Jinsi carryover ya mwaka wa kwanza ilivyotaka kunisababisha nisi-graduate chuo

Jinsi carryover ya mwaka wa kwanza ilivyotaka kunisababisha nisi-graduate chuo

Sio UDOM tu, hata hizi public Institute nyingi, hilo swala haliwezekani.
UDSM college nyingi ukiwa na coursework chini ya 16 una carry UDOM pia kuna baadhi ya college ukiwa na <16 unaingia UE fatilia mkuu
 
Hujawahi kupata sup kwa hiyo huwezi jua what others experience during "September conference". Kama walimu wangekua wanalegeza basi pangekuwa hamna wenye carryover mkuu. Mkifanya sup exam pepa linatungwa upya na ukizingua unabeba kozi hakuna kulegezewa so mtu ukichomoa sup lazima ujipongeze mkuu
Halafu usifikiri humu wote ni watoto tumesoma chuo miaka hii yenu, ntakupa mfano mmoja tu, Institute moja ya elimu ya juu miaka ya nyuma ilikua first semiste ukifeli zaidi ya module tatu kati ya sita ni disco moja kwa moja, sasa mnalegezewa, mtu anafeli zaid ya tatu na bado yupo tu anadunda.
 
Vyuo vinatofautiana
Sasa unaniitishiaje kuwa sijawahi kupata supp au sijui adha ya supp, hiyo unayoita september conference?

Na nani aliyesema kuwa mitihani ya supp ni mitihani iliyofanywa awali hivyo kurudiwa? Supp ni mitihani inayojitegemea.
 
Halafu usifikiri humu wote ni watoto tumesoma chuo miaka hii yenu, ntakupa mfano mmoja tu, Institute moja ya elimu ya juu miaka ya nyuma ilikua first semiste ukifeli zaidi ya module tatu kati ya sita ni disco moja kwa moja, sasa mnalegezewa, mtu anafeli zaid ya tatu na bado yupo tu anadunda.
Prospectus ya UDSM inasema sababu mojawapo ya mwanafunzi kuwa discontinued ni kuwa na GPA <1.8 pia kuwa na incomplete kwa kutofanya mitihani. Unavoona mkuu ni sawa kumfanya mwanafunzi awe discontinued kisa kashindwa ku-clear somo moja mara 2 tena akiwa na GPA ya above 2.5 au 3.0 huoni vyuo vingine havitendi haki kwa hilo? Naona wanafanya vizuri na vyuo vingine inabidi viige huo mfumo huwezi kumfelisha mwanafunzi kisa kafeli somo mara 2 ikiwa uwezo wa kulisoma somo anao muda pia anao na GPA ya kubakia chuo anayo. Kumbuka lengo la elimu sio kukomoana ni kuandaa wataalamu wanaolewa kada zao vizuri
 
Hongera kwa kuchomoa sup 4 mkuu hakika wewe ni legend [emoji1787]
[emoji23]bahati TU mkuu iliniangukia . Odds hazikua upande wangu..ila nikatoboa.. Kuna course Moja ya micro biology Dr alkua mnoko kinoma alibaki na wadau wakamaliza mwaka ulofata🥹
 
Ni zaidi ya miaka kumi imepita lakini nakumbuka ni km Jana tu... udsm kile chuo ni nyoko kabisa..... Nina jamaa angu tulikua tunaishi mtaa mmoja na tulisoma darasa moja o level. Baada ya kumaliza form four kil mtu alifaulu na kupangiwa shule ya serikali, kila mmoja Advance alienda kusoma shule tofauti.... Baada ya kumaliza advance tukaja kukutana udsm mimi nikisoma Education na yeye akisoma Accounts....

Akaja ku disco chuo mpaka leo sijawahi kumwona tena. Nasikia wanasema alienda kusoma diploma ya ualimu cjui wapi huko.
 
Pole man!

Mi nakumbuka mwaka was pili kwenda was tatu aiseh!sup mbili Moja ya zoology nyingine thermodynamics aiseh nilichomoa !

Chuo Kuna mambo ya ajabu sana!

Nakumbuka ghafla macho yangu yalianza kuona Giza !nywele zikapauka aiseh nilijiuliza maswali Hadi nikakosa majibu kabisa!

Niliteseka sana macho hayaoni Giza tupu na yanatoa machozi wakati was kusoma na kozi mwaka was pili ngumu sana!!nikaenda CCBRT wakapima eti hawaoni kitu!!

Nikakomaa Hadi nikashikwa kozi mbili zile!

Leo Niko fresh Huwa najiuliza ni ni kilinipata!!?


Namshukuru Mungu sana!!
Mwaka wa kwanza chuoni niliikuta hii course katika harakati za hapa na pale nikapata coursework ya 11/40 kupiga UE nikala mzinga. Kufanya sup ikanishinda nikacarry.

Mwaka wa pili nikawa natumia uzoefu kuisoma hii course darasani siingii. Lahaula coursework kutoka nina 9/40 kufanya UE sikuchomoa. July mwishoni nikaripoti field muda wa kusoma hakuna kushituka September hio kufanya sup sikuchomoa ikabidi nicarry tena (Kimoyo moyo nikajisemea next time nitaipiga KO kwenye UE tu 🤣 ngoja niikamie)

Mwaka wa mwisho mambo yakazidi kuwa mengi zaidi research na course zikawa nyingi nikajikuta narudia yale yale makosa nikawa siingii class coursework kutoka ikasoma 8/40 kupiga UE nikafeli tena kumfata Lecturer alikua mmama akaniambia "yani wewe ujikaze tu kwa coursework hiyo sidhani kama utatoboa".

July-September nilisoma kama kichaa sikuwahi soma hivi kabla soma sana vitabu, articles, zurura sana YouTube nikapiga pepa la sup Septemba nikatoboa matokeo kuja nina C nikagraduate.

Sikuwahi kufeli somo lingine zaidi ya hili katika maisha ya chuoni lakini nikiri hili somo lilinipeleka mpela mpela kila nikikumbuka sina hamu tena na kusoma.

Kitu nilichojifunza: Kosa kubwa nililolifanya ni kuruhusu kufeli sup na kubeba somo kwenda nalo mwaka unaofuata nikidhani nitapata muda wa kulisoma wakati ni tofauti kabisa muda unakuwa mdogo na mambo yanazidi kuwa mengi.
N
 
Ni zaidi ya miaka kumi imepita lakini nakumbuka ni km Jana tu... udsm kile chuo ni nyoko kabisa..... Nina jamaa angu tulikua tunaishi mtaa mmoja na tulisoma darasa moja o level. Baada ya kumaliza form four kil mtu alifaulu na kupangiwa shule ya serikali, kila mmoja Advance alienda kusoma shule tofauti.... Baada ya kumaliza advance tukaja kukutana udsm mimi nikisoma Education na yeye akisoma Accounts....

Akaja ku disco chuo mpaka leo sijawahi kumwona tena. Nasikia wanasema alienda kusoma diploma ya ualimu cjui wapi huko.
Umenikumbusha enzi hizo Conas Kuna ile wanaita departmental gpa imeenda na wengi Sana mtu ana disco na gpa ya 3. Kulikuwa na malecturer wanoko Sana hasa department ya zoology akina Kayumbo,Gamba n.k sijui Kama Bado wapo
 
Ni zaidi ya miaka kumi imepita lakini nakumbuka ni km Jana tu... udsm kile chuo ni nyoko kabisa..... Nina jamaa angu tulikua tunaishi mtaa mmoja na tulisoma darasa moja o level. Baada ya kumaliza form four kil mtu alifaulu na kupangiwa shule ya serikali, kila mmoja Advance alienda kusoma shule tofauti.... Baada ya kumaliza advance tukaja kukutana udsm mimi nikisoma Education na yeye akisoma Accounts....

Akaja ku disco chuo mpaka leo sijawahi kumwona tena. Nasikia wanasema alienda kusoma diploma ya ualimu cjui wapi huko.
Poleee yake [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Samahana naomba kuuliza jamani, ivi sheria ya mwanafunzi wa bachelor degree mwaka wa pili kutoruhusiwa kucarry somo kwenda nalo mwaka wa tatu ni vyuo vyote au ni chuo changu tu ? (Maana hii nactvet, nashindwa kuelewa)
Na je nawezaje kupata pdf ya hiyo sheria ya v
Naomba msaada.
 
Back
Top Bottom