Jinsi mapenzi ya mtoto wa Kizulu Durban South Africa yalivyotaka kunitoa roho

Shukrani mkuu. Kama nitaamua kufanya hivyo nadhani kuna matukio mengi sana ya kufurahisha, kuburudisha na kushangaza ambayo sijayaweka hapa itabidi niyaweke kwenye kitabu. Kuna jamaa yangu mbongo sasa hivi yuko UK Manchester nilisafiri naye wakati natoka Bongo. Kuna mambo aliyafanya pale Lusaka, maana tulilala hapo, pia siku zake za mwanzo tulipofika Johannesburg kabla hajatimukia England kuna stori nzuri sana ya kusisimua inayomhusu, huwa nacheka sana nikimkumbuka huyo baharia. Kwa hiyo kuna mambo mengi sana ambayo sijayaweka hapa ambayo yataongeza mvuto wa kitabu.
 
Kabisa, hapa una kitabu kizuri. Mtu akianza mwanzo anatamani kuendelea....good work, good talent. Ni mwandishi mzuri pia na makini....typos kama zipo ni chache sana. Kila la heri.
 
Jumatano mkuu. Kuweni na subra tu ndugu zangu.
Bora ukimaliza usiache kuandika kitabu
kuna Member humu jukwaani anaitwa LWANDA MAGERE alileta Tukio la Jini mwanamke toka Singida Baba yake akampeleka Musoma, alipomaliza kisa hicho akweka cua utajiri wa kikongo, akaanza kuuwa watu apate damu, alituomba twende Telegram tukamchangia huko, cha ajabu leo kasikika Redio Free Afrika saa 4 asubuhi kamwaga Story ileile, sijajua kule kalipwa au ni njia yake ya kupata waumini kwa njia ya Dini.
Naomba usiuze hadithi yake kwa vyombo vya habari bora ibane utoe kitabu na sisi tumalizie hivyo vipengele vi4 vilivyobaki.
Kuna siku watoto wetu wataandika script wacheze filamu sifa itarudi kwako
 
Ile stori ya yule jamaa toka wiki iliyopita nimemsikia akiielezea redioni. Hiyo stori niliisoma hapa na nilishangaa sana kuisikia akiielezea RFA. Nilichokigundua kwenye hiyo story ni hiki: Yule msimuliaji wa hiyo stori kule redioni sio huyu aliyeileta hapa JF. Inaonekana huyo jamaa wa redioni kaiiba hiyo stori kutokea hapa JF na kuipeleka huko redioni maana nilivyokuwa namsikiliza kama anajing'atang'ata sana kwenye kusimulia kwakwe, yaani ukimsikiliza kwa makini hana ile natural flow ya kusimulia ambayo anatakiwa aionyeshe kama mhusika wa tukio, anasimulia kama vile na yeye amesimuliwa, halafu cha pili hata kiswahili kama vile hayuko fluent ukilinganisha na maisha aliyoishi. Maana mtu kama wazazi wote walikuwa watumishi tunategemea huyo mtu ataongea kiswahili kilichonyooka kwa sababu ameishi mazingira ya kuongea kiswahili muda wote tofauti na mtu aliyekulia kijijini. Kitu kingine hiyo stori mie binafsi naiona kama ni chai. Haina uhalisia kabisa, kuna mambo mengi sana ya kufikirisha kuhusu hiyo stori.
 
Ila konda msafi kuna kitu unakosea..ahadi zako nyingi ni zile ambazo sio timilifu..last week uliahidi j5 ungeleta MKEKA wa maana..matokeo yake ukaleta story ya kawaida yenye aya kama 8 tu...hahahahha....leo tena umetujaza kuwa j5 inaisha..(binafsi naamini haitaisha j5 maana ahadi zako hazitimii)...lakini mkuu, mda mwingi upo online JF, hivi ungekuwa unaandika kidogo, una save then unakuja kuandika kidogo mwisho unamaliza unatuma si ingekuwa imeenda mbali hadi now?...Kama kweli ungekuwa na nia ungeshaimaliza maana kama mtu ukiamua kuandika kwa nusu saa tu lazima uandike kitu kirefu...

NIONAVYO MIMI..

1. Mkuu unafurahi sana unavyoona wana wanaulizia hii story kila muda. Maana kama unapata mda wa kusoma comments kwenye uzi wako na kureply, unakosaje muda wa kuandika story yako? Nahisi mkuu unafurahi kuona notifications zimejaa quotes kuhusu uzi wako.

2. Story yako imeshapoteza mvuto..watu wamesubili na wameshazoea...haina mvuto tena kama ule wa mwanzo na haija vuta tension ya watu tena... wiki hii inayoisha leo umeandika post chache na fupi kweli tofauti na ahadi yako ilivyokuwa mwanzo.

3. Sitaki nataka zako zimefanya mpaka story imekosa mvuto..HOW?, Uliwaambia watu hutaimalizia, wakakubembeleza wee mwisho ukaja na conclusion mara oooh khumbu alifariki...sasa sitaki nataka zako ndo zimeharibu utamu wa story, yaani watu wanasoma huku wanaujua mwisho wa story, ile ladha imeotea.

4. Inshu ya bundle haina logic, JF haili bundle sana na pia hata wasomaji na wana tumia bundle...as long as umeamua kuandika kwa hiarai, andika tu mkuu.
USHAURI:

Mkuu siku nyingine usilete tena story hapa JF maana unapenda sana kutrend. Unachelewesha story isiishe ili kila saa wakutaje taje..trust me, kama usingekuja na zile episodes 32 za kwanza mapema, huu uzi wako usingekuwa hai hadi leo maana watu wasingeweza kuvumilia kiu kwa kitu kisichoeleweka ila ulikuwa mjanja kuteka hisia za wtu.

HITIMISHO: Uwezo wa kuandika story ndefu kwa siku unao, nia ya kuandika unayo, muda wa kuandika unao ila tu sababu za kutoandika/kuchelewesha story HAUNA....Basi tu unapenda trending na kiki kama wasanii


Ni mimi Mtetezi wa wana JF wanaoogopa kukwambia ukweli.
 
Nilihisi utakua umeiacha njiani ingeniuma sana,
ila tunashukuru Mkuu kwa muendelezo huu. Ila hii story imekula siku ya jana na leo kuisoma hivi na bado naendelea kusaka miendelezo zaidi...
 
Khumbu nimemchora kwa taswira nyingi sana na kumuedit kila unapompa sifa zaidi[emoji28]
 
Kumchangia mleta uzi ama kutokumchangia ni suala na maamuzi binafsi. Kama unao uwezo, toa na kama huna/hutaki tulia. Mambo yakuanza kuwaita mods kwa jambo ambalo wengine wameridhia ni kuwakosea heshma. Mods hawahusiki na michango iweje tuwashurutishe kuingilia kati. Halafu mbna sijaona sehemu mtoa mada amesema ni lazima uchange?

konda msafi endelea kwa muda wako. Tuko pamoja
 
Mkuu Fohadi, kujibu comments na kuandika stori ni vitu viwili tofauti. Kuandika stori inahitaji muda. Mwanzoni nilikuwa naandika mfululizo na kuitupia mara kwa mara kwa sababu nilidhani niingeimaliza fasta tu lakini kadri muda ulivyoenda nikaona hii kitu nikitaka niielezee na ieleweke sio ya kuisha fasta. Ni stori iliyochukua muda wa miaka 6, kuna mambo mengi tu sijayaelezea lakini bado sijaimaliza. Kiufupi inahitaji utulivu sana. Leo mchana kwa sababu nimeshinda nyumbani nilitaka nipunguze mzigo kidogo, nitupie hata episode moja lakini kuna mambo ya kikazi yakaingia kati.
 
Shukrani mkuu kwa kunielewa.
 
Nilihisi utakua umeiacha njiani ingeniuma sana,
ila tunashukuru Mkuu kwa muendelezo huu. Ila hii story imekula siku ya jana na leo kuisoma hivi na bado naendelea kusaka miendelezo zaidi...
Miendelezo ipo kibao mkuu. Pekua kila page utaipata.
 
Ndio huyo huyo sema kuna wengine wanauwez wa kuandika lakn ukiwapeleka kweny kuongea unaweza kushangaa kabisa lakn ndio huyo huyo mzee wa show za kimkakat
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…