Kaka kwahyo wewe ukimsimamisha tu mwanamke unamtongoza hapo kwa hapo kama ajali?
Chukua namba, vunga nayo hata siku 1 au mbili alafu mtafute jitambulishe jenga ukaribu/urafiki kwa muda baada ya hapo mwaga sera, hakikisha unamvutia kwa sera zako muaminishe kwako yeye anafaa kwa namna yeyote ile. Haya ni kwa mwanamke wa malengo zaidi, sijui nielezeje ila sio kila ke anastahili kupata hiyo nafasi, binafsi huwa nna aina fulani ya wanawake nnaopenda kujihusisha nao, wapole na wasio waropokaji(wastaarabu) shida ipo kwenye kuwajua, ke mpole namjua hata kwa anavyotembea.
Tulia usiwe na haraka kupata mwenza sahihi sio jambo jepesi kama wengi tunavyodhani.