Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

Japo sio vizuri kukuelekeza ila kuna sehem ulikosea mapema kuhusu Iryn na mkeo. Huko mbelen itakuletea shida. Cc ni wachagga na nina mshikaji wangu alikutana na ishu kama yako. Sema yeye demu hakuwa mzur kiivyo ila mazingira yake yalimfanya jamaa akaoa mke wa pili na haikumletea shida. Hiv vitu unaviseti mapema maana kule uzeen vinageuka. Maisha yanakuwa tena sio kiasi cha hela ulichonacho ila ni kwa namna gan wewe na mkeo mnamaliza pamoja kwa upendo na kuaminiana. Trust is everything bro. Bado hujachelewa. Kuna kitu cha muhim kwaajili yako na wanao unatakiwa kukifanya ili kuileta ile bond ya familia. Trust me siku mkeo akijua kila kitu na akawa anakumbukia zawad alizokuwa analetewa na Iryn ndio trust kwako imeisha. Na kutaota chuki kali sana kwa watoto Chief. Anaweza kusamehe lakin hatasau na atasubir right time kulipiza. Msome mkeo umjue anaingilikaje ili uuvunje huo ukuta uwe huru na Iryn na mueze kujenga future yenu pamoja. Narudia Mzee hela ni sehem ndogo sana ya maisha. Familia ndio kila kitu. Na aman yako na watoto wako huko kesho itategemea na namna unavyohandle Mambo yako na mkeo tofauti na hapo mzee tarajia kuwa kama Marehemu Mengi.
You said it all, am afraid kuna namna tu asipoweka sawa huyo mke lazima atafute kisasi tena kikubwa

Sent from my SM-A042F using JamiiForums mobile app
 
Kuna shida kwenye hii thread, naambiwa Error. Nitaleta Extra Episode.
Asante sana mkuu kushare nasi. Tumeburudika. Huna baya mwanangu. Mimi nakutakia kila la kheri ufanikiwe sana mwamba. Kwa jinsi ulivyo mvumilivu,unavyopanga mipango yako. Usivyo na papara. Jinsi unavyojibu,yaani niseme tu elimu yako imekusaidia mwamba. Hongera na Asante sana INSIDER MAN .

Umezalisha kitu kipya vichwani mwa wengi waliopitia hii tred. Binafsi ilikuwa kila nikisoma,hasa hii epsode ya mwisho nilikuwa najiona kama ni mimi vile,kama ndoto fulani nzuri. Nasema umezalisha kitu kipya ksbb inakuwa kila nikipitia hii story najiona imara fulani,hata kama napitia matatizo fulani najiona mpya mwenye kuweza kuyashinda hivi.
Asante sana
 
Japo sio vizuri kukuelekeza ila kuna sehem ulikosea mapema kuhusu Iryn na mkeo. Huko mbelen itakuletea shida. Cc ni wachagga na nina mshikaji wangu alikutana na ishu kama yako. Sema yeye demu hakuwa mzur kiivyo ila mazingira yake yalimfanya jamaa akaoa mke wa pili na haikumletea shida. Hiv vitu unaviseti mapema maana kule uzeen vinageuka. Maisha yanakuwa tena sio kiasi cha hela ulichonacho ila ni kwa namna gan wewe na mkeo mnamaliza pamoja kwa upendo na kuaminiana. Trust is everything bro. Bado hujachelewa. Kuna kitu cha muhim kwaajili yako na wanao unatakiwa kukifanya ili kuileta ile bond ya familia. Trust me siku mkeo akijua kila kitu na akawa anakumbukia zawad alizokuwa analetewa na Iryn ndio trust kwako imeisha. Na kutaota chuki kali sana kwa watoto Chief. Anaweza kusamehe lakin hatasau na atasubir right time kulipiza. Msome mkeo umjue anaingilikaje ili uuvunje huo ukuta uwe huru na Iryn na mueze kujenga future yenu pamoja. Narudia Mzee hela ni sehem ndogo sana ya maisha. Familia ndio kila kitu. Na aman yako na watoto wako huko kesho itategemea na namna unavyohandle Mambo yako na mkeo tofauti na hapo mzee tarajia kuwa kama Marehemu Mengi.
Ukweli mchungu
 
Ni kweli kuficha ficha haitasaidia. Atafute muda amuambie mama J ukweli, then mama ataamua kusuka au kunyoa mapema.
Good advice kama mtoto keshazaliwa na no way mama j asije kujua Cha kufanya ni Bora Insider akamueleza yeye mwenyewe kwamba ana mtoto na bi dada Iryn na anataka kumfanya kuwa mke mdogo najua mwanzo ata mind lakini atatulia .
 
Song: The man
Artist: My ownself

VERSE 1

Oh yeah, insider man wrote the story
And we niggas had to read in harmony
And he the man fell in love with bossy lady
And bossy lady got the mimba, flew all the way to madiba
She left the AUDI Q7 to the man
But we nigass are busy arguing each other
Though we knew the man is in danger

CHORUS
That sweet love of the man himself
That left us members in a daze
That made CHAPUTA do it all night long
Ooh all night long
Those millions he earned on uber
That left us members saying "chai"
That.......
Kmmmk
 
INSIDER MAN ...achana na mambo ya kumtambulisha Iryn na mtoto Kwa wazazi wakati huu. Mama Yako ni mtu makini sana, anawezakukupa maelekezo yatakayokuweka mahali pagumu sana.

Kumbuka unatarajia kufunga ndoa(kubariki ndoa) muda si mrefu, hizi habari za mtoto zitatibua na kuibua mambo mengine. Kwa maoni yangu, ungekamilisha Hilo zoezi la ndoa kwanza, huku ukisikilizia mambo yanaendaje.

Mie nilisha ambiwa, siku ikitokea taarifa za ujauzito au mtoto wa nje ndio mwisho wa mahusiano na wife. Akasema yuko radhi kumtambulisha watoto wengi wajae fuso ila kama walipatikana kabla ya kufahamiana nae ila sio tukiwa wote.

Inabidi uongeze sasa mdogo wa hao watoto kwa Mama Jr. Naona Iryn ndio anamoto wa kukuzalia mtoto mwingine, angalia asije akasawazisha na kuongoza ligi...

Ni kweli hautaki kuendelea kulipwa mshahara kwenye kazi za Iryn, lakini hauoni kuondoka kwako inaweza kusababisha mambo yakayumba kibiashara mkapoteza wote?

Unaweza kufanya mambo mengine lakini ukaendelea ku oversee hizo biashara.

Kwenye extra episode 06 haujagusia suala la Mama Janeth na mtoto wa Iryn, hajawahi kujua wewe ndio baba wa huyo mtoto?

Kingine unakibarua kizito sana, tena sana cha kukaa mbali na akina Mary, Mdogo wake Jane, mtoto wa Mzee Juma na walimbwende wengine, siku ukijichanganya, ikathibitika pasi shaka umechepuka, Kwa akili za Iryn zilivyo, hasira zake anaweza kumshirikisha Mama Jr kuhusu hizo tabia hata kama na yeye atakua matatani lakini hatakua na cha kupoteza. Usiwaumize mioyo hao wake zako, Iryn akijua unachepuka ni bora ukajifiche Gaza.

Mwisho wa siku maamuzi unayo wewe kiongozi.
 
EXTRA EPISODE 06
BY INSIDER MAN

Kwanini nimemuita Iryn ni Mrembo wa Ajabu?


Kabla ya kuandika hii story nilipata tabu sana kwenye kuchagua kichwa kutakacho beba jina la story, lakini target ya huu uzi ilikuwa ni Iryn.

Ningeweza kuandika heading nyingi tu lakini niliona hii ndo sahihi kutokana na jinsi tulivyokutana na tulivyoishi sababu tulipitia mambo mengi sana.

Kwangu Iryn nilikuwa namuona ni mtu wa ajabu, kwanza namna tulivyo kutana, pili maisha yake kwa ujumla kwangu mimi yalikuwa yananipa maswali sana, tatu utajiri wa wazazi wake na yeye pia, nne uzuri na urembo wake.

Nilikutana na Iryn kimaajabu sana kupitia hiihii bishara ya Uber, ukisoma vizuri wakati nakutana naye ilikuwa ni usiku sana afu nimechoka. Baada ya kupata request yake nilitaka kupiga chini ile request lakini nikaamua kwenda kibishi na ndo yeye kaja kunipa heshima ya kuwa baba mtoto.

Kama ningeipiga chini ile request ina maana nisingekuja kumfahamu mtu anayeitwa Iryn kwenye Maisha yangu, kuna msemo wazungu wanasema “everything happen for a reason.”

Tukija kwenye maisha yetu halisi huenda tunapishana na baraka nyingi na connections nyingi kwa kupuuzia tu, kama wewe dereva wa Uber unapata request ya kwenda Mbagala lakini hutaki kwenda, kumbe ilikuwa ni connection kwako bila kujua.


Iryn ni moja ya mwanamke mzuri na mrembo hapa Duniani na uzuri wake ni natural sio namsifia kumpa sifa ambazo hana, hapana ni moja ya mwanamke mrembo sana na amekamilika kila Idara (Episode ya 7 nilimuelezea kidogo). Hii ilinifanya nimuone Iryn ni moja ya mwanamke wa ajabu kukutana naye kwenye maisha yangu. Kuna muda ile mwanzoni nilikuwa nahisi maybe atakuwa sio kiumbe wa kawaida. Kitu kingine suala la kuwa mtoto pekee kwa mama nalo kilifanya nimuone Iryn wa tofauti sana.

Suala la mali na utajiri ambao familia yake unao kuanzia marehem mama yake, Mzee wake na yeye pia vilikuwa vinanipa maswali sana. Mzee wake Iryn anapesa sana na huko South Africa ana ma apartments kibao anayamiliki na bado ni mfanyabiashara mkubwa.

Nimeplay part kubwa sana ya kumuweka Iryn sawa maana alikuwa ni mtu wa mawazo sana, kitendo cha kuwa naye close mara kwa mara ndo kilifanya aanze kunipenda kwa kasi ya 5G.

Licha ya kufaham nina familia ila kwake yeye ilikuwa tofauti na aliendelea kunipenda tena ni upendo wa kweli. Tumepitia mambo mengi sana na sikuyaandika yote, niliyoandika ni baadhi tu.

Baada ya Iryn kwenda South Africa hapa katikati mambo mengi sana yalitokea, na yeye alikuwa anakuja Dar kuniona kama alivyo niahidi na ilikuwa ni kwasiri sana na hakuna aliyekuwa anajua hili. Amekuja sana Dar mpaka mimba ilivyokuwa kubwa ndo akaacha kuja na toka aondoke kwenda South Africa hajawahi kuonana na mama J tena.

Pia kuna mambo mengi sana yalitokea na mazito juu ya ujauzito wake na niliishi kwa stress sana ndugu zangu. Kwa upande wake alikutana na pingamizi kubwa sana hasa upande wa ndugu, lakini all kila kitu kilikwenda sawa na mwezi June 2023 alijifungua salama na tulipata mtoto wa kike.

Nilifurahi sana kupata mtoto wa kike japo nilikuwa najua kuwa nitapata mtoto wa kike lakini baada ya kujifungua na kujihakikishia kwa macho nilifurahi sana. Before hajajifungua mwezi wa sita nilikwenda South Africa kwa mara ya pili ili niwepo wakati wa kujifungua na nilikaa kule kwa week 2.

Siku anayojifungua nilikuwa naye hospital nikishuhudia kila kitu kule leba asee kule kama mwanaume unahasira utaishia kuwapiga madoctor[emoji23][emoji23], wanachokonoa sana K kwa mikono. All nashukuru Mungu alijifungua salama kwa kupush, na kama tulivyokubaliana mimi ndo nilimpa jina mtoto.

Mtoto wetu ana miezi 5 kasoro mpaka sasa na anakua vizuri, ana afya nzuri niseme she is so beautiful jamani na nimefanana naye copyright. Pia amefanana sana na kaka yake Junior, yaani siku wakija kukaa pamoja itaonesha ni watoto wa mama mmoja maana wote wamefanana sana na mimi, hata mama J akija kumuona hatauliza mtoto ni wanani kwani tumefanana sana.

Hili suala bado imebaki kuwa siri kwangu hata wazazi hawajui mpaka sasa navyoandika hapa. December hii Iryn atakuja Dar na bado najifikiri niende naye mkoani na mtoto kwa wazazi wamuone au niendelee kuvunga tu mpaka mtoto akue, au niwape taarifa na mtoto wa nje?, hapa bado nakosa majibu.

Iryn anataka kunizalia mtoto mwingine wa pili, amesema yeye anahitaji watoto sababu anaona ndo furaha kwake na jinsi tunavyoishi hata kama tuko mbali anaona mimi natosha kuwa mume wake. Unajua Iryn anajua fika mimi sijampendea kisa pesa zake na anafahamu fika mimi sina habari na pesa zake kabisa na ninamchukulia kama mama watoto wangu.

Niilimpa greenlight kama atapata mtu sahihi awe huru kuwa naye au kuolewa, lakini amegoma kabisa hataki kuzisikia hizi habari. Yeye anasema hakuna mwanaume wa kumpenda kama jinsi mimi navyompenda na hatamani kuwa na mtu mwingine kwa heshima yangu na mtoto, pia ameridhika kuwa mchepuko.

Kwa upande mwingine nilimwambia yeye ni mke mdogo na nimempa hiko cheo na ninaandaa mpango wa kumpeleka home akaijue familia yangu maana analea damu yetu, na yeye ana hamu kubwa sana.

Kipindi alichojifungua ndo nilijihakikishia Iryn sio mtu wa kawaida, unajua walikuja watu wengi sana kumuona kule South Africa, kuanzia friends zake zake wa chuo, ndugu zake wa Ethiopia nknk.

Kwa upande wa mimi na mama J mahusiano yetu yako strong sana kwasasa, japo baada ya Iryn kuondoka kuna mambo yalitokea lakini bado tuko pamoja na familia yetu inazidi kustawi na mwakani tunatarajia kufunga Ndoa rasmi kama Mungu akitujalia uhai.

Kwa upande wa my son Junior yeye kashakua mkubwa tayari na mwakani tunategemea aanze nursery mapema na atakuwa na 2.5yrs by January. Dogo kawa mtundu sana, ni mkorofi sana kupiga watoto wenzie kwake ni kitu cha kawaida ila huji kuta akiwapiga watoto wa kike.

December Iryn atakuja kama nilivyosema awali na tutadiscus mambo mengi sana ikiwemo kuhusu project ya kufanya kule Dodoma, suala lingine nilimwambia nikimaliza chuo nataka kufanya project zangu sitaki kuwa chini yake tena.

Nilimwambia yeye ni mke wangu kuendelea kunilipa mshahara naona kama dharau, so kama vipi tufungue kampuni ya pamoja au mimi nifanye mambo yangu. Baada ya kumpa hizi taarifa naona hajazipenda na amesema yuko tayari kunisikiliza ila hataki nifanye kazi na mtu mwingine kwani bado ananitegemea sana, akija mwezi ujao ndo tutafikia muhafaka.

Plan za Iryn akimaliza chuo anataka kwenda kuishi Ufaransa na mtoto maana kuna project zake mpya anazo kule. Pia hata yeye anapenda sana kuishi Ufaransa.

Mwisho, sikuwahi kuwaza kuja kuchepuka au kuzaa na mwanamke mwingine nje na mama J, nilianza kuchepuka kutokana na kutopewa tendo kwa wakati maana kama mwanaume uvumilivu ulinishinda na kile kitendo cha kuondoka kwenda kwao kisa Prisca na huku sijatembea naye, ukweli kilinikera sana.

NB: Nitaangalia kama nitawapa muendelezo hata mwakani huko lakini siwapi promise kwa hili, nitaangalia kama kuna code zozote zimefunguka kupitia hii story mpaka sasa na kama upepo ni shwari nitaangalia namna ya kuwapa.

“Katika maisha yangu sijawai kukutana na mrembo mzuri kama IRYN, nimeona wanawake wengi hapa dsm lakini Iryn alikua ni mwanamke mzuri sana ambaye amekamilika kila idara, nyie Mungu ni fundi sana, sio shepu, matiti, sura, lips, mguu, mweupe, sauti na mguu mzuri. Ningekua na uwezo ningetuma picha yake ila ndo hivyo sitoweza.

Ni mwanamke ambaye akipita lazima ugeuke umtizame nyie, kiukweli sikuijutia kazi yangu ya uber ni moja ya kazi ambayo ilinikutanisha na warembo wengi sana.
(EPISODE 07)

kwanza hongera kwa kupata mtoto, lakini fanya hivi
1. Usifanye siri hili jambo kwani ipo siku litajulikana tu.. mpeleke Iryn na mtoto nyumbani kwenu kumtambulisha wamjue damu yako.

2. Mwambie ukweli mama J kuwa una mtoto umezaa na Iryn na usimfiche chochote. mwache yeye aamue kuolewa au aache kuolewa na wewe..usimuoe bila yeye kufahamu hili jambo na aridhie mwenyewe kuwa kuna mke mwingine.

3. Mwambie mama J kuwa utafunga ndoa ya serikali na pale kuna option ya wewe kuwa na wake wawili au zaidi ili umlinde Iryn na watoto utakaozaa naye, watoto wote wana haki kwa baba yao.. Mama J anatakiwa ajue kabisa kuwa anaolewa na wewe lakini kuna mke mwingine ambaye naye utafunga naye ndoa..

4. Usithubutu kumuoa mama J bila ya kumpa taarifa ya mke mwenzake ambaye ni Iryn..yani ajue kuwa anaolewa kama mke wa kwanza na pia kuna mke wa pili. usisahau kuwa huyo mama J ni mchaga na mtusamehe tu wanawake wa kichaga wengi huwa wanabaki wajane jiulize kwa nini.. na hasa akigundua mume wake ana wanawake wengine na watoto huko nje mawazo yao yote huwa ni kwenye mali na kuwamaliza waume zao.. tusije tukaanza kuimba parapanda bado tunakupenda Insider..

5. Mama J akikataa kuolewa na wewe kwa sababu ya kufahamishwa kuhusu Iryn basi pambana na hali yako na umuoe huyo Iryn na ikibidi uchukue mwanao ulee wote pamoja..nakuusia usifanye siri kwa mama J kwani madhara yake ni makubwa huko mbele labda kama huwajui wachaga..
 
Umetoa mawazo mazuri sana.
kwanza hongera kwa kupata mtoto, lakini fanya hivi
1. Usifanye siri hili jambo kwani ipo siku litajulikana tu.. mpeleke Iryn na mtoto nyumbani kwenu kumtambulisha wamjue damu yako.

2. Mwambie ukweli mama J kuwa una mtoto umezaa na Iryn na usimfiche chochote. mwache yeye aamue kuolewa au aache kuolewa na wewe..usimuoe bila yeye kufahamu hili jambo na aridhie mwenyewe kuwa kuna mke mwingine.

3. Mwambie mama J kuwa utafunga ndoa ya serikali na pale kuna option ya wewe kuwa na wake wawili au zaidi ili umlinde Iryn na watoto utakaozaa naye, watoto wote wana haki kwa baba yao.. Mama J anatakiwa ajue kabisa kuwa anaolewa na wewe lakini kuna mke mwingine ambaye naye utafunga naye ndoa..

4. Usithubutu kumuoa mama J bila ya kumpa taarifa ya mke mwenzake ambaye ni Iryn..yani ajue kuwa anaolewa kama mke wa kwanza na pia kuna mke wa pili. usisahau kuwa huyo mama J ni mchaga na mtusamehe tu wanawake wa kichaga wengi huwa wanabaki wajane jiulize kwa nini.. na hasa akigundua mume wake ana wanawake wengine na watoto huko nje mawazo yao yote huwa ni kwenye mali na kuwamaliza waume zao.. tusije tukaanza kuimba parapanda bado tunakupenda Insider..

5. Mama J akikataa kuolewa na wewe kwa sababu ya kufahamishwa kuhusu Iryn basi pambana na hali yako na umuoe huyo Iryn na ikibidi uchukue mwanao ulee wote pamoja..nakuusia usifanye siri kwa mama J kwani madhara yake ni makubwa huko mbele labda kama huwajui wachaga..
 
Nenda kaongee na wazazi wako pamoja na ndugu zako kuhusu kuzaa na Iryn. Toa msimamo wako kuwa utaendelea nae. Mtaitisha kikao pande zote mbili kuzungumza hili.
Mama J ataamua kuolewa nawe au la. Mwanzo utalaumiwa sana ila baadae utaonekana mwanaume jasiri. Lakini kumuoa bila hii taarifa utakuwa umemlaghai.

Sikushauri kabisaaa umwambie mama J mkiwa wawili tu; yaani wewe na yeye. Maamuzi anayoweza kuchukua hujui.
 
Nenda kaongee na wazazi wako pamoja na ndugu zako kuhusu kuzaa na Iryn. Toa msimamo wako kuwa utaendelea nae. Mtaitisha kikao pande zote mbili kuzungumza hili.
Mama J ataamua kuolewa nawe au la. Mwanzo utalaumiwa sana ila baadae utaonekana mwanaume jasiri. Lakini kumuoa bila hii taarifa utakuwa umemlaghai.

Sikushauri kabisaaa umwambie mama J mkiwa wawili tu; yaani wewe na yeye. Maamuzi anayoweza kuchukua hujui.
Sio kwamba ata kataliwa kumuoa mama j hapana. Ila kwenye ukristo hakuna wake wawili so ndoa itafungwa vizuri ila shida inaanza wewe kutaka kulazimisha uhalali wa wake wawili.

Kibinadamu tupo sawa mana ni nature ya wanaume kuwa na watot wengi toka enzi ila utashindana na imani yako mpk kufa kwako, unless uwe muslim.
 
Back
Top Bottom