konda msafi
JF-Expert Member
- Sep 5, 2018
- 1,696
- 8,763
- Thread starter
-
- #3,061
Inaendelea
Ilipofika saa 6 za usiku nikawaomba jamaa wanirudishe nyumbani maana wao walikuwa hata hawana dalili za kutaka kuondoka. Wakaniomba wamalizie vinywaji vyao kisha tutaondoka.
Tulifika mjengoni kwenye mida ya saa 8 hivi, mie nikaenda moja kwa moja kulala.
Asubuhi nikamcheki Khumbu kujihakiki kama anakuja kukutana na mimi. Akasema anakuja. Basi nikaingia bafuni kuoga, nikapata kifungua kinywa na safari ya kwenda town kukutana na Khumbu ikaanza. Hayo maeneo waliyokuwa wanakaa jamaa zangu nilikuwa hata sijui wapi pa kupandia daladala, ilibidi niwaombe washikaji wanielekeze. Jamaa wakaniambia nisubirie tutaondoka wote maana hata wao wanaelekea huko huko lakini niliwakatalia, niliwaambia nahitaji kuwahi hivyo acha tu nitumie daladala. Basi wakanielekeza sehemu ya kupandia daladala na wakanipa ufunguo wa akiba wa mjengo in case nitarudi mapema.
Safari ya town ikaanza na nikafika mapema kabla ya saa nne. Nikamcheki Khumbu kwenye simu na kumjulisha tayari nimeshafika na yeye akasema yupo njiani. …Baada ya muda akanipigia akasema tayari yupo workshop. Nikamwelekeza sehemu nilipo, nilikuwa ndani ya shopping mall. Akaniambia nitoke tukutane kwa nje. Basi nikatoka nikaenda sehemu moja hivi nje pale pavement za workshop zinapoanzia. Kuna nguzo flani fupi fupi nene za zege zenye urefu kama mita moja hivi zimepandwa kuzunguka hiyo pavement ya workshop kuzuia magari kuingia workshop kwa kutumia njia isiyo rasmi. Nikawa nimekaa kwenye hizo nguzo. Nikamwelekeza Khumbu sehemu nilipo, akaja. Alikuwa amevaa sketi ya blu ya jean inayoishia juu ya magoti, juu amevaa vest ametupia na kimkoti cha jeans. Miguu yake unaiona kabisa jinsi ilivyosimikwa vizuri. Alipofika pale na yeye akakaa kwenye nguzo halafu akanyoosha miguu. Kitendo cha yeye kukaa kwenye ile nguzo huku akiwa ameinyosha miguu kilinitia kiwewe, mnara ukasoma maana mapaja yakawa yamemwagika, si unajua mwanamke akikaa hata kama hana hips lakini huwa anaonekana ana hips. Sasa khumbu kajaliwa hips naturally halafu piga picha sasa amekaa kwenye nguzo na kunyosha miguu. Kisiketi kikapanda kidogo, mijipaja ikawa imemwagika, hips zimetanuka halafu nikimcheki miguu soft inawaka kama kamwagiwa asali. Nikawa natamani nimrukie. Basi tukasalimiana pale kisha nikamweleza kuwa narudi nyumbani. Akaniuliza “narudi nyumbani kusalimia au moja kwa moja?’ nikamwambia moja kwa moja, akaulizwa kwa nini? Nikamwelezea sababu nyingi kama kumiss nyumbani na nyingine nyingi lakini kubwa kuliko yote nikamwambia yeye ni sababu. Nikamwambia “maisha yangu yote niliyoishi South Africa sijawahi kupenda mwanamke kama ninavyokupenda kwa hiyo naona nikiendelea kuishi hapa nitaendelea kuteseka tu na huenda nikapoteza hata maisha kwa sababu yako” Akaniuliza unaondoka lini? Nikamwambia keshokutwa na tayari ticket ninayo. Naondokea OR Tambo airport. “Leo ni siku yangu ya mwisho kuwepo Durban. Kesho asubuhi naelekea Johannesburg kwa sababu keshokutwa saa nne asubuhi ndio naondoka”. Nilikuwa naongea kwa hisia kali, tone niliyokuwa natumia ilikuwa ya huzuni sana, body language niliyokuwa nayo ilikuwa ya majonzi. Nilipokuwa naongea nikamuona machozi yanamtiririka, akawa anajifuta kwa vidole. Nikamwangalia usoni nikaacha kuendelea kuongea, na yeye akaniangalia kisha akaniuliza “Kwa hiyo mimi ndio sababu unaondoka South Africa?” Nikamwambia usijisikie vibaya, kuna sababu nyingi zinazonifanya niondoke ila na wewe ni sababu mojawapo. Akaniambia “ahirisha safari ili tuwe pamoja” nikamwambia siwezi kuahirisha safari, tayari nimeshakata ticket. Nikamwambia kama unaweza twende zetu tukawe faragha japo kwa hii siku moja niliyo nayo hapa Durban. Akasema kwa leo hawezi ila kwa kesho sawa. Nikamwambia kesho sitakiwi kuwepo hapa, kesho nitakuwa safarini kwenda Johannesburg. Akasema “kama kweli unataka kuwa na mimi naomba uahirishe safari, ondoka siku nyingine”. Nikapiga mahesabu ya haraka haraka, nikaona kuahirisha safari itakuwa jambo la kipumbavu. Naweza kuahirisha safari halafu nikapigwa chenga tena, nikabaki kujuta. Nikamwambia, Khumbu kama hutaki kuwa na mimi kwa siku ya leo basi, siwezi kuahirisha safari. Na yeye akasema kama siwezi kuahirisha safari basi, kwa leo haitawezekana. Basi tukaagana pale nikiwa heart broken. Akaniambia nikifika Johannesburg nimpigie simu, pia nikifika Tanzania nimpigie. Nikainuka kwenye nguzo, nikaanza kuondoka. Nimepiga kama hatua tatu akaniita, “Konda msafi naomba urudi”. Nikasimama, nikageuka kumwangalia, akanifanyia ishara ya kuniita kwa mkono. Na mimi nikamwonyesha ishara kwa mikono kumwuliza anasemaje? Akasema njoo. Nikarudi, akaniambia “usiondoke kesho”. Nikamwangalia kisha nikatikisa kichwa kuashiria siwezi kuahirisha safari. Nikageuka, nikavuka barabara upande wa pili, nikamwangalia kama bado yupo nikamwona bado yupo ananiangalia, nikaendelea kutokomea, nikaondoka maeneo ya workshop.
Itaendelea.
Ilipofika saa 6 za usiku nikawaomba jamaa wanirudishe nyumbani maana wao walikuwa hata hawana dalili za kutaka kuondoka. Wakaniomba wamalizie vinywaji vyao kisha tutaondoka.
Tulifika mjengoni kwenye mida ya saa 8 hivi, mie nikaenda moja kwa moja kulala.
Asubuhi nikamcheki Khumbu kujihakiki kama anakuja kukutana na mimi. Akasema anakuja. Basi nikaingia bafuni kuoga, nikapata kifungua kinywa na safari ya kwenda town kukutana na Khumbu ikaanza. Hayo maeneo waliyokuwa wanakaa jamaa zangu nilikuwa hata sijui wapi pa kupandia daladala, ilibidi niwaombe washikaji wanielekeze. Jamaa wakaniambia nisubirie tutaondoka wote maana hata wao wanaelekea huko huko lakini niliwakatalia, niliwaambia nahitaji kuwahi hivyo acha tu nitumie daladala. Basi wakanielekeza sehemu ya kupandia daladala na wakanipa ufunguo wa akiba wa mjengo in case nitarudi mapema.
Safari ya town ikaanza na nikafika mapema kabla ya saa nne. Nikamcheki Khumbu kwenye simu na kumjulisha tayari nimeshafika na yeye akasema yupo njiani. …Baada ya muda akanipigia akasema tayari yupo workshop. Nikamwelekeza sehemu nilipo, nilikuwa ndani ya shopping mall. Akaniambia nitoke tukutane kwa nje. Basi nikatoka nikaenda sehemu moja hivi nje pale pavement za workshop zinapoanzia. Kuna nguzo flani fupi fupi nene za zege zenye urefu kama mita moja hivi zimepandwa kuzunguka hiyo pavement ya workshop kuzuia magari kuingia workshop kwa kutumia njia isiyo rasmi. Nikawa nimekaa kwenye hizo nguzo. Nikamwelekeza Khumbu sehemu nilipo, akaja. Alikuwa amevaa sketi ya blu ya jean inayoishia juu ya magoti, juu amevaa vest ametupia na kimkoti cha jeans. Miguu yake unaiona kabisa jinsi ilivyosimikwa vizuri. Alipofika pale na yeye akakaa kwenye nguzo halafu akanyoosha miguu. Kitendo cha yeye kukaa kwenye ile nguzo huku akiwa ameinyosha miguu kilinitia kiwewe, mnara ukasoma maana mapaja yakawa yamemwagika, si unajua mwanamke akikaa hata kama hana hips lakini huwa anaonekana ana hips. Sasa khumbu kajaliwa hips naturally halafu piga picha sasa amekaa kwenye nguzo na kunyosha miguu. Kisiketi kikapanda kidogo, mijipaja ikawa imemwagika, hips zimetanuka halafu nikimcheki miguu soft inawaka kama kamwagiwa asali. Nikawa natamani nimrukie. Basi tukasalimiana pale kisha nikamweleza kuwa narudi nyumbani. Akaniuliza “narudi nyumbani kusalimia au moja kwa moja?’ nikamwambia moja kwa moja, akaulizwa kwa nini? Nikamwelezea sababu nyingi kama kumiss nyumbani na nyingine nyingi lakini kubwa kuliko yote nikamwambia yeye ni sababu. Nikamwambia “maisha yangu yote niliyoishi South Africa sijawahi kupenda mwanamke kama ninavyokupenda kwa hiyo naona nikiendelea kuishi hapa nitaendelea kuteseka tu na huenda nikapoteza hata maisha kwa sababu yako” Akaniuliza unaondoka lini? Nikamwambia keshokutwa na tayari ticket ninayo. Naondokea OR Tambo airport. “Leo ni siku yangu ya mwisho kuwepo Durban. Kesho asubuhi naelekea Johannesburg kwa sababu keshokutwa saa nne asubuhi ndio naondoka”. Nilikuwa naongea kwa hisia kali, tone niliyokuwa natumia ilikuwa ya huzuni sana, body language niliyokuwa nayo ilikuwa ya majonzi. Nilipokuwa naongea nikamuona machozi yanamtiririka, akawa anajifuta kwa vidole. Nikamwangalia usoni nikaacha kuendelea kuongea, na yeye akaniangalia kisha akaniuliza “Kwa hiyo mimi ndio sababu unaondoka South Africa?” Nikamwambia usijisikie vibaya, kuna sababu nyingi zinazonifanya niondoke ila na wewe ni sababu mojawapo. Akaniambia “ahirisha safari ili tuwe pamoja” nikamwambia siwezi kuahirisha safari, tayari nimeshakata ticket. Nikamwambia kama unaweza twende zetu tukawe faragha japo kwa hii siku moja niliyo nayo hapa Durban. Akasema kwa leo hawezi ila kwa kesho sawa. Nikamwambia kesho sitakiwi kuwepo hapa, kesho nitakuwa safarini kwenda Johannesburg. Akasema “kama kweli unataka kuwa na mimi naomba uahirishe safari, ondoka siku nyingine”. Nikapiga mahesabu ya haraka haraka, nikaona kuahirisha safari itakuwa jambo la kipumbavu. Naweza kuahirisha safari halafu nikapigwa chenga tena, nikabaki kujuta. Nikamwambia, Khumbu kama hutaki kuwa na mimi kwa siku ya leo basi, siwezi kuahirisha safari. Na yeye akasema kama siwezi kuahirisha safari basi, kwa leo haitawezekana. Basi tukaagana pale nikiwa heart broken. Akaniambia nikifika Johannesburg nimpigie simu, pia nikifika Tanzania nimpigie. Nikainuka kwenye nguzo, nikaanza kuondoka. Nimepiga kama hatua tatu akaniita, “Konda msafi naomba urudi”. Nikasimama, nikageuka kumwangalia, akanifanyia ishara ya kuniita kwa mkono. Na mimi nikamwonyesha ishara kwa mikono kumwuliza anasemaje? Akasema njoo. Nikarudi, akaniambia “usiondoke kesho”. Nikamwangalia kisha nikatikisa kichwa kuashiria siwezi kuahirisha safari. Nikageuka, nikavuka barabara upande wa pili, nikamwangalia kama bado yupo nikamwona bado yupo ananiangalia, nikaendelea kutokomea, nikaondoka maeneo ya workshop.
Itaendelea.