Jinsi ‘mikono’ ya Serikali ilivyotishia uhuru Bunge sintofahamu ya kujiuzulu Ndugai

Jinsi ‘mikono’ ya Serikali ilivyotishia uhuru Bunge sintofahamu ya kujiuzulu Ndugai

Unaamka asubuhi unakuta barua yako ya kujiuzulu inasambaa mitandao, unashangaa "mbona mimi sijaandika hiyo!!". Alafu watu wanakiri wameshaipokea na michakato ya chama imeanza.

Unataka kutoka nje labda uongee na vyombo vya habari unakuta umewakwa chini ya ulinzi nyumbani kwako, ni umafia yaani.

Wanasema ukiua kwa upanga utakufa kwa upanga, maza asisheshangaa nayeye yakimkuta ya 'kujiuzulu' akiwa amewekwa mtu kati na 'wazalendo'.
🤣🤣🤣ubabe ubabe tu
 
Kuwa spika ni lazima uwe sponsored na Chama cha siasa ata kama wewe si Mbunge
Sawa.

Kama angekuwa na hoja nzito zenye mashiko kwa wananchi, angepata chama cha kum sponsor au hata kuanzisha faction ndani ya CCM kumpa support.

Bottom line, mtu mwenye kusimamia priciple angekuwa tayari kupigania ukweli mpaka dakika ya mwisho hata kama ilimaanisha ataukosa Uspika na ubunge. Ndugai kajiuzulu bila kupigana mpaka mwisho, ametuonesha hana principle. Pengine hata hizo hoja kazitoa kisiasa zaidi tu.

Basi Ndugai angeacha chama kimfukuze, kisimpe sponsorship, wananchi tujue kwa wazi bila speculation kwamba chama kimemfukuza Spika uanachama kwa sababu katofautiana na msimamo wa serikali.

Halafu tungepima mbivu mbichi, kama Ndugai yuko sawa au chama kiko sawa.

Sasa hivi, Ndugai, kama Ndugai alitishiwa kweli, Ndugai anakuwa katukatili haki yetu ya kujua ukweli.

Hakutuambia kwamba katishiwa, na wala hakudinda mpaka afukuzwe yuone kafukuzwa.

Imabakia watu wanafanya speculations tu.

Kuna mambo mengi yenye matatizo na watetezi wa Ndugai.

1. Kuna speculation kwamba Ndugai kalazimishwa kujiuzulu. Hizi si habari zenye kuthibitishwa vyovyote.

2. Hata kama Ndugai kalasimishwa kujiuzulu, yeye kama Spika kazi yake ni kuisimamia serikali (executive), si kuchukua amri kutoka kwenye serikali. Kwa hivyo kama kajiuzulu kwa amri kutoka juu, alistahili kujiuzulu hata kama hakushinikizwa, kwa sababu hana sifa za USpika za kusimamia anachoona ni sawa.

3. Inawezekana kabisa Ndugai kajiuzulu mwenyewe kwa woga wake, na ujinga wake wa kusema mambo bila mkakati, halafu mnailaumu bure serikali kwamba imemtisha
 
Mkuu, Watanzania ni WANAFIKI sana! Kwa wakati ule, kelele zilikuwa kila kona za kumtuhumu! Wabunge wengi wakageuka kuwa ni CHAWA wa MWENYE NGUVU kuliko SPIKA.
Ni afadhari alivyojiuzulu "mwenywe",kwani alikuwa anaelekea KUAIBISHWA!
Sema wanaccm usitutaje sisi watanzania. Maovu ya Ndugai yanajulikana ndio maana hakuna aliyemuonea huruma wala kumtetea.
 
Kama angekuwa na hoja nzito zenye mashiko kwa wananchi, angepata chama cha kum sponsor au hata kuanzisha faction ndani ya CCM kumpa support.
Kiranga we ni mtu makini sana hoja zako zinakufanya uonekane kama mtu wa kawaida hapa JF.

Katiba ya Nchi yetu imempa mamlaka Rais kumfanya mtu yeyote kitu chochote na watu woote wakamuunga mkono Rais wakakukana wewe

Rais ndiye anayetoa vyeo na maslahi yoyote kadiri anavyotaka kwa mtu yeyote. Hii influence inamfanya kila mtu ku-bow down .
 
Katiba ya Tanzania haimruhusu rais kumuondoa Spika. Unless avunje bunge na kuitisha uchaguzi mpya kwa namna ambayo hata yeye rais anaenda kuchaguliwa tena.

Sasa katika hili katiba yetu imempa nguvu vipi rais kumlazimisha Spika ajiuzulu?

Kwa cheo cha urais hapa kwetu, urais uko juu ya katiba. Kwenye makaratasi ndio inaonyesha rais hawezi kumuondoa spika. Lakini kiuhalisia rais anaweza kumuondoa yoyote kwenye cheo chake, kwa njia halali na zisizo halali. Haya tunayaona kwa macho yetu. Rejea sakata la CAG Profesa Assad.
 
Ndugai alikuwa mkuu wa muhimili, analazimishwa vipi kujiuzulu bila ya kura ya bunge kutokuwa na imani na Spika?

Angekataa kujiuzulu tuone kama wangemvua uanachama.

Na hata wangemvua uanachama, hilo lingemuondolea ubunge tu, kuwa Spika wa bunge sio lazima uwe mbunge.

Marehemu Dr. Aleck Che Mponda aligombea Uspika bila ya kuwa mbunge.

Ndugai kwa njia moja au nyingine alikubali kujiuzulu yeye mwenyewe.

Kuna mtu anaitwa Preet Bharara, huyu alijuwa US State Attorney for the Southern District of New York, a presidential appointment. Rais Trump alikuwa hampendi, akawa anamfanyia figisu ajiuzulu. Jamaa likasema sijiuzulu ng'o, nataka nione unanifukuza kazi, dunia nzima ijue nimefukuzwa kazi na Trump, sijajiuzulu.

Trump akamfukuza kazi, dunia nzima iksjua Preet Bharara amefukuzwa kazi na Donald Trump.

Kwa nini Ndugai hakusimamia anachoamini na kukataa kujiuzulu mpaka afukuzwe tuone kafukuzwa clearly bila chengachenga?
Mkuu Kiranga nahisi unakosea kusema hayo.
Unajua Katibabya Tanzania imetengeneza umungu kwa mtu anayekalia kiti cha urais.

Ndugai hakuwa na namna maana tayari wabunge walishapangwa kuanzisha hoja ya kutokuwa na imani naye.

Wapo waliomtuhumu kutaka kuwatweza utu wao yaani wanawake.

Maandalizi ya kura kutokuwa na imani naye ilishakamata kasi
 
Mkuu, Watanzania ni WANAFIKI sana! Kwa wakati ule, kelele zilikuwa kila kona za kumtuhumu! Wabunge wengi wakageuka kuwa ni CHAWA wa MWENYE NGUVU kuliko SPIKA.
Ni afadhari alivyojiuzulu "mwenywe",kwani alikuwa anaelekea KUAIBISHWA!
Hapa ninachoona kimetokea ni hiki, ni uozo juu ya uozo juu ya uozo, hakuna kitu kilichotokea kwa principle.

1. Ndugai alitoa tuhuma za deni dhidi ya serikali kisiasa, bila ya kuwa na principle za dhati, akim test rais mpya kwa kuwa hakumpenda. Unajuaje hili? Unajua hili kwa sababu hilo tatizo la kukopa lilikuwapo sana tangu enzi za Magufuli, lakini Ndugai hakuwahi kulisema.

2. Hatujui kama Ndugai alitishiwa na serikali akajiuzulu. Watu wana rukia conclusion hii tu. Pengine mwenyewe alijitafakari akaona kachemsha, akaona ni lazima awe na mahusiano mazuri na rais ili kufanya kazi (kwa ujinga tu, kwa sababu kituhiki si si lazima), akaamua kujiuzulu mwenyewe. Inawezekana pia alitishiwa. Lakini, kwa sababu hatuna ushahidi kuwa alitishiwa, the fact remains kuwa Ndugai kajiuzulu mwenyewe.

3.Kama kweli Ndugai alitishiwa, halafu hakutuambia wananchi kwamba alitishiwa na hakusimama kidete kukataa kujiuzulu, basi Ndugai automatically anakosa sifa za kuwa Spika na kutuongoza kuisimamia serikali. Mtu ambaye hawezi kusimama kujitetea yeye mwenyewe atasimama vipi kutetea wananchi?

Any way you cut it, mimi nampa Ndugai lawama.
 
Ndugai alikuwa fisadi na kapiga hela za kutosha sana Bungeni. Who knows? Perhaps alikuwa blackmailed. Uresign na kusepa silently or else..
You could be very right.Labda kasahau "If you live in a glasshouse, don't throw stones".

Lakini ukweli utabaki kuwa kajiuzulu mwenyewe na hatuna rekodi kwamba kalazimishwa.

Ndiyo maana mimi nasema hata haya madai ya kuihamakia serikali kwa kukopa yalikuwa ni maigizo tu, kuna ajenda nyingine ya kisiasa dhidi ya Rais Samia hapa.

Kwa sababu, wakati wa Magufuli rais alikopa sana, na Ndugai hakusema kitu.

Kwa hivyo Ndugai kalikoroga mwenyewe, kisiasa zaidi, si ki principle kama watu wengi wanavyoamini, likamzidia, akajiuzulu kwa kukosa calculations nzuri.

Angekuwa kweli mtu w akusimamia principle asingejiuzulu.

Wewe Spika, kazi yako kuisimamia serikali. Unaona serikali inakopa bila discipline, unaisimamia, unatishiwa hapo hapo unajiuzulu?

Unajiuzulu ili iweje? Ili wanaokopa bila discipline wakope bila discipline zaidi?

I have no sympathy for Ndugai.

Alikuwa anacheza michezo ya kisiasa akakosea calculations kwa ujinga wake.

This was not a principled man who stood for some fiscal responsibility, far from it.
 
Rais wa Tanzania ni mwenyekiti wa CCM pia.
Na ni vigumu kuitofautisha CCM na dola.
OK, kwa hiyo ushatoka kwenye katiba umeenda kwenye habari ya kwamba rais wa Jamhuri ni mwenyekiti wa CCM pia?

Hili jambo halipo katika katiba, na tushakuwa na rais wa Jamhuri Mwinyi na Mwenyekiti wa CCM Nyerere.

So, katiba si issue au ni issue hapa?
 
Kwa ufujaji wa pesa za umma aliofanya hui ujasiri unaotaka aoneshe angeutoa wapi? Ulitaka Mwenzio akanyee debe?
Sawa. Tunakubaliana Ndugai ni fisadi.

Kwa hiyo habari nzima kwamba alikuwa anaisimamia serikali isikope sana kwa uchungu wa hela za umma na principle ni uongo tu.

Alisema hivyo kwa calculations zake za kitoto za kisasa.

Ndiyo maana kashindwa hata kupata ujasiri wa kukataa kujiuzulu, hana principle anayoisimamia zaidi ya ufiosadi, atawezaje kukataa kujiuzulu?
 
Kwa cheo cha urais hapa kwetu, urais uko juu ya katiba. Kwenye makaratasi ndio inaonyesha rais hawezi kumuondoa spika. Lakini kiuhalisia rais anaweza kumuondoa yoyote kwenye cheo chake, kwa njia halali na zisizo halali. Haya tunayaona kwa macho yetu. Rejea sakata la CAG Profesa Assad.
Sawa.

Lakini kama mtu anasimamia principles zake za msingi, kwa nini aogope rais kumuondoa kwenye cheo?
 
Mkuu Kiranga nahisi unakosea kusema hayo.
Unajua Katibabya Tanzania imetengeneza umungu kwa mtu anayekalia kiti cha urais.

Ndugai hakuwa na namna maana tayari wabunge walishapangwa kuanzisha hoja ya kutokuwa na imani naye.

Wapo waliomtuhumu kutaka kuwatweza utu wao yaani wanawake.

Maandalizi ya kura kutokuwa na imani naye ilishakamata kasi
Mimi hapa naona tatizo ni kwamba Ndugai ni mnafiki tu.

Ni mnafiki na kasema mambo haya kisiasa, si kwa principle.

Ndiyo maana Magufuli kakopa sana, lakini Ndugai hakusema kitu.

Ndiyo maana Ndugai kashindwa kupigania upande wake mpaka mwisho tuone kama angevuliwa uanacahama.

Atapigania vipi principles ambazo hana to begin with?

Ndugai alikuw amnafiki tu, na alivyojiuzulu kathibitisha hilo.

No, simaanishi kwamba point yake ya kukopa sana si muhimu, it's just that aliitumia point hiyo selectively, kinafiki, kisiasa.
 
Wangeliulia mbali muosha huoshwa alimtesa sana lisu mbwa huyo
 
Kichwa cheke mwenyewe sio kizuri anaibua hoja them anaitengua ndani ya siku1 tumsaidije angekomaa tungemsapoti
 
Katiba ni issue kwa sababu lazima uwe mwanachama wa chama cha siasa ili uwe mbunge au spika. Haiwezekani kuwa na kina Kyrsten Sinema, Joe Manchin, Angus King au Bernie Sanders katika bunge la Tanzania. Kama Ndugai asingejiuzulu mwenyewe wala hata isingefikia kura hatua ya wabunge wote kupiga kura ya kuamua abaki au aondolewe.
Kiranga unalitazama suala la Ndugai ki "idealistic" zaidi. Hii bado ni Tanzania ile ile ya Nyerere ya chama kushika hatamu.
OK, kwa hiyo ushatoka kwenye katiba umeenda kwenye habari ya kwamba rais wa Jamhuri ni mwenyekiti wa CCM pia?

Hili jambo halipo katika katiba, na tushakuwa na rais wa Jamhuri Mwinyi na Mwenyekiti wa CCM Nyerere.

So, katiba si issue au ni issue hapa?
 
aombe msahaa kwa asadi maana alitka mwenyewe
 
Ndugai hajawahi kusimamia principles ndio maana ilikuwa rahisi kung'oka.
Naam. Nakubaliana na wewe.

In fact kwa nchi inayojali principles, baada ya Ndugai kumcharaza mtu bakora kwa hasira hakutakiwa hata kuwa Spika.

Kwa sababu alijionesha kuwa ni mtu aliyejawa na mzuka wa hisia kuliko kuwa na strategic thinking.

Sababu ile ile iliyomfanya ampige mtu bakora bila kufikiri image yake itaonekanaje, ndiyo imemfanya aropoke vitu bila ya kuwa na mkakati wa kufanya baada ya kusema.
 
Katiba ni issue kwa sababu lazima uwe mwanachama wa chama cha siasa ili uwe mbunge au spika. Haiwezekani kuwa na kina Kyrsten Sinema, Joe Manchin, Angus King au Bernie Sanders katika bunge la Tanzania. Kama Ndugai asingejiuzulu mwenyewe wala hata isingefikia kura hatua ya wabunge wote kupiga kura ya kuamua abaki au aondolewe.
Kiranga unalitazama suala la Ndugai ki "idealistic" zaidi. Hii bado ni Tanzania ile ile ya Nyerere ya chama kushika hatamu.
Kwa hiyo unakubali Ndugai hakusema habari za deni kwa kuwa ni idealistic defender of fiscal responsibility?
 
Back
Top Bottom