Inaendelea
Khumbu alinipeleka nilikofikia kuchukua vitu vyangu kisha akanipeleka stand kuangalia usafiri wa kunirudisha Bloemfontein. Katika mizunguko yote hiyo niliweza kunotice kuwa Khumbu bado alikuwa ananipenda ila ni kama alikuwa na commitment flani hivi zinanamfanya kuwa na wakati mgumu kunisikiliza kila ninachomwambia, maana kuna kipindi alikuwa kama anazama kwenye lindi la mawazo hivi, halafu nikiwa namweleza ni jinsi gani anayafanya maisha yangu kuwa magumu kimahusiano nilikuwa namuona kama mtu anayejutia hivi. Kulikuwa na zile moments ukimya unatawala halafu mkija kuangalia unaona kama kila mtu machozi yanamlengalenga. Aliponifikisha stand, nikashuka na yeye akashuka, tukaagana kwa kukumbatiana, sikuweza kuongea chochote maana kitendo cha kumkumbatia na kuushika mwili wake kilinifanya niingiwe na huzuni sana, nilimsikia tu akitamka maneno mawili “I’m sorry” na akaanza kujitoa mikononi mwangu, nilikuwa nimemkumbatia kuzungusha mikono yangu kiunoni kwake mpaka ikakutana, kwa hiyo akawa anaishika kwa kuiachanisha ili niweze kumuachia. Baada ya kujitoa mikononi mwangu akaingia garini akaondoka. Niliendelea kusimama pale nikimwangalia mpaka alipojichanganya kwenye magari mengine ndio nikaondoka hilo eneo.
Njiani nikiwa kwenye basi nilianza kufikiria vitu vingi sana vya kimaisha. Mojawapo nilianza kufikiria je nieendelee kuishi Bloemfontein nijenge maisha na huyu mwanamke wa Bloemfontein? Je nirudi Durban nikatafute kazi huko ili niweze kuwa karibu na Khumbu? Je nirudi Tanzania nikamthaminishe Amina na yule demu wa Sinza kisha atakayelipa zaidi nije naye South Africa? Baada ya hii graduation je niendelee kuishi South Africa yaani nijichanganye kabisa hapa niachane na mawazo ya kurudi Tanzania yaani hapa Sauzi yawe ndio maisha yangu permanent? Je nirudi Tanzania nikatafute kazi, nikaishi tu nyumbani huenda nikaishi kwa furaha zaidi? Maswali yalikuwa mengi na sikujua lipi niamue.
Baada ya graduation niliendelea na kazi huku nikiwa na huyu mwanamke wa Bloemfontein. Pia niliendelea kuwasiliana na Amina na huyu wa Sinza. Huyu wa Sinza alikuwa na sauti moja amazing. Kipindi naonana naye alikuwa mzuri sana ila kwa kuwa ilikuwa ishapita miaka mingi nilikuwa na wasiwasi kama bado ni mrembo maana wanawake huwa wanabadirika haraka sana, miaka sita kwa wanawake ni miaka mingi sana. Amina alikuwa ananitumia picha na alionekana bado analipa sana tu ila huyu wa Sinza kila nikimwomba anitumie picha alikuwa anadai nije nimuone mwenyewe kwa macho yangu ila kwa maoni yeke yeye ni mrembo wa haja. Huyu wa Sinza kitendo cha kukataa kunitumia picha kilianza kunitia wasiwasi hivyo nikaamua kutuma mtu kwenda kukutana naye ili anipe feedback. Kuna mdogo wangu alikuwa anasoma chuo flani nikampigia simu nikamwomba akamcheki huyu demu. Nikampa namba ya huyo demu na pia nikampigia simu huyo demu nikamwambia shemeji yako nimemwomba aje akusalimie ili mjuane pia apajue unapoishi ili hata kama kuna shida yoyote iwe rahisi kupatikana kwako. Demu akakubali. Dogo akaenda kumcheki na baada ya kumcheki akanipigia simu kunijulisha matokeo. Dogo akaniambia demu ni wa kawaida sana hana maajabu yoyote. Kama ni wa kula na kusepa fresh ila kama unataka kufanya naye maisha na kwa jinsi ninavyokujua unapenda kula vilivyo bora huyo hajafikia viwango vyako. Hiyo ilikuwa tathimini ya dogo. Dah! nikawa najiuliza labda huyu dogo ana jambo lake tu. Mbona demu alikuwa kifaa hivi enzi hizo, iweje awe mbovu tena? Nikasema huyu dogo anazingua, acha niendelee na mchakato wa kuwa naye karibu huyu demu. After all nishatumia gharama za kupiga simu karibia kila siku hivyo hata kama atakuwa halipi acha angalau nikafidie gharama zangu kwa kumla. Hivyo maisha ya kuendelea kuwasiliana na wote hawa wawili yaliendelea hadi niliporudi Tanzania.
Kadri siku zilivyokuwa zinasonga ndivyo nilivyozidi kupata moto wa kurudi nyumbani. Picha za Amina na Sauti ya demu wa Sinza zilikuwa zinanipa matumaini mapya ya kimapenzi. Huyu wa Sinza alikuwa na sauti nzuri hatari, nikiwa naongea naye nilikuwa hadi dushe linasimama. Amina naye hivyo hivyo, picha zilikuwa zinanichangaya sana.
Siku moja usiku mwezi wa 10, 2012 nikakata shauri la kurudi nyumbani. Niliamka usiku wa manane, nikachukua diary yangu nikaandika tarehe ya hiyo siku nikasema hii tarehe ndio tarehe niliyokata shauri na kuamua kurudi Bongo.
Kesho yake asubuhi nilipofika ofisini nikamfuata Boss wa kampuni, ni mmoja wa madirectors, nikamwambia “Leo naacha kazi”. Aliniangalia akiwa kama anashangaa, akasema nirudie tena nilichokisema, nikarudia tena “Leo naacha kazi” nilimuona kama kaduwaa. Alikuwa ana kikombe cha kahawa mkononi akakiweka kwenye mezani kisha akaniuliza vipi unaumwa? Umechanganyikiwa? Nikamjibu siumwi wala sijachanganyikiwa. Nimeamua tu niache kazi, nimeamua kurudi nyumbani. I miss home. Akasema wewe Konda msafi unacheza na maisha. Unarudi Tanzania kufanya nini? Akaanza kunipa ushauri, nakumbuka kuna maneno nayakumbuka mpaka leo aliniambia, alisema “All these achievements I have I never got them in one day I have acquired them in years. If you serve God, God will take care of you” . Akaniomba jioni baada ya kazi nisiondoke ili tupate muda wa kuzungumza zaidi. Jioni baada ya kazi nikaenda ofisini kwake. Jamaa alinishauri mambo mengi sana ya kimaisha. Akawa ananiambia sio jambo la kushangaza kama siku moja ataniona namiliki kampuni yangu hapa South Africa kama nitakuwa na nidhamu ya kazi. Pale kwenye kampuni nilikuwa nadili na suppliers wa materials na payroll. Auditor wa kampuni alikuwa Ernst and Young kwa hiyo queries zote za auditor kuhusu suppliers na payroll nilikuwa nazi-attend. Kila mwisho wa mwezi nilikuwa napelekwa na dereva wa kampuni kwa auditor. Suppliers wakipiga simu kuulizia malipo yao mimi ndio nilikuwa nadili nao au mimi kuwapigia simu kama kuna mzigo una shida au umechelewa kufika. Kuhakikisha materials yamepokelewa na kampuni ilikuwa ni kazi yangu, invoice za suppliers lazima nizihakiki kabla ya malipo. Jamaa akawa ananiambia hatashangaa siku moja akiniona nimeshakuwa Chartered Accountant kama nitavumilia, na akasema ataniunganisha na CAs ili wanipe muongozo jinsi ya kufika hapo. Kiufupi jamaa alianza kunipa elimu ya maisha mpaka nikaghairi maamuzi yangu.
Itaendelea