Jinsi ndoa ya Mabeste Ilivyovunjika

Jinsi ndoa ya Mabeste Ilivyovunjika

Mwanzilishi wa harakati za Piga Kambi Utalii wa Ndani, Lisa Karl Fickernscher ambaye alikuwa ni mke wa msanii wa Hip Pop hapa nchini Mabeste amefunguka kiundani kuhusu maisha yake na aliyekuwa mume wake.

Maisha ya wawili hao yalikuwa maarufu zaidi kupitia mtandao wa instagram ambapo watu wengi zaidi pasi kujua nyuma ya pazia ya maisha yao walikuwa wakifurahia familia yao na kutamani kuwa kama wao.

Ambapo Lisa kupitia Youtube chaneli ya simulizi na sauti amefunguka mazito ukweli kuhusu maisha ya mahusiano yao nje ya kile ambacho mashabiki wengi walikuwa wanakiona kupitia kurasa zao za mitandao ya kijamii.

Ndoa si siri tena, juzi tumeyasikia ya Stamina kupitia sanaa yake leo Lisa amefunguka kinagaubaga sababu ambazo zimepelekea kuvunja ndoa yake na Mabeste na yapita mwaka sasa tangu wawili hao kufarakana.

Akihojiwa Lisa amehadithia sababu kuu mbili za kuachana na Mabeste ambapo ametaja kuwa Mabeste alikuwa mwanaume mwenye mkono mwepesi wa kumpiga hata mbele ya watoto wake , lakini pia ameeleza kuwa Mabeste hakuwa mwanaume wa kujitoa na mtafutaji kwaajili ya familia yake.

Pili amesema kwa asilimia 80 Mabeste alikuwa hasimamii majukumu yake kama baba wa familia na mume kwake.
”Hakuwahi kusimamia majukumu yake, sikuwahi kula hela ya muziki wake,… Kuna tofauti kubwa sana kati ya mkulima anayeenda shambani analima lakini hapati mavuno kuliko yule ambaye hafanyi kitu anashonda tu nyumbani…

Mabeste alikuwa mzito sana infika stage mnagombana nageuka kama mzazi kwake namlea kama navyolea watoto” amesema Lisa
Lisa ameongezea ”Alikuwa hataki kufanya chochote, kunipenda sio kusema unanipenda kunipenda ni matendo, sikuajiliwa, mwenzangu alirelax hakuwa na wivu mwanamke nimehudumia familia miezi miwili mitatu, alikuwa hata hajiulizi natoa wapi hakuwa na wivu”.

Aidha Mabeste na Lisa wameachana yapita mwaka sasa wakiwa na watoto wawili, Kendrick na Catelyn Mabeste.
Pia tumeona kumekuwa na mfumuko wa matukio ya aina hiyo ya ndoa za watu maarufu kufarakana jambo ambalo si jema sana kwani linatishia pakubwa sana wale wanaotarajia kuingia kwenye ndoa.

Tumeona Stamina na mke ndoa yao ikiwa na doa na Stamina kupitia sanaa yake ameamua kuweka wazi kisa mkasa.
Ndoa ni fumbo zito sana, ni Mungu tuu azijalie ndoa amani, upendo na ushirikiano kwani kila ndoa ina changamoto yake ni namna tu mnavyoweza kutatua changamoto hizo ili kusogeza familia.

Share this:


Chanzo Dar24
We jamaa umeniwahi me mwenyewe nilitaka niweke Uzi unahusiana na ndoa ya mabeste na mkewe Lisa Leo Leo.
 
Hahaha ngoja wachaga waje '' Hili tatizo la U-marioo naona linazidi kushika kasi nchini vijana wakiume Tunapoteza ile sifa yetu stahiki inayotufanya tuitwe wanaume ... Hii ni mbaya sana aise
Mabeste alikuwa Marioo.

Kazi hafanyi, muziki hafanyi. Yuko Busy na media tu na neno 'Nakupeoda, Nakupenda'

Does the word Nakupenda pay bills ?

Hivi Mabeste huwa ni mchagga ?

Miaka ya karibuni vijana wa kichagga wamekuwa ma-marioo wa kutosha.

Wengine wanaolewa Ulaya wengine Bongo !

Daaah

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kuna kipindi East Africa tv walishawahi kwenda mpaka nyumbani kwake mabeste na mkewe. huyu mkewe alikuwa anaumwa kalala tu ata kuongea hawezi..

Mabeste alipambana kinoma na harambee za wadau kama East Africa TV na wengine, wakafanikiwa akapona.. hakulalamika siku zote hizo??

Swali kwanini aseme yote hayo baada ya kuachana??

Mwanamke hata umfanyie mangapi, mkiachana ataeleza mapungufu yako na vijikosa vidogo vidogo na kuvikuza...
 
Huyu Mwanamke ni Mpumbavu kufikia hatua ya kuanza kurekodi mpaka marumbano ya ndani ya ndoa ina maana kua alishapanga kumuacha jamaa.. Na kajipanga kumdhalilisha pia.
Kitu kilichomuumiza ni Mabeste kuanza kuongea kwamba sababu ya wao kuachana ni pesa. Kaongea kwenye media.

Mama wa watu imebidi atoke hewani akaelezea jinsi alivyomlea jamaa toka mwanzo mpaka wanaachana, hadi mahari alijilipia.

Ugonjwa aliokuwa anaumwa inasemekana kwamba chanzo ni familia ya Mabeste, maana mara zote Mabeste alikuwa akiwatuhumu nyumbani kwao na haelewani na wazazi wake kabla hata hajakutana na Lisa.

Idea ya kukusanya michango kwa ajili ya matibabu ni ya Lisa, na hata kuendesha accounts za Mabeste yeye ndiye alikuwa anafanya hivyo, ile concert yeye ndiye aliyeplan na kuanza kufatilia kila kitu.

Ukiweza kupata muda wa kumsikia utaelewa, na bahati mbaya kwa Mabeste, Lisa alifikia sehemu akaanza kurekodi kila walichokuwa wanazozana au kujadili.
 
Naam nikweli ...Mimi nilikuwahga karibu sana na Mona gangster Ma-beste alikuwaga anakuja pale classic sound na shetta pamoja na marehemu Pancho .... So najua kiasi baadhi ya story zao zinazo husu maisha yao ... So unachokisema ni kweli Huyo binti alijitoa sana kwa ma-beste .... Ma-beste ni msanii mwenye kipaji sana '' Lakini tatizo Hana kiu ya kutafuta mafanikio
Ni changamoto, nafikiri tuna kitu kikubwa cha kujifunza.

Ila huyo mwanamke alikuwa anampenda jamaa, maana hata kukaa walikaa kwa huyo dada.

Na ukoo mzima wa Mabeste ulikuwa haumtaki.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binafsi vijana wengi kusimamia familia hatuwezi sababu ya anasa na kujipenda kulikopitiliza kunakoleta ubinafsi ndiyo maana mjini unaweza kuta mbaba in his 50's amevaa rafu na sendo chini muda wote yupo busy ila ukienda home mke wake anafaidi anasukuma range na watoto wanasoma na mahitaji wanapata kwa wakati.... Ila kijana bado hajanunua kipochi cha gucci sijui raba kali mara ashinde saloon kuweka kijogoo. .its sad

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naam nikweli ...Mwanamke akikosa Kazi maisha Yake yote Mwanaume atamvumilia .....ila mwanaume akikosa Kazi mwezi 1 tu basi kuna hatari kubwa kwa ndoa Yake kuvunjika

Sent using Jamii Forums mobile app
Me mama yangu kamvumilia mzee wangu alikosa kazi Mwaka 1 mzima huduma zote mama ndo alikuwa ana hudumia kuanzia kulipa ada shule, kula, nauli za Baba kwenda kutafuta kazi sehemu tofauti tofauti pamoja na kumlisha Baba n.k.Mzee baba sio wanawake wote wapo hivyo.
 
Kitu kilichomuumiza ni Mabeste kuanza kuongea kwamba sababu ya wao kuachana ni pesa. Kaongea kwenye media.

Mama wa watu imebidi atoke hewani akaelezea jinsi alivyomlea jamaa toka mwanzo mpaka wanaachana, hadi mahari alijilipia.

Ugonjwa aliokuwa anaumwa inasemekana kwamba chanzo ni familia ya Mabeste, maana mara zote Mabeste alikuwa akiwatuhumu nyumbani kwao na haelewani na wazazi wake kabla hata hajakutana na Lisa.

Idea ya kukusanya michango kwa ajili ya matibabu ni ya Lisa, na hata kuendesha accounts za Mabeste yeye ndiye alikuwa anafanya hivyo, ile concert yeye ndiye aliyeplan na kuanza kufatilia kila kitu.

Ukiweza kupata muda wa kumsikia utaelewa, na bahati mbaya kwa Mabeste, Lisa alifikia sehemu akaanza kurekodi kila walichokuwa wanazozana au kujadili.

Mkuu ina maana huyu dada alimkuta Mabeste hana shughuli au? Kama alimkuta na shughuli now mambo yamekwama anamkosea sana. Naona namna mambo yakiyumba sana mwanaume akikosa kipato kuliko wanawake. Huwezi kusikia mwanaume akisema nimemuacha sababu nilikuwa namlea.

Wadada wa siku hizi pamoja na kuelimika wamekuwa tegemezi zaidi kuliko mama zetu wa zamani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu ina maana huyu dada alimkuta Mabeste hana shughuli au? Kama alimkuta na shughuli now mambo yamekwama anamkosea sana. Naona namna mambo yakiyumba sana mwanaume akikosa kipato kuliko wanawake. Huwezi kusikia mwanaume akisema nimemuacha sababu nilikuwa namlea.

Wadada wa siku hizi pamoja na kuelimika wamekuwa tegemezi zaidi kuliko mama zetu wa zamani

Sent using Jamii Forums mobile app

Kasikilizeni interview hiyo, acheni kufanya judgement kabla hamjasikiliza kesi.
 
Back
Top Bottom