Inaendelea,
Baada ya kupata kazi nikaanza harakati za kumleta Khumbu japo pia huko Bloemfontein nilipata mwanamke wa kunitoa upweke. Unajua kuna kipindi mwanaume unaweza kumpenda mwanamke kiasi kwamba hata ukiletewa wanawake wengine wazuri kumzidi huyo unayempenda lakini ukiambiwa umwache huyo uchukue hawa wengine bado unaweza usikubali kumwacha huyo unayempenda. Nadhani Khumbu alikuwa ameniingia sana rohoni kiasi kwamba wanawake wote nilikuwa nawaona hawatoshi. Kuna siku moja nilikuwa shopping mall huko Bloemfontein nikakutana na demu mmoja kisu hatari, nikamfuata na kujaribu kuanzisha mazungumzo naye, demu alikuwa anasukuma kitoroli hivi vya kufanyia shopping, nikawa namfuata nyuma nyuma akiwa anachukua vitu kwenye shelves na mimi huku nikiendelea kuimbisha, demu alikuwa anatoa ushirikiano mzuri tu, nikimwuliza kitu anajibu na yeye ananiuliza namjibu, kifupi alikuwa anaelekea kulainika lakini ingetokea nichague kati yake na Khumbu ningemchagua Khumbu.
Tulipopanga Khumbu aje kunitembelea, nilianza kufikiria huyu demu wa huku nitamkwepaje ili nipate nafasi ya kuwa na Khumbu. Kadri siku zilivyosonga akili yote ikawa inafikiria tu kumleta Khumbu maana kama kazi tayari nimeshapata, nakaa kwenye mjengo wa maana tu, pesa sio tatizo tena japo mshahara sio mkubwa kivile, ila kwa maisha ya kukaa na mwanamke unatosha kabisa.
Turudi nyuma kidogo, nilipoajiriwa Bloemfontein nilianzia kukaa nyumbani kwa mfanyakazi mwenzangu kitongoji kimoja kinaitwa Botshabelo. Nilipopata mshahara wangu wa kwanza ndio nikaenda kutafuta flat yangu. Nilipata flat ambayo alikuwa anaishi demu mmoja mwanafunzi. Tukakubaliana aniuzie kila kitu kilichokuwemo ndani. Nilimlipa kwa awamu kama nne hivi maana alikuwa anamiliki vitu vingi sana si unajua wanawake wanavyopenda kuwa na kila kitu kwenye magheto yao hivyo nisingeweza kuvilipia kwa mshahara wa mwezi mmoja. Nilipomaliza kulipa deni tukaenda kubadirisha jina la mpangaji na kuwekwa jina langu. Kule kuna ma-agent wanaopangisha nyumba, yaani ni kampuni inayojihusisha na kupangisha nyumba, kwa hiyo mpangaji ukikidhi vigezo wanakupangisha na unakuwa responsible kwa chochote kitakachotokea kwenye mjengo. Geto likawa limekamilika tayari kwa kuanza mchakato wa kumleta Khumbu.
Haya tuendelee, Nikatafuta sababu ya kugombana na yule demu ili aniache kwa muda nipate nafasi ya kuwa na Khumbu. Nilianzisha visa visivyokuwa na kichwa wala miguu, kila nikikumbuka roho huwa inanisuta sana. Nilianza tabia ya kununa nuna bila sababu ya msingi, demu akawa anashangaa nilivyobadirika. Kuna siku tulikuwa tunafanya mapenzi, kwa bahati mbaya sijui nilimkwaruza na kucha kwenye k, sijui nilimpiga pipe tu mpaka kupelekea hilo tatizo, hata sielewi, nikiwa nampelekea moto nikaona damu inatoka, ilikuwa style ya kumchumisha tembele. Nilipoona zile damu nikawa kama namgombeza, nikawa namlaumu kwa nini ananipa mzigo akiwa kwenye siku zake. Akawa anajitetea hayupo kwenye siku zake ila anadhani amechunika tu. Basi mie nikakasusa, sitaki tena kuendelea. Kila siku vitimbwi haviishi, baadae akajiongeza akaniambia tuchukue break kwanza, akaniambia anahisi kama ananibore siku hizi. Na mimi nikamwambia sawa let us have a break. Hapo lengo langu likawa limetimia.
Nikaanza mchakato wa kumtumia nauli Khumbu. Nikamwambia nimkatie kabisa ticket hukuhuku. Makampuni ya mabasi kwa South Africa unaweza kumkatia mtu tiketi kama unavyomnunulia mtu kifurushi cha tigo. Basi nikaenda shopping mall flani inaitwa Water front, mle kuna ofisi za wakala wa mabasi. Nikaamua kumfanyia booking tu badala ya kulipia kabisa. Nikamwambia hela nitakutumia ila tayari nimeshakufanyia booking kwenye mabasi ya “SA Road Link” hela nitakutumia kwenye account yako ya benki. Tukawa tumekubaliana hivyo. Kesho yake ndio alitakiwa kusafiri kuja Bloemfontein. Akanitumia namba za account yake, nikaenda kumtumia nauli na hela kidogo ya kutumia njiani.
Nilipomtumia hiyo hela nikawa namsisitiza aende akailipie hiyo ticket, na yeye akawa ananiambia muda si mrefu atatoka nyumbani ana ataelekea town kutoa hiyo hela na kwenda kuilipia ticket. Mie nikawa namwambia hakuna haja ya kwenda benki kutoa hela, yeye aende tu akalipie kwa kutumia card yake ya bank, maana ilikuwa visa debit card. Yeye akasisitiza anaenda kutoa hela, anataka kulipia kwa cash. Sikutaka kumbishia sana, nilimwacha aamue anataka kulipiaje, cha muhimu tu kesho alfajiri awe Bloemfontein. Basi tukaagana hapo, mie nikaenda zangu nyumbani kupumzika nikisubiria anijulishe kashalipia ticket. Hapo ilikuwa mida ya saa nne asubuhi.
Masaa yakazidi kwenda bila kupata feedback yeyote. Ilipofika saa tisa nikampigia kumwuliza kama amepata hiyo ticket. Akaniambia bado hata mjini hajaenda ila nisiwe na wasiwasi. Nikaanza kupata wasiwasi, huyu mwanamke huenda anataka kunichezea mchezo hapa. Huko bank atafika saa ngapi, na bank zinafungwa saa 11 na hataki kwenda kulipia kwa card yake. Nikajisemea acha nisubiri nione. Nikawa nampigia simu karibia kila baada ya nusu saa kumharakisha atoke aende kulipia hiyo ticket. Baadae ndio akaniambia yupo anadrive anaenda bank. Hapo ni kama saa 10:30 jioni, dah! Kwa huo muda nikawa na mashaka kama atakuta benki bado zipo wazi. Kwenye saa 11 hivi nikampigia tena kujua kinachoendelea simu ikawa haipatikani, nikaconclude huyu mwanamke haji, acha nipambane na hali yangu. Nilipata hasira, nikajiona bonge la fala. Nikawa namfikiria huyu dada wa watu niliyemfanyia visa mpaka akaamua kuchukua break. Niliendelea kumtafuta Khumbu kwenye simu na ikaendelea kutokupatikana. Nikawa nafikiria hivi huyu Khumbu ananionaje? Ole wake ajichanganye aje Bloemfotein. Kila nikifikiria napata hasira kinoma. Ilipofika kwenye saa mbili hivi usiku nikaona simu yake inaingia, akaanza kuniomba samahani kwa kushindwa kuja kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wake. Hapo mimi namsikiliza tu hata siongei, alipomaliza kuongea nikamwuliza swali moja tu. Lini utakuja? Akasema atanijulisha. Nikajua tu hapa hakuna kitu. Nikiwa na hasira huwa siwezi kujicontrol nilimtukana. Basi nikiwa na stress zangu nikaamua acha nijilazimishe kulala tu maana usingizi sikuwa nao kabisa. Ile nikiwa kwenye lindi la mawazo simu ikaita, kucheki hivi number inasoma “number withheld”, nikaipokea, nikawa nasikia kama watu wapo bar, jamaa aliyepiga akaniambia “I am going to kill you, just one bullet on your head”, kabla sijaongea chochote jamaa akakata simu. Hapo nikaingiwa na hofu. Kwanza nikawa najiuliza, huyu jamaa yupo wapi? Isije ikawa tayari yupo Bloemfontein ananiwinda, namba yangu kaipata wapi? Ila nikajua tu hii itakuwa sababu ya Khumbu. Nikawa najiuliza sijui nimpigie simu Khumbu nimwulize kwa nini anataka kunitoa roho? Wazo jingine likanijia labda kumpigia simu sio jambo sahihi maana huenda yupo na huyo muuaji hivyo kumpigia simu itakuwa kama naharakisha kifo changu. Basi nikaamua acha kwanza nitulie nione nini kitaendelea ila inabidi niwe makini sana.
Itaendelea, nitajitahidi leo niimalize.