?”

IRYN: “Tulikwenda Serengeti wote so wakati tunarudi tuliachana, yeye alikwenda Bukoba kutembelea kaburi la baba yake.”

MIMI: “Pole yake na vipi kuhusu suala la mimba yako mama Janeth na Mzee utawaambiaje?”

IRYN: “Usiwe na wasiwasi juu ya hili, Daddy nitamwambia mimba ni yako japo anajua wewe unamtoto, mama Janeth nitakuja kumwambia hata badae huko.”

MIMI: “Wasiwasi wangu mama Janeth akijua mimi ninafamilia afu nimekupa mimba, anaweza akaniona mimi mbaya sana na akanichukia kwa hili.”

IRYN: “Haya ni maamuzi yangu na si yake hata wale watoto zake wote kila mmoja ana baba yake, afu nimegundua siri kubwa sana kwa mama Janeth.”

MIMI: “Siri gani hiyo mummy.”

IRYN: “Tuachane na haya mambo baby not even important.”

Saa 12 tuliondoka pale beach na tulirudi home, lakini Iryn hakukaa na aliondoka kwenda kumsalimia mama J na mimi nilimwambia atanikuta namsubiri.

Baada ya Iryn kuondoka nilichukua simu yangu nikasema acha leo nimtafute Muajemi maana tulikuwa tunapishana sana na pia alikuwa hapatikaniki, nilimpigia simu kupitia Telegram lakini hakuwa online na nikamtumia ujumbe wa kumsalimia.

Baada ya lisaa kupita alinipigia simu na tuliongea mambo mengi sana, kubwa aliulizia maendeleo ya Iryn na mimi nilimwambia anaendelea vizuri na anatarajia kurudi shule kusoma, kwa upande wake alisema Iryn amemblock kwani hampati kwa call wala texts.

MIMI: “Bro! habari ya siku umekuwa adimu sana.”

MUAJEMI: “Niko salama salmini tunapishana nimekuwa busy sana, kwasasa nashinda sana Sudan na hope kuja Tanzania next month tutaonana bro, Iryn ulifikia wapi maana ulinihakikishia”

MIMI: “Bro! Iryn hana shida ila tatizo ni wewe kuwa na familia na ameachana na bwana wake wa Ufaransa kwasababu ya hii, amesema kwasasa anahitaji mwanaume asiye na familia wa kufocus naye.”

MUAJEMI: “Ohh shit, kaka nilikosea sana kumwambia nina familia.”

MIMI: “Haukukosea kaka ulikuwa sahihi kabisa, wewe ukirudi huku tutaongea vizuri, ila mwezi huu anakwenda South Africa kuendelea na masomo.”

MUAJEMI: “Unajua ameniblock nashindwa hata kumjulia hali.”

MIMI: “Mtafute hata kwa namba nyingine uzuri ana kufahamu won’t it be a problem.”

MUAJEMI: “Bro acha nikukimbie tutawasiliana.”

Baada ya kuagana na Muajemi nilikwenda zangu kukaa kwenye balcony nikipigwa na upepo mwanana wa bahari na pembeni nilikuwa na glass yangu ya wine. Ni maisha ambayo sikuwai kudream kuyaishi kama kuna siku nitakuja kaa kwa balcony namna hii, maisha kama haya nilikuwa nayaona kwa movie tu.

Baada ya dakika 20 nilisikia mtu akiniita “Baby… baby…” ni Iryn alikuwa karudi tayari, na alikuja nilikokuwa nimekaa.

MIMI: “Nambie mummy za huko ulikokuwa na umeonana na mama J?”

IRYN: “Ndo natoka hapa na nimeshinda nao, kama unavyoona ndo narudi hapa.”

Na akanikalia mapajani,

“Darling mama J kama anahisi something kinaendelea between us ila sasa naomba udownload snapchat na tutakuwa tunachat huku atleast ni safe.”

MIMI: “Haina shida nitafanya hivyo ila nafikiri tuwe tunawasiliana kwa simu, text ziwe kwa masuala muhimu na ofisi, snapchat kwa usiku.”

IRYN: “Ndo hivyo maana wewe ni mzembe sitaki kuingia uadui na mama J nampenda sana, ila kwa hili atanisamehe.”

Muda huu tulianza romance pale na tulihamia chumbani kuendeleza lecture mpaka wazungu walivyotoka darasani ndo na mimi nikasitisha lecture yangu, nikajiandaa na kuondoka kurudi home.

Baada ya kuwasili home niliingia chumbani na nilikuta box la simu ya iphone na baada ya kuliangalia niligundua ni la iphone 14 na ilibidi nishangae pale inamaana wife amenunua simu mpya?.

Baada ya wife kuingia chumbani uvumilivu ulinishinda na ikabidi nimuulize,

MIMI: “Mama J unalalamika huna Pesa afu unanunua iphone 14.”

WIFE: “Iryn ameniletea simu mpya kama zawadi, kipindi Junior anaiharibu hii simu yangu tulikuwa wote ile siku hapa home.”

MIMI: “Ooh hongera zako iko wapi niione?”

Na wife alikwenda seblen akaniletea na baada ya kuiona ilikuwa ni Iphone 14 pro Max na ilikuwa ni mwezi tayari tangu apple wa lunch simu zao mpya.

Nilitoka chumbani nilikwenda seblen kukaa na bibi na tulikuwa tunapiga story mbalimbali pale hasa za Moshi huko. Bibi ni mwongeaji sana hivyo tulikuwa tunapatana ile mbaya na alikuwa ananikubali sana.

***
Asubuhi na mapema sana niliamka kama kawaida nilikwenda jogging na baada ya kutoka tizi niliingia bafuni kuoga, nikaondoka kwenda kwa Iryn.

Baada ya kufika kwa Iryn alinipa taarifa inatakiwa kwenda Masaki kuangalia nyumba zao maana zilikuwa zinakarabatiwa na ukarabati ulianza wakati mzee amekuja.

Tuliondoka kwenda Masaki na tulianza kwanza na nyumba tuliyokwenda kuitembelea kipindi kile katoka South Africa ambayo aliachiwa na baba yake aisimamie. Baada ya kuwasili pale ilikuwa imekarabatiwa tayari kwa upande wa nje na ilikiwa imepakwa rangi inang’aa, kwa upande wa ndani mafundi walikuwa wanatengeneza furniture.

“Darling twende nyumba nyingine ipo mtaa wa pili.”

Na mimi nilishangaa pale kumbe kuna nyumba nyingine tena, baada ya kuwasili hio nyumba nyingine hata haikuwa mbali na tulitumia muda mfupi kufika mjengoni. Ilikuwa ni apartment nzuri sana ya gorofa 3 na ilikuwa inafanyiwa ukarabati na kulikuwa na msimamizi aliyepewa tenda na walikuwa wanaongea na Iryn.

Iryn baada ya kumaliza kuongea na jamaa alikuja kwangu na tukaanza maongezi

MIMI: “Na hii ni nyumba yenu?”

IRYN: “Mzee alinionesha alivyokuja alisema ameinunua recently, si unamkumbuka yule baba aliyekuja kumchukua mzee siku ile pale Coral hotel?”

MIMI: ”Ndio mummy namkumbuka.”

IRYN: “Ndo aliyemuunganishia mzee, sasa baby hizi nyumba zote na zile za mama ziko under my control ni zangu, mimi naondoka ila nitahitaji uwe unanisaidia kuzikagua, nina imani kubwa sana na wewe maana unakwenda kuwa baba mtoto wangu, naamini huta ni let down.”

MIMI: ”Hili jambo dogo sana naomba ondoa shaka, umebeba damu yangu afu nishindwe kusimamia hizi nyumba hapana kwakweli wewe ushakuwa mke wangu tayari.”

IRYN: “Twende kule kwenye zile apartments za mama nikafanye na ukaguzi.”

Episode za nyuma nilishaandika hii nyumba ya mama yake ilipo na code ipo wazi kabisa ni Masaki na baada ya kufika pale tulifanya ukaguzi na tukaondoka.

IRYN: “Baby unanipeleka kula wapi?”

MIMI: ”Kuna chimbo alinipeleka Asmah Ijumaa ni zuri sana kwa barbecue nafikiri utaenjoy.”

IRYN: “Okay twende baba mtoto.”

Ndani ya muda mfupi tuliwasili Pantaleo na tulipokelewa na mhudumu na tukaagiza chakula pale,

MIMI: “Dada naomba chips kwa mishikaki 5 ya samaki.”

IRYN: “Dada mimi naomba mishikaki ya kuku 3 na chips yai ikaushe vizuri.”

Tulitumia lisaa pale restaurant na tuliondoka kwenda Salon, baada ya kuwasili Iryn alishuka na kimfuko kidogo amekishika mkononi na tuliongozana mpaka ndani ofisini. Mle ofisini tulimkuta Asmah na Hilda wanapiga story na sisi tukawasalimia.

IRYN: “Asmah bora nimekuona mamaa nina gift yako hapa.” Na akamkabidhi pale.

“Open it..”

Na mimi ilibidi niangalie ni zawadi gani hiyo Iryn anampa Asmah?, na muda huu Asmah alitoa box la simu kwenye ule mfuko na ilikuwa ni iphone. Kwa upande wake Asmah aliishia kufurahi sana muda huu, licha ya kuwa na iphone kali lakini alipewa tena ingine na Iryn.

ASMAH: “Wow thank you bossy.”

IRYN: “Nimeamua kukupa gift ya simu ambayo nilikuwa naitumia mimi ili nikiwa sipo uwe unanikumbuka kwa kuchapa kazi kwa bidii, hio simu ni mpya kabisa maana nilikuwa naitunza sana.”

ASMAH: “Nashukuru sana bossy wangu Allah akuzidishie, na kuanzia leo nitaanza kuitumia hii.”

Kwa upande wangu nilijisemea Iryn katoa zawadi ya simu kwa Asmah huenda ana target zake anataka kuzikamilisha. Kwa upande wa Asmah yeye alikuwa kafurahi sana kwakweli na sura yake ilikuwa na furaha na yenye tabasamu.

Tuliendelea kushinda pale ofisini mpaka jioni na tukaondoka kwenda Mikocheni.


PART II

Jumanne jioni wife aliondoka kwenda kwao pamoja na bibi na dada kwaajili ya kujiandaa na safari yao ya jumatano kwenda Moshi kumalizia msiba. Niliwapa ride mpaka kwao na sikutaka kuendelea kukaa pale ukweni, hivyo nikaondoka kurudi home nikachukua baadhi ya nguo na nikaenda kwa mama kijacho wangu.

Baada ya kuwasili pale kwake niliingia ndani lakini sikumkuta lakini mazingira yalionesha yupo, nikajua kwa muda huu atakuwa swimming. Na mimi nilibadilika haraka nikaenda kwa swimming pool na kweli alikuwa anaswim pale na baada ya kuniona alionesha kufurahi sana, nikaingia kwa swimming na tukaanza kuswim pamoja ilikuwa ni burudani.

IRYN: “Baby mama J ameondoka tayari?”

MIMI: “Amekwenda kwanza kwao ila kesho asubuhi na mapema wataanza safari ya kwenda Moshi.”

IRYN: “Baby huu muda uliobaki nataka niondoke hapa nikamalizie sehemu nyingine.”

MIMI: “Unataka kwenda wapi?.”

IRYN: “Nitafute Apartment ya muda Masaki.”

MIMI: “Sawa ni wewe tu mimi nitakupa kampani.”

Wakati tukiendelea kupiga story na kuswim kwa upande mwingine kuna couple ilikuja pale swimming na sisi tukaamua kuondoka ili tuwaachie uwanja. Baada ya kurudi ndani tulibadilika na tuliamua kwenda Mlimani city kupata dinna.

Penzi lilikuwa ndo kama limechipua limeanza upya maana tulikuwa tumekaa kimahaba sana hata mtu akituona bhasi anajua wale ni wapenzi.

IRYN: “Baby guess mtoto atakuwa jinsi gani?”

MIMI: “Huyo wa kiume 100%.”

IRYN: “Napenda mtoto wa kiume but nilitamani nikuzalie wa kike ili ubalance afu wa pili awe wa kiume.”

MIMI: “Sidhani kama atakuwa wa kike kwa tarehe za mimba kupatikana na uhakika ni wa kiume huyo.”

IRYN: “Mungu naye ana mipango yake.”

MIMI: “Baby unakwenda kuwa mama ulijipanga au bahati mbaya?”

IRYN: “I don’t want to talk about this right now.”

MIMI: “Seems ulijipanga ndomana unafuraha sana.”

IRYN: “You know nothing.”

MIMI: “You are going to be the best mom.”

Baada ya kumaliza kula hatukutaka kupoteza muda na tuliondoka kurudi home na baada ya kuwasili nilichukua wine kwenye glass nikaenda kukaa kwa balcony huku napata upepo mwanana wa Bahari.

Baada ya dakika 20 Iryn naye alikuja akiwa amevaa gauni shati, inakuwa inashuka kidogo mapajani, hakuwa na bikini na akanikapandia kwa juu huku akinitizama kwa tabasamu sana na macho ya kurembua.

Aliingiza mkono ndani ya track na akaanza kuchezea bunduki yangu lakini ilikuwa iko tayari kwa vita muda mrefu sana, aliikalia kwa juu na alikuwa anaendesha gari taratibu na kwa umakini mkubwa sana na baadae tuliamua kuhamia chumbani kuendeleza match yetu pale kitandani.

Iryn ni mwanamke ambaye alikuwa hanipi limit hasa linapokuja suala la sex, nikipata hamu hata awe jikoni, seblen bhasi nitam-f*ck hana noma, na hiki kilinifanya nivutiwe naye na nimpende sana. Akiwa jikoni anapika nikiingiza mkono nikamshika kalio na hata kuliminya ndo kwanza alikuwa anafurahi, nikimkuta seblen nitafungua braa yake nitazinyonya boobs zake ndo kwanza ananipa ushirikiano, sasa kafanye huu ujinga kwa mama J kama hupigwi na mwiko huko jikoni.
•••••
Asubuhi niliamka mapema sana na nikaenda gym kupiga tizi, kwenye hizi apartments kuna room special ya mazoezi kwa wapangaji wa pale. Baada ya kutoka tizi niliingia bafuni kuoga na nikatengeza breakfast nikanywa lakini mama kijacho alikuwa bado kalala na mimi nikaondoka kwenda kazini.

Nilianza na Mikocheni kwanza na baada ya kuwasili nilikwenda ofisini kuanza kuzipitia ripoti zote za utendaji mpaka mauzo. Baada ya nusu saa Lucy aliingia ofisini na alikuwa anafika muda huu na baada ya kuniona tulisalimiana pale na alionesha kuwa na umbeya anataka kunipa,

LUCY: “Insider mambo, Iryn ni mjamzito?”

MIMI: “Sijui nianze kujibu salamu kwanza au swali?”

LUCY: “Salamu not important kwasasa, twende kwenye swali.”

MIMI: “Mimi sijui kwakweli ndo nasikia kwako hapa ila namuona sawa tu.”

LUCY: “Jana nimeona utofauti mkubwa sana kwake, alikuwa anatema sana mate hovyo na sio kawaida yake mpaka nikahisi ni mjamzito.”

MIMI: “Labda alikuwa anaumwa rafiki yangu au kuna kitu kilikuwa kimemchefua huwezi kujua, kutema mate hovyo sio kigezo cha mtu kuwa na mimba.”

LUCY: “Mh! Insider wewe ni msiri sana kama umemjaza si unasema tu mshikaji wangu utaendelea kunificha mpaka lini?”

MIMI: “Siwezi kukuficha kwa hili maana mimba haifichiki kama mahusiano itajitokeza tu, mimi naondoka kila kitu kipo sawa, labda kama kuna jambo lolote niambie kabla sijapotea.”

LUCY: “No.”

Niliondoka kwenda Masaki na wakati naendelea na majukumu yangu kwa upande mwingine simu yangu ilianza kuita na alikuwa ni Iryn akipiga na nilipokea simu yake kwa haraka sana.

Mama kijacho alikuwa analalamika nimeondoka bila kumuaga na akaniomba niwahi kurudi kwani ameni- miss. Kwa upande wangu sikutaka kuchanganya mapenzi na kazi hata kama natembea na bossy niliona suala la kazi lazima niliheshimu.

Mchana niliaga kwa Asmah naondoka na wakati natoka tulikuwa tumeongozana huku tunaongea,

ASMAH: “Insider unabahati kubwa sana wewe mwanaume kuwa na mwanamke mzuri na mrembo hata mimi nakuonea wivu.”

MIMI: “Umejuaje kama ananipenda?.”

ASMAH: “Anaonekana tu amekupenda serious, utulie sasa kama una mambo pembeni acha.”

MIMI: “Ahsante kwa ushauri wako mama.”

Niliamua kuondoka na nikarudi home maana Iryn alikuwa ananipigia sana simu mpaka kero na kama kudeka kuliongezeka.

Baada ya kufika home nilimkuta amelala seblen na alivyoniona alitabasamu na akanambia amepika tayari, hivyo alikuwa akinisubiri mimi tu ile tule.

Tulishinda wote mle ndani na ule usiku alinambia jumamosi tutakwenda makazi mapya na amepata apartment tayari ya kukaa kwa huu muda.

Dalali aliyetafuta hii apartment ni ile kampuni inayosimamia nyumba za Masaki katika upangishaji. Kwa upande mwingine alisema tukiondoka hapa ndo mazima na itabidi tukabidhi kabisa apartment ya watu japo alikuwa kabakisha mwezi mmoja.

*****
Jumamosi ndo tulikuwa tunaondoka Kwenye ile apartment ya Kawe na ile asubuhi tulianza kupanga vitu, Iryn kwa upande wake alikuwa hahitaji kuchukua kitu chochote zaidi ya nguo. Kuna vitu vingi pale nilivichukua vya muhimu kama JBL music soundbar, washing machine nknk, na kuna baadhi ya vitu tulimpa mama mlinzi.

Mchana tuliondoka pale na tulianza safari ya kwenda Masaki maana Dalali alikuwa ametuma location na anatusubiri. Apartment ilikuwa Toure road karibu na Golden Tulip hotel, baada ya kuwasili pale tulionana na Dalali, akatupeleka mpaka juu floor ya 3, niseme apartment ilikuwa ni nzuri sana, inavutia, na mazingira yalikuwa mazuri sana ndani mpaka nje, ni 5 star apartment na zilimtoka pesa mingi the bossy lady.

Baada ya kumalizana na Dalali tuliagana na akaondoka akatuacha sisi tumekaa seblen, apartment ilikuwa ni full furnished yaani inakila kitu ndani ni wewe kwenda na nguo zako tu na vitu vya jikoni.

IRYN: “Baby badae tunakwenda wapi nahamu tutoke out.”

MIMI: “Twende Maison club leo maana sijawahi kuingia pale, nilikuwa naishia kuwapeleka wateja tu.”

IRYN: “Okay baby tutaenda huko.”

MIMI: “Unakumbuka hutakiwi kunywa?”

IRYN: “Nitakunywa mocktail.”

Sababu huwa sipendi Iryn asumbuliwe kutokana na status yake ilibidi nifungue page yao ya Instagram na nikafanya booking ya table mapema kabisa.

Saa 2 usiku tulitoka kwenda kupata dinna na kwa upande wa Iryn alikuwa kapendeza sana na niliishia kumsifia njiani kote mpaka tunafika Karambezi cafe. Baada ya kuwasili pale restaurant mhudumu hakuchelewa kuja kutusikiliza na tukaagiza chakula na tukaendelea kupiga story pale huku tukisubiri food.

MIMI: “Baby ukienda South Africa utakuwa unakaa home?”

IRYN: “Nitakaa kwanza home then nitahamia kwenye apartment yangu.”

MIMI: “Kwanini usikae home na hio mimba?”

IRYN: “Kuna mdogo wangu mtoto wa mamkubwa nimemtafutia chuo South Africa so nitaishi naye pamoja, usiwe na wasiwasi baby mwanao atakuwa sawa na salama.”

MIMI: “Mamdogo hana shida? Si unajua mama wa kambo?”

IRYN: “Hana shida kabisa na ananipenda sana hata nilivyo hairisha safari amechukia sana.”

MIMI: “Natamani ningekupa hii Dunia kama zawadi pamoja na vitu vyake vyote lakini sina huu uwezo.”

IRYN: “Baby no need uliyoyafanya kwangu yanatosha, kwasasa ni zamu yangu kukupa hii Dunia. Insider wewe ndo mwanaume pekee uliyenifanya mimi kuwa na furaha, kifo cha mama yangu kilinipa mawazo sana mpaka nilijukuta namchukia daddy but today I’m happy because of you.”

MIMI: “Mimi naamini Mungu alikurudisha Tanzania kwaajili yangu na mimi nakuahidi sitokuwa na mchepuko mwingine zaidi yako na ninahapa hapa mbele yako.”

IRYN: “Insider mimi nimekupenda toka moyoni na nimeridhia kuwa mke wako wa pili kama utanipa hii nafasi.”

MIMI: “Dini yangu hairuhusu mimi kuwa na wake wawili lakini kuwa na mtoto wangu nmekupa hiko cheo.”

IRYN: “Thank you baby please tell me unataka nikufanyie kitu gani kama shukrani yangu kwako? Please tell me.”

MIMI: “Baby zawadi ya mtoto uliyonipa kwangu mimi inatosha ila nakuomba uniahidi uyo mtoto utamtunza maana utakuwa mbali na mimi.”

IRYN: “Mtoto wako nitamtunza baby ondoa wasiwasi, najua utakuwa unamiss sana ila nitakuwa nakuja Dar kwaajili yako each after 2 weeks. Tutakuwa tunashinda wote hotelini weekend nzima, but nihakikishie tutakuwa tunashinda pamoja.“

Baada ya kusikia haya maneno nilifurahi sana maana nilianza kuwaza Iryn anaondoka, coochie yake sitaiona tena na uwezo wa kwenda South mara kwa mara sina.

MIMI: “Really baby? utakuwa unakuja kwaajili yangu?”

IRYN: “I promise, baby naomba utafute passport ili nawewe uwe unakuja South Africa nataka pia twende Dubai, Paris, UK, na Netherlands nknk huko kote kuna ndugu zangu.”

MIMI: “Sawa baby hili nitalifanyia kazi soon.”

Tuliongea mambo mengi sana na Iryn na muda ulikuwa umekwenda sana, kwani saa 4 ilitugongea palepale Karambezi na tukaondoka kwenda Maison Club. Kilichofanyika ni kubadili parking tu maana Maison imepakana na Seacliff Hotel ni building zilizofuatana.

Tuliingia Maison club na tulipelekwa kwenye table yetu na mhudumu na muda huu alikuwa akisikikiza odda zetu ili atuletee vinywaji. Sababu Iryn alikuwa hanywi ilibidi aagize Mocktail na mimi Niliagiza cocktails na nilikuwa nakimbiza na shots za Tequila.

Kwa upande mwingine walikuwa wanaonekana warembo wakali sana na watu waliokuwa wanaonekana wengi ni madon. Maison huwezi kuwapata wazamiaji kwani kuingia tu lazima ufanye booking au uwe na status, huwezi kuwakuta maskini huku.

Tulidance pamoja sana huu usiku ni kama ilikuwa napewa farewell ya mwisho mwisho, kutokana na uzuri wake mama kijacho wangu aliishiwa kupigwa macho sana, na hili mimi nilikuwa nishazoea tayari na nilikuwa najiona mwamba sana kuwa na moja ya mwanamke mrembo hapa Duniani. Sisi hatukujali na tuliendelea kupeana mahaba motomoto na tulikaa mpaka saa 8 za usiku wakati mziki umeanza kukolea ndo tukaondoka kwenda kulala.

Asubuhi niliamshwa kunywa soup na alikuwa kaniandalia na viazi, baada ya kunywa nilikuwa bado na hangovers maana zilikimbiza sana shots za tequila kule Maison, hivyo nilirudi kulala tena, haikuchukua muda na yeye alikuja tukalala wote.

Mchana tulitoka kwenda kupata lunch kwenye mgahawa wa karibu na wakati tuko kwa restaurant tukipata chakula, Iryn alinambia tukirudi home kuna surprise yangu inanisubiri na mimi nilibaki najiuliza ni surprise gani tena hii?

“Baby unataka kuni surprise nini?”

“Wewe utaona hapohapo.”

Baada ya kumaliza kula tuliondoka kurudi kwenye apartment yetu na tuliingia bafuni kuoga pamoja na baada ya kumaliza alinifuta maji na taulo mwizi mzima.

IRYN: “Baby lala kitandani nataka leo nikufanyie massage utoe na uchovu.”

MIMI: “Hii leo kweli surprise nasubiri huduma yako mummy.”

Kwa upande wake alikuwa kavaa tight fupi nyeupe na sport braa nyeupe hivyo alikuwa anaonekana romantic na sex sana.

Baada ya kulala kitandani alitoa vifaa special kwaajili ya massage, na alitoa kitambaa cheupe kipya kabisa akaenda bafuni na akatoka amekilowanisha maji na akakitumbukiza kwenye heater special.

IRYN: “Baby kabla ya kufanya massage unatakiwa kukanda mwili wako kwa maji ya moto, sasa hiki kifaa ndo kazi yake hii. Si unaona nilikilowanisha na maji? Na hii heater ni special kwa kupashia joto, na hiki kitambaa ni special kwa massage na kinatunza joto kwa muda mrefu na huwa naviagiza nje.”

Baada ya dakika 3 kilikuwa tayari na alianza kunikanda kuanzia shingoni mpaka miguuni na nilikuwa nimelala chali, muda huu nilikuwa nasikia raha sana.

IRYN: “Nimeona tuanze na front side then tumalizie na back, na mara nyingi huwa napenda kufanya hivi kwa strangers.”

MIMI: “Kwanini baby?”

IRYN: “Ni hivi, upande wa mbele huwa unasisimua sana hasa kwa wanaume na hapa wengi huwa wanapata mawazo ya ngono, ukianza na mbele atapata hizi hisia na ukimalizia upande wa nyuma hisia zinakuwa chini sana. Hii ni mbinu nzuri sana kama unadeal na customers/strangers ambao huwafahamu, itakusaidia kupunguza kusumbuliwa kuombwa sex. Kwa wazungu hawana shida lakini tatizo ni waafrica na wengi wanachukulia massage ni kama sehemu ya kupata sex na sio huduma.”

MIMI: “Aisee kumbe wazungu sio wasumbufu kama waafrica.”

IRYN: “Wazungu wanaheshimu utu na anavyokuja lengo ni huduma na sio ngono, na wanaheshimu hii kazi ila waafrica wanaona kama kujiuza unavyofanya hii kazi.”

MIMI: “Ni kweli kabisa unayosema mummy.”

IRYN: “Mimi nafanya professional massage hata hivi vifaa nilivyonavyo sidhani kama kuna massage hapa bongo wanavyo labda hizi 5 star hotel na ni expensive sana.”

Na muda huu alitoa stones nyeusi na akaziweka kwa heater na akaendelea kuongea,

“Inatakiwa mteja asiwaze ngono anavyokuwa kwenye room, ki professional inatakiwa umtoe customer kwenye mawazo ya ngono na aone massage ni treatment na sio sehemu ya kupata ngono.”

MIMI: “Baby kivipi?”

IRYN: “Ni simple tu naweza kutumia natural au artificial way, wewe utaona si tupo wote hapa?”

Iryn alitoa kitu kama mask na ilikuwa inafunika macho tu na alitoa airpods zake akaziweka masikioni na akanivalisha ile mask, na akaplay music wa taratibu kama ile ya wataliano.

Muda huu alinza kunifanyia massage taratibu na kwa ufundi wa hali ya juu sana afu ukizingatia mikono yake ni laini afu ya moto. Nilikuwa nasikia raha sana hata mawazo ya ngono nilikuwa sina, ile mask aliyokuwa kanivalisha na ule mziki niliokuwa nausikia nilikuwa nahisi niko Dunia nyingine kabisa.

Niligeuka upande wa nyuma na alianza kuukanda mgongo kwanza kwa kitambaa cha moto then akaanza massage taratibu. Baadae alitoa zile stone kwa heater na akaziweka mgongoni kwa ufundi wa hali ya juu sana kwenye mti wa mgongo, raha nilizokuwa nasikia hapa ni balaa maana nilikuwa sayari nyingine kabisa.

Hakuishia hapa alitoa kifaa kama gun akawa anakipitisha mgongoni na alisema ni special kwa kunyoosha misuli, kuna muda alitoa kifaa kingine na kilikuwa kama kinanikanda mgongo na alisema kile ni special kwa kunyoosha mifupa ya uti wa mgongo.

Ni massage iliyotumia kama lisaa na nusu na baada ya kumaliza niliona utofauti mkubwa sana maana nilikuwa naona mwili umekuwa mwepesi sana ni kama nimeshusha mzigo vile.

MIMI: “Baby nasikia utofauti mkubwa sana kwenye mwili wangu.”

IRYN: “Umewaza ngono? maana nimechezea sana bunduki yako.”

MIMI: “Hamna mummy nilikuwa nafeel unaichezea lakini sikuwa nawaza ngono kabisa.”

IRYN: “Kama nilivyokwambia massage ni treatment na sio sehemu ya kupatia ngono, ila kwa hapa bongo mmezifanya kama sehemu za kupatia ngono hakuna massage mnazofanyiwa.

MIMI: “Kwa hii massage uliyonifanyia nimeamini wewe ni mtaalamu.”

IRYN: “Na vifaa vingi sana humu ndani, utazidi kuviona taratibu tukiendelea kufanya aina nyingine za massage.”

MIMI: “Baby na body to body massage inakuaje?”

IRYN: “Hiyo nitakufanyia siku nyingine japo mimi nilikuwa napenda sana kuitoa hii huduma kwa wanawake.”

MIMI: “Baby na hiyo chupa ya mafuta ni aina gani maana naona niko sawa sina mimafuta.”

IRYN: “Haya ni special for massage na ukimaliza yanakauka yenyewe kwa haraka sana”

MIMI: “Baby njoo na mimi nakufanyie massage.”

IRYN: “Mhhh really?.”

Nilimvua nguo zote na nikaanza kumfanyia massage upande wa mbele na alikuwa ananielekeza kila hatua na nikawa namfanyia kupanda juu kushuka chini, usawa wa matiti yake na baadae nilimgeuza upande wa nyuma nikaendelea kumfanyia massage. Lakini wakati nachezea makalio yake nilikosa uvumilivu na nilijukuta zoezi linabadilika na tukaanza kusex maana nilichomeka mashine kwa nyuma wakati yeye akiwa kalala kifudifudi.

Massage niliyopewa na Iryn ilikuwa ni best mpaka nikajisemea kwanini napata hizi raha mwishoni?.
(Nilifanyiwa kwanza massage na maelezo alinipa baadae maana wakati nafanyiwa massage nilikuwa Sayari nyingine.)

Jioni tulikubalina tukale dinna capetown na wakati tunakwenda tulipitia pale Salon kuwapa hi na sisi tukaendelea na safari yetu. Muda tunaopata diner pale Capetown Iryn alinambia next week before hajaondoka itabidi akae pamoja na timu yote ya Masaki na Mikocheni ili awaage na pia mama Janeth atakuwa karudi kwani alikwenda Ukraine kikazi.

Baada ya kupata dinner tuliendelea kukaa pale kwa muda mrefu, kwa Jumapili panakuwaga pazuri sana pale Capetown. Tuliendelea kukaa pale mpaka saa 4 usiku ndo tukaondoka kurudi kulala.

*****
Jumatatu mchana niliondoka na Asmah kwenda Mikocheni kuonana na Lucy ili tujadiliane suala la kikao kabla ya kutoa taarifa kwa team.

Tulikutana Golden fork ili tupate na lunch na baada ya kuwasili pale tulimkuta Lucy amefika akitusubiri mimi na Asmah. Tuliagiza chakula na mazungumzo yalikuwa yanaendelea, kwa upande mwingine Iryn alikuwa anataka kikao kianze mapema ili tupate lunch na dinner ya pamoja na baada ya hapo tungeenda kumalizia kiwanja chochote tutakacho kipenda.

Tulikubaliana pale tufanyie kikao chetu Serena Hotel na tukampa kazi Asmah ya kuanza kufuatilia ukumbi mapema na kuhusu kumalizia tuliona SamakiSamaki ingekua ndo sehemu nzuri, kiwanja pendwa.

Baada ya kumaliza maongezi mimi na Asmah tuliondoka kurudi Masaki lakini kwa upande wangu baada ya kumuacha Asmah niliamua kurudi nikakae na Iryn. Kipindi hiki nilikuwa sitamani kabisa kukaa mbali naye nilikuwa natamani muda wote tuwe wote, na njiani nilikuwa nimemchukulia pizza kwaajili ya lunch.

Baada ya kurudi nilimkuta Claire seblen na sikutegemea kama ningemkuta pale na tuliishia kusalimiana,

MIMI: “Ooh Claire za wewe sikutegemea kukuona hapa imekuwa surprise.”

CLAIRE: “Actually nimerudi jana nilikuwa Bukoba huko.”

MIMI: “Baby alinambia aisee, pole sana na za huko lakini kwa ujumla.”

CLAIRE: “Nilienda salimia ndugu zangu na kudhuru kabuli la baba.”

MIMI: “Ulifanya jambo jema shem wangu na mke wangu yuko wapi?”

Na muda huu Iryn alikuwa amekuja seblen akitokea jikoni,

IRYN: “Niko jikoni napika baby.”

MIMI: “Nilikuwa nimekuletea pizza mummy kumbe upo jikoni.”

IRYN: “Thanks hii nitaila badae.”

Tulishinda na Claire pale mpaka usiku na tukamsindikiza mpaka Marina na sisi tukarudi home kulala.

Wiki hii tuliendelea kuweka mambo sawa kuhusu kikao chetu na ile jumatano Asmah alikuwa kafanikisha suala la kufanya booking kwaajili ya kufanyia kikao chetu cha mwisho na Bossy lady.

Kwa upande mwingine Iryn dalili zake za mimba zilizidi kuonekana day after day na alianza kutapika na kupenda kula vitu vichachu vichachu na upendo wake kwangu ulizidi kuongezeka kwa kasi sana.

Siku ya alhamisi mama J alinipa taarifa kuwa jumamosi watarudi Dar lakini hatorudi home, dada wa kazi bado anawasalimia ndugu zake na kuna sintofahamu inaendelea kule kwao kuhusu dada, kwani hawataki arudi tena Dar.

Kwa upande wangu hizi taarifa zilinishtua pia,

MIMI: “Dada Junior asiporudi inakuwaje? kupata mtu kama yeye itatuchukua muda sana na hiki ni kipindi kibaya sana ukizingatia bado week urudi chuo.”

WIFE: “Mwenyewe nimechanganyikiwa hapa, baba yake alimtelekeza kuhusu shule ila sasa anasema anataka kumrudisha shule, dada anasema mzee wake ni muongo hana imani naye.”

MIMI: “Alright fanya hivi, ongea na familia yake hasa mamdogo wake na mwambie watuachie kwa mwezi mmoja huku tunatafuta dada mwingine, kwasasa tulikuwa hatuja jipanga na december atarudi.”

WIFE: “Shida ni Mzee wake anasema hataki kuona bint yake anarudi Dar tena na kama atafanya hivyo atatoa taarifa Police.”

MIMI: “Ongea kama nilivyokwambia maana kwasasa hakuna shule labda mwakani, omba wakusaidie kwa hili afu dada tutakaa naye chini tuone tunamsaidiaje, uyo Mzee wake nahisi kapatwa na wivu tu.”

WIFE: “Sawa nitakupa mrejesho.”

Siku ya Ijumaa mama Janeth aliwasili Tanzania na kubwa alikuwa karudi na binti yake Janeth, Iryn alisema twende tukamsalimie pale kwake na pia mama Janeth aliomba waonane akirudi. Kwa upande wangu nilikuwa nashauku kubwa sana ya kumuona live Janeth maana nilikuwa najua anasoma chuo huko Ulaya na nilikuwa naishia kuziona picha zake tu.

Saa 1 usiku tuliondoka kwenda kwa mama Janeth na tuliweza kupokelewa na Janeth pale seblen na waliishia kukumbatiana na Iryn kwa furaha sana na walionekana kumisiana.

Iryn alifanya utambulisho pale kwa lugha ya kiingereza,

“Insider huyu ndo Janeth mwenyewe mtoto wa kwanza wa mama na alinitambulisha mimi kwa Janeth kama Manager wa kampuni yao na mama yake.”

Janeth ni mzungu kama mama yake ni kazuri kwakweli na baada ya ule utambulisho tulisalimiana kidogo na waliendelea kuongea na Iryn. Niligundua Janeth kaja kumsalimia mama yake na hatokaa sana ataondoka kurudi Ulaya kuendelea na masomo.

Ndani ya dakika 10 mama Janeth alitoka ndani na alikuja pale seblen na tulianza maongezi pale na tulikuwa tunajadiliana masuala ya kampuni. Tulikubaliana suala la Finance liwe chini yangu lakini Iryn atakuwa kama mshauri bado, kwa upande wake Iryn alisema ataendelea kutoa ushirikiano na hakuna kitakacho haribika.

IRYN: “Mama I trust Insider nina imani naye sana naamini nakuachia mtu sahihi kwako na hakuna kitakacho haribika. Toka tumpe majukumu mapya kampuni inafanya vizuri sana hata ukiwa haupo atafanya vizuri, kwenye masuala mengine tutakuwa tunawasiliana na still report nitakuwa nazipitia.”

MAMA: “Unajua ratiba niliyopewa nitakuwa ninashinda sana Ukraine kwaajili ya masuala ya kazi nilifikiri tumuongezee mtu mmoja Insider kwa masuala ya HR.”

MIMI: “Mama no need wafanyakazi waliopo wanatosha, Hilda yuko vizuri sana, Asmah yuko vizuri kwa kule Mikocheni Lucy yuko vizuri sana. Hapa naona masuala ya HR tutakuwa tunasaidiana wote na kama kuna ushauri nitakuwa nawasiliana na wewe kupitia email.”

IRYN: “Sumaiya yuko kule kwenye kampuni ya usafi sina shida naye kwenye suala la kazi na kesho nafikiri tuwe naye kwenye kikao.”

MAMA: “Sumaya yuko vizuri na tumepata tenda 2 kubwa na ikiwemo serikalini.”

IRYN: “Mama kesho baada ya kikao cha wote nafikiri tukae na viongozi tujadiliane.”

MAMA: “Insider umemuona binti yangu Janeth?.”

MIMI: “Mama nimemuona ni mzuri sana akimaliza chuo nitamuoa kama utanipa ridhaa.”

Mama Janeth alicheka maana hakutegemea mimi kuongea vile,

MAMA: “Hili ondoa shaka mimi nitakupa.”

Muda huu Janeth alikuwa hajui nacho ongea na mama yake maana Kiswahili anajua baadhi ya maneno kama salamu. Tulikaa kwa mama Janeth mpaka saa 4 usiku ndo tukaaga pale tukaondoka.

Saa 6 usiku Iryn alianza kulalamika anajisikia vibaya na alianza kutapika kwa kasi sana nonstop na alianza kulegea kama mtu mwenye homa. Kadri muda unavyozidi kwenda alizidi kubadilika, ilibidi tuondoke twende hospital na nilimpeleka pale SALI hospital, kwa upande wangu nilianza kuchanganyikiwa maana mpaka namshusha pale hospital hata kuongea alikuwa anazungumza kwa shida.

Niliwaza kumpigia simu mama Janeth lakini Roho ikasita maana angeweza kujua Iryn ni mjamzito na Iryn alisema ile mimba hakuna anayejua zaidi yangu tu. Muda huu mimi nilikuwa na wasiwasi sana kuhusu mimba maana niliwaza inaweza isije kuwa imeharibika, na nilijisemea kama itaharibika na hii basi mimi nitakuwa moja ya wanaume wenye mkosi hapa Duniani.

Nilikaa kwenye bench nikimsubiri na baadae niliruhusiwa kuingia ndani ili niwe naye karibu maana niliwaambia yule ni mke wangu. Nilimuuliza Doctor kuhusu mimba na alisema hana shida mimba iko salama ila ni homa ya kawaida kwani anapitia mabadiliko ukizingatia ile ni mimba yake ya kwanza.

Saa 10 usiku nilitoka pale hospital na nilirudi home ili kuandaa soup kwa upande mwingine nesi alinambia atakuwa anamuangalia hivyo nikamtengenezee haraka kitu cha kula, kwani alitapika sana.

Baada ya kurudi kwa apartment nilitengeneza soup ya kuku vizuri na nilitumia kama lisaa pale na nikarudi tena hospital na nilimkuta nesi yuko room. Niliingia na soup ikiwa kwa pot na muda huu Iryn alikuwa yuko macho akiniangalia na mimi nilimsogelea nikawa karibu yake.

MIMI: “Hi baby how are you feeling now.”

IRYN: “I’m fine baby, I’m feeling much better, thank you.”

MIMI: “Don’t say that baby uhai wako ni priority yangu ya kwanza.” Na nikamkiss mdomoni.

Muda huu Nurse dizaini kama alikuwa ananionea wivu nikimbembeleza mama kijacho wangu na yeye alikuwa akitabasamu.

“Baby nimekuletea soup unywe before haijapoa jana ulitapika sana.”

Nurse alinisaidia kumimina soup kwenye kibakuli na nilisubiri ipoe kidogo na nikaanza kumnywesha pale taratibu huku nambembeleza kwa maneno matamu na alikunywa soup yote akamaliza na nikampongeza.

NURSE: “Kwa hii spidi nafikiri asubuhi mtaruhusiwa kuondoka naona amerecover vizuri, Doctor akija atarecommend.”

MIMI: “Ahsante Nurse kwa kumsaidia mke wangu .”

NURSE: “Usijali ndo kazi yetu hii.”

Saa 3 asubuhi tuliruhusiwa kuondoka maana Iryn hali yake ilikuwa sawa na tulipewa dawa pale tukaondoka, kwa upande mwingine Asmah alikuwa ameanza kunipigia simu na alinipa taarifa yuko hotelini tayari anaangalia kama mambo yamekwenda sawa.

Kwa upande wangu nilikuwa nina wasiwasi sana na Iryn kuhusu Afya yake na niliogopa asije kuumwa tena huko hotelini kwenye kikao, lakini kwa upande wake alisema yuko sawa na nisiwe na wasiwasi.


PART III

Baada ya kurudi home nilimwambia Iryn apumzike kidogo na mimi nilikwenda jikoni kumtengenezea juice ya nanasi. Baada ya kunywa juice alikwenda kulala chumbani na mimi nilianza kufanya usafi washroom alikokuwa ametapikia.

Baada ya lisaa nilimuamsha ili ajiandae kwaajili ya kwenda kwa kikao na baada ya kujiandaa tuliondoka pale home, lakini ilibidi tumpitie mama Janeth maana aliomba kampani ya usafiri ya kwenda Serena.

Baada ya kumpitia mama Janeth pale kwake, alikuwa yuko tayari na tukaondoka kwenda eneo la tukio na tulitumia muda mfupi kuwasili hotelin. Tulikuta wafanyakazi wote walikuwa wamewasili tayari na baada ya sisi kufika tuliona tupate kwanza lunch mambo mengine yaendelee.

Baada ya kupata lunch kikao kilianza 14:30 na mimi ndo niliyeanza kwa kukifungua kwa sara fupi na nikatoa maelezo mafupi kuhusu lengo la kikao cha leo ni kumuaga Bossy wetu Iryn, wengi walikuwa hawajui hivyo hizi taarifa ziliwashtua sana. Na mimi sikutaka kupoteza muda hivyo nilimkaribisha Iryn aongee na alizungumza mambo mengi sana kwa team yake,

“Guys naona mmeanza kuwa na wasiwasi baada ya kupata taarifa za mimi kuondoka lakini naenda kufanya jambo la muhimu zaidi na lenye faida kwa kampuni yetu. Nakwenda kusoma masters South Africa sitakuwa na nyinyi physically lakini nitakuwa napata ripoti zenu, hakuna kitakacho haribika naamini Insider yupo na atawaongoza vizuri, kwangu mimi sina shida naye. Nawaahidi nitakuwa nakuja kuwatembelea na wale ambao watakuwa wana perform vizuri nitakuwa na bring zawadi kwa ajili yao.”

Baada ya Iryn kumaliza kuongea nilimkaribisha mama Janeth na yeye azungumze kidogo na alizungumza mambo mengi kuhusu utendaji wa kampuni na baada ya kumaliza nilikaribisha maoni, maswali, ushauri na mapendekezo.

Tulipokea mapendekezo na maoni mengi sana kutoka kwa wafanyakazi na mimi nilikuwa ninayaandika kwa notebook ili kuyafanyia kazi na kila mtu aliweza kuongea hii siku.

Baada ya kumaliza mama Janeth alianza kuongea tena na kubwa alisema atakuja mtalamu wa masuala ya Salon na atatoa mafunzo kwa baadhi ya wafanyakazi kwa muda wa week moja na anatoka Ulaya. Mama Janeth alisema hawezi kuwafundisha wote sababu ya gharama hivyo anahitaji watu wa tano tu wa kuanza nao na hawa ndo wataongeza ujuzi kwa wengine.

Mama Janeth alisema tupendekeze majina matano matatu (3) kwa Masaki na mawili (2) kwa Mikocheni. Mama alinambia nipendekeze majina mawili moja kwa Masaki na lingine kwa Mikocheni afu yanayobaki watapiga kura wenyewe.

Kwa upande wangu nilipendekeza Hilda kwa Masaki na kwa Mikocheni nilimpendekeza Julieth maana Lucy alikuwa anarudi shule hivyo sikuona sababu ya kumpendekeza. Baada ya kupendekeza watu wangu waliobaki zilipigwa kura na washindi wakajulikana, kwa Masaki alikuwepo Rebby.

Mpaka tunamaliza kikao ilikuwa ni saa 11 jioni hivyo tulitoka kupumzika pamoja na kupiga picha za pamoja. Mama Janeth alikuwa katembea na Camera yake na tuliomba mtu pale hotelini atupige picha za pamoja pale ukumbini na zingine nyingi tulipigia nje ya hotel kama ukumbusho. (Ukienda Salon ya Masaki utaikuta hii picha pale Reception).

Muda huu kila mtu alikuwa anapiga picha na Iryn mpaka Sumaiya naye hakuwa mbali kupiga picha na Bossy lady.

Saa 1 usiku tulipata dinner ya pamoja tena palepale hotelini na wakati tunakula nilitoa taarifa ya kukutana Samakisamaki baada ya dinner ili tukamalizie usiku wetu pale. Baada ya kutoa hii taarifa niliona sura za watu zikitabasamu na niliwaambia tukutane kuanzia saa 2 usiku maeneo yale na nimefanya booking ya meza za kukaa.

Baada ya dinner Iryn alitoa bahasha ndogo kwenye mkoba wake na nilimpa Asmah azigawe kwa kila mtu na Iryn alisema zile ni zawadi zake kwa kila mtu. Iryn alitoa neno la mwisho la kutuaga pale na kubwa alisisitiza uchapakaji kazi kwa bidii na ushirikiano.

“Guys mimi nawashukuru sana kwa siku ya leo niseme nime enjoy sana kuwa na nyinyi siku ya leo na niwaombe muendelee kufanya kazi kwa bidii na ushirikiano. Namba yangu mnayo kama unashida personal usiogope kunitafuta ili tusaidiane you know I love you guys, ninawaahidi nitakuwa narudi kuwasalimia. Hizo bahasha ni zawadi yangu kwenu na niwatakie usiku mwema lakini msisahu tutakutana pale Samakisamaki, nataka kila mtu anywe anachotaka, msikose.”

Baada ya kuondoka sisi viongozi tulibaki kwaajili ya mazungumzo ili kuweka mikakati ya pamoja kuhusu kampuni ikiwemo kupeana majukumu mapya, pia mama Janeth alipendekeza mishahara iongezwe kidogo ili kufidia.

Kwa upande wa Salon hakukuwa na mambo mengi sana lakini kwa upande wa Usafi Sumaiya aliomba aongezewe mtu mmoja ili kuongeza nguvu. Mimi nilishauri tutafute mtu ambaye ana elimu ya Fedha au Uchumi ili wasaidiane kwenye masuala mbalimbali ya tender, miradi nknk. Na hii nafasi nilimuunganisha jamaa yangu, mpaka sasa anaendelea na majukumu yake pamoja na Sumaiya.

Ni kikao kifupi kilicho chukua kama nusu saa na baada ya kumaliza tuliagana pale na Mama Janeth alisema atakuja Samakisamaki kutupa kampani. Wakati tunatoka mimi nilibaki na Asmah na Hilda mle ukumbini na tukawa tunaongea pale na kubwa niliwapa pongezi kwa kusimamia kikao kwenda vizuri.

MIMI: “Asmah nafikiri mkajiandae ili tukutane Samaki, Hilda utawahi kweli mpaka Kigamboni?”

ASMAH: “Asmah nakaa naye pamoja kwa kipindi hiki.”

MIMI: “Ooh sawa sikujua hili.”

Nilishangaa sana kuona Asmah na Hilda wamekuwa mabest kwa muda mfupi sana, nilimvuta Asmah pembeni na tukaendelea na mazungumzo.

MIMI: “Nambie pesa iliyobaki ni kiasi gani?”

ASMAH: “Nina kama milioni moja na laki mbili something.”

MIMI: “Kazi iliyofanyika ni kubwa na mmenikosha sana hiyo pesa tutagawana wanne ila wewe na Hilda utachukua parcent kubwa.”

ASMAH: “Poa Insider but….”

MIMI: “But what.?” Ilibidi nigeuke kumsikiliza maana nilikuwa nishaanza kuondoka pale.

ASMAH: “You look great today, wahi bhana Iryn anakusubiri.”

MIMI: “Sawa bhana nashukuru pia.”

Baada ya kutoka niliwakuta Iryn na Sumaiya wanaongea wanacheka pale reception utafikiri sio wale watu ambao hawapatani. Na mimi ilibidi nishangae kwakweli maana sikutegemea kuona kuna siku Iryn na Sumaiya watakuwa wanacheka pamoja namna hii.

Baada ya kusogea pale karibu, Sumaiya alianza kuongea,

SUMAIYA: “Insider leo mimi na Iryn ugomvi hatuna.”

MIMI: “Kwani mlikuwa na ugomvi? Mbona hili sijawai kulijua.”

SUMAIYA: “Leo kafunguka ukweli kuwa mpo kwenye mahusiano na hapa ndo tulikuwa tunagombana kuleta ubossy wake kwenye mapenzi. Kwakua leo kanifungukia ukweli kuwa anakupenda niseme leo nabariki mapenzi yenu kwa moyo mweupe kabisa na sina kinyongo.”

IRYN: “Thank you mamaa.”

SUMAIYA: “Nataka kuona unamzalia Insider mtoto, tule na wali kabisa. Namuheshimu sana Insider kwa hizi taarifa ulizonipa, heshima yangu kwako itaongezeka.”

Nilishangaa pale hivi ndo huyu Sumaiya naye mjua mimi? Kwa Upande mwingine alikuwa kashika macho 3 nikasema huyu atakuwa kapewa simu, haiwezekani Sumaiya kuturn kwa haraka hivi, na mimi ilibidi nipoteze hii mada,

MIMI: “Baby mama Janeth yuko wapi?”

IRYN: “Katangulia kwenye gari tuondoke.”

Tuliagana na Sumaiya pale maana uber ilikuwa imemfuata tayari na sisi tukaelekea Parking tuliko park gari tukaondoka. Tulianza kumdrop mama Janeth pale kwake na akasema haina haja ya kuja kumfuata na atakuja mwenyewe pale Samakisamaki na sisi tukarudi kwenye apartment yetu.

Baada ya kuwasili pale nilikuwa naona Iryn kama hayuko sawa hivi maana alikuwa anaonekana kuwa mchovu sana,

“Baby are you ok?”

“Yeah niko poa baba mtoto I’m just tired.”

“Pole sana tuna 1 hour ya kupumzika tutakwenda saa 3 pale au kama vipi wewe lala tu.”

“Baby today’s my day I have to go.”

Saa 3 usiku tuliondoka kwenda maeneo na kwa upande mwingine team ilikuwa imewasili muda mrefu na mimi nilikuwa nimewapa taarifa kwenye group waagize wanachotaka kunywa.

Iryn alitoa offer kila mtu aagize kinywaji anacho jisikia kunywa usiku huu ila yeye kwa upande wake aliishia kuagiza Mocktail. Wapo waliagiza moet, Jameson na Hennessy yaani iikuwa ni burudani huu usiku na baada ya dakika 20 mama Janeth alikuja na bint yake Janeth na tukaendelea kunywa.

Mama Janeth alishangaa kuona Iryn anakunywa Mocktail na Iryn alimwambia yuko kwenye dozi hawezi kutumia alcohol. Pembeni yangu kulia alikuwa amekaa Sumaiya na Chupa yake ya Moet na tulikuwa tunapiga story pale,

MIMI: “Mshikaji wangu ni nini nyuma ya pazia kinaendelea wewe na Iryn? amekununua tayari?”

SUMAIYA: “Hamna chochote, nilikuwa naongea naye ndo akanambia nimpe heshima kwani tayari ni wifi yangu ndo nikafurahi kusikia hizi habari na toka muda mrefu nilikuwa najua Iryn anakupenda.”

MIMI: “Naona una macho 3 ndomana nikauliza usije kuwa umenunuliwa.”

SUMAIYA: “Hahahahaa hii kaniletea mama Janeth zawadi Insider, jana alinipigia simu nikachukue.”

MIMI: “Hongera sana I told you mama Janeth anakupenda sana.”

SUMAIYA: “Bahati tu kama wewe ulivyolamba asali kwa mrembo hapo. Insider kuanzia leo nakupa respect katika vitu ambavyo umenikosha ni pamoja na hili suala, hii pisi ni kali umetisha sana. Naona Iryn kabadilika ndani ya muda mfupi, kipindi kile nilikuambia huyu nyege zinamsumbua ukawa hunielewi, unaona sasa hata aibu anakuonea kuonesha unamkaza vizuri.”

MIMI: “Sumaiya acha kuropoka bhana ushaanza kuelewa wewe.”

SUMAIYA: “Be serious Moet ya kunisimbua mimi kichwa? na leo nakunywa tatu hizi.”

MIMI: “Wewe leta masihara kesho video zako zianze kutrend youtube, huzijui vizuri moet.”

Saa 6 usiku mama Janeth alituaga pale na aliondoka na binti yake, baada ya lisaa nilifanya malipo kwa kuchanja maana nilikuwa na card ya Iryn mfukoni. Baada ya kufanya malipo tulisogea meza zote kuwaaga na tulianza na ya kina Lucy na tukamalizia na ya kina Asmah. Mikocheni na Masaki walijitenga.

Tuliondoka kurudi kulala na baada ya kufika kwa apartment na kuingia chumbani Iryn alinisaidia kuvua nguo na mimi nikamsaidia kuvua zake na aliomba tusex pale.

MIMI: “Baby si unaumwa?”

IRYN: “Please f*ck me niko sawa kabisa.”

Baada ya kupitisha mkono wangu alikuwa wet tayari na nilikutana na joto kali sana muda huu na mimi nilimpa alichokuwa anataka, sikutaka mkamia ukizingatia alikuwa mjamzito.

Jumapili asubuhi Iryn aliniomba tukamchukue Junior ili ashinde naye siku nzima na jioni ataonana na mama J ili amuage, maana alisema kuondoka bila kumuaga haitakuwa jambo la busara.

Baada ya kupata soup aliniaga anaondoka kwenda kwa mama Janeth na akirudi tutaondoka kwenda kumchukua Junior. Muda huu mimi niliingia kujiandaa na baada ya kumaliza nilimpigia simu wife ili kumpa taarifa za kwenda kumchukua Junior lakini hakuwa anapokea simu, nikahisi atakuwa church hivyo nikampigia simu mdogo wake kumpa taarifa.

Wakati najiandaa nilikuwa nawaza hivi mama J akija kujua Iryn ana mimba yangu itakuwaje? au akija kujua nimezaa naye hapo baadae atachukua hatua gani?, ni maswali ambayo hata kwangu yalikuwa magumu lakini nilisema kila kitu kinatokea kwa mipango ya Mungu, hivyo sitakiwi kujilaumu kwa hili.

Baada ya masaa 2 Iryn alirudi na mkononi alikuwa kashikilia kimfuko na akanipa pale,

IRYN: “Baby take your gift.”

MIMI: “What is it?”

IRYN: “Just look.”

Niliangalia na kutoa box la Playstation 5 game, sikutegemea kukutana na hii zawadi ukizingatia enzi zangu za ujobless nilikuwa nacheza sana PlayStations na masela.

MIMI: “Baby thank you so much.”

IRYN: “Atleast itakukip busy usiwe unawaza wanawake.”

MIMI: “Sasa baby nitacheza na nani?”

IRYN: “Kuna game za kucheza alone sio lazima ucheze na mtu.”

MIMI: “Tuondoke tuwahi kwa Junior hata mimi nimem-miss mwanangu.”

Ilikuwa ni saa 6 mchana wakati tunaondoka Masaki na tulianza safari ya kwenda ukweni na njiani tulikuwa tunaongea sana,

IRYN: “Baby, Junior na mdogo wake watapishana miaka miwili sindio.?”

MIMI: “Exactly”

IRYN: “I wish wakue pamoja ili wajuane kuwa ni ndugu but ndo hivyo tena haitowezekana.”

MIMI: “Damu ni nzito kuliko maji watakuja kujuana tu.”

IRYN: “Hili suala liko chini yako na wewe ndo mwenye maamuzi.”

MIMI: “Ndomana nimekuambia watajuana tu.”

Baada ya kuwasili ukweni nilimchukua Junior na yeye baada ya kuniona aliishia kunifurahia na sikutaka kuendelea kupoteza muda pale ukweni, hivyo nilimuaga shem wangu nikaondoka pale.

Baada ya kuwasili kwa gari Iryn alimpakata Junior na tukaendelea na safari lakini tulikuwa hatujui tunakokwenda na mwisho wa siku tukakubaliana twende Mlimani city ili akacheze na watoto wenzake.

Baada ya kuwasili Mliman city tulikwenda kwanza kufanya shopping ya mtoto ambapo Junior aliweza kununuliwa nguo, viatu, toys bila kusahau gari nyingine kubwa ya kuendesha. Baada ya kutoka hapo tulikwenda sehemu ya watoto lakini kuna baadhi ya michezo Junior hakuruhusiwa kucheza sababu ya utoto lakini kuna baadhi aliruhusiwa awe na mtu wa kukaa naye karibu. Kw upande wangu nilimwacha na mama yake mdogo wakicheza na nilikwenda kukaa pale Samakisamaki nje nikiendelea kubuy time.

Baadae walitoka na wakaanza kucheza kwenye majani mbele ya Samakisamaki na jinsi alivyokuwa anacheza na Junior ungesema ni mwanae hata watu walikokuwa around pale bila shaka walijua ni mtoto wake. Kwa upande mwingine Junior naye anampenda sana Iryn hanaga noma kabisa na walikuja pale nilikokuwa nimekaa na aliomba funguo ya gari ili akambadilishe mtoto pampas na akirudi tule lunch.

Tulishinda Mlimani city mpaka jioni na tuliamua kuondoka, lakini Iryn aliomba tupitie kwanza Kijitonyama ili akamsalimie Rose na kumuaga kabisa. Baada ya kuwasili kwa Rose alitukaribisha ndani na alifurahi sana kutuona maana ilikuwa ni muda mrefu kidogo umepita tangu Iryn aondoke pale.

Tulitumia kama lisaa pale na tukaagana na Rose na sisi tukaondoka kuelekea na uelekeo wa Bagamoyo Road, ilikuwa ni saa 1 usiku tayari na tulikuwa tumekubaliana na mama J tukutane pale Kibo complex.

Baada ya kuwasili Kibo complex tulipanda mpaka floor ya kwanza, kuna restaurant ambapo mama J alikuwa akitusubiri. Tulifika kwenye meza aliyokuwa amekaa na tukaagiza chakula cha pamoja na story zilikuwa zinaendelea.

MAMA J : “Dear nilikuwa church leo siku nzima nimeshindwa hata kuwa pamoja na wewe.”

IRYN: “Usijali za huko Moshi? hope kila kitu kilienda sawa.”

MAMA J: “Tulimaliza salama, vipi hajawasumbua huyu chautundu?”

IRYN: “Kama unavyoona hajasumbua kabisa, na leo kaenjoy sana.”

MAMA J : “Junior anti anakuacha hutamwona tena.”

IRYN: “No nitamuona bhana nitakuwa nakuja Dar dear.”

MIMI: “Dada wa kazi mmefikia wapi?”

MAMA J : “Atakuja jumatano, Mzee amesema akiwa tayari atapiga simu ili arudi Moshi.”

MIMI: “Habari njema itabidi akirudi tukae naye chini tuone tunafanyaje maana kupata dada kama yule sijui.”

IRYN: “Dada anaondoka?”

MAMA J : “Baba yake aligoma asirudi Dar na mimi sababu anataka kumrudisha shule, nimewaomba wanisaidie kwa muda ndo amesema December mwishoni arudi.”

IRYN: “Poleni sana dada anampenda sana Junior.”

MIMI: “Hata Junior anampenda kuliko mama yake, ndomana hizi taarifa zilinishtua ukizingatia tumekaa na dada kama ndugu yetu.”

Mimi niliamua kutoka na Junior pale ili niwape uwanja wa kuzungumza wake zangu na mimi nilikuwa nacheza na Junior kwenye korido za mle ndani. Baada ya dakika 20 walikuwa wame Maliza mazungumzo yao na ilibidi tuondoke maeneo yale na mama J alifanya kurequest usafiri wa kuwarudisha kwao.

Baada ya kurudi home ule usiku Iryn alianza kubadilika tena na alikuwa kama mtu mwenye homa na alikuwa kalala kwenye coach, na mimi nilikuwa nikimchezea tumbo lake.

MIMI: “Baby naona unabadilika twende nikupeleke hospital.”

IRYN: “Mida hii ndo huwa nakuwa hivi lakini soon nitakuwa sawa.”

MIMI: “Doctor alisema sababu ni mimba yako ya kwanza inaweza kukusumbu sana.”

IRYN: “Baby hii ndo mimba yangu ya kwanza kukaa kwenye kizazi na sijawahi kuwa na historia ya kutoa mimba kwenye maisha yangu.”

MIMI: “Unajua mimi huwa siamini kama kweli umeachana na Grizz afu umekuja kuangukia kwangu.”

IRYN: “Kwakuwa unakwenda kuwa baba mtoto leo nitakuweka wazi sababu ya mimi kuachana na Grizz. Truly nilimpenda sana hata mke wake alivyokuja kufound out haikuwa sababu ya mimi kuachana naye, lakini nilikuja found out alitembea na best yangu Isabella. Pia alianza kunivunjia heshima kuniomba vitu ambavyo siwezi kuvifanya, wewe ni mtu mzima nadhani umeelewa.”

MIMI: “Pole haiwezi kukuharibia uhusiano kwenye biashara zenu?”

IRYN: “Before sijaamua kuachana naye nilikuwa tayari nina plan B ndomana sikuwa na wasiwasi tena na kama faida nimepata ya kutosha, pia kumbuka ile ni kampuni kama atafanya uhuni ninauwezo wa kushtaki mahakamani. Nashukuru alinielewa ile siku na mimi nilimwambia nina mtu wangu nataka kufocus naye kama yeye alivyo focus kwenye familia yake.”

MIMI: “Siku akija kujua huyu mtoto ni wangu itakuwaje?”

IRYN: “Hakuna tatizo why hujiamini Insider? kwamba huna hadhi ya kunizalisha?.”

MIMI: “Sijamaanisha hivyo naongelea jinsi Grizz anavyoniheshimu afu ajue nilikuwa nakula demu wake, unafikiri atanielewa?”

IRYN: “Bila mimi ungemjua Grizz?.”

MIMI: “Tuachane na hayo na hiyo Plan B unayoongelea una mpango gani?”

IRYN: “Kuna best yangu tulisoma wote chuo ni Mfaransa, kuna project tunataka kufanya pamoja na next week atakuja South Africa, tukifika muhafaka nitakwenda Ufaransa pia.”

MIMI: “Mimi nakuelewa mummy unapambana sana mkifika muhafaka utanambia ni project gani.”

IRYN: “Usijali baby ile pesa aliyonipa mama nataka niizalishie isikae kwa bank tu.”

MIMI: “Wazo zuri sana kwa hili nakuunga mkono.”

IRYN: “Twende tukalale baby.”

****
Jumatatu asubuhi baada ya kuamka Iryn alianza kupanga nguo zake kwenye bag kwaajili ya safari na mimi nilikwenda jikoni kutengeneza breakfast.

Baada ya kupata breakfast ile asubuhi tuliamua kwenda Coral beach kupoteza muda na baada ya kuwasili pale, tulikwenda moja kwa moja mpaka beach. Kule beach tulikuwa kwenye dimbwi zito la mahaba maana ndo ilikuwa siku ya mwisho kuspend tukiwa pamoja, tulitumia muda mwingi kupanga mipango mbalimbali ya maisha.

IRYN: “Baby mtoto akiwa wa kiume nitampa jina mimi ila akiwa wa kike utampa jina wewe, deal?”

MIMI: “Deal baby, but nawish awe wa kike.”

IRYN: “I wish too Darling iwe hivyo ili ufurahi.”

Mchana tulipata lunch tukiwa palepale Coral na nilimwambia turudi kwa apartment ili apumzike kwaajili ya safari ya baadae. Matokeo yake baada ya kurudi badala ya kumpuzika tulianza kusex na ilikuwa ni sex moja tamu sana ya mwishomwisho.

Jioni tulijiandaa kwa pamoja kwaajili ya kwenda Airport na Iryn alipendeza sana na niliishia kumsifia pale, lakini kwa upande mwingine nilikuwa naumia kuona akiondoka na kuniacha mkiwa na ilikuwa ni miezi 9 tayari toka tukutane kwa mara ya kwanza.

Tuliondoka jioni na tulipitia kwa Claire waagane na baada ya hapo tuliendelea na safari yetu ya kwenda JNIA terminal 3. Baada ya kuwasili Airport tulikaa pale cafe tukiendelea kubuy time na muda huu tulikuwa tunapiga story za mwisho.

IRYN: “Baby ulikutanaje na mama J mpaka mkafikia kuzaa pamoja.?”

MIMI: “It’s long story kama tulivyokutana na wewe tu, na siamini miezi 9 tuliyokaa ni kama miaka.”

IRYN: “Baby mimi naona unawasiwasi I promised you nitakuwa nakuja kwaajili yako huna haja ya kuwaza hili.”

MIMI: “Baby usijekuwa umebeba ujauzito lakini nyuma ya pazia una mipango yako.”

IRYN: “Hapana baby siwezi fanya hivyo naomba utambue nakupenda sana, na kama utavunja makubaliano yetu huyu mtoto hutakuja kumwona kabisa kwenye maisha yako, so promise me baby.”

MIMI: “Baby siko tayari kumkosa mwanangu kwa upumbavu wangu you have my word.”

IRYN: “You have my word too like I said before sitokuwa na mwanaume mwingine zaidi yako na niko tayari kukuzalia watoto wengine kama utahitaji, naomba utambue nakupenda sana.”

MIMI: “Don’t say that I love you too.”

IRYN: “Baby the first time tumekutana pale Marina nilikupenda, baada ya kujua una familia honestly niliumia sana na nilijaribu sana kukaa mbali na wewe lakini sikufanikiwa, nilijikuta naumia zaidi. Naomba utambue wewe ndo mwanaume pekee uliyeweza kurudisha furaha yangu na kunionesha maana ya maisha, nimekupa huyu mtoto kama zawadi yangu kwako na utambue wewe ni baba halali wa hiki kiumbe tumboni na huyu mtoto atakuwa ukumbusho kwangu Kwako.”

MIMI: “Nashukuru kwa kunipa hadhi ya kuwa baba mtoto wako, I love you baby.”

IRYN: “Baby tambua wewe una thamani kubwa sana kwangu na nina kuheshimu sana, pia ninafuraha ya wewe kuwa baba mtoto.”

MIMI: “One more thing baby before hatujaagana, naomba niambie exactly wewe ni nani? nikiangalia status ya mama yako, mama Janeth na Mzee wako inanipa maswali sana. Sometimes ninawaza mambo mengi sana juu yako nakosa majibu kabisa, nashindwa kuelewa wewe ni nani.”

IRYN: “Baby huna haja ya kuwa na wasiwasi na mimi, ningekuwa mtu unayemfikiria hata nisingebeba hii mimba. Muda umewadia wa kucheck-in na nimepitiliza, sitamani kukuacha but nitakuona soon my love.”

Mimi nikiwa bado kwenye mshangao sijui niseme nini, muda huu Iryn alifungua mkoba wake na alitoa card ya bank ile alonipa kipindi kile Dodoma,

“Baby nakupa hii card yangu ya bank kuna pesa humo zimebaki zitakusaidia, naomba pia umpe nguvu mama J kwenye biashara zake anazofanya nataka wewe ndo ulifanye hili jambo. Kuhusu wewe sitaki kukupangia matumuzi ya kufanya na nikirudi next time tutaongea suala la project ya kule Dodoma.”

MIMI: “Thank you baby but usijali kuhusu mama J nitaliweka sawa na liko kwenye mipango yangu.”

IRYN: “Baby naomba upokee hii card otherwise utanikera na sitoondoka.”

MIMI: “Sawa baby nashukuru kwa hili.”

IRYN: “Baby umepokea kwa mikono miwili?naomba utambue nakwenda kuwa mzazi mwenzako, na ninafanya hili toka moyoni, umeipokea hii card kutoka moyoni?”

MIMI: “Yes baby thank you so much, usiwe na wasiwasi.”

IRYN: “Nita transfer hizi amount zije kwenye account yako na hio card utanisaidia kuichoma.”

MIMI: “Sawa baby ondoa wasiwasi.”

Tulianza kupeana makiss pale bila kuwa na aibu na baada ya dakika 5 tulisogea mpaka usawa wa kuingia ndani ili acheck-in na tulikumbatiana kuagana. Sasa wakati nimetembea hatua mbili mbele nikisikia akiniita tena “Baby….”, na akarudi kwangu spidi,

“Baby… hujamuaga mwanao.”

Na mimi niliinama nikamkiss tumboni na yeye alishia kufurahi na kwa haraka alinipa tena kiss na akaniachia. Ni kitendo ambacho kilivuta sana attention ya watu maana mwanamke aliyekuwa akifanya vile ni mrembo na amekamilika kila idara.

Iryn aliendelea kunikumbatia na macho yake kama yalianza kutoa machozi,

IRYN: “Baby I’m leaving now, I’ll see you soon.”

MIMI: “I love you too baby byee it’s time.”

Na mimi nilimsubiri mpaka anaingia ndani na akaishia kunipungia mkono na mimi nikaondoka kurudi parking ili niondoke.

Baada ya kurudi parking niliingia kwa gari na nilitulia pale kwa dakika 10 huku nikiwaza,

“Iryn anakwenda kuwa mama mtoto wangu hivyo sina jinsi lazima nikubaliane na hili jambo, mimba yake ni mipango ya Mungu sina haja ya kulaumu na hili suala litabaki kuwa ni siri yangu, familia yangu nitawaambia hapo baadae sana mtoto akikua na mama J nitakuja kumwambia hapo baadae sana. Kwasasa natakiwa kutulia na nifocus na familia yangu, mama J na Iryn wananitosha kwasasa, sinahaja ya kuhangaika na wanawake wengine acha nifocus na kufanya maendeleo.”

Simu yangu ilianza kuita pale na alikuwa ni Mama J akipiga na nilitabasamu kuona simu yake pale na niliipokea.

“Baby nakuja kukuchukua turudi home na tukapate dinner ya pamoja.”

Na niliwasha gari nikaondoka kwa fujo sana pale JNIA nikiwa na Audi Q7.

THE END

Wiz Khalifa- Cameras[emoji444]

Email: insiderman1@yahoo.com

The Money Already Printed You Just Gotta Go Get It. Thank you for your time since July
[emoji120]
Nitarudiii
 
EPISODE 46

“A TRUE STORY BY INSIDER MAN”

Nilifanya kurequest usafiri kwaajili ya Mary na mimi nilichukua bajaji kwenda Changanyikeni kulala kwa Prisca.

CONTINUE..

Baada ya kuwasili kwa mama kijacho wangu Prisca nilimkuta hajalala na alikuwa bado yuko seblen anaangalia movie. Niligonga mlango na akatoka kunifungulia, muda huu aliishia kunikumbatia na makisi juu. Pale nje kuna jamaa alikuwa anaanika nguo na aliishia kutukodolea macho kwa wivu.

“Baby I have missed you so much.”

“Remember I promised you nitakuja leo.”

“Pole na Msiba hunny, da Mary umemwacha wapi?”

“Tuliachana ubungo pale yeye karudi home.”

“Kaoge kwanza then uje ule sawa?”

“Twende ukaniogeshe bwana au hutaki kuniogesha Baba Kijacho?”

“Mhh sawa honey tangulia nakuja.”

Baada ya kuoga tulikuwa chumbani tukipiga story na muda huu nilikuwa namchezea Prisca tumbo lake na yeye alikuwa ametulia tulii anasikia raha. Kwa upande mwingine Prisca alikuwa kabadilika sana kimaongezi, ule utoto wake ulikuwa umekwisha, kulikuwa na mabadiliko makubwa sana.

Tuliishia kulala tu maana nilikuwa nimechoka na uchovu sana wa safari.

Asubuhi niliamshwa kwaajili ya breakfast na kwenye simu Iryn, Mary, Muajemi, na Mama J walikuwa wamenipigia simu. Ilibidi nianze kumpigia simu Mama J na niliongea naye mbele ya Prisca huku akisikia.

WIFE: “Baba J Unaendeleaje jana ulisema unarudi mbona hujarudi?”

MIMI: “Wife sorry tulichelewa kutoka then tukapata shida njiani, hivyo tulilala Moro na soon tutaanza safari ya kurudi.”

WIFE: “Ok husband, Iryn amesema leo anaondoka jioni kwenda kwake.”

MIMI: “Sawa! Lakini mwambie asiondoke kwanza, mimi mchana nitakuwa hapo, nitampigia simu soon niongee naye.”

Na wakati naongea na mama J kwa simu Prisca alikuwa akinitizama sana na baada ya kumaliza maongezi akaanza kucheka.

“Honey una masters ya uongo inaonekana hata mimi unanidanganya vingi sana.”

“So ulitaka niseme ukweli kwamba niko kwa mchepuko?”

“Nooo! I like the way ulivyomdanganya na ameridhika kabisa hajawa na maswali tena.”

Na mimi nilikwenda zangu kulala tena maana nilikuwa na uchovu muda huu, ukijumlisha kutoka kule Mbweni mpaka Tabora nilikuwa nakosa muda wa kulala kabisa.

Mchana muda wa saa 9 nilipigiwa simu na mama wa2 na akanambia jioni atakuja kwangu kunitembelea, pia alisema ana mazungumzo na mimi kuna jambo anataka kunishirikisha.

Muda huu ilibidi nimuage Prisca na nikaondoka kurudi home Mbezi. Nilitumia bodaboda kurudi nyumbani na ilinichukua dakika 20 kufika pale, na baada ya kushuka na kuingia ndani mama J alikuja akani hug na Iryn akafuatia.

Muda huu tulitumia kuongea kuhusu habari za msiba za kule Tabora na baada ya kumaliza maongezi ya msiba nilimpa mama J taarifa za ujio wa mgeni.

MAMA J: “Vipi kuhusu Iryn tulikuwa tunapanga tuondoke ukirudi wewe.”

MIMI: “Iryn kwanini tusiondoke kesho mummy nikusaidie kutoa na vitu kule Kijitonyama?”

IRYN: “No problem Insider usiwe na wasiwasi, mama J tutakwenda kesho tuandae dina kwaajili ya wageni baadae.”

Saa 12 jioni mama wa2 alikuja nyumbani pamoja na mwanae Rachel lakini nilishangaa kuona haja ongozana na Pili.

“Mama mkwe karibu ndani hapa ndo nyumbani jisikie upo kwako.”

“Ahsante sana mkwe ukweli nimefurahi sana kupajua pia pole sana kwa msiba jamani.”

“Ahsante sana kwakweli Mzee tulijuana kwa muda mfupi na ametangulia mbele za haki, alikuwa kama mzee kwangu. Vipi mke wangu Pili yuko wapi? mbona hujaja nae?.”

“Pili amekwenda Mwanza kumsalimia Baba yake.”

“Ohh! habari njema hizi ni haki yake.”

Kipindi niko msibani mama wa2 alinijulisha kuwa Pili anafunga shule, hivyo nikamchukue lakini nilishindwa sababu ya kuwa busy na msiba.

Nilitumia muda huu kufanya utambulisho na nilianza na mama J ambaye nilimtambulisha kama mke wangu na nilimtambulisha Iryn kama ndugu yangu. Na baada ya hapo nilimtambulisha mama wa2 kama ndugu yangu wa karibu sana, na muda huu alikuwa amemshika Junior akimchezea.

“Insider una mtoto mzuri hivi napendaje watoto wa kiume mimi, yaani so handsome kama Baba yake.”

“Mama naomba nimshike mtoto na mimi please” ni sauti ya Rachel alikuwa akimwomba mama yake. Na mama wa2 alimpa mtoto Rachel ili amshike.

Saa 1 usiku tulipata dina ya pamoja na baada ya dina akina mama J waliondoka wote pale nyumbani. Waliaga wanatoka out, hivyo nikabaki mimi na mama wa2 pale nyumbani.

Baada ya kuondoka tulikuwa free kufanya maongezi pale kwa kujiachia,

“Insider ukweli nimefurahi sana kufika kwako na kuijua familia yako. Huyo dada umesema ni ndugu yako lakini anaonekana kama sio Mtanzania she’s so beautiful kuna watu walipendelewa kuumbwa.”

“Wazazi wake sio Watanzania kwa kuzaliwa ila wameishi hapa. Nambie ulisema una mazungumzo mengine na mimi.”

“Insider nashukuru Mungu nimepandishwa cheo pale ofisini na sasa nitakwenda HQ na mshahara nitalipwa mara ya 3 ya huu ninaolipwa sasa.”

“Jamani nimefurahi sana kusikia hivyo mama mkwe, mafanikio yako ni yangu. Hongera sana na Mungu akutangulie. Unategemea kuanza lini majukumu mapya?.”

“Mwezi ujao nafikiri, na vipi kuhusu suala lako la kazi nitumie CV yako au hutaki kufanya kazi Bank?”

“Napenda ila kuna deal Marehemu alisema ananitafutia so baada ya kifo chake kuna mtu amemwachia maagizo ambaye tutaonana akirudi kutoka Tabora. Acha nimsikilize afu nitakupa mrejesho mama mkwe.”

“Usiwe na wasiwasi anytime utanambia ili tufanye maarifa.”

“Vipi ni connection au uchapakazi wako tu?”

“Insider ukweli Baba Rachel kanisaidia kupanda cheo.”

“Ndo raha hii ya kuzaa na wakubwa.”

“Hahahah Insider umeanza. Nafikiri tukukimbie sasa ili nikajiandae na ratiba za kesho.”

“Acha niwapeleke ili na mimi niende kule msibani nikaangalie na maendeleo maana toka nirudi jana sijakwenda kabisa.”

Tuliondoka na mama wa2 na nilitumia ile Dualis maana Ist walikuwa wameondoka nayo akina Iryn. Na muda huu nilifanya kuwasiliana na Mary nikamwambia nampitia baada ya dakika 20 ajiandae ili twende Mbweni.

Baada ya kuingia kwa gari Mama wa2 alikuwa akishangaa sana kuona na gari nyingine.

“Insider hii ni gari mpya kabisa umenunua?”

“Hapana hii ni ya Mzee alinununua kwaajili ya mchepuko wake, alisema nisimpe mpaka awe vizuri barabarani, sasa ndo kimetokea kifo chake.”

“Aisee sijui huyo dada anahali gani kwasasa, inaonekana Mzee alikuamini sana, kukuachia gari sio kitu kidogo ujue.”

“Unachoongea ni sahihi Mama mkwe.”

Tulitumia dakika 10 kuwasili pale kwake na niliwashusha na wakati tunaagana Rachel alikuwa akiongea na mimi.

RACHEL: “Uncle Insider utakuwa unakuja kunichukua ili nikacheze na Junior sindio?”

MIMI: “Usijali Rachel nitakuwa nakuja weekend sawa?”

MAMA WA2: “Insider kafunga shule huyu hata katikati ya week sio mbaya.”

MIMI: “Sawa haina shida nitakuwa nakuja kukuchua, wewe ukim-miss nipigie simu tu.”

RACHEL: “Ok byee Uncle.” Na tuliishia kugonga mikono.

Tuliachana pale na mimi nilikwenda kumchukua Mary pale kwao na tukaanza safari ya kwenda Mbweni. Kwa upande mwingine Mary alishangaa kuona nina gari mpya na mimi sikutaka kumwambia chochote.

“Kumbe siku ile usiku ni wewe uliyemshusha Prisca pale home na hii hii gari.”

“Hahahaa ni mimi ila sikutaka kukupa salamu ile siku maana niliona muda umekwenda.”

“Tabia mbaya hiyo Insider unajua nilimfikiria vibaya sana Prisca ile siku, hata yeye hakutaka kusema ni wewe.”

Tuliwasili pale Mbweni na nilimkuta yule mlinzi pale getini akiendelea na majukumu yake. Niliamua ku-park gari nje kabisa ya geti, sikutaka kuingia nayo ndani.

Tuliingia ndani na nikawakuta baadhi ya ndugu wa Jane na marafiki zake baadhi walikuwepo na wengine walikuwa wanakuja kutoa pole. Pis Kuna baadhi ya ndugu walikuwa wameondoka tayari.

Tuliwasalimia wote na mama yake alikuwa pale sebleni nikamsogelea karibu. Nilisalimiana na mama na aliulizia mazishi yalikwendaje kule Tabora. Kwa upande mwingine mama alikuwa na wasiwasi sana kuhusu mwanae kukosa stahiki zake, maana Jane hakuwa mke halali wa ndoa.

Nilimtoa hofu mama muda huu na nikamwambia Mzee alisoma waraka kuwatambulisha wake zake wote hata Jane ametambulika kama mke wake. Na imani atapata urithi maana Mzee aliandika ameacha barua ya mirathi.

“Na wasiwasi mwanangu wasije mnyang’anya na hii nyumba, Jane akaanza kutaabika.”

“Hamna mama Mzee alisema hii nyumba kamjengea Jane, nafikiri hata hati itakuwa na Jina la Jane naamini hivyo.”

Kwa upande mwingine mama yake alinishukuru sana kwa yote niliyoyafanya pale na kujitoa kwangu kipindi chote cha msiba. Na sisi hatukaa sana bali tuliwaaga tukaondoka pale Mbweni na tulikwenda mpaka “The Wave” ya kule chini Whitesand.

Baada ya kuwasili pale, tuliingia ndani na tulitafuta angle nzuri tukakaa. Tuliagiza wine ambayo tulifanya kushara na Mary na muda huu tulikuwa tukipiga story mbalimbali.

“Insider umejitoa sana kwenye huu msiba Mungu atakulipa hata Mzee huko aliko atakuwa anaona must be proud of you.”

“Hata wewe pia Mary ulijitoa sana sikutegemea ungenipa kampani namna ile, ulijitoa kuliko hata ndugu zake Jane.”

“Insider, unajua Mzee japo nilimwona kwa mara 2, ila kifo chake kilinishtua sana.”

“Unajua mimi mpaka sasa siamini amini kama kweli Mzee ametutoka naona kama ndoto. Nikikumbuka wakati tunaongea na alikuwa akinisisitiza sana kumwangalia Jane.”

“Ni kama alikuwa anaona kifo chake inabidi uwe bega kwa bega na Jane, nafikiri Mzee alikupa Task hakutaka kukwambia ukweli.”

“Hata mimi nahisi hivyo, Mzee alinipa task Mungu asaidie Jane ajifungue salama. Nafikiri hii ndo task nayotakiwa kuhakikisha inafanikiwa.”

“Hiyo ndo point hata hivyo Insider unabahati sana ya kukutana na watu wenye hadhi tukianza na Mzee sikutegemea angekuwa na ukwasi wa namna ile.“

“Unajua sikuwahi kumwuliza Mzee kuhusu personal life yake hata siku moja, ila nilipanga this time angerudi ningemwuliza maana alisema angenitafutia kazi.”

“Nilisikia unaongea na Mzee Juma naamini atakusaidia kama kweli alipewa maagizo kutoka kwa mzee na jinsi ulivyojitoa kwenye huu msiba naamini atafanya jambo.”

“Anyway acha tuone Mzee pekee ndo angelichukulia hili suala kwa uzito sana maana kuna sehemu nilikuwa namgusa, how about Mzee Juma??”

“Ni kweli unayosema ila siamini kama anaweza kukuchinjia baharini.”

Tulitumia kama masaa 2 pale “The wave” na tuliamua kuondoka kwenda kulala. Na muda huu niliwaza kumpa pesa kidogo Mary maana nilijua lazima kafulia.

Kipindi niko msibani Tabora niliwasiliana na Muajemi na nilimpa taarifa za msiba na alinitumia milion 1 ya pole. Pia Nilimuahidi nikirudi Dar jumamosi ningemcheki maana alisema anataka tuongee kuhusu sakata la Iryn.

Hivyo, nilikuwa na million 1 kutoka kwa Muajemi, laki 5 kutoka kwa Iryn na laki 3 alizonipa Mzee Juma. Jumla nilikuwa na 1,800,000/= na sikutumia hata cent kwenye hizi pesa.

Nilimpeleka Mary mpaka kwao na wakati tuko nje getini tuliendelea kupiga story na Mary mle ndani ya gari. Baada ya nusu saa hivi tuliagana na nilimpa laki 3 kama shukrani yangu kwake.

******
Jumatatu asubuhi niliondoka pamoja na Iryn kwenda kwenye apartment yake mpya. Na toka alipie alikuwa hajawai kwenda tena maeneo yale. Baada ya kuwasili pale getini kulikuwa na mlinzi, hivyo tukafanya utambulisho kwanza.

“Kaka mimi naitwa Iryn mpangaji mpya niko “Block A” floor ya 1.”

“Karibu sana Bossy na samahani kwa usumbufu.”

“Usijali ni kazi yako hakuna ulichokosea.”

Muda huu tulifunguliwa geti na tulikwenda moja kwa moja mpaka usawa wa apartment ya Iryn ndo nikapark gari.

Baada ya kuingia ndani ya apartment Iryn alikuwa anaangalia vitu vya kununua. Baada ya hapo tuliondoka kwenda Kijitonyama kwanza, kwenda kuchukua vitu vyake.

Baada ya kuwasili pale Kijitonyama tuliingia ndani na Iryn aliingia chumbani kuanza kupanga nguo na kuweka kwenye bag. Mimi muda huu nilikuwa nafungua Home thieta maana ilikuwa inaondoka na baada ya kumaliza nilikwenda kumsaidia kutoa vitu vya chumbani na kupeleka kwenye gari.

Nilifungua drow na nikaanza kutoa vitu vya mle ndani na nilivyofungua drow ambalo lina simu nikaanza kuzitoa na kuzipanga.

IRYN: “Insider hizo simu ulisema utanitafutia mteja uliishia wapi?”

MIMI: “Nilisahau ila leo kuna mtu nitampigia naona ziko 10 idadi ni sawa?”

IRYN: “Ni sawa moja kuna dada nilimpa pale Sinza niliona peke yake hana simu inayoeleweka. Na wewe unaweza kuchukua simu moja hapo utakayoipenda.”

MIMI: “Thank you Bossy, mimi nina chukua hii 13 Pro.”

IRYN: “Kwanini sasa? Chukua hio Pro Max.”

MIMI: “Napenda simu ndogo hiyo Promax hapana.”

IRYN: “Sawa ni wewe tu mimi nimekupa uchague unayotaka kama umeipenda Pro haina shida.”

MIMI: “Na hizi zilizobaki niuzaje?”

IRYN: “Uza hizo 13 Pro Max na hiyo Samsung, hizo 13 Pro ziweke kuna dada tutawapa Saloon. Kwa hizo simu 7 zilizobaki niletee milion 14 cash, ukiuza zaidi ya hapo ni yako.”

MIMI: “Sawa afu nilikuwa nawazo, kwanini ile Saloon ya Sinza isifungwe? Wateja wa pale tukawa direct Mikocheni? Maana nimefanya Research nimegundua wateja wengi hawatoki Sinza pale.”

IRYN: “Wazo lako ni zuri sana nafikiri mwisho wa mwezi huu tuta achana na Sinza. Hata pale Mikocheni tunahama kuna ofisi kubwa niliipata tutaweza hata kupata sehemu ya storage.”

MIMI: “Ooh! hukuwahi kunishirikisha hili kabisa ulianza lini Process?”

IRYN: “Ni muda toka kipindi kile nime-kusimamisha, pia naomba week hii utaorganize kikao kila kitu utapanga wewe. Mimi utanipa ratiba, location na cost zote tutakazo incur. Nataka kuongea na wafanyakazi wangu wote mpaka wa Masaki.”

MIMI: “Sawa haina shida, nitalifanyia kazi then nitakupa mrejesho mapema.”

Baada ya hapo tuliondoka pale Kijitonyama na tulikwenda Mlimani City ambapo alikuwa anafanya shopping ya kununua vitu vya ndani pamoja na chakula. Na baada ya kumaliza shopping tuliondoka na kurudi Kawe kwenye apartment mpya.

Nilishinda pale na Iryn na siku hii nilimpigia Ugali na yeye alikuwa anapika mboga. Na baada ya lunch nilimwaga nakwenda Mbweni kwaajili ya kuangalia maendeleo ya pale.

Nilipitia pale Jambo Supermarket Bahari Beach nikanunua baadhi ya mazaga ya jikoni ya kupika na nilinunua mchele, unga, Nyama ya ng’ombe na Kuku. Nilihisi huenda wakawa wameishiwa vitu vya kupika hivyo nilijiongeza tu kwa upande wangu.

Baada ya kuwasili pale na mazaga dada alikuja kunipokea na nilimsaidia kubeba mpaka jikoni. Nilikuwa nimefaulu ule mtihani maana walikuwa wameishiwa vitu ndani.

“Kaka umejuaje kama vitu vilikuwa vimeisha ndani maana nilikuwa nawaza kukupigia lakini mama akasema niache utakuja.”

“Ungepiga tu hata msiwe na wasiwasi kwa siku nyingine.”

Na muda huu nilikwenda Seblen kuonana na mama na nilimsalimia pia pale kulikuwa na ndugu wengine wa Jane. Mpaka leo walikuwa watu watano tu wamebaki pale kwa Jane.

MAMA: “Mwanangu huyu ni mdogo wake Jane anaitwa Vicky ndo bint yangu wa mwisho. Sikuwai kukutambulisha kipindi kile cha msiba na kila ukija anakuwa ndani.”

MIMI: “Hongera mama naona pia wamefanana sana na Jane, nilikuwa namwona ila nilihisi ni mdogo wake.”

Na mudaa huu nilisalimiana na Vicky, pia alikuwa anasoma chuo hapa Dar na alikuwa 1st year.

VICKY: “Ahsante kaka tunashukuru kwa yote na kujitolea kwako kwenye familia yetu.”

MIMI: “Msijali tuko Pamoja sana ndugu zangu.”

MAMA: “Umewasiliana na Jane? na maendeleo yake yapoje? Mimi simpati kwa simu.”

MIMI: “Nimeongea naye asubuhi na weekend hii ataweza kurudi. Wakati naongea naye alikuwa kidogo kachangamka tuendelee kumwombea.”

MAMA: “Ahsante sana kidogo na amani.”

Na muda huu simu yangu alianza kuita na ile kucheki alikuwa ni Muajemi akipiga na mimi nilipokea simu yake na tukaanza mazungumzo.

Muajemi alikuwa anaomba tuonane jioni ya saa 11 ontime na mimi nilimkubalia sikuwa na pingamizi lolote.

Nilishinda pale Mbweni mpaka saa 10 jioni na niliaga nikaondoka maeneo yale. Njiani nilifanya mawasiliano na Muajemi na akanambia tukutane pale Namanga.

Niliendesha gari mpaka Namanga na mapema nilikuwa nimefika tayari. Baada ya kufika maeneo yale nilimpigia simu na akaniambia yuko showroom ambayo ipo opposite na mataa ya Namanga.

Nilidrive mpaka pale Showroom na nikapark gari nje nikaingia ndani. Baada ya kuingia ndani niliweza kuonana na Muajemi na tukasalimiana kwa kugonga tano. Na muda huu tulianza kuongea na alinipa pole ya Msiba na maongezi mengine mengi yaliendelea.

“Bro! sitaki kukupotezea muda ila nina zawadi kwaajili ya Iryn naomba uipeleke kwa niaba yangu.”

“Ni zawadi gani hiyo Bro?”

“Twende nikuoneshe Bro!.”

Tuliongozana na Muajemi na baada ya mwendo wa hatua 10 hivi alinionesha gari kama zawadi ya Iryn. Mbele yangu ilikuwa inaonekana Mercedes Benz kwa nyuma ikisomeka “S-550” something like that. Na colour yake ni rangi ya maziwa “pearl” na ilikuwa inang’aa sana muda huu.

“Nataka umpelekee Iryn hii gari.”

EPISODE 47[emoji116]
Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu
46
 
Katika nyuzi bora humu na zenye mafunzo nilizozisoma humu ya kwanza ni ile "NAITWA ANALYSE NA HII NDIO STORI YA MAISHA YANGU" na yapili ni hii yako.. INSIDEE..

Nyie mnajua kulezea na halina mba mba mba.

All the best to you
 
EPISODE 47

“A TRUE STORY BY INSIDER MAN”

CONTINUE…..

Muda ule ilibidi nishangae kwanza maana niliona Muajemi kama karogwa hivi na sio akili zake. Niliona Muajemi ni kama hajitambui na hajui anafanya nini.

MUAJEMI: “Bro! unaionaje hii gari? Nataka umpelelekee Iryn kama zawadi.”

MIMI: “Bro! ushailipia tayari hii gari?”

MUAJEMI: “Bado nataka kwanza utoe comment then nifanye malipo ili uondoke nayo.”

Na kipindi hiki chote kulikuwa na Jamaa mwenye asili ya uarabu akiwa makini sana na sisi. Maana alijua kabisa gari imeuzwa anasubiri maokoto tu kutoka kwa Muajemi.

MIMI: “Bro! samahani naomba tuongee mara moja then tutarudi.”

MUAJEMI: “Sawa haina shida, unataka tuongelee wapi?”

MIMI: “Nafikiri twende pale mbele kuna kamgahawa tukae kabisa.”

Tulitoka pale na tulikwenda moja kwa moja mpaka Mgahawa wa Best bite na tulikaa pale tukaanza maongezi.

MIMI: “Bro! najua una mapenzi na upendo wa kweli kwa Iryn. I really appreciate your efforts, nimekuwa na wewe bega kwa bega toka mwanzo mpaka sasa, lakini kwa hili sikuungi mkono kabisa.”

MUAJEMI: “Kwanini Bro! mimi nafanya kutoka moyoni kabisa na nilikuwa na mpango wa kumnunulia gari toka muda mrefu sana.”

MIMI: “Sawa Bro! cha kwanza inatakiwa utambue unadeal na aina gani ya mwanamke. Iryn hana shida na gari ni vile hajataka kununua na hata akitaka gari mama yake aliacha Range sport mpya kabisa ipo kwa mama yake mlezi. Haya yote unafanya ili uweze kumuwin lakini unashindwa kutambua Iryn sio dizaini ya Wanawake wenye njaa. What if kama nitampelekea zawadi ya gari na akaikataa? umejaribu kuwaza hivi? Na vipi kwa upande wako utajisikiaje?.”

MUAJEMI: “Kaka upo sahihi sasa unanishauri ni nini hapa?”

MIMI: “Ni simple tu ili kuepusha haya kutokea. Iryn ni mtu mzima tayari anajitambua huna haja ya kuendelea kuzunguka mbuyu tena, kwasasa nenda direct. Omba appointment ya kuonana naye najua hawezi kukukatalia, this time itabidi umchane ukweli na usifiche hata kitu kimoja mwambie ukweli kuhusu maisha yako na mipango yako kwake.”

MUAJEMI: “Bro unaona ni sawa kumwambia direct? Vipi kama atanichomolea si itakuwa matatizo?”

MIMI: “Point yangu acha kupoteza muda kwa mwanamke, utapoteza pesa, utatoa hata zawadi ya figo lakini kama hakupendi- hakupendi ndo wanawake walivyo. Mpaka sasa mnafahamiana tayari vya kutosha don’t waste your time Bro! Kaa naye chini mpe ukweli ibaki yeye kuamua tu kama yuko in or out.”

MUAJEMI: “Kaka naona upo sahihi itabidi niombe appointment naye weekend hii.”

MIMI: “Yeah fanya hivo, akikubali sasa hapo unampelekea gari kama zawadi ili kukazia mapenzi ila kwasasa utakwama hata yeye atakushangaa sana atakuona bwege. Na ikitokea kakuchomolea wewe achana naye pisi kali zipo kibao, wewe unapesa huwezi kosa pisi kali sehemu yoyote Duniani.”

MUAJEMI: “Sawa Bro! leo umeongea point ila wasiwasi wangu akikataa.”

MIMI: “Mwanaume kuogopa kukataliwa ni udhaifu mkubwa sana inatakiwa ujiamini hata kama akikutalia chukulia simple madem wako wengi tu. Sasa ni bora ukataliwe au uendelee kupoteza muda? Na kumbuka nilikwambia before kwamba Iryn ana mtu wake Ufaransa anampa kila kitu anachotaka, hata yeye hana shida.”

MUAJEMI: “Sawa Bro! Acha mimi niende tutawasiliana.”

Tuliagana na Muajemi na alitoa laki 1 kwaajili ya mafuta ya gari na akaondoka. Niliamua kumchana ukweli Muajemi ili aisendelee kupoteza pesa. Maana niliona kuna siku itaweza kuleta shida hata pesa alizokuwa ananipa ni sababu ya Iryn wala sio kingine.

Iikuwa ni saa 12 jioni baada ya kuachana na Muajemi mimi nilielekea Mlimani moja kwa moja. Kuna jamaa nilikwenda kuonana naye mitaa ile kwaajili ya kufanya biashara ya zile simu.

Baada ya kuonana na kuridhika na zile simu, tulikubaliana kwa simu zote 7 atanipa 16,800,000/=. Na jamaa hakutaka kuchezea ile bahati na alifanya kutransfer Pesa kwenye account yangu ya bank.

Niliondoka maeneo yale ya Mlimani na nilikwenda chuo kumchukua Prisca mama kijacho wangu ili tupate Dinna ya pamoja. Na baada ya kuwasili pale chuo ilibidi nimsubiri atoke class na baada ya nusu saa alikuwa katoka tayari akiwa pamoja na Eva.

Tulitoka pale chuo na tulikwenda mpaka mlimani city pale Instanbul restaurant kwaajili ya dinna. Kila mtu aliagiza anachopenda kula na muda huu story zilikuwa zikiendelea pale.

MIMI: “Nambieni wake zangu masomo yanakwendaje.?”

Niliishiwa kupigwa jicho kali sana na Prisca muda huu.

EVA: “Shem hongera sana unakwenda kuwa Baba soon.”

PRISCA: “Awe Baba mara ngapi?”

MIMI: “Ahsante sana shemela wangu leo itabidi unipe namba zako incase of anything uwe unanipigia.”

EVA: “Sawa shem haina shida.”

PRISCA: “Baby itabidi nianze kwenda clinic mapema.”

MIMI: “Subiri kwanza ufikishe week 8 ndo uanze kwenda kwasasa mapema sana.”

EVA: “Hata mimi nilimwambia leo bado mapema sana, naona anatamani sana kuwa mama.”

Nilikaa na akina Prisca mpaka saa 3 usiku kasoro nikawaambia warequest usafiri na mimi nikaondoka kuelekea kwa Iryn.

Baada ya kufika pale na kuingia ndani nilikuta hakuna mtu ndani lakini simu ilikuwa seblen kuonesha mtu yuko around. Nilisubiri kama dakika 10 lakini mtu simwoni, nikakumbuka kuna swimming pool nilihisi atakuwa huko.

Baada ya kuzunguka na kwenda upande wa swimming pool nilimkuta kule akiwa anaswim kama mtu ambaye hana stress na maisha, na alikuwa peke yake.

“Nimekusubiri sana kumbe upo huko mummy.”

“Insider ingia bhasi na wewe maji ya moto hadi raha.”

“Mimi siingii humo ndani fanya kutoka twende ndani tukaongee.”

“Usinambie leo hii hutaki kuswim na mimi.”

“Muda umekwenda kuna jambo nataka tuzungumze muhimu.”

“We can talk there mbona kuna utulivu wa kutosha hapa. Anyway twende ndani hata hivyo nimekaa sana kwenye maji.”

Tulirudi ndani muda huu tukiwa tumeongozana njiani, na Iryn alikuwa katangulia kwa mbele, so nilikuwa kwa nyuma nikamtizama maungo yake kwa matamanio.

MIMI: “Iryn Mungu alikuumba sana Mummy.”

IRYN: “Insider toka nyuma yangu tangulia mbele.”

Baada ya kuingia ndani aliingia chumbani na baada ya dakika 10 alitoka kavaa tayari.

IRYN: “Insider unajambo gani?”

MIMI: “Kwamba sikuhizi umeanza kunionea aibu mpaka umeenda kubadilika? Hujui nilikuwa naona raha kukuangalia ukiwa vile?”

IRYN: “Natoka tukiachana hapa na utanipeleka Mikocheni Plaza nikale Pizza.”

MIMI: “Ok sawa, nimeshauza simu tayari nipe account namba nifanye kutransfer pesa zako.”

IRYN: “Sawa twende bhasi njiani nitakupa utatransfer.”

Na muda huu alikuwa akiniinua kwenye coach kwa kunibembeleza.

Ilibidi nimepeleke Mikocheni Plaza pale Pizza Hut na baada ya kuwasili alining’ang’ania simsubiri ili turudi wote tena. Ukweli sikuwa na jinsi ilibidi twende wote mpaka ndani japo nilikuwa natamani kurudi home mapema.

Iryn aliingia ndani kuweka odda na baada ya dakika 5 alitoka akaja akakaa kwenye bench kwa pale nje. Na muda huu kuna jamaa alikuwa anakuja upande wetu ni kama alikuwa amem-target Iryn sasa aliponiona mimi dizaini kama alipiga U-turn.

IRYN: “Uyo mshenzi alikuwa ananitongoza eti alikuwa anataka kunilipia Pizza nikamgomea. Akaanza kuniomba namba ya simu, baadae akanambia unakaa wapi, nikamwambia nimekaa nje na mme wangu.”
Na muda huu Iryn alikuwa anacheka sana.

MIMI: “Sasa hapa ndo alikuwa anakufuata? Maana niliona alikuwa anakuja kwa ajili yako.”

IRYN: “Alikuwa haamini nafikiri sasa kweli kaprove. Why Tanzanian men’s are not smart?”

MIMI: “Sio Tanzania tu ni Dunia nzima acha uchawi wako kwa Watanzania.”

IRYN: “Sawa bhana, ngoja nikachukue juice. Insider nikuletee juice gani?”

MIMI: “Nichagulie nzuri for me.”

Iryn aliondoka na muda huu jamaa alikuwa akiniangalia sana dizaini alikuwa haamini macho yake kama mimi ndo mme wa Iryn. Na Iryn alivyorudi alinikisi shavuni kwa makusudi, nilihisi anamuumiza jamaa tu.

MIMI: “Noana umeamua kumchoma Moyo Jamaa.”

IRYN: “Nimekukisi sababu ya kunipa kampani wala sio sababu ya huyo mshenzi.”

MIMI: “Sawa mrembo wangu wa Dunia kula Pizza tuondoke nimem-miss mama J wangu leo.”

IRYN: “Hongera zako mimi mpaka nionane na Grizmann. Afu ratiba zetu zitaendelea soon nakosa Pesa nyingi sana kwakweli.”

MIMI: “Iryn bado unawaza kuendelea na hizo Biashara?”

IRYN: “Insider kazi ni kazi hutakiwi kuchagua, mimi ni mzuri nina kipaji cha massaji kwanini niache Pesa zinipite?. Afu nilikupa offa ya kukufanyia massage lakini unaringa, na hii kwaajili ya afya yako. Kumbuka unakaa sana kwenye gari unahitaji kunyooshwa huo mgongo shauri yako.”

MIMI: “Kweli itabidi unifanyie matibabu Doctor.”

IRYN: “Tuondoke mimi niko full hapa bebe.”

Na muda huu tuliondoka huku jamaa akituangalia kwa wivu sana na Iryn alikuwa kaniwekea mkono kiunoni, kwa mtu anayetuona kwa mara ya kwanza angejua sisi ni wapenzi.

Nilimpeleka Iryn kwake na mimi nikarudi home muda ule maana ilikuwa ni saa 5 kasoro usiku.

Kwa upande mwingine kwenye zile simu za Iryn nilikuwa nimepata 2,800,000/= kama udalali baada ya kuziuza.

*********
Jumatano asubuhi nilipigiwa simu kutoka kwa mama Janeth na aliomba tuonane saa 6 mchana pale ofisini kwake Masaki.

Mapema sana kwenye saa 6 kasoro mchana nilikuwa nimewasili pale na nilikwenda moja kwa moja mpaka getini na gari. Mama Janeth alisema nikifika pale niingie na gari ndani moja kwa moja nisipark nje.

“Bro! habari yako unakwenda wapi?”

“Nakwenda kuonana na Mrs Carter.”

“Wewe ni nani na una appointment naye?”

“Sasa nitakuja kwenye Organization kubwa kama hii bila kuwa na appointment?”

“Embu subiri kwanza tufanye mawasiliano.”

Nilisubiri pale getini kama dakika 3 hivi ndo nikaruhusiwa kuingia ndani. Na baada ya kupark gari niliwasiliana na Mama Janeth na akanambia nimsubiri pale sehem ya visitors anakuja.

Ilimchukua kama dakika 15 mama Janeth kutoka na baada ya kufika pale nilipokuwa nimekaa tulisalimiana na akanambia tuongozane, na muda huu tulikwenda moja kwa moja mpaka kwenye ofisi yake.

“Insider karibu sana Jisikie huru hii ni ofisi yenu usiwe na wasiwasi.”

“Ahsante sana mama kwanza nashukuru kwa kunipa wito wa kufika kwenye organization kubwa kama hii.”

“Mnaruhusiwa kuja mbona sema Watanzania hampo active kama nchi zingine.”

“Sijawai kujua hili mama.”

“Mnaruhusiwa kuvisit kama unataka elimu anything unapewa. Nimekuita hapa kwanza pole na msiba mwanangu, Iryn alinipa taarifa zote na alinambia mazishi yalifanyika Tabora.”

“Ndio mama nashukuru lakini kazi ya Mungu haina makosa, japo inaumiza sana kuondokewa na mtu muhimu kwenye maisha.”

“Poleni sana, nilitamani sana tuonane maana wewe ni moja ya member wa kampuni yetu na kazi yako inaonekana nikushukuru kwa hili. Nilipita pale ofisini nikaona umeweka mazingira mazuri, umepanda miti na maua kwakweli ulinifurahisha sana.”

“Ahsante sana mama ni moja ya majukumu yangu ya kiofisi huna haja ya kushukuru wakati unanilipa mshahara.”

“Jambo lingine naomba uniwie radhi kwa kutokukurudia mapema lakini ujumbe wako niliupata kwa kuchelewa sana. Nilikuwa huko Ukraine tunafanya tafiti so I was very busy that time na dada alituma mail kwenye account yangu binafsi, angetumia ya ofisi ingekuwa haraka sana kuipata.”

“Usijali mama kuwa na amani Iryn alishanambia hayo yote tayari, kipindi kile nilikuwa kwenye wakati mgumu sana. Iryn aliondoka bila kuniaga afu akawa hapatikani kwa simu, nikapata wazo la kwenda kwako lakini nikaambiwa umehama. Nikaamua kuja hapa ofisini ndo HR akanambia niache taarifa zangu atakutumia.”

“Pole sana pale tulihama, wakati umeleta mzigo weekend tulihama. Niliamua kuhamia nyumba yangu maana landlord alipandisha rent, nikaona bora nikakae nyumba yangu ili niwe huru.”

“Ni kweli kabisa mama upo sahihi kodi zina kera sana.”

Kwa ufupi mama Janeth alifurahi sana kwa kumjali sana Iryn maana alisema before mimi Iryn alikuwa ni mtu wa mawazo sana na alikuwa anajifungia ndani. Lakini baada ya kukutana na mimi amebadilika sana amekuwa mchangamfu na furaha sana.

Mama Janeth alinishukuru sana na aliniomba niendelee kuwa karibu na Iryn ili amsahau mama yake kabisa.

Ni mazungumzo yaliyochukua kama dakika 45 na baada ya hapo alinipeleka kwa yule HR wa siku ile na akanitambulisha kama mwanae. Yule HR alishangaa sana na alikuwa anani-changamkia sana muda huu.

Baada ya yote Mama Janeth alisema tukapate lunch ya pamoja na tulikwenda kupata lunch pale Epi d’or.”

Muda ule tukiwa pale mgahawani tulikuwa tunaongea mambo mengi sana na Mama Janeth kuhusu maisha na mambo mengine. Kwa upande wake mama Janeth alikuwa na furaha sana na jambo lingine alikuwa anahisi mimi nina mahusiano ya kimapenzi na Iryn.

Baada ya lunch nilimrudisha Mama Janeth ofisini kwake na tukaagana. Wakati niko njiani nilifanya mawasiliano na Dullah maana nilimwambia nikirudi toka Tabora msibani ningemjulisha.

Nilimwambia Dullah juu ya maamuzi yangu ya kuachana na biashara ya Uber kama ukumbusho wangu kwa Mzee Pama. Japo alinipinga sana na haya maamuzi yangu lakini ilibidi akubaliane tu na mimi, kwanza biashara ilishakuwa ngumu sana kipindi hiki. Dullah alinisisitiza sana Uber wakirudi niendelee na kazi lakini nilimwambia nitaajiri dereva, na haya yote ni sababu ya heshima yangu kwa Mzee Pama.

*******
Kesho yake jioni ambayo ni alhamis niliamua kupitia saloon zote kufanya ukaguzi pamoja na kuwapa taarifa Lucy na Sumaiya kuhusu kikao cha weekend.

Niliona ni busara kuwashirikisha katika mipango ya kikao kwa ujumla, sambamba na eneo la kufanyia. Iryn aliniachia hili suala mimi kama operation manager lakini na mimi niliona sinabudi kuwashirikisha akina Lucy kama partners wangu.

Nilianza na Lucy pale Mikocheni na baada ya kumshirikisha alitoa wazo tutafute sehemu nzuri ya uwazi na baada ya hapo twende sehemu tukamalizie bata.

Tuliagana na Lucy na nilikwenda moja kwa moja mpaka Masaki kwaajili ya kuonana na Sumaiya. Wakati nawasili pale dizaini kama aliniona hivyo alitoka na akaja parking na akafungua mlango wa gari akakaa siti ya mbele.

“Mtoto unapenda magari wewe.”

“Hakuna mwanamke asiyependa gari Insider.”

“Naona leo umependeza sana na hiko kigauni chako kinafanya viamke vilivyo lala.”

“Kwa mwanaume Rijali ni kawaida so siwezi kukushangaa wewe kama ni kweli. Niambie unajambo gani kutoka kwa Queen, maana leo kanipigia simu eti ananisalimia, toka lini Queen anipigie simu akanisalimia?.”

“Si Bossy wako? hutaki akujulie hali mfanyakazi wake ?”

“Yule anahisi mimi nakupea ni wivu tu umemjaa, maskini anafikiri tunanyanduana.”

“Mama Janeth alikutoa wapi wewe? Maana sijawahi kukutana na mwanamke mwenye mdomo kama wewe.”

Sumaiya ni mwanamke asili yake ni Tanga anakimwili portable afu mweupe madem wa Tanga nadhani mnawajua vizuri. Kingine alikuwa mwongeaji sana afu hanaga aibu kabisa.

Niliongea na Sumaiya kuhusu suala la kikao Jumamosi na yeye alishauri tutafute Hotel au sehemu yoyote ya wazi ili tufanye kikao chetu na baada ya hapo tutoke out.

Ushauri wa Sumaiya niliona una mantiki
Maana tungekuwa 17 kwa idadi ya wote, Masaki kuna wafanyakazi 7, Mikocheni 5, Sinza 3 , bado mimi na Iryn. Jumla hapo tunakuwa 17 so hotel ndo ilikuwa sehemu sahihi ya kufanyia kikao.

Baada ya maongezi Sumaiya aliomba nimsubiri ili nimpe lift mpaka Morocco na ilikuwa ni usiku umeanza kuingia.

Nilimsubiri kwa nusu saa ndo alitoka na tukaondoka, sasa kutokana na story za njiani nilijikuta nampeleka Sumaiya mpaka kwake. Alikuwa anakaa Kinondoni mitaa ya Gavana kule kama unakwenda Biafra. Na lengo langu lilikuwa nikatokee mataa ya Biafra then Morocco afu niunge na Bagamoyo road.

“Insider si unapitia kwangu upajue? Kufika mpaka hapa na usiingie kwangu haitakuwa vizuri.”

“Sawa twende nikapajue kwako.”

Baada ya kuwasili kwake alishuka akafungua geti na mimi nikaingiza gari nikapark tukaingia ndani kwake. Alikuwa amepanga apartment nzuri ya Jiko, sebule, na masta.

“Nani anakulipia kodi hapa? sitaki matatizo.”

“Angekuwa analipa kodi mwanaume mwenzako hata nisinge kuingiza ndani.”

Na muda huu nilimvuta kwangu kwa nguvu na nikamshika makalio yake.

“Makalio yenyewe huna ya kushika.”
Na nikaendelea kuyapapasa na kuyaminya minya.

Niliona Sumaiya kashaanza kulegea taratibu na yeye akanipa tongue tukaanza romance pale asee ilikuwa ni mtifuano, nikambeba nikamtupia kwa coach. Na kalivyo portable vile hata sikuwa na tumia nguvu kubwa sana kumbeba.

Sikutaka hata kumcheleweshea kabisa nikamvua kigauni chake, uwii alikuwa na bikini afu kwa juu hakuvaa chochote nilikuwa naziona chuchu zake live zilivyosimama wima, uzuri zilikuwa zina jaa kwenye mikono yangu maana alikuwa ana vifuu vidogo sana.

Nilianza kuvinyonya taratibu pale na yeye alishakuwa yuko Dunia nyingine muda mrefu sana. Kisima chake kilikuwa kishaanza kutoa chemchem tayari na mimi niliendeleza maunyama yangu taratibu hata sikuwa na mapepe maana kuku ni wangu haraka za nini?.

Muda huu Sumaiya alikuwa kashaanza kupapasa mtwangio wangu ili nianze kutwanga kinu. Na mimi palepale nimlaza chali na nikambetua kwa juu kidogo ndani ya sekunde alikiaa chaaah!, niliiachana bikini yake vipande viwili. Na muda huu nilikuwa nashuhudia something hot between her legs na alikuwa kashave kabisa.

Nilimkunja vizuri kabisa kwaajili ya kumtwanga lakini nilikumbuka sina kinga, sikutaka suala la Prisca lijirudie tena hivyo nikamuacha palepale.

“Insider unashida gani?”

“Do you have a condoms?”

“No sina.”

“Siwezi kuendelea bila condom acha nikanunue chap then nakuja tuendelee.”

Na muda huu Sumaiya alikuwa mpole ikabidi nimwambie nakwenda pharmacy kununua then narudi, hata yeye hakuwa na cha kusema.

EPISODE 48[emoji116]
Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu
Nimefika
 
EPISODE 70
A TRUE STORY BY INSIDER MAN

FINAL EPISODE


PART I
Kitendo cha Iryn kusema tuachane ilikuwa ni trap ameniwekea na kubwa alitaka kujua mienendo yangu na Asmah. Iryn alikuwa hana imani kabisa na Asmah maana alikuwa anaamini mimi na Asmah tuna mahusiano ya siri sana hata kitendo cha kumpandisha cheo alitaka tuwe close ili abaini kama kuna something fishy kinaendelea kati yetu.

Bossy lady aliniwekea mashushushu/maspy wa kufuatilia movement zangu zote hasa nikiwa na Asmah, kuna ambao walikuwa pale ofisini na wengine wa nje. Nilivyokuwa ninatoka na Asmah kwenda kumtembeza kwaajili ya mazoezi ya mguu alikuwa anapata hizi taarifa.

Taarifa za kwenda apartment ya Asmah alikuwa anapata hizi taarifa kupitia hawa mashushushu wake ambao walikuwa wananifuatulia na Asmah kila move. Hawa mashushushu wake mimi siwafahamu hata sikujua kama ninafuatiliwa namna hii.

Baada ya Asmah kurudi kazini akiwa mgonjwa ukaribu wetu uliongezeka sana ukizingatia nilikuwa nampa kampani ya mazoezi, kwenda kula lunch na hata kumpa lift ya usafiri mpaka kwake. Kitendo cha mimi kuwa karibu sana na Asmah yeye alihisi sisi ni wapenzi wa muda mrefu sana na aliumia sana kwa hili.

Kwanini Iryn alifanya hivi?

CONTINUE…..


Niliichana ile bahasha kwa juu na nikatoa barua ambayo ilikuwa imekunjwa na baada ya kuifungua niliona ameandika mambo mengi sana kwenye ile karatasi na mimi sikutaka kuisoma, nikaendelea kuangalia vitu vingine vilivyokuwa kwenye ile bahasha.

Ndani ya bahasha kulikuwa na bahasha nyingine ndogo na baada ya kuifungua nilitoa picha tatu (3) ndogo za black and white na ile kuziangalia vizuri nilijua zimeprintiwa baada ya kuchukua vipimo vya “Ultra sound”. Pia ndani ya ile bahasha ndogo kulikuwa na form inayoonesha matokeo ya vipimo na pale juu ilikua imeandikwa “Saifee hospital” na niliisoma kwa makini sana na nikagundua Iryn ana ujauzito wa week 4 tayari.

“Ooh shit Iryn ana mimba yangu? Impossible”
Na muda huu nilianza kuingiwa na wasiwasi juu ya Iryn na niliwaza anaweza kutoa ile mimba kwa hasira zake, acha niende kwake mapema before it’s too late. Kwa upande mwingine ile barua sikutaka kuisoma kabisa maana niliona haina umuhimu na mimi sikutaka kujua alivyokuwa kaviandika mle ndani.

Muda huu nikiwa bado kwenye mawazo niliendelea kuwaza,

“Huenda Iryn aliamua kukaa mbali na mimi baada ya kujua ana ujauzito wangu, acha niende kwake ndo nitajua vizuri hukohuko.”

Kwa upande mwingine Asmah alikuwa akiendelea kupiga simu na ilibidi nimtumie ujumbe wa kumwambia nimepata emergence na nitamrudia badae kidogo.

Niliondoka pale ofisini kwa spidi sana kuelekea kwa Iryn na baada ya kuwasili pale kwake niliiona Audi ikiwa pale parking na nikajua huyu yupo ndani na mimi nilipanda kwenda kwake kwa spidi sana.

Nilifungua na kuingia ndani na pale seblen kulikuwa na bag kubwa kama mtu ambaye anataka kusafiri na ilibidi niende mpaka chumbani kwake na nilimkuta akipanga nguo kitandani. Kwa upande wake alishtuka baada ya kuniona ni kama hakutegemea angeniona muda ule pale kwake, na muda huu hasira zake zilianza kupanda kwa kasi sana na akasimama.

IRYN: “Insider what are you doing here? get out of my sight. I don’t want to see you again.”

MIMI: “Baby calm down please, unatumia hasira naomba nisikilize, tuzungumze hili jambo.”

IRYN: “Umenielewa nilichokwambia? Sitaki kukuona hapa naomba uondoke.”

Mkononi nilikuwa nimeshika ile bahasha na nikaifungua nikatoa zile picha za nikamuonesha,

MIMI: “Hiki ndo kimenileta hapa tujadili maana una damu yangu na haya mengine uliyoandika sijasoma na sitaki kujua uliandika nini.”

Na nikachana chana ile bahasha mbele yake huku anashuhudia.

“Baby naomba tukae chini tuongee please, I need just 5 minutes.”

Iryn hasira zilizidi kumpanda na alianza kutoa kigugumizi na koo lilianza kuvimba, ukweli sikuwahi kuona hasira za Iryn kama hii siku.

IRYN: “In..si..der I said get out before I do something bad.”

MIMI: “Really? Something bad?, I know you can do it, letme help you.”

Nilifungua drow ya bedside na nikatoka gun nikaiweka kitandani,

“Take it and do whatever you want”

Nilipiga magoti chini ile “Hands on your knees” na niligeukia upande wa mlango ili nisione action atakayoichukua, muda huu hata mimi akili zangu zilikuwa zimerukwa na nilikuwa siogopi kufa kabisa.

Baada ya dakika niliona mtu akinishika bega na akaanza kuongea,

IRYN: “Insider please stand up.”

Na machozi yalikuwa yakimtoka mithili ya chemichem na macho yalikuwa mekundu sana,

MIMI: “Can’t you do it?”

Na mimi nilisimama tukawa tunaangaliana na nilimsogelea nikaanza kumfuta machozi yake kwa kitambaa changu na haikuchukua muda tukaanza kupeana denda za pupa. Alikuwa kavaa skin jeans, tayari kwa kuondoka na niliishusha mpaka usawa wa magoti na nikamgeuza na kumuinamisha ashike kitanda na nilichomeka mashine kwa nyuma. Pia alikuwa kasuka rasta ndefu na nilizikunja zile rasta zake kwenye mkono wangu, kama mtu anaye endesha farasi na nikawa nahit kwa spidi sana. Niseme hata mimi sikuwa kwenye akili yangu na nilisikia akianza kulalamika pale,

IRYN: “Insider stop I am pregnant.”

Lakini mimi hata sikuwa na habari naye kabisa, muda huu nilikuwa busy sana kutafuta bao la kufutia machozi,

IRYN: “Baby you’re hurting me stop it.”

Ilibidi nimuache na muda huu risasi ziliruka kwa spidi sana na ziliishia kumchafua paja zake kwa nyuma maana wazungu walitoka wengi sana. Muda huu nilimvua nguo zote na zoezi likaanza upya tena ni kama tulikuwa tume-misiana na minyanduo iliendelea mpaka tukawa hoi.

Tulikwenda kuoga na baada ya kutoka bafuni tulikuwa tumelala kitandani na mimi nilikuwa nachezea tumbo lake taratibu sana kama nalibusu kitovuni na wakati nalichezea alikuwa akitabasamu sana,

MIMI: “Baby ulikuwa unakwenda wapi? ndo ulitaka kunikimbia baba mtoto?”

IRYN: “Ungechelewa usingenikuta hapa na jumapili nilikuwa naondoka kwenda south, kila kitu nilikuandikia kwa barua but for now It does not matter.”

MIMI: “Ndo ujue wewe ni wangu na ulikuja Tanzania kwaajili yangu, unataka kusahau ni jinsi gani nimekupambania mpaka leo tumefikia hapa.?”

IRYN: “I appreciate that, Insider unaniumiza sana hisia zangu nashindwa kuelewa wewe Mwanaume unanini? Why I can’t let you go?. I used to love Grizz but when comes to you hit me different why?…why?.”

MIMI: “Mimi leo nataka tumalize mzizi wa fitina, wewe ushakua mama mtoto wangu na una damu yangu tay…..”

Iryn alinikatisha pale maongezi yangu,

IRYN: “Insider nambie wewe na Asmah mna siri gani? please be honesty.”

MIMI: “Leo na confess kila kitu kwako nataka tuachane na hizi drama, Asmah sijawahi kuwa naye kwenye mahusiano ila tumesex kipindi kile naanza kwenda Masaki kuchukua na kupeleka bidhaa ndo tulifahamiana na kupelekea hivyo, lakini mpaka sasa hatujawahi kukutana tena, niseme ilikuwa ni bahati mbaya.”

IRYN: “Leo umesema ukweli nilikuwa najua hili kwa muda mrefu sana, na bado unakwenda kwake mpaka sasa na juzi tu umeshinda na Asmah mpaka saa 4 usiku taarifa zako ninazo zote.“

MIMI: “Ni kweli kwa Asmah nimekwenda mara 2 usiku na nilikuwa nampa lift mpaka kwake, wewe unaelewa fika Asmah ni mgonjwa na mimi ndo nilikuwa namsadia kufanya mazoezi ya mguu na kama napata muda nilikuwa nampeleka kwake, lakini hakuna tulichokuwa tunafanya na yeye anaheshimu hili.”

IRYN: “Doesn’t make sense to me, anyway labda nimwambie kitu ambacho ulishindwa kufahamu kipindi nimekutumia ile voice note.”

MIMI: “Unataka kusema uliniwekea trap?”

IRYN: “Exactly na nilifanya makusudi.”

Iryn alinambia baada ya kutambua ana mimba yangu aliona ni bora ajitenge mbali na mimi ili nisijue na alikuwa anawaza abebe au asibebe maana alikuwa hana imani na mimi kabisa. Kwa upande wake aliamua kutengeneza trap ili ajue tabia yangu, kwani aliamini mimi siwezi kukubali kuishi bila mchepuko na wasiwasi wake ulikuwa kwa Asmah na alitafuta spy wake wa kufuatilia movement zangu na Asmah.

MIMI: “Kwa hili umezingua sana ni vile una damu yangu nisingekusamehe, na kwanini umeshika mimba bila ridhaa yangu?”

IRYN: “Stupid question, you cummed inside me and now pretending to ask why I’m pregnant?, ulitakiwa ufurahi sijafanya maamuzi mabaya kwa mambo unayo fanya.”

MIMI: “Alright mimi nimepokea hili jambo kwa mikono miwili na niko tayari kuwa baba, lakini naomba kwasasa usije home maana mama J kashaanza kuhisi something fishy kinaendelea kati yetu.”

IRYN: “Naomba umuheshimu mama J, mimi nimechagua kuwa hivi ila Insider letme tell you something, nikija kubaini una mwanamke mwingine nje na mimi huyu mtoto hutakuja kumuona machoni mwako, kama kweli unampenda huyu mtoto bhasi naomba utulie, sasa fanya mistake kama utakuja kumuona mwanao na niko serious sitanii.”

MIMI: “Mimi nimechagua mtoto na naomba uniamini mimi sina huo ujinga please.”

IRYN: “I’m just warning you usije ukafikiri natania fanya ujinga na hutokuja kuniona mimi na mwanao.”

MIMI: “Baby usindoke mpaka mwisho wa mwezi nataka niendelee kukaa na wewe na Ahsante kwa kunibebea mtoto najua hii ni heshima umenipa.”

IRYN: “Sawa darling mimi nitaondoka mwisho wa mwezi kwaajili yako.”

Saa yangu ilikuwa inaonesha ni saa 5 usiku na mimi nilisema siwezi kulala pale kwa Iryn, lazima nirudi home, hivyo ilibidi nimuage.

MIMI: “Baby mimi naondoka kwenda home see you tomorrow mapema.”

IRYN: “No problem msalimie mama J.”

Tulitoka wote mpaka parking na aliniaga kwa kuni kiss shavuni na nikaondoka maeneo yale, lakini wakati niko njiani nilikuwa nawaza sana suala la mimba ya Iryn, nilihisi kama ndoto hivi na nikajisemea kesho nitakwenda naye hospital ili na mimi nikajihakikishie.

Nilijisemea kama kweli nitaprove Iryn ana mimba yangu nitamfanya kuwa mchepuko wangu wa siri na siji kuchepuka na mwanamke mwingine yoyote. Hata ile kauli yake aliyosema nikifanya ujinga sitamwona mtoto ilikuwa ikinijia sana kichwani na kutoka na nilishindwa kujua kwanini asisitizie sana hili.

Asubuhi niliamka mapema sana, niliingia kuoga na nikaondoka kwenda kwa Iryn. Baada ya kuwasili pale kwake alikuwa bado kalala na ilibidi nimpigie simu na akatoka kunifungulia mlango.

MIMI: “Good morning mama kijacho.”

IRYN: “Hahaha good morning too darling, bora umekuja mapema ili twende na supermarket tukipata breakfast.”

MIMI: “Twende nikakusaidie kuandaa breakfast.”

Tuliingia jikoni wote na yeye alikuwa anapika chapati za maji na mimi nilikuwa nina tengeneza soup. Wakati tunapata breakfast nilimwambia tutakwenda hospital wote ili nikajihakikishie kuhusu mimba yake.

Mchana tuliondoka kwenda Masaki na tulianza kwenda SALI International hospital ambayo ipo Masaki near na Coral hotel. Baada ya kufika pale na kufuata taratibu zote tulipelekwa chumba special kwaajili ya kuchukuliwa vipimo vya ultra sound na mimi nilikuwa pembeni nikishuhudia.

Ukweli niliweza kujihakikishia kwa macho yangu Iryn ni mjamzito na nilimsogelea Iryn akiwa bado kalala na nikamkiss,

MIMI: “Baby you’re going to be a mom, I’m proud of you.”

Kwa upande wake Iryn alikuwa na furaha sana kwakweli na doctor alikuwa anaongea pale afu alikuwa mhindi,

DOC: “Hongereni sana mimba ni salama na haina shida kabisa na hakikisha unamlinda mjamzito anakuwa salama na anakula chakula bora.”

MIMI: “Doc hili ondoa shaka kabisa.”

Nilichukua simu yake na nikampiga picha akiwa vilevile tumbo wazi kama ukumbusho.

Doctor alitupongeza san na alitupa ushauri na akasema itapendeza tukichukua vipimo kwa wote mpaka vya damu. Tuliona ni ushauri mzuri ukitegemea tunakwenda kuwa wazazi ni busara tukajuana, baada ya vipimo majibu yalionesha sisi ni wazima wa afya kabisa na hatuna kasoro wala shida yoyote.

Tuliondoka hospital kwa furaha sana na tulikwenda moja kwa moja mpaka Salon, ilituchukua chini ya dakika 5 kuwasili ofisini na nilipark gari tukaingia ndani.

Baada ya kuingia ndani Hilda aikuwa yuko pale reception na tukamsalimia wote kwa pamoja na Iryn alikuwa anapita kila room kuwasalimia wafanyakazi na mimi nilikwenda ofisini.

Ndani ofisini alikuwepo Asmah na baada ya kuniona alianza kunimind sana kwa kumchomesha jana ukizingatia tulikuwa tumekubaliana vizuri kabisa. Kwa upande wangu ilibidi nimwombe msamaha kwa suala la jana na nikampa sababu za uongo ili atulie.

Haikuchukua muda Iryn aliingia ofisini na akakaa kwenye coach na akawa anaongea na Asmah pale,

IRYN: “Asmah mpenzi wangu unaendeleaje na mguu wako?”

ASMAH: “Niko poa dear, thanks kwa Insider kanisaidia sana mpaka nimekuwa sawa.”

Kwa upande wangu nilijifanya niko busy na mambo yangu kama siwasikii vile kumbe sikio langu lilikuwa linadaka mawimbi vizuri sana.

IRYN: “Alinambia alikuwa anakupigisha tizi, I’m glad umepona

ASMAH: “Thank you so much bossy, Insider ana Roho nzuri sana.”

IRYN: “Asmah wewe sijawai kukupa gift ila nitakupa gift nzuri sana, mimi nitaondoka soon nataka nikuachie ukumbusho.”

ASMAH: “Jamani unaondoka kwenda wapi tena?”

IRYN: “Nakwenda shule dear.”

ASMAH: “Thank you bossy nitashukuru sana.”

Saa 3 usiku tuliondoka pale ofisini na tulipitia pale Golden fork Mikocheni kupata dinner kwanza. Baada ya kuwasili pale tulitafuta angle nzuri ya pembeni tukakaa na tukaagiza chakula,

MIMI: “Baby wewe ni mjamzito tayari sitegemei kuona unatumia kilevi.”

IRYN: “I know baby siwezi nikatumia kilevi wala chochote chenye negative effects kwa mtoto tumboni. Baby leo si tunakwenda kulala wote?”

MIMI: “Baby nitarudi home sitaki kumkera mama J wangu, but good news anaondoka jumatano na familia yao kwenda kumalizia msiba Moshi so tutakuwa wote.”

IRYN: “Sawa no problem but nimekumiss sana”

MIMI: “Kesho nitakuja asubuhi na mapema kwako nikuf*ck mpaka useme poo.”

IRYN: “No problem wewe wahi home.”

Tulikaa pale mpaka saa 4 usiku na tukaondoka Iryn ndo alisimamia usukani na alinipeleka mpaka kwangu maana kupitia gari pale kwake niliona uvivu.

Baada ya kurudi home nilikuta wife na bibi wamelala lakini dada na Junior walikuwa seblen wamekaa, tangu Junior aanze kutembea alikuwa mgumu sana kulala na kukesha kwake ilikuwa ni kawaida. Niliingia room kuoga na baada ya hapo nilirudi seblen kumchukua Junior na tukaenda kulala.

Asubuhi niliamshwa na mama J na alikuwa akijaandaa kwenda kanisani,

WIFE: “Baba J hauendi church leo?”

MIMI: “Leo siendi mke wangu nimechoka sana afu kuna sehem nataka kwenda.”

WIFE: “Jana hujarudi na gari umeiacha wapi?”

MIMI: “Ndo huko nataka kwenda jana gari ilinizingua ipo kwa fundi.”

WIFE: “Mapema hivi? wamekuuzia mkweche bora ungeagiza Japan tu.”

MIMI: “Tatizo dogo tu sema jana tulikosa kifaa maduka yalikuwa yamefungwa.”

WIFE: “Na hii Dualis ya watu unarudisha lini?

MIMI: “Dada mpaka ajifungue nitampelekea gari yake, ameomba niendelee kukaa nayo, church leo unakwenda misa ya pili?”

WIFE: “Ratiba yangu ya kanisani ndo inaonesha hivyo, byee mimi naondoka mpenzi wangu.”

MIMI: “Niombee na ukirudi naomba tudiscuss suala la dada.”

WIFE: “Sawa pia tunaondoka jumatano kwenda Moshi kumalizia msiba na sina hela kipindi hiki.”

MIMI: “Badae tutaongea hili.”

Baada ya wife kuondoka sikutaka hata kwenda bafuni kuoga na nilijisemea nitaoga hukohuko kwa Iryn, nilibadilika chap na nikachukua bodaboda nikaondoka.

Niliwasili kwa mama kijacho wangu mapema sana na baada ya kuingia ndani yeye alikuwa jikoni anaosha vyombo na nilimkumbatia kwa nyuma, tukaanza kuongea pale,

IRYN: “Baby ulikuwa hupokei simu zangu.”

MIMI: “Nilikuwa nimepanda bodaboda nisingeweza kupokea, umepika nini nasikia njaa hapa.”

IRYN: “Kuna maziwa mkate na maini”

MIMI: “Acha nijisevie wewe endelea na kazi zako.”

IRYN: “Badae itabidi nikamsalimie mama J na Junior.”

MIMI: “Sawa ni wewe tu ila utakwenda peke yako”

IRYN: “No problem I will go there alone.”

Baada ya kupata chai mimi nilikwenda kuoga na baada ya nusu saa Iryn alikuja chumbani na tukaanza kwichikwichi pale, ila ilikuwa ni ile kwichi ya taratibu sana maana alikuwa mjamzito.

Mchana tuliamua kwenda kubarizi beach na tulikwenda Malaika beach haipo mbali na apartment yake. Wakati tuko pale tulikuwa tunaongea masuala mengi na kuhusu masomo yake huko South Africa, kwa upande wangu nilitaka kujua atawezaje kusoma akiwa na mimba?

MIMI: “Baby unakwenda shule utaweza mikiki na hali hii?”

IRYN: “Baby hata sio tatizo masters haina mambo mengi na nitafanya vizuri.”

MIMI: “Claire best yako yuko wapi?”

IRYN: “Tulikwenda Serengeti wote so wakati tunarudi tuliachana, yeye alikwenda Bukoba kutembelea kaburi la baba yake.”

MIMI: “Pole yake na vipi kuhusu suala la mimba yako mama Janeth na Mzee utawaambiaje?”

IRYN: “Usiwe na wasiwasi juu ya hili, Daddy nitamwambia mimba ni yako japo anajua wewe unamtoto, mama Janeth nitakuja kumwambia hata badae huko.”

MIMI: “Wasiwasi wangu mama Janeth akijua mimi ninafamilia afu nimekupa mimba, anaweza akaniona mimi mbaya sana na akanichukia kwa hili.”

IRYN: “Haya ni maamuzi yangu na si yake hata wale watoto zake wote kila mmoja ana baba yake, afu nimegundua siri kubwa sana kwa mama Janeth.”

MIMI: “Siri gani hiyo mummy.”

IRYN: “Tuachane na haya mambo baby not even important.”

Saa 12 tuliondoka pale beach na tulirudi home, lakini Iryn hakukaa na aliondoka kwenda kumsalimia mama J na mimi nilimwambia atanikuta namsubiri.

Baada ya Iryn kuondoka nilichukua simu yangu nikasema acha leo nimtafute Muajemi maana tulikuwa tunapishana sana na pia alikuwa hapatikaniki, nilimpigia simu kupitia Telegram lakini hakuwa online na nikamtumia ujumbe wa kumsalimia.

Baada ya lisaa kupita alinipigia simu na tuliongea mambo mengi sana, kubwa aliulizia maendeleo ya Iryn na mimi nilimwambia anaendelea vizuri na anatarajia kurudi shule kusoma, kwa upande wake alisema Iryn amemblock kwani hampati kwa call wala texts.

MIMI: “Bro! habari ya siku umekuwa adimu sana.”

MUAJEMI: “Niko salama salmini tunapishana nimekuwa busy sana, kwasasa nashinda sana Sudan na hope kuja Tanzania next month tutaonana bro, Iryn ulifikia wapi maana ulinihakikishia”

MIMI: “Bro! Iryn hana shida ila tatizo ni wewe kuwa na familia na ameachana na bwana wake wa Ufaransa kwasababu ya hii, amesema kwasasa anahitaji mwanaume asiye na familia wa kufocus naye.”

MUAJEMI: “Ohh shit, kaka nilikosea sana kumwambia nina familia.”

MIMI: “Haukukosea kaka ulikuwa sahihi kabisa, wewe ukirudi huku tutaongea vizuri, ila mwezi huu anakwenda South Africa kuendelea na masomo.”

MUAJEMI: “Unajua ameniblock nashindwa hata kumjulia hali.”

MIMI: “Mtafute hata kwa namba nyingine uzuri ana kufahamu won’t it be a problem.”

MUAJEMI: “Bro acha nikukimbie tutawasiliana.”

Baada ya kuagana na Muajemi nilikwenda zangu kukaa kwenye balcony nikipigwa na upepo mwanana wa bahari na pembeni nilikuwa na glass yangu ya wine. Ni maisha ambayo sikuwai kudream kuyaishi kama kuna siku nitakuja kaa kwa balcony namna hii, maisha kama haya nilikuwa nayaona kwa movie tu.

Baada ya dakika 20 nilisikia mtu akiniita “Baby… baby…” ni Iryn alikuwa karudi tayari, na alikuja nilikokuwa nimekaa.

MIMI: “Nambie mummy za huko ulikokuwa na umeonana na mama J?”

IRYN: “Ndo natoka hapa na nimeshinda nao, kama unavyoona ndo narudi hapa.”

Na akanikalia mapajani,

“Darling mama J kama anahisi something kinaendelea between us ila sasa naomba udownload snapchat na tutakuwa tunachat huku atleast ni safe.”

MIMI: “Haina shida nitafanya hivyo ila nafikiri tuwe tunawasiliana kwa simu, text ziwe kwa masuala muhimu na ofisi, snapchat kwa usiku.”

IRYN: “Ndo hivyo maana wewe ni mzembe sitaki kuingia uadui na mama J nampenda sana, ila kwa hili atanisamehe.”

Muda huu tulianza romance pale na tulihamia chumbani kuendeleza lecture mpaka wazungu walivyotoka darasani ndo na mimi nikasitisha lecture yangu, nikajiandaa na kuondoka kurudi home.

Baada ya kuwasili home niliingia chumbani na nilikuta box la simu ya iphone na baada ya kuliangalia niligundua ni la iphone 14 na ilibidi nishangae pale inamaana wife amenunua simu mpya?.

Baada ya wife kuingia chumbani uvumilivu ulinishinda na ikabidi nimuulize,

MIMI: “Mama J unalalamika huna Pesa afu unanunua iphone 14.”

WIFE: “Iryn ameniletea simu mpya kama zawadi, kipindi Junior anaiharibu hii simu yangu tulikuwa wote ile siku hapa home.”

MIMI: “Ooh hongera zako iko wapi niione?”

Na wife alikwenda seblen akaniletea na baada ya kuiona ilikuwa ni Iphone 14 pro Max na ilikuwa ni mwezi tayari tangu apple wa lunch simu zao mpya.

Nilitoka chumbani nilikwenda seblen kukaa na bibi na tulikuwa tunapiga story mbalimbali pale hasa za Moshi huko. Bibi ni mwongeaji sana hivyo tulikuwa tunapatana ile mbaya na alikuwa ananikubali sana.

***
Asubuhi na mapema sana niliamka kama kawaida nilikwenda jogging na baada ya kutoka tizi niliingia bafuni kuoga, nikaondoka kwenda kwa Iryn.

Baada ya kufika kwa Iryn alinipa taarifa inatakiwa kwenda Masaki kuangalia nyumba zao maana zilikuwa zinakarabatiwa na ukarabati ulianza wakati mzee amekuja.

Tuliondoka kwenda Masaki na tulianza kwanza na nyumba tuliyokwenda kuitembelea kipindi kile katoka South Africa ambayo aliachiwa na baba yake aisimamie. Baada ya kuwasili pale ilikuwa imekarabatiwa tayari kwa upande wa nje na ilikiwa imepakwa rangi inang’aa, kwa upande wa ndani mafundi walikuwa wanatengeneza furniture.

“Darling twende nyumba nyingine ipo mtaa wa pili.”

Na mimi nilishangaa pale kumbe kuna nyumba nyingine tena, baada ya kuwasili hio nyumba nyingine hata haikuwa mbali na tulitumia muda mfupi kufika mjengoni. Ilikuwa ni apartment nzuri sana ya gorofa 3 na ilikuwa inafanyiwa ukarabati na kulikuwa na msimamizi aliyepewa tenda na walikuwa wanaongea na Iryn.

Iryn baada ya kumaliza kuongea na jamaa alikuja kwangu na tukaanza maongezi

MIMI: “Na hii ni nyumba yenu?”

IRYN: “Mzee alinionesha alivyokuja alisema ameinunua recently, si unamkumbuka yule baba aliyekuja kumchukua mzee siku ile pale Coral hotel?”

MIMI: ”Ndio mummy namkumbuka.”

IRYN: “Ndo aliyemuunganishia mzee, sasa baby hizi nyumba zote na zile za mama ziko under my control ni zangu, mimi naondoka ila nitahitaji uwe unanisaidia kuzikagua, nina imani kubwa sana na wewe maana unakwenda kuwa baba mtoto wangu, naamini huta ni let down.”

MIMI: ”Hili jambo dogo sana naomba ondoa shaka, umebeba damu yangu afu nishindwe kusimamia hizi nyumba hapana kwakweli wewe ushakuwa mke wangu tayari.”

IRYN: “Twende kule kwenye zile apartments za mama nikafanye na ukaguzi.”

Episode za nyuma nilishaandika hii nyumba ya mama yake ilipo na code ipo wazi kabisa ni Masaki na baada ya kufika pale tulifanya ukaguzi na tukaondoka.

IRYN: “Baby unanipeleka kula wapi?”

MIMI: ”Kuna chimbo alinipeleka Asmah Ijumaa ni zuri sana kwa barbecue nafikiri utaenjoy.”

IRYN: “Okay twende baba mtoto.”

Ndani ya muda mfupi tuliwasili Pantaleo na tulipokelewa na mhudumu na tukaagiza chakula pale,

MIMI: “Dada naomba chips kwa mishikaki 5 ya samaki.”

IRYN: “Dada mimi naomba mishikaki ya kuku 3 na chips yai ikaushe vizuri.”

Tulitumia lisaa pale restaurant na tuliondoka kwenda Salon, baada ya kuwasili Iryn alishuka na kimfuko kidogo amekishika mkononi na tuliongozana mpaka ndani ofisini. Mle ofisini tulimkuta Asmah na Hilda wanapiga story na sisi tukawasalimia.

IRYN: “Asmah bora nimekuona mamaa nina gift yako hapa.” Na akamkabidhi pale.

“Open it..”

Na mimi ilibidi niangalie ni zawadi gani hiyo Iryn anampa Asmah?, na muda huu Asmah alitoa box la simu kwenye ule mfuko na ilikuwa ni iphone. Kwa upande wake Asmah aliishia kufurahi sana muda huu, licha ya kuwa na iphone kali lakini alipewa tena ingine na Iryn.

ASMAH: “Wow thank you bossy.”

IRYN: “Nimeamua kukupa gift ya simu ambayo nilikuwa naitumia mimi ili nikiwa sipo uwe unanikumbuka kwa kuchapa kazi kwa bidii, hio simu ni mpya kabisa maana nilikuwa naitunza sana.”

ASMAH: “Nashukuru sana bossy wangu Allah akuzidishie, na kuanzia leo nitaanza kuitumia hii.”

Kwa upande wangu nilijisemea Iryn katoa zawadi ya simu kwa Asmah huenda ana target zake anataka kuzikamilisha. Kwa upande wa Asmah yeye alikuwa kafurahi sana kwakweli na sura yake ilikuwa na furaha na yenye tabasamu.

Tuliendelea kushinda pale ofisini mpaka jioni na tukaondoka kwenda Mikocheni.


PART II

Jumanne jioni wife aliondoka kwenda kwao pamoja na bibi na dada kwaajili ya kujiandaa na safari yao ya jumatano kwenda Moshi kumalizia msiba. Niliwapa ride mpaka kwao na sikutaka kuendelea kukaa pale ukweni, hivyo nikaondoka kurudi home nikachukua baadhi ya nguo na nikaenda kwa mama kijacho wangu.

Baada ya kuwasili pale kwake niliingia ndani lakini sikumkuta lakini mazingira yalionesha yupo, nikajua kwa muda huu atakuwa swimming. Na mimi nilibadilika haraka nikaenda kwa swimming pool na kweli alikuwa anaswim pale na baada ya kuniona alionesha kufurahi sana, nikaingia kwa swimming na tukaanza kuswim pamoja ilikuwa ni burudani.

IRYN: “Baby mama J ameondoka tayari?”

MIMI: “Amekwenda kwanza kwao ila kesho asubuhi na mapema wataanza safari ya kwenda Moshi.”

IRYN: “Baby huu muda uliobaki nataka niondoke hapa nikamalizie sehemu nyingine.”

MIMI: “Unataka kwenda wapi?.”

IRYN: “Nitafute Apartment ya muda Masaki.”

MIMI: “Sawa ni wewe tu mimi nitakupa kampani.”

Wakati tukiendelea kupiga story na kuswim kwa upande mwingine kuna couple ilikuja pale swimming na sisi tukaamua kuondoka ili tuwaachie uwanja. Baada ya kurudi ndani tulibadilika na tuliamua kwenda Mlimani city kupata dinna.

Penzi lilikuwa ndo kama limechipua limeanza upya maana tulikuwa tumekaa kimahaba sana hata mtu akituona bhasi anajua wale ni wapenzi.

IRYN: “Baby guess mtoto atakuwa jinsi gani?”

MIMI: “Huyo wa kiume 100%.”

IRYN: “Napenda mtoto wa kiume but nilitamani nikuzalie wa kike ili ubalance afu wa pili awe wa kiume.”

MIMI: “Sidhani kama atakuwa wa kike kwa tarehe za mimba kupatikana na uhakika ni wa kiume huyo.”

IRYN: “Mungu naye ana mipango yake.”

MIMI: “Baby unakwenda kuwa mama ulijipanga au bahati mbaya?”

IRYN: “I don’t want to talk about this right now.”

MIMI: “Seems ulijipanga ndomana unafuraha sana.”

IRYN: “You know nothing.”

MIMI: “You are going to be the best mom.”

Baada ya kumaliza kula hatukutaka kupoteza muda na tuliondoka kurudi home na baada ya kuwasili nilichukua wine kwenye glass nikaenda kukaa kwa balcony huku napata upepo mwanana wa Bahari.

Baada ya dakika 20 Iryn naye alikuja akiwa amevaa gauni shati, inakuwa inashuka kidogo mapajani, hakuwa na bikini na akanikapandia kwa juu huku akinitizama kwa tabasamu sana na macho ya kurembua.

Aliingiza mkono ndani ya track na akaanza kuchezea bunduki yangu lakini ilikuwa iko tayari kwa vita muda mrefu sana, aliikalia kwa juu na alikuwa anaendesha gari taratibu na kwa umakini mkubwa sana na baadae tuliamua kuhamia chumbani kuendeleza match yetu pale kitandani.

Iryn ni mwanamke ambaye alikuwa hanipi limit hasa linapokuja suala la sex, nikipata hamu hata awe jikoni, seblen bhasi nitam-f*ck hana noma, na hiki kilinifanya nivutiwe naye na nimpende sana. Akiwa jikoni anapika nikiingiza mkono nikamshika kalio na hata kuliminya ndo kwanza alikuwa anafurahi, nikimkuta seblen nitafungua braa yake nitazinyonya boobs zake ndo kwanza ananipa ushirikiano, sasa kafanye huu ujinga kwa mama J kama hupigwi na mwiko huko jikoni.
•••••
Asubuhi niliamka mapema sana na nikaenda gym kupiga tizi, kwenye hizi apartments kuna room special ya mazoezi kwa wapangaji wa pale. Baada ya kutoka tizi niliingia bafuni kuoga na nikatengeza breakfast nikanywa lakini mama kijacho alikuwa bado kalala na mimi nikaondoka kwenda kazini.

Nilianza na Mikocheni kwanza na baada ya kuwasili nilikwenda ofisini kuanza kuzipitia ripoti zote za utendaji mpaka mauzo. Baada ya nusu saa Lucy aliingia ofisini na alikuwa anafika muda huu na baada ya kuniona tulisalimiana pale na alionesha kuwa na umbeya anataka kunipa,

LUCY: “Insider mambo, Iryn ni mjamzito?”

MIMI: “Sijui nianze kujibu salamu kwanza au swali?”

LUCY: “Salamu not important kwasasa, twende kwenye swali.”

MIMI: “Mimi sijui kwakweli ndo nasikia kwako hapa ila namuona sawa tu.”

LUCY: “Jana nimeona utofauti mkubwa sana kwake, alikuwa anatema sana mate hovyo na sio kawaida yake mpaka nikahisi ni mjamzito.”

MIMI: “Labda alikuwa anaumwa rafiki yangu au kuna kitu kilikuwa kimemchefua huwezi kujua, kutema mate hovyo sio kigezo cha mtu kuwa na mimba.”

LUCY: “Mh! Insider wewe ni msiri sana kama umemjaza si unasema tu mshikaji wangu utaendelea kunificha mpaka lini?”

MIMI: “Siwezi kukuficha kwa hili maana mimba haifichiki kama mahusiano itajitokeza tu, mimi naondoka kila kitu kipo sawa, labda kama kuna jambo lolote niambie kabla sijapotea.”

LUCY: “No.”

Niliondoka kwenda Masaki na wakati naendelea na majukumu yangu kwa upande mwingine simu yangu ilianza kuita na alikuwa ni Iryn akipiga na nilipokea simu yake kwa haraka sana.

Mama kijacho alikuwa analalamika nimeondoka bila kumuaga na akaniomba niwahi kurudi kwani ameni- miss. Kwa upande wangu sikutaka kuchanganya mapenzi na kazi hata kama natembea na bossy niliona suala la kazi lazima niliheshimu.

Mchana niliaga kwa Asmah naondoka na wakati natoka tulikuwa tumeongozana huku tunaongea,

ASMAH: “Insider unabahati kubwa sana wewe mwanaume kuwa na mwanamke mzuri na mrembo hata mimi nakuonea wivu.”

MIMI: “Umejuaje kama ananipenda?.”

ASMAH: “Anaonekana tu amekupenda serious, utulie sasa kama una mambo pembeni acha.”

MIMI: “Ahsante kwa ushauri wako mama.”

Niliamua kuondoka na nikarudi home maana Iryn alikuwa ananipigia sana simu mpaka kero na kama kudeka kuliongezeka.

Baada ya kufika home nilimkuta amelala seblen na alivyoniona alitabasamu na akanambia amepika tayari, hivyo alikuwa akinisubiri mimi tu ile tule.

Tulishinda wote mle ndani na ule usiku alinambia jumamosi tutakwenda makazi mapya na amepata apartment tayari ya kukaa kwa huu muda.

Dalali aliyetafuta hii apartment ni ile kampuni inayosimamia nyumba za Masaki katika upangishaji. Kwa upande mwingine alisema tukiondoka hapa ndo mazima na itabidi tukabidhi kabisa apartment ya watu japo alikuwa kabakisha mwezi mmoja.

*****
Jumamosi ndo tulikuwa tunaondoka Kwenye ile apartment ya Kawe na ile asubuhi tulianza kupanga vitu, Iryn kwa upande wake alikuwa hahitaji kuchukua kitu chochote zaidi ya nguo. Kuna vitu vingi pale nilivichukua vya muhimu kama JBL music soundbar, washing machine nknk, na kuna baadhi ya vitu tulimpa mama mlinzi.

Mchana tuliondoka pale na tulianza safari ya kwenda Masaki maana Dalali alikuwa ametuma location na anatusubiri. Apartment ilikuwa Toure road karibu na Golden Tulip hotel, baada ya kuwasili pale tulionana na Dalali, akatupeleka mpaka juu floor ya 3, niseme apartment ilikuwa ni nzuri sana, inavutia, na mazingira yalikuwa mazuri sana ndani mpaka nje, ni 5 star apartment na zilimtoka pesa mingi the bossy lady.

Baada ya kumalizana na Dalali tuliagana na akaondoka akatuacha sisi tumekaa seblen, apartment ilikuwa ni full furnished yaani inakila kitu ndani ni wewe kwenda na nguo zako tu na vitu vya jikoni.

IRYN: “Baby badae tunakwenda wapi nahamu tutoke out.”

MIMI: “Twende Maison club leo maana sijawahi kuingia pale, nilikuwa naishia kuwapeleka wateja tu.”

IRYN: “Okay baby tutaenda huko.”

MIMI: “Unakumbuka hutakiwi kunywa?”

IRYN: “Nitakunywa mocktail.”

Sababu huwa sipendi Iryn asumbuliwe kutokana na status yake ilibidi nifungue page yao ya Instagram na nikafanya booking ya table mapema kabisa.

Saa 2 usiku tulitoka kwenda kupata dinna na kwa upande wa Iryn alikuwa kapendeza sana na niliishia kumsifia njiani kote mpaka tunafika Karambezi cafe. Baada ya kuwasili pale restaurant mhudumu hakuchelewa kuja kutusikiliza na tukaagiza chakula na tukaendelea kupiga story pale huku tukisubiri food.

MIMI: “Baby ukienda South Africa utakuwa unakaa home?”

IRYN: “Nitakaa kwanza home then nitahamia kwenye apartment yangu.”

MIMI: “Kwanini usikae home na hio mimba?”

IRYN: “Kuna mdogo wangu mtoto wa mamkubwa nimemtafutia chuo South Africa so nitaishi naye pamoja, usiwe na wasiwasi baby mwanao atakuwa sawa na salama.”

MIMI: “Mamdogo hana shida? Si unajua mama wa kambo?”

IRYN: “Hana shida kabisa na ananipenda sana hata nilivyo hairisha safari amechukia sana.”

MIMI: “Natamani ningekupa hii Dunia kama zawadi pamoja na vitu vyake vyote lakini sina huu uwezo.”

IRYN: “Baby no need uliyoyafanya kwangu yanatosha, kwasasa ni zamu yangu kukupa hii Dunia. Insider wewe ndo mwanaume pekee uliyenifanya mimi kuwa na furaha, kifo cha mama yangu kilinipa mawazo sana mpaka nilijukuta namchukia daddy but today I’m happy because of you.”

MIMI: “Mimi naamini Mungu alikurudisha Tanzania kwaajili yangu na mimi nakuahidi sitokuwa na mchepuko mwingine zaidi yako na ninahapa hapa mbele yako.”

IRYN: “Insider mimi nimekupenda toka moyoni na nimeridhia kuwa mke wako wa pili kama utanipa hii nafasi.”

MIMI: “Dini yangu hairuhusu mimi kuwa na wake wawili lakini kuwa na mtoto wangu nmekupa hiko cheo.”

IRYN: “Thank you baby please tell me unataka nikufanyie kitu gani kama shukrani yangu kwako? Please tell me.”

MIMI: “Baby zawadi ya mtoto uliyonipa kwangu mimi inatosha ila nakuomba uniahidi uyo mtoto utamtunza maana utakuwa mbali na mimi.”

IRYN: “Mtoto wako nitamtunza baby ondoa wasiwasi, najua utakuwa unamiss sana ila nitakuwa nakuja Dar kwaajili yako each after 2 weeks. Tutakuwa tunashinda wote hotelini weekend nzima, but nihakikishie tutakuwa tunashinda pamoja.“

Baada ya kusikia haya maneno nilifurahi sana maana nilianza kuwaza Iryn anaondoka, coochie yake sitaiona tena na uwezo wa kwenda South mara kwa mara sina.

MIMI: “Really baby? utakuwa unakuja kwaajili yangu?”

IRYN: “I promise, baby naomba utafute passport ili nawewe uwe unakuja South Africa nataka pia twende Dubai, Paris, UK, na Netherlands nknk huko kote kuna ndugu zangu.”

MIMI: “Sawa baby hili nitalifanyia kazi soon.”

Tuliongea mambo mengi sana na Iryn na muda ulikuwa umekwenda sana, kwani saa 4 ilitugongea palepale Karambezi na tukaondoka kwenda Maison Club. Kilichofanyika ni kubadili parking tu maana Maison imepakana na Seacliff Hotel ni building zilizofuatana.

Tuliingia Maison club na tulipelekwa kwenye table yetu na mhudumu na muda huu alikuwa akisikikiza odda zetu ili atuletee vinywaji. Sababu Iryn alikuwa hanywi ilibidi aagize Mocktail na mimi Niliagiza cocktails na nilikuwa nakimbiza na shots za Tequila.

Kwa upande mwingine walikuwa wanaonekana warembo wakali sana na watu waliokuwa wanaonekana wengi ni madon. Maison huwezi kuwapata wazamiaji kwani kuingia tu lazima ufanye booking au uwe na status, huwezi kuwakuta maskini huku.

Tulidance pamoja sana huu usiku ni kama ilikuwa napewa farewell ya mwisho mwisho, kutokana na uzuri wake mama kijacho wangu aliishiwa kupigwa macho sana, na hili mimi nilikuwa nishazoea tayari na nilikuwa najiona mwamba sana kuwa na moja ya mwanamke mrembo hapa Duniani. Sisi hatukujali na tuliendelea kupeana mahaba motomoto na tulikaa mpaka saa 8 za usiku wakati mziki umeanza kukolea ndo tukaondoka kwenda kulala.

Asubuhi niliamshwa kunywa soup na alikuwa kaniandalia na viazi, baada ya kunywa nilikuwa bado na hangovers maana zilikimbiza sana shots za tequila kule Maison, hivyo nilirudi kulala tena, haikuchukua muda na yeye alikuja tukalala wote.

Mchana tulitoka kwenda kupata lunch kwenye mgahawa wa karibu na wakati tuko kwa restaurant tukipata chakula, Iryn alinambia tukirudi home kuna surprise yangu inanisubiri na mimi nilibaki najiuliza ni surprise gani tena hii?

“Baby unataka kuni surprise nini?”

“Wewe utaona hapohapo.”

Baada ya kumaliza kula tuliondoka kurudi kwenye apartment yetu na tuliingia bafuni kuoga pamoja na baada ya kumaliza alinifuta maji na taulo mwizi mzima.

IRYN: “Baby lala kitandani nataka leo nikufanyie massage utoe na uchovu.”

MIMI: “Hii leo kweli surprise nasubiri huduma yako mummy.”

Kwa upande wake alikuwa kavaa tight fupi nyeupe na sport braa nyeupe hivyo alikuwa anaonekana romantic na sex sana.

Baada ya kulala kitandani alitoa vifaa special kwaajili ya massage, na alitoa kitambaa cheupe kipya kabisa akaenda bafuni na akatoka amekilowanisha maji na akakitumbukiza kwenye heater special.

IRYN: “Baby kabla ya kufanya massage unatakiwa kukanda mwili wako kwa maji ya moto, sasa hiki kifaa ndo kazi yake hii. Si unaona nilikilowanisha na maji? Na hii heater ni special kwa kupashia joto, na hiki kitambaa ni special kwa massage na kinatunza joto kwa muda mrefu na huwa naviagiza nje.”

Baada ya dakika 3 kilikuwa tayari na alianza kunikanda kuanzia shingoni mpaka miguuni na nilikuwa nimelala chali, muda huu nilikuwa nasikia raha sana.

IRYN: “Nimeona tuanze na front side then tumalizie na back, na mara nyingi huwa napenda kufanya hivi kwa strangers.”

MIMI: “Kwanini baby?”

IRYN: “Ni hivi, upande wa mbele huwa unasisimua sana hasa kwa wanaume na hapa wengi huwa wanapata mawazo ya ngono, ukianza na mbele atapata hizi hisia na ukimalizia upande wa nyuma hisia zinakuwa chini sana. Hii ni mbinu nzuri sana kama unadeal na customers/strangers ambao huwafahamu, itakusaidia kupunguza kusumbuliwa kuombwa sex. Kwa wazungu hawana shida lakini tatizo ni waafrica na wengi wanachukulia massage ni kama sehemu ya kupata sex na sio huduma.”

MIMI: “Aisee kumbe wazungu sio wasumbufu kama waafrica.”

IRYN: “Wazungu wanaheshimu utu na anavyokuja lengo ni huduma na sio ngono, na wanaheshimu hii kazi ila waafrica wanaona kama kujiuza unavyofanya hii kazi.”

MIMI: “Ni kweli kabisa unayosema mummy.”

IRYN: “Mimi nafanya professional massage hata hivi vifaa nilivyonavyo sidhani kama kuna massage hapa bongo wanavyo labda hizi 5 star hotel na ni expensive sana.”

Na muda huu alitoa stones nyeusi na akaziweka kwa heater na akaendelea kuongea,

“Inatakiwa mteja asiwaze ngono anavyokuwa kwenye room, ki professional inatakiwa umtoe customer kwenye mawazo ya ngono na aone massage ni treatment na sio sehemu ya kupata ngono.”

MIMI: “Baby kivipi?”

IRYN: “Ni simple tu naweza kutumia natural au artificial way, wewe utaona si tupo wote hapa?”

Iryn alitoa kitu kama mask na ilikuwa inafunika macho tu na alitoa airpods zake akaziweka masikioni na akanivalisha ile mask, na akaplay music wa taratibu kama ile ya wataliano.

Muda huu alinza kunifanyia massage taratibu na kwa ufundi wa hali ya juu sana afu ukizingatia mikono yake ni laini afu ya moto. Nilikuwa nasikia raha sana hata mawazo ya ngono nilikuwa sina, ile mask aliyokuwa kanivalisha na ule mziki niliokuwa nausikia nilikuwa nahisi niko Dunia nyingine kabisa.

Niligeuka upande wa nyuma na alianza kuukanda mgongo kwanza kwa kitambaa cha moto then akaanza massage taratibu. Baadae alitoa zile stone kwa heater na akaziweka mgongoni kwa ufundi wa hali ya juu sana kwenye mti wa mgongo, raha nilizokuwa nasikia hapa ni balaa maana nilikuwa sayari nyingine kabisa.

Hakuishia hapa alitoa kifaa kama gun akawa anakipitisha mgongoni na alisema ni special kwa kunyoosha misuli, kuna muda alitoa kifaa kingine na kilikuwa kama kinanikanda mgongo na alisema kile ni special kwa kunyoosha mifupa ya uti wa mgongo.

Ni massage iliyotumia kama lisaa na nusu na baada ya kumaliza niliona utofauti mkubwa sana maana nilikuwa naona mwili umekuwa mwepesi sana ni kama nimeshusha mzigo vile.

MIMI: “Baby nasikia utofauti mkubwa sana kwenye mwili wangu.”

IRYN: “Umewaza ngono? maana nimechezea sana bunduki yako.”

MIMI: “Hamna mummy nilikuwa nafeel unaichezea lakini sikuwa nawaza ngono kabisa.”

IRYN: “Kama nilivyokwambia massage ni treatment na sio sehemu ya kupatia ngono, ila kwa hapa bongo mmezifanya kama sehemu za kupatia ngono hakuna massage mnazofanyiwa.

MIMI: “Kwa hii massage uliyonifanyia nimeamini wewe ni mtaalamu.”

IRYN: “Na vifaa vingi sana humu ndani, utazidi kuviona taratibu tukiendelea kufanya aina nyingine za massage.”

MIMI: “Baby na body to body massage inakuaje?”

IRYN: “Hiyo nitakufanyia siku nyingine japo mimi nilikuwa napenda sana kuitoa hii huduma kwa wanawake.”

MIMI: “Baby na hiyo chupa ya mafuta ni aina gani maana naona niko sawa sina mimafuta.”

IRYN: “Haya ni special for massage na ukimaliza yanakauka yenyewe kwa haraka sana”

MIMI: “Baby njoo na mimi nakufanyie massage.”

IRYN: “Mhhh really?.”

Nilimvua nguo zote na nikaanza kumfanyia massage upande wa mbele na alikuwa ananielekeza kila hatua na nikawa namfanyia kupanda juu kushuka chini, usawa wa matiti yake na baadae nilimgeuza upande wa nyuma nikaendelea kumfanyia massage. Lakini wakati nachezea makalio yake nilikosa uvumilivu na nilijukuta zoezi linabadilika na tukaanza kusex maana nilichomeka mashine kwa nyuma wakati yeye akiwa kalala kifudifudi.

Massage niliyopewa na Iryn ilikuwa ni best mpaka nikajisemea kwanini napata hizi raha mwishoni?.
(Nilifanyiwa kwanza massage na maelezo alinipa baadae maana wakati nafanyiwa massage nilikuwa Sayari nyingine.)

Jioni tulikubalina tukale dinna capetown na wakati tunakwenda tulipitia pale Salon kuwapa hi na sisi tukaendelea na safari yetu. Muda tunaopata diner pale Capetown Iryn alinambia next week before hajaondoka itabidi akae pamoja na timu yote ya Masaki na Mikocheni ili awaage na pia mama Janeth atakuwa karudi kwani alikwenda Ukraine kikazi.

Baada ya kupata dinner tuliendelea kukaa pale kwa muda mrefu, kwa Jumapili panakuwaga pazuri sana pale Capetown. Tuliendelea kukaa pale mpaka saa 4 usiku ndo tukaondoka kurudi kulala.

*****
Jumatatu mchana niliondoka na Asmah kwenda Mikocheni kuonana na Lucy ili tujadiliane suala la kikao kabla ya kutoa taarifa kwa team.

Tulikutana Golden fork ili tupate na lunch na baada ya kuwasili pale tulimkuta Lucy amefika akitusubiri mimi na Asmah. Tuliagiza chakula na mazungumzo yalikuwa yanaendelea, kwa upande mwingine Iryn alikuwa anataka kikao kianze mapema ili tupate lunch na dinner ya pamoja na baada ya hapo tungeenda kumalizia kiwanja chochote tutakacho kipenda.

Tulikubaliana pale tufanyie kikao chetu Serena Hotel na tukampa kazi Asmah ya kuanza kufuatilia ukumbi mapema na kuhusu kumalizia tuliona SamakiSamaki ingekua ndo sehemu nzuri, kiwanja pendwa.

Baada ya kumaliza maongezi mimi na Asmah tuliondoka kurudi Masaki lakini kwa upande wangu baada ya kumuacha Asmah niliamua kurudi nikakae na Iryn. Kipindi hiki nilikuwa sitamani kabisa kukaa mbali naye nilikuwa natamani muda wote tuwe wote, na njiani nilikuwa nimemchukulia pizza kwaajili ya lunch.

Baada ya kurudi nilimkuta Claire seblen na sikutegemea kama ningemkuta pale na tuliishia kusalimiana,

MIMI: “Ooh Claire za wewe sikutegemea kukuona hapa imekuwa surprise.”

CLAIRE: “Actually nimerudi jana nilikuwa Bukoba huko.”

MIMI: “Baby alinambia aisee, pole sana na za huko lakini kwa ujumla.”

CLAIRE: “Nilienda salimia ndugu zangu na kudhuru kabuli la baba.”

MIMI: “Ulifanya jambo jema shem wangu na mke wangu yuko wapi?”

Na muda huu Iryn alikuwa amekuja seblen akitokea jikoni,

IRYN: “Niko jikoni napika baby.”

MIMI: “Nilikuwa nimekuletea pizza mummy kumbe upo jikoni.”

IRYN: “Thanks hii nitaila badae.”

Tulishinda na Claire pale mpaka usiku na tukamsindikiza mpaka Marina na sisi tukarudi home kulala.

Wiki hii tuliendelea kuweka mambo sawa kuhusu kikao chetu na ile jumatano Asmah alikuwa kafanikisha suala la kufanya booking kwaajili ya kufanyia kikao chetu cha mwisho na Bossy lady.

Kwa upande mwingine Iryn dalili zake za mimba zilizidi kuonekana day after day na alianza kutapika na kupenda kula vitu vichachu vichachu na upendo wake kwangu ulizidi kuongezeka kwa kasi sana.

Siku ya alhamisi mama J alinipa taarifa kuwa jumamosi watarudi Dar lakini hatorudi home, dada wa kazi bado anawasalimia ndugu zake na kuna sintofahamu inaendelea kule kwao kuhusu dada, kwani hawataki arudi tena Dar.

Kwa upande wangu hizi taarifa zilinishtua pia,

MIMI: “Dada Junior asiporudi inakuwaje? kupata mtu kama yeye itatuchukua muda sana na hiki ni kipindi kibaya sana ukizingatia bado week urudi chuo.”

WIFE: “Mwenyewe nimechanganyikiwa hapa, baba yake alimtelekeza kuhusu shule ila sasa anasema anataka kumrudisha shule, dada anasema mzee wake ni muongo hana imani naye.”

MIMI: “Alright fanya hivi, ongea na familia yake hasa mamdogo wake na mwambie watuachie kwa mwezi mmoja huku tunatafuta dada mwingine, kwasasa tulikuwa hatuja jipanga na december atarudi.”

WIFE: “Shida ni Mzee wake anasema hataki kuona bint yake anarudi Dar tena na kama atafanya hivyo atatoa taarifa Police.”

MIMI: “Ongea kama nilivyokwambia maana kwasasa hakuna shule labda mwakani, omba wakusaidie kwa hili afu dada tutakaa naye chini tuone tunamsaidiaje, uyo Mzee wake nahisi kapatwa na wivu tu.”

WIFE: “Sawa nitakupa mrejesho.”

Siku ya Ijumaa mama Janeth aliwasili Tanzania na kubwa alikuwa karudi na binti yake Janeth, Iryn alisema twende tukamsalimie pale kwake na pia mama Janeth aliomba waonane akirudi. Kwa upande wangu nilikuwa nashauku kubwa sana ya kumuona live Janeth maana nilikuwa najua anasoma chuo huko Ulaya na nilikuwa naishia kuziona picha zake tu.

Saa 1 usiku tuliondoka kwenda kwa mama Janeth na tuliweza kupokelewa na Janeth pale seblen na waliishia kukumbatiana na Iryn kwa furaha sana na walionekana kumisiana.

Iryn alifanya utambulisho pale kwa lugha ya kiingereza,

“Insider huyu ndo Janeth mwenyewe mtoto wa kwanza wa mama na alinitambulisha mimi kwa Janeth kama Manager wa kampuni yao na mama yake.”

Janeth ni mzungu kama mama yake ni kazuri kwakweli na baada ya ule utambulisho tulisalimiana kidogo na waliendelea kuongea na Iryn. Niligundua Janeth kaja kumsalimia mama yake na hatokaa sana ataondoka kurudi Ulaya kuendelea na masomo.

Ndani ya dakika 10 mama Janeth alitoka ndani na alikuja pale seblen na tulianza maongezi pale na tulikuwa tunajadiliana masuala ya kampuni. Tulikubaliana suala la Finance liwe chini yangu lakini Iryn atakuwa kama mshauri bado, kwa upande wake Iryn alisema ataendelea kutoa ushirikiano na hakuna kitakacho haribika.

IRYN: “Mama I trust Insider nina imani naye sana naamini nakuachia mtu sahihi kwako na hakuna kitakacho haribika. Toka tumpe majukumu mapya kampuni inafanya vizuri sana hata ukiwa haupo atafanya vizuri, kwenye masuala mengine tutakuwa tunawasiliana na still report nitakuwa nazipitia.”

MAMA: “Unajua ratiba niliyopewa nitakuwa ninashinda sana Ukraine kwaajili ya masuala ya kazi nilifikiri tumuongezee mtu mmoja Insider kwa masuala ya HR.”

MIMI: “Mama no need wafanyakazi waliopo wanatosha, Hilda yuko vizuri sana, Asmah yuko vizuri kwa kule Mikocheni Lucy yuko vizuri sana. Hapa naona masuala ya HR tutakuwa tunasaidiana wote na kama kuna ushauri nitakuwa nawasiliana na wewe kupitia email.”

IRYN: “Sumaiya yuko kule kwenye kampuni ya usafi sina shida naye kwenye suala la kazi na kesho nafikiri tuwe naye kwenye kikao.”

MAMA: “Sumaya yuko vizuri na tumepata tenda 2 kubwa na ikiwemo serikalini.”

IRYN: “Mama kesho baada ya kikao cha wote nafikiri tukae na viongozi tujadiliane.”

MAMA: “Insider umemuona binti yangu Janeth?.”

MIMI: “Mama nimemuona ni mzuri sana akimaliza chuo nitamuoa kama utanipa ridhaa.”

Mama Janeth alicheka maana hakutegemea mimi kuongea vile,

MAMA: “Hili ondoa shaka mimi nitakupa.”

Muda huu Janeth alikuwa hajui nacho ongea na mama yake maana Kiswahili anajua baadhi ya maneno kama salamu. Tulikaa kwa mama Janeth mpaka saa 4 usiku ndo tukaaga pale tukaondoka.

Saa 6 usiku Iryn alianza kulalamika anajisikia vibaya na alianza kutapika kwa kasi sana nonstop na alianza kulegea kama mtu mwenye homa. Kadri muda unavyozidi kwenda alizidi kubadilika, ilibidi tuondoke twende hospital na nilimpeleka pale SALI hospital, kwa upande wangu nilianza kuchanganyikiwa maana mpaka namshusha pale hospital hata kuongea alikuwa anazungumza kwa shida.

Niliwaza kumpigia simu mama Janeth lakini Roho ikasita maana angeweza kujua Iryn ni mjamzito na Iryn alisema ile mimba hakuna anayejua zaidi yangu tu. Muda huu mimi nilikuwa na wasiwasi sana kuhusu mimba maana niliwaza inaweza isije kuwa imeharibika, na nilijisemea kama itaharibika na hii basi mimi nitakuwa moja ya wanaume wenye mkosi hapa Duniani.

Nilikaa kwenye bench nikimsubiri na baadae niliruhusiwa kuingia ndani ili niwe naye karibu maana niliwaambia yule ni mke wangu. Nilimuuliza Doctor kuhusu mimba na alisema hana shida mimba iko salama ila ni homa ya kawaida kwani anapitia mabadiliko ukizingatia ile ni mimba yake ya kwanza.

Saa 10 usiku nilitoka pale hospital na nilirudi home ili kuandaa soup kwa upande mwingine nesi alinambia atakuwa anamuangalia hivyo nikamtengenezee haraka kitu cha kula, kwani alitapika sana.

Baada ya kurudi kwa apartment nilitengeneza soup ya kuku vizuri na nilitumia kama lisaa pale na nikarudi tena hospital na nilimkuta nesi yuko room. Niliingia na soup ikiwa kwa pot na muda huu Iryn alikuwa yuko macho akiniangalia na mimi nilimsogelea nikawa karibu yake.

MIMI: “Hi baby how are you feeling now.”

IRYN: “I’m fine baby, I’m feeling much better, thank you.”

MIMI: “Don’t say that baby uhai wako ni priority yangu ya kwanza.” Na nikamkiss mdomoni.

Muda huu Nurse dizaini kama alikuwa ananionea wivu nikimbembeleza mama kijacho wangu na yeye alikuwa akitabasamu.

“Baby nimekuletea soup unywe before haijapoa jana ulitapika sana.”

Nurse alinisaidia kumimina soup kwenye kibakuli na nilisubiri ipoe kidogo na nikaanza kumnywesha pale taratibu huku nambembeleza kwa maneno matamu na alikunywa soup yote akamaliza na nikampongeza.

NURSE: “Kwa hii spidi nafikiri asubuhi mtaruhusiwa kuondoka naona amerecover vizuri, Doctor akija atarecommend.”

MIMI: “Ahsante Nurse kwa kumsaidia mke wangu .”

NURSE: “Usijali ndo kazi yetu hii.”

Saa 3 asubuhi tuliruhusiwa kuondoka maana Iryn hali yake ilikuwa sawa na tulipewa dawa pale tukaondoka, kwa upande mwingine Asmah alikuwa ameanza kunipigia simu na alinipa taarifa yuko hotelini tayari anaangalia kama mambo yamekwenda sawa.

Kwa upande wangu nilikuwa nina wasiwasi sana na Iryn kuhusu Afya yake na niliogopa asije kuumwa tena huko hotelini kwenye kikao, lakini kwa upande wake alisema yuko sawa na nisiwe na wasiwasi.


PART III

Baada ya kurudi home nilimwambia Iryn apumzike kidogo na mimi nilikwenda jikoni kumtengenezea juice ya nanasi. Baada ya kunywa juice alikwenda kulala chumbani na mimi nilianza kufanya usafi washroom alikokuwa ametapikia.

Baada ya lisaa nilimuamsha ili ajiandae kwaajili ya kwenda kwa kikao na baada ya kujiandaa tuliondoka pale home, lakini ilibidi tumpitie mama Janeth maana aliomba kampani ya usafiri ya kwenda Serena.

Baada ya kumpitia mama Janeth pale kwake, alikuwa yuko tayari na tukaondoka kwenda eneo la tukio na tulitumia muda mfupi kuwasili hotelin. Tulikuta wafanyakazi wote walikuwa wamewasili tayari na baada ya sisi kufika tuliona tupate kwanza lunch mambo mengine yaendelee.

Baada ya kupata lunch kikao kilianza 14:30 na mimi ndo niliyeanza kwa kukifungua kwa sara fupi na nikatoa maelezo mafupi kuhusu lengo la kikao cha leo ni kumuaga Bossy wetu Iryn, wengi walikuwa hawajui hivyo hizi taarifa ziliwashtua sana. Na mimi sikutaka kupoteza muda hivyo nilimkaribisha Iryn aongee na alizungumza mambo mengi sana kwa team yake,

“Guys naona mmeanza kuwa na wasiwasi baada ya kupata taarifa za mimi kuondoka lakini naenda kufanya jambo la muhimu zaidi na lenye faida kwa kampuni yetu. Nakwenda kusoma masters South Africa sitakuwa na nyinyi physically lakini nitakuwa napata ripoti zenu, hakuna kitakacho haribika naamini Insider yupo na atawaongoza vizuri, kwangu mimi sina shida naye. Nawaahidi nitakuwa nakuja kuwatembelea na wale ambao watakuwa wana perform vizuri nitakuwa na bring zawadi kwa ajili yao.”

Baada ya Iryn kumaliza kuongea nilimkaribisha mama Janeth na yeye azungumze kidogo na alizungumza mambo mengi kuhusu utendaji wa kampuni na baada ya kumaliza nilikaribisha maoni, maswali, ushauri na mapendekezo.

Tulipokea mapendekezo na maoni mengi sana kutoka kwa wafanyakazi na mimi nilikuwa ninayaandika kwa notebook ili kuyafanyia kazi na kila mtu aliweza kuongea hii siku.

Baada ya kumaliza mama Janeth alianza kuongea tena na kubwa alisema atakuja mtalamu wa masuala ya Salon na atatoa mafunzo kwa baadhi ya wafanyakazi kwa muda wa week moja na anatoka Ulaya. Mama Janeth alisema hawezi kuwafundisha wote sababu ya gharama hivyo anahitaji watu wa tano tu wa kuanza nao na hawa ndo wataongeza ujuzi kwa wengine.

Mama Janeth alisema tupendekeze majina matano matatu (3) kwa Masaki na mawili (2) kwa Mikocheni. Mama alinambia nipendekeze majina mawili moja kwa Masaki na lingine kwa Mikocheni afu yanayobaki watapiga kura wenyewe.

Kwa upande wangu nilipendekeza Hilda kwa Masaki na kwa Mikocheni nilimpendekeza Julieth maana Lucy alikuwa anarudi shule hivyo sikuona sababu ya kumpendekeza. Baada ya kupendekeza watu wangu waliobaki zilipigwa kura na washindi wakajulikana, kwa Masaki alikuwepo Rebby.

Mpaka tunamaliza kikao ilikuwa ni saa 11 jioni hivyo tulitoka kupumzika pamoja na kupiga picha za pamoja. Mama Janeth alikuwa katembea na Camera yake na tuliomba mtu pale hotelini atupige picha za pamoja pale ukumbini na zingine nyingi tulipigia nje ya hotel kama ukumbusho. (Ukienda Salon ya Masaki utaikuta hii picha pale Reception).

Muda huu kila mtu alikuwa anapiga picha na Iryn mpaka Sumaiya naye hakuwa mbali kupiga picha na Bossy lady.

Saa 1 usiku tulipata dinner ya pamoja tena palepale hotelini na wakati tunakula nilitoa taarifa ya kukutana Samakisamaki baada ya dinner ili tukamalizie usiku wetu pale. Baada ya kutoa hii taarifa niliona sura za watu zikitabasamu na niliwaambia tukutane kuanzia saa 2 usiku maeneo yale na nimefanya booking ya meza za kukaa.

Baada ya dinner Iryn alitoa bahasha ndogo kwenye mkoba wake na nilimpa Asmah azigawe kwa kila mtu na Iryn alisema zile ni zawadi zake kwa kila mtu. Iryn alitoa neno la mwisho la kutuaga pale na kubwa alisisitiza uchapakaji kazi kwa bidii na ushirikiano.

“Guys mimi nawashukuru sana kwa siku ya leo niseme nime enjoy sana kuwa na nyinyi siku ya leo na niwaombe muendelee kufanya kazi kwa bidii na ushirikiano. Namba yangu mnayo kama unashida personal usiogope kunitafuta ili tusaidiane you know I love you guys, ninawaahidi nitakuwa narudi kuwasalimia. Hizo bahasha ni zawadi yangu kwenu na niwatakie usiku mwema lakini msisahu tutakutana pale Samakisamaki, nataka kila mtu anywe anachotaka, msikose.”

Baada ya kuondoka sisi viongozi tulibaki kwaajili ya mazungumzo ili kuweka mikakati ya pamoja kuhusu kampuni ikiwemo kupeana majukumu mapya, pia mama Janeth alipendekeza mishahara iongezwe kidogo ili kufidia.

Kwa upande wa Salon hakukuwa na mambo mengi sana lakini kwa upande wa Usafi Sumaiya aliomba aongezewe mtu mmoja ili kuongeza nguvu. Mimi nilishauri tutafute mtu ambaye ana elimu ya Fedha au Uchumi ili wasaidiane kwenye masuala mbalimbali ya tender, miradi nknk. Na hii nafasi nilimuunganisha jamaa yangu, mpaka sasa anaendelea na majukumu yake pamoja na Sumaiya.

Ni kikao kifupi kilicho chukua kama nusu saa na baada ya kumaliza tuliagana pale na Mama Janeth alisema atakuja Samakisamaki kutupa kampani. Wakati tunatoka mimi nilibaki na Asmah na Hilda mle ukumbini na tukawa tunaongea pale na kubwa niliwapa pongezi kwa kusimamia kikao kwenda vizuri.

MIMI: “Asmah nafikiri mkajiandae ili tukutane Samaki, Hilda utawahi kweli mpaka Kigamboni?”

ASMAH: “Asmah nakaa naye pamoja kwa kipindi hiki.”

MIMI: “Ooh sawa sikujua hili.”

Nilishangaa sana kuona Asmah na Hilda wamekuwa mabest kwa muda mfupi sana, nilimvuta Asmah pembeni na tukaendelea na mazungumzo.

MIMI: “Nambie pesa iliyobaki ni kiasi gani?”

ASMAH: “Nina kama milioni moja na laki mbili something.”

MIMI: “Kazi iliyofanyika ni kubwa na mmenikosha sana hiyo pesa tutagawana wanne ila wewe na Hilda utachukua parcent kubwa.”

ASMAH: “Poa Insider but….”

MIMI: “But what.?” Ilibidi nigeuke kumsikiliza maana nilikuwa nishaanza kuondoka pale.

ASMAH: “You look great today, wahi bhana Iryn anakusubiri.”

MIMI: “Sawa bhana nashukuru pia.”

Baada ya kutoka niliwakuta Iryn na Sumaiya wanaongea wanacheka pale reception utafikiri sio wale watu ambao hawapatani. Na mimi ilibidi nishangae kwakweli maana sikutegemea kuona kuna siku Iryn na Sumaiya watakuwa wanacheka pamoja namna hii.

Baada ya kusogea pale karibu, Sumaiya alianza kuongea,

SUMAIYA: “Insider leo mimi na Iryn ugomvi hatuna.”

MIMI: “Kwani mlikuwa na ugomvi? Mbona hili sijawai kulijua.”

SUMAIYA: “Leo kafunguka ukweli kuwa mpo kwenye mahusiano na hapa ndo tulikuwa tunagombana kuleta ubossy wake kwenye mapenzi. Kwakua leo kanifungukia ukweli kuwa anakupenda niseme leo nabariki mapenzi yenu kwa moyo mweupe kabisa na sina kinyongo.”

IRYN: “Thank you mamaa.”

SUMAIYA: “Nataka kuona unamzalia Insider mtoto, tule na wali kabisa. Namuheshimu sana Insider kwa hizi taarifa ulizonipa, heshima yangu kwako itaongezeka.”

Nilishangaa pale hivi ndo huyu Sumaiya naye mjua mimi? Kwa Upande mwingine alikuwa kashika macho 3 nikasema huyu atakuwa kapewa simu, haiwezekani Sumaiya kuturn kwa haraka hivi, na mimi ilibidi nipoteze hii mada,

MIMI: “Baby mama Janeth yuko wapi?”

IRYN: “Katangulia kwenye gari tuondoke.”

Tuliagana na Sumaiya pale maana uber ilikuwa imemfuata tayari na sisi tukaelekea Parking tuliko park gari tukaondoka. Tulianza kumdrop mama Janeth pale kwake na akasema haina haja ya kuja kumfuata na atakuja mwenyewe pale Samakisamaki na sisi tukarudi kwenye apartment yetu.

Baada ya kuwasili pale nilikuwa naona Iryn kama hayuko sawa hivi maana alikuwa anaonekana kuwa mchovu sana,

“Baby are you ok?”

“Yeah niko poa baba mtoto I’m just tired.”

“Pole sana tuna 1 hour ya kupumzika tutakwenda saa 3 pale au kama vipi wewe lala tu.”

“Baby today’s my day I have to go.”

Saa 3 usiku tuliondoka kwenda maeneo na kwa upande mwingine team ilikuwa imewasili muda mrefu na mimi nilikuwa nimewapa taarifa kwenye group waagize wanachotaka kunywa.

Iryn alitoa offer kila mtu aagize kinywaji anacho jisikia kunywa usiku huu ila yeye kwa upande wake aliishia kuagiza Mocktail. Wapo waliagiza moet, Jameson na Hennessy yaani iikuwa ni burudani huu usiku na baada ya dakika 20 mama Janeth alikuja na bint yake Janeth na tukaendelea kunywa.

Mama Janeth alishangaa kuona Iryn anakunywa Mocktail na Iryn alimwambia yuko kwenye dozi hawezi kutumia alcohol. Pembeni yangu kulia alikuwa amekaa Sumaiya na Chupa yake ya Moet na tulikuwa tunapiga story pale,

MIMI: “Mshikaji wangu ni nini nyuma ya pazia kinaendelea wewe na Iryn? amekununua tayari?”

SUMAIYA: “Hamna chochote, nilikuwa naongea naye ndo akanambia nimpe heshima kwani tayari ni wifi yangu ndo nikafurahi kusikia hizi habari na toka muda mrefu nilikuwa najua Iryn anakupenda.”

MIMI: “Naona una macho 3 ndomana nikauliza usije kuwa umenunuliwa.”

SUMAIYA: “Hahahahaa hii kaniletea mama Janeth zawadi Insider, jana alinipigia simu nikachukue.”

MIMI: “Hongera sana I told you mama Janeth anakupenda sana.”

SUMAIYA: “Bahati tu kama wewe ulivyolamba asali kwa mrembo hapo. Insider kuanzia leo nakupa respect katika vitu ambavyo umenikosha ni pamoja na hili suala, hii pisi ni kali umetisha sana. Naona Iryn kabadilika ndani ya muda mfupi, kipindi kile nilikuambia huyu nyege zinamsumbua ukawa hunielewi, unaona sasa hata aibu anakuonea kuonesha unamkaza vizuri.”

MIMI: “Sumaiya acha kuropoka bhana ushaanza kuelewa wewe.”

SUMAIYA: “Be serious Moet ya kunisimbua mimi kichwa? na leo nakunywa tatu hizi.”

MIMI: “Wewe leta masihara kesho video zako zianze kutrend youtube, huzijui vizuri moet.”

Saa 6 usiku mama Janeth alituaga pale na aliondoka na binti yake, baada ya lisaa nilifanya malipo kwa kuchanja maana nilikuwa na card ya Iryn mfukoni. Baada ya kufanya malipo tulisogea meza zote kuwaaga na tulianza na ya kina Lucy na tukamalizia na ya kina Asmah. Mikocheni na Masaki walijitenga.

Tuliondoka kurudi kulala na baada ya kufika kwa apartment na kuingia chumbani Iryn alinisaidia kuvua nguo na mimi nikamsaidia kuvua zake na aliomba tusex pale.

MIMI: “Baby si unaumwa?”

IRYN: “Please f*ck me niko sawa kabisa.”

Baada ya kupitisha mkono wangu alikuwa wet tayari na nilikutana na joto kali sana muda huu na mimi nilimpa alichokuwa anataka, sikutaka mkamia ukizingatia alikuwa mjamzito.

Jumapili asubuhi Iryn aliniomba tukamchukue Junior ili ashinde naye siku nzima na jioni ataonana na mama J ili amuage, maana alisema kuondoka bila kumuaga haitakuwa jambo la busara.

Baada ya kupata soup aliniaga anaondoka kwenda kwa mama Janeth na akirudi tutaondoka kwenda kumchukua Junior. Muda huu mimi niliingia kujiandaa na baada ya kumaliza nilimpigia simu wife ili kumpa taarifa za kwenda kumchukua Junior lakini hakuwa anapokea simu, nikahisi atakuwa church hivyo nikampigia simu mdogo wake kumpa taarifa.

Wakati najiandaa nilikuwa nawaza hivi mama J akija kujua Iryn ana mimba yangu itakuwaje? au akija kujua nimezaa naye hapo baadae atachukua hatua gani?, ni maswali ambayo hata kwangu yalikuwa magumu lakini nilisema kila kitu kinatokea kwa mipango ya Mungu, hivyo sitakiwi kujilaumu kwa hili.

Baada ya masaa 2 Iryn alirudi na mkononi alikuwa kashikilia kimfuko na akanipa pale,

IRYN: “Baby take your gift.”

MIMI: “What is it?”

IRYN: “Just look.”

Niliangalia na kutoa box la Playstation 5 game, sikutegemea kukutana na hii zawadi ukizingatia enzi zangu za ujobless nilikuwa nacheza sana PlayStations na masela.

MIMI: “Baby thank you so much.”

IRYN: “Atleast itakukip busy usiwe unawaza wanawake.”

MIMI: “Sasa baby nitacheza na nani?”

IRYN: “Kuna game za kucheza alone sio lazima ucheze na mtu.”

MIMI: “Tuondoke tuwahi kwa Junior hata mimi nimem-miss mwanangu.”

Ilikuwa ni saa 6 mchana wakati tunaondoka Masaki na tulianza safari ya kwenda ukweni na njiani tulikuwa tunaongea sana,

IRYN: “Baby, Junior na mdogo wake watapishana miaka miwili sindio.?”

MIMI: “Exactly”

IRYN: “I wish wakue pamoja ili wajuane kuwa ni ndugu but ndo hivyo tena haitowezekana.”

MIMI: “Damu ni nzito kuliko maji watakuja kujuana tu.”

IRYN: “Hili suala liko chini yako na wewe ndo mwenye maamuzi.”

MIMI: “Ndomana nimekuambia watajuana tu.”

Baada ya kuwasili ukweni nilimchukua Junior na yeye baada ya kuniona aliishia kunifurahia na sikutaka kuendelea kupoteza muda pale ukweni, hivyo nilimuaga shem wangu nikaondoka pale.

Baada ya kuwasili kwa gari Iryn alimpakata Junior na tukaendelea na safari lakini tulikuwa hatujui tunakokwenda na mwisho wa siku tukakubaliana twende Mlimani city ili akacheze na watoto wenzake.

Baada ya kuwasili Mliman city tulikwenda kwanza kufanya shopping ya mtoto ambapo Junior aliweza kununuliwa nguo, viatu, toys bila kusahau gari nyingine kubwa ya kuendesha. Baada ya kutoka hapo tulikwenda sehemu ya watoto lakini kuna baadhi ya michezo Junior hakuruhusiwa kucheza sababu ya utoto lakini kuna baadhi aliruhusiwa awe na mtu wa kukaa naye karibu. Kw upande wangu nilimwacha na mama yake mdogo wakicheza na nilikwenda kukaa pale Samakisamaki nje nikiendelea kubuy time.

Baadae walitoka na wakaanza kucheza kwenye majani mbele ya Samakisamaki na jinsi alivyokuwa anacheza na Junior ungesema ni mwanae hata watu walikokuwa around pale bila shaka walijua ni mtoto wake. Kwa upande mwingine Junior naye anampenda sana Iryn hanaga noma kabisa na walikuja pale nilikokuwa nimekaa na aliomba funguo ya gari ili akambadilishe mtoto pampas na akirudi tule lunch.

Tulishinda Mlimani city mpaka jioni na tuliamua kuondoka, lakini Iryn aliomba tupitie kwanza Kijitonyama ili akamsalimie Rose na kumuaga kabisa. Baada ya kuwasili kwa Rose alitukaribisha ndani na alifurahi sana kutuona maana ilikuwa ni muda mrefu kidogo umepita tangu Iryn aondoke pale.

Tulitumia kama lisaa pale na tukaagana na Rose na sisi tukaondoka kuelekea na uelekeo wa Bagamoyo Road, ilikuwa ni saa 1 usiku tayari na tulikuwa tumekubaliana na mama J tukutane pale Kibo complex.

Baada ya kuwasili Kibo complex tulipanda mpaka floor ya kwanza, kuna restaurant ambapo mama J alikuwa akitusubiri. Tulifika kwenye meza aliyokuwa amekaa na tukaagiza chakula cha pamoja na story zilikuwa zinaendelea.

MAMA J : “Dear nilikuwa church leo siku nzima nimeshindwa hata kuwa pamoja na wewe.”

IRYN: “Usijali za huko Moshi? hope kila kitu kilienda sawa.”

MAMA J: “Tulimaliza salama, vipi hajawasumbua huyu chautundu?”

IRYN: “Kama unavyoona hajasumbua kabisa, na leo kaenjoy sana.”

MAMA J : “Junior anti anakuacha hutamwona tena.”

IRYN: “No nitamuona bhana nitakuwa nakuja Dar dear.”

MIMI: “Dada wa kazi mmefikia wapi?”

MAMA J : “Atakuja jumatano, Mzee amesema akiwa tayari atapiga simu ili arudi Moshi.”

MIMI: “Habari njema itabidi akirudi tukae naye chini tuone tunafanyaje maana kupata dada kama yule sijui.”

IRYN: “Dada anaondoka?”

MAMA J : “Baba yake aligoma asirudi Dar na mimi sababu anataka kumrudisha shule, nimewaomba wanisaidie kwa muda ndo amesema December mwishoni arudi.”

IRYN: “Poleni sana dada anampenda sana Junior.”

MIMI: “Hata Junior anampenda kuliko mama yake, ndomana hizi taarifa zilinishtua ukizingatia tumekaa na dada kama ndugu yetu.”

Mimi niliamua kutoka na Junior pale ili niwape uwanja wa kuzungumza wake zangu na mimi nilikuwa nacheza na Junior kwenye korido za mle ndani. Baada ya dakika 20 walikuwa wame Maliza mazungumzo yao na ilibidi tuondoke maeneo yale na mama J alifanya kurequest usafiri wa kuwarudisha kwao.

Baada ya kurudi home ule usiku Iryn alianza kubadilika tena na alikuwa kama mtu mwenye homa na alikuwa kalala kwenye coach, na mimi nilikuwa nikimchezea tumbo lake.

MIMI: “Baby naona unabadilika twende nikupeleke hospital.”

IRYN: “Mida hii ndo huwa nakuwa hivi lakini soon nitakuwa sawa.”

MIMI: “Doctor alisema sababu ni mimba yako ya kwanza inaweza kukusumbu sana.”

IRYN: “Baby hii ndo mimba yangu ya kwanza kukaa kwenye kizazi na sijawahi kuwa na historia ya kutoa mimba kwenye maisha yangu.”

MIMI: “Unajua mimi huwa siamini kama kweli umeachana na Grizz afu umekuja kuangukia kwangu.”

IRYN: “Kwakuwa unakwenda kuwa baba mtoto leo nitakuweka wazi sababu ya mimi kuachana na Grizz. Truly nilimpenda sana hata mke wake alivyokuja kufound out haikuwa sababu ya mimi kuachana naye, lakini nilikuja found out alitembea na best yangu Isabella. Pia alianza kunivunjia heshima kuniomba vitu ambavyo siwezi kuvifanya, wewe ni mtu mzima nadhani umeelewa.”

MIMI: “Pole haiwezi kukuharibia uhusiano kwenye biashara zenu?”

IRYN: “Before sijaamua kuachana naye nilikuwa tayari nina plan B ndomana sikuwa na wasiwasi tena na kama faida nimepata ya kutosha, pia kumbuka ile ni kampuni kama atafanya uhuni ninauwezo wa kushtaki mahakamani. Nashukuru alinielewa ile siku na mimi nilimwambia nina mtu wangu nataka kufocus naye kama yeye alivyo focus kwenye familia yake.”

MIMI: “Siku akija kujua huyu mtoto ni wangu itakuwaje?”

IRYN: “Hakuna tatizo why hujiamini Insider? kwamba huna hadhi ya kunizalisha?.”

MIMI: “Sijamaanisha hivyo naongelea jinsi Grizz anavyoniheshimu afu ajue nilikuwa nakula demu wake, unafikiri atanielewa?”

IRYN: “Bila mimi ungemjua Grizz?.”

MIMI: “Tuachane na hayo na hiyo Plan B unayoongelea una mpango gani?”

IRYN: “Kuna best yangu tulisoma wote chuo ni Mfaransa, kuna project tunataka kufanya pamoja na next week atakuja South Africa, tukifika muhafaka nitakwenda Ufaransa pia.”

MIMI: “Mimi nakuelewa mummy unapambana sana mkifika muhafaka utanambia ni project gani.”

IRYN: “Usijali baby ile pesa aliyonipa mama nataka niizalishie isikae kwa bank tu.”

MIMI: “Wazo zuri sana kwa hili nakuunga mkono.”

IRYN: “Twende tukalale baby.”

****
Jumatatu asubuhi baada ya kuamka Iryn alianza kupanga nguo zake kwenye bag kwaajili ya safari na mimi nilikwenda jikoni kutengeneza breakfast.

Baada ya kupata breakfast ile asubuhi tuliamua kwenda Coral beach kupoteza muda na baada ya kuwasili pale, tulikwenda moja kwa moja mpaka beach. Kule beach tulikuwa kwenye dimbwi zito la mahaba maana ndo ilikuwa siku ya mwisho kuspend tukiwa pamoja, tulitumia muda mwingi kupanga mipango mbalimbali ya maisha.

IRYN: “Baby mtoto akiwa wa kiume nitampa jina mimi ila akiwa wa kike utampa jina wewe, deal?”

MIMI: “Deal baby, but nawish awe wa kike.”

IRYN: “I wish too Darling iwe hivyo ili ufurahi.”

Mchana tulipata lunch tukiwa palepale Coral na nilimwambia turudi kwa apartment ili apumzike kwaajili ya safari ya baadae. Matokeo yake baada ya kurudi badala ya kumpuzika tulianza kusex na ilikuwa ni sex moja tamu sana ya mwishomwisho.

Jioni tulijiandaa kwa pamoja kwaajili ya kwenda Airport na Iryn alipendeza sana na niliishia kumsifia pale, lakini kwa upande mwingine nilikuwa naumia kuona akiondoka na kuniacha mkiwa na ilikuwa ni miezi 9 tayari toka tukutane kwa mara ya kwanza.

Tuliondoka jioni na tulipitia kwa Claire waagane na baada ya hapo tuliendelea na safari yetu ya kwenda JNIA terminal 3. Baada ya kuwasili Airport tulikaa pale cafe tukiendelea kubuy time na muda huu tulikuwa tunapiga story za mwisho.

IRYN: “Baby ulikutanaje na mama J mpaka mkafikia kuzaa pamoja.?”

MIMI: “It’s long story kama tulivyokutana na wewe tu, na siamini miezi 9 tuliyokaa ni kama miaka.”

IRYN: “Baby mimi naona unawasiwasi I promised you nitakuwa nakuja kwaajili yako huna haja ya kuwaza hili.”

MIMI: “Baby usijekuwa umebeba ujauzito lakini nyuma ya pazia una mipango yako.”

IRYN: “Hapana baby siwezi fanya hivyo naomba utambue nakupenda sana, na kama utavunja makubaliano yetu huyu mtoto hutakuja kumwona kabisa kwenye maisha yako, so promise me baby.”

MIMI: “Baby siko tayari kumkosa mwanangu kwa upumbavu wangu you have my word.”

IRYN: “You have my word too like I said before sitokuwa na mwanaume mwingine zaidi yako na niko tayari kukuzalia watoto wengine kama utahitaji, naomba utambue nakupenda sana.”

MIMI: “Don’t say that I love you too.”

IRYN: “Baby the first time tumekutana pale Marina nilikupenda, baada ya kujua una familia honestly niliumia sana na nilijaribu sana kukaa mbali na wewe lakini sikufanikiwa, nilijikuta naumia zaidi. Naomba utambue wewe ndo mwanaume pekee uliyeweza kurudisha furaha yangu na kunionesha maana ya maisha, nimekupa huyu mtoto kama zawadi yangu kwako na utambue wewe ni baba halali wa hiki kiumbe tumboni na huyu mtoto atakuwa ukumbusho kwangu Kwako.”

MIMI: “Nashukuru kwa kunipa hadhi ya kuwa baba mtoto wako, I love you baby.”

IRYN: “Baby tambua wewe una thamani kubwa sana kwangu na nina kuheshimu sana, pia ninafuraha ya wewe kuwa baba mtoto.”

MIMI: “One more thing baby before hatujaagana, naomba niambie exactly wewe ni nani? nikiangalia status ya mama yako, mama Janeth na Mzee wako inanipa maswali sana. Sometimes ninawaza mambo mengi sana juu yako nakosa majibu kabisa, nashindwa kuelewa wewe ni nani.”

IRYN: “Baby huna haja ya kuwa na wasiwasi na mimi, ningekuwa mtu unayemfikiria hata nisingebeba hii mimba. Muda umewadia wa kucheck-in na nimepitiliza, sitamani kukuacha but nitakuona soon my love.”

Mimi nikiwa bado kwenye mshangao sijui niseme nini, muda huu Iryn alifungua mkoba wake na alitoa card ya bank ile alonipa kipindi kile Dodoma,

“Baby nakupa hii card yangu ya bank kuna pesa humo zimebaki zitakusaidia, naomba pia umpe nguvu mama J kwenye biashara zake anazofanya nataka wewe ndo ulifanye hili jambo. Kuhusu wewe sitaki kukupangia matumuzi ya kufanya na nikirudi next time tutaongea suala la project ya kule Dodoma.”

MIMI: “Thank you baby but usijali kuhusu mama J nitaliweka sawa na liko kwenye mipango yangu.”

IRYN: “Baby naomba upokee hii card otherwise utanikera na sitoondoka.”

MIMI: “Sawa baby nashukuru kwa hili.”

IRYN: “Baby umepokea kwa mikono miwili?naomba utambue nakwenda kuwa mzazi mwenzako, na ninafanya hili toka moyoni, umeipokea hii card kutoka moyoni?”

MIMI: “Yes baby thank you so much, usiwe na wasiwasi.”

IRYN: “Nita transfer hizi amount zije kwenye account yako na hio card utanisaidia kuichoma.”

MIMI: “Sawa baby ondoa wasiwasi.”

Tulianza kupeana makiss pale bila kuwa na aibu na baada ya dakika 5 tulisogea mpaka usawa wa kuingia ndani ili acheck-in na tulikumbatiana kuagana. Sasa wakati nimetembea hatua mbili mbele nikisikia akiniita tena “Baby….”, na akarudi kwangu spidi,

“Baby… hujamuaga mwanao.”

Na mimi niliinama nikamkiss tumboni na yeye alishia kufurahi na kwa haraka alinipa tena kiss na akaniachia. Ni kitendo ambacho kilivuta sana attention ya watu maana mwanamke aliyekuwa akifanya vile ni mrembo na amekamilika kila idara.

Iryn aliendelea kunikumbatia na macho yake kama yalianza kutoa machozi,

IRYN: “Baby I’m leaving now, I’ll see you soon.”

MIMI: “I love you too baby byee it’s time.”

Na mimi nilimsubiri mpaka anaingia ndani na akaishia kunipungia mkono na mimi nikaondoka kurudi parking ili niondoke.

Baada ya kurudi parking niliingia kwa gari na nilitulia pale kwa dakika 10 huku nikiwaza,

“Iryn anakwenda kuwa mama mtoto wangu hivyo sina jinsi lazima nikubaliane na hili jambo, mimba yake ni mipango ya Mungu sina haja ya kulaumu na hili suala litabaki kuwa ni siri yangu, familia yangu nitawaambia hapo baadae sana mtoto akikua na mama J nitakuja kumwambia hapo baadae sana. Kwasasa natakiwa kutulia na nifocus na familia yangu, mama J na Iryn wananitosha kwasasa, sinahaja ya kuhangaika na wanawake wengine acha nifocus na kufanya maendeleo.”

Simu yangu ilianza kuita pale na alikuwa ni Mama J akipiga na nilitabasamu kuona simu yake pale na niliipokea.

“Baby nakuja kukuchukua turudi home na tukapate dinner ya pamoja.”

Na niliwasha gari nikaondoka kwa fujo sana pale JNIA nikiwa na Audi Q7.

THE END

Wiz Khalifa- Cameras[emoji444]

Email: insiderman1@yahoo.com

The Money Already Printed You Just Gotta Go Get It. Thank you for your time since July
[emoji120]
Insider, hongera na pia pole pole kwa uliyoyapitia.

Ushauri wangu kwako. Fanya kila namna usimpoteze Irene wala mama J. You can do it if you want, you're the man. Everything is possible.
 
Kuna mwamba mwingine mtoto wa buguruni wakuitwa BM X6 sijui naye aliishiaga wapi?? Kuna waandishi wakali mno, ila hawamalizi simulizi, sijui Ni ubize au Ni kitu gani jamani. Ila ninawaombea kheir mpate muda mmalizie stori zenu
 
EPISODE 47

“A TRUE STORY BY INSIDER MAN”

CONTINUE…..

Muda ule ilibidi nishangae kwanza maana niliona Muajemi kama karogwa hivi na sio akili zake. Niliona Muajemi ni kama hajitambui na hajui anafanya nini.

MUAJEMI: “Bro! unaionaje hii gari? Nataka umpelelekee Iryn kama zawadi.”

MIMI: “Bro! ushailipia tayari hii gari?”

MUAJEMI: “Bado nataka kwanza utoe comment then nifanye malipo ili uondoke nayo.”

Na kipindi hiki chote kulikuwa na Jamaa mwenye asili ya uarabu akiwa makini sana na sisi. Maana alijua kabisa gari imeuzwa anasubiri maokoto tu kutoka kwa Muajemi.

MIMI: “Bro! samahani naomba tuongee mara moja then tutarudi.”

MUAJEMI: “Sawa haina shida, unataka tuongelee wapi?”

MIMI: “Nafikiri twende pale mbele kuna kamgahawa tukae kabisa.”

Tulitoka pale na tulikwenda moja kwa moja mpaka Mgahawa wa Best bite na tulikaa pale tukaanza maongezi.

MIMI: “Bro! najua una mapenzi na upendo wa kweli kwa Iryn. I really appreciate your efforts, nimekuwa na wewe bega kwa bega toka mwanzo mpaka sasa, lakini kwa hili sikuungi mkono kabisa.”

MUAJEMI: “Kwanini Bro! mimi nafanya kutoka moyoni kabisa na nilikuwa na mpango wa kumnunulia gari toka muda mrefu sana.”

MIMI: “Sawa Bro! cha kwanza inatakiwa utambue unadeal na aina gani ya mwanamke. Iryn hana shida na gari ni vile hajataka kununua na hata akitaka gari mama yake aliacha Range sport mpya kabisa ipo kwa mama yake mlezi. Haya yote unafanya ili uweze kumuwin lakini unashindwa kutambua Iryn sio dizaini ya Wanawake wenye njaa. What if kama nitampelekea zawadi ya gari na akaikataa? umejaribu kuwaza hivi? Na vipi kwa upande wako utajisikiaje?.”

MUAJEMI: “Kaka upo sahihi sasa unanishauri ni nini hapa?”

MIMI: “Ni simple tu ili kuepusha haya kutokea. Iryn ni mtu mzima tayari anajitambua huna haja ya kuendelea kuzunguka mbuyu tena, kwasasa nenda direct. Omba appointment ya kuonana naye najua hawezi kukukatalia, this time itabidi umchane ukweli na usifiche hata kitu kimoja mwambie ukweli kuhusu maisha yako na mipango yako kwake.”

MUAJEMI: “Bro unaona ni sawa kumwambia direct? Vipi kama atanichomolea si itakuwa matatizo?”

MIMI: “Point yangu acha kupoteza muda kwa mwanamke, utapoteza pesa, utatoa hata zawadi ya figo lakini kama hakupendi- hakupendi ndo wanawake walivyo. Mpaka sasa mnafahamiana tayari vya kutosha don’t waste your time Bro! Kaa naye chini mpe ukweli ibaki yeye kuamua tu kama yuko in or out.”

MUAJEMI: “Kaka naona upo sahihi itabidi niombe appointment naye weekend hii.”

MIMI: “Yeah fanya hivo, akikubali sasa hapo unampelekea gari kama zawadi ili kukazia mapenzi ila kwasasa utakwama hata yeye atakushangaa sana atakuona bwege. Na ikitokea kakuchomolea wewe achana naye pisi kali zipo kibao, wewe unapesa huwezi kosa pisi kali sehemu yoyote Duniani.”

MUAJEMI: “Sawa Bro! leo umeongea point ila wasiwasi wangu akikataa.”

MIMI: “Mwanaume kuogopa kukataliwa ni udhaifu mkubwa sana inatakiwa ujiamini hata kama akikutalia chukulia simple madem wako wengi tu. Sasa ni bora ukataliwe au uendelee kupoteza muda? Na kumbuka nilikwambia before kwamba Iryn ana mtu wake Ufaransa anampa kila kitu anachotaka, hata yeye hana shida.”

MUAJEMI: “Sawa Bro! Acha mimi niende tutawasiliana.”

Tuliagana na Muajemi na alitoa laki 1 kwaajili ya mafuta ya gari na akaondoka. Niliamua kumchana ukweli Muajemi ili aisendelee kupoteza pesa. Maana niliona kuna siku itaweza kuleta shida hata pesa alizokuwa ananipa ni sababu ya Iryn wala sio kingine.

Iikuwa ni saa 12 jioni baada ya kuachana na Muajemi mimi nilielekea Mlimani moja kwa moja. Kuna jamaa nilikwenda kuonana naye mitaa ile kwaajili ya kufanya biashara ya zile simu.

Baada ya kuonana na kuridhika na zile simu, tulikubaliana kwa simu zote 7 atanipa 16,800,000/=. Na jamaa hakutaka kuchezea ile bahati na alifanya kutransfer Pesa kwenye account yangu ya bank.

Niliondoka maeneo yale ya Mlimani na nilikwenda chuo kumchukua Prisca mama kijacho wangu ili tupate Dinna ya pamoja. Na baada ya kuwasili pale chuo ilibidi nimsubiri atoke class na baada ya nusu saa alikuwa katoka tayari akiwa pamoja na Eva.

Tulitoka pale chuo na tulikwenda mpaka mlimani city pale Instanbul restaurant kwaajili ya dinna. Kila mtu aliagiza anachopenda kula na muda huu story zilikuwa zikiendelea pale.

MIMI: “Nambieni wake zangu masomo yanakwendaje.?”

Niliishiwa kupigwa jicho kali sana na Prisca muda huu.

EVA: “Shem hongera sana unakwenda kuwa Baba soon.”

PRISCA: “Awe Baba mara ngapi?”

MIMI: “Ahsante sana shemela wangu leo itabidi unipe namba zako incase of anything uwe unanipigia.”

EVA: “Sawa shem haina shida.”

PRISCA: “Baby itabidi nianze kwenda clinic mapema.”

MIMI: “Subiri kwanza ufikishe week 8 ndo uanze kwenda kwasasa mapema sana.”

EVA: “Hata mimi nilimwambia leo bado mapema sana, naona anatamani sana kuwa mama.”

Nilikaa na akina Prisca mpaka saa 3 usiku kasoro nikawaambia warequest usafiri na mimi nikaondoka kuelekea kwa Iryn.

Baada ya kufika pale na kuingia ndani nilikuta hakuna mtu ndani lakini simu ilikuwa seblen kuonesha mtu yuko around. Nilisubiri kama dakika 10 lakini mtu simwoni, nikakumbuka kuna swimming pool nilihisi atakuwa huko.

Baada ya kuzunguka na kwenda upande wa swimming pool nilimkuta kule akiwa anaswim kama mtu ambaye hana stress na maisha, na alikuwa peke yake.

“Nimekusubiri sana kumbe upo huko mummy.”

“Insider ingia bhasi na wewe maji ya moto hadi raha.”

“Mimi siingii humo ndani fanya kutoka twende ndani tukaongee.”

“Usinambie leo hii hutaki kuswim na mimi.”

“Muda umekwenda kuna jambo nataka tuzungumze muhimu.”

“We can talk there mbona kuna utulivu wa kutosha hapa. Anyway twende ndani hata hivyo nimekaa sana kwenye maji.”

Tulirudi ndani muda huu tukiwa tumeongozana njiani, na Iryn alikuwa katangulia kwa mbele, so nilikuwa kwa nyuma nikamtizama maungo yake kwa matamanio.

MIMI: “Iryn Mungu alikuumba sana Mummy.”

IRYN: “Insider toka nyuma yangu tangulia mbele.”

Baada ya kuingia ndani aliingia chumbani na baada ya dakika 10 alitoka kavaa tayari.

IRYN: “Insider unajambo gani?”

MIMI: “Kwamba sikuhizi umeanza kunionea aibu mpaka umeenda kubadilika? Hujui nilikuwa naona raha kukuangalia ukiwa vile?”

IRYN: “Natoka tukiachana hapa na utanipeleka Mikocheni Plaza nikale Pizza.”

MIMI: “Ok sawa, nimeshauza simu tayari nipe account namba nifanye kutransfer pesa zako.”

IRYN: “Sawa twende bhasi njiani nitakupa utatransfer.”

Na muda huu alikuwa akiniinua kwenye coach kwa kunibembeleza.

Ilibidi nimepeleke Mikocheni Plaza pale Pizza Hut na baada ya kuwasili alining’ang’ania simsubiri ili turudi wote tena. Ukweli sikuwa na jinsi ilibidi twende wote mpaka ndani japo nilikuwa natamani kurudi home mapema.

Iryn aliingia ndani kuweka odda na baada ya dakika 5 alitoka akaja akakaa kwenye bench kwa pale nje. Na muda huu kuna jamaa alikuwa anakuja upande wetu ni kama alikuwa amem-target Iryn sasa aliponiona mimi dizaini kama alipiga U-turn.

IRYN: “Uyo mshenzi alikuwa ananitongoza eti alikuwa anataka kunilipia Pizza nikamgomea. Akaanza kuniomba namba ya simu, baadae akanambia unakaa wapi, nikamwambia nimekaa nje na mme wangu.”
Na muda huu Iryn alikuwa anacheka sana.

MIMI: “Sasa hapa ndo alikuwa anakufuata? Maana niliona alikuwa anakuja kwa ajili yako.”

IRYN: “Alikuwa haamini nafikiri sasa kweli kaprove. Why Tanzanian men’s are not smart?”

MIMI: “Sio Tanzania tu ni Dunia nzima acha uchawi wako kwa Watanzania.”

IRYN: “Sawa bhana, ngoja nikachukue juice. Insider nikuletee juice gani?”

MIMI: “Nichagulie nzuri for me.”

Iryn aliondoka na muda huu jamaa alikuwa akiniangalia sana dizaini alikuwa haamini macho yake kama mimi ndo mme wa Iryn. Na Iryn alivyorudi alinikisi shavuni kwa makusudi, nilihisi anamuumiza jamaa tu.

MIMI: “Noana umeamua kumchoma Moyo Jamaa.”

IRYN: “Nimekukisi sababu ya kunipa kampani wala sio sababu ya huyo mshenzi.”

MIMI: “Sawa mrembo wangu wa Dunia kula Pizza tuondoke nimem-miss mama J wangu leo.”

IRYN: “Hongera zako mimi mpaka nionane na Grizmann. Afu ratiba zetu zitaendelea soon nakosa Pesa nyingi sana kwakweli.”

MIMI: “Iryn bado unawaza kuendelea na hizo Biashara?”

IRYN: “Insider kazi ni kazi hutakiwi kuchagua, mimi ni mzuri nina kipaji cha massaji kwanini niache Pesa zinipite?. Afu nilikupa offa ya kukufanyia massage lakini unaringa, na hii kwaajili ya afya yako. Kumbuka unakaa sana kwenye gari unahitaji kunyooshwa huo mgongo shauri yako.”

MIMI: “Kweli itabidi unifanyie matibabu Doctor.”

IRYN: “Tuondoke mimi niko full hapa bebe.”

Na muda huu tuliondoka huku jamaa akituangalia kwa wivu sana na Iryn alikuwa kaniwekea mkono kiunoni, kwa mtu anayetuona kwa mara ya kwanza angejua sisi ni wapenzi.

Nilimpeleka Iryn kwake na mimi nikarudi home muda ule maana ilikuwa ni saa 5 kasoro usiku.

Kwa upande mwingine kwenye zile simu za Iryn nilikuwa nimepata 2,800,000/= kama udalali baada ya kuziuza.

*********
Jumatano asubuhi nilipigiwa simu kutoka kwa mama Janeth na aliomba tuonane saa 6 mchana pale ofisini kwake Masaki.

Mapema sana kwenye saa 6 kasoro mchana nilikuwa nimewasili pale na nilikwenda moja kwa moja mpaka getini na gari. Mama Janeth alisema nikifika pale niingie na gari ndani moja kwa moja nisipark nje.

“Bro! habari yako unakwenda wapi?”

“Nakwenda kuonana na Mrs Carter.”

“Wewe ni nani na una appointment naye?”

“Sasa nitakuja kwenye Organization kubwa kama hii bila kuwa na appointment?”

“Embu subiri kwanza tufanye mawasiliano.”

Nilisubiri pale getini kama dakika 3 hivi ndo nikaruhusiwa kuingia ndani. Na baada ya kupark gari niliwasiliana na Mama Janeth na akanambia nimsubiri pale sehem ya visitors anakuja.

Ilimchukua kama dakika 15 mama Janeth kutoka na baada ya kufika pale nilipokuwa nimekaa tulisalimiana na akanambia tuongozane, na muda huu tulikwenda moja kwa moja mpaka kwenye ofisi yake.

“Insider karibu sana Jisikie huru hii ni ofisi yenu usiwe na wasiwasi.”

“Ahsante sana mama kwanza nashukuru kwa kunipa wito wa kufika kwenye organization kubwa kama hii.”

“Mnaruhusiwa kuja mbona sema Watanzania hampo active kama nchi zingine.”

“Sijawai kujua hili mama.”

“Mnaruhusiwa kuvisit kama unataka elimu anything unapewa. Nimekuita hapa kwanza pole na msiba mwanangu, Iryn alinipa taarifa zote na alinambia mazishi yalifanyika Tabora.”

“Ndio mama nashukuru lakini kazi ya Mungu haina makosa, japo inaumiza sana kuondokewa na mtu muhimu kwenye maisha.”

“Poleni sana, nilitamani sana tuonane maana wewe ni moja ya member wa kampuni yetu na kazi yako inaonekana nikushukuru kwa hili. Nilipita pale ofisini nikaona umeweka mazingira mazuri, umepanda miti na maua kwakweli ulinifurahisha sana.”

“Ahsante sana mama ni moja ya majukumu yangu ya kiofisi huna haja ya kushukuru wakati unanilipa mshahara.”

“Jambo lingine naomba uniwie radhi kwa kutokukurudia mapema lakini ujumbe wako niliupata kwa kuchelewa sana. Nilikuwa huko Ukraine tunafanya tafiti so I was very busy that time na dada alituma mail kwenye account yangu binafsi, angetumia ya ofisi ingekuwa haraka sana kuipata.”

“Usijali mama kuwa na amani Iryn alishanambia hayo yote tayari, kipindi kile nilikuwa kwenye wakati mgumu sana. Iryn aliondoka bila kuniaga afu akawa hapatikani kwa simu, nikapata wazo la kwenda kwako lakini nikaambiwa umehama. Nikaamua kuja hapa ofisini ndo HR akanambia niache taarifa zangu atakutumia.”

“Pole sana pale tulihama, wakati umeleta mzigo weekend tulihama. Niliamua kuhamia nyumba yangu maana landlord alipandisha rent, nikaona bora nikakae nyumba yangu ili niwe huru.”

“Ni kweli kabisa mama upo sahihi kodi zina kera sana.”

Kwa ufupi mama Janeth alifurahi sana kwa kumjali sana Iryn maana alisema before mimi Iryn alikuwa ni mtu wa mawazo sana na alikuwa anajifungia ndani. Lakini baada ya kukutana na mimi amebadilika sana amekuwa mchangamfu na furaha sana.

Mama Janeth alinishukuru sana na aliniomba niendelee kuwa karibu na Iryn ili amsahau mama yake kabisa.

Ni mazungumzo yaliyochukua kama dakika 45 na baada ya hapo alinipeleka kwa yule HR wa siku ile na akanitambulisha kama mwanae. Yule HR alishangaa sana na alikuwa anani-changamkia sana muda huu.

Baada ya yote Mama Janeth alisema tukapate lunch ya pamoja na tulikwenda kupata lunch pale Epi d’or.”

Muda ule tukiwa pale mgahawani tulikuwa tunaongea mambo mengi sana na Mama Janeth kuhusu maisha na mambo mengine. Kwa upande wake mama Janeth alikuwa na furaha sana na jambo lingine alikuwa anahisi mimi nina mahusiano ya kimapenzi na Iryn.

Baada ya lunch nilimrudisha Mama Janeth ofisini kwake na tukaagana. Wakati niko njiani nilifanya mawasiliano na Dullah maana nilimwambia nikirudi toka Tabora msibani ningemjulisha.

Nilimwambia Dullah juu ya maamuzi yangu ya kuachana na biashara ya Uber kama ukumbusho wangu kwa Mzee Pama. Japo alinipinga sana na haya maamuzi yangu lakini ilibidi akubaliane tu na mimi, kwanza biashara ilishakuwa ngumu sana kipindi hiki. Dullah alinisisitiza sana Uber wakirudi niendelee na kazi lakini nilimwambia nitaajiri dereva, na haya yote ni sababu ya heshima yangu kwa Mzee Pama.

*******
Kesho yake jioni ambayo ni alhamis niliamua kupitia saloon zote kufanya ukaguzi pamoja na kuwapa taarifa Lucy na Sumaiya kuhusu kikao cha weekend.

Niliona ni busara kuwashirikisha katika mipango ya kikao kwa ujumla, sambamba na eneo la kufanyia. Iryn aliniachia hili suala mimi kama operation manager lakini na mimi niliona sinabudi kuwashirikisha akina Lucy kama partners wangu.

Nilianza na Lucy pale Mikocheni na baada ya kumshirikisha alitoa wazo tutafute sehemu nzuri ya uwazi na baada ya hapo twende sehemu tukamalizie bata.

Tuliagana na Lucy na nilikwenda moja kwa moja mpaka Masaki kwaajili ya kuonana na Sumaiya. Wakati nawasili pale dizaini kama aliniona hivyo alitoka na akaja parking na akafungua mlango wa gari akakaa siti ya mbele.

“Mtoto unapenda magari wewe.”

“Hakuna mwanamke asiyependa gari Insider.”

“Naona leo umependeza sana na hiko kigauni chako kinafanya viamke vilivyo lala.”

“Kwa mwanaume Rijali ni kawaida so siwezi kukushangaa wewe kama ni kweli. Niambie unajambo gani kutoka kwa Queen, maana leo kanipigia simu eti ananisalimia, toka lini Queen anipigie simu akanisalimia?.”

“Si Bossy wako? hutaki akujulie hali mfanyakazi wake ?”

“Yule anahisi mimi nakupea ni wivu tu umemjaa, maskini anafikiri tunanyanduana.”

“Mama Janeth alikutoa wapi wewe? Maana sijawahi kukutana na mwanamke mwenye mdomo kama wewe.”

Sumaiya ni mwanamke asili yake ni Tanga anakimwili portable afu mweupe madem wa Tanga nadhani mnawajua vizuri. Kingine alikuwa mwongeaji sana afu hanaga aibu kabisa.

Niliongea na Sumaiya kuhusu suala la kikao Jumamosi na yeye alishauri tutafute Hotel au sehemu yoyote ya wazi ili tufanye kikao chetu na baada ya hapo tutoke out.

Ushauri wa Sumaiya niliona una mantiki
Maana tungekuwa 17 kwa idadi ya wote, Masaki kuna wafanyakazi 7, Mikocheni 5, Sinza 3 , bado mimi na Iryn. Jumla hapo tunakuwa 17 so hotel ndo ilikuwa sehemu sahihi ya kufanyia kikao.

Baada ya maongezi Sumaiya aliomba nimsubiri ili nimpe lift mpaka Morocco na ilikuwa ni usiku umeanza kuingia.

Nilimsubiri kwa nusu saa ndo alitoka na tukaondoka, sasa kutokana na story za njiani nilijikuta nampeleka Sumaiya mpaka kwake. Alikuwa anakaa Kinondoni mitaa ya Gavana kule kama unakwenda Biafra. Na lengo langu lilikuwa nikatokee mataa ya Biafra then Morocco afu niunge na Bagamoyo road.

“Insider si unapitia kwangu upajue? Kufika mpaka hapa na usiingie kwangu haitakuwa vizuri.”

“Sawa twende nikapajue kwako.”

Baada ya kuwasili kwake alishuka akafungua geti na mimi nikaingiza gari nikapark tukaingia ndani kwake. Alikuwa amepanga apartment nzuri ya Jiko, sebule, na masta.

“Nani anakulipia kodi hapa? sitaki matatizo.”

“Angekuwa analipa kodi mwanaume mwenzako hata nisinge kuingiza ndani.”

Na muda huu nilimvuta kwangu kwa nguvu na nikamshika makalio yake.

“Makalio yenyewe huna ya kushika.”
Na nikaendelea kuyapapasa na kuyaminya minya.

Niliona Sumaiya kashaanza kulegea taratibu na yeye akanipa tongue tukaanza romance pale asee ilikuwa ni mtifuano, nikambeba nikamtupia kwa coach. Na kalivyo portable vile hata sikuwa na tumia nguvu kubwa sana kumbeba.

Sikutaka hata kumcheleweshea kabisa nikamvua kigauni chake, uwii alikuwa na bikini afu kwa juu hakuvaa chochote nilikuwa naziona chuchu zake live zilivyosimama wima, uzuri zilikuwa zina jaa kwenye mikono yangu maana alikuwa ana vifuu vidogo sana.

Nilianza kuvinyonya taratibu pale na yeye alishakuwa yuko Dunia nyingine muda mrefu sana. Kisima chake kilikuwa kishaanza kutoa chemchem tayari na mimi niliendeleza maunyama yangu taratibu hata sikuwa na mapepe maana kuku ni wangu haraka za nini?.

Muda huu Sumaiya alikuwa kashaanza kupapasa mtwangio wangu ili nianze kutwanga kinu. Na mimi palepale nimlaza chali na nikambetua kwa juu kidogo ndani ya sekunde alikiaa chaaah!, niliiachana bikini yake vipande viwili. Na muda huu nilikuwa nashuhudia something hot between her legs na alikuwa kashave kabisa.

Nilimkunja vizuri kabisa kwaajili ya kumtwanga lakini nilikumbuka sina kinga, sikutaka suala la Prisca lijirudie tena hivyo nikamuacha palepale.

“Insider unashida gani?”

“Do you have a condoms?”

“No sina.”

“Siwezi kuendelea bila condom acha nikanunue chap then nakuja tuendelee.”

Na muda huu Sumaiya alikuwa mpole ikabidi nimwambie nakwenda pharmacy kununua then narudi, hata yeye hakuwa na cha kusema.

EPISODE 48[emoji116]
Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu
.
 
SASA MKUU JITU LINACOMMENT LIPO BIHARAMULO HUKO, AU KATAVI HANA EXPOSURE YOYOTE MAISHANI MWAKE, ANAKULA UGALI WA MTAMA NA VISAMAKI BAR ZAKE ANAZOZIONA NI VILABU VYA POMBE ZA KIENYEJI UNADHANI WATAACHA KUMPOSTI NYANI ANAKUNYWA CHAI HEHEH. ATAJULIA WAPI TABLE ZA NAMNA HII BUDGET YAKE KWA MWAKA MILLION TATU TU ZA SHAMBANI KULIMA. HALAFU WANAKUTANA JF NA STORY KAMA HII ILIYOJIKITA JIJINI DAR ES SALAAM.

Sent using Jamii Forums mobile app
Daah natamani kuelewa ulichokiandika lakin naona nimeshindwa
 
Back
Top Bottom