Jinsi nilivyotapeliwa na mtu niliyedhani ni mhitaji kumbe ni tapeli

Jinsi nilivyotapeliwa na mtu niliyedhani ni mhitaji kumbe ni tapeli

Pole sana mimi pia niliwahi kutapeliwa na mtu aliyejifanya mhitaji na mimi huruma ikanijaa basi nikatapeliwa,kitendo hicho kimenifanya niwe mzito sana kusaidia mtu nisiyemfahamu,niliumia mno,nawachukia matapeli na majambazi hata nikimkuta anachomwa moto naongezea kuni
Hupaswi kuwachukia bali unapaswa kuwaombea......kimsingi ni kwamba wamekwama na ni wahitaji lakini wanatumia njia zisizofaa kijapatia kipato......
 
Habari ndugu wapendwa na natumaini sote tu wazima wa afya na walio na mitihani ya maradhi au changamoto mbali mbali Mungu awapiganie ili sote tuishi kwa raha na kukiri utukufu wa Mungu.

Nimeamua kuileta habari hii ambayo ilinitokea mimi mwenyewe ili iwe kama funzo kwa wengine wenye mioyo ya kusaidia wanadamu wenzao wenye uhitaji lakini badala yake wanakutana na matapeli.

Nakumbuka siku fulani miezi kadhaa nyuma nilipanda dala dala kituo cha Mwembechai nikiwa naelekea Sinza, pembeni yangu alikuwa ameketi kijana mmoja wa makamo hivi huku mkono wake wa kulia akiwa ameushikilia huku akigugumia kwa maumivu makali.

Kilio chake kilivuta hisia zangu kama mwanadamu na kutaka kujua zaidi alipatwa na jambo gani, basi katika maelezo yake machache na alinifunulia kile kiganja kilichokuwa kimevimba kwa kutunga usaha mzito huku akisema kuwa hana msaada wowote nikadhamiria kumsaidia.

Alisema kuwa alikuwa anahitaji kiasi kama 15,000/= ili akapasuliwe ule uvimbe na kusafishwa kidonda. Yeye alisema ni dereva wa magari madogo ya mizigo na maskani yake ni pale Manzese Bakhresa kwa hali hiyo anashindwa kufanya shughuli zake za udereva hivyo kukosa kipato na kupelekea kudhoofu kutokana na lishe duni, pale nilimpatia kiasi kama 20,000/= ili akajitibie na nikampatia mawasiliano yangu ili awe ananipa maendeleo ya kidonda chake na kwa msaada zaidi.

Baada ya pale tukawa tunawasiliana na yule kijana kuhusu maendeleo ya kidonda chake na nikawa kila siku namtumia 7,000/= kwa ajili ya kujikimu huku akijiuguza kidonda chake, baada ya masiku kadhaa nikamuuliza wewe unatokea mkoa gani akaniambia anatokea mkoa wa Tanga. Nikamwambia kwanini nisimpe nauli arudi Tanga kwa wazazi kupumzika akijiuguza taratibu mpaka atakapotengemaa ndipo arejee mjini maana kwa mujibu wa maelezo yake ni kwamba hata pakulala hana maana alifukuzwa baada ya kushindwa kulipia pango, basi tukakubaliana kesho yake ajiandae ili nimtumie nauli ili aende nyumbani kupumzika, kesho yake nikamtumia 50,000/= nikiamini itamtosha nauli ya Tanga na hela kidogo ya kujikimu.

Baada ya masaa kama 7 nikiamini ameshaondoka mjini kwenda Tanga, akanipigia Simu kwa namba ya mtu mwingine maana yeye hakuwa na simu, aliniambia kuwa ameshafika Stendi Kange lakini amepungukiwa na nauli maana amebakiwa na 5,000/= hivyo mpaka afike kwao hiyo hela haitoshi. Kuanzia hapo akili yangu ikawa na mashaka kwa kuwa Tanga napafahamu inawezekana vipi kutoka Dar mpaka Tanga atumie 45,000/= ? Sikumtumia hela nilimwambia nipo bize kidogo.

Baada kama dakika 10 nikatumia namba nyingine kumpigia yule aliyenipigia nilimpa msichana aongee naye ili nijue yupo wapi, ikagundua kuwa yule alikuwa Manzese darajani na hakuwa Tanga, nikawapigia watu waliokuwa wanampa simu niongee naye na nilipokuwa nawatumia kumtumia hela, wote wakanithibitishia kuwa yule jamaa yupo Pale pale Dar na alikuwa ni muokota makopo ya plastiki maarufu na pia mtumiaji mkubwa dawa za kulevya hata wakati namtumia fedha walijua mimi ni ndugu yake na mara nyingi anautumia mkono wake uliojaa usaha kujipatia kipato huo ndio ukawa mwisho wa mimi na yeye, na yote niliyomsaidia nikamwachia Mungu.

Nb;
Tuwe macho na tunaodhania wanahitaji misaada.
pole sana na Mungu atakulipa na ndo maana umejua!
 
Pole kwake, hongera kwako mkuu.

Miaka ya nyuma nilikuwa ninafanya kazi sehemu fulani kipato cha chini mnooooo, ila sikuacha kutoa chochote kila Ijumaa kwa wazee waliopita kuomba msaada.

Kati yao alikuwepo Bibi mmoja ambaye nilikuwa namuandalia ya kwake hata nisipokuwa nayo akiba yangu ila yeye nilijitahidi kumpa.

Siku moja akaja nikampa. Akasema anaomba apumzike kidogo baadae akajifunika(akiamini amejificha) akaanza kuhesabu pesa. Ukweli ni kwamba alikuwa na kiasi kinachozidi hata mshahara wangu wa mwezi mzima.

Tangu pale nimejifunza kutoa zaidi kwenye vituo vya mayatima au mitaani ambapo naona kabisa maisha halisi ya mtu. Na nimeegemea kwa watoto zaidi.
Huku kishapu kuna mzee anasafiri kila baada ya miezi 6 kuenda mombasa na Nairobi kule kazi yake ni omba omba kama ya hao wa gogo, ila pale ndo tajuri ana maduka na nyumba hapa senta ana wake wawili na mashamba mengi.....omba omba imekua kazi nzuri ukipata sehemu nzuri na kilema au kasoro nzuri kwenye mwili wako, utapiga pesa paka basi.
 
Huku kishapu kuna mzee anasafiri kila baada ya miezi 6 kuenda mombasa na Nairobi kule kazi yake ni omba omba kama ya hao wa gogo, ila pale ndo tajuri ana maduka na nyumba hapa senta ana wake wawili na mashamba mengi.....omba omba imekua kazi nzuri ukipata sehemu nzuri na kilema au kasoro nzuri kwenye mwili wako, utapiga pesa paka basi.
Hayo ndo mawazo ya wajinga
 
Dah poleni sana.

Niliwahi kumhifadhi Dogo mmoja hata sikuwa namjua alikuja kunililia shida kuwa katoka huko kwao hana pa kula wala pa kuishi,Dogo akaniambia ana ujuzi Wa kunyoa,nikamtafutia job kwa mama mmoja alikuwa mke Wa mkurugenzi Wa manispaa alikuwa na salon yake hapa town.

Akakbidhiwa saloni apige job,Dogo alipiga kazi kama mwezi hivi,Dah sitakaa nisahau mama aliponipigia simu kunijulisha kuwa salauni imekombwa kula kitu,Dogo sijui pa kumpata,
mbaya zaidi alipita pia na baiskeli ya Kijana Wa duka LA Jirani na hiyo salon.

Pona yangu ilibidi nimweleze ukweli,Dah mama akanielewa akanipa somo LA kutomwamini mtu usiyemfahamu,ila toka Siku hiyo nimekuwa makini though bado natapeliwaga ila so kwa kiwango hicho tena.
 
Umenikumbusha miezi miwili iliyopita nikiwa pale studio nasubiri daladala niende kariakoo akaja kaka mmoja mdogo mdgo umri kati ya miaka 17-19. Akaniambia dada samahani mimi naulizia machinga complex ipo wapi, mimi nikasahau ilipo nikamwambia mh hata sikumbuki ipo wapil akasema yeye ametoka singida huku amekumbatia begi lake kama wa bush haswa aliepewa story dar kuna matapeli, akaniambia ni wachimbaji wadogo wa madinj hivyo wamepata na yeye ameambia aje huku auze maana wananunua kwa bei nzuri huko machinga complex,
Ikabidi nianze kumshauri.kwanza nikamwambia mimi machinga complex sipakumbuki ipo wapi ila ukiwa unamuuliza mtu usipende kumueleza shida yako yote sababu hujui yupi atakua mwema kwako na yupi mbaya. Basi ikabidi nimpigie mume wangu kumuuliza hivi machanga complex ipo wapi, huku napiga kuna baba yupo pembeni yangu mtu mzima yule kijana akaanza kumuuliza tena yule baba machinga xomplex ni wapi na akaanza kumuelezea habari ya yeye kuja kuuza haya madini, ikabidi nimvute yule kaka nimkumbushe awe makini asubiri mme wangu apokee sim anielekeze ni wapi na asirudie tena kuwaambia watu kila kitu kuhusu yeye. Bas yule baba akaamuelekeza machinga ni wapi, huku bado nasubiri daladala yule kaka akaanza kuniambia dada nisaidie nisije nkatapeliwa na bla bla nyingi, kilichokuja nitokea hata sielewi nilijikuta science sina simu wala pesa , ikabidi niombe msaada wa nauli nirudi nyumban.
Mpak leo naomba Mungu amuongoze yule kaka, unajitoa kumsaidia mtu kwa moyo kumbe ni tapeli.
Niliapa sitosaidia tena wapita njia lkn bado najiuliza kila mtu akila hiki kiapo tutaishi vipi maana na mimi nilisaidiwa nauli ya kurudi kwangu.
Kubwa ni kuwa makini matapeli ni wengi sana na sijui wengine wanatumia dawa gani maana niliumwa almost wiki nzima na nikawa napoteza kumbukumbu
 
Habari ndugu wapendwa na natumaini sote tu wazima wa afya na walio na mitihani ya maradhi au changamoto mbali mbali Mungu awapiganie ili sote tuishi kwa raha na kukiri utukufu wa Mungu.

Nimeamua kuileta habari hii ambayo ilinitokea mimi mwenyewe ili iwe kama funzo kwa wengine wenye mioyo ya kusaidia wanadamu wenzao wenye uhitaji lakini badala yake wanakutana na matapeli.

Nakumbuka siku fulani miezi kadhaa nyuma nilipanda dala dala kituo cha Mwembechai nikiwa naelekea Sinza, pembeni yangu alikuwa ameketi kijana mmoja wa makamo hivi huku mkono wake wa kulia akiwa ameushikilia huku akigugumia kwa maumivu makali.

Kilio chake kilivuta hisia zangu kama mwanadamu na kutaka kujua zaidi alipatwa na jambo gani, basi katika maelezo yake machache na alinifunulia kile kiganja kilichokuwa kimevimba kwa kutunga usaha mzito huku akisema kuwa hana msaada wowote nikadhamiria kumsaidia.

Alisema kuwa alikuwa anahitaji kiasi kama 15,000/= ili akapasuliwe ule uvimbe na kusafishwa kidonda. Yeye alisema ni dereva wa magari madogo ya mizigo na maskani yake ni pale Manzese Bakhresa kwa hali hiyo anashindwa kufanya shughuli zake za udereva hivyo kukosa kipato na kupelekea kudhoofu kutokana na lishe duni, pale nilimpatia kiasi kama 20,000/= ili akajitibie na nikampatia mawasiliano yangu ili awe ananipa maendeleo ya kidonda chake na kwa msaada zaidi.

Baada ya pale tukawa tunawasiliana na yule kijana kuhusu maendeleo ya kidonda chake na nikawa kila siku namtumia 7,000/= kwa ajili ya kujikimu huku akijiuguza kidonda chake, baada ya masiku kadhaa nikamuuliza wewe unatokea mkoa gani akaniambia anatokea mkoa wa Tanga. Nikamwambia kwanini nisimpe nauli arudi Tanga kwa wazazi kupumzika akijiuguza taratibu mpaka atakapotengemaa ndipo arejee mjini maana kwa mujibu wa maelezo yake ni kwamba hata pakulala hana maana alifukuzwa baada ya kushindwa kulipia pango, basi tukakubaliana kesho yake ajiandae ili nimtumie nauli ili aende nyumbani kupumzika, kesho yake nikamtumia 50,000/= nikiamini itamtosha nauli ya Tanga na hela kidogo ya kujikimu.

Baada ya masaa kama 7 nikiamini ameshaondoka mjini kwenda Tanga, akanipigia Simu kwa namba ya mtu mwingine maana yeye hakuwa na simu, aliniambia kuwa ameshafika Stendi Kange lakini amepungukiwa na nauli maana amebakiwa na 5,000/= hivyo mpaka afike kwao hiyo hela haitoshi. Kuanzia hapo akili yangu ikawa na mashaka kwa kuwa Tanga napafahamu inawezekana vipi kutoka Dar mpaka Tanga atumie 45,000/= ? Sikumtumia hela nilimwambia nipo bize kidogo.

Baada kama dakika 10 nikatumia namba nyingine kumpigia yule aliyenipigia nilimpa msichana aongee naye ili nijue yupo wapi, ikagundua kuwa yule alikuwa Manzese darajani na hakuwa Tanga, nikawapigia watu waliokuwa wanampa simu niongee naye na nilipokuwa nawatumia kumtumia hela, wote wakanithibitishia kuwa yule jamaa yupo Pale pale Dar na alikuwa ni muokota makopo ya plastiki maarufu na pia mtumiaji mkubwa dawa za kulevya hata wakati namtumia fedha walijua mimi ni ndugu yake na mara nyingi anautumia mkono wake uliojaa usaha kujipatia kipato huo ndio ukawa mwisho wa mimi na yeye, na yote niliyomsaidia nikamwachia Mungu.

Nb;
Tuwe macho na tunaodhania wanahitaji misaada.
7000 kila siku?Sawa Kidukulilo..
 
Mimi nilikutana na Mtu kipindi kile cha mfungo wa Ramadhani akanisimamisha akaniambia hajala tangu jana ivi basi yeye anatumia ARV akasema nimpe ata elfu moja akapate chai anywe zile dawa. Nikampa buku tano kwa vile alinionesha kile kichupa cha Dawa nimekaaa kama masaa ma3 hivi namuona yule jamaa amelewa yupo chakali yupo na wenzie niliumia sana.

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Habari ndugu wapendwa na natumaini sote tu wazima wa afya na walio na mitihani ya maradhi au changamoto mbali mbali Mungu awapiganie ili sote tuishi kwa raha na kukiri utukufu wa Mungu.

Nimeamua kuileta habari hii ambayo ilinitokea mimi mwenyewe ili iwe kama funzo kwa wengine wenye mioyo ya kusaidia wanadamu wenzao wenye uhitaji lakini badala yake wanakutana na matapeli.

Nakumbuka siku fulani miezi kadhaa nyuma nilipanda dala dala kituo cha Mwembechai nikiwa naelekea Sinza, pembeni yangu alikuwa ameketi kijana mmoja wa makamo hivi huku mkono wake wa kulia akiwa ameushikilia huku akigugumia kwa maumivu makali.

Kilio chake kilivuta hisia zangu kama mwanadamu na kutaka kujua zaidi alipatwa na jambo gani, basi katika maelezo yake machache na alinifunulia kile kiganja kilichokuwa kimevimba kwa kutunga usaha mzito huku akisema kuwa hana msaada wowote nikadhamiria kumsaidia.

Alisema kuwa alikuwa anahitaji kiasi kama 15,000/= ili akapasuliwe ule uvimbe na kusafishwa kidonda. Yeye alisema ni dereva wa magari madogo ya mizigo na maskani yake ni pale Manzese Bakhresa kwa hali hiyo anashindwa kufanya shughuli zake za udereva hivyo kukosa kipato na kupelekea kudhoofu kutokana na lishe duni, pale nilimpatia kiasi kama 20,000/= ili akajitibie na nikampatia mawasiliano yangu ili awe ananipa maendeleo ya kidonda chake na kwa msaada zaidi.

Baada ya pale tukawa tunawasiliana na yule kijana kuhusu maendeleo ya kidonda chake na nikawa kila siku namtumia 7,000/= kwa ajili ya kujikimu huku akijiuguza kidonda chake, baada ya masiku kadhaa nikamuuliza wewe unatokea mkoa gani akaniambia anatokea mkoa wa Tanga. Nikamwambia kwanini nisimpe nauli arudi Tanga kwa wazazi kupumzika akijiuguza taratibu mpaka atakapotengemaa ndipo arejee mjini maana kwa mujibu wa maelezo yake ni kwamba hata pakulala hana maana alifukuzwa baada ya kushindwa kulipia pango, basi tukakubaliana kesho yake ajiandae ili nimtumie nauli ili aende nyumbani kupumzika, kesho yake nikamtumia 50,000/= nikiamini itamtosha nauli ya Tanga na hela kidogo ya kujikimu.

Baada ya masaa kama 7 nikiamini ameshaondoka mjini kwenda Tanga, akanipigia Simu kwa namba ya mtu mwingine maana yeye hakuwa na simu, aliniambia kuwa ameshafika Stendi Kange lakini amepungukiwa na nauli maana amebakiwa na 5,000/= hivyo mpaka afike kwao hiyo hela haitoshi. Kuanzia hapo akili yangu ikawa na mashaka kwa kuwa Tanga napafahamu inawezekana vipi kutoka Dar mpaka Tanga atumie 45,000/= ? Sikumtumia hela nilimwambia nipo bize kidogo.

Baada kama dakika 10 nikatumia namba nyingine kumpigia yule aliyenipigia nilimpa msichana aongee naye ili nijue yupo wapi, ikagundua kuwa yule alikuwa Manzese darajani na hakuwa Tanga, nikawapigia watu waliokuwa wanampa simu niongee naye na nilipokuwa nawatumia kumtumia hela, wote wakanithibitishia kuwa yule jamaa yupo Pale pale Dar na alikuwa ni muokota makopo ya plastiki maarufu na pia mtumiaji mkubwa dawa za kulevya hata wakati namtumia fedha walijua mimi ni ndugu yake na mara nyingi anautumia mkono wake uliojaa usaha kujipatia kipato huo ndio ukawa mwisho wa mimi na yeye, na yote niliyomsaidia nikamwachia
Habari ndugu wapendwa na natumaini sote tu wazima wa afya na walio na mitihani ya maradhi au changamoto mbali mbali Mungu awapiganie ili sote tuishi kwa raha na kukiri utukufu wa Mungu.

Nimeamua kuileta habari hii ambayo ilinitokea mimi mwenyewe ili iwe kama funzo kwa wengine wenye mioyo ya kusaidia wanadamu wenzao wenye uhitaji lakini badala yake wanakutana na matapeli.

Nakumbuka siku fulani miezi kadhaa nyuma nilipanda dala dala kituo cha Mwembechai nikiwa naelekea Sinza, pembeni yangu alikuwa ameketi kijana mmoja wa makamo hivi huku mkono wake wa kulia akiwa ameushikilia huku akigugumia kwa maumivu makali.

Kilio chake kilivuta hisia zangu kama mwanadamu na kutaka kujua zaidi alipatwa na jambo gani, basi katika maelezo yake machache na alinifunulia kile kiganja kilichokuwa kimevimba kwa kutunga usaha mzito huku akisema kuwa hana msaada wowote nikadhamiria kumsaidia.

Alisema kuwa alikuwa anahitaji kiasi kama 15,000/= ili akapasuliwe ule uvimbe na kusafishwa kidonda. Yeye alisema ni dereva wa magari madogo ya mizigo na maskani yake ni pale Manzese Bakhresa kwa hali hiyo anashindwa kufanya shughuli zake za udereva hivyo kukosa kipato na kupelekea kudhoofu kutokana na lishe duni, pale nilimpatia kiasi kama 20,000/= ili akajitibie na nikampatia mawasiliano yangu ili awe ananipa maendeleo ya kidonda chake na kwa msaada zaidi.

Baada ya pale tukawa tunawasiliana na yule kijana kuhusu maendeleo ya kidonda chake na nikawa kila siku namtumia 7,000/= kwa ajili ya kujikimu huku akijiuguza kidonda chake, baada ya masiku kadhaa nikamuuliza wewe unatokea mkoa gani akaniambia anatokea mkoa wa Tanga. Nikamwambia kwanini nisimpe nauli arudi Tanga kwa wazazi kupumzika akijiuguza taratibu mpaka atakapotengemaa ndipo arejee mjini maana kwa mujibu wa maelezo yake ni kwamba hata pakulala hana maana alifukuzwa baada ya kushindwa kulipia pango, basi tukakubaliana kesho yake ajiandae ili nimtumie nauli ili aende nyumbani kupumzika, kesho yake nikamtumia 50,000/= nikiamini itamtosha nauli ya Tanga na hela kidogo ya kujikimu.

Baada ya masaa kama 7 nikiamini ameshaondoka mjini kwenda Tanga, akanipigia Simu kwa namba ya mtu mwingine maana yeye hakuwa na simu, aliniambia kuwa ameshafika Stendi Kange lakini amepungukiwa na nauli maana amebakiwa na 5,000/= hivyo mpaka afike kwao hiyo hela haitoshi. Kuanzia hapo akili yangu ikawa na mashaka kwa kuwa Tanga napafahamu inawezekana vipi kutoka Dar mpaka Tanga atumie 45,000/= ? Sikumtumia hela nilimwambia nipo bize kidogo.

Baada kama dakika 10 nikatumia namba nyingine kumpigia yule aliyenipigia nilimpa msichana aongee naye ili nijue yupo wapi, ikagundua kuwa yule alikuwa Manzese darajani na hakuwa Tanga, nikawapigia watu waliokuwa wanampa simu niongee naye na nilipokuwa nawatumia kumtumia hela, wote wakanithibitishia kuwa yule jamaa yupo Pale pale Dar na alikuwa ni muokota makopo ya plastiki maarufu na pia mtumiaji mkubwa dawa za kulevya hata wakati namtumia fedha walijua mimi ni ndugu yake na mara nyingi anautumia mkono wake uliojaa usaha kujipatia kipato huo ndio ukawa mwisho wa mimi na yeye, na yote niliyomsaidia nikamwachia Mungu.

Nb;
Tuwe macho na tunaodhania wanahitaji misaada.

Nb;
Tuwe macho na tunaodhania wanahitaji misaada.
Hawa ndo husababisha wahitaji wa Kweli washindwe kusaidiwa, ..... usichoke kutenda mema Mungu atakulipa “
 
Habari ndugu wapendwa na natumaini sote tu wazima wa afya na walio na mitihani ya maradhi au changamoto mbali mbali Mungu awapiganie ili sote tuishi kwa raha na kukiri utukufu wa Mungu.

Nimeamua kuileta habari hii ambayo ilinitokea mimi mwenyewe ili iwe kama funzo kwa wengine wenye mioyo ya kusaidia wanadamu wenzao wenye uhitaji lakini badala yake wanakutana na matapeli.

Nakumbuka siku fulani miezi kadhaa nyuma nilipanda dala dala kituo cha Mwembechai nikiwa naelekea Sinza, pembeni yangu alikuwa ameketi kijana mmoja wa makamo hivi huku mkono wake wa kulia akiwa ameushikilia huku akigugumia kwa maumivu makali.

Kilio chake kilivuta hisia zangu kama mwanadamu na kutaka kujua zaidi alipatwa na jambo gani, basi katika maelezo yake machache na alinifunulia kile kiganja kilichokuwa kimevimba kwa kutunga usaha mzito huku akisema kuwa hana msaada wowote nikadhamiria kumsaidia.

Alisema kuwa alikuwa anahitaji kiasi kama 15,000/= ili akapasuliwe ule uvimbe na kusafishwa kidonda. Yeye alisema ni dereva wa magari madogo ya mizigo na maskani yake ni pale Manzese Bakhresa kwa hali hiyo anashindwa kufanya shughuli zake za udereva hivyo kukosa kipato na kupelekea kudhoofu kutokana na lishe duni, pale nilimpatia kiasi kama 20,000/= ili akajitibie na nikampatia mawasiliano yangu ili awe ananipa maendeleo ya kidonda chake na kwa msaada zaidi.

Baada ya pale tukawa tunawasiliana na yule kijana kuhusu maendeleo ya kidonda chake na nikawa kila siku namtumia 7,000/= kwa ajili ya kujikimu huku akijiuguza kidonda chake, baada ya masiku kadhaa nikamuuliza wewe unatokea mkoa gani akaniambia anatokea mkoa wa Tanga. Nikamwambia kwanini nisimpe nauli arudi Tanga kwa wazazi kupumzika akijiuguza taratibu mpaka atakapotengemaa ndipo arejee mjini maana kwa mujibu wa maelezo yake ni kwamba hata pakulala hana maana alifukuzwa baada ya kushindwa kulipia pango, basi tukakubaliana kesho yake ajiandae ili nimtumie nauli ili aende nyumbani kupumzika, kesho yake nikamtumia 50,000/= nikiamini itamtosha nauli ya Tanga na hela kidogo ya kujikimu.

Baada ya masaa kama 7 nikiamini ameshaondoka mjini kwenda Tanga, akanipigia Simu kwa namba ya mtu mwingine maana yeye hakuwa na simu, aliniambia kuwa ameshafika Stendi Kange lakini amepungukiwa na nauli maana amebakiwa na 5,000/= hivyo mpaka afike kwao hiyo hela haitoshi. Kuanzia hapo akili yangu ikawa na mashaka kwa kuwa Tanga napafahamu inawezekana vipi kutoka Dar mpaka Tanga atumie 45,000/= ? Sikumtumia hela nilimwambia nipo bize kidogo.

Baada kama dakika 10 nikatumia namba nyingine kumpigia yule aliyenipigia nilimpa msichana aongee naye ili nijue yupo wapi, ikagundua kuwa yule alikuwa Manzese darajani na hakuwa Tanga, nikawapigia watu waliokuwa wanampa simu niongee naye na nilipokuwa nawatumia kumtumia hela, wote wakanithibitishia kuwa yule jamaa yupo Pale pale Dar na alikuwa ni muokota makopo ya plastiki maarufu na pia mtumiaji mkubwa dawa za kulevya hata wakati namtumia fedha walijua mimi ni ndugu yake na mara nyingi anautumia mkono wake uliojaa usaha kujipatia kipato huo ndio ukawa mwisho wa mimi na yeye, na yote niliyomsaidia nikamwachia Mungu.

Nb;
Tuwe macho na tunaodhania wanahitaji misaada.
Wala usisikitike, ulitenda wajibu wako kama mtu muungwana! Mungu atakulipa! Maisha na yaendelee.
 
Back
Top Bottom