Jinsi Iran ilivyojipata chini ya utawala wa Ki-Ayatollah

Jinsi Iran ilivyojipata chini ya utawala wa Ki-Ayatollah

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Kabla ya Iran kutawaliwa katika mfumo wake wa sasa wa Ki- Ayatollah ilikuwa ikitawaliwa kwa mfumo aina fulani karibia na Ufalme hivi ambao watawala wake walikuwa wakiitwa Shah.

Mashah wawili wa mwisho, baba na mtoto wake walitokana na mapinduzi ya ufalme halisi wa muda mrefu wa Qajar mwaka 1925 ambapo Shah Reza Pahalavi alimpindua Ahmed Shah Qajar na baadaye yeye mwenyewe akapinduliwa na kurithiwa na mtoto wake Mohammed Reza Pahlavi mwaka 1941 aliyekuwa Shah wa wa mwisho wa Iran.

Ufalme wa Qajar uliopinduliwa na mashah wawili waliotokana na mapinduzi walikuwa ni watu wapenda mabadiliko ya kisasa sana, lakini zaidi sana Shah wa mwisho, Reza Pahlavi. Huyu aliipelekea mbio Iran kipindi hicho inaitwa Persia katika kukumbatia usasa (modernization).

Aliweka rasmi katika sheria kuwa Persia(Iran) ni taifa secular(lisilio la kidini), aliwapa wanawake uhuru wote walioutaka, alipiga marufuku wanawake kuva hijab au niqab sehemu nyingi za umma ni pia aliweka uzito wanawake wanaovaa mavazi hayo kuajiriwa katika kazi za umma, alisisitiza na alitoa elimu dunia kwa raia wake, alijenga miondombinu mingi ya kisasa ya barabara, reli, hospitali n.k Lengo lake hasa alitaka kuipeleka Iran njia ya Uturuki ya Mustafa Kemal Atartuk.

Hii spidi kubwa ya mabadiliko ndiyo iliwaibua mashia akina Ayatollah na makundi mengine mengi ya wahafidhina waliotokea katika mlengo wa kidini.

Hawa ni watu waliokuwa na mtazamo wa kizamani sana waliokuwa washamba na maamuma kabisa wa ulimwengu wa kisasa. Walitofautiana na kukosana vibaya sana na Shah Mohammed Reza katika mipango yake ya usasa (modernisation) hadi ikabidi aanze kutumia udikteta kulazimisha mabadiliko. Akaanza kuwafunga wapinzani wake na wengine akawapeleka uhamishoni akiwemo Khomeini(hili lilikuwa mojawapo ya kosa kubwa sana kwake kwani Khomeini alianza kuzungukazunguka mataifa mengine kama Iraq, Uturuki na mwishowe Ufaransa akiendeleza harakati zake ndani ya Iran).

Miaka ya 1970- biashara ya mafuta ikawa mbaya sana pia uchumi wa Iran ukazorota vibaya sana kutokana na kupungua mapato hali iliyozidisha nguvu kwa wapinzani wa Shaha hadi wakaweza kumpindua mwaka 1979 na wakaanzisha mfumo wa Ki-Ayatollah na kufuta au kugeuza mabadiliko karibia yote waliyoanzisha wakina Shah watatu wa mwisho.
 
Bora Tanzania hata kuna uhuru kiasi kwa raia kufanya mambo yao,
Sasa mbona hiyo Iran inayo ongozwa na washamba na wenye mawazo ya kizamani mpaka sasa ina miliki kila aina ya kitu cha kisasa, wakati nchi yako yenye viongozi wajanja na wenye mawazo ya kisasa bado ipo kwenye giza na ujima?

Kama ndo hivyo basi na sisi Tz tunahitaji viongozi washamba ili angalau tufikie hata robo ya maendeleo ya Iran.
 
Sasa mbona hiyo Iran inayo ongozwa na washamba na wenye mawazo ya kizamani mpaka sasa ina miliki kila aina ya kitu cha kisasa, wakati nchi yako yenye viongozi wajanja na wenye mawazo ya kisasa bado ipo kwenye giza na ujima?

Kama ndo hivyo basi na sisi Tz tunahitaji viongozi washamba ili angalau tufikie hata robo ya maendeleo ya Iran.
Sawa ila sisi hatuko tayari kuweka sheria katili za kiarabu za karne ya saba kwa kisingizio cha dini kwa sababu kwanza sisi kila moja ana uhuru wa kuamini apendavyo.
 
Sasa kama hayo ma ayatola ni mabaya kwanini iran imezidi kusonga mbele, kwanini isirudi nyuma ama kubaki palepale kama sisi huku DANGANYIKA tunavyopiga hatua kurudi nyuma kimtindo.
Inategemea unailinganisha Iran na nchi gani,
Iran GDP per capita ni 4700USD ambayo inazidiwa hata na Botswana na Namibia,
 
Sawa ila sisi hatuko tayari kuweka sheria katili za kiarabu za karne ya saba kwa kisingizio cha dini kwa
sababu kwanza sisi kila moja ana uhuru wa kuamini apendavyo.

Kwahiyo kwako usasa ni wanawake kuvaa uchi na kupishana gest kufanya uzinzi badala ya kufanya kazi?
Mbona hiyo serikali yako haijakupa uhuru wa kuamini nje ya CCM kwa kuweka sheria za kuhakikisha CCM inatawala milele?
Mbona hiyo serikali yako haijakupa uhuru wa kujikwamua kwenye umasikini?
Huo uhuru wa kuamini unacho kitaka si ndo umeleta akina mwamposa wanao tapeli na kutia watu umasikini?
Huo uhuru wa kuamini unacho kitaka si ndo umeleta akina makanzie aliye uwa mamia ya watu kwa njaa?

Nyinyi mko kwenye usasa wa kinadharia wakati wao wako kwenye usasa wa kivitendo.
Na ndio maana Iran , Qtaar, UAE,Saudia ,Malasia zinahesabika kuwa n nchi za ulimwengu wa kwanza na wa pili wakati nyinyi wenye uhuru unao usema mnahesabika kama dunia ya tatu ,yaani watu wa mwisho kabisa hapa duniani ambao mnaishi maisha yaliyo pitwa na wakati.
 
Kabla ya Iran kutawaliwa katika mfumo wake wa sasa wa Ki- Ayatollah ilikuwa ikitawaliwa kwa mfumo aina fulani karibia na Ufalme hivi ambao watawala wake walikuwa wakiitwa Shah.

Mashah wawili wa mwisho, baba na mtoto wake walitokana na mapinduzi ya ufalme halisi wa muda mrefu wa Qajar mwaka 1925 ambapo Shah Reza Pahalavi alimpindua Ahmed Shah Qajar na baadaye yeye mwenyewe akapinduliwa na kurithiwa na mtoto wake Mohammed Reza Pahlavi mwaka 1941 aliyekuwa Shah wa wa mwisho wa Iran.

Ufalme wa Qajar uliopinduliwa na mashah wawili waliotokana na mapinduzi walikuwa ni watu wapenda mabadiliko ya kisasa sana, lakini zaidi sana Shah wa mwisho, Reza Pahlavi. Huyu aliipelekea mbio Iran kipindi hicho inaitwa Persia katika kukumbatia usasa (modernization).

Aliweka rasmi katika sheria kuwa Persia(Iran) ni taifa secular(lisilio la kidini), aliwapa wanawake uhuru wote walioutaka, alipiga marufuku wanawake kuva hijab au niqab sehemu nyingi za umma ni pia aliweka uzito wanawake wanaovaa mavazi hayo kuajiriwa katika kazi za umma, alisisitiza na alitoa elimu dunia kwa raia wake, alijenga miondombinu mingi ya kisasa ya barabara, reli, hospitali n.k Lengo lake hasa alitaka kuipeleka Iran njia ya Uturuki ya Mustafa Kemal Atartuk.

Hii spidi kubwa ya mabadiliko ndiyo iliwaibua mashia akina Ayatollah na makundi mengine mengi ya wahafidhina waliotokea katika mlengo wa kidini.

Hawa ni watu waliokuwa na mtazamo wa kizamani sana waliokuwa washamba na maamuma kabisa wa ulimwengu wa kisasa. Walitofautiana na kukosana vibaya sana na Shah Mohammed Reza katika mipango yake ya usasa (modernisation) hadi ikabidi aanze kutumia udikteta kulazimisha mabadiliko. Akaanza kuwafunga wapinzani wake na wengine akawapeleka uhamishoni akiwemo Khomeini(hili lilikuwa mojawapo ya kosa kubwa sana kwake kwani Khomeini alianza kuzungukazunguka mataifa mengine kama Iraq, Uturuki na mwishowe Ufaransa akiendeleza harakati zake ndani ya Iran).

Miaka ya 1970- biashara ya mafuta ikawa mbaya sana pia uchumi wa Iran ukazorota vibaya sana kutokana na kupungua mapato hali iliyozidisha nguvu kwa wapinzani wa Shaha hadi wakaweza kumpindua mwaka 1979 na wakaanzisha mfumo wa Ki-Ayatollah na kufuta au kugeuza mabadiliko karibia yote waliyoanzisha wakina Shah watatu wa mwisho.
Chuki zako hazitakufikisha popote,hao unaowaita washamba wamekuzidi kila sekta ktk linchi lako
 
Sasa mbona hiyo Iran inayo ongozwa na washamba na wenye mawazo ya kizamani mpaka sasa ina miliki kila aina ya kitu cha kisasa, wakati nchi yako yenye viongozi wajanja na wenye mawazo ya kisasa bado ipo kwenye giza na ujima?

Kama ndo hivyo basi na sisi Tz tunahitaji viongozi washamba ili angalau tufikie hata robo ya maendeleo ya Iran.
Huyu ni punguani tu,hao anaowaita washamba wanakaribia kumiliki mpaka silaha za nyuklia
 
Kwahiyo kwako usasa ni wanawake kuvaa uchi na kupishana gest kufanya uzinzi badala ya kufanya kazi?
Ukishavaa umevaa, hakuna kuvaa uchi,
Huu ndio ushamba walio nao Wa-Iran wanaosumbua nao raia kupitia Guidance/Morality police.
Wewe mwenyewe unaweza kukuta ulizaliwa kwa uzinzi
 
Kabla ya Iran kutawaliwa katika mfumo wake wa sasa wa Ki- Ayatollah ilikuwa ikitawaliwa kwa mfumo aina fulani karibia na Ufalme hivi ambao watawala wake walikuwa wakiitwa Shah.

Mashah wawili wa mwisho, baba na mtoto wake walitokana na mapinduzi ya ufalme halisi wa muda mrefu wa Qajar mwaka 1925 ambapo Shah Reza Pahalavi alimpindua Ahmed Shah Qajar na baadaye yeye mwenyewe akapinduliwa na kurithiwa na mtoto wake Mohammed Reza Pahlavi mwaka 1941 aliyekuwa Shah wa wa mwisho wa Iran.

Ufalme wa Qajar uliopinduliwa na mashah wawili waliotokana na mapinduzi walikuwa ni watu wapenda mabadiliko ya kisasa sana, lakini zaidi sana Shah wa mwisho, Reza Pahlavi. Huyu aliipelekea mbio Iran kipindi hicho inaitwa Persia katika kukumbatia usasa (modernization).

Aliweka rasmi katika sheria kuwa Persia(Iran) ni taifa secular(lisilio la kidini), aliwapa wanawake uhuru wote walioutaka, alipiga marufuku wanawake kuva hijab au niqab sehemu nyingi za umma ni pia aliweka uzito wanawake wanaovaa mavazi hayo kuajiriwa katika kazi za umma, alisisitiza na alitoa elimu dunia kwa raia wake, alijenga miondombinu mingi ya kisasa ya barabara, reli, hospitali n.k Lengo lake hasa alitaka kuipeleka Iran njia ya Uturuki ya Mustafa Kemal Atartuk.

Hii spidi kubwa ya mabadiliko ndiyo iliwaibua mashia akina Ayatollah na makundi mengine mengi ya wahafidhina waliotokea katika mlengo wa kidini.

Hawa ni watu waliokuwa na mtazamo wa kizamani sana waliokuwa washamba na maamuma kabisa wa ulimwengu wa kisasa. Walitofautiana na kukosana vibaya sana na Shah Mohammed Reza katika mipango yake ya usasa (modernisation) hadi ikabidi aanze kutumia udikteta kulazimisha mabadiliko. Akaanza kuwafunga wapinzani wake na wengine akawapeleka uhamishoni akiwemo Khomeini(hili lilikuwa mojawapo ya kosa kubwa sana kwake kwani Khomeini alianza kuzungukazunguka mataifa mengine kama Iraq, Uturuki na mwishowe Ufaransa akiendeleza harakati zake ndani ya Iran).

Miaka ya 1970- biashara ya mafuta ikawa mbaya sana pia uchumi wa Iran ukazorota vibaya sana kutokana na kupungua mapato hali iliyozidisha nguvu kwa wapinzani wa Shaha hadi wakaweza kumpindua mwaka 1979 na wakaanzisha mfumo wa Ki-Ayatollah na kufuta au kugeuza mabadiliko karibia yote waliyoanzisha wakina Shah watatu wa mwisho.
Umeiruka historia kubwa ya Iran.

Mwaka 1953 yalifanyika mapinduzi yalioongozwa na Uingereza na Wamarekani kumpindua Waziri Mkuu aliyekuwepo madarakani kidemokrasia na kuwapa vibaraka wao kina Shah madaraka yote.

"The 1953 Iranian coup d'état, known in Iran as the 28 Mordad coup d'état (Persian: کودتای ۲۸ مرداد), was the U.S.- and British-instigated, Iranian army-led overthrow of the elected Prime Minister Mohammad Mosaddegh in favor of strengthening the monarchical rule of the shah, Mohammad Reza Pahlavi, on 19 August 1953, ...

Soma zaidi:

 
Umeiruka historia kubwa ya Iran.

Mwaka 1953 yalifsnyiks mapinduzi yalioongjzwa na Uingereza na Wamarekani kumpindua Waziri Mkuu aliyekuwepo madarakani kidemokrasia na kuwapa vibaraka wao kina Shah madaraka yote.

"The 1953 Iranian coup d'état, known in Iran as the 28 Mordad coup d'état (Persian: کودتای ۲۸ مرداد), was the U.S.- and British-instigated, Iranian army-led overthrow of the elected Prime Minister Mohammad Mosaddegh in favor of strengthening the monarchical rule of the shah, Mohammad Reza Pahlavi, on 19 August 1953, ...

Soma zaidi:

Hilo ni somo lingine pana la vita baridi kati ya West na Soviet block. Wamarekani walifanya kosa kuwasikiliza Uingereza kuhusu Mohammad Mosaddegh kutaka kutafisha makampuni yao ya mafuta, lakini pia kilichokuwa kinawapa hofu zaidi ni Iran kuangukia mikononi mwa Wakomunisti katika huo mvurugano wa kiuchumi uliokuwa unaendelea.
 
Back
Top Bottom