SEASON 02
CHAPTER 41
“BY INSIDER MAN”
CONTINUE:
Kwa upande wangu, sikutarajia hata kidogo kukutana na mama mkubwa. Niliposogea, nilimsalimia kwa heshima. Alinijibu kwa upole, kisha akaniangalia kwa makini, macho yake yakitua pia kwa Aria aliyekuwa kamshika. Sekunde chache zilivyopita, alinitazama tena na kusema kwa sauti tulivu, “Umefanana sana na mtoto.” Kabla sijapata nafasi ya kujibu, Mama Janeth naye alidakia, akinitazama kwa tabasamu na kusema, “Ni kweli kabisa, mnafanana sana wewe na Aria.”
Niliishia kutabasamu baada ya kusikia maneno yale kutoka kwa mama mkubwa, kisha nikatafuta sehemu ya kuketi. Sebleni palikuwa na wageni wengi sana, hali iliyonifanya nijisikie kutokuwa na utulivu, lakini sikuwa na namna. Nilibaki pale, nikijaribu kuzoea hali ile, huku nikionesha utulivu ambao sikuwa nao ndani yangu.
Baada ya dakika nyingi kupita, niliamua kwenda chumbani kwa Iryn ili kumsalimia na kumjulia hali. Nilipofika, niligundua hakuwa peke yake, alikuwa na wageni wawili. Niliwasalimia wote kwa heshima, na bila kusita, Iryn alinitambulisha kwa marafiki zake akisema, “Hawa ni marafiki zangu, tumesoma nao chuo Ufaransa.”
Nilimuuliza Iryn kuhusu maendeleo ya kidonda chake, na aliniambia kuwa anaendelea vizuri kabisa. Tulipokuwa tunaendelea kuzungumza, ghafla Jimmy aliingia chumbani. Mara tu Iryn alipomuona, uso wake ulibadilika kabisa.
JIMMY: “Hata ukininunia, freshy tu."
IRYN: “Jimmy, nakuchukia sana!"
JIMMY: “Hujaanza leo, na sishangai kabisa.”
IRYN: “Jana ulimpeleka wapi Insider?”
Jimmy alinitazama kwa wasiwasi, akihisi labda nimemueleza Iryn kuhusu tulikokuwa usiku huo. Nilimpa ishara kuwa sina ufahamu wowote juu ya jambo hilo.
JIMMY: “Sawa, tulienda Soho kuburudika, na tulirudi salama."
Iryn, akiwa amekasirika, alitazama pembeni na kuona bakuli karibu yake. Alilichukua kisha akamrushia Jimmy kwa hasira, huku akimfyonza kwa dhihaka.
Na wakati huu, Amara aliingia chumbani na kuanza kuuliza, “Shida ni nini?" Jimmy, kwa haraka, alimnyanyua juu juu na kutoka naye hadi sebleni. Lilikuwa tukio la ghafla na la kufurahisha, kiasi kwamba kila mtu aliishia kucheka, hata wageni.
Niliamua kuondoka chumbani ili kumpa Iryn nafasi na wageni wake. Hata hivyo, wakati nilipokuwa natoka, ghafla nilisikia akiniita kwa sauti ya upole, “Subiri kidogo...”
IRYN: “Darling, where are you going?”
MIMI: “Nipo mke wangu, huna haja ya kuwa na wasiwasi.”
IRYN: “Usije ukanitoroka kama jana ulivyofanya.”
MIMI: “ Leo nipo na wewe baby.”
Baada ya kurudi sebleni, nilitambua kuwa watu watatu hawakuwepo, nao ni dada yangu, Vivian, na Samantha. Nilipouliza, niliambiwa kuwa walitoka kwenda supermarket kununua vitu kwa ajili ya mama mtoto.
Baada ya takriban saa moja, mzee Virgil aliwasili na familia yake yote. Ilikuwa siku ya kipekee kwani niliweza kuwafahamu wadogo zake wote kupitia mama mdogo, kasoro kaka yake ambaye mzee alimzaa na mwanamke mwingine.
Mchana tulikula chakula cha pamoja, ambacho kiliagizwa kutoka kwa wapishi wa nje. Baada ya lunch, mama Janeth alitusalimu na kutuaga, akituambia kwamba anaondoka kwa safari ya kwenda Tanzania, kisha ataendelea na safari yake kwenda Marekani (USA).
Kabla ya mama Janeth kuondoka, tulipata nafasi ya kuzungumza. Nilimshukuru sana kwa kujitoa kwake na kuhakikisha Iryn anajifungua salama. Mama Janeth alinituliza, akisema kwa upole, “Iryn ni binti yangu, huna haja ya kunishukuru kwa hili.”Maneno yake yalikuwa ya faraja, yakiniondolea wasiwasi.
Jioni nilikutana na dada yangu, na tukatafuta sehemu tulivu kwa ajili ya mazungumzo yetu. Mara tu baada ya kuketi, dada alianza kuzungumza kwa hisia, akilalamika kuhusu tabia zangu mpya ambazo nimeanza kuonesha waziwazi mbele ya mama J. Aliuliza kwa upole lakini kwa msisitizo, “Kipindi kile ulipolala nje, ulikuwa wapi?” Akiongeza kwa tahadhari, alisema, “Na kama utathubutu kunidanganya, itakuwa ndio mwisho wa maongezi yetu.” Maneno yake yalikuwa na uzito, yakinifanya nifikirie kwa makini kuhusu majibu yangu.
Niliwaza pale na kuamua ni bora niwe mkweli ili tuweze kumaliza mambo haya.
MIMI: “Nilikuwa na mwanamke mwingine.”
SISTER: “Una matatizo gani? Tuliongea vizuri kabisa kuhusu haya, lakini bado unaendelea kuyafanya. Je, unanidharau mimi dada yako? Nilitegemea utaanza kufocus na watoto wako, lakini unazidi kuhangaika na wanawake wengine?”
MIMI: “Dada yangu, najua nimezingua. Mwanamke huyu alinifata Dodoma mwenyewe, na kipindi kile nilikuwa nimegombana na mama J, na Iryn alikuwa hana dalili za kurudi.”
Majibu yangu yalimfanya dada yangu aonekane mwenye wasiwasi zaidi, lakini pia nilijua ni muhimu kuwa mkweli ili kuweza kuendelea mbele.
SISTER: “Nisikilize kwa makini, bro. Usinione kama mjinga kukusaidia na kesi zako za kila siku ambazo unafanya kwa makusudi. Leo nakupa onyo la mwisho, kama una wanawake nje na hawa mama watoto wako, nikaja kupata kesi, utakuwa umefunga kufuli la mimi kukusaidia.”
MIMI: “Dada yangu, usifike huko, nimekuelewa na sitokuangusha.”
SISTER: “Na kilichofanya uondoke bila kumuaga mama J ni nini? Unaonesha dharau kama hizi kwa mke wako.”
MIMI: “Mimi naondoka tumegombana kwa sababu alimpigia mama yangu simu na kumwambia nililala nje. Niliona ananichonganisha na mama yetu, kwa kitu ambacho hana ushahidi nacho.”
SISTER: “Unataka kuachana na mama J, kisa Iryn?. Ukitaka mambo yako yaanze kuharibika tena, bhasi jichanganye ufanye huo ujinga unaotaka kuufanya, utayakumbuka maneno yangu.”
MIMI: “Siwezi kumuacha mama J, hili nakuapia dada yangu.”
Baada ya kumaliza tofauti zetu, dada aliniahidi kunisaidia kuliweka sawa suala la Iryn. Alinishauri nisubiri mtoto afike miezi sita ndipo nianze hatua za kuwaambia wazazi. Alisema ni bora nianze kumshirikisha mzee, na kisha yeye ndiye atakayemwambia mama. Maneno yake yaliniweka katika hali ya matumaini, kwani nilijua kwamba kwa msaada wake, naweza kupata njia sahihi ya kukabiliana na hali hii.
Dada alinionyesha mbinu ya kuanza kumuandaa kisaikolojia mama J, akisema kwamba nianze kufanya hivi taratibu ili aanze kuhisi mapema kuwa nina mtoto nje. Hata hivyo, nilishindwa kumuelewa alimaanisha nini, hivyo ilibidi nimuulize.
MIMI: “Mbinu gani natakiwa kuanza kuitumia?”
SISTER: “Katika maongezi yenu, unaweza kumuuliza, 'Hivi, ukija kufahamu kuwa nina mtoto nje, utafanyaje?' Inatakiwa uwe unamuuliza mara kwa mara hadi pale atakapozoea na kuona ni jambo la kawaida.”
MIMI: “Dada yangu, sio kwa mama J, hachelewi kulianzisha.”
SISTER: “Hawezi kufanya chochote kwa sababu atakuwa hana ushahidi. Kwa mara ya kwanza atapata shida kadri anavyozidi kusikia kutoka kwako, lakini atazoea na kuona ni jambo la kawaida. Wewe cha kuzingatia ni kuwa unachukua note ya majibu anayotoa, na utakuwa unanitumia.”
Maneno yake yalikuwa na maana, lakini nilihisi bado kuna changamoto kubwa katika kutekeleza mbinu hiyo. Lakini dada alizidi kukazia kwamba mbinu hii itaanza kumuandaa kisaikolojia, na baada ya muda atazoea hali hiyo. Alisisitiza kwamba hata nitakapokuja kumpa taarifa rasmi, haitaleta shida sana na atakuwa na uwezo wa kuelewa vizuri. Maneno yake yalinipa matumaini, kwani niliweza kuona uwezekano wa kumfikia mama J kwa njia ambayo ingekuwa rahisi na ya busara.
Kuhusu suala la kumpa taarifa rasmi, dada alishauri ni bora nisubiri hadi nitakapomalizana na wazee na kila kitu kipo sawa. Alisema kwamba ni hapo ndipo nianze hatua za kumwambia mama J. Dada alinihakikishia kwamba atanisaidia kadri anavyoweza kwa kutumia uwezo wake wote hadi mambo yawe sawa. Maneno yake yalijenga imani ndani yangu, na nilihisi kuwa na msaada wa dada yangu kutanisaidia kukabiliana na changamoto hii.
Baada ya kumaliza maongezi yetu muhimu, dada aliniaga na kuniambia kwamba kesho, Jumapili, ataondoka kurudi Tanzania. Alisisitiza kwamba pindi nitakaporudi Dar es Salaam, nimtaarifu ili aje tuyaweke sawa na mama J.
Nilimuuliza dada kama amelipia tiketi ya ndege, naye akasema kwamba wifi yake, Iryn, alikuwa amelipia tayari na amemwingizia pesa nyingi kwenye akaunti yake, ingawa hakutaka pesa hizo. Dada alifungua app ya benki na kunionesha kiasi ambacho aliingiziwa, na nilibaki nikishangaa.
Mwishoni, dada alinipongeza kwa kuwa baba, akisema kuwa Aria ni damu yetu halali. Maneno yake yalinipa furaha kubwa na kunitia moyo zaidi. Tuliagana kwa kukumbatiana, kisha tukarudi ndani kuendelea na mambo mengine, kwani tulikuwa tumetumia muda mwingi sana kwenye maongezi yetu.
Kibarazani, akina Jimmy walikuwa wanacheza last card, na mimi nilijiunga nao, tukawa jumla wanne: Mimi, Jimmy, Vivian, na Samantha. Mchezo ulikuwa mzuri sana, maana tulianza hadi kuweka hela kwa mshindi, na hali hiyo ilifanya ushindani uwe mkali. Baadaye, dada alikuja na tukawa jumla watano, na mchezo ukawa na ladha mpya, huku kila mmoja akijaribu kushinda kwa njia yake. Kicheko na furaha vilijaza hewa, na ilikuwa ni fursa nzuri ya kuondoa mawazo na kufurahia muda pamoja.
Ninataka niwaambie kuhusu undugu wa Jimmy, Iryn, Vivian, na Samantha. Ninarudisha hadi chapter 9, siku ambayo nilifika Ethiopia kwa mara ya kwanza. Katika siku hiyo, dada watatu walikuja kumpokea Iryn, ambapo alinitambulisha. Yule dada mkubwa ndiye alikuwa Vivian, mtoto wa Pili wa mama mkubwa, huku Jimmy akiwa mtoto wa kwanza akifuatiwa na mdogo wake katika wale wawili waliokuwa wamekuja kumpokea Iryn.
Hawa watatu wa kwanza, Vivian, Jimmy, na mdogo wao, wanatoka kwenye tumbo moja, wakiwa na mama na baba mmoja, ingawa baba yao alishatangulia mbele za haki. Mama mkubwa alizaa watoto wengine wawili na mume mwingine, Samantha na mdogo wake wa mwisho. Huyu mdogo wa mwisho ndiye mmoja kati ya wale dada wawili wadogo ambao Iryn alinifahamisha kama wadogo zake.
Mama mkubwa ana jumla ya watoto watano. Watatu wa kwanza wanashiriki baba mmoja, wakati hawa wawili wa mwisho wanashiriki baba mwingine. Kati ya watoto hao watano, Jimmy pekee ndiye mtoto wa kiume. Kwa Iryn, watoto hawa ni kama binamu zake (cousins), ingawa yeye hupenda kuwaita dada na kaka.
Nilikaa sana pale nyumbani, na hatimaye mimi na Jimmy tuliondoka saa 6 usiku kurudi hotelini. Nilipitia mapokezi kuchukua kadi yangu, na dada wa mapokezi akaniambia kuwa kuna ujumbe wangu. Alinipa kadi na kikaratasi kidogo. Nilielewa kinachoendelea mara moja, na Jimmy aliona yote hayo, akabaki kutabasamu.
Baada ya kuingia chumbani, nilifungua kile kinote na kugundua kuwa ilikuwa ni namba ya simu ya Nala. Niliweka pembeni na kuelekea bafuni kuoga. Baada ya kumaliza kuoga, nilijilaza kitandani, nikiwa nimechoka lakini mawazo yakiwa hayajakaa sawa. Nilianza kuyapitia kwa kina yale mazungumzo yangu na sister, nikitafakari maana yake na mwelekeo wa mambo.
Ukweli ni kwamba, Sister alizungumza mambo mengi sana, lakini kubwa kuliko yote, aliniapia kwamba nikifanya makosa tena, basi atajiondoa kabisa kwenye huu msala, na niachwe nipambane peke yangu. Sister ndiye kiungo muhimu katika kufanikisha hili jambo, hivyo niliona ni busara kutulia na kuwekeza nguvu zangu kwa umakini kwenye familia zangu.
Niliwaza sana kuhusu wazo la kumuacha Mary, lakini kila nilipofikiria, nilijikuta nikipoteza nguvu kwa sababu bado nampenda. Hata hivyo, kutokana na ushauri wa Sister, niliona sina budi kufanya hivyo. Ni bora nimuache mapema kuliko kusubiri na kuleta matatizo makubwa zaidi huko mbeleni.
Niliwaza sana na hatimaye nikaamua kwamba nitakaporudi Dar es Salaam, nitamtafuta Mary ili tuzungumze wazi kuhusu hili suala. Kilichonipa faraja kidogo ni kwamba Mary tayari alikuwa anafahamu kinachoendelea kuhusu mahusiano yangu na Iryn, hivyo nilihisi mazungumzo yetu yangeweza kuwa ya uwazi zaidi.
Jambo lingine lililoanza kunisumbua kichwani ni jinsi wazazi wangu watakavyopokea taarifa za mimi kuzaa na Iryn. Swali kubwa lililozunguka mawazoni mwangu lilikuwa, je, watalichukuliaje suala hili? Nilijua kuwa na mtihani mgumu mbele yangu, lakini kwa sababu Sister aliahidi kunisaidia, nilijisemea kwamba kila kitu kitakuwa sawa. Hata hivyo, sikupuuza uzito wa hali hiyo.
Kwa upande wangu, nilitamani sana kuona Junior na Aria wakifahamiana tangu utotoni ili waweze kujenga uhusiano wa karibu na bond nzuri. Kuhusu hili suala, nilihisi mzee ndiye anayeweza kunipa ushauri mzuri zaidi. Hivyo, nilianza kupata hamasa ya kumtafuta mapema ili tuweze kuzungumza na kupanga namna bora ya kufanikisha hili.
*****
Asubuhi, baada ya kuamka, nilimpigia simu mama J ili kumsalimia, lakini hakupokea, hivyo nilihisi labda alikuwa ameenda kanisani. Niliingia bafuni haraka kuoga na kujiandaa ili tuweze kwenda kwa mama mtoto. Ilikuwa saa mbili asubuhi, na nilihisi muda ulikuwa unayoyoma. Nilimpigia simu Jimmy kumjulisha kuwa tuanze safari, lakini naye hakuwa akipokea. Hatimaye, nikaamua kwenda kumgongea chumbani kwake.
Baada ya kufika kwenye chumba chake, maana yeye alikuwa floor ya juu, niligonga mlango na alitoka kufungua. Alikuwa haja jiandaa, hivyo nilipompa taarifa ya kuondoka, aliniambia nimsubiri ajiandae haraka. Nikamwambia atanikuta kwenye restaurant nikimsubiri.
Nilielekea kwenye restaurant kupata kifungua kinywa, na wakati huo nilikuwa nawasiliana na Iryn, ambaye alikuwa akinisisitizia nianze safari mapema ili niweze kucheza na mtoto. Baada ya nusu saa, nilimuona Jimmy akiwa ameongozana na mwanamke mwenye asili ya kizungu, na nikahisi huenda alikuwa amelala naye. Hali hii iliniacha na maswali mengi kichwani mwangu.
Walipofika, waliketi pamoja nami, na Jimmy alifanya utambulisho wa kawaida, na mimi pia nilimsalimia yule dada. Waliagiza kifungua kinywa, na baada ya kumaliza, tuliondoka kwenye eneo hilo, tukimwacha dada akisubiri usafiri wa kumpeleka kwake.
Wakati tuko kwenye Uber, nilianza kumuuliza Jimmy maswali kuhusu yule mwanamke. Nilikuwa na hamu ya kujua zaidi kuhusu mahusiano yao, na jinsi alivyomjua.
MIMI: “Bro, yule ni nani tena?”
JIMMY: “Tulikutana juzi Soho club, tukabadilishana namba, jana baada ya kuchat naye, nilimpanga aje hotelini akakubali.”
MIMI: “She’s a hoe?”
JIMMY: “I don’t think so, anafanyia kazi kwenye moja ya ubalozi hapa South Africa.”
Nilibaki kimya, nikitafakari kwa undani. Jimmy alikuwa amenishinda kabisa kwa tabia zake. Nilijiuliza mara ngapi ameweza kukutana na wanawake kama yule, na ni wangapi mpaka sasa? Spidi yake ilikuwa ya kutisha, na ilinifanya nishindwe kuelewa vizuri mwelekeo wake. Nilijikuta nawaza kama angeweza kudhibiti hali hii, au kama ilikuwa sehemu ya maisha yake ya kila siku.
Baada ya kuwasili, mazingira yalionekana kuwa kimya na tulivu sana. Tulipofika kibarazani, mtoto wa Jimmy alionekana akicheza peke yake. Jimmy alimnyanyua kwa furaha, kisha tukaingia ndani kuzungumza na mama mtoto ili tupate kujua ratiba ya siku ile.
Pale sebuleni, dada yangu alikuwa amemshika mtoto, na tukaingia kwenye mazungumzo kuhusu safari yake. Alisema anatarajia kuanza safari saa 11 jioni. Wakati huo, Iryn alitoka sebuleni na kuja kukaa pembeni yangu. Alionekana kuzidi kuimarika kadri siku zilivyokuwa zinaenda, jambo lililonipa faraja. Mazungumzo yetu yaliendelea kwa utulivu, na hali ilikuwa ya amani.
Baada ya kula chakula cha mchana, mimi, dada yangu, na mama mkubwa tuliamua kuwa na kikao chetu binafsi. Tulitafuta utulivu nje kwenye bustani, mbali na kelele na muingiliano wa watu wengine. Hapa tuliweza kuzungumza kwa uwazi na utulivu, tukijadili mambo muhimu bila usumbufu wowote. Mazingira yalikuwa tulivu, na kikao kilikuwa na uzito wa kipekee.
Mama alianza kwa kumshukuru sana sister kwa kujitolea kwake kwa kipindi chote hadi Iryn alipojifungua. Sister alisaidia sana, hasa kwenye mazoezi na mbinu mbalimbali za kuhakikisha Iryn anajifungua salama. Kwa kuwa sister yangu tayari alikuwa na watoto wawili, alikuwa na uzoefu mwingi ambao ulimsaidia kumwelekeza Iryn vyema wakati wa ujauzito na hadi wakati wa kujifungua. Mama alionyesha shukrani za dhati kwa mchango wake mkubwa.
Ukiachana na yote, Sister aliweza pia kutengeneza mahusiano mazuri sana na wifi zake, kama Vivian na Samantha. Wote walionekana kumpenda sana dada yangu kwa jinsi alivyojitoa na kujali. Uhusiano wao ulijengeka kwa upendo na uelewa, na hilo lilifanya familia kuwa karibu zaidi.
Kuhusu suala la mimi kumpa mimba binti yake, mama alisema hawezi kusema lolote kwa sababu Iryn mwenyewe alifanya maamuzi yake, na ni mtu mzima ambaye anaelewa vyema anachokifanya. Alionyesha kutambua kwamba Iryn alikuwa na uwezo wa kuchukua maamuzi yake binafsi, na hakutaka kuingilia zaidi. Hii ilileta hali ya unafuu kidogo, ingawa suala hilo bado lilikuwa na uzito wake.
Mama aliniuliza swali ambalo lilikuwa zito kulijibu:
“Una mpango na malengo gani juu ya Iryn?"
Nilihisi uzito wa swali hilo, lakini nilijua dhumuni la mama kuuliza ni nini. Nikajua kwamba ni muhimu kufikiri kwa umakini na kuepuka kutoa ahadi ambazo huenda nisitekeleze. Kwa kutumia busara na tahadhari, nilimjibu hivi:
MIMI: “Asante mama kwa kuniuliza swali hili muhimu. Ninamuheshimu sana Iryn na ninatambua nafasi yake katika maisha yangu. Nimeliona hili suala kwa uzito wake, na ninataka kuhakikisha kwamba mimi na Iryn tunajenga msingi mzuri wa ushirikiano, hasa kwa ajili ya ustawi wa mtoto wetu. Nataka tuchukue mambo hatua kwa hatua, huku tukijadiliana na kupanga vizuri mustakabali wa familia yetu. Ninaendelea kutafakari juu ya mpango mzuri na utakaokuwa bora kwa wote, na nataka kuhakikisha kwamba kila kitu kinawekwa wazi na kwa manufaa ya pande zote mbili.”
Mama na Sister waliniangalia kimya kwa muda, wakitafakari majibu yangu. Mama, hasa, alionekana kutotarajia jibu langu. Niliona machoni mwake kwamba alitarajia kitu tofauti, labda ahadi thabiti au mpango ulio wazi zaidi kuhusu mustakabali wangu na Iryn.
MAMA: “Naona umejibu kwa hekima, lakini bado sijapata uhakika. Wewe na Iryn, mna mpango wa kuwa pamoja au hili ni suala tu la mtoto?”
MIMI: “Naelewa unavyohisi mama, na ni swali lenye uzito. Kwa sasa, mimi na Iryn tunaendelea kuzungumza juu ya mstakabali wetu. Kipaumbele chetu kikubwa ni kuhakikisha mtoto anakua katika mazingira bora, lakini bado tupo kwenye hatua ya kufikiria kwa kina jinsi ya kutatua hali yetu ya kibinafsi. Siwezi kusema kwa hakika wakati huu, ila nataka iwe wazi kwamba sitamtelekeza Iryn wala mtoto wetu.”
MAMA: “Hilo ni jambo jema kusikia, lakini ningependa kuona mnapanga mustakabali wenye utulivu zaidi, hasa kwa ajili ya binti yangu. Matarajio yangu ni kwamba, kama kuna upendo na nia njema, basi mtachukua hatua ya kusonga mbele pamoja.”
MIMI: “Ninakubaliana na wewe kabisa mama, Iryn ni mtu muhimu kwangu na sina mpango wa kufanya maamuzi ya haraka bila kufikiria kila mtu aliyehusika. Ni muhimu kwangu kwamba wote tunakuwa na maelewano mazuri kwa ajili ya mtoto na hatimae, kwa Iryn pia.”
MAMA: “Nashukuru kwa uwazi wako, ningependa tu kuona unachukua hatua thabiti, maana Iryn anastahili uhakika. Si kwamba nakuwekea shinikizo, lakini ningependa kuona binti yangu akiwa kwenye mikono salama.”
MIMI: “Naelewa mama, na ninakuhakikishia kwamba natilia maanani kila kitu unachosema. Nitafanya kila niwezalo kuhakikisha mambo yanaenda vizuri kwa Iryn na mtoto wetu.”
Mama aliniangalia kwa makini, na nilihisi alikua akiwaza, labda akijiuliza, “Huyu jamaa ana akili sana.” Nilijua kuwa niliyajibu maswali yake yote kwa umakini na hekima. Hata dada yangu alionesha tabasamu, akionyesha kushangazwa na jinsi nilivyoweza kujibu maswali ya mama kwa njia ambayo haikuniingiza kwenye mtego.
Mama aliendelea na mazungumzo, akasema angependa kuwajua wazazi wetu, akisisitiza kuwa ni muhimu kwa mustakabali wa mtoto. Aliongeza kwamba sasa sisi tumeshakuwa muunganiko wa familia, na ni muhimu kuimarisha uhusiano huu kwa kuhakikisha kila mmoja anajua historia na asili ya mwingine. Mama alionyesha kuwa na hamu ya kujenga mshikamano ndani ya familia yetu, ili mtoto apate msingi mzuri wa malezi na urithi wa kihisia.
Baada ya kumaliza mazungumzo yetu, Sister alijiandaa kwa ajili ya safari yake ya kurudi Tanzania. Hali ilikuwa ya huzuni kidogo, lakini pia ya furaha kwa sababu tulikuwa tumepata muda mzuri wa kuzungumza na kujenga uhusiano wetu zaidi.
Saa 9 mchana, Sister alitoka na begi lake na kutuaga pale sebuleni. Tulitoka nje na kupiga picha za pamoja kama kumbukumbu ya wakati wetu mzuri pamoja. Baada ya hapo, mimi na Vivian tulimpa kampani hadi uwanja wa ndege. Safari hiyo ilikuwa ya furaha, ingawa tulihisi huzuni kidogo kwa sababu ya kuachana. Tulizungumza mengi katika gari, tukijadili mipango ya baadaye na sister kuahidi kukutana tena na kina Vivian hivi karibuni.
Tukiwa airport, tulizungumza mambo mengi sana, na Sister aliendelea kunisitiza kwamba nitakaporudi Dar es Salaam, nimpe taarifa ili aje nyumbani kuweka sawa masuala yangu na mama J. Kabla ya kucheck in, aligana na Vivian kwa kukumbatiana kwa upendo, na niliona jinsi walivyokuwa na uhusiano mzuri. Baada ya hapo, tuliondoka maeneo hayo, tukielekea nyumbani, tukiwa njiani story na Vivian ziliendelea na niseme hawa mashem zangu wananikubali na tunapatana sana.
Usiku, niliwasiliana na mama J pamoja na mwanangu Junior. Nilimdanganya kwamba nipo China nikifuatilia mzigo, na baada ya hapo nitatoka kwenda South Africa kumuona Iryn, ambaye amejifungua mtoto. Mama J hakutoa maoni mengi kuhusu hilo, zaidi alisema atawasiliana na Iryn kumpa hongera. Ingawa alionekana kutokuwa sawa na hali hiyo, nilijua ujumbe wangu ulikuwa umemfikia.
*****
Wiki inayofuata, ambayo ilikuwa ni wiki ya kwanza ya mwezi wa 7, idadi ya wageni iliongezeka sana pale kwa Iryn. Ndugu zake kutoka Ethiopia walifika, na pia marafiki zake wa chuo waliosoma pamoja Ufaransa walikuwa wakija na kuondoka. Sebuleni, kila kona ilikuwa imejaa zawadi za mtoto, na hapo ndipo nilipogundua kwa kweli kwamba Iryn alikuwa na mtandao mpana wa watu. Hali hiyo ilionyesha jinsi alivyokuwa akipendwa na kuungwa mkono na watu wengi, na ilifanya moyo wangu ujaze faraja na kujivunia kuwa sehemu ya maisha yake.
Siku ya Jumatano, mama mkubwa aliondoka kurudi Ethiopia ili kuendelea na majukumu yake. Pia, dada wa kazi kutoka Ethiopia alifika nyumbani kusaidia katika kazi mbalimbali. Iryn alieleza kuwa hakutaka dada wa kazi mwenyeji kwa sababu ya tabia zao, hivyo alihitaji mtu ambaye wangeweza kuendana kiutamaduni. Hali hiyo ilionyesha umuhimu wa mazingira yanayofanana na utamaduni wao, na niliona ni busara kwa Iryn kuchagua mtu ambaye angeweza kuleta utulivu na uelewano katika familia.
Siku ya Jumapili, Jimmy pamoja na familia yake waliondoka kurudi Ethiopia, hivyo aliyebaki ni dada Vivian. Baada ya kuondoka kwa Jimmy, nilienda kukaa na Iryn, maana idadi ya watu ilikuwa imepungua, na mle ndani tulikuwa jumla watano. Hali hiyo ilituletea fursa nzuri ya kuzungumza kwa undani zaidi na kujenga uhusiano wetu.
Wiki ya pili ya mwezi wa 7, Jumatatu, bibi yao ‘Momo’ alifika South Africa kumuona kitukuu chake. Aliwasili jioni, na mimi na Samantha tulikwenda kumpokea pale airport. Momo, ambaye sasa ana umri wa miaka 70, ni bibi mwenye uzoefu wa maisha, lakini bado ana nguvu za kujiendesha. Momo ana tabia ya kutabasamu na kuwa na nishati, na nilijua kwamba uwepo wake ungeongeza furaha na umoja katika familia yetu.
Tangu tupo kwenye gari hadi tulipofika nyumbani, Bibi alikuwa na furaha sana na alionyesha hamu kubwa ya kumuona kitukuu wake. Alikuwa akizungumza kwa lugha yao ya nyumbani, lakini Samantha alikuwa ananiambia kila kilichokuwa kinaendelea, akitafsiri maneno ya bibi kwa urahisi. Ilikuwa ni furaha kubwa kusikia shauku ya bibi, na niliweza kuhisi upendo wake wa dhati kwa familia.
Baada ya kufika nyumbani, Iryn hakuwa mbali kumpokea bibi yake, na walikumbatiana kwa furaha na kumkaribisha ndani. Kitu cha kwanza bibi alichomba ni kumuona kitukuu wake, na alifurahi sana baada ya kumuona. Uso wake ulijawa na tabasamu la furaha, na Iryn alionekana pia akifurahia moment hiyo. Nilijua kuwa bibi alikuwa na matumaini makubwa kwa ajili ya kitukuu chake, na nilihisi furaha kuona jinsi familia ilivyokuwa ikijenga uhusiano mzuri katika kizazi tofauti.
Baada ya bibi kurudi nyumbani, mazingira yalichangamka sana, kwani bibi ni mwongeaji sana, na wajukuu zake wanampenda sana. Bibi alisema ataendelea kukaa na Iryn na hafikirii kurudi Ethiopia mapema, jambo lililomfanya Iryn ajisikie vizuri. Iryn ni mjukuu ambaye bibi yake anampenda sana, na hii ni kwa sababu Iryn humjali sana bibi yake, akimpa huduma na kumuhudumia kwa upendo.
Kwa upande wangu, tangu nilipofika South Africa, tayari wiki mbili zilikuwa zimepita, na nilipanga kuondoka Jumapili ya weekend. Niliangalia hali yangu na kugundua kwamba kuendelea kukaa huku kungeweza kuathiri mambo yangu mengi, kuanzia kampuni hadi biashara zangu. Nilijua ni muhimu kurejea nyumbani ili kusimamia masuala yangu na kuhakikisha kila kitu kinaenda sawa. Ingawa nilifurahia wakati niliokuwa pamoja na Iryn na familia, nilihisi ni lazima nitafute njia ya kuleta uwiano kati ya majukumu yangu ya kifamilia na biashara zangu.
Kesho yake asubuhi, nilimfata Iryn chumbani ili niweze kuzungumza naye kuhusu suala langu la kuondoka. Pembeni yake kulikuwa na diary, hivyo niliichukua na kuanza kuisoma. Niliona alikuwa akiandika mipango yake, na nilicheka baada ya kuona ameandika mpango wa kuanza gym.
Of course, alikuwa ameanza kunenepa sana kutokana na kuwa mama na vyakula anavyokula, lakini bado haikufanya apoteze uzuri na shape yake. Kinyume chake, niliona kuwa mabadiliko hayo yaliongeza mvuto wake, na alikuwa akionekana kuwa na uzuri wa kipekee ambao unakuja na umama.
MAMA ARIA: “Darling, unacheka nini?”
MIMI: “Nimefurahi kuona una mpango wa kuanza Gym, lakini bado mapema sana.”
MAMA ARIA: “I know, baada ya miezi 3 nitaanza mazoezi ya kupunguza huu mwili.”
Nami, nikasogea kukaa pembeni yake;
MIMI: “Nimekumiss baby mama.”
Iryn alianza kuangalia usawa wa bunduki yangu na akanishika kidevu changu na tukaanza kuangaliana pale;
MAMA ARIA: “Are you horny?”
MIMI: “Ofcourse yes.”
MAMA ARIA: “Pole! nadhani unakumbuka siwezi kusex kwasasa hadi nipone vizuri, doctor alishauri baada ya miezi 3, ila mwezi ujao nitaenda kuangalia maendeleo.”
MIMI: “Naelewa usijali, mimi nitavumilia kwa hili.”
Usawa wa matiti yake ulionekana kulowa maziwa, kwani chuchu zake zilikuwa bado zimesimama. Baada ya kumuona vile, ilibidi nimwambie kwamba analowa, akicheka kidogo kwa aibu. Alijua kwamba hali hiyo ni ya kawaida kwa mama anapokuwa katika kipindi hiki, lakini nilijua kwamba ilikuwa ni muhimu kwake kujisikia vizuri kuhusu mwili wake.
MAMA ARIA: “Mwanao hataki kunyonya, halafu mama yake nina maziwa mengi sana. Uwe unamsaidia mwanao kunyonya, kwani naishia kuyakamua na kuyamwaga. Nikupe unyonye? Yatakusaidia kiafya.”
Nilihisi aibu baada ya kusikia haya maneno kutoka kwa Iryn. Aliponigeukia na kunipa ishara ya kunyonya, sikuona sababu ya kukataa, kwani alikuwa anayamwaga. Nilijisemea, si afadhali nikanywa mimi kuliko yamwagwe. Nilianza kuyanyonya taratibu hadi aliposema basi, ndio kuacha na yalikuwa ni matamu sana.
MAMA ARIA: “Vipi matamu?”
MIMI: “Yeah! Aria anafaidi sana.”
MAMA ARIA: “Mwanao mpole kama wewe, naona huyu atarithi tabia zako.”
MIMI: “Bado mtoto, akikua ndio tutajua tabia zake, hata Junior alikuwa mpole kama Aria, ila sasahivi ni balaa.”
Tulipoanza mazungumzo yetu, alizungumzia suala lake la kurudi shule na akaniambia kuwa analiwazia kwa umakini. Nami nikamshirikisha mpango wangu wa kurudi shule mwezi wa kumi, ambapo alinisisitiza kwa upendo kuwa ni vema nisomee masomo yangu ya masters nchini Afrika Kusini ili tuwe karibu na mtoto wetu.
Ingawa wazo hilo lilikuwa zuri, nilijua kuwa kulikuwa na changamoto nyingi zinazoweza kufanya isiwezekane. Hivyo, nilimpatia jibu lililofikiriwa vizuri, ambalo alielewa kwa upole na busara.
Nilimwambia kwa upole,
“Baby mama, nikisomea huku, kumbuka kuwa mambo mengi yanaweza kuyumba, kuanzia kampuni yako hadi miradi yangu. Ufuatiliaji wa karibu ni muhimu sana. Acha mimi nisomee Dar ili niwe karibu na biashara zetu. Kuhusu Aria, nitakuwa nakuja mara kwa mara kuwasalimu, siwezi kukaa muda mrefu bila kumuona binti yangu. Kama vile wakati wa ujauzito wako ulivyokuwa ukija Dar es Salaam mara kwa mara, sasa ni zamu yangu kuja Cape Town. Tutaendelea kuwa karibu, hata kama nitakuwa huku.”
Mama Aria alifurahi sana kusikia maneno yangu, na hakuwa na la kusema zaidi. Baadaye, nilimueleza kuhusu mpango wangu wa kuondoka Jumapili. Hata hivyo, kwenye suala la kuondoka, alionekana kulipokea tofauti na aliniomba niondoke mwisho wa mwezi. Nilijaribu kumsihi kwa upole, na kumuomba aniruhusu niondoke wiki ijayo, huku nikiahidi kuwa nitarudi mapema kwa ajili ya sherehe ya "Simchat Bat" ya mtoto wetu.
Baada ya kumaliza mazungumzo yetu, aliamua kwenda kuoga. Wakati huo, Aria alikuwa ameamka, hivyo nilimbeba na kutoka naye sebleni ili tupate muda wa kukaa pamoja. Sikuwa na shughuli nyingi za kufanya kipindi hicho nikiwa Afrika Kusini, zaidi ya kutumia muda wangu mwingi kucheza na Aria. Sikutoka kwenda sehemu yoyote mara kwa mara, isipokuwa tu kwenda supermarket pale panapohitajika.
Haikupita muda mrefu kabla mama Aria hajarudi kwenye seating room, na kunijulisha kuhusu ujio wa mgeni. Aliniambia kuwa anayekuja ni kaka yake, ambaye ni wa kwanza kwa upande wa mama mwingine. Nilikuwa nimeshaongelea kidogo kuhusu huyu kaka yake, katika Season 1: EP10.
Mchana ule, kaka yake alifika nyumbani kumsalimia Iryn pamoja na mtoto, akiwa ameongozana na mpenzi wake. Hii ilikuwa mara yangu ya kwanza kumuona kaka yake kwa upande wa baba. Ni kijana mwenye haiba fulani ya "manton," kwa mbali anataka kuendana na rappa AKA.
Tulisalimiana pale, kisha tukaingia kwenye mazungumzo ambapo alinikaribisha sana Afrika Kusini kwa ukarimu. Iryn akaanza kumuuliza kaka yake kuhusu maisha na kazi kwa ujumla. Ingawa kaka yake Iryn yuko vizuri kiuchumi, tatizo lake kubwa ni matumizi ya madawa, jambo ambalo limemuharibu sana. Niliwahi kugusia kuhusu hili hapo awali.
Baada ya kupata chakula cha mchana kwa pamoja, kaka yake na mpenzi wake waliondoka. Mama Aria kisha alinipa taarifa nyingine kwamba siku ya Jumamosi tungeenda nyumbani kwa baba yake. Aliongeza kuwa kuna mambo kadhaa watakayokwenda kuyapanga na mzee wake, na akaniambia atanishirikisha katika hayo mazungumzo siku hiyo.
*****
Hatimaye, siku ya Jumamosi ilifika, siku ambayo ilikuwa ni ya kwenda kwa mzee Virgil, baba mkwe wangu. Mzee Virgil alikuwa akija mara kwa mara nyumbani kumuona mjukuu wake, na kitendo cha Iryn kujifungua kilimfurahisha sana. Hakuwa na maswali mengi kuhusu malengo yangu kwa binti yake, wala hakujishughulisha na hilo. Kile kilichomgusa zaidi kilikuwa ni upendo mkubwa aliokuwa nao kwa mjukuu wake. Ilionekana kana kwamba alikuwa akitamani kwa muda mrefu sana kupata mjukuu, na sasa alikuwa akifurahia kila muda aliokuwa naye.
Saa nne asubuhi, gari lilikuja kutuchukua kwa ajili ya safari ya kwenda nyumbani kwa mzee Virgil. Tuliondoka watatu tu, mimi, Iryn, na Samantha. Safari yetu ilikuwa na umbali wa takriban kilomita 45 hadi kufika nyumbani kwa mzee, Somerset West, ambayo iko pembezoni mwa Cape Town. Huu ni sawa na umbali wa kutoka Mwenge hadi Bagamoyo. Njia ilikuwa nzuri, na tulikuwa na mazungumzo mazuri kwenye gari, tukiwa na hamu ya kufika na kumtembelea mzee.
Mzee aliamua kujenga na kuishi nje kidogo ya mji wa Cape Town, na tulivyoanza kuingia katika maeneo haya, nilikuwa nikiona majumba ya kifahari ambayo yalivutia sana macho yangu. Mazingira ya hapa ni kama Ulaya, ni masafi, na kote ni lami, hakuna vumbi. Nyumba zimepangiliwa kwa ustadi wa hali ya juu, mandhari yake ikiwa ya kijani kibichi. Wakati tunaingia Somerset, tulikuwa tukipishana na magari ya kifahari, hali iliyoongeza uzuri wa eneo hili.
Gari lilipaki nje ya geti kubwa, na haikuchukua muda mrefu likafunguliwa, ingawa pale getini hakuonekana mtu yeyote aliyefungua. Tulipofika ndani, gari lilitembea kwa mwendo wa takriban mita 100, na njiani tulipishana na bustani nzuri ya kuvutia.
Baada ya kufika usawa wa nyumba, tulishuka na mbele yangu nikaona bonge la mjengo wa kifahari, aina ya villa. Ilikuwa nyumba kubwa ya kisasa ya ghorofa moja, na kila kipengele chake kilionekana kuwa kimepangwa kwa umaridadi. Ujenzi wa nyumba hiyo ulikuwa wa kisasa na wa kuvutia, ukionyesha ushawishi wa hali ya juu wa usanifu. Ilionekana kama ni mahali pazuri pa kuishi, ambapo mandhari ya karibu iliongeza uzuri na raha ya mazingira.
Wakati huu, mama yake mdogo alitoka kutupokea akiwa na wanae, na haikuchukua muda mzee Virgil akatoka kumkaribisha binti yake. Alikuwa na furaha kubwa sana kutuona na aliomba kumbeba Aria, Mzee Virgil alionyesha upendo mkubwa kwa mjukuu wake.
Nilisikia sauti ya upole kutoka kwa Iryn ikinikaribisha kwa furaha:
“Baba Aria, hapa ndiyo nyumbani, karibu sana.”
Tulipokuwa tunaingia ndani, nilikutana na bonge la msebule uliojaa mapambo ya thamani kubwa kama crystals na marbles. Nimeingia katika nyumba nyingi za kifahari, lakini sebule ya kwa Mzee Virgil ilikuwa ya kipekee kabisa. Ukarabati wa ndani ulikuwa wa kiwango cha juu, na kila kipande cha samani na mapambo kilionyesha umaridadi na mtindo wa kipekee, ikifanya iwe mahali pa kuvutia.
Iryn alianza kunitambulisha kwa wadogo zake wa pale nyumbani kwa upande wa mama mdogo. Mama mdogo ana watoto watatu tu; mtoto wa kwanza ni wa kike, ambaye nilimfahamu nikiwa hospitalini, alikuwa akitarajia kuanza chuo mwaka huo na wawili ni wa kiume, wenye umri wa miaka 13 na 8. Walionekana kufurahia kuniona na walikuwa na shauku ya kujua kuhusu mimi, hali ambayo ilileta maongezi yawe mengi zaidi.
Baada ya lisaa, wageni watano walifika, na kati yao, mmoja tu alikuwa na asili ya Afrika; wengine wote walikuwa wazungu. Kati ya wageni hao, mmoja alikuwa ni babu, na aliomba amshike Aria. Mzee Virgil alifanya utambulisho pale, akimwambia Iryn kwamba wale ni ndugu zake. Iryn alifurahi sana kusikia hivyo, kwani kwa upande wake alikuwa kwenye mission ya kuwasogeza karibu ndugu wote wa upande wa baba yake. Hali hiyo ilileta hisia za umoja na furaha, na ilikuwa ni fursa nzuri kwa familia kukutana na kuimarisha uhusiano wao.
Tulipata chakula cha mchana pamoja, na baada ya wageni kuondoka, Iryn alitoka nje na mzee wake kufanya mazungumzo. Walionekana kuwa na mazungumzo ya karibu na ya kina, hii ilikuwa ni nafasi nzuri kwao kujadili mambo ya familia na kujenga msingi mzuri wa ushirikiano.
Wakati huu, nilikuwa na mama mdogo tukifanya mazungumzo, ambapo aliendelea kunikaribisha kwa ukarimu. Alizungumza kwa upole, akielezea furaha yake kuwa na familia pamoja na jinsi alivyovutiwa na ujio wangu.
Baada ya lisaa, Iryn aliniita nitoke nje ili tuweze kuzungumza na mzee wake. Alimweleza baba yake jinsi ambavyo nimekuwa msaada mkubwa sana katika biashara zake. Mzee wake alishukuru kwa dhati na kusema niendelee kuwa na moyo huo huo. Alionyesha furaha kubwa kwa mimi kuwa sehemu ya familia yake.
Kuhusu suala la kumzalisha binti yake, mzee hakuwa na neno lolote la kukatisha tamaa. Badala yake, alitutakia mafanikio mema na kusema angetamani kuona tukifika mbali zaidi katika maisha yetu.
Mzee aliondoka pamoja na mjukuu wake, na kutuacha mimi na Iryn tukiendelea na mazungumzo yetu. Iryn alianza kunishirikisha kuhusu kazi kubwa aliyonayo katika kuzisimamia kampuni za baba yake. Aliniambia kuhusu mali mbalimbali anazomiliki baba yake hapa Afrika Kusini, ikiwa ni pamoja na apartments, mashamba ya zabibu, na kampuni ambayo ni miongoni mwa waexporter wakubwa wa wines.
Alielezea jinsi alivyohusika katika kusimamia shughuli hizi na jinsi anavyopanga mipango ya kuziendeleza zaidi. Hali hiyo ilionyesha kiwango cha juu cha kujitolea kwake na uelewa wa biashara, na ilinipa mtazamo mzuri kuhusu familia yao na malengo yao ya kifamilia.
Tangu siku ile tulipokutana na Iryn na kuanza mahusiano yetu, hakujawahi kuwa na wakati ambapo alitaja utajiri wa baba yake. Badala yake, alijikita zaidi katika kunieleza kuhusu majukumu aliyokabidhiwa ya kuwa msimamizi wa kampuni za baba yake. (SEASON 1: EP40)
Hii ndiyo siku nilipogundua kwamba mzee Virgil si mtu wa kawaida, kwani ana utajiri wa kutisha. Lakini ukimwona, unaweza kumchukulia kuwa mtu wa kawaida sana. Kama mnavyojua, wazungu hawana tabia ya kujionesha kama wana fedha, tofauti na sisi Waafrika, ambao mara nyingi tunapenda maonyesho ya kifahari.
Iryn aliendelea kunieleza jinsi mzee wake alivyotokea kunikubali sana. Aliniambia kwamba amemshauri atulie nami, kwani kwa sasa wanaume wengi hawaaminiki. Maneno hayo yalikuwa ya faraja kutoka kwa Iryn, yakiwa na uzito wa maana. Nilimuhakikishia kuwa nitajitahidi kumsaidia kadri ya uwezo wangu, kwa sababu uaminifu ni msingi wa mahusiano yetu.
Nilimuuliza Iryn kuhusu mgawanyo wa mali za mzee na jinsi anavyowaangalia watoto wengine, wakiwemo Smith na kaka yake mkubwa, ambapo jumla yao ni watoto sita wa mzee Virgil. Iryn alijibu kwamba hadi sasa, watoto wanne tu wanatambulika rasmi, ambao ni yeye pamoja na wadogo zake watatu kwa upande wa mamdogo. Aliongeza kuwa kuhusu kaka yake na Smith, bado hawajazungumza na mzee wao kuhusu suala hilo, lakini wanatarajia kuangalia namna nyingine ya kufanikisha mambo yao.
MIMI: “Na vipi kuhusu mama mdogo?”
IRYN: “Mama mdogo si mmoja wa mrithi wa hizi mali. Alifunga ndoa ya mkataba na mzee, na moja ya makubaliano ni kwamba hatahusika kwenye urithi wa mali zaidi ya watoto tu.”
MIMI: “Baba yako ni genius sana.”
IRYN: “Mali nyingi sana mzee kazipata akiwa na mama yangu. Ndiyo maana unaona mimi nikiwa kipaumbele cha kwanza, hata wakati ambapo hatuko kwenye maelewano na mzee. Kwa upande wake, alikuwa anapata tabu sana kuhusu hili.”
Iryn alikuwa huru kunifungukia mambo mengi sana. Alisema kwamba hata kitendo cha kuzaa na mimi si kwamba alikurupuka tu kufanya maamuzi hayo, bali alifikiria kuhusu mustakabali wake na mali za baba yake. Alieleza kwamba kipindi kile baada ya kurudi kutoka South Africa kumwona mzee wake, aliona kuna umuhimu wa kuwa na watoto ambao wataweza kurithi mali hizo, kwani hata yeye atakufa.
Iryn alifikiria kwa kina na kugundua kwamba hakuna mtu anayemuamini zaidi yangu kwa sasa. Alijisemea atafanya kila mbinu ili anizalie mtoto, lakini lengo lake kubwa ni kuhakikisha urithi wa mali za baba yake unakuwa salama. Aliendelea kueleza kwamba, mama mkubwa wake na ndugu zake wanamuona kama mjinga sana, lakini hawajui mipango yake ya siri. Hakuwa na nia ya kuona mali ambazo mama yake alizichuma na baba yake zikipotea kwa watoto wengine. Kwa hiyo, alichukua maamuzi haya magumu, lakini yaliyojikita katika manufaa ya kizazi chake.
Nilishusha pumzi ndefu sana, nikijisemea kwamba kumbe Iryn yuko very calculated na alikuwa na mipango mikubwa ambayo sikuwa na habari nayo. Nilikuwa bado siamini kwamba Iryn anaweza kubeba mimba kwa sababu ya kijinga kama aliyokuwa akinambia, lakini leo ndiyo nimeelewa kuwa alikuwa anawaza extra miles. Iryn alikuwa na malengo ya dhati, na sasa nilianza kuelewa uzito wa maamuzi yake.
IRYN: “Baba Aria, naomba nisamehe sana kwa kutokushirikisha hili mapema, nilijua ipo siku ungekuja kujua ukweli. Nilikuwa nauwezo wa kuzaa na mwanaume yoyote yule ninayemtaka hata kwa kumlipa na nikapata mtoto, lakini niliona wewe ndio unafaa.”
MIMI: “Naomba tuachane na haya, Aria ni mtoto wetu tuangalie namna gani ya kumlea na kumtunza ili tuje tujisifu kuwa naye.”
IRYN: “Babu yake kafurahi sana kumuona, ndio mjukuu wake wa kwanza. Pia unakumbuka nilikwambia kuhusu afya ya mzee wangu? Hana maisha marefu sana hapa duniani ni pesa tu zinafanya anaendelea kuishi.”
MIMI: “Nakumbuka baby, naamini ataishi muda mrefu zaidi hapa duniani, tusichoke kumuombea.”
IRYN: “Natamani kupata mtoto mwingine, hata nikiwa natembea barabarani, kushoto nina Aria na kulia nina mdogo wake nakuwa na bodyguards wangu.”
MIMI: “Naona unanipa greenlight ya kukupa mimba ya pili.”
IRYN: “Yes! Why not, unafikiri atakuwa nani zaidi yako?”
MIMI: “Sawa baby subiri kwanza Aria akue mengine tutapanga.”
Baada ya mazungumzo marefu, tulianza kutembea na kutalii mazingira ya nyumba yao. Aisee, nyumba yao imezungukwa na bustani nzuri, huku ukubwa wa kiwanja ukiwa kama ekari tano. Tuliposhuka chini, tulikuta mizabibu mingi imepandwa, kuzunguka upande wa nyuma nakutana na swimming pool mbili, moja ya wakubwa na nyingine kwa ajili ya watoto. Nyumba hiyo ilikuwa na mvuto wa kipekee, na mbele zaidi kulikuwa na nyumba ndogo ya wafanyakazi ambao kazi yao ni kutengeneza zile bustani na kumwagilia mimea.
Nilishindwa kuelewa kwanini Iryn ameshindwa kukaa na baba yake na ameamua kupanga aishi peke yake. Sikutaka kumuuliza kuhusu hili, kwani nilijua Iryn ana akili sana na huwa hafanyi jambo lolote bila sababu. Nilihisi kuwa kuna mambo mengi nyuma ya uamuzi wake, lakini kwa heshima yake, niliona bora nisubiri hadi atakapojisikia kuzungumzia.
Saa mbili usiku, tulipata dinner ya pamoja, na baada ya hapo tuliagana kuwa tunaondoka. Walitusindikiza hadi nje, ambapo dereva alikuwa amekuja kutufuata tayari. Tukiwa pale nje, mzee aliendelea kuongea na binti yake, na nilipata fursa ya kubaini upendo mkubwa sana alionao kwa Iryn. Mazungumzo yao yalionyesha uhusiano wa karibu na wa kipekee kati yao, na ilikuwa wazi kwamba Iryn alikuwa na nafasi maalum katika moyo wa baba yake.
Dereva aliyekuwa amekuja kutufuata ni ameajiriwa na mzee na kazi yake ni kwaajili ya kuwapeleka watoto shule na kuwarudisha, au kuwapeleka matembezini.
*****
Wiki ya tatu, nilipanga kuondoka Cape Town siku ya Ijumaa, nikijitayarisha kurudi Dar es Salaam na kuendelea na ratiba zangu za kila siku. Hata hivyo, nikiwa South sikuwa na kazi yoyote ya kufanya zaidi, nilijikuta nikicheza sana na Aria, kwani hiyo ndiyo ilikuwa shughuli pekee iliyonipa furaha na kunifanya nijisikie hai.
Kwa upande wa Mary, mawasiliano yetu yalikuwa yanaendelea vizuri, na yeye kwa upande wake alionyesha wazi hamu ya kuniona na alitaka anione mapema iwezekanavyo. Alikuwa akiendelea kuniambia kwa kusisitiza ni kwa sababu ya kutamani kuungana tena na mimi, na alilalamika kidogo kuhusu kuchelewa kwangu kurudi.
Siku ya Jumatano, nilitoka na Iryn kwenda kukagua biashara yake ya saloon, ambayo ni kubwa sana na ina wafanyakazi wengi. Iryn alionekana kuguswa sana na hali ya wafanyakazi, akilalamika kuhusu jinsi watoto wa South walivyo wavivu katika kazi zao. Alisema anafikiria kuandaa mpango wa kuajiri watu kutoka nchi za jirani ili kuongeza ufanisi na kuleta mabadiliko chanya katika biashara yake.
Ijumaa usiku, kabla ya safari yangu, nilikuwa na mazungumzo ya mwisho na baby mama yangu. Katika mazungumzo yetu, habari kubwa aliyonipa ilikuwa kuhusu kufuatilia kampuni ya mzee wake, ambayo alidhulumiwa na wabongo. Alionyesha wasiwasi kuhusu jinsi anavyoweza kusaidia katika kurejesha haki na kuleta uwazi katika mambo haya.
Nakumbuka niliwagusia kidogo kuhusu kampuni za ujenzi na umeme ambazo baba yake alikuwa anazimiliki hapa Dar es Salaam, mwanzoni mwa Season 1: EP 10. Baada ya Rais JPM kuingia madarakani mambo yalibadilika kwa kiasi kikubwa, hasa katika masuala ya tenda na kuamua kufunga kampuni na kurejea South ili kuendeleza kampuni zake zingine, huku akikabiliana na changamoto nyingi kutokana na mabadiliko hayo.
Kuna kampuni moja ya masuala ya electronics ambayo baba yake aliiacha, lakini wabongo wazee wa fursa walicheza na umiliki wake. Ingawa mzee wake alionekana kupotezea suala hilo, Iryn alisisitiza kwamba hali hii haiwezekani na alitaka kuchukua hatua dhidi ya watu waliofanya uhuni huo. Alijua kuwa alikuwa na hati zote zinazohitajika, na hivyo alikusudia kudeal na wahusika ili kurejesha haki na kumaliza tatizo hilo.
Iryn alinikabidhi hati zote na kuniagiza nianze kufuatilia suala hili pamoja na mwanasheria. Alinisihi sana kuhakikisha tunafanikiwa katika juhudi hizi. Aliongeza kuwa atarudi Tanzania mwezi Desemba kuangalia maendeleo ya kesi hiyo, na pia tutajadili kuhusu mradi wa kufanya Dodoma. Alionekana kuwa na matumaini kwamba kwa pamoja tunaweza kupata suluhisho na kuendeleza mipango yetu ya baadaye.
Niliingia chumbani kujiandaa, na Iryn alinifuatia kwa nyuma, akinikumbatia huku akizungusha mikono yake mbele yangu. Tulianza kukumbatiana kwa mahaba mazito, na hisia zangu zilianza kuwa na nguvu sana, kwani ilikuwa muda mrefu sijaonja ile furaha. Hali yangu ilizidi kuwa mbaya, nikijua jinsi nilivyokuwa na tamaa ya kuwa karibu naye. Tulianza kupigana makisi ya mwisho mwisho lakini sikuwa na uwezo wa kufanya chochote, sababu ya afya yake. Alichokifanya mama mtoto, alikoki RPG kwa mkono wake laini, hadi pale ambapo risasi za moto zilipotoka kwa kasi.
Nilihisi mabadiliko katika mwili wangu, na nikapata wepesi wa haraka. Tulikwenda kuoga pamoja, na nilijiandaa kwa haraka ili niweze kuongea kidogo na Momo na kumuaga kabisa. Nilitaka kuhakikisha kuwa kila kitu kiko sawa kabla ya kuondoka.
Nilimshukuru Momo kwa uwepo wake nyumbani, kwani alikuwa anatusaidia sana kucheza na mtoto. Nilimuaga kwa kumkiss shavuni, na kisha tukaanza safari yetu kwenda airport. Niliongozana na Iryn pamoja na Samantha, ambao walinipa kampani na njiani tulikuwa tunapiga story za mwisho.
Baada ya kufika uwanja wa ndege, niliagana na mama Aria, kwani sikutaka aanze kunisubiri hadi nimalize mchakato wa kucheck-in. Sikuona haja ya wao kufanya hivyo. Nilianza kwa kumkumbatia Samantha, na nikamalizia kwa kumkumbatia mama mtoto. Cha ajabu, alinionyesha upendo kwa kunipa na ulimi, na hiyo ilileta hisia mpya za mshangao na furaha.
Saa 7 usiku, safari yangu ya kurudi Dar es Salaam ilianza, na njiani kote nilikuwa na furaha sana. Nikiwa kwenye ndege, mawazo yangu yalizunguka kuhusiana na watoto wangu, Junior na Aria. Nilitamani sana kuona wanangu wakianza kujuana mapema na kutembeleana, kwani ni damu zangu. Nikaona kuna umuhimu wa kumtafuta mzee wangu na kumshirikisha kuhusu jambo hili mapema ili kila kitu kiwe wazi. Nilijisemea, "I'm running out of time; let me do this." Hali hiyo ilinipa msukumo wa kutenda haraka ili kuhakikisha familia yangu inakuwa na muungano mzuri.
THE END OF SEASON 2
Thank you for your time!