Jinsi gani ya kukabiliana na wizi/utapeli unaotokana na kusemeshwa na kupumbazwa na mtu usiyemjua?

Jinsi gani ya kukabiliana na wizi/utapeli unaotokana na kusemeshwa na kupumbazwa na mtu usiyemjua?

Ukiweza kujizuia na tamaa za pesa za haraka ,
Kamwe huwezi kutapeliwa

Nakumbuka siku moja zamani kidogo,
Nilikuwa pale ubungo maji,, Daresalam.
kabla ya hii barabara ya mwendo Kasi kujengwa.

Niliisubiri daladala kwa muda mrefu baadae daladala la posta likafika,
nikatulia zangu mbele kwa dereva

Kati ya watu tuliokuwapo ndani ya daladala alikuwapo dada mmoja umri kama 30 hivi,

Muda wote alikuwa na wasiwasi kama ana Jambo linamsumbuwa..

Baada ya daladala kufika kituo cha manzese,
Yule dada alifunguwa mkoba wake akatoa bahasha fulani ya rangi ya kakhi,

Baada ya kufunguwa alipiga Kelele kwa sauti

'''Mama!! Nimetapeliwa,""
Nitamueleza nini mume wangu.

Ikabidi nijaribu kumbembeleza na kujuwa kulikoni?
Baada ya kumsikiliza kwa makini,

Nikagunduwa tamaa ya pesa za haraka hupelekea kutapeliwa..

Yule dada alitoka na mumewe kimara,
Wote wakashuka kituo cha ubungo maji,Ila walikuwa na safari tofauti.

Mumewe akavuka barabara upande wa pili wa jengo la Tanesco ,
Ili akapande magari yanayoelekea buguruni.
Wakati huo bado Pana stand ya daladala pale ubungo Tanesco.

Sasa yule dada anasema wakati anaagana na mumewe,
Alipita Kaka mmoja akadondosha bahasha fulani ya rangi ya khaki.

Yule dada aliiona Ile bahasha akataka kumuita yule kaka aliyoangusha Ile bahasha,

Akatokea jamaa mwingine akaokota Ile bahasha,mbele ya yule dada.
Akaifunguwa Ile bahasha ilikuwa na pesa kibunda cha noti ndani yake.

Kabla hajakaa Sawa akarudi yule Kaka wa mwanzo aliyedondosha Ile bahasha akaja kuulizia pale.

Nimeangusha bahasha ina 1.5 million,
Yule Kaka alilalamika pale mbele za watu,
Lakini jamaa alikana kuokota Ile bahasha.

Pale pale yule jamaa aliyeokota bahasha akamwambiya yule dada,
Hizi ni pesa nyingi,
Na huyu kijana lazima atarudi tena kabla daladala halijaja,

Sasa chukuwa hii bahasha nisubiri kituo cha mbele pale shekilango.
Mimi nakuja.
Jamaa alimwambiya yule dada

Muda wote mume wa yule dada yupo upande wa pili anaona tukio zima,
Ikabidi ampigie simu mkewe ,
vipi mbona upo na hao jamaa kuna nini?
Dada akamwambiya ni jamaa tu mgeni anauliza njia,
Lakini mumewe bado akawa anasumbuwa kwa simu,
Mwisho dada akawa hapokei simu ya mumewe.

Kilichofata baada ya dada kupewa bahasha,
Yule jamaa aliyeokota bahasha, akamwambiya yule dada,

Sasa Mimi nakuamini vipi?
Kukupa 1.5 milion wakati sikujuwi?

""Kama vipi niachie simu yako,''
Tangulia shekilango kituoni,
"Nakuja tugawane."
Dada alikuwa na simu nzr Sana smart.

Kabla dada hajatoa maamuzi ya kutoa simu ,
Yule aliyeangusha pochi akarudi tena,
Akasema jamani nimeangusha milioni na nusu,
Atakayeona bahasha plz ni pesa za Ada ya chuo.
Please, please,jamaa alijiliza pale kituoni

Yule dada akaona simu kitu gani mbele ya 1.5.
Akampa jamaa simu,
Akaingia ndani ya gari.

Kufika manzese ndy dada akaamua kufunguwa Ile bahasha ili azihesabu pesa vizuri.

Anakutana na makaratasi yaliyopangwa vzr kama kibunda cha noti

Na mbaya zaidi hata yule dada mwenyewe,
alipanga kumdhulumu aliyeokota bahasha,
Sababu aliambiwa ashuke shekilango,
Matokeo yake akaamua kupitiliza kituo hadi manzese..


Tamaa hupelekea kutapeliwa.

Huyu kweli tamaa ilikuwa online tena kifurushi cha mwezi unlimited [emoji16]
 
Hivi hkna dawa ya ukikutana na pisi kali ukimsalimia2 tayari unabeba2 kiulaini hadi geto Mbona matapeli wa ivyo cjawackia
Niliwahi kukutana na dogo mmoja ila ni zamani miaka ya 2001 alikuwaga mtoto wa mganga maarufu kijijini kwetu miaka hiyo
Yule dogo alikuwaga kachanjiwa dawa akimshika mkono demu tu hapohapo demu analegea anamfuata jamaa anaenda kula zigo
 
[emoji23][emoji23]mkuu sijasikia mtaani, waliobiwa naowajua ni watu wa karibu.. Halafu tahadhari ni bora kuliko ajali
Just use you common sense na endelea na hamsini zako bipa kushangaa

Kwa nini uanzishe story ghafla tu na strangers uliokutana nao barabarani? Ndio maana mnaibiwa. Pole
 
Kila nikikumbuka nalia mie [emoji24][emoji24][emoji24]

Ilikua 2019 December, npo 1St yr na 1st semester, ilikua ni pale posta pale karibu na bunge primary,

Ni weekend ilikua nkatoka zangu home, nkamtembelea shost angu pale IFM, bas nkafika palee chuon tuka meet then tukatoka kuelekea Coco beach, tuka enjoy huko then tukarud nikamuacha pale chuon kwake, mie naondoka kurud home, bas natembea tyuuh kufika karibu na pale shule nakutan na mkaka kwa kumtazama nilihis ni mwanachuo pia, coz alikua na muonekano huo.

Akaanza kunisemesha mara story kidg nkashangaa namkabizi mkoba ulikua na 180k, na cm ndogo, na funguo za ghetto, nkampa na cm kubwa niliyoshka mkononon, hata sijui nilimpaje, tukaachana tena kwaa kuagana vizuri, Mie nkaenda kupanda boda huyo home,

Fahamu imekuja kurudi nipo kwenye boda, najishangaa cna cm, mkoba pia, yaan hata sikua naelewa, kufika home jamaa inabidi nimpe naul yake nabaki kuhaha, ikabidi niingie ndani nkaomba msaada wa yule boda kuvunja kufuli nkaingia ndan nkatoa hela nkampa akaondoka, nilianza kulia mie hapo hadi kamasi,

Wallah sitasahau lile tukio kamweee. Na lilinipa funzo hapa dar, now hata marafiki siwaamini akuuuh. [emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]

Kila nikikumbukaga sometimes naliaa tyuuh. Dar hapana kwa kweli khaaaaah.
Duh! Pole sana
 
Habari wakuu

Kwa muda mrefu nimekutana na kesi mbalimbali za watu kuibiwa kwa namna ya kupumbazwa akili ( hypnosis).

Unakutana na mtu anakusalimia, ukishaitikia tu ndo kosa lako[emoji51][emoji51] .. Unakuja kushtuka ulishampa simu, wengine huenda hata bank na kutoa hela na kuwapa hao matapeli.[emoji2365] imagine enzi niko sekondari kuna classmate yeye aliwapa mpaka mkanda wake wa kiunoni manzese pale[emoji16]

Binafsi sijawahi kukutwa na hayo maswaibu, ila najiuliza ni nini kinga ya watu kama hao au hii mbinu ina Apply kwa baadhi ya watu tu ?
Hakuna ''wizi wa kusemeshwa'' bali huu ni utapeli. Kinachotokea ni kwamba watu wanalaghaiwa kwa maneno mpaka wanajikuta wanatoa vitu walivyonavyo kwa sababu ya tamaa zao! Narudia tena. Huu ni utapeli wa maneno tu na anayekusemesha anatumia udhaifu na tamaa zako kukupiga. Namna ya kukabiliana na huu utapeli ni kutopenda short-cut au vitu vya bure na kuepuka kuzoeana na watu ambao huwajui kwa urahisi. Hivi dunia ya leo mtu anakukuta anaanza kukusemesha semesha na kukuzoea ghafla wewe unakubalije?
 
Hii imewakuta watu watatu tofauti ninaowafahamu sijui hawa wezi wanatumia dawa gani

Wa kwanza; Huyu yeye alizubaishwa Mwenge na akawapa kiasi cha pesa alichokuwa nacho pale, akaja nao mpaka anapoishi huko Skanska akawapatia Akiba, kama haitoshi akakopa kwa jirani akawapatia, akakopa kwa ndugu pia akawapatia. Baada ya jamaa kusepa ndo anakuja kustuka baada ya kuongeleshwa, ilikuwa kilio kuanza kulipa madeni.

Wa pili ni huko Bonyokwa, huyu dada yeye alipumbazwa akawapatia simu, pesa na bado akaenda nao kwake akaanza kuwapa vitu vya ndani. Majirani walipomuuliza mama fulani unahama? Fahamu zikamrudia jamaa hapo washasepa fasta.

Wa tatu ni mdada wangu wa kazi; na akaambiwa mambo ya nyota, pia akaambiwa ndani una akiba ya fedha akajibu ndiyo. Alikuwa na simu lakini hakuwapa na wala hawakuongozana but alivyofika nyumbani akaenda kukoga na simu aliweka kitandani but alivyotoka kuoga akakuta bahasha, kufungua akakuta mche wa sabuni, ile akiba nayo imetoweka. Kilio chake hakikuwa cha nchi hii ikabidi tu nimpatie simu na akiba yake.

Kwa haya mafunzo, wapendwa tuwe makini. Najua si rahisi kutomwongelesha mtu lakini tujitahidi kuepuka mitego ya namna hii.
Wote hawa walitapeliwa kwa tamaa zao za kupenda vya bure. Hakuna cha dawa wala nini. Mimi nimejaribi kuuliza sana kwa undani kuhusu watu waliodai walitapeliwa kwa kutumia ''dawa'' lakini katika cases zote niligundua kitu kimoja. Walitekwa kimawazo kwa tamaa zao za kupenda short cut na walipokwisha kupoteza mali au fedha zao wakazingizia kuwa hawakuwa na ufahamu.
 
Kanuni ya maisha ya mjini ni kutoshabikia chochote usichokijua na kutofuatilia chochote kisicho kuhusu au kisicho na maslahi kwako. Mambo ya kusalimia salimia watu usiowajua ni upuuzi. Fanya yako, unaanza kumuuliza mtu habari za mchana humjui hakujui akikuambia ananjaa utampa chakula? Unakuta mtu yuko bussy kuanhalia karata tatu hajui 50% ya waliopo.pale ni wamoja. Acha kushangaa mjini utaumia
Asante sana mkuu. Kwale watu waliofika nchi zilizoendelea kama Ulaya watakuelewa lakini kwa wabongo wengi hawawezi. Eti dunia ya leo unaanza kuzoeana na mtu ghafla humjui wala hakujui!
 
Wote hawa walitapeliwa kwa tamaa zao za kupenda vya bure. Hakuna cha dawa wala nini. Mimi nimejaribi kuuliza sana kwa undani kuhusu watu waliodai walitapeliwa kwa kutumia ''dawa'' lakini katika cases zote niligundua kitu kimoja. Walitekwa kimawazo kwa tamaa zao za kupenda short cut na walipokwisha kupoteza mali au fedha zao wakazingizia kuwa hawakuwa na ufahamu.
Kuna dawa inaitwa Scopolamine....unaweza kuangalia documentary hapo chini



Pia soma:
 
Ila Dar nyoso sana mm ndomana nikiwa na hela sicheki na mtu kwenye daladala kabisa haswa pale Mlimani City ndo pabaya pale kuna rafiki yangu kipindi niko Advance mama ake alikuwa hawezi pirika ikitokea huwa anampa Card mwanae akatoe pesa za matumizi.

Ile kutoka tu pale mlimani City wana hawa hapa Salimia wakaanza story za nyota jamaa akawapa pesa alizotoa kwenye ATM na Simu fahamu zilimjia baada ya kufika kwamama yake kwao Full kilio asahau ile siku.

Ila hawa jamaa kwa haraka na fikra zinazonijia aidha wanatumia Jini au Dawa na haswa zaidi ni jini kitendo cha kuitikia inamaana ummempa ruksa jini akuvae na akutawale na akuamrishe na wengi wahanga niwanawake kuliko wanaume na haswa ukiwa mchafu, pombe na mtu wazinaa ni rahisi sana kufanikiwa kwao.
Kungekuwa na wizi wa kutumia jini au dawa mjini hakuna mtu angepona au kuepuka. Watu wangekuwa wanapigwa kila siku na kila saa. Na wezi wangekuwa wanatumia kitu kama mwezi mmoja tu kuiba na wangekuwa matajiri wa kutupwa. Infact matajiri wakubwa kwenye kila mkoa wangekuwa ni hao wezi kwani fedha zingekuwa zinaingia kama utani.
 
Ndo hayohayo mapepo mkuu nishazunguka sana kwenye minada ya mifugo kuna mzee rafiki yangu sana huwa anatafuna mizizi na kumpiga kofi muuzaji hachomoi lazima anunue kwa bei anayotaka. Na mfugaji akili inamjia mnyama yuko kwenye Gari nikawa namdadisi nikajua mpaka chimbo anapoenda huko Kwa Babuu, ni Jini na hizo dawa maana baada ya mda lazima urudi ukarenew[emoji1787][emoji3]
Fiksi. Kamba! Chai!
 
Tatizo wabongo tunapenda sana salamu mtu Hata hakujui humjui mmekutana tu anakusalimia,haya mambo huez kukuta Kenya yan mpaka nilishangaa pale Nairobi kila mtu yuko bize ila bongo sasa haha unaeza pita sehemu usiposalimia wanamind hatar yes sio mbaya but asilimia kubwa hao matapeli wanaanza kukusalimia na kukuongelesha ukijibu tu imekula kwako anyways tuwe makini barabarani huko sio kila mtu anania njema!
 
Mwaka 2014 nilikutana nao Bamaga nilikua naelekea sayansi nipo kwa mguu nilikutana na huyo kaka anaulizia hospitali jina nimesahau nikamuambia sipajui muda huo huo akatokea kaka mwingine, huyu kaka alienisimamisha mara ya kwanza akamsimamisha yule kaka mwingine akamuuliza hiyo hospital yeye akasema anaijua ipo barabara ya kuelekea Sinza ila hana muda anielekeze mimi nimpeleke.

Sijawah elewa nini kilitokea kweli niliondoka nao tumefika karibu na Afrikasana nikajiuliza naenda huku kufanyaje nikawaambia jamani mnanipotezea muda wewe kaka unaeijua hiyo hospital mpeleke mwenyewe mie nna safar zangu wakaanza kulalamika tusaidiane mimi nikasepa. Nipo njiani kurudi nikawa najiuliza ilikuaje nikaondoka nao ila hawa hawakuniibia chochote nilikua na begi la mgongoni lina nguo, simu na hela kidogo tu.

Toka pale sijawahi kutana tena na watu wa namna ile ila stori za watu kuibiwa kwa namna hizi zipo nyingi sana.
 
Mwaka 2014 nilikutana nao Bamaga nilikua naelekea sayansi nipo kwa mguu nilikutana na huyo kaka anaulizia hospitali jina nimesahau nikamuambia sipajui muda huo huo akatokea kaka mwingine, huyu kaka alienisimamisha mara ya kwanza akamsimamisha yule kaka mwingine akamuuliza hiyo hospital yeye akasema anaijua ipo barabara ya kuelekea Sinza ila hana muda anielekeze mimi nimpeleke.

Sijawah elewa nini kilitokea kweli niliondoka nao tumefika karibu na Afrika sana nikajiuliza naenda huku kufanyaje nikawaambia jamani mnanipotezea muda wewe kaka unaeijua hiyo hospital mpeleke mwenyewe mie nna safar zangu wakaanza kulalamika tusaidiane mimi nikasepa. Nipo njiani kurudi nikawa najiuliza ilikuaje nikaondoka nao ila hawa hawakuniibia chochote nilikua na begi la mgongoni lina nguo, simu na hela kidogo tu.

Toka pale sijawahi kutana tena na watu wa namna ile ila stori za watu kuibiwa kwa namna hizi zipo nyingi sana.
Duuuuuh poleeeh ila ungeibiwa km usingeshtuka yaan.
 
Kutapeliwa hakuna formula kabisa

unaweza kutapeliwa na mtu wako wa karibu, i.e ndugu jamaa ama marafiki

watu wasiokujua watatumia madawa kukupiga.

kuna mganga ashanisimulia jinsi watu wanavyoenda kwake kutafuta hizo dawa.

Hayo madawa huwa yanachanganywa na dawa za mvuto pamoja na kupewa mapepo maalum ya utambuzi na kupumbaza.

Madawa mengine makali wanayotoa ni ya kusahaulisha wadeni, kuua kesi mahakamani, n.k

hii dunia ni nzito sana sio kama tunavyoijua
Huu ni uongo wa hali ya juu alikuambia huyo mganga. Watu kama nyie ndiyo huwa mnatapeliwa sasa. Unaona aliweza kukuaminisha kuwa anaweza kufanya wadeni wako wasahau kama wanakudai au ushinde kesi hata kama umekosa! Utapeli ndivyo unavyofanya kazi na hakuna dawa wala pepo wala jini. Mtu anakuaminisha anaweza kufanya kitu fulani ambacho una shida nacho, anakuteka kimawazo wewe unakuwa umejikita kwenye ile ''habari njema'' uliyopewa na kusahau mengine yote. Anakupiga. BTW kutapeliwa na ndugu au jamaa au rafiki hii ni kesi nyingine kabisa kabisa na sidhani inaweza kukwepeka hasa kwa maisha yetu ya kiafrika.
 
Back
Top Bottom