Jinsi mapenzi ya mtoto wa Kizulu Durban South Africa yalivyotaka kunitoa roho

Jinsi mapenzi ya mtoto wa Kizulu Durban South Africa yalivyotaka kunitoa roho

Inaendelea,

Nilipompa hiyo rand 20, akainuka na kwenda kutafuta sehemu ya kula (kunywa chai). Alivyoinuka hapo ndio niliweza kuuona uzuri wake. Nakumbuka hadi leo alikuwa amevaa top nyeusi mikono mirefu na jeans ya blue. Alikuwa ametokelezea hatari. Kwa wale waliofika South Africa watakubaliana na mimi, wanawake wa kisauzi wapo njema sana kwenye maumbo. Anyway, demu alikuwa kifaa cha haja. Alikuwa ana umbo lililokatika vyema. Alikuwa na tako zuri, kubwa la wastani, ila kwa bongo ataonekana ana bonge la tako, Sio yale matako makubwa ya kufuru ya wasouth Africa, sura pia ilikuwa sio haba, ngozi chocolate color. Kwa ufupi Khumbu alikuwa mrembo sana. Hadi masela wangu walimkubali kwa kila kitu. Nadhani South Africa inaongoza kwa wanawake wenye matako makubwa. Kwenye matako wanawake wa Dizonga wako njema, wakina Sanchi mnaowaona wana mizigo ni takataka tu ukimpeleka Dizonga.

Basi tukaagana pale yeye akaenda kutafuta chakula na mimi nikavuka barabara nikaenda kununua chai na vitafunio, nikarudi zangu golini.

Nikanywa chai kama kawaida, Chaduma akapita nikamwambia tayari nishakunywa chai. Baadae kidogo demu nikamuona kwa mbali anakuja, ila akawa kama anaangaza angaza kama kapotea hivi maana kuna matents mengi yanayouza viatu vya kike na yamepangana, ila kwa kuwa mie tayari nishamuona nikawa kama nampungia mkono hivi ili anione. Akafika golini, nikampa kiti akakaa. Tukaanza kupiga stori sasa. Nikamwelezea mimi ni nani, nafanya nini na mambo mengine. Na yeye akanielezea anaitwa Khumbu, anakaa township moja inaitwa Inanda, na mambo mengine ya hapa na pale. Tukabadirishana namba za simu, tukapanga tutaonana jioni baada ya mimi kufunga. Baada ya demu kuondoka masela wangu walianza kuniuliza, huyu demu umempata wapi? Wewe kweli una mavumba, umekuja juzi tu tayari umepata demu kisu hivi? Mie nikawaeleza jinsi nilivyokutana na demu muda mfupi uliopita.

Jioni mida ya kufunga Khumbu akawa amekuja pale golini. Nikampa kiti akawa ananisubiria tufunge ili tuweze kuangalia kama tutaondoka wote au amekuja tu kwa ajili ya maongezi zaidi. Jamaa zangu walipomuona amerudi wakawa wananitania “Leo uhakika”. Baada ya kumaliza kufunga ikabidi nianze kuongea naye, halafu alikuja akiwa kabadilisha nguo. Kumbe alienda nyumbani kabisa, hivyo alivyorudi ile jioni alikuwa ametoka nyumbani na amekuja kwa ajili yangu. Jamaa yangu akaniuliza, vipi tunaondoka wote (kwenye gari )au mtakuja kivyenu? Maana kwa kawaida huwa tukifunga tuonaodoka wote kurudi nyumbani kwenye gari yake. Nikamgeukia demu nikamwuliza, vipi twende home basi ili ukapajue. Demu hakuwa na kipingamizi. So tukazama ndani ya gari tukaanza safari ya kuelekea geto. Jamaa yangu akaniambia misosi yetu ya kibongo huko magetoni huyu hawezi kula hivyo acha tupitie KFC tumnunulie kitu cha kwenye mabox, basi gari ikaingia KFC kwenye drive thru, tukachukua kitu cha box tukasepa.

Tukafika geto, demu nikampaki sebuleni, nikaingia jikoni kupika misosi yetu ya kibongo huku yeye akiendelea kula msosi wake wa KFC. Kumbuka mie nalala kwenye kale kastore pamoja na mshikaji mwingine homeboy, mdogo wake na huyu jamaa yetu mwenye gari. Huyu jamaa ninaye lala naye alikuwa mtu wa tungi sana. Mkifunga goli ile jioni yeye anaelekea bar kukutana na wabongo wengine wanywaji, hivyo kurudi kwake mpaka saa 5 au 6 hivi usiku, sometimes anaweza kulala kwa masela wake huko. Baada ya demu kumaliza kula nikamwonyesha chumba ”changu” ili akabadili nguo afanye mchakato wa kuoga. Hivyo akaingia chumbani (store), akajiweka, akavaa kanga akaingia bafuni kuoga. Najua watu wataanza kusema hii ni chai kwa kuona demu wa kisauzi anavaaje kanga, au kapataje kanga. Kwa taarifa yenu Khumbu alikuwa na kanga, na kila siku alipokuwa ananitembelea alikuwa anakuja na kanga. Kanga south Africa zipo, sijui wanazitoa Swaziland, maana waswaziland ndio huwa nawaona wanavaa kanga, anyaway sijui alikuwa ananunua wapi ila kanga alikuwa nazo za kutosha.

Baada ya kumaliza kupika mimi na jamaa yangu na Mburundi tukawa tunakula hapo sebuleni. Utaratibu ilikuwa ni kupika kwa zamu, na kula wote pamoja.

Demu akamaliza kuoga akarudi chumbani. Na mimi baada ya kumaliza kula nikaenda kuoga, nikamaliza kuoga nikaenda chumbani. Ila hapo katikati tayari nishampigia simu mwana kuwa leo nimevusha hivyo kama vipi atalala sebuleni kwenye makochi au aendelee kuruka nyoka mpaka asubuhi.

Inaendelea
Sehemu ya tatu
Samahani mkuu, kuna sehemu ukiulizwa sababu ya kifo cha Khumbu, ukajibu urembo wake ndo uliomponza? Sasa kuna uhusiano gani kati ya kubanwa mbavu na kufariki na kuponzwa na urembo wake?
 
Samahani mkuu, kuna sehemu ukiulizwa sababu ya kifo cha Khumbu, ukajibu urembo wake ndo uliomponza? Sasa kuna uhusiano gani kati ya kubanwa mbavu na kufariki na kuponzwa na urembo wake?
Very good question. Yaani wewe ingekuwa ni mtihani ungepata extra max kwa kusoma between the lines na kugundua kitu ambacho wengi hawakukiona. Kuna scenerio nyingi tu sikuzisimulia kwa sababu ningezisimulia huu uzi ungechukua muda mrefu sana kuisha. So nakuomba upotezee tu kwa sababu uzi tulishaufunga.
 
Very good question. Yaani wewe ingekuwa ni mtihani ungepata extra max kwa kusoma between the lines na kugundua kitu ambacho wengi hawakukiona. Kuna scenerio nyingi tu sikuzisimulia kwa sababu ningezisimulia huu uzi ungechukua muda mrefu sana kuisha. So nakuomba upotezee tu kwa sababu uzi tulishaufunga.
Nafikiri mkuu konda msafi ingekuwa busara ukamjibu hilo swali kwa njia ambayo ni fupi na ya kueleweka. "Curiosity killed a Cat"
 
Bonge la story. Zaidi ya mahusiano uliyokuwa nayo kuna la kujifunza hapa. Maisha ni safari.
 
Mwaka 2008 niliingia Durban baada ya kuitwa na jamaa zangu waliokuwa huko. Hawa jamaa zangu tuna undugu pia. Kaka yao kaoa shangazi yetu, na pia kaka yetu kaoa dada yao, ni kama tumeoleana, wao wameoa kwetu na sisi tumeoa kwao. Pia hawa jamaa tumesoma shule moja ya msingi japo madarasa tofauti.

Historia fupi kabla sijaingia Durban. Nilifika South Africa toka 2003. Nilifikia Johannesburg. Joburg nilienda kama volunteer kwenye taasisi moja ya kidini ambayo nisingependa kuitaja. Nikiwa naendelea kufanya kazi kwenye hiyo taasisi niliwaomba wanisaidie kumalizia elimu nyangu ya sekondari. Walinikubalia na process zikaanza kufanyika. Ilibidi nirudi Tanzania kwa ajili ya kwenda shule niliyokuwa nasoma ili kupata nyaraka za kuonyesha nimesoma mpaka level gani maana nilitoka bongo nikiwa hata sijamaliza form three. Mambo yalienda vizuri na niliweza kuanza masomo kwenye shule moja inaitwa Mosupatsela High School iliyopo kwenye kitongoji kinaitwa Kagiso. Kagiso ipo karibu na suburb moja inaitwa Krugersdorp. Nilimaliza high school 2007, na 2009 nikafanikiwa kuingia chuo. Mwaka 2008 ndio nikapata mawasiliano na hao ndugu zangu waliopo Durban, Kwa Zulu Natal.

Huko Joburg sio kwamba sikuwa na mahusiano, mahusiano nilikuwa nayo ila nimeamua kuongelea mahusiano ya Durban maana vurugu za Durban naweza kusema kama ni jembe basi mpini ulivunjikia Durban. Kuna mambo kila nikiyakumbuka yanafurahisha na kuhuzunisha. Durban kuna mambo mengi nimeyafanya, mengine siko proud nayo kabisa. Mojawapo ni hili la mshikaji kumleta demu gheto na tukamla wote wawili, demu mwenyewe alilidhia. Hili wala sitaliongelea.

Mwaka 2008 nikawa nimeingia Durban. Nilipanda basi sehemu moja inaitwa Park station mida ya saa tatu usiku. Saa tisa alfajiri nikawa nimetia timu stand ya mabasi Durban. Nikawacheki wenyeji wangu kwenye simu, wakasema nisubiri kupambazuke watanifuata. Asubuhi jamaa zangu wakaja na kipira kunichukua. Break ya kwanza nikapelekwa sehemu moja inaitwa “the workshop”. The workshop ipo downtown Durban, ipo karibu tu na kituo cha mabasi. Kipindi hicho masela wangu walikuwa na goli la viatu vya kike. Tulipofika hapo workshop jamaa wakawa wanafunga tent ili wapange viatu tayari kwa biashara. Baada ya kumaliza kupanga viatu na movements za watu kwenda kazini zishaanza kuwa nyingi jamaa akaniambia sasa ni muda wa kunipeleka magetoni nikapumzike kwanza. Tukaingia kwenye ndinga na safari ya kwenda magetoni ikaanza. Tukiwa tunaelekea magetoni jamaa akapitia KFC ili nipate kitu cha kwenye mabox kwa ajili ya msosi. Jamaa walikuwa wamepanga sehemu moja inaitwa Rossburg. Walikuwa wamechukua flat nzima yaani floor nzima. Kwenye hiyo flat walikuwa wanashare watu watatu. Flat ilikuwa na vyumba vitatu, sebule moja kubwa, jiko na bafu. Pia kulikuwa na kichumba kimoja kwa ajili ya store. Sasa kwenye hicho kichumba nilikuwa nalala mimi na mshikaji mmoja ambaye pia ni homeboy. Nyumba nzima tulikuwa watu watano, yaani Jamaa zangu wawili walioniita (ni mtu na mdogo wake), Mburundi mmoja, jamaa mmoja Mbongo alikuwa akiitwa baba Isa, na mimi sasa. Hawa jamaa wote walikuwa na mademu zao wa kizulu. So siku ya kwanza ikaisha kwa kupumzika.

Siku ya pili jamaa wakaniambia nikiamka nifanye mpango wa chai kisha nipande taxi kwenda workshop wanakofanyia biashara. Kule daladala zinaitwa taxi. Kule taxi zinaitwa “meter taxi”. Ukisema taxi unamaanisha daladala. Nilipoamka, nikafanya utastaarabu wa chai kisha nikapanda taxi kuelekea workshop. Jamaa enzi hizo walikuwa wanaamuka saa 11 alfajiri kwa ajili ya kujiandaa kwenda kufungua goli. Saa 12 asubuhi yatari wapo kazini. (Sasa hivi jamaa hawauzi tena viatu, wanafanya biashara za magari, ni madon wakubwa. Sembe inalipa).

Maisha rasmi ya Durban yakaanza. Nikawa kila siku naamka alfajiri tunaenda kufungua goli la viatu. Biashara ilikuwa nzuri sana hasa siku za Jumamosi na Jumapili. Workshop siku za Jumamosi na Jumapili ilikuwa inajaa watu sana. Of course hata siku zingine watu walikuwa wanajaa lakini siku za weekends ilikuwa funga kazi. Watu wa Durban na vitongoji vyake siku za weekends ndio siku za kwenda kutembea town. Na ndio siku wabongo huzitumia kwenda kupiga mchomoko maana watu huondoka familia nzima na kwenda town kufurahia maisha. Pia shamrashamra za weekend huko huanza Ijumaa. (Mchomoko ni wizi wa kwenda kuvunja majumba na kuingia ndani na kuiba). Kule ukitaka kumjua kama demu ni wako na anakupenda muombe muonane siku za weekends. Demu wa South Africa, hasa Durban huwezi kumpata siku za weekends. Siku zingine zote utampata lakini weekends never ever. Akija siku ya weekend huyo ni wako na anakupenda.

Safari yangu ya mahusiano nikiwa Durban.

Kuna mademu watano ambao nilijihusisha nao kwa ukamilifu. Achana na wale wakuokota na kupiga na kusepa. Ila nitamuongelea huyu mmoja ambaye aliuteka moyo wangu, nikawa kama zezeta. Na hii ndio sababu imenifanya nianzishe huu uzi baada ya kumkumbuka huyu mtoto wa kizulu na drama zake zilizotaka kunitoa uhai.

Picha linaanza kama ifuatavyo:

Kama nilivosema saa 12 asubuhi tayari tupo workshop tunafunga tent kwa ajili ya kupanga viatu. Kazi ya kufunga tent na kupanga viatu ilikuwa inachukua kama masaa mawili hivi au saa moja na nusu hivi. Kwa hiyo kwenye saa mbili hivi tunakuwa tushamaliza kupanga viatu, na kuanza kutafuta chai. Kulikuwa na mbongo (jamaa) mmoja alikuwa anatupitishia chai na chapati. So, mida ya saa mbili hivi atatuletea chai na chapati. Jina lake alikuwa anaitwa Chaduma. Nadhani masela wa Durban kama wamo humu JF watakuwa wamemnyaka huyu mwamba na huenda wakanijua, ila nitajitahidi kuficha codes zote muhimu ili nisitambulike. Sometimes chapati za Chaduma zilikuwa zinakifu hivyo mtu unaamua kwenda kufungua kinywa sehemu nyingine. Dah! Chaduma alikuwa na maneno ya shombo hatari. Usipokula chapati zake atakusema kwa wabongo balaa. Kwa hiyo sometimes unaamua kula chapati za Chaduma kwa kuogopa kwenda kusemwa kwa wabongo kwamba unaringa.

Siku moja nilichoka kula chapati za Chaduma nikaamua kwenda kutafuta chakula sehemu nyingine. Hiyo siku ndio siku niliyokutana na kipenzi changu Khumbu Mkhize.

Nilipomaliza kufunga tent na kupanga viatu, kabla Chaduma hajafika nikaamua kwenda kufuata chai na vitafunio sehemu moja hivi. Hiyo sehemu ni ng’ambo ya pili kutoka workshop, yaani unatoka nje ya workshop, unavuka barabara ndio unaifikia hiyo sehemu. So, wakati nataka kuvuka barabara nikamuona msichana amekaa kwenye kingo ya barabara kajiinamia kama mtu yupo kwenye lindi la mawazo hivi. Basi nikamsogelea, nikamsemesha. Nikamsalimia, kisha nikamwuliza, vipi? Kulikoni asubuhi hii upo hapa? Akaniambia ana njaa. Nikimcheki ni binti mdogo tu, alikuwa na miaka 18 (nilikuja kujua umri wake baadae tulipokuja kuwa wapenzi). Basi nikampa rand 20 akale, nikamwelekeza goli langu (ninapofanyia kazi) ili akimaliza kula aje tufahamiane zaidi.

Nimechoka kuandika nipumzike kidogo, itaendelea.

Kusoma muendelezo bofya

SEHEMU YA PILI

SEHEMU YA TATU

SEHEMU YA NNE

SEHEMU YA TANO

SEHEMU YA SITA

SEHEMU YA SABA

SEHEMU YA NANE

SEHEMU YA TISA

SEHEMU YA KUMI

SEHEMU YA KUMI NA MOJA

SEHEMU YA KUMI NA MBILI

SEHEMU YA KUMI NA TATU

SEHEMU YA KUMI NA NNE

SEHEMU YA KUMI NA TANO

SEHEMU YA KUMI NA SITA

SEHEMU YA KUMI NA SABA

SEHEMU YA KUMI NA NANE

SEHEMU YA KUMI NA TISA

SEHEMU YA ISHIRINI

SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA

SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI

SEHEMU YA ISHIRINI NA TATU

SEHEMU YA ISHIRINI NA NNE

SEHEMU YA ISHIRINI NA TANO

SEHEMU YA ISHIRINI NA SITA

SEHEMU YA ISHIRINI NA SABA

SEHEMU YA ISHIRINI NA NANE

SEHEMU YA ISHIRINI NA TISA

SEHEMU YA THELATHINI

SEHEMU YA THELATHINI NA MOJA

SEHEMU YA THELATHINI NA MBILI

SEHEMU YA THELATHINI NA TATU

SEHEMU YA THELATHINI NA NNE

Good
 
Siku moja nilichoka kula chapati za Chaduma nikaamua kwenda kutafuta chakula sehemu nyingine. Hiyo siku ndio siku niliyokutana na kipenzi changu Khumbu Mkhize.

Nilipomaliza kufunga tent na kupanga viatu, kabla Chaduma hajafika nikaamua kwenda kufuata chai na vitafunio sehemu moja hivi. Hiyo sehemu ni ng’ambo ya pili kutoka workshop, yaani unatoka nje ya workshop, unavuka barabara ndio unaifikia hiyo sehemu. So, wakati nataka kuvuka barabara nikamuona msichana amekaa kwenye kingo ya barabara kajiinamia kama mtu yupo kwenye lindi la mawazo hivi. Basi nikamsogelea, nikamsemesha. Nikamsalimia, kisha nikamwuliza, vipi? Kulikoni asubuhi hii upo hapa? Akaniambia ana njaa. Nikimcheki ni binti mdogo tu, alikuwa na miaka 18 (nilikuja kujua umri wake baadae tulipokuja kuwa wapenzi). Basi nikampa rand 20 akale, nikamwelekeza goli langu (ninapofanyia kazi) ili akimaliza kula aje tufahamiane zaidi.
Ahsante kwa simulizi nzuri.
Naomba nimuongelee Khumbu (the character) kwa namna tofauti kidogo na konda msafi pia (the character). Konda msafi hakufika Durban kwa bahati mbaya, hata kukatisha masomo haikuwa bahati mbaya vile vile ndiyo maana akafanikiwa kumalizia masomo yake.

Kwangu Khumbu ni binadamu ambaye alikuwa wa kipekee sana na konda msafi alibahatika kupewa kazi ya kumlinda na kumuepusha na mabalaa ya hapa duniani. Khumbu (the character) ni binti ambaye alikulia kwenye mazingira magumu na alipitia mambo ambayo yalimuathiri kiasi fulani. Kutokana na hayo 'alijiapiza' kuwa hataki kuja kuishi maisha ya shida na watoto wake waje kuwa na maisha mazuri na wapate vile ambavyo hakuvipata. Kutokana na hilo moyo wake ulikuwa umeshapigwa ganzi na alikuwa na mission moja tu ya kufanikiwa.

Upekee wa Khumbu tunaanza kuuona kwa kukutanishwa na konda msafi, sio kila mja hupata bahati hii. Nafsi ya Khumbu inamtambua konda msafi bila shida na bila kipingamizi wanafahamiana na mengine kuendelea. Ningekuwa na uwezo wa kuelezea tukio hili kiroho ningelielezea kwa kirefu lakini elimu yangu huko haijitoshelezi kumuelewesha mwingine. Hii ni moja ya udhaifu wa kizazi cha sasa, kama ambavyo shuleni hatufundishwi kuhusu fedha na mifumo yake ndivyo pia hatufundishwi kuhusu mambo ya kiroho. Dini ni sehemu ndogo tu ndiyo maana dini zipo nyingi, hakuna ubishi kuwa jamii zetu kwa miaka mingi zilikuwa na taratibu za kuendesha mambo yake kiroho walitambua kama kuna MTU anazaliwa au kama kuna mabalaa yanakuja na nini cha kufanya.

Turudi kwa Khumbu, waswahili wanaweza kusema binti huyu alikuwa na nyota kali na mafanikio ya konda msafi yaliunganishwa na nyota yake. Konda msafi ndiyo mtu pekee aliyekuwa anamfanya Khumbu kujiona naye ni mtu (hasa baada ya bibi kufariki) kwahiyo uwepo wake ulikuwa ni kama kamba aliyofungwa Khumbu ili asipitilize au asijisahau katika matendo yake. Siku zote Khumbu alikuwa ana amani kwasababu anajua chochote kitakachotokea kuna mtu anayejali na kuna kimbilio sehemu.

Changamoto zote zilizotokea kati ya hawa wawili zilikuwa ni za kuwajenga, hasa konda msafi. Kugombana kulisaidia aweze kumaliza chuo hata kuja kupata kazi baadae, kwa maneno mengine kuna vikwazo viliwekwa ili konda msafi abaki kwenye jukumu lake kuu la kuwa 'guardian angel' wa Khumbu. Kama konda msafi angeweza kutambua mapema na angekuwa na misingi mizuru kiroho bila shaka simulizi hii ingekuwa na uelekeo tofauti kidogo hata kama matokeo ya mwisho yangebaki vile vile.

Kama katika maisha yako ukipata bahati ya kukutanishwa na Khumbu basi jitahidi utimize jukumu lako, kama ukibahatika kukutanishwa na konda msafi ushukuru na usiufanye moyo wako kuwa mgumu. Sio lazima Khumbu na konda msafi wawe wapenzi, wanaweza kuwa jinsi moja, wanaweza kuwa wafanyakazi sehemu moja, majirani au watu wa rika tofauti kabisa.

Hongera kwa konda msafi kwa kumfanya Khumbu aishi na kujiona ni mtu anayethaminiwa, kitu alichokikosa sehemu kubwa ya maisha yake. Khumbu alishindwa kukiri kwa kinywa chake namna maisha yake yalivyobadilika kutokana na kukutana na konda msafi lakini hii haikuwa siri, macho yake, moyo wake na tone yake viliongea.
 
Ahsante kwa simulizi nzuri.
Naomba nimuongelee Khumbu (the character) kwa namna tofauti kidogo na konda msafi pia (the character). Konda msafi hakufika Durban kwa bahati mbaya, hata kukatisha masomo haikuwa bahati mbaya vile vile ndiyo maana akafanikiwa kumalizia masomo yake.

Kwangu Khumbu ni binadamu ambaye alikuwa wa kipekee sana na konda msafi alibahatika kupewa kazi ya kumlinda na kumuepusha na mabalaa ya hapa duniani. Khumbu (the character) ni binti ambaye alikulia kwenye mazingira magumu na alipitia mambo ambayo yalimuathiri kiasi fulani. Kutokana na hayo 'alijiapiza' kuwa hataki kuja kuishi maisha ya shida na watoto wake waje kuwa na maisha mazuri na wapate vile ambavyo hakuvipata. Kutokana na hilo moyo wake ulikuwa umeshapigwa ganzi na alikuwa na mission moja tu ya kufanikiwa.

Upekee wa Khumbu tunaanza kuuona kwa kukutanishwa na konda msafi, sio kila mja hupata bahati hii. Nafsi ya Khumbu inamtambua konda msafi bila shida na bila kipingamizi wanafahamiana na mengine kuendelea. Ningekuwa na uwezo wa kuelezea tukio hili kiroho ningelielezea kwa kirefu lakini elimu yangu huko haijitoshelezi kumuelewesha mwingine. Hii ni moja ya udhaifu wa kizazi cha sasa, kama ambavyo shuleni hatufundishwi kuhusu fedha na mifumo yake ndivyo pia hatufundishwi kuhusu mambo ya kiroho. Dini ni sehemu ndogo tu ndiyo maana dini zipo nyingi, hakuna ubishi kuwa jamii zetu kwa miaka mingi zilikuwa na taratibu za kuendesha mambo yake kiroho walitambua kama kuna MTU anazaliwa au kama kuna mabalaa yanakuja na nini cha kufanya.

Turudi kwa Khumbu, waswahili wanaweza kusema binti huyu alikuwa na nyota kali na mafanikio ya konda msafi yaliunganishwa na nyota yake. Konda msafi ndiyo mtu pekee aliyekuwa anamfanya Khumbu kujiona naye ni mtu (hasa baada ya bibi kufariki) kwahiyo uwepo wake ulikuwa ni kama kamba aliyofungwa Khumbu ili asipitilize au asijisahau katika matendo yake. Siku zote Khumbu alikuwa ana amani kwasababu anajua chochote kitakachotokea kuna mtu anayejali na kuna kimbilio sehemu.

Changamoto zote zilizotokea kati ya hawa wawili zilikuwa ni za kuwajenga, hasa konda msafi. Kugombana kulisaidia aweze kumaliza chuo hata kuja kupata kazi baadae, kwa maneno mengine kuna vikwazo viliwekwa ili konda msafi abaki kwenye jukumu lake kuu la kuwa 'guardian angel' wa Khumbu. Kama konda msafi angeweza kutambua mapema na angekuwa na misingi mizuru kiroho bila shaka simulizi hii ingekuwa na uelekeo tofauti kidogo hata kama matokeo ya mwisho yangebaki vile vile.

Kama katika maisha yako ukipata bahati ya kukutanishwa na Khumbu basi jitahidi utimize jukumu lako, kama ukibahatika kukutanishwa na konda msafi ushukuru na usiufanye moyo wako kuwa mgumu. Sio lazima Khumbu na konda msafi wawe wapenzi, wanaweza kuwa jinsi moja, wanaweza kuwa wafanyakazi sehemu moja, majirani au watu wa rika tofauti kabisa.

Hongera kwa konda msafi kwa kumfanya Khumbu aishi na kujiona ni mtu anayethaminiwa, kitu alichokikosa sehemu kubwa ya maisha yake. Khumbu alishindwa kukiri kwa kinywa chake namna maisha yake yalivyobadilika kutokana na kukutana na konda msafi lakini hii haikuwa siri, macho yake, moyo wake na tone yake viliongea.
R.I.P khumbu!

Though jamaa anagoma kuelezea kifo chake
 
Hatimaye nimeimaliza leo hii story hongera zako mkuu kwa story nzuri ya kusisimua ja yenye Mafunzo mengi.

Japokua najua kuna details nyingi sana hujaziweka ila Bado burudani umeitoa to the maximum kongele zako na Asanteh mkuu.
 
Hii tabia ya kuleta story kama episodes za HBO sijui mmetoa wapi. Acheni utiaji. Anyway, mwenye link(s) kuanzia sehemu ya 30 acheze kama yeye tafadhali, wengine hatuna brain cells za kupitia kila page.
 
Back
Top Bottom